SIMULIZI: Nisamehe Grace

SIMULIZI: Nisamehe Grace

NISAMEHE GRACE - 14



Ilipoishia….

Baada ya kula nilijitupa kitandani na kujipumzisha huku nikipanga kesho yake asubuhi nianze ile kazi ya kumtafuta kipenzi changu Nairath pamoja na wale watoto wangu wawili.

Songa nayo…

Kile kitendo cha kushiba na kujitupa kitandani ndani ya ile hotel ya Gulf of Oman kilifanya nilale usingizi mzito sana kwa sababu ya ule uwingi wa uchovu niliokua nao ambao ulitokana na urefu wa ile safari yangu ya kutoka nchini Tanzania mpaka kufika nchini humo.
kiukweli ulikua ni usingizi mzito sana kwani nakumbuka nilikuja kuamka majira ya saa 3 za asubuhi na kukuta tayari kukiwa kumekwisha pambazuka.
baada tu ya kuamka nilienda moja kwa moja mpaka bafuni kuoga na kubadilisha nguo zangu kisha nikaagiza chai na mara baada ya kuinywa na kuimaliza nilichukua vile vielelezo vyote muhimu vya Nairath nilivyopewa na yule mamdogo wake kule masaki, ikiwemo namba ya yake ya simu, picha zake, pamoja na anuani yake na kisha nikaianza ile kazi yangu ya kumtafuta Nairath ambaye mpaka wakati huo alikua amelazwa katika hospitali ya Good health ambayo kutokana na maelezo ya yule mamdogo wake hospitali hiyo haikua mbali sana na nyumbani kwa wazazi wake na Nairath.
ilikua ni majira ya saa 4 asubuhi muda nilio ianza ile kazi ya kumtafuta Nairath kwani baada tu ya kutoka mle hotelini Gulf of Oman nikiwa pamoja na vile vielelezo mkononi nilienda moja kwa moja mpaka sehemu vilipokuwepo vituo vya tax.

‘Hey can you rush me to Good health hospital?’
(unaweza kunikimbiza Good health hospitali)
nilimuuliza dereva tax niliyemkuta kituoni.

‘Yea, why not’(ndio kwanini niseweze) alinijibu.
‘It cost how much’(inagharimu sh.ngapi) nilimuuliza.
‘50 dollars only’(dola 50 tu,sawa na tsh elfu 80) alinijibu.
‘Ok lets go’(sawa twende) nilimwambia huku nikiingia ndani ya tax.

Safari ya kuelekea hospitali ya Good health ilianza huku ule uwingi wa watu waliokua wakikatiza na kupita barabarani ukimfanya yule dereva aliyekua na asili ya kiafrika aendeshe gari polepole sana na kwa umakini mkubwa kitu kilichofanya niitumie fursa hiyo kuutazama na kuufaidi uzuri wa jiji hilo la Musqat lilionekana kujengeka na kuzawadiwa wanawake warembo sana ambao walisababisha nishindwe kujizuia kuyatua macho yangu juu ya nyuso zao na kufaidi uzuri wa sura zao ambazo kwa asilimia kubwa zilikua zimesitiliwa na vazi la hijabu.

‘you are looking like a stranger here’(unaonekana kama mgeni hapa)
yule dereva aliniuliza na kuukatisha ule ukimya uliokua umetawala ndani ya gari mara
baada ya kugundua kua nilikua nikiutazama sana ule mji.

‘Yes I am stranger’(ndio mimi ni mgeni) nilimjibu.
‘Where do you come from?’(umetokea wapi) aliniuliza.

‘Im from Tanzania’(nimetokea Tanzania) nilimjibu.
‘Tanzaniaaa’ aliniuliza kwa mshangao.

‘Yes Tanzania’(ndio Tanzania) nilimjibu tena.
‘I am a Tanzanian too’(mimi pia ni mtanzania) yule dereva aliniambia.

‘Can you speak Swahili?’(unaweza kuongea kiswahili) nilimuuiza.
‘Yeah I can’ (ndio ninaweza) alinijibu ambapo baada ya kunijibu tulianza kuongea kiswahili na kupiga stori nyingi sana kana kwamba tulikua marafiki wa muda mrefu hadi tulipofika pale hospitalini Good health.
tulitumia muda wa zaidi ya dakika 45 mpaka kufika pale hospitalini Good health ambapo baada kufika nilimlipa yule dereva hela yake lakini kwa uwingi wa wema na ukarimu wa watanzania alikataa kuzipokea na kusema kua amenisaidia kama ndugu yake na pia aka ahidi kunisubiri mpaka nitakapomaliza shida zangu pale hospitali ili aweze kunirudisha tena mpaka kule Musqat mjini.
nilishuka garini na kumuacha yule dereva akinisubiri kama alivyoniahidi kisha kwa mara ya kwanza nikaanza kupiga hatua zangu kuingia ndani ya ile hospitali ya Good health iliyokua imejengwa kisasa na kwa ustadi mkubwa kiasi cha kufanya uzuri wake ushindwe kutofautiana sana na uzuri wa ile hospitali ya Guangzhou ya kule nchini China sehemu alipokua amelazwa Grace muda mrefu sana uliopita.
niliingia hadi ndani hospitalini na kwenda moja kwa moja mpaka sehemu ya mapokezi na kukuta wadada wawili wakiwa wamevalia sare nyeupe.

‘Hii I’m Javier Hernandez, niliwasalimia wale wadada wawili mara baada ya kuwafikia na nikawakabidhi zile picha za Nairath kisha kwa kutumia lugha ya kingereza nikaanza kuwaambia kwa ufupi yale matatizo yote yaliyonikuta mimi pamoja na Nairath tokea siku ya kwanza tulipokutana pale chuoni St.Anna hadi wakati huo nilipokua pale hospitalini Good health.
kiukweli yale matatizo yangu yalionekana kuwagusa sana na kufanya washindwe kujizuia kulengwa na machozi ya huzuni kitu kilichosababisha niamini kuwa warabu walikua ni wepesi sana wa kulia.
kitendo cha wale wadada kuanza kudondokwa na machozi ya huzuni kilifanya nimalize zaidi ya dakika 2 pale mapokezi bila ya wao kunijibu wala kunisemesha neno lolote lakini ghafla wakiwa katika kulia kwao mmoja wao alianza ku type jina la Nairath Fa-thiya ndani ya ile kompyuta kubwa ya hapo mapokezi na ndani ya muda mchache majibu yote yaliyoendana na kufanana na ile searching aliyoifanya yalikuja na kufanya waanze kuniambia kila kitu juu ya Nairath kuanzia siku alipoenda pale hospitalini hadi wodi aliyolazwa pamoja na maendeleo yake ya kila siku.
lakini licha ya wema wote huo pamoja na kuguswa kwao wale wadada walinikatalia kwenda kumuona Nairath wodini mpaka nitakapo ruhusiwa na ndugu wake wa karibu kama utaratibu wa hospitali hiyo ulivyokua unasema.

Kitendo cha wale wadada wa mapokezi kunikatalia kwenda kuingia wodini kumuona Nairath na kushindwa kuambia ugonjwa uliokua ukimsumbua pamoja na maendeleo yake kilionekana kunitisha sana na kufanya niingiwe na wasiwasi mkubwa kua pengine huenda hali yake ikawa mbaya zaidi ndio maana walikua wakinificha.
lakini sikua na jinsi zaidi ya kukubaliana na hali halisi kua ni lazima nisubirie ruhusa kutoka kwa ndugu zake wa karibu na Nairath ambao bila shaka walikua ni wazazi wake mama pamoja na baba yake.

Nilitoka pale mapokezi kwa huzuni na uchungu mkubwa na kurudi mpaka kwa yule rafiki yangu dereva tax ambaye nilimkuta akiwa ananisubiri kama alivyoniahidi hapo awali.
nilimuomba radhi kwa sababu ya kumchelewesha baada tu ya kumfikia kisha nikamueleza uhalisia wa ile hali kua ni lazima nisubiri hospitalini hapo kwa zaidi ya masaa matatu mpaka wazazi wake na Nairath watakapokuja kumuona binti yao ndipo waweze kunipa ruhusa ya mimi kuungana nao kwenda kumuona yule kipenzi changu.

‘Sikiliza mimi ni mwenyeji sana hapa Oman hebu nenda kawaombe location pamoja na namba ya nyumba ya wazazi wake ili tuwafuate huko kuliko tusubiri hapa maana hayo masaa matatu ni mengi sana’
yule rafiki yangu mpya dereva tax aliniambia.

‘Ooh ni wazo zuri sana, tena nimekumbuka kila kitu ninacho’ nilimjibu kwa furaha huku nikimkabidhi ile anuani niliyopewa na yule mamdogo wake na Nairath kule masaki siku chache zilizopita.

Baada ya kumpa ile anuani aliisoma na kuniambia kua huo mtaa haukua mbali sana na kutoka pale hospitalini ni kama mwendo wa dakika 10 hadi 15 kwa gari napo inategemea na uwingi wa watumiaji wa barabara kwa siku hiyo kwani wakiwa wachache inaweza isizidi hata dakika 7 hadi 8.
nilijikuta nikimshukuru sana yule dereva tax rafiki yangu mpya hasa kwa sababu ya kujitolea kwake kunisaidia kwani alipoisoma tu ile anuani tuliingia ndani ya lile gari lake na kuanza kuelekea sehemu walipokua wakiishi wazazi wake na Nairath huku nikimuomba Mungu njia nzima kua anisaidie wale wazazi wasije wakanigombeza kwa sababu ya yale yote niliyoyafanya hadi ku sababisha matatizo yote hayo.

Tulifanikiwa kufika salama mpaka nyumbani kwa wazazi wake na Nairath kwa msaada mkubwa wa ile anuani.
tulibisha hodi mbele ya mlango mkubwa wa nyumba hiyo iliyoonekana kuwa na uzuri wa aina yake na kuueleza wazi kabisa uwezo na utajiri waliokua nao bwana na bibi Fa-thiya wazazi wa Nairath.
haikupita muda mlango ule ulikuja kufunguliwa na binti mmoja aliyeonekana kufanana sana na Nairath akaonekana kusimama mbele yetu ambapo baada ya kumueleza shida yetu alitukaribisha ndani ya nyumba hiyo kwa ukarimu mkubwa sana kutupeleka moja kwa moja mpaka sebuleni na kumkuta mama mmoja wa makomo ya kati ya umri wa miaka 40 hadi 55 akiwa anacheza na watoto wawili wazuri sana waliokua na ngozi nyeupe ya kuvutia na yenye kung’aa sana huku yule mtoto wa kike akionekana kufanana sana na mimi kitu kilichofanya nisihitaji hata akili ya memkwa kujua kua walikua ni watoto wangu Javier Hernandez pamoja na Grace Hernandez.

Kitendo cha kuwaona wale watoto wangu kwa mara ya kwanza kilinifanya nishindwe kuizuia furaha yangu kubwa iliyonipata ghaflaa kwani bila hata kumsalimia yule mama tuliyemkuta pale sebuleni nilipaza sauti yangu kwa nguvu na kuwaita wale watoto majina yao Javier na Grace kwa kilio cha furaha huku nikiwasogelea kwenda kuwakumbatia.

….itaendelea….

ABCDEFGHIJKLMNOPQRSTUVWXYZ
 
NISAMEHE GRACE - 15



Ilipoishia…..

Kwa mara ya kwanza niliwaona watoto na kwa furaha kubwa nikawakimbili na kuwakumbati huku nikiwaita majina yao pasipo hata kumsalimu yule mama niliyemkuta akicheza nao.

Songa nayo…

‘Javier and Grace Hernandez I love you so much my kids’ nilisema kwa furaha huku nikiwakimbilia wale watoto na kuwakumbatia pasipo hata kumsalimu yule mama niliyemkuta akicheza nao pale sebuleni kitu kilicho mshtua sana.

‘who are you?’(wewe ni nani) yule mama aliniuliza kwa mshangao.

‘Im a father of those two kids’(ni baba wa hao watoto wawili) nilimjibu.

‘youre a Javier Harnandez, the one who betray our daughter?’
(wewe ndiye Javier Hernandez, uliyemsaliti binti yetu) aliniuliza kwa sauti kubwa yenye kujaa ukali ndani yake huku akiwachukua wale watoto kutoka mikononi mwangu na kuwakalisha kitini kitendo kilichoniumiza sana na kuiharibu ile furaha kubwa niliyokua nayo.

Sauti yake ya ukali ilimfanya baba yake na Nairath mzee Al-jabri Fa-thiya atoke chumbani mwake na kuja mpaka pale sebuleni tulipokua tumekaa ambapo alianza kuniuliza maswali mengi mazito huku akinigombeza kwa kwa ukali mwingi sababu ya yale yote niliyofanya juu ya binti yao mpaka kusababisha matatizo yote hayo kutokea.
mzee Fa-thiya na mkewe walinigombeza sana hawakutaka kuniona kabisa mbele ya macho yao wala ndani ya nyumba yao kwani walidiriki kunifukuza mimi pamoja na yule rafiki yangu dereva tax ambaye muda wote huo alikua amekaa kimya huku kile kitendo chao cha kuanza kuongea kiswahili kikionekana kunipa mwanya wa kujitetea.

‘naombeni mnipe nafasi ya kuwaelezea tafadhali’ niliwaomba huku nikilia.

‘unadhani tutakuelewa’ waliniuliza.

‘ndio nitasema kila kitu kuanzia mwanzo’ niliwajibu.

Majibu hayo yalifanya wanipe nafasi ya kuwaeleza kila kitu na bila kuchelewa nilianza kusema kila kitu wazi pasipo kuficha hata neno moja kwa sababu nilijua wazi kua ni lazima Nairath alikwisha waambia kila kitu hapo awali.
nilisema kila kitu wazi tokea siku nilipokutana na Grace pamoja na ule ukaribu wetu ambao ulikufa baada ya mimi kukutana tena na Nairath na kuanzisha mahusiano ya kimapenzi pale chuoni St.Anna sehemu yalipoanzia yale matatizo yote ambayo yalitokana na kuanza kuumwa kwa Grace.
maneno yangu yalionekana kumgusa kila mtu huku kile kitendo cha kuzidi kuwaambia kuhusu ule ugonjwa wa Grace uliomfanya apoteze fahamu kwa mwezi mmoja kikionekana kumtoa machozi kila mtu aliyekuwepo pale sebleni si yule rafiki yangu, si wazazi wake na Nairath, si yule binti aliyetufungulia mlango wala si mimi kwani kila mtu alijikuta akilia huku sauti za vilio hivyo zikionekana kuongezeka kadri nilivyozidi kusimulia juu ya ile safari ya kwenda China kumtibia Grace na kukaa huko kwa zaidi ya miezi 6 na kidogo.

‘kwanini ulimsaliti binti yetu kwa kukaa huko China muda mrefu hivyo’ mzee Fa-thiya aliniuliza.

‘sikumsaliti na ndio maana nipo hapa’

Nilimjibu kwa uchungu mkubwa na nikaanza kuwaambia tena juu ya kile kitendo cha kinyama alichonifanyia mzee Sebastian baba yake na Grace cha kunitelekeza na binti yake na kutoroka na hati yangu ya kusafiria na kusababisha nikae huko nchini China kwa muda mrefu kiasi cha kuonekana kana kwamba nilikua nimemsaliti.
wazazi wake na Nairath walinielewa lakini hawakua tayari kunisamehe kabisa kwa sababu waliniona kama muuaji na mtu niliyeyaharibu sana maisha ya binti yao huyo na kufanya ashinwe kutimiza malengo yake aliyojiwekea.

‘sidhani kama tutakusamehe naamini hata Nairath pia hatoweza’ aliniambia.

‘haijalishi, ninachohitaji ni kumuona tena na kuwaona watoto wangu’ niliwajibu.

Hakuna mtu aliyenisemesha wala kunijibu tena mara baada ya kuwaambia hayo maneno kwani ukimya ulitawala kwa dakika kadhaa na ghafla yule binti aliyetufungulia mlango hapo awali aliwanyanyua watoto wangu na kuwasogeza mpaka kwangu sehemu nilipokua nimekaa na yule rafiki yangu kwa mara nyingine nikawakumbatia na kuwabusu.
watoto wangu walianza kulia baada tu ya mimi kuwashika na kuwakumbatika kiukweli kilio chao kiliniumiza sana kwa sababu sio kwamba walikua wakilia kwa ajili ya utoto wao bali walilia kwa sababu ya sura yangu kua ngeni machoni kwao na kutonifahamu mimi kitu kilichosababisha nafsi yangu izidi kuumia na kunisuta zaidi kwa kuwakosesha wale watoto mapenzi ya kibaba toka walipokua tumboni mwa Nairath hadi hapo walipofikia.

Licha ya kulia kwao sikutaka kuwaacha bali niliwabembeleza huku nikizitazama sura zao za kitoto zilizokua za kupendeza sana kwa sababu ya ule uzuri wa rangi nyeupe waliyoichukua kwa Nairath huku yule mtoto wa kike akionekana sana kufanana na mama yangu mzazi kwa sababu ya kufanana sana na mimi wakati yule wa kiume akionekana kufanana sana na Nairath ambaye mpaka muda huo alikua hospitalini.

‘hongera kaka ni wazuri mno’ yule rafiki yangu aliniambia huku akiwatazama.

‘asante nashukuru sana’ nilimjibu.

Niliwashukuru sana wazazi wake na Nairath kwanza kwa sababu ya kuulea ule ujauzito wangu aliokuja nao binti yao wakati alipoondoka Tanzania na kuniachia ile barua pili nliwashukuru kwa wema wa kuwalea wale watoto wangu ambao ilikua ni jukumu langu kuwalea wote wao pamoja na mama yao Nairath.
na baada ya kuwashukuru niliwaomba ruhusa ya kwenda kumuona binti yao kama ulivyokua ule utaratibu wa pale hospitalini Good health kua ni lazima upate ruhusa kutoka kwa ndugu wa karibu wa mgonjwa ndipo uweze kumuona lakini cha ajabu walinikatalia.
nilishangazwa sana na majibu yao ya kukataa mimi nisiende kumuona Nairath kusema kweli wazazi wake na Nairath walinishangaza sana kwani pamoja na kuwabembeleza sana tena kwa machozi bado walitia ugumu kunielewa, niliumia sana kwani licha ya kuwaambia ukweli wote na kuthibitisha wazi kua nina mpenda sana binti yao bado hawakunielewa hata kidogo na hawakutaka kusikia kabisa hiyo habari ya kuongozana nao hospitali.

‘kwanini hamtaki kuniruhusu’ niliwaliza kwa wasiwasi mwingi.

‘nadhani inatosha kuwaona watoto wako tafadhali muache binti yetu afe kwa amani’ mzee Fa-thiya alinijibu.

Majibu yake yenye utata mwingi, yalifanya maswali mfululizo yasiyokua na majibu yaushambulie ufahamu wangu kwani nilibaki nimeduwaa huku nikishindwa cha kufanya.

‘kwanini afe? kwani hali yake ikoje na anasumbuliwa na nini’ niliuliza.

‘Javier, inaniuma sana huwezi kuamini kua Nairath ni muathirika wa virusi vya ukimwi’ mama yake na Nairath aliniambia huku akilia kwa huzuni.

‘whaaaaat!!! Nairath ni muathirika?’ niliuliza kwa mshangao.

‘ndio ni muathirika tena wa muda mrefu sana’ aliniambia huku akizidi kulia.

‘mama hebu niweke wazi mbona sikuelewi’ nilimuuliza tena kwa kutahamaki.

‘najua utaumia sana lakini hatuwezi kuubadilisha ukweli Nairath ni muathirika toka mwaka 2006 alipokua na umri wa miaka 19 alipata ajari mbaya sana ya gari na ndipo tulipomkimbiza hospitali na katika haraka ya kuyaokoa maisha yake inasadikika aliongezewa damu yenye maambukizi kutoka kwa mtu asiyefahamika kwa sababu damu zote zilizokuwepo kwenye bank ya hospitali hiyo hazikuendana na group la damu ya Nairath’ mama yake aliniambia.

Yale majibu hayakuishia kunihuzunisha tu bali yalinikatisha sana tamaa ya maisha nilijua wazi kua ni lazima nitakua nimeathirika nililia sana na kwa mara ya kwanza nikayaamini maneno ya wahenga kua si kila king’aacho ni dhahabu vingine ni adhabu.
harufu ya kifo ilianza kusikika puani mwangu huku kwa mbali nikaanza kuiona sura ya Grace ambaye bila shaka nae alikua ameathirika kwa sababu ya kushiriki nae tendo la ndoa nilijikuta nikitamani sana kumchukia Nairath kwa sababu ya aliyoyafanya kwangu lakini nilishindwa kwa sababu kiukweli nilikua nampenda sana.
nilijuta sana kwanini nilimkataa Grace pia nikajilaumu kwanini sikwendwa kupima pindi Nairath alipozikubali hisia zangu na kunishawishi tufanye mapenzi tena bila kinga,

‘wewe ni muuaji, umempa ukimwi Grace kama haitoshi umemtoroka’ nafsi yangu ilianza kunisuta huku maneno hayo yakisikika kwa nguvu sana katika masikio yangu yote mawili kitu kilichofanya nione kama Israel mtoa roho alikua akikatiza mbele yangu.
niliwatazama sana wale watoto wangu nikalia kwa sauti kuu ya uchungu huku nikimuomba Mungu awaepushe na yale maambukizi kwa sababu nilijua kua inawezekana watoto wasiambukizwe lakini kama tu mama atawahi hospitali na kupewa chanjo na tiba zote.

‘Najua nitakufa!! Nisameheni sana wanangu sitaki kuwaacha muishi bila baba’ nilizidi kulia huku nikiongea kwa kuchanganyikiwa na ghafla nikamuona yule rafiki yangu dereva tax akianguka chini na kupiga magoti kisha akaanza kulia.

‘Nisameheni sana ndugu zangu mimi ndiye ni..l..i..y.e.m.u..onge..ze..a’ alisema kwa kujiuma uma uma tena kwa kigugumizi na kufanya kila mtu amuangalie kwa macho ya hasira.


….itaendelea….

ABCDEFGHIJKLMNOPQRSTUVWXYZ
 
NISAMEHE GRACE - 16



Ilipoishia…

Mimi ndiye niliyemuongezea binti yenu damu yenye maambukizi….

Songa nayo…

Ilikua ni siku ya jumatatu tarehe 23 mwezi wa 10 mwaka 2006 siku nilipokua daktari wa zamu katika hospitali ya Wadi Muqshin ambapo majira ya saa 2 na nusu usiku binti mmoja mwenye umri wa kati ya miaka 19-20 aliletwa akiwa amezirai huku akionekana kupoteza damu nyingi sana kwa sababu ya yale majeraha aliyokua nayo ambayo yalitokana na ajali mbaya ya gari baada ya kumpokea mimi pamoja na timu yangu tulimpeleka mpaka katika chumba cha upasuaji kwa ajili ya kumsafisha yale majeraha pamoja na kuyashona.’ yule dereva tax alisema.

Na baada ya kumfikisha katika chumba cha upasuaji kitu cha kwanza ilikua ni lazima tumuongezee damu na hapo ndipo matatizo yalipoanzia maana damu zote za group 0 zilikua zimeisha katika bank ya hospitali hiyo kitu kilichofanya mimi pamoja na wale madaktari wenzangu tupime damu zetu na ndipo damu yangu ikaendana na damu ya binti yenu lakini nilisita kabisa kumuongezea damu yangu maana nilijua wazi kua nilikua nimeathirika.

‘hebu muongeze damu tusipofanya hivyo ni lazima atakufa’ madaktari wenzangu waliniambia.

‘najua kua atakufa lakini mimi ni muathirika’ niliwajibu.

‘wewe ni daktari lazima ujue thamani ya uhai wa mgonjwa wako hebu muongezee tu maana inaweza kuusogeza uhai wake hata miaka 5 mbele huoni ni afadhali kuliko akifa hapa’ waliniambia.

Yale maneno ya madaktari wenzangu yalifanya nimtazame kwa huruma yule binti aliyekua ameletwa pale hospitalini na wasamaria wema akiwa amezirai kitu kilichopelekea kufanya yale maamuzi magumu ya kutoa damu yangu yenye maambukizi na kumuongezea ili kuyaokoa maisha yake yaliyoonekana kuelekea ukiongoni na hapo ndipo nilipoamua kutoa damu yangu yenye maambukizi na kumuongezea’ yule dereva tax aliyasema yote hayo huku akilia kama mtoto mdogo mbele ya wazazi wake na Nairath angali akiwa bado amepiga magoti.

‘si bora ungeacha binti yetu afe kuliko anavyoteseka hivi sasa’ mama Nairath alimwambia huku na yeye akilia kwa sababu ya ule upendo na uchungu wa kimama.

‘hakustahili kufa sababu alikua bado binti mdogo sana’ yule dereva tax alisema.

‘tutauamini vipi kama kweli haukukusudia?.’ Mzee Fa-thiya alimuuliza
‘sikukusudia kabisa ndio maana baada ya tukio hilo nilijiwajibisha mimi mwenyewe kwa kuacha kazi na kua dereva tax huku nikiamini siku moja katika mizunguko yangu nitaweza kuonana na binti huyo ili niweze kumuomba msamaha juu ya kile niliyomfanyia lakini nilizunguka karibu miji yote ya hapa Oman pasipo kumuona ma mdio maana nimeshindwa kujizuia kujisema hapa ili miweze kusamehewa na kuitubu dhambi hii iliyonitesa na kunitafuna kwa muda mrefu sana’ alisema.

Sote hatukumjibu chochote bali tuliishia kumuangalia kwa macho yenye hasira na huzuni nyingi hakuna hata mmoja kati yetu aliyetambua thamani ya ule wema wake alioutenda wala uzito wa yale machozi yake yaliyokua yakimdondoka na kukisindikiza kile kilio chake kikubwa cha uchungu kwani wote tuliishia kumhukumu ingawa kiukweli alikua ametenda wema mkubwa ulioyasogeza maisha ya Nairath kufikia mpaka muda huo aliokua amelazwa pale hospitalini Good health.

‘haijalishi umetenda wema kiasi gani kamwe hatutokusamehe mpaka pale binti yetu atakapo kusamehe yeye mwenyewe ndipo nasi tutakusamehe’ mzee Fa-thiya alisema.

Na baada ya maongezi hayo mazito yenye kuumiza sana safari ya kuelekea hospitalini Good health kumuona Nairath ilianza huku ile kesi yangu pamoja na makosa yangu yote niliyotenda yakionekana kuamia juu ya yule dereva tax.
haikua safari ndefu sana kwani baada ya mwendo wa karibu dakika 10 tulifanikiwa kufika salama mpaka pale hospitalini Good health na kisha tukaanza kupiga hatua huku nikiwa nimewabeba watoto wangu kuelekea sehemu ilipokuwepo wodi aliyokua amelazwa Nairath ambapo baada ya mwendo wa kama dakika 2 na nusu hivi tuliifikia wodi hiyo.

‘Nairaaaaaaaaaath!!!! nimekuja hapa kwa ajili yako’ nilisema mara tu baada ya kuingia wodini na kumuona Nairath akiwa amelala kisha nikamkimbilia na kumkumbatia nusura ya kuwaangusha wale watoto wetu.
lakini cha ajabu Nairath hakunijibu kitu sababu ya kushindwa kuongea bali aliishia tu kuniangalia mimi pamoja na wale watoto wetu niliokua nimewabeba.
sikuweza kabisa kuyazuia machozi yasinitoke baada tu ya kumuona Nairath kiukweli nililia sana sikuataka kuamini kama niliyemuona hapo ndiye yule Nairath niliyeonana nae kule St.Anna university muda mrefu uliopita maana Nairath huyu niliyemuona hospitalini hapo alikua amekonda sana bila huruma vipele viliushambulia mwili wake na kuuharibu sana uzuri wa ile sura yake kwani yale macho yake makubwa meupe ya duara yalionekana kuingia ndani ya sura yake huku zile pua zake nyembamba zikionekana kukonda sana na kubaki mifupa mitupu wakati ile midomo yake iliyokua imezawadiwa lips laini ilionekana kujaa vidonda na kukauka kabisa huku zile nywele zake nzuri nyeusi alizokua akipenda kuzilaza kwa nyumba zikionekana kunyonyoka sana na kua kama kuku aliyenyonyolewa kwenye maji ya moto.

Sote tulilia sana hasa yule dereva tax alionekana kulia sana huku akimuomba Nairath msamaha kwa sababu ya kumsababishia mateso yote hayo kwa kumuongezea ile damu yake yenye maambukizi.

‘nisamehe sana binti sikukusudia kabisa kukufanyia hivi’ yule dereva tax alimwambia Nairath huku akilia na kumsimulia kisa kizima jinsi kilivyokua siku ile ambayo Nairath alipata ajali.
Maneno yalionekana kumuumiza sana Nairath ambaye naye alianza kulia huku akionekana kuilazimisha ile midomo yake iliyokua imekauka na kujaa vidonda iseme chochote.

‘u.s.i.ja.l.i ni.me.ku.s.amehe.. i.li.k.u.a ni .kwa..a.j.i.li .yangu’ Nairath alimwambia kwa shida kwa sababu ya maumivu ya vile vidonda vilivyokua vimeushambulia mdomo wake bila huruma na kisha baada ya kumwambia yule dereva tax Nairath aliinita kwa shida tena.

‘Javier na.ku.pe.nda s.an.a, na.o.mba .u.nisa.me.he kabla s.ijafa’ Nairath alinambia.

‘nikusamehe kwa lipi wakati mimi ndiye niliyekukosea tafadhali naomba usiseme hivyo wewe haufi Nairath’ nilimwambia.

‘Javier ni.liku.ku.bali a.ngali ,nili.jua .kua nimea.th.i.ri.ka ni.kwa.sababu n.ili.ku.a na.kup.enda .sana..ndi.o. maana nilishind.w.a ku.ku.ambia. ukweli.’ aliniambia.

‘youre not a crime but love is a crime’
(wewe sio muhalifu mapenzi ndio mahalifu) nilimwambia.

Hivyo ndivyo ilivyokua kwani hali ya Nairath ilizidi kua mbaya siku hadi siku yani kila siku ikawa ni afadhali ya jana kitu kilichofanya nikae pale nchini Oman kwa muda wa miezi mitatu huku nikisaidiana na wazazi wake pamoja na yule dereva tax kumuuguza Nairath mpaka siku alipokuja kufariki dunia tarehe 26 mwezi wa 9 siku ya jumatano ambayo kamwe sitakuja kuisahau katika maisha yangu.
na baada ya kifo chake niliendelea kukaa pale Oman mpaka arobaini yake ilipopita ambapo kwa shingo upande wazazi wake walikubali kunikabidhi wale watoto wangu ili nirudi nao nchini Tanzania huku wakiomba niwalee na kuwatunza katika maadili mema yampendezayo Mungu.

‘asanteni sana kwa wema wenu nitawalea watoto hawa katika maadili mema’ niliwashukuru huku nikiwaaidi kusaidiana na yule mamdogo wake na Nairath aliyeko masaki katika kuwalea hao watoto wangu.

Wao pia walinishukuru sana, wakanitakia kila la heri halafu wakanizawadia na albamu kubwa mbili zilizojaa picha za marehemu Nairath kwa ajili ya kumbukumbu na mwisho tukaagana kwa huzuni kubwa huku wakiniomba isiwe mwisho kwenda tena Oman kuwasalimu na kuwapeleka wajukuu zao kuwasalimia.

Na baada ya kuagana nao niliondoka na wale watoto wangu pamoja na yule dereva tax ambaye mpaka wakati huo alikua amekua kama ndugu mpaka Fahud sehemu yalipokuwepo makaburi ambapo baada ya kufika sote tulikwenda moja kwa moja mpaka mahali lilipokuwepo kaburi la Nairath ambalo kwa mara ya mwisho nililiwekea maua pamoja na kumsalia Nairath dua langu la mwisho.

‘kwa heri Nairath kamwe sitakusahau nahaidi nitawalea watoto wetu kama tulivyokua tumejipangia hapo awali katika zile nyakati zetu za furaha pale St.Anna’ nilisema huku nikipiga hatua zangu kuelekea garini na kuianza ile safari yetu ya kurudi hotelini pale Gulf of Oman.

Tulifika salama mpaka pale hotelini Gulf of Oman sehemu nilipoagana na yule rafiki yangu dereva tax ambaye alihaidi kunitafuta pindi atakapo rejea nyumbani nchini Tanzania.

‘kila la heri sitokusahau’
‘mimi pia sitokusahau kila la heri’ tuliagana.

Ilikua ni huzuni kubwa sana katika kuagana kwetu ambapo baada ya kumaliza niliingia mpaka hotelini nikiwa pamoja na wale watoto wangu na nikaanza kupanga mizigo yangu pamoja na kile chumba nilichokikabidhi siku hiyo muda mchache kabla ya kwenda airport kuianza ile safari ya kurejea nyumbani nchini Tanzania.

Nilienda mpaka airport pale Musqat mjini nikiwa pamoja na watoto wangu sote tukaingia ndani ya ndege ya Oman airways mali ya serikali hiyo na baada ya kuingia safari yetu ya kuelekea nyumbani nchini Tanzania ikaanza.
licha ya ule urefu wa safari pamoja na usumbufu nilioupata kutoka kwa wale malaika wangu wadogo tulifanikiwa kufika na kutua salama juu ya kiwanja cha ndege cha mwl Julias Nyerere na bila kuchelewa nilichukua tax nikapakia mizigo yangu pamoja na wale watoto wangu na safari ya kuelekea nyumbani kwa wazazi wangu ikaanza huku hofu kubwa ikionekana kuuvaa mwili wangu kwa sababu ya kuogopa kupokea taarifa zozote mbaya za Grace pamoja na lawama zilizokua zikisubiri kunishambulia.

Tulifika salama mpaka nyumbani kwa wazazi wangu na baada ya kufika kwa wasiwasi mwingi na hofu kubwa niliusogelea ule mlango wa kuingilia sebleni huku nikiwa nimewabeba watoto wangu pamoja na ile mizigo yangu.
sikuamini kabisa nilichokiona mara tu baada ya mimi kuingia ndani.

Nilimuona mama yangu mzazi akiwa anacheza na mtoto mdogo wa kike ambaye alionekana kufanana sana na Grace.
‘mama mwanao nimerudi naomba unisamehe sana mama’ nilisema huku nikilia na kuwashusha wale watoto wangu kisha nikapiga magoti na kumsogelea.
‘karibu sana mwanangu’ mama alinijibu huku akinikumbatia kwa furaha.

‘asante mama naomba unisamehe sana’ nilimwambia.
‘nisha kusamehe mwanangu’ alinijibu.
‘asante mama vipi Grace yuko wapi’ nilimuuliza kwa hofu kubwa kwa sababu ya kuogopa kunyeshewa mvua ya lawama.

‘Grace alifariki mwanangu pole sana babaa’ aliniambia
‘whaaaaat! ilikuajeee’ nilimuuliza kwa mshangao sababu ya kutoamini alichokisema.

‘mwanangu Grace alifanikiwa kujifungua salama mtoto wa kike ambaye ndiye huyu hapa lakini baada ya kutoka hospitali na kurudi nyumbani kwenu kule mbezi beach alikutana na barua yako juu ya meza uliyomuandikia kuhusu kwenda kwako huko Oman kumtafuta Nairath kiukweli barua hiyo ndiyo ilikua chanzo kikubwa cha kifo chake kwani baada ya kuisoma tu presha ilimpanda akaanguka chini na kupoteza fahamu kitu kilichofanya arudi tena hospitali ambako alilazwa siku 3 na siku ya 4 saa 5 na nusu usiku akaaga dunia pasipo hata kumpa jina mtoto wake.’ mama aliniambia.

‘ni makosa yangu mama, kwa hiyo huyu ni mwanangu’ nilimuuliza.
‘ndiyo ni mwanao kabisa’ mama alinijibu.
‘mmempa jina gani?’ nilimuuliza tena.
‘tuliamua kumpa jina la Nairath kama ishara ya kuwakumbuka nyote’ alisema.
‘Nairaaaath!!?’ nilimuuliza kwa mshangao.
‘ndio anaitwa Nairath mbona umeshtuka’ aliniuliza huku nae akianza kulia.
‘mama Nairath nae amefariki na hawa hapa ni watoto wetu huyu wa kiume anaitwa Javier,na huyu wa kike anaitwa Grace’

Nilimwambia mama yangu huku nikizidi kulia na kumuelezea kila kitu na baada ya kumueleza aliwasogelea na kuwakumbatia huku na mimi kwa mara ya kwanza nikimnyanyua yule mtoto wangu na Grace na kumkumbatia kwa furaha na huzuni nyingi kwa sababu ya jina lake la Nairath kunikumbusha yale yote yaliyotokea kule Oman .
baada ya hayo yote mama alitutarishia chakula nika kila na kukimaliza kisha nae kwa mara ya kwanza akaenda kuwaogesha wale wajukuu wake wawili nilioenda nao na kuwanywesha maziwa ya kopo aliyokua akiyatumia yule Nairath mdogo na ghafla akiwa katika kuwanywesha baba yangu mzee Hernandez aliingia ndani akiwa ametoka national stadium kuangalia mpira na baada ya kuingia tulisalimiana akawaona wajukuu wake wapya tukaongea mengi na kisha tukaenda kulala.

Nilikuja kuamka majira ya saa 3 asubuhi kwa sababu ya uchovu, nikamsaidia mama yangu kuwaogesha wale watoto wangu nikanywa chai halafu nikampigia simu yule rafiki yangu kipenzi bwana Khamis Rajabu aliyekua akiishi kule masaki nikamuomba ampitie yule mamdogo wake na Nairath ambaye naye alikua akiishi masaki na wote waje nyumbani.
kwa wema mkubwa yule rafiki yangu alitii kwani walikuja wote nyumbani majira ya saa 5 asubuhi na tukaongea mengi wakawaona watoto wangu na kisha nikawaomba tuende sote mpaka nyumbani kwa mzee Sebastian tena kwa mara nyingine walikubali tukanda sote mpaka nyumbani kwa mzee Sebastiana na mkewe sehemu tulipoongea na kusameheana kabisa kila kitu huku tukionyana na kupeana tahadhari ili haya yote yasije kujirudia tena.

Tulisameheana kabisa na kusahau kila kitu kisha wakanipeleka mpaka sehemu lilipokuwepo kaburi ka Grace ambapo nilitoa heshima zangu za mwisho nikamuombea dua na kisha nikamuomba msamaha kwa sababu ya kukisababisha kifo chake.

‘Nisamehe Grace’ nilisema huku nikilia na kulitazama kaburi lake.

‘Javier usilie sana maana ulimpoteza Grace na sasa hivi unae Grace ulimpoteza Nairath na sasa hivi unae Nairath bila kusahau nyongeza ya Javier Hernandez’ yule rafiki yangu aliniambia.

‘ni kweli ninao wote lakini hii hainizuii kumuomba msamhama’ nilimwambia huku nikizidi kusema

‘kamwe sijatujia sababu ya kushindwa kutimiza ndoto zangu za kuwa daktari wa upasuaji wa neva na saikolojia bali nitajutia kwa sababu ya kusabisha kifo chako na kutoutambua upendo wako kwangu hakika kamwe sitokuasau.
Mmhhh Nisamehe Grace.

Na maisha yakaendelea kama kawaida.

….mwisho…

ABCDEFGHIJKLMNOPQRSTUVWXYZ
 
NISAMEHE GRACE - 16



Ilipoishia…

Mimi ndiye niliyemuongezea binti yenu damu yenye maambukizi….

Songa nayo…

Ilikua ni siku ya jumatatu tarehe 23 mwezi wa 10 mwaka 2006 siku nilipokua daktari wa zamu katika hospitali ya Wadi Muqshin ambapo majira ya saa 2 na nusu usiku binti mmoja mwenye umri wa kati ya miaka 19-20 aliletwa akiwa amezirai huku akionekana kupoteza damu nyingi sana kwa sababu ya yale majeraha aliyokua nayo ambayo yalitokana na ajali mbaya ya gari baada ya kumpokea mimi pamoja na timu yangu tulimpeleka mpaka katika chumba cha upasuaji kwa ajili ya kumsafisha yale majeraha pamoja na kuyashona.’ yule dereva tax alisema.

Na baada ya kumfikisha katika chumba cha upasuaji kitu cha kwanza ilikua ni lazima tumuongezee damu na hapo ndipo matatizo yalipoanzia maana damu zote za group 0 zilikua zimeisha katika bank ya hospitali hiyo kitu kilichofanya mimi pamoja na wale madaktari wenzangu tupime damu zetu na ndipo damu yangu ikaendana na damu ya binti yenu lakini nilisita kabisa kumuongezea damu yangu maana nilijua wazi kua nilikua nimeathirika.

‘hebu muongeze damu tusipofanya hivyo ni lazima atakufa’ madaktari wenzangu waliniambia.

‘najua kua atakufa lakini mimi ni muathirika’ niliwajibu.

‘wewe ni daktari lazima ujue thamani ya uhai wa mgonjwa wako hebu muongezee tu maana inaweza kuusogeza uhai wake hata miaka 5 mbele huoni ni afadhali kuliko akifa hapa’ waliniambia.

Yale maneno ya madaktari wenzangu yalifanya nimtazame kwa huruma yule binti aliyekua ameletwa pale hospitalini na wasamaria wema akiwa amezirai kitu kilichopelekea kufanya yale maamuzi magumu ya kutoa damu yangu yenye maambukizi na kumuongezea ili kuyaokoa maisha yake yaliyoonekana kuelekea ukiongoni na hapo ndipo nilipoamua kutoa damu yangu yenye maambukizi na kumuongezea’ yule dereva tax aliyasema yote hayo huku akilia kama mtoto mdogo mbele ya wazazi wake na Nairath angali akiwa bado amepiga magoti.

‘si bora ungeacha binti yetu afe kuliko anavyoteseka hivi sasa’ mama Nairath alimwambia huku na yeye akilia kwa sababu ya ule upendo na uchungu wa kimama.

‘hakustahili kufa sababu alikua bado binti mdogo sana’ yule dereva tax alisema.

‘tutauamini vipi kama kweli haukukusudia?.’ Mzee Fa-thiya alimuuliza
‘sikukusudia kabisa ndio maana baada ya tukio hilo nilijiwajibisha mimi mwenyewe kwa kuacha kazi na kua dereva tax huku nikiamini siku moja katika mizunguko yangu nitaweza kuonana na binti huyo ili niweze kumuomba msamaha juu ya kile niliyomfanyia lakini nilizunguka karibu miji yote ya hapa Oman pasipo kumuona ma mdio maana nimeshindwa kujizuia kujisema hapa ili miweze kusamehewa na kuitubu dhambi hii iliyonitesa na kunitafuna kwa muda mrefu sana’ alisema.

Sote hatukumjibu chochote bali tuliishia kumuangalia kwa macho yenye hasira na huzuni nyingi hakuna hata mmoja kati yetu aliyetambua thamani ya ule wema wake alioutenda wala uzito wa yale machozi yake yaliyokua yakimdondoka na kukisindikiza kile kilio chake kikubwa cha uchungu kwani wote tuliishia kumhukumu ingawa kiukweli alikua ametenda wema mkubwa ulioyasogeza maisha ya Nairath kufikia mpaka muda huo aliokua amelazwa pale hospitalini Good health.

‘haijalishi umetenda wema kiasi gani kamwe hatutokusamehe mpaka pale binti yetu atakapo kusamehe yeye mwenyewe ndipo nasi tutakusamehe’ mzee Fa-thiya alisema.

Na baada ya maongezi hayo mazito yenye kuumiza sana safari ya kuelekea hospitalini Good health kumuona Nairath ilianza huku ile kesi yangu pamoja na makosa yangu yote niliyotenda yakionekana kuamia juu ya yule dereva tax.
haikua safari ndefu sana kwani baada ya mwendo wa karibu dakika 10 tulifanikiwa kufika salama mpaka pale hospitalini Good health na kisha tukaanza kupiga hatua huku nikiwa nimewabeba watoto wangu kuelekea sehemu ilipokuwepo wodi aliyokua amelazwa Nairath ambapo baada ya mwendo wa kama dakika 2 na nusu hivi tuliifikia wodi hiyo.

‘Nairaaaaaaaaaath!!!! nimekuja hapa kwa ajili yako’ nilisema mara tu baada ya kuingia wodini na kumuona Nairath akiwa amelala kisha nikamkimbilia na kumkumbatia nusura ya kuwaangusha wale watoto wetu.
lakini cha ajabu Nairath hakunijibu kitu sababu ya kushindwa kuongea bali aliishia tu kuniangalia mimi pamoja na wale watoto wetu niliokua nimewabeba.
sikuweza kabisa kuyazuia machozi yasinitoke baada tu ya kumuona Nairath kiukweli nililia sana sikuataka kuamini kama niliyemuona hapo ndiye yule Nairath niliyeonana nae kule St.Anna university muda mrefu uliopita maana Nairath huyu niliyemuona hospitalini hapo alikua amekonda sana bila huruma vipele viliushambulia mwili wake na kuuharibu sana uzuri wa ile sura yake kwani yale macho yake makubwa meupe ya duara yalionekana kuingia ndani ya sura yake huku zile pua zake nyembamba zikionekana kukonda sana na kubaki mifupa mitupu wakati ile midomo yake iliyokua imezawadiwa lips laini ilionekana kujaa vidonda na kukauka kabisa huku zile nywele zake nzuri nyeusi alizokua akipenda kuzilaza kwa nyumba zikionekana kunyonyoka sana na kua kama kuku aliyenyonyolewa kwenye maji ya moto.

Sote tulilia sana hasa yule dereva tax alionekana kulia sana huku akimuomba Nairath msamaha kwa sababu ya kumsababishia mateso yote hayo kwa kumuongezea ile damu yake yenye maambukizi.

‘nisamehe sana binti sikukusudia kabisa kukufanyia hivi’ yule dereva tax alimwambia Nairath huku akilia na kumsimulia kisa kizima jinsi kilivyokua siku ile ambayo Nairath alipata ajali.
Maneno yalionekana kumuumiza sana Nairath ambaye naye alianza kulia huku akionekana kuilazimisha ile midomo yake iliyokua imekauka na kujaa vidonda iseme chochote.

‘u.s.i.ja.l.i ni.me.ku.s.amehe.. i.li.k.u.a ni .kwa..a.j.i.li .yangu’ Nairath alimwambia kwa shida kwa sababu ya maumivu ya vile vidonda vilivyokua vimeushambulia mdomo wake bila huruma na kisha baada ya kumwambia yule dereva tax Nairath aliinita kwa shida tena.

‘Javier na.ku.pe.nda s.an.a, na.o.mba .u.nisa.me.he kabla s.ijafa’ Nairath alinambia.

‘nikusamehe kwa lipi wakati mimi ndiye niliyekukosea tafadhali naomba usiseme hivyo wewe haufi Nairath’ nilimwambia.

‘Javier ni.liku.ku.bali a.ngali ,nili.jua .kua nimea.th.i.ri.ka ni.kwa.sababu n.ili.ku.a na.kup.enda .sana..ndi.o. maana nilishind.w.a ku.ku.ambia. ukweli.’ aliniambia.

‘youre not a crime but love is a crime’
(wewe sio muhalifu mapenzi ndio mahalifu) nilimwambia.

Hivyo ndivyo ilivyokua kwani hali ya Nairath ilizidi kua mbaya siku hadi siku yani kila siku ikawa ni afadhali ya jana kitu kilichofanya nikae pale nchini Oman kwa muda wa miezi mitatu huku nikisaidiana na wazazi wake pamoja na yule dereva tax kumuuguza Nairath mpaka siku alipokuja kufariki dunia tarehe 26 mwezi wa 9 siku ya jumatano ambayo kamwe sitakuja kuisahau katika maisha yangu.
na baada ya kifo chake niliendelea kukaa pale Oman mpaka arobaini yake ilipopita ambapo kwa shingo upande wazazi wake walikubali kunikabidhi wale watoto wangu ili nirudi nao nchini Tanzania huku wakiomba niwalee na kuwatunza katika maadili mema yampendezayo Mungu.

‘asanteni sana kwa wema wenu nitawalea watoto hawa katika maadili mema’ niliwashukuru huku nikiwaaidi kusaidiana na yule mamdogo wake na Nairath aliyeko masaki katika kuwalea hao watoto wangu.

Wao pia walinishukuru sana, wakanitakia kila la heri halafu wakanizawadia na albamu kubwa mbili zilizojaa picha za marehemu Nairath kwa ajili ya kumbukumbu na mwisho tukaagana kwa huzuni kubwa huku wakiniomba isiwe mwisho kwenda tena Oman kuwasalimu na kuwapeleka wajukuu zao kuwasalimia.

Na baada ya kuagana nao niliondoka na wale watoto wangu pamoja na yule dereva tax ambaye mpaka wakati huo alikua amekua kama ndugu mpaka Fahud sehemu yalipokuwepo makaburi ambapo baada ya kufika sote tulikwenda moja kwa moja mpaka mahali lilipokuwepo kaburi la Nairath ambalo kwa mara ya mwisho nililiwekea maua pamoja na kumsalia Nairath dua langu la mwisho.

‘kwa heri Nairath kamwe sitakusahau nahaidi nitawalea watoto wetu kama tulivyokua tumejipangia hapo awali katika zile nyakati zetu za furaha pale St.Anna’ nilisema huku nikipiga hatua zangu kuelekea garini na kuianza ile safari yetu ya kurudi hotelini pale Gulf of Oman.

Tulifika salama mpaka pale hotelini Gulf of Oman sehemu nilipoagana na yule rafiki yangu dereva tax ambaye alihaidi kunitafuta pindi atakapo rejea nyumbani nchini Tanzania.

‘kila la heri sitokusahau’
‘mimi pia sitokusahau kila la heri’ tuliagana.

Ilikua ni huzuni kubwa sana katika kuagana kwetu ambapo baada ya kumaliza niliingia mpaka hotelini nikiwa pamoja na wale watoto wangu na nikaanza kupanga mizigo yangu pamoja na kile chumba nilichokikabidhi siku hiyo muda mchache kabla ya kwenda airport kuianza ile safari ya kurejea nyumbani nchini Tanzania.

Nilienda mpaka airport pale Musqat mjini nikiwa pamoja na watoto wangu sote tukaingia ndani ya ndege ya Oman airways mali ya serikali hiyo na baada ya kuingia safari yetu ya kuelekea nyumbani nchini Tanzania ikaanza.
licha ya ule urefu wa safari pamoja na usumbufu nilioupata kutoka kwa wale malaika wangu wadogo tulifanikiwa kufika na kutua salama juu ya kiwanja cha ndege cha mwl Julias Nyerere na bila kuchelewa nilichukua tax nikapakia mizigo yangu pamoja na wale watoto wangu na safari ya kuelekea nyumbani kwa wazazi wangu ikaanza huku hofu kubwa ikionekana kuuvaa mwili wangu kwa sababu ya kuogopa kupokea taarifa zozote mbaya za Grace pamoja na lawama zilizokua zikisubiri kunishambulia.

Tulifika salama mpaka nyumbani kwa wazazi wangu na baada ya kufika kwa wasiwasi mwingi na hofu kubwa niliusogelea ule mlango wa kuingilia sebleni huku nikiwa nimewabeba watoto wangu pamoja na ile mizigo yangu.
sikuamini kabisa nilichokiona mara tu baada ya mimi kuingia ndani.

Nilimuona mama yangu mzazi akiwa anacheza na mtoto mdogo wa kike ambaye alionekana kufanana sana na Grace.
‘mama mwanao nimerudi naomba unisamehe sana mama’ nilisema huku nikilia na kuwashusha wale watoto wangu kisha nikapiga magoti na kumsogelea.
‘karibu sana mwanangu’ mama alinijibu huku akinikumbatia kwa furaha.

‘asante mama naomba unisamehe sana’ nilimwambia.
‘nisha kusamehe mwanangu’ alinijibu.
‘asante mama vipi Grace yuko wapi’ nilimuuliza kwa hofu kubwa kwa sababu ya kuogopa kunyeshewa mvua ya lawama.

‘Grace alifariki mwanangu pole sana babaa’ aliniambia
‘whaaaaat! ilikuajeee’ nilimuuliza kwa mshangao sababu ya kutoamini alichokisema.

‘mwanangu Grace alifanikiwa kujifungua salama mtoto wa kike ambaye ndiye huyu hapa lakini baada ya kutoka hospitali na kurudi nyumbani kwenu kule mbezi beach alikutana na barua yako juu ya meza uliyomuandikia kuhusu kwenda kwako huko Oman kumtafuta Nairath kiukweli barua hiyo ndiyo ilikua chanzo kikubwa cha kifo chake kwani baada ya kuisoma tu presha ilimpanda akaanguka chini na kupoteza fahamu kitu kilichofanya arudi tena hospitali ambako alilazwa siku 3 na siku ya 4 saa 5 na nusu usiku akaaga dunia pasipo hata kumpa jina mtoto wake.’ mama aliniambia.

‘ni makosa yangu mama, kwa hiyo huyu ni mwanangu’ nilimuuliza.
‘ndiyo ni mwanao kabisa’ mama alinijibu.
‘mmempa jina gani?’ nilimuuliza tena.
‘tuliamua kumpa jina la Nairath kama ishara ya kuwakumbuka nyote’ alisema.
‘Nairaaaath!!?’ nilimuuliza kwa mshangao.
‘ndio anaitwa Nairath mbona umeshtuka’ aliniuliza huku nae akianza kulia.
‘mama Nairath nae amefariki na hawa hapa ni watoto wetu huyu wa kiume anaitwa Javier,na huyu wa kike anaitwa Grace’

Nilimwambia mama yangu huku nikizidi kulia na kumuelezea kila kitu na baada ya kumueleza aliwasogelea na kuwakumbatia huku na mimi kwa mara ya kwanza nikimnyanyua yule mtoto wangu na Grace na kumkumbatia kwa furaha na huzuni nyingi kwa sababu ya jina lake la Nairath kunikumbusha yale yote yaliyotokea kule Oman .
baada ya hayo yote mama alitutarishia chakula nika kila na kukimaliza kisha nae kwa mara ya kwanza akaenda kuwaogesha wale wajukuu wake wawili nilioenda nao na kuwanywesha maziwa ya kopo aliyokua akiyatumia yule Nairath mdogo na ghafla akiwa katika kuwanywesha baba yangu mzee Hernandez aliingia ndani akiwa ametoka national stadium kuangalia mpira na baada ya kuingia tulisalimiana akawaona wajukuu wake wapya tukaongea mengi na kisha tukaenda kulala.

Nilikuja kuamka majira ya saa 3 asubuhi kwa sababu ya uchovu, nikamsaidia mama yangu kuwaogesha wale watoto wangu nikanywa chai halafu nikampigia simu yule rafiki yangu kipenzi bwana Khamis Rajabu aliyekua akiishi kule masaki nikamuomba ampitie yule mamdogo wake na Nairath ambaye naye alikua akiishi masaki na wote waje nyumbani.
kwa wema mkubwa yule rafiki yangu alitii kwani walikuja wote nyumbani majira ya saa 5 asubuhi na tukaongea mengi wakawaona watoto wangu na kisha nikawaomba tuende sote mpaka nyumbani kwa mzee Sebastian tena kwa mara nyingine walikubali tukanda sote mpaka nyumbani kwa mzee Sebastiana na mkewe sehemu tulipoongea na kusameheana kabisa kila kitu huku tukionyana na kupeana tahadhari ili haya yote yasije kujirudia tena.

Tulisameheana kabisa na kusahau kila kitu kisha wakanipeleka mpaka sehemu lilipokuwepo kaburi ka Grace ambapo nilitoa heshima zangu za mwisho nikamuombea dua na kisha nikamuomba msamaha kwa sababu ya kukisababisha kifo chake.

‘Nisamehe Grace’ nilisema huku nikilia na kulitazama kaburi lake.

‘Javier usilie sana maana ulimpoteza Grace na sasa hivi unae Grace ulimpoteza Nairath na sasa hivi unae Nairath bila kusahau nyongeza ya Javier Hernandez’ yule rafiki yangu aliniambia.

‘ni kweli ninao wote lakini hii hainizuii kumuomba msamhama’ nilimwambia huku nikizidi kusema

‘kamwe sijatujia sababu ya kushindwa kutimiza ndoto zangu za kuwa daktari wa upasuaji wa neva na saikolojia bali nitajutia kwa sababu ya kusabisha kifo chako na kutoutambua upendo wako kwangu hakika kamwe sitokuasau.
Mmhhh Nisamehe Grace.

Na maisha yakaendelea kama kawaida.

….mwisho…

ABCDEFGHIJKLMNOPQRSTUVWXYZ
Daaahhh.... Tang nizaliwe hii ndo Riwaya ya pil kunitoa machoz.... Ya kwanza n mfadhili enz hzo nkiwa 4m six...!

#Kaz nzur.... Hongera sana mkuu[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]

°•°Faith •Hope •Charity•°•
 
Asante sana mkuu, nakushuru kwa support.
Daaahhh.... Tang nizaliwe hii ndo Riwaya ya pil kunitoa machoz.... Ya kwanza n mfadhili enz hzo nkiwa 4m six...!

#Kaz nzur.... Hongera sana mkuu[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]

°•°Faith •Hope •Charity•°•

ABCDEFGHIJKLMNOPQRSTUVWXYZ
 
NISAMEHE GRACE - 16



Ilipoishia…

Mimi ndiye niliyemuongezea binti yenu damu yenye maambukizi….

Songa nayo…

Ilikua ni siku ya jumatatu tarehe 23 mwezi wa 10 mwaka 2006 siku nilipokua daktari wa zamu katika hospitali ya Wadi Muqshin ambapo majira ya saa 2 na nusu usiku binti mmoja mwenye umri wa kati ya miaka 19-20 aliletwa akiwa amezirai huku akionekana kupoteza damu nyingi sana kwa sababu ya yale majeraha aliyokua nayo ambayo yalitokana na ajali mbaya ya gari baada ya kumpokea mimi pamoja na timu yangu tulimpeleka mpaka katika chumba cha upasuaji kwa ajili ya kumsafisha yale majeraha pamoja na kuyashona.’ yule dereva tax alisema.

Na baada ya kumfikisha katika chumba cha upasuaji kitu cha kwanza ilikua ni lazima tumuongezee damu na hapo ndipo matatizo yalipoanzia maana damu zote za group 0 zilikua zimeisha katika bank ya hospitali hiyo kitu kilichofanya mimi pamoja na wale madaktari wenzangu tupime damu zetu na ndipo damu yangu ikaendana na damu ya binti yenu lakini nilisita kabisa kumuongezea damu yangu maana nilijua wazi kua nilikua nimeathirika.

‘hebu muongeze damu tusipofanya hivyo ni lazima atakufa’ madaktari wenzangu waliniambia.

‘najua kua atakufa lakini mimi ni muathirika’ niliwajibu.

‘wewe ni daktari lazima ujue thamani ya uhai wa mgonjwa wako hebu muongezee tu maana inaweza kuusogeza uhai wake hata miaka 5 mbele huoni ni afadhali kuliko akifa hapa’ waliniambia.

Yale maneno ya madaktari wenzangu yalifanya nimtazame kwa huruma yule binti aliyekua ameletwa pale hospitalini na wasamaria wema akiwa amezirai kitu kilichopelekea kufanya yale maamuzi magumu ya kutoa damu yangu yenye maambukizi na kumuongezea ili kuyaokoa maisha yake yaliyoonekana kuelekea ukiongoni na hapo ndipo nilipoamua kutoa damu yangu yenye maambukizi na kumuongezea’ yule dereva tax aliyasema yote hayo huku akilia kama mtoto mdogo mbele ya wazazi wake na Nairath angali akiwa bado amepiga magoti.

‘si bora ungeacha binti yetu afe kuliko anavyoteseka hivi sasa’ mama Nairath alimwambia huku na yeye akilia kwa sababu ya ule upendo na uchungu wa kimama.

‘hakustahili kufa sababu alikua bado binti mdogo sana’ yule dereva tax alisema.

‘tutauamini vipi kama kweli haukukusudia?.’ Mzee Fa-thiya alimuuliza
‘sikukusudia kabisa ndio maana baada ya tukio hilo nilijiwajibisha mimi mwenyewe kwa kuacha kazi na kua dereva tax huku nikiamini siku moja katika mizunguko yangu nitaweza kuonana na binti huyo ili niweze kumuomba msamaha juu ya kile niliyomfanyia lakini nilizunguka karibu miji yote ya hapa Oman pasipo kumuona ma mdio maana nimeshindwa kujizuia kujisema hapa ili miweze kusamehewa na kuitubu dhambi hii iliyonitesa na kunitafuna kwa muda mrefu sana’ alisema.

Sote hatukumjibu chochote bali tuliishia kumuangalia kwa macho yenye hasira na huzuni nyingi hakuna hata mmoja kati yetu aliyetambua thamani ya ule wema wake alioutenda wala uzito wa yale machozi yake yaliyokua yakimdondoka na kukisindikiza kile kilio chake kikubwa cha uchungu kwani wote tuliishia kumhukumu ingawa kiukweli alikua ametenda wema mkubwa ulioyasogeza maisha ya Nairath kufikia mpaka muda huo aliokua amelazwa pale hospitalini Good health.

‘haijalishi umetenda wema kiasi gani kamwe hatutokusamehe mpaka pale binti yetu atakapo kusamehe yeye mwenyewe ndipo nasi tutakusamehe’ mzee Fa-thiya alisema.

Na baada ya maongezi hayo mazito yenye kuumiza sana safari ya kuelekea hospitalini Good health kumuona Nairath ilianza huku ile kesi yangu pamoja na makosa yangu yote niliyotenda yakionekana kuamia juu ya yule dereva tax.
haikua safari ndefu sana kwani baada ya mwendo wa karibu dakika 10 tulifanikiwa kufika salama mpaka pale hospitalini Good health na kisha tukaanza kupiga hatua huku nikiwa nimewabeba watoto wangu kuelekea sehemu ilipokuwepo wodi aliyokua amelazwa Nairath ambapo baada ya mwendo wa kama dakika 2 na nusu hivi tuliifikia wodi hiyo.

‘Nairaaaaaaaaaath!!!! nimekuja hapa kwa ajili yako’ nilisema mara tu baada ya kuingia wodini na kumuona Nairath akiwa amelala kisha nikamkimbilia na kumkumbatia nusura ya kuwaangusha wale watoto wetu.
lakini cha ajabu Nairath hakunijibu kitu sababu ya kushindwa kuongea bali aliishia tu kuniangalia mimi pamoja na wale watoto wetu niliokua nimewabeba.
sikuweza kabisa kuyazuia machozi yasinitoke baada tu ya kumuona Nairath kiukweli nililia sana sikuataka kuamini kama niliyemuona hapo ndiye yule Nairath niliyeonana nae kule St.Anna university muda mrefu uliopita maana Nairath huyu niliyemuona hospitalini hapo alikua amekonda sana bila huruma vipele viliushambulia mwili wake na kuuharibu sana uzuri wa ile sura yake kwani yale macho yake makubwa meupe ya duara yalionekana kuingia ndani ya sura yake huku zile pua zake nyembamba zikionekana kukonda sana na kubaki mifupa mitupu wakati ile midomo yake iliyokua imezawadiwa lips laini ilionekana kujaa vidonda na kukauka kabisa huku zile nywele zake nzuri nyeusi alizokua akipenda kuzilaza kwa nyumba zikionekana kunyonyoka sana na kua kama kuku aliyenyonyolewa kwenye maji ya moto.

Sote tulilia sana hasa yule dereva tax alionekana kulia sana huku akimuomba Nairath msamaha kwa sababu ya kumsababishia mateso yote hayo kwa kumuongezea ile damu yake yenye maambukizi.

‘nisamehe sana binti sikukusudia kabisa kukufanyia hivi’ yule dereva tax alimwambia Nairath huku akilia na kumsimulia kisa kizima jinsi kilivyokua siku ile ambayo Nairath alipata ajali.
Maneno yalionekana kumuumiza sana Nairath ambaye naye alianza kulia huku akionekana kuilazimisha ile midomo yake iliyokua imekauka na kujaa vidonda iseme chochote.

‘u.s.i.ja.l.i ni.me.ku.s.amehe.. i.li.k.u.a ni .kwa..a.j.i.li .yangu’ Nairath alimwambia kwa shida kwa sababu ya maumivu ya vile vidonda vilivyokua vimeushambulia mdomo wake bila huruma na kisha baada ya kumwambia yule dereva tax Nairath aliinita kwa shida tena.

‘Javier na.ku.pe.nda s.an.a, na.o.mba .u.nisa.me.he kabla s.ijafa’ Nairath alinambia.

‘nikusamehe kwa lipi wakati mimi ndiye niliyekukosea tafadhali naomba usiseme hivyo wewe haufi Nairath’ nilimwambia.

‘Javier ni.liku.ku.bali a.ngali ,nili.jua .kua nimea.th.i.ri.ka ni.kwa.sababu n.ili.ku.a na.kup.enda .sana..ndi.o. maana nilishind.w.a ku.ku.ambia. ukweli.’ aliniambia.

‘youre not a crime but love is a crime’
(wewe sio muhalifu mapenzi ndio mahalifu) nilimwambia.

Hivyo ndivyo ilivyokua kwani hali ya Nairath ilizidi kua mbaya siku hadi siku yani kila siku ikawa ni afadhali ya jana kitu kilichofanya nikae pale nchini Oman kwa muda wa miezi mitatu huku nikisaidiana na wazazi wake pamoja na yule dereva tax kumuuguza Nairath mpaka siku alipokuja kufariki dunia tarehe 26 mwezi wa 9 siku ya jumatano ambayo kamwe sitakuja kuisahau katika maisha yangu.
na baada ya kifo chake niliendelea kukaa pale Oman mpaka arobaini yake ilipopita ambapo kwa shingo upande wazazi wake walikubali kunikabidhi wale watoto wangu ili nirudi nao nchini Tanzania huku wakiomba niwalee na kuwatunza katika maadili mema yampendezayo Mungu.

‘asanteni sana kwa wema wenu nitawalea watoto hawa katika maadili mema’ niliwashukuru huku nikiwaaidi kusaidiana na yule mamdogo wake na Nairath aliyeko masaki katika kuwalea hao watoto wangu.

Wao pia walinishukuru sana, wakanitakia kila la heri halafu wakanizawadia na albamu kubwa mbili zilizojaa picha za marehemu Nairath kwa ajili ya kumbukumbu na mwisho tukaagana kwa huzuni kubwa huku wakiniomba isiwe mwisho kwenda tena Oman kuwasalimu na kuwapeleka wajukuu zao kuwasalimia.

Na baada ya kuagana nao niliondoka na wale watoto wangu pamoja na yule dereva tax ambaye mpaka wakati huo alikua amekua kama ndugu mpaka Fahud sehemu yalipokuwepo makaburi ambapo baada ya kufika sote tulikwenda moja kwa moja mpaka mahali lilipokuwepo kaburi la Nairath ambalo kwa mara ya mwisho nililiwekea maua pamoja na kumsalia Nairath dua langu la mwisho.

‘kwa heri Nairath kamwe sitakusahau nahaidi nitawalea watoto wetu kama tulivyokua tumejipangia hapo awali katika zile nyakati zetu za furaha pale St.Anna’ nilisema huku nikipiga hatua zangu kuelekea garini na kuianza ile safari yetu ya kurudi hotelini pale Gulf of Oman.

Tulifika salama mpaka pale hotelini Gulf of Oman sehemu nilipoagana na yule rafiki yangu dereva tax ambaye alihaidi kunitafuta pindi atakapo rejea nyumbani nchini Tanzania.

‘kila la heri sitokusahau’
‘mimi pia sitokusahau kila la heri’ tuliagana.

Ilikua ni huzuni kubwa sana katika kuagana kwetu ambapo baada ya kumaliza niliingia mpaka hotelini nikiwa pamoja na wale watoto wangu na nikaanza kupanga mizigo yangu pamoja na kile chumba nilichokikabidhi siku hiyo muda mchache kabla ya kwenda airport kuianza ile safari ya kurejea nyumbani nchini Tanzania.

Nilienda mpaka airport pale Musqat mjini nikiwa pamoja na watoto wangu sote tukaingia ndani ya ndege ya Oman airways mali ya serikali hiyo na baada ya kuingia safari yetu ya kuelekea nyumbani nchini Tanzania ikaanza.
licha ya ule urefu wa safari pamoja na usumbufu nilioupata kutoka kwa wale malaika wangu wadogo tulifanikiwa kufika na kutua salama juu ya kiwanja cha ndege cha mwl Julias Nyerere na bila kuchelewa nilichukua tax nikapakia mizigo yangu pamoja na wale watoto wangu na safari ya kuelekea nyumbani kwa wazazi wangu ikaanza huku hofu kubwa ikionekana kuuvaa mwili wangu kwa sababu ya kuogopa kupokea taarifa zozote mbaya za Grace pamoja na lawama zilizokua zikisubiri kunishambulia.

Tulifika salama mpaka nyumbani kwa wazazi wangu na baada ya kufika kwa wasiwasi mwingi na hofu kubwa niliusogelea ule mlango wa kuingilia sebleni huku nikiwa nimewabeba watoto wangu pamoja na ile mizigo yangu.
sikuamini kabisa nilichokiona mara tu baada ya mimi kuingia ndani.

Nilimuona mama yangu mzazi akiwa anacheza na mtoto mdogo wa kike ambaye alionekana kufanana sana na Grace.
‘mama mwanao nimerudi naomba unisamehe sana mama’ nilisema huku nikilia na kuwashusha wale watoto wangu kisha nikapiga magoti na kumsogelea.
‘karibu sana mwanangu’ mama alinijibu huku akinikumbatia kwa furaha.

‘asante mama naomba unisamehe sana’ nilimwambia.
‘nisha kusamehe mwanangu’ alinijibu.
‘asante mama vipi Grace yuko wapi’ nilimuuliza kwa hofu kubwa kwa sababu ya kuogopa kunyeshewa mvua ya lawama.

‘Grace alifariki mwanangu pole sana babaa’ aliniambia
‘whaaaaat! ilikuajeee’ nilimuuliza kwa mshangao sababu ya kutoamini alichokisema.

‘mwanangu Grace alifanikiwa kujifungua salama mtoto wa kike ambaye ndiye huyu hapa lakini baada ya kutoka hospitali na kurudi nyumbani kwenu kule mbezi beach alikutana na barua yako juu ya meza uliyomuandikia kuhusu kwenda kwako huko Oman kumtafuta Nairath kiukweli barua hiyo ndiyo ilikua chanzo kikubwa cha kifo chake kwani baada ya kuisoma tu presha ilimpanda akaanguka chini na kupoteza fahamu kitu kilichofanya arudi tena hospitali ambako alilazwa siku 3 na siku ya 4 saa 5 na nusu usiku akaaga dunia pasipo hata kumpa jina mtoto wake.’ mama aliniambia.

‘ni makosa yangu mama, kwa hiyo huyu ni mwanangu’ nilimuuliza.
‘ndiyo ni mwanao kabisa’ mama alinijibu.
‘mmempa jina gani?’ nilimuuliza tena.
‘tuliamua kumpa jina la Nairath kama ishara ya kuwakumbuka nyote’ alisema.
‘Nairaaaath!!?’ nilimuuliza kwa mshangao.
‘ndio anaitwa Nairath mbona umeshtuka’ aliniuliza huku nae akianza kulia.
‘mama Nairath nae amefariki na hawa hapa ni watoto wetu huyu wa kiume anaitwa Javier,na huyu wa kike anaitwa Grace’

Nilimwambia mama yangu huku nikizidi kulia na kumuelezea kila kitu na baada ya kumueleza aliwasogelea na kuwakumbatia huku na mimi kwa mara ya kwanza nikimnyanyua yule mtoto wangu na Grace na kumkumbatia kwa furaha na huzuni nyingi kwa sababu ya jina lake la Nairath kunikumbusha yale yote yaliyotokea kule Oman .
baada ya hayo yote mama alitutarishia chakula nika kila na kukimaliza kisha nae kwa mara ya kwanza akaenda kuwaogesha wale wajukuu wake wawili nilioenda nao na kuwanywesha maziwa ya kopo aliyokua akiyatumia yule Nairath mdogo na ghafla akiwa katika kuwanywesha baba yangu mzee Hernandez aliingia ndani akiwa ametoka national stadium kuangalia mpira na baada ya kuingia tulisalimiana akawaona wajukuu wake wapya tukaongea mengi na kisha tukaenda kulala.

Nilikuja kuamka majira ya saa 3 asubuhi kwa sababu ya uchovu, nikamsaidia mama yangu kuwaogesha wale watoto wangu nikanywa chai halafu nikampigia simu yule rafiki yangu kipenzi bwana Khamis Rajabu aliyekua akiishi kule masaki nikamuomba ampitie yule mamdogo wake na Nairath ambaye naye alikua akiishi masaki na wote waje nyumbani.
kwa wema mkubwa yule rafiki yangu alitii kwani walikuja wote nyumbani majira ya saa 5 asubuhi na tukaongea mengi wakawaona watoto wangu na kisha nikawaomba tuende sote mpaka nyumbani kwa mzee Sebastian tena kwa mara nyingine walikubali tukanda sote mpaka nyumbani kwa mzee Sebastiana na mkewe sehemu tulipoongea na kusameheana kabisa kila kitu huku tukionyana na kupeana tahadhari ili haya yote yasije kujirudia tena.

Tulisameheana kabisa na kusahau kila kitu kisha wakanipeleka mpaka sehemu lilipokuwepo kaburi ka Grace ambapo nilitoa heshima zangu za mwisho nikamuombea dua na kisha nikamuomba msamaha kwa sababu ya kukisababisha kifo chake.

‘Nisamehe Grace’ nilisema huku nikilia na kulitazama kaburi lake.

‘Javier usilie sana maana ulimpoteza Grace na sasa hivi unae Grace ulimpoteza Nairath na sasa hivi unae Nairath bila kusahau nyongeza ya Javier Hernandez’ yule rafiki yangu aliniambia.

‘ni kweli ninao wote lakini hii hainizuii kumuomba msamhama’ nilimwambia huku nikizidi kusema

‘kamwe sijatujia sababu ya kushindwa kutimiza ndoto zangu za kuwa daktari wa upasuaji wa neva na saikolojia bali nitajutia kwa sababu ya kusabisha kifo chako na kutoutambua upendo wako kwangu hakika kamwe sitokuasau.
Mmhhh Nisamehe Grace.

Na maisha yakaendelea kama kawaida.

….mwisho…

ABCDEFGHIJKLMNOPQRSTUVWXYZ

Nimesikitisha sana...

Kwa ujinga wa Javier, nilitamani sana awakose wote... na ndivyo imetokea...

Chpater Closed...


Cc: mahondaw
 
Asante mkuu nitarekebisha makosa katika simulizi zingine
MKUU upo vizuri kwa uandishi mzuri kwa kweli. ila umemaliza simulizi pasipo kueleza hadhira ukweli, Je! waliobakia walibaki salama or naowalikuwa wameathirika na vvu kati ya baba na watoto.

ABCDEFGHIJKLMNOPQRSTUVWXYZ
 
Back
Top Bottom