Simulizi: Pendo Huru

Simulizi: Pendo Huru

XAVERY LUOGA
“PENDO HURU’
0672493994

EPISODE 18
Walisogea na miale yao ya moto hadi kando na walipo Saleh na Zawadi. Kizuri hadi wakati huo hawakuonekana.

Mioyo yao ilikuwa inadunda mno utadhani ng’ombe ambaye anachinjwa. Walikuwa ni wasumbufu wa roho. Walihemeana wao kwa wao bila kuruhusu pumzi zao kufikiwa na watu waliopo karibu yao.

Jamani kuna watu wanahisia!! Kha!!. Ibo alipofika karibu na kichaka hicho kilichofunikwa na miti midogo na nyasi ngumu, alisimamisha msafara na kutoa hotuba fupi. Hotuba ambayo iliambatana na kusitishwa kwa msafara huo hadi kesho yake asubuhi.

“Vijana wangu!, sasa tupumzike hapa hadi kesho asubuhi. Hawapo mbali hawa washenzi!, kinachonipa kiburi ni huyu Malaya!. Hawezi kabisa kukimbia, mwanamke ni mwanamke tu. Kwahiyo hata kama wakimbie vipi kuna mawili tu. Niwashike au washikwe na wanyama humu wafe wote!, hawana umuhimu kabisa..” Ibo aliishiwa kauli kabisa, maneno yake japo yalikuwa ya ujasili lakini yaliashilia kukataa tamaa. hakuja akitafutacho kipo karibu kumtazama.

Msafara ikaweka kambi mahari hapo. Vijana wawili kutoka nyuma ambao walishikilia mzoga wa mnyama walikuaja mbele ya kiongozi wao na kuanza kuandaa chakula.

Waliweka kabisa kitoweo kwa jinsi shughuli ya kusaka binadamu ilivyonzito. Wakachinja, wakachuna!, wakala na kisaza!!,.

wakapeana majukumu ya kulinda kwa masaa ili kuwa huru na uhai wao. Kiongozi akatangaza kujipendelea.

“Ndaku na Poye!, Mnatosha kabisa. Mtalinda hadi asubuhi”. Akatoa amri Ibo. Hakuna aliyepinga. Aliabudiwa kama Mfalme ajaye.

“Tunatokaje hapa mpenzi!” ilikuwa ni kauli ya Zawadi kuelekea kwa Saleh ambaye macho yake yalikuwa bize kuangalia kinachotendeka na watu hao.

“Mhhh!, hapa tuwe kimya tu!, tuwe wavumulivu Zawadi”. Aliongea Saleh ambaye hakuwa na hata plani kichwani kwake.

Naaam! Dakika chache tu palinuka moshi sehemu ile, tayari ibo na wenzake walishapata msosi. Walikula na kuacha nyama ikiteketea katika mkungu kwenye moto. Walilala karibia wote lakini sio hawa askari wawili walioambiwa walinde usiku kucha. Walikuwa imara sana kwa kipindi kirefu. Walisimama tu. Walikuwa kama masanamu kwa kipindi kirefu.

“Kwaa! Kwaa! Kwaaah!” hatua za askari mmoja wapo zilisogea hadi mahali mwenzake alipo, akamuuma sikio na mwingine kutikisa kichwa kuashilia kwamba wamekubaliana.

Aliyeenda kwa mwingine akaongoza njia kwenda walipo kina Zawadi na Saleh. Alipofika kando akashusha kaniki yake na kumimina kojo la nguvu. Kojo lililonuka harufu ya nyama iliyoozea tumboni.

Baada hapo akapandisha kaniki yake na kurudi alipokuwa mwanzo. Miguu akanyoosha kusini na kichwa magharibi. Akalala askari yule na kumwacha mmoja ambaye yaonekana walikubaliana kuwa wanalinda kwa zamu. Itakapofika mda wa kulala yeye basi atamwamusha mwenzake. Walikubaliana hivyo.

Ikapita punde kirefu kimya kikatawala. Hakuna dalili za kupumua kutoka kwa askari aliyeachiwa zamu. Alipokaa hakutikisika. Alikuwa kimya tu.

“Subiri hapo usitoke!” Saleh alimwambia Zawadi asitoke pale alipo na kuelekea pale walipo wale wakina Ibo.

Akamkagua yule askari ambaye alilala wakati macho yapo wazi. Aliachama tu mdomo wazi macho wazi, alilala kishujaa sana.

Saleh akanyata hadi pale palipo na zile nyama kwenye ule moto akakongowa moja ya nyama yenye unafuu pale, nyingine zilikuwa zinaelekea kuungaua moja kwa moja. Akajihakikishia usalama wa sehemu anayorudi alipofika karibu akaita kwa sauti ya upole.
“Zai, Zawadi!. Pita huku tukimbie!, Usipige kelele!” alimwita Zawadi huku akiwa amekumbatia nyama hiyo tumboni kwake.

Zawadi akatoka kwa ustadi na hatimaye akawa nje ya hicho kichaka. Wakatokomea sehemu nyingine ambayo walihishi ni salama zaidi. Saleh na Zawadi sasa waliusogeza msitu bila kuangalia wapi wanakanyaga. Lilikuwa ni giza totoro.

Hakuna tumaini la kufikia mbele lakini walienda tu. Walienda bila ramani wala mtu wa kuwaongoza. Waliongozwa na hisia wawili hawa.

Walisogea mbele hadi kuona walipo panatosha kabisa kuweka makazi mapya. Wakajificha tena kwenye kichaka wapete angalau chakula kilicholetwa na adui zao.

Hii inaitwa mwombee kheri adui wako. Au wenye misemo yao wanasema mgeni njoo mwenyeji apone. Walifakamia chakula hicho bila kuulizana ilikuwa ni nyama ya nini walikula tu kwa baa la njaa walilokuwa nalo. Mate yao yakawa kinywaji. Walikula kushiba.

“Saleh!, kwani ni dhambi kukupenda?” Lilikuwa ni swali lenye majibu ya kuchanganya sana, swali ambalo wakina Socrates na plato walishindwa kuleta majibu yaliyostaiki.

“Hapana, kwani kuna dhambi gani mimi kukupenda wewe?” Naye sadiki akamuunga na swali lake pasi kumpa jibu sahihi.

Wakajikuta wanasahau wapo sehemu gani. Walisahau kabisa kukumbuka kama wanatafutwa.

Wakazama dunia hile ambayo kwa nchi tofauti na Tegemeo hairuhusiwi kwa vijana chini umri wa miaka kumi na nane. Walizamia huko miaka kenda rudi.

Bahari ikawa bahari, vumbi likawa vumbi, mwezi ukazima na jua kuchomoza. Hatimaye wakazinduka mapema kabla asubuhi kufika. Walijikuta wameenza kulowa kabisa. Maajabu!! Wamelowa!, wamelowaje?!.

“Mvua!” wote wakahamaki kwa pamoja?, mvua itoke wapi msimu wa kiangazi Malindi nzima. Likawa jambo gumu kulifafanua. Walianza kutapatapa kulowa na mvua hiyo ambayo ilionesha haina utani kabisa. iliamua kunyesha.

“Khaa!” wakainuka pale walipo wakikumbatiana kwa baridi. Waliona haya kwa hali waliyojikutanayo Ahsubui hiyo. Kulianza kupambazuka.

Zawadi alishamtunuku Saleh penzi usiku ule, naye Saleh alishaonesha makucha yake kwenye pendo la Zawadi. wote walikuwa si haba. japo hakuna mzoefu kati yao lakini walifanya tosha kuwaridhisha. Wakazoeana sana. Wakabaki kukumbatiana tu.

“Saleh wanakujaa!” Zawadi alipiga kelele za kumshitua Saleh, lakini kelele hizo ziliwakuta hadi wakina Ibo na kufanya wao kuonekana.

Hawakujali mvua Saleh na Zawadi tayari walishikana mikono kuanza safari ya kumkombia adui huku unaonekana. Walijitahidi sana kukimbia kadili ya uwezo wao.

Hawakuwa karibu karibu kusema kwamba labda wangewashika kwa urahisi. Walionekana kwa mbali sana. Ikawa nafuu kwao kupata na nafasi ya kupumua japo kwa dakika. Japo Zawadi alikuwa anakimbia kwa 'kusokwa', kufa kupona lakini yeye alikuwa anaona raha tu. Yupo karibu na mtu anayempenda. Hakuwa na shaka kabisa Zawadi. alishaanza kupenda hii michezo ya kukimbizana.

Ibo na askari wake waliotambulika kama mashujaa Malindi, waliendelea kuzifuatilia hatua za wawili hawa kila pande. Walikuwa usawa mmoja lakini umbali tofauti. Waliwaona tu waleee!. Wakakaza mwendo na kwenda mbele.

Kwa upande wa Saleh na Zawadi wao walikuwa hawajui wanaenda wapi. Walizunguka tu msitu mzima pasi na sehemu ya makazi ya watu kutokea.

Walizunguka sana. Na hatimaye Zawadi kukataa pumzi. Akakaa chini akisubili mapigo ya moyo yakae sawa. Alichoka Zawadi. Presha ikapanda kwa Saleh. Hakuna na la kufanya. Akaanza kubuni mbinu za kuwachelewesha wanaowatafuta.... Jamani mwanamke vitani? .

ITAENDELEA Episode ya 19.
Join Group SAYARI YA SIMULIZI SAYARI YA SIMULIZI 🗺

Starxav
 
XAVERY EMMANUEL LUOGA
“PENDO HURU’
0672493994

EPISODE 19
Kwa upande wa Saleh na Zawadi wao walikuwa hawajui wanaenda wapi. Walizunguka tu msitu mzima pasi na sehemu ya makazi ya watu kutokea.

Walizunguka sana. Na hatimaye Zawadi kukataa pumzi. Akakaa chini akisubili mapigo ya moyo yakae sawa. Alichoka Zawadi. Presha ikapanda kwa Saleh. Hakuna na la kufanya. Akaanza kubuni mbinu za kuwachelewesha wanaowatafuta.

Alimvua Zawadi mkufu wake na kuugawanya. Mwingine akautupia upande mwingine na mwingine upande mwingine. Akamnyanyua Zawadi na kusogea nae kando kidogo. Bado wakina Ibo walikuwa wakiotea tu sehemu ambayo wawili hao wamepita. miti na vichaka viliwachanganya.

Saleh akaanza kuandaa zana za kivita. Akatafuta miti iliyo kama fimbo nyingi akazingaunga tu na kamba za miti mikubwa. Akatengezeza mitego kazaa kwa kuzifunga kwenye nyasi na nyingine jii ya miti. Saleh alikuwa vizuri katika uwindaji.

Baada yapo akasogea mbele na Zawadi ambaye japo alikuwa anakimbia lakini sio mkimbio ule wa matumaini. Zawadi alichoka kukimbizwa bila sababu. Akawa anakimbia kizembe zembe. Uliitwa mwendo wa kike kike.

Ibo na askari wake hatimaye wakaingia kingi, hiyo yote juu ya kufuata mabaki ys mkufu wa Zawadi uliowekwa mtego kama Chambo. Watatu kati yao wakavamia mtego na kuwarusha mbali. Mungu mkubwa!, hawakufa. Wakasimama kwa muda kutafakari jambo hilo.

“Alaah!. Angalieni chini!, chini chini nimesema” aliwaambia askari wake ambao bado hawajapata dhahama ya mtego huo.

Wakarudi kuwatazama wenzao watatu walioathirika. Wakawaganga japo kwa shida lakini wakawa sawa ila walitembe kwa manati. Ikawa hauweni kwa kina Saleh kuchanja mbuga.

“Wawili bakini na hawa, piteni kwa upande huu, mimi na wewe huku!, huku nimesema” Ibo alikuwa ni mtu wa amri tu.

Aliamrisha wagonjwa wale wabaki na wengine wawili wakiangalia afya yao. Wengne wakagawanyishwa eneo lingine na Ibo akaondoka na mmoja na kumfikia jumla ya askari wote kumi na moja.

Saleh bado alikuwa na Zawadi wake mikononi, walitembea sana. baada ya kuona wapo umbali mrefu toka walipowatelekeza waasi wao.

Ajabu!! Mvua ilikuwa imeshakata. hakukuwa hata na dalili ya Mawingu. Jua kali Lilikuwa kando yao. Kwa majira ya kizee zee ilikuwa ni saa nne na unusu ya asubuhi. Bado walikuwa ndani ya msitu na kutokuja wapi wanaenda. Msitu ulikuwa ni mkubwa mno.

Wengine watano walipatwa na dhahama ya mtego wa pili wa saleh!, watatu kati yao walinusurika na wawili kupoteza maisha. Walifakamia kamba iliyotegwa kwenye nyasi kwa ustadi mkubwa iliyobeba gogo nyepesi kwa juu. Kwa mstuko walirushwa na gogo hilo hadi kwenye shimo lilipo karibu na mtego ilipo. Walioanguka vibaya walipoteza maisha hapo hapo.
Walikuwa waili tu na kubaki watatu, watano hawa ni wale waliopita upande tofauti na Ibo na wale wengne ambao wawili majeruhi. Msafara ukawa mzito kwelikweli. Ibo alijidai kukwepa kila kishawishi bado alikuwa imara sasa.

Mzunguko wa msitu ukawachanganya Saleh na Zawadi walikutana na nyjia nyingi zilizotawanyika bila kuonyesha zinaenda wapi.

Wakachagua njia ya kulia kuelekea mbele kupata msaada. Walipita moja kwa moja kwa mwendo wa taratibu bila shaka na hofu. Zawadi alitembea huku akijigonga gonga mabegani mwa Saleh kimahaba. Alikuwa ni full of love. Alifurahi sana Zawadi. Nafsi yake ilipata pa kumfikia. Aliona yupo ndani ya mjengo wa mahaba. Wenye kujengwa na tabasamu alipendae. Jingo lenye macho ya dhahabu na mguu wa bia. Jingo lililopo mbinguni. Wakakanyaga mafuta taratibu kuelekea mbele.

“Mamaa!” Zawadi aligumia.
“Nini!!” aliruka Saleh.
“Mdudu!” alishikwa na woga Zawadi huku mikono yake ikimshika Saleh kwa kumvuta. Aliona kinyonga.

“Sasa! huyu mdudu humjui Zai!”
“Hahahahaha!, amenistua tu!” alicheka Zawadi. Aliona sasa ni muda wa matani. Wala hakuwaza juu ya msako ambao unaendelea juu yao.

Wakacheka kwa ushilikiano wa aina yake. Wakasonga mbele.

“Tititititiiti!” kishindo kilisikia. Zawadi na Saleh walikuwa mbali kimaongezi, hawakusikia kitu.

“Ngruuuuuh!” mngurumo ukasikika nyuma yao. Hapa wote walisikia. Ukawapa nafasi ya kugeuka na kutazama mgurumo huo wa kuogofya.

“Simba!” nafsi ya Zawadi ikahema kwa nguvu. Mkojo ukawa langoni kukaribia kutoka.

Akaanza mbio Zawadi lakini alishikwa na Saleh na kusimamishwa. Alimuwai kabla hajaonekana anapiga hatua na kumvutia mnyama huyo wa mwituni.

Saleh akambana Zawadi kifuani kifuani kwake, asipige kelele. Wakatulia tuli kimwili lakini kiroho Zawadi hakuwa pale tena. Alikuwa anasali zile sara za mwishomwisho za kuzaliwa marehemu. Kimya kikatanda.

Mwenye macho haambiwi tazama. Simba huyo akapita kando yao bila kufanya chochote kile. Aliranda randa kwa mbele na mwisho kusimama. Alisimama Simba.

“Ngruuuuuuh!” akaunguruma tena kwa hasira. Saleh akashuhudia mtetemeko wa Zawadi ambao uliupita ule wa Simba. Zawadi alikuwa anaogopa sana.

Jambo la kushangaza simba huyo mwenye umbo lililowapita Zawadi na Saleh zaidi y mara mbili alipita tena alipo Saleh na Zawadi. Hakuwatazama katu.

Akatimua zake mbio na kurudi nyuma alikotoka mwanzo. Nadhani aliona wenye haki wa kuangamizwa msituni humo, tena wengi kuliko hao wawili.

Akawaacha Saleh na Zawadi wasonge mbele. Walitembea kwa hofu na mashaka huku macho yao yakihakikisha ujio mpya wa simba huyo kama atarudi tena au la. Lakini hakuna! hakurudi simba huyo. Na hawakumuona tena.

Kutembea kwao kilikomea katika kichochoro ambacho kilionyesha kinaelekea mabondeni. Wakasonga huko japo kutafuta lolote. Njaa iliwasokota mno. Wakaenda mbele.

Njia hiyo iliwapeleka hadi katika bonde moja kubwa lililotenganisha upande mmoja na mwingine. Pande hizo mbili zilitenganishwa na mto huo.

Wakapata nafuu ya kuyaona maji. Wakafakamia. Hakika mungu alikuwa upande wao. Waliyaona mafanikio. zile pumzi zilizokua zinakimbia mkukumkuku, sasa zilisimama na kutilia.

“Saleh!, tukifika tutaishi pamoja!” ilikuwa ni ndoto ya Zawadi ambaye bado alikuwa anatoa kuwa ni rahisi sana kuvuka katika msitu huo. Saleh alimwangalia tu na kutabasamu.

“Usijali Zawadi, nakupenda sana!” Saleh akarudisha wema wa maneno kwa Zawadi. Hawakuacha wote kutabasamu. Walitabasamu.

Baada ya kufakamia maji ya mto huo wakakaa kwanza chini kupanga njia gani wanapita. Hakukuwa na njia itakayo wawezesha kupita upande wa pili.

“Zawadi, ivi unajua kuwa tunatakiwa tupite kulekule tulipotoka?” aliuliza Saleh kana kwamba Zawadi atakuwa na jibu la tofauti.

“Ah! Eeh!, kulee kwenye pachapacha nyingi?” aliuliza Zawadi.

“Ndio kipenzi. Lakini…!” aligomea katikati Saleh.

“Ivi kwanini Baba anafanya hivi Saleh!” Zawadi alipotezea lakini ya Saleh na kumjenga hoja mpya.

“Malindi imekuwa kinyume na nilivyofikilia. Sina damu kabisa na Baba yangu. Yaani sijapata kumpenda baba huyu toka enzi za ujana wangu. Ananilinda tu!, sina uhuru!, Saleh!!” aliongea Zawadi na mwisho alijikuta anaongea peke yake. Saleh alikuwa katika mawazo mazito. Hakuwa pale kabisa. Aliwaza Ushindi mpya! ushindi wa kuishinda Malindi....
..............

HAYAAA!, Bado tupo Msituni Malindi. Saleh na Zawadi wameshinda mbio HURU , na sasa wapo katika fikra ya Mapinduzi ya kweli. Tukumbuke Sadiki naye alikus njiani kuelekea Msituni. Kipi kinaendelea..?

ITAENDELEA........


Starxav
 
XAVERY EMMANUEL LUOGA
“PENDO HURU’
0672493994

EPISODE 20
“Malindi imekuwa kinyume na nilivyofikilia. Sina damu kabisa yani na Baba yangu. Yaani sijapata kumpenda baba huyu toka enzi za ujana wangu. Ananilinda tu!, sina uhuru!, Saleh!!” aliongea Zawadi na mwisho alijikuta anaongea peke yake. Saleh alikuwa katika mawazo mazito. Hakuwa pale kabisa.

“Zawadi!” aliita Saleh akiwa bado macho yake amekazia pembeni kana kwamba kuna jambo zito linataka kumtoka.

“Abee!” akaitika Zawadi.

“Baba yako sio mtu mwema kwa kweli!” aliongea Saleh.

“Nisamehe sana Saleh!, najua yaliyokukuta ni mimi ndio sababu. Pole jamani!” aliongea Zawadi na mchozi ukamtoka. Saleh bado alikuwa bize na maongezi aliyoyakusudia yeye.

“Zawadi!!, Liwalo na liwe, Mimi na wewe ndiye tutakaye ibadili Malindi!” alimaliza Saleh na kumfanya Zawadi asimamisha shingo yake kama twiga.

“Unamaaana….!, turudi?” aliuliza Zawadi.

“Ndio Zawadi, Malindi ni azina yangu. Lazima nirudi!” aliongea Saleh bila maelewano na Zawadi. Saleh alishaingiwa na tamaa ya utawala kutoka kwa baba yake. Alimfikilia sana na Ibo.

“Zawadi!, kama mimi na wewe tutafia huku, au mimi na wewe tutapotea Malindi, basi Ibo bila shaka atakuwa mtawala wa Malindi!. Apo tutakuwa tunajenga au tunabobomoa?.” Aliuliza Saleh.

“Mhh!, Saleh mimi nakusikiliza wewe tu. Tupo pamoja tutakufa wote.” Alijifunga kitanzi Zawadi.

“Sasa Zawadi hakuna namna ya kuogopa. Tunarudi kijijini!. Liwalo na liwe. Familia zetu zipo huko. Lazima Malindi yafanyike mapinduzi!” Saleh sasa alikuwa anaweza kikomandoo. Japo kuwa alikuwa mbichi kabisa katika masuara ya kupigana lakini kwa sasa alijawa na roho ya kupambana hadi mwisho.

“Sawa Saleh, sasa. Da!!, ko tunarudi!” Zawadi aliongea akijikuna kichwani kwake kuashilia hakuwa hata na hamu kumuonea baba yake. Alifuata tu amri ya mtu pekee ampendaye. Alikuwa bendera Zawadi. akafuata upepo.

“Zawadi, changamoto kubwa hapa ni njia!. Unajua kwanini nimesema hivo?”

“Sa si ndio unambie” aliongea Zawadi akijisogeza karibu na kifua cha Saleh.

“Unajua tuna siku nzima tupo huku na hatujui wapi tunaenda?, huu msitu unavitu vya ajabu sana na nashangaa hadi sasa bado tupo salama. Punde tu tumekoswa na simba! chupuchupu. Sasa kwa ushairi wangu mimi naona tu turudi. Tutapotokea ndio hapo hapo. Mana sijui hata kama nusu ya huu msitu tumefika. Turudi Zawadi!” Saleh alishinikiza.

“Jamani Saleh!, aya!” Zawadi hakuwa na pingamizi.

Wakanyanyuana hapo walipo na kusogea hatua moja. mara ghafla yowe upande wa pili wa mto likasikika.

“Ibo!” akatamka Zawadi, alisikia sauti la yowe la Ibo. Wakakaa kimya kusikia tena. Kweli!, sauti ikasikika tena.

Ilikuwa sauti ya Ibo ambayo ilisikika kwa hofu sana. Alikuwa anashambuliwa na kitu kikali. Ghafla sauti hiyo ikakata. Ilikuwa ni upande wa pili wa mto walipo wakina Saleh na Sadiki. bila shaka Ibo kapata tatizo. tamaa zake zikamwishia hapo.

“Tukimbie!” Saleh akamshika mkono Zawadi na mbio za kutoka hapo zikifuata. Walitoka mbio kufuata ile njia, walifika hadi pale ilipo njia panda ya njia nyingi. Wakakutana na mzoga wa mguu wa mtu ambao umetokwa kutafunwa sio mda maharufu.

“Jamni inamaana simba ndio…” kabla hajamaliza Tayari Saleh alishamvuta hadi kumtoa sehemu hile. Ilikuwa anatisha kwa damu. Walipita njia ileile ambayo walipita mwanzo kwa kuwa ilikuwa moja tu kabla ya kugawanyika. Walitoka nduki mno.

Mungu sio athumani, walifika hadi yale maeneo ambayo walitega mtego wao wa kwanza. Hawakuwaona wale askari wawili ambao walifariki kutokana na mtego. Walikuwa katika shimo, hawakuonekana.

Wakasonga mbele Saleh na Zawadi. Walitumia mda mchache sana kukimbia. Safari hii zilikuwa ni mbio za Ushindi. Waliongozana kama upepo na hewa. Walipita hadi katika mtego wa kwanza waliona umeteguka lakini nao hakuna maiti. Wakasonga mbele.

Harakaharaka hadi pale katika kile kichaka walichojificha siku waliyolala wote. Walikuta mvua inaendelea kunyesha sehemu hiyo bila mchezo. ilikua inanyesha sehemu hiyo tu basi. Haya ndio maajabu ya Msitu Malindi.

Ilikuwa mvua kubwa sana lakini hawakujali. Waliamua wawili hawa. Saleh mbele, Zawadi nyuma. Mguu kwa mguu hadi Malindi. Kwenda kufumua hitimisho la utawala na uhuru. Hawakuridhika na mambo ambayo yanatendeka kinyume na historia ya Malindi.

Saleh alishajuwa kuwa yeye ndio mtoto wa Mfalme kwa upande wa kiume kwa hiyo yeye ndiye anayetakiwa kuongeza Malindi kama mtoto wa Mfalme. Walijipiga piga kwa safari yao ya uchovu hadi kufika mwanzo kabisa mwa msitu.

Walikua na Mungu watu hawa, walitumia alama walizoziacha kurudi walikotoka, mitego na sehemu kadha wa kadha walizozikumbuka ziliwaongozavyema. sasa wapo nje ya msitu.

Walitoka hawakuamini kwa namna matukio ya mule ndani yalivyo ya kushangaza kutoka kwao nje walikuta kukavu kabisa. Hakuna hata chembe ya mvua wala majimaji yotokayo na mvua.

“Saleh!, Saleh!!” Sauti ilisikika nyuma yao. Wakageuka.

“Sa-Sadiki?” Zawadi alipagawa. Alikuwa Sadiki nyuma yao. Alikuwa hoi kwa mbio.

“Hakika Mungu ni mkubwa. Nilikuwa nawafukuzia toka mbali sana!, niliwaona waleee!” aliongea Sadiki akionyesha kuhema.

“Kaka sasa ulijuaje tupo huku?” aliuliza Saleh.

“Kijiji kimechafuka. Kila mmoja anaimba Saleh Saleh. Mapinduzi yanaipindua Malindi.” Aliongea sentensi zisizoeleweka Sadiki.

“Unamaana gani?” aliuliza tena Saleh.

“Kaka!, Niliacha watu wamekusanyika huko. Kuna mengi Malindi. Twende tukajionee.” Alimaliza Sadiki. Hakutaka kueleza kila jambo, kwani hakuwepo. Yeye alikuwa kuwasaka watu hao wawili. na hatimaye aliwapata kwa urahisi sana. Wakaungana na sasa kuwa watatu. ilikua familia sasa.... familia ya mageuzi, familia ya mapinduzi.

Ibo na wenzake wakabaki ndani ya msitu kama mizoga ya kuliwa na wayama. Walitafunwa kama nyama na ndege kupitia mabaki yao... Hakika tutamkumbuka Ibo. kwa makubwa aliyofanya!.
..........

Moto unaenda kuwaka Malindi. kipi kitajiri baada ya watu watatu kutoka wazima kabisa msituni Malindi?..

ITAENDELEA....

Starxav
 
Hahaha umechoka lakini saa 6 usiku wa manane upo unazurura.
IBU kafa kaliwa na simba, Saleh na Zawadi wamekutana na Sadik sasa wote wanajiandaa kurudi Malindi.
Summary hiyo

Usiku wa manane ndiyo mzuri, hauna fujo wala purukushani... ni wewe na Mungu wako...

Ibo kafa kizembe...
Salehe na zawadi hata baada ya kukimbizwa koote huko lakini wamefanya matusi msituni...

Unanisimulia kwani hii ni bed time story...



Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom