Simulizi: Penzi lisilo Na Mwisho

Simulizi: Penzi lisilo Na Mwisho

Sehemu ya 46

Huko akamkuta Aisha akiwa kitandani. Alikuwa akilia kama mtoto. Machozi yalikuwa yakimbubujika mashavuni mwake, alionekana kama mtu mwenye maumivu makali mno.

Razak akaanza kumsogelea, alipomfikia, akamshika bega kwa nyumba na kumkumbatia kwa nyua. Aisha hakunyamaza, ndiyo kwanza kilio chake kikaongezeka.

“Naomba unisamehe mpenzi....” alisema Razak kwa sauti ndogo karibu kabisa na sikio la Aisha.
“Naomba uniache Razak, naomba uniache....”

“Hapana! Nimekosa mpenzi, nakiri hilo ila huu si muda wa kukaa na kukasirika, utakasirika mpaka muda gani? Utalia mpaka muda gani? Nimekosa, ninakiri, ninahitaji msamaha wako,” alisema Razak huku akimbembeleza Aisha.
“Nina muda gani mpaka nife?” aliuliza Aisha, Razak akabaki kimya.

“Nimekuuliza wewe...”
“Nisikilize Aisha...”
“Kwanza niambie....”

“Aisha....”
“Utaniambia au huniambii?”
“Aisha...ninaumia....”
“Najua unaumia, niambie nimebakiza muda gani kufa?”

“Miezi miwili...”
“Kwa nini hukuniambia kabla?”
“Kwa sababu sikutaka kukuona unalia, unajua ni kiasi gani ninakupenda. Moyoni niliumia sana lakini sikuwa na jinsi, nilitakiwa kukubaliana na hali halisi iliyokuwepo.

“Aisha, siku ambayo ulilalamika maumivu makali ya tumbo, nilikupeleka hospitali, nadhani unakumbuka....” alisema Razak.
“Ikawaje?”
“Tulipofika huko, wakaniambia kwamba una kansa ya utumbo mkubwa,” alijibu Razak.

“Halafu.....”
“Wakaniambia kwamba utakufa kwani ni terminal cancer...”
“Ndiyo nini hiyo?”
“Kansa ambayo ni lazima ufe...” alisema Razak, Aisha akaanza kulia.

“Aisha...niliumia sana moyoni lakini sikuwa na jinsi, nilitamani kukuona unapona, nikatoka hapa na kukupeleka India kwa kudhani kwamba majibu yangebadilika, kilichonisikitisha, yaliendelea kubaki hivyohivyo kwamba ni lazima ufe...Aisha, ninakupenda, sitaki nikuache, ninataka niendelee kuwa nawe mpaka siku ya mwisho ya uhai wangu...” alisema Razak.

Maneno hayo yaliuchoma moyo wa Aisha, akashindwa kuelewa ni kitu gani alitakiwa kufanya. Alikumbuka kwamba alipelekwa India na mpenzi wake, kote huko ilikuwa ni kumtafutia tiba, apone na kuwa mzima kabisa.

Huo haukuwa mwisho wa uhusiano wao, Aisha akamsamehe Razak na kumkumbatia kwani maneno aliyoyasema yalimchoma sana na hata kama angelia na kukasirika, bado ukweli ungebaki palepale kwamba ni lazima afe.

“Ninakupenda Aisha...nina mapenzi yasiyokwisha moyoni mwangu, haijalishi utaishi kwa kipindi gani, NI LAZIMA NIKUOE...” alisema Razak huku akimwangalia msichana wake usoni.
“Kweli?”
“Ndiyo! Ni lazima nikuoe....”

Huo ndiyo ulikuwa msimamo wake, mchumba wake alikuwa kwenye hali mbaya lakini hakutaka kumuacha, alimwambia wazi kwamba alitaka kumuoa hivyo akahakikisha kwamba mipango ya harusi iliyokuwa ikifanyia iendelee zaidi japokuwa muda mwingi wote wawili walionekana kutokuwa na furaha.

Baada ya kukatika mwezi mmoja, hapo ndipo sherehe ya harusi kubwa ikaanza kufanyika na Aisha kuolewa na Razak, harusi ambayo ilihudhuriwa na watoto wengi wa mitaani ambao walikula na kunywa mpaka kusaza.

“Mbona hauna furaha Razak, umekuwa mume wa Aisha...” alisema rafiki yake Rajabu.

“Nina furaha Rajabu...”
“Hapana bwana, huwa haupo hivyo, hebu changamka kidogo...” alisema Rajabu huku akimtingishatingisha Razak.

Alitamani kuwa na furaha lakini hilo halikuwezekana hata kidogo, mke wake aliyekuwa akimpenda alibakiza mwezi mmoja tu wa kuishi. Huo ndiyo ulikuwa muda wa kumfariji, ndiyo ulikuwa muda wa kumuonyeshea ni jinsi gani alikuwa akimpenda.

Kipindi hicho Razak hakutaka kufanya kitu chochote kile, aliamua kuachana na biashara zake na kuanza kuwa karibu zaidi na mkewe. Kila siku alijitahidi kumfurahisha kwani alijua kwamba yeye ndiye alikuwa furaha yake bila kufanya hivyo, Aisha angeteseka sana nafsini mwake.

Mara nyingi alimchukua na kumpeleka katika mitoko mbalimbali hasa katika fukwe za baharini na hata kwenye hoteli kubwa. Alitaka afurahie maisha yake ya mwisho na msichana huyo.

Walipokuwa wakirudi nyumbani, walijifungia ndani, hawakutoka nje, huko walizungumza mengi huku Razak akimwambia Aisha ni jinsi gani alikuwa akimpenda kwa moyo wa dhati kwamba hata kama alikuwa kwenye kiti cha walemavu, kukaribia kufa lakini bado alimuoa.

“Nitakupenda mpaka kifo changu...” alisema Razak kwa sauti ya chini, kwa kumsikiliza tu alionekana kukata tamaa.

“Nitakupenda pia, hakika umekuwa mtu muhimu sana katika maisha yangu, japokuwa tumekaa kwa kipindi kifupi lakini umenionyeshea jinsi mapenzi yalivyo, sikudhani kama kuna mtu anaweza kupenda kama unavyonipenda...”

alisema Aisha huku machozi yakimbubujika kwa maumivu makali.
“Ugonjwa si kitu, tangu siku ya kwanza nilikupenda na ninakuahidi kukupenda milele,” alisema Razak.

“Kweli?”
“Niamini mke wangu...” alisema Razak na kisha kumkumbatia.

Siku hiyo ikapita, siku zikaendelea kukatika na mwisho wa siku kubakia siku mbili kabla ya mwezi kumalizika, alichokifanya Razak ni kumuita Aisha na kukaa aye sebuleni, mbele ya wazazi wake, alikuwa ameshika karatasi moja ndefu iliyokuwa na maneno mengi, alitaka kuisoma mahali hapo, alitaka kumsomea mke wake kwani hakuwa na zaidi ya siku tatu za kuishi.

Muda wote huo, hapo sebuleni Aisha alikuwa mtu wa kulia tu, hakukuwa na kitu alichotokea kukichukia kama ugonjwa wa kansa ambao ulimfanya kubakiza saa chache kabla ya kufariki dunia.
*****

Je nini kitaendelea...
 
Sehemu ya 47

Kila mtu alikuwa kimya mahali hapo, Aisha alikuwa ametulia kwenye kiti chake, alitulia tuli huku akimwangalia mume wake ambaye muonekano wake tu ulionyesha ni jinsi gani alikuwa na mawazo tele, hata ule mwili aliokuwa nao kipindi kile cha nyuma, siku ya kwanza aliyoonana nayo hakuwa nao tena.

Razak alibaki kimya, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, hakuamini kama yeye ndiye aliandika barua hiyo ambayo aliiweka kwa ajili ya mke wake aliyebakisha muda mchache kabla ya kufa kutokana na kansa ya utumbo mpana aliyokuwa nayo.

“Aisha mke wangu, kabla ya kukusomea nilichokiandika, jua kwamba ninakupenda sana,” alisema Razak kwa sauti ndogo huku akimwangalia mke wake usoni.
“Nakupenda pia mume wangu....” alisema Aisha kwa sauti ya chini kabisa.

“Nimeandika haya kama maneno yangu ya mwisho-mwisho kwa ajili yako, najua utaumia lakini kitu ambacho ninataka kukuonyeshea ni jinsi gani ninakupenda, na jinsi gani nimepigania uhai wako kwa nguvu zangu zote” alisema Razak na Aisha kutingisha kichwa.

Hapohapo akaanza kuisoma barua hiyo....
Mke wangu Aisha, ninayaandika maneno haya huku moyo wangu ukiwa kwenye maumivu makali, siamini kile ninachokipitia, siamini kama mwisho wetu ungekuwa wenye kuumiza namna hii na wakati mwanzo wetu ulikuwa ni wa furaha tele.

Ninaumia kukuona ulivyo, ninaumia kila ninapoyaona machozi yako.

Hakika umekuwa mwanamke aliyebadilisha maisha yangu, kuniletea furaha ambayo leo inanifanya kuwa nilivyo, ila pamoja na kuniletea furaha hiyo, Mungu hataki niwe nayo, Mungu hakutaka kuniona nikitabasamu kila ninapokuangalia na ndiyo maana leo hii, ninalia, ninahuzunika, ninakosa nguvu, sina faraja, moyo wangu umejeruhiwa, yote hii ni kwa sababu ya maisha yako, yote ni kwa sababu ya ugonjwa wa kansa unaoumwa.

Nilikuja kwako nikiwa na mapenzi ya dhati, nakumbuka siku ya kwanza kukuona kule ufukweni, nilikuwa mtu niliyekata tamaa, nilikuwa mtu niliyetafuta msaada wa maji jangwani, kipindi hicho ndicho nilitoka kutendwa na msichana ambaye kila siku aliniambia ananipenda, aliniambia mimi wa thamani kwake.

Sikuamini kama ningeweza kupenda tena kwani bado moyo wangu ulikuwa na kidonda kibichi kabisa ila baada ya kukuona, moyo wangu ukapata ahueni kabla ya kupona kabisa.

Sikuangalia kama ulikuwa ombaomba mitaani, sikuangalia utajiri wangu, umasikini wako na utajiri wangu uliunganishwa na kitu kimoja kiitwacho MAPENZI.

Siku zikapita, tuliyafurahia mapenzi lakini baada ya usiku mmoja kuumwa na kukupeleka hospitali, hakika ndiyo ulikuwa usiku uliobadilisha kila kitu.

Ukaumwa utumbo, nikaambiwa kwamba una kansa ya utumbo mpana isiyopona.
Niliumia sana, nililia sana siku hiyo kwani ulikuwa kitu muhimu sana kwangu, sikutaka kukubaliana na majibu, hivyo nikaamua kukupeleka nchini India kwa kuamini kwamba inawezekana majibu yangebadilika.

Niliondoka na wazazi wangu kwenda huko, tulipofika, ukafanyiwa vipimo. Kilichoniuma zaidi, kilichonifanya kulia zaidi ni pale tulipoambiwa kwamba una miezi mitatu ya kuishi, yaani mwezi mmoja baada ya ndoa yetu.

Nilichanganyikiwa sana mke wangu, nilimuomba sana Mungu japo afanye muujiza, muujiza utakaoirudisha afya yake kama zamani lakini pamoja na kuomba sana, Mungu akakunyima uponyaji.

Ninakubaliana na kosa nililolifanya la kutokukwambia kwamba una kansa, nilijaribu kukuangalia, hali uliyokuwa nayo, nikahisi kwamba ningesababisha maumivu zaidi au hata kuukatisha uhai wako haraka mno, hivyo nikanyamaza.

Siku uliponiambia una ujauzito wangu, hakika sikufurahi, sikutarajia kuona mtoto wangu akifa siku chache zijazo, niliumia sana lakini bado sikuwa na jinsi, nikaubadilisha uso wangu, nikaweka tabasamu pana japokuwa moyo wangu ulikuwa ukiwaka kwa maumivu makali.
Aisha mke wangu! Nakuahidi kwamba nitaendelea kukupenda.

Kama nilivyokupenda ukiwa mgonjwa, nikakuoa katika hali hiyohiyo uliyokuwa nayo, basi jua kwamba hata kifo kitakapotutenganisha, bado upendo wangu hautoweza kufutika mpaka nitakapoondoka katika dunia hii.

Fedha si kitu zaidi ya uhai, nilitumia kila kiasi kilichohitaji kwa ajili yako, nilitumia fedha kupingana na majibu ya madaktari, nilitaka kuwaonyeshea kwamba fedha ndiyo kila kitu.

Mke wangu Aisha, ninaumia, sina pa kukimbilia tena, nimebaki nikiangalia nione nini kitakachoendelea kwani kama kuishi muda mrefu kungehitaji fedha, ningetumia utajiri wangu wote kwa ajili yako.

Nakupenda mke wangu, na nitakupenda maisha yangu yote.

Razak alipomaliza kusoma maneno hayo, akautuliza uso wake chini, machozi yaliendelea kumtoka, kuumia kwa moyo wake hakukuacha, hakukuwa na kitu kilichomuumiza kama kumuona mke wake akiwa amebakiza siku chache za kuishi.

Wazazi wake wakamsogelea na kuanza kumbembeleza kwa kumpigapiga mgongoni. Hapohapo Razak akasimama na kumfuata mke wake pale alipokaa kwenye kile kiti cha matairi, alipomfikia, akapiga magoti mbele yake.

“Ninakupenda mke wangu...” alisema Razak huku akimwangalia mke wake usoni.

Aisha alikuwa kimya kitini pale, alikuwa akiangalia sehemu moja tu, macho yake yalitulia, hayakuhama kitu kilichowafanya wazazi wake Razak kushtuka kwa kudhani kwamba msichana huyo alikuwa marehemu.

“Aisha...Aisha...Aisha...” aliita mama yake Razak lakini msichana huyo akawa kimya.
Razak akayainua macho yake na kumwangalia mke wake, macho yake yalitulia vilevile kama yalivyokuwa.

Alishtuka, hakuamini alichokuwa akikiona, alijaribu kumuamsha mke wake lakini alitulia tuli, aliposikiliza mapigo ya moyo, yalikuwa yametulia, Aisha alikuwa amefariki dunia kitini hapo.
“Mke wangu...mke wangu...” aliita Razak huku akimtingisha Aisha.

“Mke wangu amka uniangalie, amka uongee nami, mke wangu amka, bado mapema mno kufa, usiniache, amka uniangalie...” alisema Razak, hakuacha kumtingisha Aisha.

Hakukuwa na kilichoendelea, kila kitu walichoambiwa ndicho hicho kilichotokea mahali hapo. Razak alijitahidi sana kumuamsha Aisha lakini mwanamke huyo huyo hakuamka, aliendelea kubaki kimya, kimya milele.

Razak aliumia sana, siku hiyo, ilikuwa ni kelele ndani ya nyumba, Razak aliomboleza lakini machozi yake yote hayo hayakubadilisha kitu chochote kile.

Baba yake akapiga simu katika Hospitali ya St. Peters ambao walifika nyumbani hapo, wakauchukua mwili tayari kwa kuondoka nao. Razak hakutaka kubaki nyumbani, naye akaingia ndani ya gari na kuanza kuelekea hospitalini.

Njiani, muda wote Razak alikuwa akiendelea kumuamsha Aisha huku akilia, bado aliamini kwamba mwanamke huyo angeamka na kuanza kumwangalia tena.

Safari hiyo ikaishia katika hospitali waliyokuwa wakimpeleka, machela ikaletwa, mwili ukapandishwa na kuanza kusukumwa kuelekea ndani. Razak hakutaka kuuachia mwili, bado aliendelea kwenda nao huku akimtaka kufumbua macho na kumwangalia tena.

Alipofikishwa katika chumba husika, Razak akaambiwa asubiri nje kwenye benchi. Akakaa hapo na kuanza kulia.
Hata dakika nyingi hazikupita, wazazi wake wakafika mahali hapo, wakamfuata na kuanza kumbeleleza tena kwani bado alikuwa akilia japokuwa kwa sauti ya chini.

Siku hiyo ilikuwa ni siku yenye maumivu makali, hakuamini kama kweli mke wake aliyempenda alikufa kwa ugonjwa wa kansa uliomsumbua kwa muda wa miezi mitatu tu.

Taarifa zilitoka ndani ya chumba kile zilithibitisha kwamba Aisha alikuwa amekufa hivyo walitakiwa kupanga mazishi na hatimaye msichana huyo aweze kuzikwa.

“Kwa nini Aisha? Kwa nini Mungu aliamua kumchukua kutoka kwangu?” aliuliza Razak huku akilia lakini hakukuwa na mtu aliyekuwa na majibu zaidi ya kumfariji tu.

Taarifa zikaanza kusambazwa kila kona, kila aliyesikia, alihuzunika, hakuamini kama msichana yule alikuwa amefariki mwezi mmoja baada ya kuolewa. Katika mazishi hayo, walifika watu mbalimbali, wafanyabiashara wakubwa, watu maarufu lakini pia watoto wa mitaani, kila mtu alitaka kumzika Aisha.

Saa saba mchana walikuwa makaburini. Hapo ndipo Razak alipolia sana mpaka watu wengine kumuonea huruma kwani hata maneno aliyokuwa akiyazungumza kuhusu mke wake, yalimgusa kila mtu mahali hapo hasa watu walipojua kwamba msichana huyo alifariki huku akiwa na mimba.

“Jamani mumewe anatia huruma...” alisikika mwanaume mmoja.
“Wewe acha tu, kufiwa na mke mwenye mimba, hakika inauma sana,” alisema jamaa mwingine.

Miongoni mwa watu waliokusanyika katika mazishi hayo alikuwa Hashimu, muda wote alikuwa pembeni ya Ahmad na Mohammedi, alikuwa akilia, hakuamini kama msichana aliyekuwa akimpenda tangu zamani alikuwa amefariki dunia.

Kwa kumwangalia, alionekana mtu aliyekuwa mgonjwa kabisa, mwili mwake ulikonda mno, kansa ya koo ilimmaliza na kumfanya kutokuwa na furaha hata kidogo. Mashine yake ya kuzungumzia haikutoka kooni mwake, hiyo ndiyo iliyompa nguvu ya kuzungumza japokuwa kwa shida mno.

Mara baada ya shekhe kuzungumza maneno mengi ya kuhusu maandiko ya vitabu vya dini, akamaliza na hatimaye kaburi la Aisha kufukiwa huku nyuma yake kukiwa na maumivu makubwa.
“Pole sana Razak...” alisema Hashimu, alikuwa akimpa pole Razak.

“Asante sana...”
Huo haukuwa mwisho wa yeye kufika makaburini hapo, mara kwa mara alifika na kukaa pembeni ya kaburi la mke wake. Moyo wake ulikuwa na mapenzi ya dhati, mapenzi yasiyokwisha moyoni mwake.

Japokuwa Aisha hakuwa pamoja naye kimwili lakini kiroho, kila siku msichana huyo alikuwa pamoja naye. Hakubandua picha za marehemu mke wake zilizokuwa ukutani, aliziacha ili iwe kumbukumbu katika maisha yake yote.

Na hata kuoa, hakutana tena zaidi ya picha zile zote kuyaandika maneno makubwa yaliyosomeka ENDLESS LOVE akimaanisha MAPENZI YASIYO NA MWISHO.

MWISHO...
 
Sehemu ya 47

Kila mtu alikuwa kimya mahali hapo, Aisha alikuwa ametulia kwenye kiti chake, alitulia tuli huku akimwangalia mume wake ambaye muonekano wake tu ulionyesha ni jinsi gani alikuwa na mawazo tele, hata ule mwili aliokuwa nao kipindi kile cha nyuma, siku ya kwanza aliyoonana nayo hakuwa nao tena.

Razak alibaki kimya, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, hakuamini kama yeye ndiye aliandika barua hiyo ambayo aliiweka kwa ajili ya mke wake aliyebakisha muda mchache kabla ya kufa kutokana na kansa ya utumbo mpana aliyokuwa nayo.

“Aisha mke wangu, kabla ya kukusomea nilichokiandika, jua kwamba ninakupenda sana,” alisema Razak kwa sauti ndogo huku akimwangalia mke wake usoni.
“Nakupenda pia mume wangu....” alisema Aisha kwa sauti ya chini kabisa.

“Nimeandika haya kama maneno yangu ya mwisho-mwisho kwa ajili yako, najua utaumia lakini kitu ambacho ninataka kukuonyeshea ni jinsi gani ninakupenda, na jinsi gani nimepigania uhai wako kwa nguvu zangu zote” alisema Razak na Aisha kutingisha kichwa.

Hapohapo akaanza kuisoma barua hiyo....
Mke wangu Aisha, ninayaandika maneno haya huku moyo wangu ukiwa kwenye maumivu makali, siamini kile ninachokipitia, siamini kama mwisho wetu ungekuwa wenye kuumiza namna hii na wakati mwanzo wetu ulikuwa ni wa furaha tele.

Ninaumia kukuona ulivyo, ninaumia kila ninapoyaona machozi yako.

Hakika umekuwa mwanamke aliyebadilisha maisha yangu, kuniletea furaha ambayo leo inanifanya kuwa nilivyo, ila pamoja na kuniletea furaha hiyo, Mungu hataki niwe nayo, Mungu hakutaka kuniona nikitabasamu kila ninapokuangalia na ndiyo maana leo hii, ninalia, ninahuzunika, ninakosa nguvu, sina faraja, moyo wangu umejeruhiwa, yote hii ni kwa sababu ya maisha yako, yote ni kwa sababu ya ugonjwa wa kansa unaoumwa.

Nilikuja kwako nikiwa na mapenzi ya dhati, nakumbuka siku ya kwanza kukuona kule ufukweni, nilikuwa mtu niliyekata tamaa, nilikuwa mtu niliyetafuta msaada wa maji jangwani, kipindi hicho ndicho nilitoka kutendwa na msichana ambaye kila siku aliniambia ananipenda, aliniambia mimi wa thamani kwake.

Sikuamini kama ningeweza kupenda tena kwani bado moyo wangu ulikuwa na kidonda kibichi kabisa ila baada ya kukuona, moyo wangu ukapata ahueni kabla ya kupona kabisa.

Sikuangalia kama ulikuwa ombaomba mitaani, sikuangalia utajiri wangu, umasikini wako na utajiri wangu uliunganishwa na kitu kimoja kiitwacho MAPENZI.

Siku zikapita, tuliyafurahia mapenzi lakini baada ya usiku mmoja kuumwa na kukupeleka hospitali, hakika ndiyo ulikuwa usiku uliobadilisha kila kitu.

Ukaumwa utumbo, nikaambiwa kwamba una kansa ya utumbo mpana isiyopona.
Niliumia sana, nililia sana siku hiyo kwani ulikuwa kitu muhimu sana kwangu, sikutaka kukubaliana na majibu, hivyo nikaamua kukupeleka nchini India kwa kuamini kwamba inawezekana majibu yangebadilika.

Niliondoka na wazazi wangu kwenda huko, tulipofika, ukafanyiwa vipimo. Kilichoniuma zaidi, kilichonifanya kulia zaidi ni pale tulipoambiwa kwamba una miezi mitatu ya kuishi, yaani mwezi mmoja baada ya ndoa yetu.

Nilichanganyikiwa sana mke wangu, nilimuomba sana Mungu japo afanye muujiza, muujiza utakaoirudisha afya yake kama zamani lakini pamoja na kuomba sana, Mungu akakunyima uponyaji.

Ninakubaliana na kosa nililolifanya la kutokukwambia kwamba una kansa, nilijaribu kukuangalia, hali uliyokuwa nayo, nikahisi kwamba ningesababisha maumivu zaidi au hata kuukatisha uhai wako haraka mno, hivyo nikanyamaza.

Siku uliponiambia una ujauzito wangu, hakika sikufurahi, sikutarajia kuona mtoto wangu akifa siku chache zijazo, niliumia sana lakini bado sikuwa na jinsi, nikaubadilisha uso wangu, nikaweka tabasamu pana japokuwa moyo wangu ulikuwa ukiwaka kwa maumivu makali.
Aisha mke wangu! Nakuahidi kwamba nitaendelea kukupenda.

Kama nilivyokupenda ukiwa mgonjwa, nikakuoa katika hali hiyohiyo uliyokuwa nayo, basi jua kwamba hata kifo kitakapotutenganisha, bado upendo wangu hautoweza kufutika mpaka nitakapoondoka katika dunia hii.

Fedha si kitu zaidi ya uhai, nilitumia kila kiasi kilichohitaji kwa ajili yako, nilitumia fedha kupingana na majibu ya madaktari, nilitaka kuwaonyeshea kwamba fedha ndiyo kila kitu.

Mke wangu Aisha, ninaumia, sina pa kukimbilia tena, nimebaki nikiangalia nione nini kitakachoendelea kwani kama kuishi muda mrefu kungehitaji fedha, ningetumia utajiri wangu wote kwa ajili yako.

Nakupenda mke wangu, na nitakupenda maisha yangu yote.

Razak alipomaliza kusoma maneno hayo, akautuliza uso wake chini, machozi yaliendelea kumtoka, kuumia kwa moyo wake hakukuacha, hakukuwa na kitu kilichomuumiza kama kumuona mke wake akiwa amebakiza siku chache za kuishi.

Wazazi wake wakamsogelea na kuanza kumbembeleza kwa kumpigapiga mgongoni. Hapohapo Razak akasimama na kumfuata mke wake pale alipokaa kwenye kile kiti cha matairi, alipomfikia, akapiga magoti mbele yake.

“Ninakupenda mke wangu...” alisema Razak huku akimwangalia mke wake usoni.

Aisha alikuwa kimya kitini pale, alikuwa akiangalia sehemu moja tu, macho yake yalitulia, hayakuhama kitu kilichowafanya wazazi wake Razak kushtuka kwa kudhani kwamba msichana huyo alikuwa marehemu.

“Aisha...Aisha...Aisha...” aliita mama yake Razak lakini msichana huyo akawa kimya.
Razak akayainua macho yake na kumwangalia mke wake, macho yake yalitulia vilevile kama yalivyokuwa.

Alishtuka, hakuamini alichokuwa akikiona, alijaribu kumuamsha mke wake lakini alitulia tuli, aliposikiliza mapigo ya moyo, yalikuwa yametulia, Aisha alikuwa amefariki dunia kitini hapo.
“Mke wangu...mke wangu...” aliita Razak huku akimtingisha Aisha.

“Mke wangu amka uniangalie, amka uongee nami, mke wangu amka, bado mapema mno kufa, usiniache, amka uniangalie...” alisema Razak, hakuacha kumtingisha Aisha.

Hakukuwa na kilichoendelea, kila kitu walichoambiwa ndicho hicho kilichotokea mahali hapo. Razak alijitahidi sana kumuamsha Aisha lakini mwanamke huyo huyo hakuamka, aliendelea kubaki kimya, kimya milele.

Razak aliumia sana, siku hiyo, ilikuwa ni kelele ndani ya nyumba, Razak aliomboleza lakini machozi yake yote hayo hayakubadilisha kitu chochote kile.

Baba yake akapiga simu katika Hospitali ya St. Peters ambao walifika nyumbani hapo, wakauchukua mwili tayari kwa kuondoka nao. Razak hakutaka kubaki nyumbani, naye akaingia ndani ya gari na kuanza kuelekea hospitalini.

Njiani, muda wote Razak alikuwa akiendelea kumuamsha Aisha huku akilia, bado aliamini kwamba mwanamke huyo angeamka na kuanza kumwangalia tena.

Safari hiyo ikaishia katika hospitali waliyokuwa wakimpeleka, machela ikaletwa, mwili ukapandishwa na kuanza kusukumwa kuelekea ndani. Razak hakutaka kuuachia mwili, bado aliendelea kwenda nao huku akimtaka kufumbua macho na kumwangalia tena.

Alipofikishwa katika chumba husika, Razak akaambiwa asubiri nje kwenye benchi. Akakaa hapo na kuanza kulia.
Hata dakika nyingi hazikupita, wazazi wake wakafika mahali hapo, wakamfuata na kuanza kumbeleleza tena kwani bado alikuwa akilia japokuwa kwa sauti ya chini.

Siku hiyo ilikuwa ni siku yenye maumivu makali, hakuamini kama kweli mke wake aliyempenda alikufa kwa ugonjwa wa kansa uliomsumbua kwa muda wa miezi mitatu tu.

Taarifa zilitoka ndani ya chumba kile zilithibitisha kwamba Aisha alikuwa amekufa hivyo walitakiwa kupanga mazishi na hatimaye msichana huyo aweze kuzikwa.

“Kwa nini Aisha? Kwa nini Mungu aliamua kumchukua kutoka kwangu?” aliuliza Razak huku akilia lakini hakukuwa na mtu aliyekuwa na majibu zaidi ya kumfariji tu.

Taarifa zikaanza kusambazwa kila kona, kila aliyesikia, alihuzunika, hakuamini kama msichana yule alikuwa amefariki mwezi mmoja baada ya kuolewa. Katika mazishi hayo, walifika watu mbalimbali, wafanyabiashara wakubwa, watu maarufu lakini pia watoto wa mitaani, kila mtu alitaka kumzika Aisha.

Saa saba mchana walikuwa makaburini. Hapo ndipo Razak alipolia sana mpaka watu wengine kumuonea huruma kwani hata maneno aliyokuwa akiyazungumza kuhusu mke wake, yalimgusa kila mtu mahali hapo hasa watu walipojua kwamba msichana huyo alifariki huku akiwa na mimba.

“Jamani mumewe anatia huruma...” alisikika mwanaume mmoja.
“Wewe acha tu, kufiwa na mke mwenye mimba, hakika inauma sana,” alisema jamaa mwingine.

Miongoni mwa watu waliokusanyika katika mazishi hayo alikuwa Hashimu, muda wote alikuwa pembeni ya Ahmad na Mohammedi, alikuwa akilia, hakuamini kama msichana aliyekuwa akimpenda tangu zamani alikuwa amefariki dunia.

Kwa kumwangalia, alionekana mtu aliyekuwa mgonjwa kabisa, mwili mwake ulikonda mno, kansa ya koo ilimmaliza na kumfanya kutokuwa na furaha hata kidogo. Mashine yake ya kuzungumzia haikutoka kooni mwake, hiyo ndiyo iliyompa nguvu ya kuzungumza japokuwa kwa shida mno.

Mara baada ya shekhe kuzungumza maneno mengi ya kuhusu maandiko ya vitabu vya dini, akamaliza na hatimaye kaburi la Aisha kufukiwa huku nyuma yake kukiwa na maumivu makubwa.
“Pole sana Razak...” alisema Hashimu, alikuwa akimpa pole Razak.

“Asante sana...”
Huo haukuwa mwisho wa yeye kufika makaburini hapo, mara kwa mara alifika na kukaa pembeni ya kaburi la mke wake. Moyo wake ulikuwa na mapenzi ya dhati, mapenzi yasiyokwisha moyoni mwake.

Japokuwa Aisha hakuwa pamoja naye kimwili lakini kiroho, kila siku msichana huyo alikuwa pamoja naye. Hakubandua picha za marehemu mke wake zilizokuwa ukutani, aliziacha ili iwe kumbukumbu katika maisha yake yote.

Na hata kuoa, hakutana tena zaidi ya picha zile zote kuyaandika maneno makubwa yaliyosomeka ENDLESS LOVE akimaanisha MAPENZI YASIYO NA MWISHO.

MWISHO...
Simulizi nzuri niiyoifuatilia, big up Shunie
 
Sehemu ya 47

Kila mtu alikuwa kimya mahali hapo, Aisha alikuwa ametulia kwenye kiti chake, alitulia tuli huku akimwangalia mume wake ambaye muonekano wake tu ulionyesha ni jinsi gani alikuwa na mawazo tele, hata ule mwili aliokuwa nao kipindi kile cha nyuma, siku ya kwanza aliyoonana nayo hakuwa nao tena.

Razak alibaki kimya, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, hakuamini kama yeye ndiye aliandika barua hiyo ambayo aliiweka kwa ajili ya mke wake aliyebakisha muda mchache kabla ya kufa kutokana na kansa ya utumbo mpana aliyokuwa nayo.

“Aisha mke wangu, kabla ya kukusomea nilichokiandika, jua kwamba ninakupenda sana,” alisema Razak kwa sauti ndogo huku akimwangalia mke wake usoni.
“Nakupenda pia mume wangu....” alisema Aisha kwa sauti ya chini kabisa.

“Nimeandika haya kama maneno yangu ya mwisho-mwisho kwa ajili yako, najua utaumia lakini kitu ambacho ninataka kukuonyeshea ni jinsi gani ninakupenda, na jinsi gani nimepigania uhai wako kwa nguvu zangu zote” alisema Razak na Aisha kutingisha kichwa.

Hapohapo akaanza kuisoma barua hiyo....
Mke wangu Aisha, ninayaandika maneno haya huku moyo wangu ukiwa kwenye maumivu makali, siamini kile ninachokipitia, siamini kama mwisho wetu ungekuwa wenye kuumiza namna hii na wakati mwanzo wetu ulikuwa ni wa furaha tele.

Ninaumia kukuona ulivyo, ninaumia kila ninapoyaona machozi yako.

Hakika umekuwa mwanamke aliyebadilisha maisha yangu, kuniletea furaha ambayo leo inanifanya kuwa nilivyo, ila pamoja na kuniletea furaha hiyo, Mungu hataki niwe nayo, Mungu hakutaka kuniona nikitabasamu kila ninapokuangalia na ndiyo maana leo hii, ninalia, ninahuzunika, ninakosa nguvu, sina faraja, moyo wangu umejeruhiwa, yote hii ni kwa sababu ya maisha yako, yote ni kwa sababu ya ugonjwa wa kansa unaoumwa.

Nilikuja kwako nikiwa na mapenzi ya dhati, nakumbuka siku ya kwanza kukuona kule ufukweni, nilikuwa mtu niliyekata tamaa, nilikuwa mtu niliyetafuta msaada wa maji jangwani, kipindi hicho ndicho nilitoka kutendwa na msichana ambaye kila siku aliniambia ananipenda, aliniambia mimi wa thamani kwake.

Sikuamini kama ningeweza kupenda tena kwani bado moyo wangu ulikuwa na kidonda kibichi kabisa ila baada ya kukuona, moyo wangu ukapata ahueni kabla ya kupona kabisa.

Sikuangalia kama ulikuwa ombaomba mitaani, sikuangalia utajiri wangu, umasikini wako na utajiri wangu uliunganishwa na kitu kimoja kiitwacho MAPENZI.

Siku zikapita, tuliyafurahia mapenzi lakini baada ya usiku mmoja kuumwa na kukupeleka hospitali, hakika ndiyo ulikuwa usiku uliobadilisha kila kitu.

Ukaumwa utumbo, nikaambiwa kwamba una kansa ya utumbo mpana isiyopona.
Niliumia sana, nililia sana siku hiyo kwani ulikuwa kitu muhimu sana kwangu, sikutaka kukubaliana na majibu, hivyo nikaamua kukupeleka nchini India kwa kuamini kwamba inawezekana majibu yangebadilika.

Niliondoka na wazazi wangu kwenda huko, tulipofika, ukafanyiwa vipimo. Kilichoniuma zaidi, kilichonifanya kulia zaidi ni pale tulipoambiwa kwamba una miezi mitatu ya kuishi, yaani mwezi mmoja baada ya ndoa yetu.

Nilichanganyikiwa sana mke wangu, nilimuomba sana Mungu japo afanye muujiza, muujiza utakaoirudisha afya yake kama zamani lakini pamoja na kuomba sana, Mungu akakunyima uponyaji.

Ninakubaliana na kosa nililolifanya la kutokukwambia kwamba una kansa, nilijaribu kukuangalia, hali uliyokuwa nayo, nikahisi kwamba ningesababisha maumivu zaidi au hata kuukatisha uhai wako haraka mno, hivyo nikanyamaza.

Siku uliponiambia una ujauzito wangu, hakika sikufurahi, sikutarajia kuona mtoto wangu akifa siku chache zijazo, niliumia sana lakini bado sikuwa na jinsi, nikaubadilisha uso wangu, nikaweka tabasamu pana japokuwa moyo wangu ulikuwa ukiwaka kwa maumivu makali.
Aisha mke wangu! Nakuahidi kwamba nitaendelea kukupenda.

Kama nilivyokupenda ukiwa mgonjwa, nikakuoa katika hali hiyohiyo uliyokuwa nayo, basi jua kwamba hata kifo kitakapotutenganisha, bado upendo wangu hautoweza kufutika mpaka nitakapoondoka katika dunia hii.

Fedha si kitu zaidi ya uhai, nilitumia kila kiasi kilichohitaji kwa ajili yako, nilitumia fedha kupingana na majibu ya madaktari, nilitaka kuwaonyeshea kwamba fedha ndiyo kila kitu.

Mke wangu Aisha, ninaumia, sina pa kukimbilia tena, nimebaki nikiangalia nione nini kitakachoendelea kwani kama kuishi muda mrefu kungehitaji fedha, ningetumia utajiri wangu wote kwa ajili yako.

Nakupenda mke wangu, na nitakupenda maisha yangu yote.

Razak alipomaliza kusoma maneno hayo, akautuliza uso wake chini, machozi yaliendelea kumtoka, kuumia kwa moyo wake hakukuacha, hakukuwa na kitu kilichomuumiza kama kumuona mke wake akiwa amebakiza siku chache za kuishi.

Wazazi wake wakamsogelea na kuanza kumbembeleza kwa kumpigapiga mgongoni. Hapohapo Razak akasimama na kumfuata mke wake pale alipokaa kwenye kile kiti cha matairi, alipomfikia, akapiga magoti mbele yake.

“Ninakupenda mke wangu...” alisema Razak huku akimwangalia mke wake usoni.

Aisha alikuwa kimya kitini pale, alikuwa akiangalia sehemu moja tu, macho yake yalitulia, hayakuhama kitu kilichowafanya wazazi wake Razak kushtuka kwa kudhani kwamba msichana huyo alikuwa marehemu.

“Aisha...Aisha...Aisha...” aliita mama yake Razak lakini msichana huyo akawa kimya.
Razak akayainua macho yake na kumwangalia mke wake, macho yake yalitulia vilevile kama yalivyokuwa.

Alishtuka, hakuamini alichokuwa akikiona, alijaribu kumuamsha mke wake lakini alitulia tuli, aliposikiliza mapigo ya moyo, yalikuwa yametulia, Aisha alikuwa amefariki dunia kitini hapo.
“Mke wangu...mke wangu...” aliita Razak huku akimtingisha Aisha.

“Mke wangu amka uniangalie, amka uongee nami, mke wangu amka, bado mapema mno kufa, usiniache, amka uniangalie...” alisema Razak, hakuacha kumtingisha Aisha.

Hakukuwa na kilichoendelea, kila kitu walichoambiwa ndicho hicho kilichotokea mahali hapo. Razak alijitahidi sana kumuamsha Aisha lakini mwanamke huyo huyo hakuamka, aliendelea kubaki kimya, kimya milele.

Razak aliumia sana, siku hiyo, ilikuwa ni kelele ndani ya nyumba, Razak aliomboleza lakini machozi yake yote hayo hayakubadilisha kitu chochote kile.

Baba yake akapiga simu katika Hospitali ya St. Peters ambao walifika nyumbani hapo, wakauchukua mwili tayari kwa kuondoka nao. Razak hakutaka kubaki nyumbani, naye akaingia ndani ya gari na kuanza kuelekea hospitalini.

Njiani, muda wote Razak alikuwa akiendelea kumuamsha Aisha huku akilia, bado aliamini kwamba mwanamke huyo angeamka na kuanza kumwangalia tena.

Safari hiyo ikaishia katika hospitali waliyokuwa wakimpeleka, machela ikaletwa, mwili ukapandishwa na kuanza kusukumwa kuelekea ndani. Razak hakutaka kuuachia mwili, bado aliendelea kwenda nao huku akimtaka kufumbua macho na kumwangalia tena.

Alipofikishwa katika chumba husika, Razak akaambiwa asubiri nje kwenye benchi. Akakaa hapo na kuanza kulia.
Hata dakika nyingi hazikupita, wazazi wake wakafika mahali hapo, wakamfuata na kuanza kumbeleleza tena kwani bado alikuwa akilia japokuwa kwa sauti ya chini.

Siku hiyo ilikuwa ni siku yenye maumivu makali, hakuamini kama kweli mke wake aliyempenda alikufa kwa ugonjwa wa kansa uliomsumbua kwa muda wa miezi mitatu tu.

Taarifa zilitoka ndani ya chumba kile zilithibitisha kwamba Aisha alikuwa amekufa hivyo walitakiwa kupanga mazishi na hatimaye msichana huyo aweze kuzikwa.

“Kwa nini Aisha? Kwa nini Mungu aliamua kumchukua kutoka kwangu?” aliuliza Razak huku akilia lakini hakukuwa na mtu aliyekuwa na majibu zaidi ya kumfariji tu.

Taarifa zikaanza kusambazwa kila kona, kila aliyesikia, alihuzunika, hakuamini kama msichana yule alikuwa amefariki mwezi mmoja baada ya kuolewa. Katika mazishi hayo, walifika watu mbalimbali, wafanyabiashara wakubwa, watu maarufu lakini pia watoto wa mitaani, kila mtu alitaka kumzika Aisha.

Saa saba mchana walikuwa makaburini. Hapo ndipo Razak alipolia sana mpaka watu wengine kumuonea huruma kwani hata maneno aliyokuwa akiyazungumza kuhusu mke wake, yalimgusa kila mtu mahali hapo hasa watu walipojua kwamba msichana huyo alifariki huku akiwa na mimba.

“Jamani mumewe anatia huruma...” alisikika mwanaume mmoja.
“Wewe acha tu, kufiwa na mke mwenye mimba, hakika inauma sana,” alisema jamaa mwingine.

Miongoni mwa watu waliokusanyika katika mazishi hayo alikuwa Hashimu, muda wote alikuwa pembeni ya Ahmad na Mohammedi, alikuwa akilia, hakuamini kama msichana aliyekuwa akimpenda tangu zamani alikuwa amefariki dunia.

Kwa kumwangalia, alionekana mtu aliyekuwa mgonjwa kabisa, mwili mwake ulikonda mno, kansa ya koo ilimmaliza na kumfanya kutokuwa na furaha hata kidogo. Mashine yake ya kuzungumzia haikutoka kooni mwake, hiyo ndiyo iliyompa nguvu ya kuzungumza japokuwa kwa shida mno.

Mara baada ya shekhe kuzungumza maneno mengi ya kuhusu maandiko ya vitabu vya dini, akamaliza na hatimaye kaburi la Aisha kufukiwa huku nyuma yake kukiwa na maumivu makubwa.
“Pole sana Razak...” alisema Hashimu, alikuwa akimpa pole Razak.

“Asante sana...”
Huo haukuwa mwisho wa yeye kufika makaburini hapo, mara kwa mara alifika na kukaa pembeni ya kaburi la mke wake. Moyo wake ulikuwa na mapenzi ya dhati, mapenzi yasiyokwisha moyoni mwake.

Japokuwa Aisha hakuwa pamoja naye kimwili lakini kiroho, kila siku msichana huyo alikuwa pamoja naye. Hakubandua picha za marehemu mke wake zilizokuwa ukutani, aliziacha ili iwe kumbukumbu katika maisha yake yote.

Na hata kuoa, hakutana tena zaidi ya picha zile zote kuyaandika maneno makubwa yaliyosomeka ENDLESS LOVE akimaanisha MAPENZI YASIYO NA MWISHO.

MWISHO...
Thanks shunie
 
Sehemu ya 47

Kila mtu alikuwa kimya mahali hapo, Aisha alikuwa ametulia kwenye kiti chake, alitulia tuli huku akimwangalia mume wake ambaye muonekano wake tu ulionyesha ni jinsi gani alikuwa na mawazo tele, hata ule mwili aliokuwa nao kipindi kile cha nyuma, siku ya kwanza aliyoonana nayo hakuwa nao tena.

Razak alibaki kimya, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, hakuamini kama yeye ndiye aliandika barua hiyo ambayo aliiweka kwa ajili ya mke wake aliyebakisha muda mchache kabla ya kufa kutokana na kansa ya utumbo mpana aliyokuwa nayo.

“Aisha mke wangu, kabla ya kukusomea nilichokiandika, jua kwamba ninakupenda sana,” alisema Razak kwa sauti ndogo huku akimwangalia mke wake usoni.
“Nakupenda pia mume wangu....” alisema Aisha kwa sauti ya chini kabisa.

“Nimeandika haya kama maneno yangu ya mwisho-mwisho kwa ajili yako, najua utaumia lakini kitu ambacho ninataka kukuonyeshea ni jinsi gani ninakupenda, na jinsi gani nimepigania uhai wako kwa nguvu zangu zote” alisema Razak na Aisha kutingisha kichwa.

Hapohapo akaanza kuisoma barua hiyo....
Mke wangu Aisha, ninayaandika maneno haya huku moyo wangu ukiwa kwenye maumivu makali, siamini kile ninachokipitia, siamini kama mwisho wetu ungekuwa wenye kuumiza namna hii na wakati mwanzo wetu ulikuwa ni wa furaha tele.

Ninaumia kukuona ulivyo, ninaumia kila ninapoyaona machozi yako.

Hakika umekuwa mwanamke aliyebadilisha maisha yangu, kuniletea furaha ambayo leo inanifanya kuwa nilivyo, ila pamoja na kuniletea furaha hiyo, Mungu hataki niwe nayo, Mungu hakutaka kuniona nikitabasamu kila ninapokuangalia na ndiyo maana leo hii, ninalia, ninahuzunika, ninakosa nguvu, sina faraja, moyo wangu umejeruhiwa, yote hii ni kwa sababu ya maisha yako, yote ni kwa sababu ya ugonjwa wa kansa unaoumwa.

Nilikuja kwako nikiwa na mapenzi ya dhati, nakumbuka siku ya kwanza kukuona kule ufukweni, nilikuwa mtu niliyekata tamaa, nilikuwa mtu niliyetafuta msaada wa maji jangwani, kipindi hicho ndicho nilitoka kutendwa na msichana ambaye kila siku aliniambia ananipenda, aliniambia mimi wa thamani kwake.

Sikuamini kama ningeweza kupenda tena kwani bado moyo wangu ulikuwa na kidonda kibichi kabisa ila baada ya kukuona, moyo wangu ukapata ahueni kabla ya kupona kabisa.

Sikuangalia kama ulikuwa ombaomba mitaani, sikuangalia utajiri wangu, umasikini wako na utajiri wangu uliunganishwa na kitu kimoja kiitwacho MAPENZI.

Siku zikapita, tuliyafurahia mapenzi lakini baada ya usiku mmoja kuumwa na kukupeleka hospitali, hakika ndiyo ulikuwa usiku uliobadilisha kila kitu.

Ukaumwa utumbo, nikaambiwa kwamba una kansa ya utumbo mpana isiyopona.
Niliumia sana, nililia sana siku hiyo kwani ulikuwa kitu muhimu sana kwangu, sikutaka kukubaliana na majibu, hivyo nikaamua kukupeleka nchini India kwa kuamini kwamba inawezekana majibu yangebadilika.

Niliondoka na wazazi wangu kwenda huko, tulipofika, ukafanyiwa vipimo. Kilichoniuma zaidi, kilichonifanya kulia zaidi ni pale tulipoambiwa kwamba una miezi mitatu ya kuishi, yaani mwezi mmoja baada ya ndoa yetu.

Nilichanganyikiwa sana mke wangu, nilimuomba sana Mungu japo afanye muujiza, muujiza utakaoirudisha afya yake kama zamani lakini pamoja na kuomba sana, Mungu akakunyima uponyaji.

Ninakubaliana na kosa nililolifanya la kutokukwambia kwamba una kansa, nilijaribu kukuangalia, hali uliyokuwa nayo, nikahisi kwamba ningesababisha maumivu zaidi au hata kuukatisha uhai wako haraka mno, hivyo nikanyamaza.

Siku uliponiambia una ujauzito wangu, hakika sikufurahi, sikutarajia kuona mtoto wangu akifa siku chache zijazo, niliumia sana lakini bado sikuwa na jinsi, nikaubadilisha uso wangu, nikaweka tabasamu pana japokuwa moyo wangu ulikuwa ukiwaka kwa maumivu makali.
Aisha mke wangu! Nakuahidi kwamba nitaendelea kukupenda.

Kama nilivyokupenda ukiwa mgonjwa, nikakuoa katika hali hiyohiyo uliyokuwa nayo, basi jua kwamba hata kifo kitakapotutenganisha, bado upendo wangu hautoweza kufutika mpaka nitakapoondoka katika dunia hii.

Fedha si kitu zaidi ya uhai, nilitumia kila kiasi kilichohitaji kwa ajili yako, nilitumia fedha kupingana na majibu ya madaktari, nilitaka kuwaonyeshea kwamba fedha ndiyo kila kitu.

Mke wangu Aisha, ninaumia, sina pa kukimbilia tena, nimebaki nikiangalia nione nini kitakachoendelea kwani kama kuishi muda mrefu kungehitaji fedha, ningetumia utajiri wangu wote kwa ajili yako.

Nakupenda mke wangu, na nitakupenda maisha yangu yote.

Razak alipomaliza kusoma maneno hayo, akautuliza uso wake chini, machozi yaliendelea kumtoka, kuumia kwa moyo wake hakukuacha, hakukuwa na kitu kilichomuumiza kama kumuona mke wake akiwa amebakiza siku chache za kuishi.

Wazazi wake wakamsogelea na kuanza kumbembeleza kwa kumpigapiga mgongoni. Hapohapo Razak akasimama na kumfuata mke wake pale alipokaa kwenye kile kiti cha matairi, alipomfikia, akapiga magoti mbele yake.

“Ninakupenda mke wangu...” alisema Razak huku akimwangalia mke wake usoni.

Aisha alikuwa kimya kitini pale, alikuwa akiangalia sehemu moja tu, macho yake yalitulia, hayakuhama kitu kilichowafanya wazazi wake Razak kushtuka kwa kudhani kwamba msichana huyo alikuwa marehemu.

“Aisha...Aisha...Aisha...” aliita mama yake Razak lakini msichana huyo akawa kimya.
Razak akayainua macho yake na kumwangalia mke wake, macho yake yalitulia vilevile kama yalivyokuwa.

Alishtuka, hakuamini alichokuwa akikiona, alijaribu kumuamsha mke wake lakini alitulia tuli, aliposikiliza mapigo ya moyo, yalikuwa yametulia, Aisha alikuwa amefariki dunia kitini hapo.
“Mke wangu...mke wangu...” aliita Razak huku akimtingisha Aisha.

“Mke wangu amka uniangalie, amka uongee nami, mke wangu amka, bado mapema mno kufa, usiniache, amka uniangalie...” alisema Razak, hakuacha kumtingisha Aisha.

Hakukuwa na kilichoendelea, kila kitu walichoambiwa ndicho hicho kilichotokea mahali hapo. Razak alijitahidi sana kumuamsha Aisha lakini mwanamke huyo huyo hakuamka, aliendelea kubaki kimya, kimya milele.

Razak aliumia sana, siku hiyo, ilikuwa ni kelele ndani ya nyumba, Razak aliomboleza lakini machozi yake yote hayo hayakubadilisha kitu chochote kile.

Baba yake akapiga simu katika Hospitali ya St. Peters ambao walifika nyumbani hapo, wakauchukua mwili tayari kwa kuondoka nao. Razak hakutaka kubaki nyumbani, naye akaingia ndani ya gari na kuanza kuelekea hospitalini.

Njiani, muda wote Razak alikuwa akiendelea kumuamsha Aisha huku akilia, bado aliamini kwamba mwanamke huyo angeamka na kuanza kumwangalia tena.

Safari hiyo ikaishia katika hospitali waliyokuwa wakimpeleka, machela ikaletwa, mwili ukapandishwa na kuanza kusukumwa kuelekea ndani. Razak hakutaka kuuachia mwili, bado aliendelea kwenda nao huku akimtaka kufumbua macho na kumwangalia tena.

Alipofikishwa katika chumba husika, Razak akaambiwa asubiri nje kwenye benchi. Akakaa hapo na kuanza kulia.
Hata dakika nyingi hazikupita, wazazi wake wakafika mahali hapo, wakamfuata na kuanza kumbeleleza tena kwani bado alikuwa akilia japokuwa kwa sauti ya chini.

Siku hiyo ilikuwa ni siku yenye maumivu makali, hakuamini kama kweli mke wake aliyempenda alikufa kwa ugonjwa wa kansa uliomsumbua kwa muda wa miezi mitatu tu.

Taarifa zilitoka ndani ya chumba kile zilithibitisha kwamba Aisha alikuwa amekufa hivyo walitakiwa kupanga mazishi na hatimaye msichana huyo aweze kuzikwa.

“Kwa nini Aisha? Kwa nini Mungu aliamua kumchukua kutoka kwangu?” aliuliza Razak huku akilia lakini hakukuwa na mtu aliyekuwa na majibu zaidi ya kumfariji tu.

Taarifa zikaanza kusambazwa kila kona, kila aliyesikia, alihuzunika, hakuamini kama msichana yule alikuwa amefariki mwezi mmoja baada ya kuolewa. Katika mazishi hayo, walifika watu mbalimbali, wafanyabiashara wakubwa, watu maarufu lakini pia watoto wa mitaani, kila mtu alitaka kumzika Aisha.

Saa saba mchana walikuwa makaburini. Hapo ndipo Razak alipolia sana mpaka watu wengine kumuonea huruma kwani hata maneno aliyokuwa akiyazungumza kuhusu mke wake, yalimgusa kila mtu mahali hapo hasa watu walipojua kwamba msichana huyo alifariki huku akiwa na mimba.

“Jamani mumewe anatia huruma...” alisikika mwanaume mmoja.
“Wewe acha tu, kufiwa na mke mwenye mimba, hakika inauma sana,” alisema jamaa mwingine.

Miongoni mwa watu waliokusanyika katika mazishi hayo alikuwa Hashimu, muda wote alikuwa pembeni ya Ahmad na Mohammedi, alikuwa akilia, hakuamini kama msichana aliyekuwa akimpenda tangu zamani alikuwa amefariki dunia.

Kwa kumwangalia, alionekana mtu aliyekuwa mgonjwa kabisa, mwili mwake ulikonda mno, kansa ya koo ilimmaliza na kumfanya kutokuwa na furaha hata kidogo. Mashine yake ya kuzungumzia haikutoka kooni mwake, hiyo ndiyo iliyompa nguvu ya kuzungumza japokuwa kwa shida mno.

Mara baada ya shekhe kuzungumza maneno mengi ya kuhusu maandiko ya vitabu vya dini, akamaliza na hatimaye kaburi la Aisha kufukiwa huku nyuma yake kukiwa na maumivu makubwa.
“Pole sana Razak...” alisema Hashimu, alikuwa akimpa pole Razak.

“Asante sana...”
Huo haukuwa mwisho wa yeye kufika makaburini hapo, mara kwa mara alifika na kukaa pembeni ya kaburi la mke wake. Moyo wake ulikuwa na mapenzi ya dhati, mapenzi yasiyokwisha moyoni mwake.

Japokuwa Aisha hakuwa pamoja naye kimwili lakini kiroho, kila siku msichana huyo alikuwa pamoja naye. Hakubandua picha za marehemu mke wake zilizokuwa ukutani, aliziacha ili iwe kumbukumbu katika maisha yake yote.

Na hata kuoa, hakutana tena zaidi ya picha zile zote kuyaandika maneno makubwa yaliyosomeka ENDLESS LOVE akimaanisha MAPENZI YASIYO NA MWISHO.

MWISHO...

Inafurahisha na kusikitisha sana...

Siku zote kizuri hakidumu...

Chapter Closed...


Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom