XAVERY EMMANUEL LUOGA
“PENDO HURU’
0672493994
EPISODE 19
Kwa upande wa Saleh na Zawadi wao walikuwa hawajui wanaenda wapi. Walizunguka tu msitu mzima pasi na sehemu ya makazi ya watu kutokea.
Walizunguka sana. Na hatimaye Zawadi kukataa pumzi. Akakaa chini akisubili mapigo ya moyo yakae sawa. Alichoka Zawadi. Presha ikapanda kwa Saleh. Hakuna na la kufanya. Akaanza kubuni mbinu za kuwachelewesha wanaowatafuta.
Alimvua Zawadi mkufu wake na kuugawanya. Mwingine akautupia upande mwingine na mwingine upande mwingine. Akamnyanyua Zawadi na kusogea nae kando kidogo. Bado wakina Ibo walikuwa wakiotea tu sehemu ambayo wawili hao wamepita. miti na vichaka viliwachanganya.
Saleh akaanza kuandaa zana za kivita. Akatafuta miti iliyo kama fimbo nyingi akazingaunga tu na kamba za miti mikubwa. Akatengezeza mitego kazaa kwa kuzifunga kwenye nyasi na nyingine jii ya miti. Saleh alikuwa vizuri katika uwindaji.
Baada yapo akasogea mbele na Zawadi ambaye japo alikuwa anakimbia lakini sio mkimbio ule wa matumaini. Zawadi alichoka kukimbizwa bila sababu. Akawa anakimbia kizembe zembe. Uliitwa mwendo wa kike kike.
Ibo na askari wake hatimaye wakaingia kingi, hiyo yote juu ya kufuata mabaki ys mkufu wa Zawadi uliowekwa mtego kama Chambo. Watatu kati yao wakavamia mtego na kuwarusha mbali. Mungu mkubwa!, hawakufa. Wakasimama kwa muda kutafakari jambo hilo.
“Alaah!. Angalieni chini!, chini chini nimesema” aliwaambia askari wake ambao bado hawajapata dhahama ya mtego huo.
Wakarudi kuwatazama wenzao watatu walioathirika. Wakawaganga japo kwa shida lakini wakawa sawa ila walitembe kwa manati. Ikawa hauweni kwa kina Saleh kuchanja mbuga.
“Wawili bakini na hawa, piteni kwa upande huu, mimi na wewe huku!, huku nimesema” Ibo alikuwa ni mtu wa amri tu.
Aliamrisha wagonjwa wale wabaki na wengine wawili wakiangalia afya yao. Wengne wakagawanyishwa eneo lingine na Ibo akaondoka na mmoja na kumfikia jumla ya askari wote kumi na moja.
Saleh bado alikuwa na Zawadi wake mikononi, walitembea sana. baada ya kuona wapo umbali mrefu toka walipowatelekeza waasi wao.
Ajabu!! Mvua ilikuwa imeshakata. hakukuwa hata na dalili ya Mawingu. Jua kali Lilikuwa kando yao. Kwa majira ya kizee zee ilikuwa ni saa nne na unusu ya asubuhi. Bado walikuwa ndani ya msitu na kutokuja wapi wanaenda. Msitu ulikuwa ni mkubwa mno.
Wengine watano walipatwa na dhahama ya mtego wa pili wa saleh!, watatu kati yao walinusurika na wawili kupoteza maisha. Walifakamia kamba iliyotegwa kwenye nyasi kwa ustadi mkubwa iliyobeba gogo nyepesi kwa juu. Kwa mstuko walirushwa na gogo hilo hadi kwenye shimo lilipo karibu na mtego ilipo. Walioanguka vibaya walipoteza maisha hapo hapo.
Walikuwa waili tu na kubaki watatu, watano hawa ni wale waliopita upande tofauti na Ibo na wale wengne ambao wawili majeruhi. Msafara ukawa mzito kwelikweli. Ibo alijidai kukwepa kila kishawishi bado alikuwa imara sasa.
Mzunguko wa msitu ukawachanganya Saleh na Zawadi walikutana na nyjia nyingi zilizotawanyika bila kuonyesha zinaenda wapi.
Wakachagua njia ya kulia kuelekea mbele kupata msaada. Walipita moja kwa moja kwa mwendo wa taratibu bila shaka na hofu. Zawadi alitembea huku akijigonga gonga mabegani mwa Saleh kimahaba. Alikuwa ni full of love. Alifurahi sana Zawadi. Nafsi yake ilipata pa kumfikia. Aliona yupo ndani ya mjengo wa mahaba. Wenye kujengwa na tabasamu alipendae. Jingo lenye macho ya dhahabu na mguu wa bia. Jingo lililopo mbinguni. Wakakanyaga mafuta taratibu kuelekea mbele.
“Mamaa!” Zawadi aligumia.
“Nini!!” aliruka Saleh.
“Mdudu!” alishikwa na woga Zawadi huku mikono yake ikimshika Saleh kwa kumvuta. Aliona kinyonga.
“Sasa! huyu mdudu humjui Zai!”
“Hahahahaha!, amenistua tu!” alicheka Zawadi. Aliona sasa ni muda wa matani. Wala hakuwaza juu ya msako ambao unaendelea juu yao.
Wakacheka kwa ushilikiano wa aina yake. Wakasonga mbele.
“Tititititiiti!” kishindo kilisikia. Zawadi na Saleh walikuwa mbali kimaongezi, hawakusikia kitu.
“Ngruuuuuh!” mngurumo ukasikika nyuma yao. Hapa wote walisikia. Ukawapa nafasi ya kugeuka na kutazama mgurumo huo wa kuogofya.
“Simba!” nafsi ya Zawadi ikahema kwa nguvu. Mkojo ukawa langoni kukaribia kutoka.
Akaanza mbio Zawadi lakini alishikwa na Saleh na kusimamishwa. Alimuwai kabla hajaonekana anapiga hatua na kumvutia mnyama huyo wa mwituni.
Saleh akambana Zawadi kifuani kifuani kwake, asipige kelele. Wakatulia tuli kimwili lakini kiroho Zawadi hakuwa pale tena. Alikuwa anasali zile sara za mwishomwisho za kuzaliwa marehemu. Kimya kikatanda.
Mwenye macho haambiwi tazama. Simba huyo akapita kando yao bila kufanya chochote kile. Aliranda randa kwa mbele na mwisho kusimama. Alisimama Simba.
“Ngruuuuuuh!” akaunguruma tena kwa hasira. Saleh akashuhudia mtetemeko wa Zawadi ambao uliupita ule wa Simba. Zawadi alikuwa anaogopa sana.
Jambo la kushangaza simba huyo mwenye umbo lililowapita Zawadi na Saleh zaidi y mara mbili alipita tena alipo Saleh na Zawadi. Hakuwatazama katu.
Akatimua zake mbio na kurudi nyuma alikotoka mwanzo. Nadhani aliona wenye haki wa kuangamizwa msituni humo, tena wengi kuliko hao wawili.
Akawaacha Saleh na Zawadi wasonge mbele. Walitembea kwa hofu na mashaka huku macho yao yakihakikisha ujio mpya wa simba huyo kama atarudi tena au la. Lakini hakuna! hakurudi simba huyo. Na hawakumuona tena.
Kutembea kwao kilikomea katika kichochoro ambacho kilionyesha kinaelekea mabondeni. Wakasonga huko japo kutafuta lolote. Njaa iliwasokota mno. Wakaenda mbele.
Njia hiyo iliwapeleka hadi katika bonde moja kubwa lililotenganisha upande mmoja na mwingine. Pande hizo mbili zilitenganishwa na mto huo.
Wakapata nafuu ya kuyaona maji. Wakafakamia. Hakika mungu alikuwa upande wao. Waliyaona mafanikio. zile pumzi zilizokua zinakimbia mkukumkuku, sasa zilisimama na kutilia.
“Saleh!, tukifika tutaishi pamoja!” ilikuwa ni ndoto ya Zawadi ambaye bado alikuwa anatoa kuwa ni rahisi sana kuvuka katika msitu huo. Saleh alimwangalia tu na kutabasamu.
“Usijali Zawadi, nakupenda sana!” Saleh akarudisha wema wa maneno kwa Zawadi. Hawakuacha wote kutabasamu. Walitabasamu.
Baada ya kufakamia maji ya mto huo wakakaa kwanza chini kupanga njia gani wanapita. Hakukuwa na njia itakayo wawezesha kupita upande wa pili.
“Zawadi, ivi unajua kuwa tunatakiwa tupite kulekule tulipotoka?” aliuliza Saleh kana kwamba Zawadi atakuwa na jibu la tofauti.
“Ah! Eeh!, kulee kwenye pachapacha nyingi?” aliuliza Zawadi.
“Ndio kipenzi. Lakini…!” aligomea katikati Saleh.
“Ivi kwanini Baba anafanya hivi Saleh!” Zawadi alipotezea lakini ya Saleh na kumjenga hoja mpya.
“Malindi imekuwa kinyume na nilivyofikilia. Sina damu kabisa na Baba yangu. Yaani sijapata kumpenda baba huyu toka enzi za ujana wangu. Ananilinda tu!, sina uhuru!, Saleh!!” aliongea Zawadi na mwisho alijikuta anaongea peke yake. Saleh alikuwa katika mawazo mazito. Hakuwa pale kabisa. Aliwaza Ushindi mpya! ushindi wa kuishinda Malindi....
..............

HAYAAA!, Bado tupo Msituni Malindi. Saleh na Zawadi wameshinda mbio HURU , na sasa wapo katika fikra ya Mapinduzi ya kweli. Tukumbuke Sadiki naye alikus njiani kuelekea Msituni. Kipi kinaendelea..?
ITAENDELEA........
Starxav