Simulizi: Pendo Huru

Simulizi: Pendo Huru

XAVERY EMMANUEL LUOGA
“PENDO HURU’
0672493994

EPISODE 21
SEHEMU YA TISA.

Patashika nguo chanika!.
Saleh, Sadiki na Zawadi wakatimba hadi karibu na kasri ya mfalme. Kila mmoja alikuwa na roho ya uchungu ya kufanya mapinduzi Malindi. Saleh, hakutaka tena kushuhudia mauaji yanayoendelea kutoka kila siku pasi wananchi kujua. Sadiki naye hakutaka kabisa kuona uhuru wa Malindi ukiendelea kupeperushwa mbali na upepo wa utawala mbovu. Zawadi naye ni mapenzi tu. Yeye alibeba bendera ya upendo. Mwenye haki na apende. Tena apende bure pasi na sarafu ya rushwa au kikwazo kingine. Watatu hao wakabeba mapinduzi ya miaka zaidi ya miamoja toka kujulikana kwa Malindi. na sasa walikua moto wa kuotea mbali.

Naaaam!, wakaingia hadi ndani ya himaya ya mfalme, hakukuwa na mlinzi hata mmoja mlangoni. Ikashangaza. Lakini ilikuwa hauweni kwao. Wakasogea hadi karibu na mlango wa kuinglia ndani. Nako hakuna hata dalili ya kuwepo na mtu.

Zawadi akasogeza mlango kuangalia kama kuna watu ndani. Mlango ulikuwa ni mwepesi kufunguka. Akafungua lakini ndani hakuna mtu.

“Zawadi, Dada Zawadi!, wapo Mbio ndefu!” Mmoja wa mfakazi wa kasri ya Mfalme ambaye pia alikuwa ni mpambe wa Zawadi alikuja akitokwa na mbio hadi walipo.

“Wanafanya nini!” aliuliza Zawadi kutaka ufafanuzi.

“Wamekusanyika wote. Sasa wanakaribia kujaa uwanja. Kumechafuka!” alitoa taarifa.

“Na wewe kwanini upo hapa!” aliuliza Zawadi maana kama wote wapo uwanjani kwa nini amerudi.

“Ramani. Nimeambiwa nije nichukue ramani.”

“Ya wapi? Na ipo wapi?”

“Ya Malindi nzima. Ipo katika chumba cha Mfalme.”

“Unapajua ilipo?”

“Hapana nimeelekezwa na Mama, nije kuchukua.” Alijieleza kadili alivyoulizwa.

“Subiri!”. Akatoa amri Zawadi na kuingia ndani pekeyake. Dakika sita mbele akatoka na karatasi.

“Ndio hiyo?” akahoji saleh, hakujibiwa.

“Twende!!” likatoka tamko kutoka kwa malkia. Wote wakamfuata, kuelekea uwanja wa Malindi.

Uwamja wa Malindi wa Mbio Ndefu upo mita chache sana karibu na lango la hemaya ya mtukufu Mfalme. Uwanja ambao hushughulisha shughuli nyingi kijijini Malindi. Vikao vyote vya kijiji na matamasha mbalimbali yote yalifanyika huko. Leo kulikuwa na kikao cha kijiji kizima. Siku zote zilikuwa za kushurutishwa kwa kufanyishwa kazi za kuzalisha mazoa bila idhini yao na hatimaye robo ya mazao hao unapeleka kwa Mfalme. ilikua inakera kuliko maelezo, nilime mimi ale mfalme?, Hapanaa!.

Leo uwanja ulipoa mno. sura za huzuni zilitamalaki kila kona. Msiba!, kulikua na msiba.

Wenye mchozi wa karibu tayari ushawatoka hadi kukauka, mwenye sauti kubwa alilia hadi ndege kupeperuka. Mwenye mashetani yalipanda hadi kufika mbinguni. Kila mtu alishiliki huzuni hii kadili awezavyo ilimradi tu iwe imemgusa.

Mbele kabisa ya jukwaa kulikuwa na sanduku ambapo watu walishatangaziwa kuwa aliyekuwepo humo ni mtukufu Mfalme. Mfalme alifaliki mda mchache kabla ya mkusanyiko huo, inaonekana kwa uzee wake alfaliki pindi tu aliposukumwa na Zena. alikufa mazima mfalme.

Pembeni yake alikuwepo Mama Zawadi. Mke pekee wa Mkubwa wa Marehemu Mfalme Bana. Alikuwa mwingi wa chozi pembeni ya sanduku alikolala mume wake. Alikuwa na jambo zito la kusema siku hii.

Mda huo tayari Saleh, Sadiki na Zawadi walishatia timu. Wote walisimama kuendelea kusikiliza na kuona waliyoyashuhudia. Bado hakukuwa na taarifa sahihi walizozipata watatu hao kuusu Mfalme. Walikuwa hawajui taarifa ya kifo.

“Dada, mama anasubiri ramani!” yule Binti alitoa dukuduku lake baada ya kuona Zawadi ameshikilia ramani na hana mpango wa kusogea mbele. Alikuwa anachezesha tu kichwa cheke kumtazama Baba yake ambaye alihisi anakisasi nae lakini katu, hakumuona. Akampa ramani yule Binti. Mbio kuelekea mbele hadi kwenye jukwaa. Akampa ramani mama zawadi na kisha kushuka chini ya jukaa. Mama Zawadi alisubiri ramani ili amwage Mchele hadharani.

Mama Zawadi alichukua mda kabla ajaanza kuzungumzia ukweli wote uliomuhusu. Alikuwa na funda la siri moyoni ambalo lilidumu kwa kindi cha utoto hadi ukubwa wake. Leo lilimshuka kueleza ukweli. Akaanza kuongea baada ya kufuta machozi yaliyoanza kukauka. alilia hadi mara saba, uso ulimkauka kwa kukosa chozi la nane.

“Salamu tena ndugu zangu wa Malindi” alianza kwa salamu lakini hakuna aliyeitikia. Umati uliipisha salamu hiyo na kutoweka angani. Kimya kikatanda.

“Mnisamehe sana kwa kugoma kuongea toka mwanzoni. Nilichokuwa nakisubili ni hiki hapa!” aliinua ramani juu na kuonyesha bila kufungua. Akaendelea.

“Napenda kutoa historia hii kama ifuatavyo. Kitakacho funguliwa humu, ndio kitafunguliwa pia mioyoni mwenu!” baada maneno hayo umati ulishituka. Ukaanza kunong’ona kwa sekunde kisha kuwa kimya. Saleh, Sadiki na Zawadi macho na masikio yao walielekeza juu ya jukwaa.

“AH!, Ndugu zangu wa Malindi. Kijiji chetu kipo ndani ya nchi ya Tegemeo. Ilo kila mtu analijua.!” Aliongea tena akipisha mate yaingie vizuri kooni na kuendelea. Alikuwa na hofu Mama Zawadi.

“Kwaramani, hiki ni kijiji ambacho kimebarikiwa kuwa na maliasili nyingi sana, ikiwemo madini, mafuta na msitu mkubwa wa Malindi. Tuachane na madini pamoja na mafuta kwa maana hakuna mwenye utaalamu wa kufukua vitu hivyo!. Tuje hapa kwenye msitu.

Mwanzo kabisa wa utawala wa nchi ya Tegemeo kulikuwa na vita vikubwa sana. Vita ambavyo viliusisha vijiji takribani nane, vijiji vyote Vilikuwa ndani ya utawala wa nchi ya Tegemeo.

Vita hivyo vilihusishwa katika kugambania kijiji chetu cha Malindi. Lengo kubwa ni umiliki wa mali hizi tatu nilizozitaja hapo juu. Mali mabayo iliwavutia vijiji vingi ni kuwa huu msitu wa Malindi kuwa na ukaribu na kijiji chetu.

Msitu huu ni wa asili!, haujapandwa. Hapo mwanzo Inasemekana ulikuwa mdogo tu, ulitenganisha baina ya vijiji vyote nane. Mapambano yaliyoendelea kutoka katika dhama hizo yalisambalatisha kila kijiji na kubaki na kijiji cha Malindi pekee.

NINA maana kwamba wanamalindi waliungana na kupambana na vijiji vingine saba na hatimaye kushinda. Malindi ilisambaratisha kila kijiji. hatimaye tukabaki wenyewe nchi nzima.

Toka hapo vijiji vyote saba havikuwahi kuonekana tokea hapo na msitu ulizidi kuwa mkubwa na tishio. Jambo lisiloaminika ni kuwa, eti msitu huu wa Malindi pia ni muunganiko wa vijiji vingine saba vilivyopotea kwa utata. baada ya vijiji hivyo kuwa havina watu basi msitu ulisambaa hadi huko. hakuna aliyewahi kutoka nje ya Malindi. pia inasemekana pia, jambo la kukua kwa msitu ni ghadhabu za mizimu ambazo zilikasilika baada hakuona vijiji nane vinataa ya kumwaga damu.

Hivyo dhana ya msitu wa ajabu ilianza kutokea toka kipindi hiko cha mababu.” Aliishia hapo Mama Zawadi na kugawa ramani hiyo kwa mtu aliyepo karibu ili kushuudia anachokiongea. Kisha akaendelea.

“Ah toka hapo Malindi ikabaki kuwa Malindi ya amani tele. Utawala ukarishishwa na kulisishwa. Matambiko kadhaa yakawa yanatolewa mwanzo kabisa wa msitu huu. Ilikuwa jadi yetu. Labda nisiende mabli sana. Ngoja nieleze kipindi hiki ambapo hata mimi nilikuwepo.

Mwanzoni kabisa baada ya kuzaliwa mimi, wazazi wangu wote wawili walifariki kwa ajali ya moto. Nilikuwa nje ya nyumba wakati inaungua. Sikujua sababu wala chanzo cha moto huo. Ila tu ni mapenzi mabaya ya baadhi wa watu.

Baada hapo nikaenda moja kwamoja kushi kwa Mzee mmoja hizi jina lake alikuwaaa… anaitwaaa… ah!, eeeh! Bi Mpembe. Huko nilikuta pia anaishi na kijana mdogo rika yangu naye alikuwa ni wa kike.

Tuliishi kwa kupewa kila kitu kwa usawa lakini kama mjuavyo chuki haimtupi mtu. Nikakumbwa na chuki. Nikamchukia mwenzangu kwa kuwa alikuwa na baati sana kuliko mimi. Alikuwa na umbo nzuri sana la kuvutia kama Zena, ila yeye alikuwa mtoto mtoto.

Basi siku moja tukapata tenda ya kwenda ya kwenda kusafisha nyumba ya Mfalme. Wote tukawa mstari wa mbele kwenda kufanya usafi huko. Kwa bahati nzuri mwenzangu alielewana vizuri na Mfalme na hatimaye akawa naye na mahusiano na kushikishwa mimba. Kwa woga wa mizimu akatoroshwa mbele yangu na kupelekwa kuishi mbali huko ambako taarifa niliyoipata kuwa aliaambiwa atoe hiyo mimba lakini alizaa.

Mimi nikampiga gepu kwa kuwa karibu na Mfalme kama mjakazi wake lakini sikufanikiwa kumuingilia kimahusiano. Siku zikapita chache sana Mfalme Bana ambaye ndiye baba wa Mfalme huyu alipoteza maisha na utawala ukabaki kwa mtoto wake wa pekee wa kiume ambauye ndiye huyu hapa chini.” Zawadi alishituka baada ya kuona Mama yake anaonyesha sanduku lile.

"Baba amefariki?" alijiuliza Zawadi, alianza kukosa nguvu. Saleh akachukua nafasi ya kumliwaza. Akapoa kidogo na Wakaendelea na kusikiliza taarifa ngeni masikioni mwao juu ya ubinafsi wa mke wa Mfalme Mama Zawadi....

JIUNGE na kundi la SAYARI YA SIMULIZI FACEBOOK KWA TAARIFA ZAIDI KUHUSU SIMULIZI MBALIMBALI: VITU VINGI NITAWEKA HUKO. SAYARI YA SIMULIZI 🗺
..........
Naam historia Mpya inaanza kutengenezwa Malindi.... tukiwa katika sehemu za mwisho mwisho. mchango wako ni muhimu sana....

ITAENDELEA....

Starxav
 
XAVERY EMMANUEL LUOGA
“PENDO HURU’
0672493994

EPISODE 22
Mimi nikampiga gepu kwa kuwa karibu na Mfalme kama mjakazi wake lakini sikufanikiwa kumuingilia kimahusiano.

Siku zikapita chache sana Mfalme Baba ambaye ndiye baba wa Mfalme huyu alipoteza maisha na utawala ukabaki kwa mtoto wake wa pekee wa kiume ambaye ndiye huyu hapa chini.” Zawadi alishituka baada ya kuona Mama yake anaonyesha sanduku lile. Saleh akachukua nafasi ya kumliwaza. Akapoa kidogo. Wakaenelea na kusikiliza.

“Basi kwa huyu nilifanikiwa kwa kweli, nilijiweka naye karibu sana hadi kuwa naye kimausiano. Ikaja sasa siku nikashuhudia msichana yule aliyefukuzwa na mimba yake yupo tena kijijini na sasa ni Mchezaji ngoma maharufu kijiji kizima. Nilijaribu kumchunguza kama kuna yeyote yule anakumbuka historia yake lakini hakuna.

Kwa kuwa nilishampoteza katika harakati zangu basi nikaone abaki hai kuendelea kutuburudisha. Wakati huo mimi ni mke wa pili wa Mfalme, na nilikuwa bado sijamzalia kwa maana alikuwa anatafuta sana mtoto wa kiume.

Kuna kipindi nilimuona dada yule akiwa na mtoto wake wa kiume wakiongea siri hii ambayo tunaijua wachache. Nikaona ataninyima hamani.

Nikamsakazia mtoto wake aungane na majeshi kupambana na kiumbe cha ajabu huko msituni Malindi na hatimaye nilifanikiwa kwani kijana wake alifariki hukohuko.

Mtoto huyo nilimpoteza kwa kuwa alikuwa na viashilia vya kuja kuwa mtawala wa Malindi. Nikapata wivu kwani mimi ndio nilitaka niwe mke mkubwa na mtoto wangu awe mtawala wa Malindi.

Siku si nyingi nikashika ujauzito wa kwanza. Mtoto akawa wa kike. Nilichukia na kwa bahati nzuri tena, mtoto huyo alifariki akiwa na wiki mbili tu. Sasa sikujua kama Binti yule niliyemchukia mwanzo kwa kuzaa na baba wa mume wangu ndiye huyuhuyu tena aliyezaa na mume wangu. Nilipata habari kuwa Binti huyo amezaa mtoto ila sikupata kujua ni mtoto gani amezaa.

Nikafanya tena njama za kumpoteza na akapotea. Akawa mbali na kijiji. Alee mtoto wake hukohuko, asijiusishe na mambo ya utawala,

Na pia kumbe, siku hizo hizo mke wa kwanza wa Mfalme alijifungua nae mtoto wake wa kike. Kwa hiyo akawa mtoto wa kwanza katika utawala wake na mrithi wake hadi atakapopatikana wa kiume.

Mimi nikashika tena ujauzito na kujifungua tena mtoto wa kike, safari hii nilichepuka mimi, nilienda nje.... nilifanya mapenzi na mfanyakazi wake mume wangu na hatimaye kumuua baada ya kuzaa naye mtoto huyo.

Sikutaka siri hii ijulikane. Nilifanya hivyo kwa kutafuta mtoto wa kiume kwa maana nilijua Mfalme mbegu zake zimeshindwa kuzalisha wa kiume.

Na hitimisho nikapata huyo mtoto wa kike tena. Mtoto ambaye niliamua tu kulea bila baba yake mzazi kwa sababu ya mke mwenzangu na yeye alikuwa na mtoto wa kike. nikaona haina shida” Alinyamaza Mama Zawadi kuacha umati ule ushike vichwa na kutafakari mazito ambayo yeye anayaongea kwa wepesi sana. Hakujali!, baada ya hapo akaendelea.

“Basi nenda, rudi, kufika mwaka tu, tukapoteza mke mkubwa na mtoto wake. Walipatwa na gonjwa moja wote wawili wakafa.

Wakaacha laana kwa Mfalme ya kuwa na mtoto wa kike wa kwanza kutoka kwangu naye si mwingine ni Zawadi” alilopoka Mama Zawadi!. Watu wakalipuka tena. Zawadi alinyong’onyea na kupata mshituko. Alizima kwa dadika tu mikononi mwa Saleh. Kila mtu akageuka nyuma kuangalia nani huyo aliye na mshituko wa kufanya mpaka kuzimia.

“Zawadi.. Masikini!!...” wote walinyong’onyea. Walimuonea huruma mtoto huyo aliyelelewa na mama katili hadi ukubwa wake pasi kujua asili yake. Wote wakarudisha macho jukwaani ambapo Mama Zawadi bado alikuwa akiongea pasi kujua kama wakina Zawadi na Saleh wapo hapo.

Basi nikaishi kwa kufa na kupona kuahakikisha kuwa mtawala wa eneo hili ni mwanangu. Nilisahau kabisa kuwa kuna mwanaume yupo na ni mtawala halisi wa falme hii. Mtoto ambaye alichinjiwa sadaka ya miungu yote ya Malindi.

Jambo la mwisho ni kuwa nilifurahi sana pale ambapo nilisikia mtoto wangu Zawadi amepata mtu anayempenda sana.

Mtoto huyo ndiye mtoto halisi wa Mfalme. Nilijua mama yake alishapoteza kumbukumbu juu ya siri hii kwa maana hadi mtoto wao kuwa na mahusiano na mwanangu basi itakuwa njia sahihi ya kupata Mfalme bora na anayesadiki na sio chaguo la mume wangu Ibo.

Nilipenda mtoto huyo amuoe mwanangu kwa gharama zozote zile. Nilimtoa hadi nje ya miliki hii ya Mfalme kuhakikisha kuwa anapata kukutana na huyo kijana.

Lengo ni kuwa wakishaoana basi mwanangu atakuwa malkia na huyo ni Mfalme. Atakuwa Mfalme wa kupachikwa mioyoni mwa watu lakini ukweli ndio huo kuwa yeye ndiye!, yeye ndiye Mfalme.
Saleh ni Mfalme wa Malindi” Mama Zawadi aliishia hapo. alitaja jina Saleh.

Kwa maovu aliyofanya Mama Sadiki alishuka kwa matusi na kejeri za watu. Wachache kati yao walianza kuimba nyimbo ya mapinduzi ya Malindi kwa kutaja jina la kiongozi mpya ambaye ndiye anasadiki achukue milki hii. japo hawajui wapi alipo.

Saleh kijana mpevu,
Miliki yako I mbavu,
Ipate kuto kuwa mabavu
Ongoza pasi shaka angavu
Saleh jembe, jembe jembe!” X2

Walianza kuimba watu na kuitikia wote kwa pamoja. Wengi walikuwa hawamfahamu Saleh. Ila walijikuta tu wanaimba. Walifurahi kujua ukweli kuhusu uongozi wao.

Aliposhushwa Mama Zawadi akapanda juu Mama Saleh. Pia wengi hawakumjua kuwa ndiye mama wa Saleh. Waliomjua walipiga mbinja na vigelegele vya kufa mtu. Akakaa sawa kwa sauti kubwa akarudisha ujana wake kwa ujasiri na kuzungumzia kwa sauti kila mmjoja asikie.

Mimi ndiye Mama Saleh!” aliongea hadi hapo na kuacha umati uitike kwa kuimba nyimbo waliyoanzisha mwanzo. Waliimba hadi mwisho na kuacha kumruhusu kuendelea kusikia anayapi ya kusema....

....... Leo zinashuka mbili, na kesho Tunamaliza mchazo mapema.
Natanguliza Shukrani !.

ITAENDELEA...

Starxav
 
XAVERY EMMANUEL LUOGA
“PENDO HURU’
0672493994

EPISODE 23
Mimi ndiye Mama Saleh!” aliongea hadi hapo na kuacha umati uitike kwa kuimba nyimbo waliyoanzisha mwanzo. Waliimba hadi mwisho na kuacha kumruhusu kuendelea kusikia anayapi ya kusema.

“Hiyo ni historia fupi sana ya Malindi!, ipo bado historia kubwa sana. Aliyelala hapa ndiye Baba wa mwanangu Saleh. Alikuwa mtu mshenzi sana kwa kulala na wanawake na kuwatishia wasiseme. Ilikuwa ni kinyume na tamaduni na matakwa ya ufalme. Aliwachinjwa vijana wengi sana, tena sana ambao makaburi yao yanaozea ndani ya Msitu wa Malindi.

Nasikitika kuwaambia kuwa vijana wetu wawili wote wamepotea katika msitu huo wa Malindi ambapo walikimbilia huko kutokana na mateso waliyoyapata kutoka kwa Mfalme. ni Saleh na Zawadi. Sisi nasi tulishaamuliwa kifo na Mfalme. sababu tu mwenzetu ametoka na binti yake?.

Tulikuja kufunguliwa na Binti Zena, Zena popote ulipo, naomba uje!” aliita Mama Zawadi lakini kimya kikatanda. hakuna Zena pale.

Kila mtu akawa anaulizia kuhusu Zena, mara akaja juu Mama yake Zena na kumnong’oneza Mama Saleh kuwa Binti yake hajamuona maeneo hayo. Hayupo.

Mama Saleh akakumbuka kuwa Zena yupo katika ile nyumba iliyopo mashambani akisikitika juu ya kuhusika na kifo cha mfale. Saleh na Sadiki hawakusikia maelezo hayo walikuwa bize kumuamsha Zawadi adi akaamka. Akamka Zawadi.

“Samahani Zena hayupo kwa sasa ila ashukuliwe sana. Sasa inatakiwa vijana kadhaa wazame katika msitu wa Malindi, kwenda kuwatafuta vijana hao. Kwa sasa watakuwa watatu, Saleh, Zawadi na Sadiki ambaye alienda huko kuwafuata vijana wenzake.” Alipomaliza hapo Sadiki akiwa nyuma akaanza kupiga kelele kuashilia walikuwepo eneo hilo.

Wachache waliokuwa wanamfahamu Sadiki walianza kipiga kelele tena kuwa vijana hao wapo mahali hapo.

Sadiki kwa sifa akamyanyua Saleh mkono. Saleh ambaye alikua upande wake wa kushoto, kulia alikuwa Zawadi. Watu walimwona na Zawadi yupo upande huo wakampokea kwa shangwe.

“Mwanangu!” Mama Saleh sasa naye alimwona mtoto wake, alikuwa salama salimini. Alitamani aruke jukwaa hilo atue alipo mtoto wake lakini uzee ulimkataza kwani angeweza kuvunja mifupa yake yote. Akatulia.

Watu walihamaki sana na kumjua Saleh. Hakika walifarijika mno. Walianza tena kuimba nyimbo hile bila mtu yeyote kuanzishwa.

Waliopo karibu na Saleh na Zawadi na Sadiki waliwabeba mkukumkuku, juu kwa juu huku wakishangilia uhuru wa Malindi. Walijua siri iliyojificha. Saleh ndiye Mfalme.

Waliimba huku wakiwapeleka kina Saleh mbele katika jukaa. Kila mmoja pale chini aliitaji kabisa kumbeba Mfalme huyo ambaye bado hajatawazwa.

Waliwabeba Saleh, Sadiki na Zawadi hadi mbele. Zawadi ambaye alikuwa na kilio mwanzo akapata muwemko wa furaha. Akapata penzi la kweli sasa kutoka kwa umati ule wa Malindi.

Hatimaye Saleh akashushwa hadi chini mbele ya jukaa. Akasimama akiangaza kwa jinsi umati mzima ulivyopendeza kwa kuimba nyimbo ambayo ilitungwa hapohapo na kusherehesha umati mzima. Kila mtu aliimba. mwili ulimsisimka Saleh. katu hakuwahi kuwaza jambo kama hilo.

“Ndugu zangu wa Malindi!” aliongea hivyo kupunguza fujo zilizoishia kupisha Saleh azungumze neno.

“Nashukuru sana Mama yangu, Baba yangu, Rafiki yangu, Zawadi, Majirani, rafiki na kila mtu Malindi.” Alianza kwa salamu na kupitia nyuso zote ambazo zilijipanga upande ule wa jukwaa. Alikuwa Mama na Baba yake, Mama Zawadi, Sala, Baba na Mama Sadiki pamoja na Mama Zena. Wote walikuwa pale chini upande wa pili wa jukwaa. akaangaza kwa mashaka na kuona idadi haijatimia.

“Wapi alipo Zena!” akauliza kwa kuondoa kinyongo. Mama yake Zena alitikisa kichwa tu kwa kuona aibu. Aliona haya kwa kumlazimisha kijana wake kuwa kimapenzi na Saleh, ambaye tayari alishampenda mdada mwingine.

Saleh akarudisha kichwa katika umati wa watu na kuwapa hotuba mpya na safi. Masikio yote Malindi nzima yakawa yake.

“Ndugu zangu, nadhani kila kitu kipo wazi sasa. Tusikejerike na Mambo ambayo yalishapita!, Mfalme aliyepita japo kuwa alikuwa na maovu mengi sana lakini ni jambo jema kama tutakumbuka mambo yake mazuri kwa kilinda vizuri na kufanya amani japo kwa watu wachache kwa maana sio wote mliokuwa mnajua madhaifu ya Baba yangu!.” Neno la mwisho "Baba" lilitoa chozi Saleh.

Alionekana ametokwa na Chozi. Hakujua hata sababu ya kumpoteza baba yake. Lakini zambi zake zilitosha kabisa kufanyiwa mapinduzi. Akalifuta chozi hilo na kuwa imara sasa.

“Jamani, licha kuhangaika hapa na pale, mimi, Zawadi na Sadiki ndio watu pekee ambao inasadikika kuwa tumeingia hadi ndani kabisa ya msitu bila kudhulika na kitu chochote. Ingawa kuwa tulitumiwa watu wabaya watuangamize wakina Ibo na askari wengine wa Mfalme lakini kwa nguvu za miungu wameshindwa.

Hakuna wa kunisimulia kuhusu msitu wa Malindi. Nimeona kila kitu cha Malindi ndani ya msitu huu. Jamani tuishi kwa amani na kusamehena sana kama Mama yangu alivyomsamehe Mama Zawadi. Nasi tuushi katika huu mfano.

Pia nipende kuwaasa wazazi hasa wa watoto wa kike kuwaacha mabinti zao katika kueleza hisia zao juu ya suala la ndoa. Kwani kupitia mkasa huu wa mapenzi ndio umefanya mpaka leo kukosa kiongozi mwenye weredi na mstahiki wa utawala. Walioongoza hakustahiki kabisa ndio maana mambo mengi yalikuwa yanakwama.

Kwa sasa Malindi ni nchi na sio kijiji tena. Jina la Tegemeo sasa limefutwa rasmi na tunachora tena upya ramani ya Malindi.

Sambamba na hiyo naomba leo hii hii baada ya kutawazwa mimi kama Mfalme hapa Malindi nitateua watu ambao watasimama kama washauri hapa Malindi. Utamaduni pia utaendelea kuabudiwa kila mwishoni mwa wiki na si mwaka tena.” Akaacha kuongea kuacha kwanza watu wamalize kupiga makofi kisha akaendelea.

“Hakika kuanzia leo hamtajutia kamwe kuwa hapa. Hili ni Pendo huru kwangu!, nawapenda nyote wanamalindi!.” Alimaliza Saleh na kisha akasogea mzee wa makamo.. Mzee huyo hakuongea sana zaidi ya kusalimia na kuendelea na kazi yake.

“Chacha wajuu zangu, mesikia maneno ya kijana wetu huyu. Chacha miye ndiye namsimika chacha kuwa mfalme,. Aya tuchangilie chacha!” alikuwa ni mzee wa kimira ambaye alikabidhiwa manyanga yote ya kutawaza wafalme. Alisogeza vifaa vyake na kufanya matambiko ya awali kabla ya kumvika taji Saleh......

Swali ni Je Wapi yupo Zena?
Tukutane kumaliza hii kitu kesho, Mungu akijaalia uhai.
"Funzo ulipatalo mpe na mwenzako"
ITAENDELEA...

Starxav
 
XAVERY EMMANUEL LUOGA
“PENDO HURU’
0672493994

EPISODE 24
SEHEMU YA MWIISHO..
“Chacha wajuu zangu, mesikia maneno ya kijana wetu huyu. Chacha miye ndiye namsimika chacha kuwa mfalme,. Aya tuchangilie chacha!” alikuwa ni mzee wa kimila ambaye alikabidhiwa manyanga yote ya kutawaza wafalme. Alisogeza vifaa vyake na kufanya matambiko ya awali kabla ya kumvika taji Saleh.

Naaam!, sasa Saleh ni Mfalme mpya wa Malindi. Watu walishangilia sana. Si tu walishangilia kwa kuwa walipata uongozi mpya. Hapana bali ni kufukuliwa kwa uozo ulozikwa mda mrefu sana walipata amani sana. Saleh akaaga kwa stairi ya aina yake.

“Ndugu zangu wanamalindi, mmepata Mflame mdogo sana kuwai kutokea. Leo juu ya umati huu natangaza kuwa Zawadi ndiye malkia wa Malindi.” Saleh kwa sifa akaacha kwanza watu waserebuke walipomaliza akaendelea.

“Hahaha aya bhana, pia nitumie nafasi hii kutangaza kuwa Sadiki atakuwa na mamlaka ya chini yangu na kiongozi wa miungu na mambo yote yanayohusu taaluma hiyo. Zena!, zena naye atakuwa kiongozi wa wanawake wote pamoja na kiongozi wa michezo na mashirika yote yanayohusu furaha. Mengine tutaendelea kutangaziana lakini kwa sasa. Watu wachache tutatoka hapa na kuelekea alipo Zena. Kwani naye ni mchango wa mimi kuwepo hapa. Pasi yeye basi sijui kama pendo hili lingedumu.” Mfalme Saleh aliyamaliza hayo huku akiandamana na Malkia wake Zawadi, mdogo mdogo na mataji yao kuelekea sehemu ambako Inasemekana Zena amejifungia huko.

Sadiki na wazazi wa pande zote mbili sala, na wengine walijiinga kwenda kumchukua na shujaa huyo wa kike kwa jina la Zena. Walifika. Walifika kwenye ile nyumba ambayo ipo mashambani lakini kulikuwa na kimya tu upande wa nje.

Wote walisimama kusubiri Mfalme atoe amri. Lakini haikuwa hivyo aliingia mwenyeze Mfalme. Aliingia hadi ndani.

“Zena!” aliita Saleh.

“Mungu wangu!!”. Mshituko!, Mfalme alipiga kelele kufanya waliopo nje wang’ang’ane kuingia ndani.

“Jamani!” Mama Zena aligumia baada ya kuona mtoto wake amejitundika na nguo yake juu ya nyumba hiyo.

“Khaa!” Saleh alipatwa na mshangao. Alishindwa kabisa kutoa msaada kwa Binti huyo ambaye alishaanza kuning’inia hapo kitambo kirefu tu.

“Jamani mwanangu! Hiiiiii!” Mama Zena ustahimilivu ulimshinda. Alipiga ukungu wa kufa mtu.

“Jamni mimi mwanangu kwanini umefanya hivi lakini?” Mama Zena bado alikuwa na maswali mengi sana juu ya mwanaye. Alishindwa ajibiwe lipi. Marehemu hakuwa na uhai. Alikufa mapema sana.

“Daaaah! Asee!, umekufa tu, umekufa tu zena kweli?! Bila sababu??. Aaahii!” Saleh aliungana na Mama Zena kuleta kilio Malindi.

“Hakupaswa kufa leo mwanangu. Mda bado lakini… kwanini hiviii!”

.”Mama Zena kwani kuna lolote?, Mbona ah!, mbona kama…” aliishia hapo Saleh. Aligundua kitu moyoni mwa Mama Zena.

“Jamani mimi Mwanangu, mhuuu!. Mwanangu alikuwa na Vi…. Uwii!, amewahi kufa lakini.”

“Mama sikuelewi kuna nini!” Saleh alishindwa kabisa kumwelewa Mama Zena akatoka nje kutoka na harufu ndani humo.
Mama Zena naye alitoka nje huku bado mikono ikiwa kichwani, alitingwa kabisa yani.

“Mama kuna lolote kuhusu mwaneo?” Saleh aliendelea kuhoji, aliona Mama Zena kuna kitu anatamani kuongea lakini anashindwa

“Ah!! hamna kitu baba!, ila alisema mwanangu!, alisema kabla.. alisema hana siku nyingi maana gonjwa lilianza kumtafuna.

“Gonjwa?” aliuliza Saleh kwa mshangao.

“Ndio baba. Mwanangu amepata ugonjwa wa ajabu sana. Mwanangu alikuwa njia, watu walipita tu. Mwanangu ameua wengi sana”.

“Mama kuwa muwazi basi!, sikuelewi unajua!”.

“Ah yani ni hivi, mwanangu mimi alipatwa na huu ugonjwa wa kisasa. Si unakumbuka kuna muda alitokea yule mganga na kutuonesha dalili za ugonjwa sijui. Ndo alisema unaitwa ukimwi?” alisimulia kwa kuuliza akiwa bado anababaika.

“Ukimwi?” akauliza tena Mfalme Saleh.

“Ndio baba. Mwanangu baada ya kuona kuwa gonjwa hilo halina tiba na licha kuwa alishapatwa basi akaamua kujitoa kwa kijiji kizima kwa kushiriki zinaa na kila mtu. Hakuangalia lika wala nini. Lakini hapa mwishoni alitulia kwakweli!” Mama Zawadi alizema hilo mbele ya watu waliopo pale.
Tayari askari wa Mfalme walishatoa mwili wa Zena katika ile nyumba na kumleta nje!

“Hmmm!” Saleh alihema kwa kuepuka kifo. Mama na Baba Saleh yaliwashuka. Walinywea kwa kumlazimisha Saleh amuoe Zena.

“Nisamehe baba, kwani mimi nilijua hilo na sikutoa taarifa mapema.” Aliomba msamaha mama zena huku akianza kipiga magoti lakini alidakwa na Saleh na kuinuliwa.

“Mama kama imetokea hakuna budi kuchukua taadhari. Kama ugonjwa huu uliotabiliwa na mababu umesambaa basi hakuna budi kujikinga na kuwa waangalifu zaidi. Nahahidi kuanzishwa shule za watoto na watu wazima ambazo zitatoa elimu juu ya hili suara.

Malindi ya sasa itakuwa inajulikana katika kila kona duniani, japo kuwa mimi sikusoma wala kujua mengi lakini najua kabisa kuna sehemu ambazo zipo mbali na hapa tayari wana hii elimu.

Kwa mujibu wa Mganga aliyeleta taarifa, ugonjwa huu uliletwa na wale wanajeshi enzi hizo waliopigania juu ya vita vya Tegemeo. Hakuna budi kuanza kwa kusafisha njia toka hapa kupitita Msitu Malindi hadi sehemu ambazo wameelimika. Ili tulete mambo ya shule huku na watoto wetu wasome.

Njia itatobelewa kuanzia mwezi ujao hadi siku za mbeleni Malindi itakuwa taifa kubwa lenye kujitegemea….” Alimaliza Saleh.
**********

Toka hapo Malindi ikawa mfano wa utawala bora. Mapenzi ya dhati na ushirikiano wa kufa na kupona. Walijenga shule nyingi sana, hospitali na miundombinu mingine. Zote hizo zilikuwa ni jitihada za Mfalme Saleh.

Malindi ya sasa haikuwa ile ya utamaduni tena. Ikawa Malindi ya sayansi na teknolojia. Kila kitu kilikuwa pambe. Watu walisahau pombe na kunywa bia. Wakastaharibika Malindi.

Saleh alipoteza Mama na baba yake kutokana na uzee vilevile Sadiki na Zawadi pia. Saleh na Zawadi walizaa watoto wawili mmoja wa kwanza alikuwa ni Suleiman, na wa pili aliitwa Sala jina kutoka kwa Mke Sadiki.

Jambo lililoshangaza wengi ni kuwa, Saleh, Zawadi na Sadiki uzeeni walipawa na gonjwa lisilojulikana tiba yake. tabiri zilionesha ni athari za kuingia MSITU MALINDI bila kutrmbelea mizimu ya kijiji hicho. waliugua taratibu sana kipindi chao cha uzee.. hiyo haikuwa tishio. watu walishafaidi matunda yao tayari. hata walipopotea.... Mambo yaliendelea kuwa mazuri.

Maisha yakawa ya furaha na kutoweka kwa utawala wa ufalme.

Hatimaye kukawa na mfumo mpya wa urahisi. Na Suleiman mtoto wa kwanza wa Saleh akawa rahisi wa kwanza tangu kuanzishwa kwa Malindi.

‘****** MWISHO*******
XAVERY EMMANUEL LUOGA
Wasiliana nami kupitia 0672493994.
kwa maoni ushauri na jambo lolote la kufanikisha taaluma hii.
Natanguliza Shukurani kwa tuliokuwa Mwanzo hadi Mwisho....

MWISHO wa PENDO HURU ni mwanzo wa SIMULIZI nyingine.
Ahsante.

Starxav
 
Shukrani sana..... Simulizi ya ANGAMIZO inapatikana kwa Tshs 1000 tu. mwanzo hadi mwisho..
namba ya mawasiliano ni 0672493994

Karibuni...

Starxav
 
XAVERY EMMANUEL LUOGA
“PENDO HURU’
0672493994

EPISODE 24
SEHEMU YA MWIISHO..
“Chacha wajuu zangu, mesikia maneno ya kijana wetu huyu. Chacha miye ndiye namsimika chacha kuwa mfalme,. Aya tuchangilie chacha!” alikuwa ni mzee wa kimila ambaye alikabidhiwa manyanga yote ya kutawaza wafalme. Alisogeza vifaa vyake na kufanya matambiko ya awali kabla ya kumvika taji Saleh.

Naaam!, sasa Saleh ni Mfalme mpya wa Malindi. Watu walishangilia sana. Si tu walishangilia kwa kuwa walipata uongozi mpya. Hapana bali ni kufukuliwa kwa uozo ulozikwa mda mrefu sana walipata amani sana. Saleh akaaga kwa stairi ya aina yake.

“Ndugu zangu wanamalindi, mmepata Mflame mdogo sana kuwai kutokea. Leo juu ya umati huu natangaza kuwa Zawadi ndiye malkia wa Malindi.” Saleh kwa sifa akaacha kwanza watu waserebuke walipomaliza akaendelea.

“Hahaha aya bhana, pia nitumie nafasi hii kutangaza kuwa Sadiki atakuwa na mamlaka ya chini yangu na kiongozi wa miungu na mambo yote yanayohusu taaluma hiyo. Zena!, zena naye atakuwa kiongozi wa wanawake wote pamoja na kiongozi wa michezo na mashirika yote yanayohusu furaha. Mengine tutaendelea kutangaziana lakini kwa sasa. Watu wachache tutatoka hapa na kuelekea alipo Zena. Kwani naye ni mchango wa mimi kuwepo hapa. Pasi yeye basi sijui kama pendo hili lingedumu.” Mfalme Saleh aliyamaliza hayo huku akiandamana na Malkia wake Zawadi, mdogo mdogo na mataji yao kuelekea sehemu ambako Inasemekana Zena amejifungia huko.

Sadiki na wazazi wa pande zote mbili sala, na wengine walijiinga kwenda kumchukua na shujaa huyo wa kike kwa jina la Zena. Walifika. Walifika kwenye ile nyumba ambayo ipo mashambani lakini kulikuwa na kimya tu upande wa nje.

Wote walisimama kusubiri Mfalme atoe amri. Lakini haikuwa hivyo aliingia mwenyeze Mfalme. Aliingia hadi ndani.

“Zena!” aliita Saleh.

“Mungu wangu!!”. Mshituko!, Mfalme alipiga kelele kufanya waliopo nje wang’ang’ane kuingia ndani.

“Jamani!” Mama Zena aligumia baada ya kuona mtoto wake amejitundika na nguo yake juu ya nyumba hiyo.

“Khaa!” Saleh alipatwa na mshangao. Alishindwa kabisa kutoa msaada kwa Binti huyo ambaye alishaanza kuning’inia hapo kitambo kirefu tu.

“Jamani mwanangu! Hiiiiii!” Mama Zena ustahimilivu ulimshinda. Alipiga ukungu wa kufa mtu.

“Jamni mimi mwanangu kwanini umefanya hivi lakini?” Mama Zena bado alikuwa na maswali mengi sana juu ya mwanaye. Alishindwa ajibiwe lipi. Marehemu hakuwa na uhai. Alikufa mapema sana.

“Daaaah! Asee!, umekufa tu, umekufa tu zena kweli?! Bila sababu??. Aaahii!” Saleh aliungana na Mama Zena kuleta kilio Malindi.

“Hakupaswa kufa leo mwanangu. Mda bado lakini… kwanini hiviii!”

.”Mama Zena kwani kuna lolote?, Mbona ah!, mbona kama…” aliishia hapo Saleh. Aligundua kitu moyoni mwa Mama Zena.

“Jamani mimi Mwanangu, mhuuu!. Mwanangu alikuwa na Vi…. Uwii!, amewahi kufa lakini.”

“Mama sikuelewi kuna nini!” Saleh alishindwa kabisa kumwelewa Mama Zena akatoka nje kutoka na harufu ndani humo.
Mama Zena naye alitoka nje huku bado mikono ikiwa kichwani, alitingwa kabisa yani.

“Mama kuna lolote kuhusu mwaneo?” Saleh aliendelea kuhoji, aliona Mama Zena kuna kitu anatamani kuongea lakini anashindwa

“Ah!! hamna kitu baba!, ila alisema mwanangu!, alisema kabla.. alisema hana siku nyingi maana gonjwa lilianza kumtafuna.

“Gonjwa?” aliuliza Saleh kwa mshangao.

“Ndio baba. Mwanangu amepata ugonjwa wa ajabu sana. Mwanangu alikuwa njia, watu walipita tu. Mwanangu ameua wengi sana”.

“Mama kuwa muwazi basi!, sikuelewi unajua!”.

“Ah yani ni hivi, mwanangu mimi alipatwa na huu ugonjwa wa kisasa. Si unakumbuka kuna muda alitokea yule mganga na kutuonesha dalili za ugonjwa sijui. Ndo alisema unaitwa ukimwi?” alisimulia kwa kuuliza akiwa bado anababaika.

“Ukimwi?” akauliza tena Mfalme Saleh.

“Ndio baba. Mwanangu baada ya kuona kuwa gonjwa hilo halina tiba na licha kuwa alishapatwa basi akaamua kujitoa kwa kijiji kizima kwa kushiriki zinaa na kila mtu. Hakuangalia lika wala nini. Lakini hapa mwishoni alitulia kwakweli!” Mama Zawadi alizema hilo mbele ya watu waliopo pale.
Tayari askari wa Mfalme walishatoa mwili wa Zena katika ile nyumba na kumleta nje!

“Hmmm!” Saleh alihema kwa kuepuka kifo. Mama na Baba Saleh yaliwashuka. Walinywea kwa kumlazimisha Saleh amuoe Zena.

“Nisamehe baba, kwani mimi nilijua hilo na sikutoa taarifa mapema.” Aliomba msamaha mama zena huku akianza kipiga magoti lakini alidakwa na Saleh na kuinuliwa.

“Mama kama imetokea hakuna budi kuchukua taadhari. Kama ugonjwa huu uliotabiliwa na mababu umesambaa basi hakuna budi kujikinga na kuwa waangalifu zaidi. Nahahidi kuanzishwa shule za watoto na watu wazima ambazo zitatoa elimu juu ya hili suara.

Malindi ya sasa itakuwa inajulikana katika kila kona duniani, japo kuwa mimi sikusoma wala kujua mengi lakini najua kabisa kuna sehemu ambazo zipo mbali na hapa tayari wana hii elimu.

Kwa mujibu wa Mganga aliyeleta taarifa, ugonjwa huu uliletwa na wale wanajeshi enzi hizo waliopigania juu ya vita vya Tegemeo. Hakuna budi kuanza kwa kusafisha njia toka hapa kupitita Msitu Malindi hadi sehemu ambazo wameelimika. Ili tulete mambo ya shule huku na watoto wetu wasome.

Njia itatobelewa kuanzia mwezi ujao hadi siku za mbeleni Malindi itakuwa taifa kubwa lenye kujitegemea….” Alimaliza Saleh.
**********

Toka hapo Malindi ikawa mfano wa utawala bora. Mapenzi ya dhati na ushirikiano wa kufa na kupona. Walijenga shule nyingi sana, hospitali na miundombinu mingine. Zote hizo zilikuwa ni jitihada za Mfalme Saleh.

Malindi ya sasa haikuwa ile ya utamaduni tena. Ikawa Malindi ya sayansi na teknolojia. Kila kitu kilikuwa pambe. Watu walisahau pombe na kunywa bia. Wakastaharibika Malindi.

Saleh alipoteza Mama na baba yake kutokana na uzee vilevile Sadiki na Zawadi pia. Saleh na Zawadi walizaa watoto wawili mmoja wa kwanza alikuwa ni Suleiman, na wa pili aliitwa Sala jina kutoka kwa Mke Sadiki.

Jambo lililoshangaza wengi ni kuwa, Saleh, Zawadi na Sadiki uzeeni walipawa na gonjwa lisilojulikana tiba yake. tabiri zilionesha ni athari za kuingia MSITU MALINDI bila kutrmbelea mizimu ya kijiji hicho. waliugua taratibu sana kipindi chao cha uzee.. hiyo haikuwa tishio. watu walishafaidi matunda yao tayari. hata walipopotea.... Mambo yaliendelea kuwa mazuri.

Maisha yakawa ya furaha na kutoweka kwa utawala wa ufalme.

Hatimaye kukawa na mfumo mpya wa urahisi. Na Suleiman mtoto wa kwanza wa Saleh akawa rahisi wa kwanza tangu kuanzishwa kwa Malindi.

‘****** MWISHO*******
XAVERY EMMANUEL LUOGA
Wasiliana nami kupitia 0672493994.
kwa maoni ushauri na jambo lolote la kufanikisha taaluma hii.
Natanguliza Shukurani kwa tuliokuwa Mwanzo hadi Mwisho....

MWISHO wa PENDO HURU ni mwanzo wa SIMULIZI nyingine.
Ahsante.

Starxav

Demu ameacha orodha, mtaani kuna utata, na orodha inavyoonesha kuna warembo wa kusaza...

Idadi ndefu inasubiriwa, sijui ni nani wenyewe wanajinua....

Hahahaha...

Chapter Closed...



Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom