Mtunzi: XAVERY LUOGA
Simulizi: “PENDO HURU’
Namba: 0672493994
EPISODE 12
“Mimi nilikuwa tu nasikia akilalamika usiku wa kuamkia leo, eti oh!, mimi simpenzi Ibo sijui, mimi sijui nampenda Saleh sijui!...”
“Kelele!” Tatari alishashusha kibao Mfalme. Aliona Mke wake anaongea upuuzi. Tena upuuzi wa viwango wa juu. Akamuwasha kofi. Kilio kikashika hatamu. Nyumba ikatikisika. Mama Zawadi alikuwa katika kipindi kigumu kutetea penzi la mtoto wake.
*********
Zawadi yeye alishafika kando ya Bustani ya kina saleh. Ni pale pale kwenye lile jiwe ambalo aliwafuma Saleh na Zena wakifanya uzinzi. Kwa kuwa haikuwa siku ya kazi. Saleh na Sadiki walikuwepo hapo kubadilishana mawazo.
“Sa.. Saleh!” Zawadi aliwashitua wawili hao pale walipo. Sadiki ataachaje kutabasamu. Akakohoa tu na kumkalibisha.
“Zawadi, heshima kwako!. Mbona hata wapambe huna!. Vipi kuhusu usalama wako?”
“Jamani Sadikii hongera kaka angu kwa kipaji. Nilifurahi sana jana!, mimi hata sitaki vya ulinzi, wananinyima amani. Na piaa nilitaka niwe huru” akajibu Zawadi akikaribia karibu na walipo Sadiki na Saleh.
“Asante bhana, tunajitahidi hivyo hivyo, hakuna namna hapo Zawadi. Lakini mhhh!, nawe. Unajua ni hatari sana bila hata mlinzi mmoja na kulivyo mbali huku!”
“Usijali!!, vipi Saleh!, mbona kimya sana!” Zawadi alimshitua Saleh ambaye alikua anaonesha sura ya aibu. akikumbuka kwa jinsi alivyofumaniwa siku hiyo. Sadiki akaona awaache wazungumze.
“Konho! Mhu mhu!, sasa Saleh. Ngoja nikusanye haya majani hapa!” Sadiki alitafuta gia ya kutokea.
“Hii jamanii, unatukimbia!”
“Hapana Zawadi!” aliyasema hayo akiwa ameshapiga hatua. Alitoweka Sadiki.
“We mwanume!, mambo!” alianzisha mazungumzo Zawadi.
“Zawadi!, Nashindwa hata niongee nini mbele yako Malkia!” alijitosa Saleh. Moyo wake ulimsuta sana kutamka maneno ambayo kwa upande wake yalikuwa mazito haswa.
“Zawa..” alitaka kuongea tena Saleh.
“Shiii!!!!” Zawadi hakuruhusu hata Saleh ajieleze. Alishajua anatoka kuomba samahani kwa kitendo alichokutwa anafanya na Zena.
“Saleh!, nimeumia sana kwa kipindi kirefu. Naona unachelewa kusema!. Mimi nakupenda Saleh!” Zawadi akajimwaga. Alikuwa mwingi wa tabasamu usoni. akaweka aibu na mambo ya tamaduni kando. akavunja mwiko kusema ukweli.
Saleh aliisi mapicha picha ya marehemu Bruce lee!, yanakaribia kumuumbua. Alihamaki sana kwa mtoto wa kike kama yule kutangaza Alleluya kuu adharani.
“Zawadi!” Saleh akaita kwa mshituko. Alijua Zawadi amevunja amri za mababu. Lakini akanyamazishwa tena.
“Saleh!, huna cha kunidanganya jamani!. Nakupenda sana na haijalishi, haijalishi Saleh nakupenda.” Sasa Zawadi aliona anachoongea aeleweki akapandisha sauti,ili miti, mawe, milima, mito na viumbe vilivyo hai vimsikie.
“Nakupenda Saleh!!” kitendo kilimshangaza sana Saleh. Hata Sadiki ambaye hakuwa mbali sana na eneo hilo, neno nakupenda alilisikia. Ataachaje kughuna sasa. Alighuna Sadiki na kuendelea na mambo yake.
“Zawadi, samahani, nimeshindwa kuwa wa kwanza kukuambia kuhofia Baba yako?”
“Kwani unampenda Baba? au mimi?” akaulizwa swali lililo mbabaisha. Likamyumbisha na kumweka sawa.
“Aaah! Yaani..” alikosa cha kuongea Saleh. Alikuwa anatetemeka kama ile tetemeko ya kipindi kile kule Japani.
“Za..wa..di.. di.” Hakutamka vizuri neno hilo tayari walikuwa sayari nyingine. Kwa mara ya kwanza tangu azaliwe kristo katika karne za mwanzo. Mtoto wa Mfalme anagawa penzi kwa Saleh. Ilikuwa mara ya kwanza kwa Zawadi kuchanganya mate na kiumbe kingine chenye uhai. Lakini mara ya pili kwa Saleh kumimina kimimika chake kwa Mwana feki wa Mfalme. Ilikuwa ni vaisivesa.
Walishikana kisawasawa ili wasiache mapema wanachokifanya. Aibu ikanishika mtazamaji. Nikasogea kando kuwaacha wawe huru. Wafanye wee hadi wachoke. Wakanyonyana hadi kuishiwa. Wakawa kando kando wakichokeana. Walikuwa palepale katika jiwe la Ushindi. Jiwe lililo na upako kwa Saleh. Jiwe lenye bahati ya kumkutanisha na wanawake wawili tofauti.
“Najiskia huru sana leo Mpenzi!” ilikuwa kauli ya Zawadi pembeni mwa Saleh. Walikuwa bado wamekumbatiana na kuruhusu sauti zao zibishane masikioni. Zote zilikuwa na maneno matamu. Ziliwaiingia haswa juu ya penzi lao huru na changa. Mambo yakawa moto na kuacha majivu Malindi. Kamayalivyo matanga. Matanga bhana huja baada ya msiba. Ukatokea msiba mzito kando yao. hakuna aliye amini.
“Heiiiiiyi!!” ulikuwa mshituko wa sauti nzito wa kuogofya. Sauti kali kutoka kwa ndugu Ibo. Mtu katili na jasiri kwa wakati mmoja. Mtu aliyebeba alama ya hatari Malindi. Mtu pekee awezaye kubeba umati wote wa Malindi begani bila kuumia. Alikuwa Ibo kando yao. Wakaachana Saleh na Zawadi, Saleh alikua anatetemeka tu,.
“Kamata wote!!” akatoa amri katika jeshi lake alilokuja nalo kuwatafuta.
Hawakuwa mbali, tayari walikuwa mikononi mwa utawala mpya wa Mfalme. Nafsi ya Saleh iliongea na nafsi ya mama yake huku ikimkumbusha tu, “Si nilikuambia mwanngu!”. Akafumba macho kuacha lolote litokee juu yake. Ashapenda. Yupo tayari kutokwa uhai. Wakashikwa wote wawili.
“Tuachee!” sauti ya Zawadi ilimfanya Sadiki naye asogee sehemu ya tukio. Alichungulia tu kuona kwa jinsi rafiki yake anavyotiwa nguvuni na kuondolewa mahali hapo. Supu ilishaingia nzi tayari. Alileta kirusi cha magonjwa. Hakuna budi kuimwaga. Akaacha waondoke!. Katu hakujitokeza Sadiki.
Walitoka mkukumkuku na Saleh na Zawadi kama watu walioshikwa ugoni. Moja kwa moja wakakatisha vichochoro hadi barabara kuu, mwendo wa haraka kuifuata kasri ya Mfalme. Uharaka wao uliendana na kasi ya muda. Walifika muda muwafaka. Walipitiliza mpaka ‘tiii’ kwa mfalme.
“Mbona wawili!, au ndiye mshauli wa kutoroka kwa mwanangu?” alihoji mfalme kwa ukakasi.
“Tumewakuta huko, wamekumbatiana, kijana rafiki wa yule mshindi.. nani…!, Sadiki. Huyu anaitwa Saleh!” alimaliza Ibo. ulikua utambulisho usio na maneno mengi.
“Saleh!!” alirudia jina lile Mfalme.
“Ndio Mtukufu Mfalme.”
“We mtoto!, ni kweli wewe ndio Swalehe?” aliita Mfalme huku akiita jina jingine kabisa kurahisisha matamshi.
“Ndi.... ndio, ndio Mtukufu!”. alijibu Saleh.
“Shwaaaah!” kofi likasikika.
“Wewe ndio unaniharibia mtoto wangu?!, mwanaharamu wewe!” Mfalme sasa alikuwa na jazba. Alitamani kumkula kabisa Saleh. Huyu ndio mtibua mpango. Kipingamizi kikubwa hiki kwa penzi la Binti yake.
“Baabaaa!, Mwache Saleh jamani. Sio kosa lake, niadhibu mimi” Zawadi akatoa neno la msaada, halikusaidia.
“Kelele!!” Mfalme alikuwa moto kwelikweli, hakuna alichosikia. Mama Zawadi alishafungiwa ndani. Alikuwa anachungulia tuna na kulia chinichini. Hakuwa na la kufanya. alijutia zile dadika kumi alizotoa zimegeuka vita vya Mapezi Malindi.
“Zawadi umekuwa Malaya sana!, umenipaka matope tayari umeni..ni..ni…” Uzee alimfanya mfalme kuwa legevu, alitumia nguvu nyingi sana kuongea na kufanya aliyoyafanya. Mfalme aliitaji msaidizi. Akashusha sauti yake.
“Kwahiyo huyu ndio unampenda eh!” aliuliza kwa mtego.
“Ndio Baba nampenda Saleh. Nampenda. Nipo tayari ku-u-u-faa!” Zawadi aliweka bayana. Mfalme akachoka. Akashindwa nini afanye juu ya aibu hii ambaye mtoto wake ameionesha mbele ya Ibo mwenyewe.
“Mwanangu chagua moja!, kuolewa na ninayemtaka mimi au nimuue huyu Saleh na uolewe kwa lazima”. Akapewa njia ya kupita. Zote zilikuwa zina miba kwake. Akalia sana Zawadi hakuna kilichomtoka mdomoni.
“Toa wote kafungie huko. Baada ya masaa ishilini na nne watabadili maamuzi” mfalme alitoa agizo kwa kijana wake kuwa akawaweke vijana hao sehemu ambaye itawafanya siku ya pili yake kubadili maamuzi yao. Aliwaamuru wapelekwe eneo la mateso.
Naaam!, baada ya muda tu tayari Ibo alishawafunga kila mmoja wao sehemu yake. Aliwatenganisha Saleh na Zawadi, ilikuwa ni oda kutoka kwa mfalme.
“Saleh nilikuonya wewe!, ukawa mbishi. Sasa umeingia katika kumi na nane zangu. Hakika nakuhaidi hata kama mfalme atakuacha hai, mimi sitafanya hilo jambo. Utakufa mikononi mwangu Saleh. Zawadi ni wangu, mimi ndiye mmiliki halali wa hii himaya. Huna kitu Saleh” yalikuwa ni maneno ya Ibo akiwa anamfunga kamba mikono yake juu ya mti Saleh.
Lilikuwa ni eneo kwaajili ya mateso. Eneo ambalo Lilikuwa lipo kama magereza kwa watu wanaovunja sheria na kumkosea Mfalme. Huko ndiko walikoozea Saleh na Zawadi. Wote walifungwa, haikujalisha nani na yupi. Unacheo gani au huna cheo. Wote walifungwa, Saleh akifungwa sehemu ambayo ilikuwa inatope chini la kutosha. Zawadi yeye alifungwa katika chumba chake. Chumba maalumu kabisa kwa ajili ya mateso ya watoto wa kike. Walitelekezwa huko pasi na msaada...

Naaaam, Malindi inateketea kwa Moto. Nini Zena atafanya akisikia Saleh na Zawadi wameshikwa pamoja?, Je baba na Mama Saleh watapokeaje hizo taarifa, wapenzi wawii wapo katika Mateso ya saa ishirini na nne kujiuliza kuhusu penzi lao. hakika "Pendo Huru"...
*******
ITAENDELEA EPISODE 13
Join Group

SAYARI YA SIMULIZI 🗺
like, Comment and Share...!
Starxav