XAVERY EMMANUEL LUOGA
“PENDO HURU’
0672493994
EPISODE 24
SEHEMU YA MWIISHO..
“Chacha wajuu zangu, mesikia maneno ya kijana wetu huyu. Chacha miye ndiye namsimika chacha kuwa mfalme,. Aya tuchangilie chacha!” alikuwa ni mzee wa kimila ambaye alikabidhiwa manyanga yote ya kutawaza wafalme. Alisogeza vifaa vyake na kufanya matambiko ya awali kabla ya kumvika taji Saleh.
Naaam!, sasa Saleh ni Mfalme mpya wa Malindi. Watu walishangilia sana. Si tu walishangilia kwa kuwa walipata uongozi mpya. Hapana bali ni kufukuliwa kwa uozo ulozikwa mda mrefu sana walipata amani sana. Saleh akaaga kwa stairi ya aina yake.
“Ndugu zangu wanamalindi, mmepata Mflame mdogo sana kuwai kutokea. Leo juu ya umati huu natangaza kuwa Zawadi ndiye malkia wa Malindi.” Saleh kwa sifa akaacha kwanza watu waserebuke walipomaliza akaendelea.
“Hahaha aya bhana, pia nitumie nafasi hii kutangaza kuwa Sadiki atakuwa na mamlaka ya chini yangu na kiongozi wa miungu na mambo yote yanayohusu taaluma hiyo. Zena!, zena naye atakuwa kiongozi wa wanawake wote pamoja na kiongozi wa michezo na mashirika yote yanayohusu furaha. Mengine tutaendelea kutangaziana lakini kwa sasa. Watu wachache tutatoka hapa na kuelekea alipo Zena. Kwani naye ni mchango wa mimi kuwepo hapa. Pasi yeye basi sijui kama pendo hili lingedumu.” Mfalme Saleh aliyamaliza hayo huku akiandamana na Malkia wake Zawadi, mdogo mdogo na mataji yao kuelekea sehemu ambako Inasemekana Zena amejifungia huko.
Sadiki na wazazi wa pande zote mbili sala, na wengine walijiinga kwenda kumchukua na shujaa huyo wa kike kwa jina la Zena. Walifika. Walifika kwenye ile nyumba ambayo ipo mashambani lakini kulikuwa na kimya tu upande wa nje.
Wote walisimama kusubiri Mfalme atoe amri. Lakini haikuwa hivyo aliingia mwenyeze Mfalme. Aliingia hadi ndani.
“Zena!” aliita Saleh.
“Mungu wangu!!”. Mshituko!, Mfalme alipiga kelele kufanya waliopo nje wang’ang’ane kuingia ndani.
“Jamani!” Mama Zena aligumia baada ya kuona mtoto wake amejitundika na nguo yake juu ya nyumba hiyo.
“Khaa!” Saleh alipatwa na mshangao. Alishindwa kabisa kutoa msaada kwa Binti huyo ambaye alishaanza kuning’inia hapo kitambo kirefu tu.
“Jamani mwanangu! Hiiiiii!” Mama Zena ustahimilivu ulimshinda. Alipiga ukungu wa kufa mtu.
“Jamni mimi mwanangu kwanini umefanya hivi lakini?” Mama Zena bado alikuwa na maswali mengi sana juu ya mwanaye. Alishindwa ajibiwe lipi. Marehemu hakuwa na uhai. Alikufa mapema sana.
“Daaaah! Asee!, umekufa tu, umekufa tu zena kweli?! Bila sababu??. Aaahii!” Saleh aliungana na Mama Zena kuleta kilio Malindi.
“Hakupaswa kufa leo mwanangu. Mda bado lakini… kwanini hiviii!”
.”Mama Zena kwani kuna lolote?, Mbona ah!, mbona kama…” aliishia hapo Saleh. Aligundua kitu moyoni mwa Mama Zena.
“Jamani mimi Mwanangu, mhuuu!. Mwanangu alikuwa na Vi…. Uwii!, amewahi kufa lakini.”
“Mama sikuelewi kuna nini!” Saleh alishindwa kabisa kumwelewa Mama Zena akatoka nje kutoka na harufu ndani humo.
Mama Zena naye alitoka nje huku bado mikono ikiwa kichwani, alitingwa kabisa yani.
“Mama kuna lolote kuhusu mwaneo?” Saleh aliendelea kuhoji, aliona Mama Zena kuna kitu anatamani kuongea lakini anashindwa
“Ah!! hamna kitu baba!, ila alisema mwanangu!, alisema kabla.. alisema hana siku nyingi maana gonjwa lilianza kumtafuna.
“Gonjwa?” aliuliza Saleh kwa mshangao.
“Ndio baba. Mwanangu amepata ugonjwa wa ajabu sana. Mwanangu alikuwa njia, watu walipita tu. Mwanangu ameua wengi sana”.
“Mama kuwa muwazi basi!, sikuelewi unajua!”.
“Ah yani ni hivi, mwanangu mimi alipatwa na huu ugonjwa wa kisasa. Si unakumbuka kuna muda alitokea yule mganga na kutuonesha dalili za ugonjwa sijui. Ndo alisema unaitwa ukimwi?” alisimulia kwa kuuliza akiwa bado anababaika.
“Ukimwi?” akauliza tena Mfalme Saleh.
“Ndio baba. Mwanangu baada ya kuona kuwa gonjwa hilo halina tiba na licha kuwa alishapatwa basi akaamua kujitoa kwa kijiji kizima kwa kushiriki zinaa na kila mtu. Hakuangalia lika wala nini. Lakini hapa mwishoni alitulia kwakweli!” Mama Zawadi alizema hilo mbele ya watu waliopo pale.
Tayari askari wa Mfalme walishatoa mwili wa Zena katika ile nyumba na kumleta nje!
“Hmmm!” Saleh alihema kwa kuepuka kifo. Mama na Baba Saleh yaliwashuka. Walinywea kwa kumlazimisha Saleh amuoe Zena.
“Nisamehe baba, kwani mimi nilijua hilo na sikutoa taarifa mapema.” Aliomba msamaha mama zena huku akianza kipiga magoti lakini alidakwa na Saleh na kuinuliwa.
“Mama kama imetokea hakuna budi kuchukua taadhari. Kama ugonjwa huu uliotabiliwa na mababu umesambaa basi hakuna budi kujikinga na kuwa waangalifu zaidi. Nahahidi kuanzishwa shule za watoto na watu wazima ambazo zitatoa elimu juu ya hili suara.
Malindi ya sasa itakuwa inajulikana katika kila kona duniani, japo kuwa mimi sikusoma wala kujua mengi lakini najua kabisa kuna sehemu ambazo zipo mbali na hapa tayari wana hii elimu.
Kwa mujibu wa Mganga aliyeleta taarifa, ugonjwa huu uliletwa na wale wanajeshi enzi hizo waliopigania juu ya vita vya Tegemeo. Hakuna budi kuanza kwa kusafisha njia toka hapa kupitita Msitu Malindi hadi sehemu ambazo wameelimika. Ili tulete mambo ya shule huku na watoto wetu wasome.
Njia itatobelewa kuanzia mwezi ujao hadi siku za mbeleni Malindi itakuwa taifa kubwa lenye kujitegemea….” Alimaliza Saleh.
**********
Toka hapo Malindi ikawa mfano wa utawala bora. Mapenzi ya dhati na ushirikiano wa kufa na kupona. Walijenga shule nyingi sana, hospitali na miundombinu mingine. Zote hizo zilikuwa ni jitihada za Mfalme Saleh.
Malindi ya sasa haikuwa ile ya utamaduni tena. Ikawa Malindi ya sayansi na teknolojia. Kila kitu kilikuwa pambe. Watu walisahau pombe na kunywa bia. Wakastaharibika Malindi.
Saleh alipoteza Mama na baba yake kutokana na uzee vilevile Sadiki na Zawadi pia. Saleh na Zawadi walizaa watoto wawili mmoja wa kwanza alikuwa ni Suleiman, na wa pili aliitwa Sala jina kutoka kwa Mke Sadiki.
Jambo lililoshangaza wengi ni kuwa, Saleh, Zawadi na Sadiki uzeeni walipawa na gonjwa lisilojulikana tiba yake. tabiri zilionesha ni athari za kuingia MSITU MALINDI bila kutrmbelea mizimu ya kijiji hicho. waliugua taratibu sana kipindi chao cha uzee.. hiyo haikuwa tishio. watu walishafaidi matunda yao tayari. hata walipopotea.... Mambo yaliendelea kuwa mazuri.
Maisha yakawa ya furaha na kutoweka kwa utawala wa ufalme.
Hatimaye kukawa na mfumo mpya wa urahisi. Na Suleiman mtoto wa kwanza wa Saleh akawa rahisi wa kwanza tangu kuanzishwa kwa Malindi.
‘****** MWISHO*******
XAVERY EMMANUEL LUOGA
Wasiliana nami kupitia 0672493994.
kwa maoni ushauri na jambo lolote la kufanikisha taaluma hii.

Natanguliza Shukurani kwa tuliokuwa Mwanzo hadi Mwisho....
MWISHO wa PENDO HURU ni mwanzo wa SIMULIZI nyingine.
Ahsante.
Starxav