The Professor
JF-Expert Member
- Apr 30, 2013
- 2,223
- 4,587
NISAMEHE GRACE-01
Anza nayo..
“Grace Sebastian ni msichana aliyetokea kunipenda sana tokea siku ya kwanza nilipoonana nae chuoni kila mara nilipokua nikikutana nae hakuchoka kunitamkia wazi kua ananipenda kiukweli siwezi kueleza ni jinsi gani binti huyu alivyokua akinipenda kwani alijaribu kufanya kila njia ilimradi aweze kuushawishi moyo wangu ili uweze kuzikubali hisia zake lakini kwa bahati mbaya hakufanikiwa kwani moyo wangu haukuonekana kushawishika hata kidogo sio kwa sababu alikua mbaya bali kwa sababu ya moyo wangu kuzidiwa na nguvu ya macho yangu ambayo yalitokea kuvutiwa sana na uzuri wa msichana mmoja aitwae Nairath ambaye alionekana kuwa chotara wa kiarabu, kusema ukweli nilitokea kumpenda sana Nairath ambaye ndiye aliyekua ameuteka na kuuvutia moyo wangu kiasi cha kuufanya ushindwe kuzikubali hisia za Grace ambaye kiukweli alionekana kunipenda sana tena kwa dhati kwani licha ya kumueleza wazi na kumuambia ukweli kua sikua nikimpenda bado hakuchoka kuacha kunipenda.
yote haya yalikua ni ndani ya chuo kikuu cha kimataifa cha Mt.Anna kilichopo katikati ya jiji la Dar es salaam sehemu na mahali ambapo nilikutana na wasichana hao wawili ambao kiukweli walitokea kuyabadilisha na kuyayumbisha sana maisha yangu kiasi cha kufanya nishindwe kuyafikia malengo yangu na kushindwa kuwasahau na kuwatoa kabisa katika kumbukumbu za maisha yangu.
Ilikua ni tarehe 9 mwezi wa 4 mwaka 2011 wakati ambapo kwa mara ya kwanza nilikua nikipiga hatua zangu kuingia ndani ya majengo makubwa ya kisasa ya chuo hicho cha Mt.Anna kilichokua kikimilikiwa na familia moja ya kitajiri sana kutoka nchini Ujerumani.
Nilikua ninaenda kuchukua degree yangu ya kwanza ya udaktari katika magonjwa ya upasuaji wa neva pamoja na baadhi ya masomo ya saikolojia ambayo toka ningali mtoto mdogo nilikua na nikitamani sana kuja kuwa daktari hasa katika mambo hayo ya upasuaji wa neva pamoja na saikolojia.
basi mara baada ya kuingia ndani ya chuo hicho nilianza kuyatembelea maeneo yake ya ndani huku nikiyaangalia majengo yake marefu ya ghorofa yaliyokua yamejengwa kwa ustadi mkubwa sana huku nikizifurahia kuta zake zilizokua zimepambwa kwa rangi nyeupe pamoja na madirisha makubwa ya vioo yaliyoonekana kuyapendezesha sana majengo hayo ya ghorofa hakika nilihisi ni lazima ningepata mafanikio makubwa sana ndani ya chuo hicho cha kisasa kilichoonekana kuwa na karibu kila kitu kilichokua kikihitajika katika masomo ya kidaktari kuanzia mahabara mpaka maktaba na sehemu mbali mbali za kufanyia majaribio.
Basi baada ya kumaliza juma moja pale chuoni siku moja majira ya saa 5 asubuhi muda wa mapumziko nikiwa ninarandaranda ndani ya bustani za chuo hicho huku mawazo pamoja na akili zangu zote zikiwa zimeelekea ndani ya kitabu cha hadithi kiitwacho ‘I will be back’ nilichokua nikikisoma kwa makini sana huku miguu yangu ikijivuta vuta kwenye majani yenye rangi ya dhahabu yaliyokua yamepandikizwa katika kila kiunga wakati ambapo mwanga wa jua na kivuli ulikua ukionekana kuchezacheza juu ya matawi ya miti mikubwa iliyokua ndani ya bustanini hiyo.
Ghafla!! Nikiwa katika kusoma kitabu hicho cha hadithi kikichokua kimeandikwa na mwandishi mashuhuri sana aitwae Fredrick Libena nilishtuka kuona msichana mmoja wa umri wa kati ya miaka 23 – 25 akiwa mita chache mbele yangu huku akiwa anapiga hatua zake kuja sehemu nilipokua nimekaa kiasi cha kufanya nizifunike kurasa za kile kitabu nilichokua nikikisoma ambapo mara tu baada ya yule msichana kunifikia alinisalimia kisha akaketi mahali nilipokua nimekaa na kuanza kuniambia maneno ambayo kiukweli sikutegemea kabisa kuyasikia kutoka katika midomo ya binti huyo aliyeonekana kuwa na uzuri wa aina yake.
Kiukweli sikutaka kuyaamini kabisa maneno aliyokua ameniambia msichana huyo ambaye alikua amejitambulisha kwangu kwa jina la Grace Sebastian kitendo cha msichana huyo kuniambia kuwa ananipenda kilifanya nijione ni kama nilikua ndotoni kiasi cha kufanya akili yangu iwe ngumu kuamini kama kweli masikio yangu yalikua yameisikia vyema sauti laini ya binti huyo iliyoonekana kujaa utulivu wa hali ya juu kabisa.
Grace alikua ni mwanamke mzuri sana nakumbuka alikua na uchangamfu fulani ambao nilikua nikiupenda sana kifupi alikua mchangamfu sana kila mahali alionekana kuongea na kila mtu alikua ni mwepesi wa kucheka kiukweli kwa muda mchache nilioongea naye alifanya nijisikie vizuri sana hakika Grace alinivutia kwa kila kitu kuanzia nywele zake zilizouzunguka uso wake katika mtindo maarufu wa afro huku zaidi ya yote haiba na uchangamfu wake ukionekana kunivutia zaidi toka mwanzo kwa sababu ya mimi kua mkimya mwenye kuwaza mambo yangu na yeye kuonekana kuwa mwema na mchangamfu sana.
Sikumjibu kitu chochote mara baaada ya yeye kuwa ameniambia maneno hayo sio kwa sababu sikua nikimpenda bali ni kwa sababu ndio ilikua mara yangu ya kwanza katika maisha yangu kutamkiwa na mwanamke kua alikua akinipenda tena mwanamke ambaye ndio kwanza nilikua nimeonana nae siku chache huku yale yote tuliyayaongea ndio yakiwa maongezi yetu ya kwanza kabisa toka nionane nae.
Lilikua ni jambo gumu sana kumkataa msichana mzuri kama Grace ambaye alionekana kunivutia sana lakini pia ilikua ngumu sana kumkubalia Grace hasa kwa sababu ndio kwanza tulikua tumefahamiana nilijikuta nikimuomba Grace anipe muda wa kufahamiana kiundani zaidi huku nikimuomba kwanza tuwe marafiki mpaka pale muda ambao ningeona unafaa kwa sisi kuwa wapenzi utakapofika nashukuru Mungu kwani Grace alinielewa huku akisisitiza niweze kumfikiria kiundani zaidi kwa sababu alikua ametokea kunipenda sana kiasi cha kufanya ashindwe kujizuia kunitamkia hisia zake.
hapo ndipo urafiki na ukaribu wangu Grace ulipoanzia mara kwa mara Grace alionekana kuufurahia sana ule ukaribu wetu huku akinisaidia kwa kila kitu kutokana na uwezo na utajiri wa wazazi wake kiasi cha mpaka kufikia hatua ambapo watu wengi pale chuoni walianza kudhani kuwa nilikua nikitembea na Grace kiasi cha kuwafanya baadhi ya wanafunzi wenzangu ikiwemo na baadhi ya marafiki zangu waje kunipongeza huku wengine wakionekana kunitania sana kwa kusema walikua wakinionea wivu kwa sababu nilikua nikiufaidi uzuri wa sura na umbo aliokua nao Grace kitu ambacho kiukweli hakikua hivyo.
Ukaribu wangu mimi na Grace ulionekana kuwa wa furaha sana kiasi cha kufanya mpaka Grace aamini kua nilikua nimemkubali ombi lake ambalo kiukweli kwa ukaribu tuliokua nao sikua sikihitaji tena kumwambia kuwa nilikua nikimpenda kwa sababu mimi mwenyewe nilijikuta nikiwa ndani ya mapenzi mazito na Grace ambaye mpaka wakati huo sikua nimemtamkia wazi kama nilikua nikimpenda ingawa kiukweli mimi mwenye nilikua nikijihisi kuwa nilikua nikimpenda ten asana.
nakumbuka ukaribu wetu huo wa furaha ulidumu kwa muda wa miezi miwili na nusu mpaka ilipofika siku moja ambayo nilikwenda chuoni kwa kuchelewa na kwa sababu ya mvua kubwa iliyoonekana kunyesha ndani ya jiji zima la Dar es salaam kiasi cha kufanya nifike chuoni nikiwa nimelowana na kumkuta msichana mzuri sana aliyeonekana kuwa chotara wa kiarabu ambaye alionekana kuwa mgeni darasani humo akiwa ameketi juu ya kiti pamoja na meza yangu ya kukalia.
“ hii ni nafasi yangu lakini kwa sababu ya uzuri wako nitakuachia”
Nilijikuta nikimwambia yule mwanamke niliyemkuta amekaa juu ya kiti changu kwa sauti tena bila kujizuia huku nikiziinua hatua zangu kuelekea sehemu ilipokuwepo stoo ya chuo hicho kwa ajili ya kuchukua kiti kingine kiasi cha kufanya darasa zima pamoja na uyo msichana mwenyewe waonekane kuvunjika mbavu kwa kucheka sana huku kile kitendo cha mvua ile kunyesha kikionekana kutowapa ma lecture nafasi ya kuingia darasani kabisa.
Basi mara baada ya kuchukua kiti kingine nilikwenda kukiweka sehemu ileile ilipokuwepo nafasi nyangu mahali ambapo yule msichana mrembo alikua amekaa na mara baada ya kukiweka kile kiti na kukaa kabla hata sijamsemesha neno lolote yule msichana alinishukuru sana na kuniomba samahani kwa usumbufu huku akinitolea tabasamu zuri sana ambalo kiukweli liliufanya moyo wangu uanze kuzisahau habari za Grace ambaye mpaka wakati huo hakua bado amefika darasani.
“Usijali karibu sana ninaitwa Javier jisikie hupo nyumbani sawa kabisa na huko utokako”
Nilijikuta nikimwambia msichana yule huku nikijitambulisha jina langu ambapo mara baada ya kujitambulisha na yeye pia alijitambulisha kua alikua anaitwa Nairath na alikua amehamia chuoni hapo mara baada ya kuwa amemaliza masomo yake ya awali ya udaktari katika visiwa vya Oman.
Hapo ndipo ukaribu wetu mimi na Grace ulipooanza kuharibika kwani moyo wangu uligundua mara moja kua ulikua umeshaanza kumpenda sana Nairath kiasi cha kuanza kuuvunja ule ukaribu niliokua nao kati yangu mimi na Grace.
Nairath alikua mwanamke mrembo na mzuri sana pengine kuliko hata Grace hivyo ndivyo moyo ulivyokua umegundua hasa mara baada ya macho kuwa yakiuangalia uzuri wa Nairath kila siku huku yeye mwenyewe akiishia kutabasamu tu kila mara alipokua akigundua kuwa nilikua nikimuangalia sana.
uso wake mwembamba uliokua umepambwa kwa ngozi laini nyeupe huku macho makubwa meupe mazuri makubwa ya duara, pua yake ndefu nyembamba pamoja na midomo yake mizuri iliyokua imezawadiwa lips nzuri nyembamba laini sana zenye rangi nyekundu vikionekana kuupamba sana uso wa Nairath huku nywele zake ndefu nyeusi alizozilaza kwa nyuma zikionekana kunivutia zaidi kuliko ata ule uchangamfu wa Grace kiasi cha kufanya nishindwe kujizuia kumsahau Grace ambaye maskini ya Mungu alionekana kunipenda sana na kuumia kwa ajili yangu lakini sikua na jinsi zaidi ya kuzifuata hisia za moyo wangu.
Ilifika hatua nikashindwa kujizuia kabisa kumwambia ukweli Grace kuwa sikua nikimpenda kwa sababu kiukweli nilimuona amegeuka kua kero kutokana na kunisumbua mara kwa mara hasa kila alipokua akiniona nikiwa nimesimama au nikiwa ninaongea na Nairath ambaye mpaka wakati huo tulikua tumekua marafiki wa karibu kabisa kiasi cha kufanya nisiwe na wasiwasi wa kusubiria majibu atakayonipa mara tu baada ya mimi kumwambia kua nilikua nikimpenda sana.
“nisamehe sana Javier kwa kukusumbua kiukweli nakupenda sana siwezi kuishi bila wewe”
Grace aliniambia maneno hayo huku akiwa amepiga magoti na kulia kwa uchungu sana kiasi cha kuyafanya machozi yaliyokua yakitoka machoni kwake yazilowanishe nguo zake alizokua amezivaa.
Kiukweli sikua nikifurahi kumuona Grace akilia kwa sababu yangu nilikua nikiumia sana kumuona msichana yule mdogo tena wa familia ya kitajiri akiumia na kuteseka kwa sababu yangu na wala sikua nikimfanyia kusudi bali ni kwa sababu ya mapenzi mazito niliyokua nayo juu ya Nairath.
“Grace usilie! Kwa sababu yangu najua kuwa unanipenda sana na ninakushukuru sana kwa
Kunipenda lakini fahamu wazi sitoweza kuwa na wewe naomba unielewes Grace”
Nilijikuta nikimwambia Grace huku na mimi bila kujizuia nikashangaa mvua kubwa ya machozi ikianza kunyesha machoni kwagu huku ikisindikizwa na kilio kikubwa cha kwikwi.
Hivyo ndivyo ilivyokua lakini pamoja na hayo yote bado Grace hakuacha kunipenda mara kadhaa alikua akiniomba anirudishe nyumbani kwetu kwa gari lake aina ya Rv4 sikua nikimkatalia kwa sababu nilijua kama nikifanya hivyo lazima atazidi kuumia sana.
kitendo cha Nairath kuyakubali maombi yangu yangu ya kimapenzi ndicho kilichoonekana kumuumiza sana Grace kitu ambacho hata mimi mwenyewe nilikiona wazi kabisa kwani afya yake ilionekana kuanza kudhoofika sana kiasi hata cha Grace kuanza kulazwa hospitalini na kuongezewa maji mara kwa mara kwa sababu ya msongo wa mawazo aliokua nao.
ilifika hatua Grace akaumwa sana kiasi cha kuwafanya wazazi wake waje nyumbani kwetu kuongea na mimi pamoja na wazazi wangu huku wakiahidi kunipa kila kitu ninachokitaka kama endapo ningekubali kuwa na mtoto wao ambaye alionekana kuumwa ugonjwa wa kichaa cha mapenzi kwa sababu yangu.
kiukweli kitendo cha wazazi wake na Grace bwana na bibi Sebastian kuja nyumbani kwetu na kuongea kila kitu mbele ya wazazi wangu kilimuumiza kila mtu kwani kwa mara ya kwanza toka nizaliwe nilimuona mama yangu akilia machozi tena sio machozi ya furaha kusema labda mwanae nilikua naoa bali yalikua ni machozi ya huzuni ambayo kiukweli kila yalipokua yanadondoka sakafuni ndivyo nilivyojikuta na mimi nikianza kulia kiasi cha kufanya nijaribu kuulazimisha moyo wangu umsahau Nairath kitu ambacho kilionekana kuwa zaidi ya mchezo wa kuigiza ambao haukua na director kwani nilishindwa kabisa kiasi cha kuwafanya wazazi wa pande zote mbili wakubaliane na matokeo kitu ambacho kilionekana kuuweka uhai wa Grace matatani.
hivyo ndivyo hali halisi ilivyokua upande wa Grace ambaye aliukataa mpango wa wazazi wake kumtafutia chuo kingine nchini Marekani kwa sababu ya kuogopa kukaa mbali na mimi kwani licha ya wazazi wake kuamini kua huenda mpango huo ungemsaidia lakini Grace hakua tayari hata kidogo kwani aliamini kuwa ni lazima angekufa kama angekaa bila kuniona kwa muda wa wiki moja mfululizo.
Kadri siku zilivyozidi kwenda ndivyo mapenzi yangu mimi na Nairath yalivyozidi kuongezeka kiasi cha kuzidi kuihatarisha afya ya Grace ambaye ilifikia hatua mpaka akawa anapumulia mashine kwa sababu ya mawazo mazito aliyokua nayo kuonekana kuipandisha sana presha yake.
kiukweli hakuna aliyedhani kama Grace atapona hasa kwa sababu ya afya yake kuonekana kudhoofika zaidi ya ilivyokua safari za mwanzo hasa kile kitendo cha Grace kufungiwa mipira ya oksijeni kilisababisha darasa letu ligubikwe na huzuni kubwa huku baadhi ya wanafunzi wenzetu wakianza kunihukumu mimi kua nilikua muuaji kwa sababu ya kuwa chanzo cha matatizo ya Grace kiasi cha kutoridhika na hukumu yao hio isiyo ya haki na kuanza kumzonga na kumuandama sana Nairath ambaye mpaka wakati huo nilikua nikimuona ni kama ndiye pumziko la maisha yangu.
Itaendelea…..
nb: hii ni simulizi yangu ya kwanza kuiandika mwaka 2014 ko mapungufu yoyote tuvumilie, asanteni.
Sent using Jamii Forums mobile app
Anza nayo..
“Grace Sebastian ni msichana aliyetokea kunipenda sana tokea siku ya kwanza nilipoonana nae chuoni kila mara nilipokua nikikutana nae hakuchoka kunitamkia wazi kua ananipenda kiukweli siwezi kueleza ni jinsi gani binti huyu alivyokua akinipenda kwani alijaribu kufanya kila njia ilimradi aweze kuushawishi moyo wangu ili uweze kuzikubali hisia zake lakini kwa bahati mbaya hakufanikiwa kwani moyo wangu haukuonekana kushawishika hata kidogo sio kwa sababu alikua mbaya bali kwa sababu ya moyo wangu kuzidiwa na nguvu ya macho yangu ambayo yalitokea kuvutiwa sana na uzuri wa msichana mmoja aitwae Nairath ambaye alionekana kuwa chotara wa kiarabu, kusema ukweli nilitokea kumpenda sana Nairath ambaye ndiye aliyekua ameuteka na kuuvutia moyo wangu kiasi cha kuufanya ushindwe kuzikubali hisia za Grace ambaye kiukweli alionekana kunipenda sana tena kwa dhati kwani licha ya kumueleza wazi na kumuambia ukweli kua sikua nikimpenda bado hakuchoka kuacha kunipenda.
yote haya yalikua ni ndani ya chuo kikuu cha kimataifa cha Mt.Anna kilichopo katikati ya jiji la Dar es salaam sehemu na mahali ambapo nilikutana na wasichana hao wawili ambao kiukweli walitokea kuyabadilisha na kuyayumbisha sana maisha yangu kiasi cha kufanya nishindwe kuyafikia malengo yangu na kushindwa kuwasahau na kuwatoa kabisa katika kumbukumbu za maisha yangu.
Ilikua ni tarehe 9 mwezi wa 4 mwaka 2011 wakati ambapo kwa mara ya kwanza nilikua nikipiga hatua zangu kuingia ndani ya majengo makubwa ya kisasa ya chuo hicho cha Mt.Anna kilichokua kikimilikiwa na familia moja ya kitajiri sana kutoka nchini Ujerumani.
Nilikua ninaenda kuchukua degree yangu ya kwanza ya udaktari katika magonjwa ya upasuaji wa neva pamoja na baadhi ya masomo ya saikolojia ambayo toka ningali mtoto mdogo nilikua na nikitamani sana kuja kuwa daktari hasa katika mambo hayo ya upasuaji wa neva pamoja na saikolojia.
basi mara baada ya kuingia ndani ya chuo hicho nilianza kuyatembelea maeneo yake ya ndani huku nikiyaangalia majengo yake marefu ya ghorofa yaliyokua yamejengwa kwa ustadi mkubwa sana huku nikizifurahia kuta zake zilizokua zimepambwa kwa rangi nyeupe pamoja na madirisha makubwa ya vioo yaliyoonekana kuyapendezesha sana majengo hayo ya ghorofa hakika nilihisi ni lazima ningepata mafanikio makubwa sana ndani ya chuo hicho cha kisasa kilichoonekana kuwa na karibu kila kitu kilichokua kikihitajika katika masomo ya kidaktari kuanzia mahabara mpaka maktaba na sehemu mbali mbali za kufanyia majaribio.
Basi baada ya kumaliza juma moja pale chuoni siku moja majira ya saa 5 asubuhi muda wa mapumziko nikiwa ninarandaranda ndani ya bustani za chuo hicho huku mawazo pamoja na akili zangu zote zikiwa zimeelekea ndani ya kitabu cha hadithi kiitwacho ‘I will be back’ nilichokua nikikisoma kwa makini sana huku miguu yangu ikijivuta vuta kwenye majani yenye rangi ya dhahabu yaliyokua yamepandikizwa katika kila kiunga wakati ambapo mwanga wa jua na kivuli ulikua ukionekana kuchezacheza juu ya matawi ya miti mikubwa iliyokua ndani ya bustanini hiyo.
Ghafla!! Nikiwa katika kusoma kitabu hicho cha hadithi kikichokua kimeandikwa na mwandishi mashuhuri sana aitwae Fredrick Libena nilishtuka kuona msichana mmoja wa umri wa kati ya miaka 23 – 25 akiwa mita chache mbele yangu huku akiwa anapiga hatua zake kuja sehemu nilipokua nimekaa kiasi cha kufanya nizifunike kurasa za kile kitabu nilichokua nikikisoma ambapo mara tu baada ya yule msichana kunifikia alinisalimia kisha akaketi mahali nilipokua nimekaa na kuanza kuniambia maneno ambayo kiukweli sikutegemea kabisa kuyasikia kutoka katika midomo ya binti huyo aliyeonekana kuwa na uzuri wa aina yake.
Kiukweli sikutaka kuyaamini kabisa maneno aliyokua ameniambia msichana huyo ambaye alikua amejitambulisha kwangu kwa jina la Grace Sebastian kitendo cha msichana huyo kuniambia kuwa ananipenda kilifanya nijione ni kama nilikua ndotoni kiasi cha kufanya akili yangu iwe ngumu kuamini kama kweli masikio yangu yalikua yameisikia vyema sauti laini ya binti huyo iliyoonekana kujaa utulivu wa hali ya juu kabisa.
Grace alikua ni mwanamke mzuri sana nakumbuka alikua na uchangamfu fulani ambao nilikua nikiupenda sana kifupi alikua mchangamfu sana kila mahali alionekana kuongea na kila mtu alikua ni mwepesi wa kucheka kiukweli kwa muda mchache nilioongea naye alifanya nijisikie vizuri sana hakika Grace alinivutia kwa kila kitu kuanzia nywele zake zilizouzunguka uso wake katika mtindo maarufu wa afro huku zaidi ya yote haiba na uchangamfu wake ukionekana kunivutia zaidi toka mwanzo kwa sababu ya mimi kua mkimya mwenye kuwaza mambo yangu na yeye kuonekana kuwa mwema na mchangamfu sana.
Sikumjibu kitu chochote mara baaada ya yeye kuwa ameniambia maneno hayo sio kwa sababu sikua nikimpenda bali ni kwa sababu ndio ilikua mara yangu ya kwanza katika maisha yangu kutamkiwa na mwanamke kua alikua akinipenda tena mwanamke ambaye ndio kwanza nilikua nimeonana nae siku chache huku yale yote tuliyayaongea ndio yakiwa maongezi yetu ya kwanza kabisa toka nionane nae.
Lilikua ni jambo gumu sana kumkataa msichana mzuri kama Grace ambaye alionekana kunivutia sana lakini pia ilikua ngumu sana kumkubalia Grace hasa kwa sababu ndio kwanza tulikua tumefahamiana nilijikuta nikimuomba Grace anipe muda wa kufahamiana kiundani zaidi huku nikimuomba kwanza tuwe marafiki mpaka pale muda ambao ningeona unafaa kwa sisi kuwa wapenzi utakapofika nashukuru Mungu kwani Grace alinielewa huku akisisitiza niweze kumfikiria kiundani zaidi kwa sababu alikua ametokea kunipenda sana kiasi cha kufanya ashindwe kujizuia kunitamkia hisia zake.
hapo ndipo urafiki na ukaribu wangu Grace ulipoanzia mara kwa mara Grace alionekana kuufurahia sana ule ukaribu wetu huku akinisaidia kwa kila kitu kutokana na uwezo na utajiri wa wazazi wake kiasi cha mpaka kufikia hatua ambapo watu wengi pale chuoni walianza kudhani kuwa nilikua nikitembea na Grace kiasi cha kuwafanya baadhi ya wanafunzi wenzangu ikiwemo na baadhi ya marafiki zangu waje kunipongeza huku wengine wakionekana kunitania sana kwa kusema walikua wakinionea wivu kwa sababu nilikua nikiufaidi uzuri wa sura na umbo aliokua nao Grace kitu ambacho kiukweli hakikua hivyo.
Ukaribu wangu mimi na Grace ulionekana kuwa wa furaha sana kiasi cha kufanya mpaka Grace aamini kua nilikua nimemkubali ombi lake ambalo kiukweli kwa ukaribu tuliokua nao sikua sikihitaji tena kumwambia kuwa nilikua nikimpenda kwa sababu mimi mwenyewe nilijikuta nikiwa ndani ya mapenzi mazito na Grace ambaye mpaka wakati huo sikua nimemtamkia wazi kama nilikua nikimpenda ingawa kiukweli mimi mwenye nilikua nikijihisi kuwa nilikua nikimpenda ten asana.
nakumbuka ukaribu wetu huo wa furaha ulidumu kwa muda wa miezi miwili na nusu mpaka ilipofika siku moja ambayo nilikwenda chuoni kwa kuchelewa na kwa sababu ya mvua kubwa iliyoonekana kunyesha ndani ya jiji zima la Dar es salaam kiasi cha kufanya nifike chuoni nikiwa nimelowana na kumkuta msichana mzuri sana aliyeonekana kuwa chotara wa kiarabu ambaye alionekana kuwa mgeni darasani humo akiwa ameketi juu ya kiti pamoja na meza yangu ya kukalia.
“ hii ni nafasi yangu lakini kwa sababu ya uzuri wako nitakuachia”
Nilijikuta nikimwambia yule mwanamke niliyemkuta amekaa juu ya kiti changu kwa sauti tena bila kujizuia huku nikiziinua hatua zangu kuelekea sehemu ilipokuwepo stoo ya chuo hicho kwa ajili ya kuchukua kiti kingine kiasi cha kufanya darasa zima pamoja na uyo msichana mwenyewe waonekane kuvunjika mbavu kwa kucheka sana huku kile kitendo cha mvua ile kunyesha kikionekana kutowapa ma lecture nafasi ya kuingia darasani kabisa.
Basi mara baada ya kuchukua kiti kingine nilikwenda kukiweka sehemu ileile ilipokuwepo nafasi nyangu mahali ambapo yule msichana mrembo alikua amekaa na mara baada ya kukiweka kile kiti na kukaa kabla hata sijamsemesha neno lolote yule msichana alinishukuru sana na kuniomba samahani kwa usumbufu huku akinitolea tabasamu zuri sana ambalo kiukweli liliufanya moyo wangu uanze kuzisahau habari za Grace ambaye mpaka wakati huo hakua bado amefika darasani.
“Usijali karibu sana ninaitwa Javier jisikie hupo nyumbani sawa kabisa na huko utokako”
Nilijikuta nikimwambia msichana yule huku nikijitambulisha jina langu ambapo mara baada ya kujitambulisha na yeye pia alijitambulisha kua alikua anaitwa Nairath na alikua amehamia chuoni hapo mara baada ya kuwa amemaliza masomo yake ya awali ya udaktari katika visiwa vya Oman.
Hapo ndipo ukaribu wetu mimi na Grace ulipooanza kuharibika kwani moyo wangu uligundua mara moja kua ulikua umeshaanza kumpenda sana Nairath kiasi cha kuanza kuuvunja ule ukaribu niliokua nao kati yangu mimi na Grace.
Nairath alikua mwanamke mrembo na mzuri sana pengine kuliko hata Grace hivyo ndivyo moyo ulivyokua umegundua hasa mara baada ya macho kuwa yakiuangalia uzuri wa Nairath kila siku huku yeye mwenyewe akiishia kutabasamu tu kila mara alipokua akigundua kuwa nilikua nikimuangalia sana.
uso wake mwembamba uliokua umepambwa kwa ngozi laini nyeupe huku macho makubwa meupe mazuri makubwa ya duara, pua yake ndefu nyembamba pamoja na midomo yake mizuri iliyokua imezawadiwa lips nzuri nyembamba laini sana zenye rangi nyekundu vikionekana kuupamba sana uso wa Nairath huku nywele zake ndefu nyeusi alizozilaza kwa nyuma zikionekana kunivutia zaidi kuliko ata ule uchangamfu wa Grace kiasi cha kufanya nishindwe kujizuia kumsahau Grace ambaye maskini ya Mungu alionekana kunipenda sana na kuumia kwa ajili yangu lakini sikua na jinsi zaidi ya kuzifuata hisia za moyo wangu.
Ilifika hatua nikashindwa kujizuia kabisa kumwambia ukweli Grace kuwa sikua nikimpenda kwa sababu kiukweli nilimuona amegeuka kua kero kutokana na kunisumbua mara kwa mara hasa kila alipokua akiniona nikiwa nimesimama au nikiwa ninaongea na Nairath ambaye mpaka wakati huo tulikua tumekua marafiki wa karibu kabisa kiasi cha kufanya nisiwe na wasiwasi wa kusubiria majibu atakayonipa mara tu baada ya mimi kumwambia kua nilikua nikimpenda sana.
“nisamehe sana Javier kwa kukusumbua kiukweli nakupenda sana siwezi kuishi bila wewe”
Grace aliniambia maneno hayo huku akiwa amepiga magoti na kulia kwa uchungu sana kiasi cha kuyafanya machozi yaliyokua yakitoka machoni kwake yazilowanishe nguo zake alizokua amezivaa.
Kiukweli sikua nikifurahi kumuona Grace akilia kwa sababu yangu nilikua nikiumia sana kumuona msichana yule mdogo tena wa familia ya kitajiri akiumia na kuteseka kwa sababu yangu na wala sikua nikimfanyia kusudi bali ni kwa sababu ya mapenzi mazito niliyokua nayo juu ya Nairath.
“Grace usilie! Kwa sababu yangu najua kuwa unanipenda sana na ninakushukuru sana kwa
Kunipenda lakini fahamu wazi sitoweza kuwa na wewe naomba unielewes Grace”
Nilijikuta nikimwambia Grace huku na mimi bila kujizuia nikashangaa mvua kubwa ya machozi ikianza kunyesha machoni kwagu huku ikisindikizwa na kilio kikubwa cha kwikwi.
Hivyo ndivyo ilivyokua lakini pamoja na hayo yote bado Grace hakuacha kunipenda mara kadhaa alikua akiniomba anirudishe nyumbani kwetu kwa gari lake aina ya Rv4 sikua nikimkatalia kwa sababu nilijua kama nikifanya hivyo lazima atazidi kuumia sana.
kitendo cha Nairath kuyakubali maombi yangu yangu ya kimapenzi ndicho kilichoonekana kumuumiza sana Grace kitu ambacho hata mimi mwenyewe nilikiona wazi kabisa kwani afya yake ilionekana kuanza kudhoofika sana kiasi hata cha Grace kuanza kulazwa hospitalini na kuongezewa maji mara kwa mara kwa sababu ya msongo wa mawazo aliokua nao.
ilifika hatua Grace akaumwa sana kiasi cha kuwafanya wazazi wake waje nyumbani kwetu kuongea na mimi pamoja na wazazi wangu huku wakiahidi kunipa kila kitu ninachokitaka kama endapo ningekubali kuwa na mtoto wao ambaye alionekana kuumwa ugonjwa wa kichaa cha mapenzi kwa sababu yangu.
kiukweli kitendo cha wazazi wake na Grace bwana na bibi Sebastian kuja nyumbani kwetu na kuongea kila kitu mbele ya wazazi wangu kilimuumiza kila mtu kwani kwa mara ya kwanza toka nizaliwe nilimuona mama yangu akilia machozi tena sio machozi ya furaha kusema labda mwanae nilikua naoa bali yalikua ni machozi ya huzuni ambayo kiukweli kila yalipokua yanadondoka sakafuni ndivyo nilivyojikuta na mimi nikianza kulia kiasi cha kufanya nijaribu kuulazimisha moyo wangu umsahau Nairath kitu ambacho kilionekana kuwa zaidi ya mchezo wa kuigiza ambao haukua na director kwani nilishindwa kabisa kiasi cha kuwafanya wazazi wa pande zote mbili wakubaliane na matokeo kitu ambacho kilionekana kuuweka uhai wa Grace matatani.
hivyo ndivyo hali halisi ilivyokua upande wa Grace ambaye aliukataa mpango wa wazazi wake kumtafutia chuo kingine nchini Marekani kwa sababu ya kuogopa kukaa mbali na mimi kwani licha ya wazazi wake kuamini kua huenda mpango huo ungemsaidia lakini Grace hakua tayari hata kidogo kwani aliamini kuwa ni lazima angekufa kama angekaa bila kuniona kwa muda wa wiki moja mfululizo.
Kadri siku zilivyozidi kwenda ndivyo mapenzi yangu mimi na Nairath yalivyozidi kuongezeka kiasi cha kuzidi kuihatarisha afya ya Grace ambaye ilifikia hatua mpaka akawa anapumulia mashine kwa sababu ya mawazo mazito aliyokua nayo kuonekana kuipandisha sana presha yake.
kiukweli hakuna aliyedhani kama Grace atapona hasa kwa sababu ya afya yake kuonekana kudhoofika zaidi ya ilivyokua safari za mwanzo hasa kile kitendo cha Grace kufungiwa mipira ya oksijeni kilisababisha darasa letu ligubikwe na huzuni kubwa huku baadhi ya wanafunzi wenzetu wakianza kunihukumu mimi kua nilikua muuaji kwa sababu ya kuwa chanzo cha matatizo ya Grace kiasi cha kutoridhika na hukumu yao hio isiyo ya haki na kuanza kumzonga na kumuandama sana Nairath ambaye mpaka wakati huo nilikua nikimuona ni kama ndiye pumziko la maisha yangu.
Itaendelea…..
nb: hii ni simulizi yangu ya kwanza kuiandika mwaka 2014 ko mapungufu yoyote tuvumilie, asanteni.
Sent using Jamii Forums mobile app