XAVERY LUOGA
“PENDO HURU’
0672493994
EPISODE 17
SEHEMU YA NANE
Saleh na Zawadi waliamua kutoweka kabisa kijijini, waliamua kabisa kuachana Malindi na kutaka kukimbilia kijiji cha mbali. Kijiji cha Malindi kilikuwa na ukubwa wa aina yake. Huwezi kutoka ndani ya kijiji hicho kirahisi rahisi.
“Mpenzi, ni kweli njia ndio hii?” Zawadi alianza kuwa na mashaka juu ya njia iliyopo mbele yao.
Ni kweli walikuwa mbali na Malindi lakini, njia iliyopo mbele yao ilionesha kutisha. Msitu wa Malindi ulikuwa mbele yao. Kwa historia ya mwanzo Saleh alishawai ambiwa na Mama yake kuwa Msitu huo ndio alama ya Udhaifu wa Kijiji chao. Mambo mengi maovu hutendeka mwanzoni tu mwa mistu huo.
Toka histora ya Malindi ishike hatamu haijawai sikika mtu wa aina yoyoyte kuvuka salama katika mistu huo kutokea upande wa pili, hii ni juu ya kutisha kwa mistu huu wa asili.
Ilisemekana ndani ya msitu huo, kuna wanyama wakali sana na mambo ya ajabu ya kutisha. Kabla ya kutoka sehemu ya mwanzoni mwa mistu huo kuna bango kubwa la kuonesha taadhari juu ya mistu huo wa Malindi.
“Zawadi!, hakuna njia, hatuma imani tena na maisha yetu. Bora wewe Zawadi unaweza samehewa, vipi kuhusu mimi? Sina budi kufa kishujaa ndani ya mistu huu lakini si kupata mateso yale niliyokimbia. Zawadi, Nakupenda. Tuwe na imani tu. Tukaishi mbali hiki sio kijiji. Baba yako ni mtu mbaya sana Zawadi” Saleh alionesha yupo katika fikra za kuikimbia Malindi. Mateso aliyopata kutoka kwa Ibo na Mfalme yalikuwa sababu tosha kwa Salah kuondoka.
“Nipo tayari tufe wote Saleh, sina nguvu kwako!” Zawadi naye akajimwaga kifuani kwa Saleh, wakakumbatiana kwa kuianza safari mpya ya kuvuka misitu na kuishi mbali.
Mapenzi yao yalikolezwa na imani ya kweli ya upendo. Zawadi alikubali kuvua taji ya umalkia na kulitupilia mbali. Saleh naye hakuona umuhimu wa Wazazi, hakuwafikilia hata kidogo. Jamani mapenzi kigeugeu!!.
Naaam Miguu yao sasa ikawa ndani ya mistu wa Malindi, misitu wenye historia ya kutisha kijijini kizima. Kila mtu alijua fika kuvuka katika mistu huo ni hatari mno hata kujaribu tu.
Sasa roho za Saleh na Zawadi walikabidhi kwa Mababu zao wawasimamie na kutokea upande wa pili, angali katika historia hakuna aliyewahi kuvuka msitu huo. Malindi ilikuwa Malindi kweli. Kijiji kizima kilivikwa na Msitu Malindi.
Waliipita miti kadhaa kuchanja mbuga kwenye msitu huo. Ilikuwa miti ya wastani, miti halisi kabisa ya kuwakaribisha wageni wote kwa bashasha ya aina yake. Uzuri wa msitu huo ulionekana tu kwa kelele na shangwe za ndege wake kuruka juu kwa kidedea.
kulikuwa hakuna ule upepo unaosemwa na wakazi wa eneo la Malindi kwamba katika msitu huo kuna upepo mkubwa sana. Kulikuwa kimya na hewa ya oksijeni ambavyo vilipokezana tu kuhema.
Zawadi alikuwa mgeni wa kila kitu, alikuwa mtu wa kushangaa tu kila hatua ambayo wanasonga mbele. Msitu ulikuwa ni wa kuvutia hadi kuwafanya kusahau shida za walikotoka.
Walizidi kusonga mbele bila kujali kigiza ambacho ndio kwanza kinaanza kukimbiza mwanga wa jioni kuelekea usiku. Hatua ya Saleh iligusa kitu cha ajabu chini lakini akapotezea na kusonga mbele. Hakutaka kumtisha mpenzi wake kwa kile ambacho amekiona. Wakasonga mbele.
Punde tu Saleh akaona tena kitu cha kutisha, Alichokiona sasa kilikuwa ni mfano halisi wa kile alichokiona mwanzo. Mwanzo aliona fuvu la kichwa cha binadamu, lakini kwa sasa aliona mwili mzima wa binadamu ambao haukuwa na muda mrefu toka utelekezwe. Kwa kutishwa na kitu hicho bado alikuwa na ujasiri wa kumzuia Zawadi asione anachoona yeye. Malindi ilikuwa na maovu nyuma ya panzia, hakuna anayejuwa.
Hatua kwa hatua, huku Saleh kule Zawadi, wote walijitosa katika msitu huu kutafuta njia ya kutoweka Malindi. Hawakujua ukubwa wa msitu ni udogo wa maisha yao. Wakasonga mbele.
“Mamaaaa ah!” ilikuwa sauti ya Zawadi ambayo ililenga kushitushwa na jambo. Mbele ya macho ya Saleh na Zawadi kulikuwa na mizoga mingi sana ya binadamu. Wengi walikuwa wameoza na kubaki mafuvu tu na wengine ndio kwanza wabichi, hawakufua hata dafu ya kuozeana kwa wiki mbili tu. Walikufa angali bado mvua yanyesha. Hawakukauka. miili yao ilikua bado mibichii.
Kilio cha nguvu kikamtoka Zawadi akiwa kifuani mwa Saleh, alijificha kutoona unyama ule wa aina yake.
“Saleh me siwezi!, naogopa!!” Zawadi aling’ang’ana kwa kuomba Saleh afanye jambo ambalo halita mfanya apoteze roho yake mapema kiasi kile. Tamaa ya kurudi nyuma ikaingia..
“Phoooooooo!, Phoo Phonhoooooo!” sauti ya pembe la ngombe ikasikika nyuma yao.
“Wanatutafuta!” Zawadi akaacha kulia ghafla na roho ya ujasili ikamwingia, katu hakuangalia tena ile mizoga ya watu waliotelekezwa pale, akamshika mkono Saleh na kwenda mbele, alijua kabisa sauti ya pembe hilo la Ng'ombe hutumiwa na Ibo ty. tena sehemu za hatari.
“Saleh!!, wakitushika hawa watatufanya kama hawa watu hawa chini. Tukimbie jamani.” Zawadi alizidi kumshika Saleh na kumkokota kama anamlazimisha kukimbia.
Moyo wa Saleh ulishikwa na machungu mazito mara baada ya kuona kuwa mauti ya mamia waliotelekezwa. Mwili mzima ulikufa ganzi. Alikokotwa tu na Zawadi.
Walikimbia mno kuwapoteza wanaowatafuta. Zawadi alishajua mlio ule wa pembe la ngombe ni kuwa kuna watu wanawatafuta na wapo karibu yao, lengo lao la kipiga pembe hilo ni kuwa waliona ishara za watu wanaowatafuta kando, hivyo walipiga ili wakusanyike kwa lengo la kutembea pamoja kwani wapo karibu kuwakamata. Zawadi alijua hili. Alichukua hatua ya kukimbia na Saleh, kufa au kupona kwake. Lazima watoke Malindi.
Kwa binadamu ambaye damu ndio chanzo chake cha uhai, lazima achoke. Binadamu sio mashine. Hiyo iliwakuta wapendanao hawa Saleh na Zawadi ambao walibweteka katika kichaka kimoja ambacho wote waliona salama kujificha walishafika kukaribia nusu ya safari ya kuvuka msitu wa Malindi.
Usiku tayari ulishakaribia katika mboni za binadamu hawa. Kwa mbali waliona watu wanakuja upande waliojificha wao. Walikuwa wamebeba miale ya moto kuwatafuta kwa udi na uvumba.
Walikuwa wanaume wengi sana na wa kutosha. Wote walishiba kisawasawa, lakini hawakutisha sana kama alivyotisha Ibo. Ibo alikuwa haonekani kabisa kwa weusi wake. Japo alikuwa kiongozi wa msafara lakini hakuonekana. Alikuwa mweusi pyuu! Ibo. Ilo hakujali, alichojali ni kupatikana kwa mwandani wake Zawadi na mbaya wake Saleh. Wote walikuwa wanahitajika kwa nyakati mahususi kabisa.
Walisogea na miale yao ya moto hadi kando na walipo Saleh na Zawadi. Kizuri hadi wakati huo hawakuonekana.
Mioyo yao ilikuwa inadunda mno utadhani ng’ombe wa Shinyanga ambaye anachinjwa kutokana na shida ndogo tu, 'Sherehe ya mtoto', Walikuwa ni wasumbufu wa roho. Walihemeana wao kwa wao bila kuruhusu pumzi zao kufikiwa na watu waliopo karibu yao. Vifua vilibana na kuachia... wote walidhibiti pumzi zao kwa Makini...
.........

FUATANA NAMI KATIKA SEHEMU YA KUMI NA NANE YA MKASA HUU...
SAYARI YA SIMULIZI 🗺
ITAENDELEA
Starxav