Sehemu ya 26
Nusrat Twaha: Tulikutana katika Ukumbi wa Maisha Basement, akatokea kunipenda sana lakini hakujua ni kwa namna gani angenipata, hivyo akamtumia rafiki yangu wa kike, Minah ambaye naye nilimkosakosa.
Minah akanifuata na kuniambia kwamba nilikuwa napendwa, nikakubali, nikawa na Nusrat, tukafanya mengi, akapagawa nami ila ndiyo hivyo, muda wangu wa mwezi mmoja umetimia, hivyo nitammwaga kama wengine.
Sabrina Seif: Nilipomuona kwa mara ya kwanza, nilimpenda kidogo, nilimtaka niwe naye katika miezi yangu miwili ya kuwa hapa Tanzania kabla sijarudi Dubai. Sikujua ningempata vipi hivyo nikamtumia Minah, akanirekebishia na hivyo nipo naye.
Kama kumpenda, nampenda ila kwa asilimia tano tu. Nimemchezea kama wengine, nimemfanya ninachotaka kumfanya na sasa hivi nimemchoka, kama ilivyokuwa kwa wasichana wengine, hata naye huyu Sabrina nitamwaga japokuwa anapenda sana ndoa, kila nikikaa naye, anazungumzia ndoa tu.
Kashanifumania na Nusrat, nimemzugazuga tu, hivyo nammwaga kama kawaida kisha kurudi zangu Dubai. Kwa kifupi, siwezi kupenda, yule Shamsia ndiye aliyeharibu kila kitu. Baada ya kummwaga huyu, mwingine atakuja tu. Nafanya haya yote kama kisasi cha kuumizwa zamani.
Je nini kitaendelea.....