Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,971
- Thread starter
- #161
Sehemu ya 43
Ulikuwa ni mpango kabambe ulioandaliwa kwa ajili ya kuhakikisha kwamba mzee Bruno anauawa haraka iwezekanavyo pasipo mtu yeyoite yule kufahamu chochote.
Kitu alichokifanya Hashimu ni kuandaa mipango yake, akaelekea katika Hospitali ya St. Louis na kuzungumza na madaktari.
Kwanza lilikuwa jambo gumu kuwashawishi lakini baada ya kuweka mezani kitita cha shilingi milioni kumi kila mmoja, wakakubaliana naye na hivyo kujiandaa kwa ajili ya kumpokea mzee Bruno ambaye angeletwa mahali hapo huku akiwa kwenye maumivu makali ya tumbo.
“Nimeshawapanga madaktari, cha msingi umebaki wewe tu,” alisema Hashimu, alikuwa akimwambia bi Rosemary.
“Safi sana, ngoja niandae hiyo sumu, kwa hiyo nimuwekee hapa nyumbani au?” aliuliza bi Rosemary.
“Hapana! Hiyo haitakiwi kufanyika hapa. Ikifanyika hapa itakuwa ni rahisi sana kugundulika, cha msingi mchukue na mpeleke kwenye mgahawa wa kifahari, huko ndipo utamuwekea kwenye kinywaji,” alisema Hashimu.
Wakakubaliana na siku hiyo usiku bi Rosemary akaonyesha mapenzi makubwa kwa mume wake kiasi kwamba mzee huyo akabaki akiwa na mshangao tu.
Alichukuliwa na kupelekwa bafuni kuoga, mapenzi aliyopewa siku hiyo yalikuwa motomoto na yalimkumbusha kipindi kile cha nyuma enzi za uchumba wao.
“Leo siamini kama unanionyeshea mapenzi haya,” alisema mzee Bruno.
“Nimeamua kukudhihirishia kwamba ninakupenda japokuwa siku hizi upo sana bize,” alisema mwanamke huyo.
“Ni biashara tu, ila usijali, kila kitu kitakuwa poa.”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
Bi Rosemary akamkumbatia mumewe huku akiwa na furaha tele, moyo wake ulikuwa na kiu kubwa ya kumuua mzee huyo, kila alipomwangalia, aliiona chuki kali ikiukamata moyo wake, hakumpenda mumewe kwa sababu tu alikuwa kizuizi kikubwa cha yeye kujiachia na mpenzi wake mpya, Hashimu.
Bi Rosemary akamwambia mume wake kwamba usiku wa siku hiyo alitaka kutoka naye mtoko wa usiku kwa ajili ya kwenda kula chakula. Hilo halikuwa tatizo kabisa, kwake, alipenda kufanya hivyo kwa kipindi kirefu japokuwa ubize ulimbana sana.
Kitendo cha kukubaliana naye, tayari kilimpa uhakika mwanamke huyo kwamba hatimaye angeweza kumuua mumewe na kuwa na mwanaume mwingine, tena mfanyakazi ambaye alifika hapo akiwa mikono mitupu kabisa.
“Umefikia wapi?”
“Kila kitu tayari, ndiyo natoka naye sasa hivi, yupo sebuleni ananisubiri...” alisema bi Rosemary baada ya kupigiwa simu na Hashimu.
“Basi sawa....si unajua wapi pa kwenda?”
“Ndiyo! Si ulisema Mlimani Lounge?”
“Ndiyo! Hapohapo...”
“Hakuna tatizo.”
Baada ya kujiandaa, akaelekea sebuleni ambapo akamkuta mumewe akimsubiria, alipomuona tu, mwanaume huyo akaachia tabasamu pana, kwa kila kitu kilichokuwa kikitokea usiku wa siku hiyo, kwake kilikuwa kama ndoto na hakukumbuka mara ya mwisho kutoka na mkewe mtoko wa usiku ulikuwa lini.
Wakaingia garini na kuanza kuelekea huko. Njia nzima bi Rosemary alikuwa akizungumza maneno ya kimahaba tu huku akimpigapiga mumewe kwa vikofi vyenye uchochezi wa mahaba humo garini.
Walichukua dakika ishirini tu wakaanza kuingia katika mgahawa huo ambapo wakaifuata meza moja, wakamuita mhudumu na kisha kumuagizia vinywaji.
“Una nini?” alimuuliza mhudumu.
“Pombe au soft drink?”
“Pombe...”
“Zipo zote, ila pombe kali tu...”
“Naomba Johnny Walker...”
“Mimi naomba Sant Anna..”
Wakabaki wawili hao mahali hapo, wakati kila kitu kikiendelea, tayari Hashimu alikuwa amekwishafika mahali hapo, alikaa kwa kujificha sana huku akiwaangalia watu hao wawili wakiyafurahia maisha.
Moyo wake ulimuuma mno, alimpenda mwanamke huyo, kilipita kipindi kirefu pasipo kulala naye na yote hayo yalisababishwa na huyo mzee ambaye piga ua ilikuwa ni lazima afe haraka iwezekanavyo.
Vinywaji vikaletwa, wakaanza kunywa. Stori za hapa na pale zilikuwa zikiendelea kama kawaida. Muda wote bi Rosemary alikuwa akiiangalia glasi ile namna ilivyokuwa ikienda mdomoni na mezani.
Sumu yake aina ya Cyanide ilikuwa kwenye mkoba wake, alichokitaka ni kuona mumewe akijisahau na kuweza kufanya yake. Pombe ziliendelea kuagizwa na mzee huyo akinywa kwa pupa.
“Fanya mambo...” aliisoma meseji ikiwa imeingia kwenye simu yake.
“Si unaona bado anakunywa, nitafanyaje sasa?”
“Hebu njoo huku karibu na choo chenu,” aliandika Hashimu.
Hilo halikuwa tatizo, alichokifanya mwanamke huyo ni kumuaga mumewe kwamba alikuwa akienda chooni, akaenda huko ambapo moja kwa moja akakutana na Hashimu.
“Unaremba sana mpenzi...tatizo nini?”
“Si mwenye umeona!”
“Ni kazi nyepesi mno...hebu kucha zako...”
Kwa Hashimu kazi wala haikuonekana kua kubwa, alichomwambia ni kuichukua dawa hiyo ya unga na kuiweka katika kucha zake ndefu kisha kuelekea kwenye ile meza na kujifanya kama anaishika glasi yake kumywesha kwa mapenzi motomoto na kuiruhusu sumu ile kuingia kwenye chupa.
Kwa mbinu aliyokuwa amepewa, hakukuwa na tatizo hata mara moja, akafanya kama alivyoambiwa na kurudi kwenye meza. Huku sumu ile ikiendelea kuwa kwenye kucha ya kidole shahada akachukua glasi aliyokuwa akiitumia mumewe iliyokuwa na pombe na kuiinua tayari kwa kumnywesha.
“Kama zamani jamani...nakupenda mpenzi wangu...” alisema mwanamke huyo kwa sauti ya chini, wakati glasi ikielekea kwenye mdomo wa mumewe, tayari sumu ile ikaingia ndani ya pombe ile, mzee Bruno alipokunywa, akanywa na ile sumu.
Mzee Bruno hakujua kitu chochote kile, aliendelea kunywa pombe mfululizo, baada ya dakika tano tu, akatulia, akalishika tumbo lake na kuanza kulalamikia maumivu makali ya tumbo.
Bi Rosemary akaanza kumpozapoza lakini hakuacha, bado aliendelea kuugulia kwa maumivu makali hali iliyowafanya hata wahudumu wengine kusogea katika meza hiyo.
“Kuna nini jamani?” aliuliza mhudumu mmoja.
“Mume wangu ana aleji na pombe, alihisi kwamba amepona kumbe bado, jamani nisaidieni nimpeleke hospitali...” alisema bi Rosemary.
Wahudumu hao wakaanza kumbeba na kumpeleka ndani ya gari. Bado mzee Bruno aliendelea kulia kwa maumivu makali, gari lilipoondoka mahali hapo kuelekea hospitali, naye Hashimu akatoka, akaingia ndani ya gari lake na kuanza kulifuatilia mpaka lilipofika katika Hospitali ya St. Louis iliyokuwa Mikocheni B.
“Amekwishakufa,” alisema bi Rosemary mara baada ya kulipaki gari lake nje ya jengo la hospitali hiyo, akateremka na kuanza kupiga kelele za kuomba msaada ambapo manesi wakamletea machela, wakautoa mwili wa mumewe na kuanza kuuingiza ndani.
Muda wote bi Rosemary alikuwa akilia, alijifanya kutokuamini kama kweli mumewe alikuwa hoi, alimshika na kulia sana, machozi yalimtoka mfululizo mpaka naye kutaka kuingia kwenye chumba cha upasuaji, yote hayo aliyoyafanya, alionekana kuwa muigizaji mzuri hata zaidi ya Jacob Steven.
“Nataka kuingia na mume wangu....nataka kuingia na mume wangu....” alipiga kelele bi Rosemary.
Je nini kitaendelea.....
Ulikuwa ni mpango kabambe ulioandaliwa kwa ajili ya kuhakikisha kwamba mzee Bruno anauawa haraka iwezekanavyo pasipo mtu yeyoite yule kufahamu chochote.
Kitu alichokifanya Hashimu ni kuandaa mipango yake, akaelekea katika Hospitali ya St. Louis na kuzungumza na madaktari.
Kwanza lilikuwa jambo gumu kuwashawishi lakini baada ya kuweka mezani kitita cha shilingi milioni kumi kila mmoja, wakakubaliana naye na hivyo kujiandaa kwa ajili ya kumpokea mzee Bruno ambaye angeletwa mahali hapo huku akiwa kwenye maumivu makali ya tumbo.
“Nimeshawapanga madaktari, cha msingi umebaki wewe tu,” alisema Hashimu, alikuwa akimwambia bi Rosemary.
“Safi sana, ngoja niandae hiyo sumu, kwa hiyo nimuwekee hapa nyumbani au?” aliuliza bi Rosemary.
“Hapana! Hiyo haitakiwi kufanyika hapa. Ikifanyika hapa itakuwa ni rahisi sana kugundulika, cha msingi mchukue na mpeleke kwenye mgahawa wa kifahari, huko ndipo utamuwekea kwenye kinywaji,” alisema Hashimu.
Wakakubaliana na siku hiyo usiku bi Rosemary akaonyesha mapenzi makubwa kwa mume wake kiasi kwamba mzee huyo akabaki akiwa na mshangao tu.
Alichukuliwa na kupelekwa bafuni kuoga, mapenzi aliyopewa siku hiyo yalikuwa motomoto na yalimkumbusha kipindi kile cha nyuma enzi za uchumba wao.
“Leo siamini kama unanionyeshea mapenzi haya,” alisema mzee Bruno.
“Nimeamua kukudhihirishia kwamba ninakupenda japokuwa siku hizi upo sana bize,” alisema mwanamke huyo.
“Ni biashara tu, ila usijali, kila kitu kitakuwa poa.”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
Bi Rosemary akamkumbatia mumewe huku akiwa na furaha tele, moyo wake ulikuwa na kiu kubwa ya kumuua mzee huyo, kila alipomwangalia, aliiona chuki kali ikiukamata moyo wake, hakumpenda mumewe kwa sababu tu alikuwa kizuizi kikubwa cha yeye kujiachia na mpenzi wake mpya, Hashimu.
Bi Rosemary akamwambia mume wake kwamba usiku wa siku hiyo alitaka kutoka naye mtoko wa usiku kwa ajili ya kwenda kula chakula. Hilo halikuwa tatizo kabisa, kwake, alipenda kufanya hivyo kwa kipindi kirefu japokuwa ubize ulimbana sana.
Kitendo cha kukubaliana naye, tayari kilimpa uhakika mwanamke huyo kwamba hatimaye angeweza kumuua mumewe na kuwa na mwanaume mwingine, tena mfanyakazi ambaye alifika hapo akiwa mikono mitupu kabisa.
“Umefikia wapi?”
“Kila kitu tayari, ndiyo natoka naye sasa hivi, yupo sebuleni ananisubiri...” alisema bi Rosemary baada ya kupigiwa simu na Hashimu.
“Basi sawa....si unajua wapi pa kwenda?”
“Ndiyo! Si ulisema Mlimani Lounge?”
“Ndiyo! Hapohapo...”
“Hakuna tatizo.”
Baada ya kujiandaa, akaelekea sebuleni ambapo akamkuta mumewe akimsubiria, alipomuona tu, mwanaume huyo akaachia tabasamu pana, kwa kila kitu kilichokuwa kikitokea usiku wa siku hiyo, kwake kilikuwa kama ndoto na hakukumbuka mara ya mwisho kutoka na mkewe mtoko wa usiku ulikuwa lini.
Wakaingia garini na kuanza kuelekea huko. Njia nzima bi Rosemary alikuwa akizungumza maneno ya kimahaba tu huku akimpigapiga mumewe kwa vikofi vyenye uchochezi wa mahaba humo garini.
Walichukua dakika ishirini tu wakaanza kuingia katika mgahawa huo ambapo wakaifuata meza moja, wakamuita mhudumu na kisha kumuagizia vinywaji.
“Una nini?” alimuuliza mhudumu.
“Pombe au soft drink?”
“Pombe...”
“Zipo zote, ila pombe kali tu...”
“Naomba Johnny Walker...”
“Mimi naomba Sant Anna..”
Wakabaki wawili hao mahali hapo, wakati kila kitu kikiendelea, tayari Hashimu alikuwa amekwishafika mahali hapo, alikaa kwa kujificha sana huku akiwaangalia watu hao wawili wakiyafurahia maisha.
Moyo wake ulimuuma mno, alimpenda mwanamke huyo, kilipita kipindi kirefu pasipo kulala naye na yote hayo yalisababishwa na huyo mzee ambaye piga ua ilikuwa ni lazima afe haraka iwezekanavyo.
Vinywaji vikaletwa, wakaanza kunywa. Stori za hapa na pale zilikuwa zikiendelea kama kawaida. Muda wote bi Rosemary alikuwa akiiangalia glasi ile namna ilivyokuwa ikienda mdomoni na mezani.
Sumu yake aina ya Cyanide ilikuwa kwenye mkoba wake, alichokitaka ni kuona mumewe akijisahau na kuweza kufanya yake. Pombe ziliendelea kuagizwa na mzee huyo akinywa kwa pupa.
“Fanya mambo...” aliisoma meseji ikiwa imeingia kwenye simu yake.
“Si unaona bado anakunywa, nitafanyaje sasa?”
“Hebu njoo huku karibu na choo chenu,” aliandika Hashimu.
Hilo halikuwa tatizo, alichokifanya mwanamke huyo ni kumuaga mumewe kwamba alikuwa akienda chooni, akaenda huko ambapo moja kwa moja akakutana na Hashimu.
“Unaremba sana mpenzi...tatizo nini?”
“Si mwenye umeona!”
“Ni kazi nyepesi mno...hebu kucha zako...”
Kwa Hashimu kazi wala haikuonekana kua kubwa, alichomwambia ni kuichukua dawa hiyo ya unga na kuiweka katika kucha zake ndefu kisha kuelekea kwenye ile meza na kujifanya kama anaishika glasi yake kumywesha kwa mapenzi motomoto na kuiruhusu sumu ile kuingia kwenye chupa.
Kwa mbinu aliyokuwa amepewa, hakukuwa na tatizo hata mara moja, akafanya kama alivyoambiwa na kurudi kwenye meza. Huku sumu ile ikiendelea kuwa kwenye kucha ya kidole shahada akachukua glasi aliyokuwa akiitumia mumewe iliyokuwa na pombe na kuiinua tayari kwa kumnywesha.
“Kama zamani jamani...nakupenda mpenzi wangu...” alisema mwanamke huyo kwa sauti ya chini, wakati glasi ikielekea kwenye mdomo wa mumewe, tayari sumu ile ikaingia ndani ya pombe ile, mzee Bruno alipokunywa, akanywa na ile sumu.
Mzee Bruno hakujua kitu chochote kile, aliendelea kunywa pombe mfululizo, baada ya dakika tano tu, akatulia, akalishika tumbo lake na kuanza kulalamikia maumivu makali ya tumbo.
Bi Rosemary akaanza kumpozapoza lakini hakuacha, bado aliendelea kuugulia kwa maumivu makali hali iliyowafanya hata wahudumu wengine kusogea katika meza hiyo.
“Kuna nini jamani?” aliuliza mhudumu mmoja.
“Mume wangu ana aleji na pombe, alihisi kwamba amepona kumbe bado, jamani nisaidieni nimpeleke hospitali...” alisema bi Rosemary.
Wahudumu hao wakaanza kumbeba na kumpeleka ndani ya gari. Bado mzee Bruno aliendelea kulia kwa maumivu makali, gari lilipoondoka mahali hapo kuelekea hospitali, naye Hashimu akatoka, akaingia ndani ya gari lake na kuanza kulifuatilia mpaka lilipofika katika Hospitali ya St. Louis iliyokuwa Mikocheni B.
“Amekwishakufa,” alisema bi Rosemary mara baada ya kulipaki gari lake nje ya jengo la hospitali hiyo, akateremka na kuanza kupiga kelele za kuomba msaada ambapo manesi wakamletea machela, wakautoa mwili wa mumewe na kuanza kuuingiza ndani.
Muda wote bi Rosemary alikuwa akilia, alijifanya kutokuamini kama kweli mumewe alikuwa hoi, alimshika na kulia sana, machozi yalimtoka mfululizo mpaka naye kutaka kuingia kwenye chumba cha upasuaji, yote hayo aliyoyafanya, alionekana kuwa muigizaji mzuri hata zaidi ya Jacob Steven.
“Nataka kuingia na mume wangu....nataka kuingia na mume wangu....” alipiga kelele bi Rosemary.
Je nini kitaendelea.....
ntaanza nayo baada ya kz sawa eenh.?

