Simulizi: Namchukia Mama Yangu

Sehemu ya 25

Niliingia ndani, nilipotupa macho kwa mbele nilishtuka kumuona mzee Sambi na mkewe wa mwanaume mwingine akiwa na mkewe wakizungumza.

Sikujua walikuwa wakizungumza nini na wale watu. Nilirudi nje haraka ili wasinione, wakati huo nao walionekana wanatoka, niliwachungulia kupitia kwenye tundu la mlangoni na kuona wote wakiingia kwenye gari zao ili waondoke.

Nilimuona mlinzi akisogea mlangoni kufungua geti, nilijificha nyuma ya mti uliokuwepo pale. Baada ya muda gari zilitoka na kuelekea mjini. Pamoja na kuyaona yale yote bado sikujua nini kinaendelea.

Magari yalipotoka na geti kufungwa nilisogea getini ili kutaka kujua zaidi ya ile nyumba yangu. Niligonga geti na mlinzi alitoka na kuniuliza:

“Nikusaidie nini dada, kama kazi sasa hivi hakuna nyumba imemalizika. “
“Sina shida hiyo.”

“Una shida gani?”
“Samahani kaka una muda gani hapa?”
“Una maanisha kuwepo hapa kivipi?”
“Kikazi.”

“Huu mwezi wa pili, kwani vipi?” mlinzi alionesha kunishangaa.

“Ndiyo maana unifahamu.”
“Kwani wewe nani?”
“Mimi...”
Nilianza kujitambulisha kwa kifupi.
“Sasa mbona sijawahi kukuona pia nyumba hii ni ya mkewe mzee Sambi.”

“Ndiyo wanavyosema?” niliuliza macho yamenitoka pima.
“Ndiyo, muda wote ulikuwa wapi?”
“Nilikuwa naumwa.”

“Mmh! Pole sana, kwa kweli siwezi kuchangia chochote labda muonane na mzee.”
“Sawa, na wale watu wamekuja kufanya nini?”
“Ni wapangaji ambao nielezwa wanaingia wiki ijayo.”

“Mmh! Asante.”
“Pole sana dada yangu kama unayosema ni kweli, siamini kama mzee yule anaweza kukufanyia ubaya huo. Basi hata ugonjwa wako naamini mkewe anahusika.”

“Kaka yangu wacha niende.”
“Lakini kama una hati za kiwanja utapata haki yako.”
“Aliichukua.”

“Basi nenda mahakamani nina imani utetezi wako utakusaidia kupata haki yako.”
Japokuwa maneno ya yule kaka yalikuwa yana ushauri mzuri, lakini muda ule yalikuwa yakinivuruga. Niliondoka bila kumuaga na kuelekea zangu barabara ambako nilichukua daladala hadi Mwenge kisha nilipanda za Tandika mpaka nyumbani.

Njia nzima sikupata jibu kuhusu mzee Sambi kwenda na mkewe kwenye nyumba yangu. Kilichonishtua zaidi kusikia ile nyumba ni ya mke wa mzee Sambi. Moyo uliniuma na kutokwa machozi njia nzima mtandio haukucheza mbali na uso wangu kwa ajili ya kufuta machozi.

Nilipofika nyumba nilikwenda chumbani kwangu na kuendelea kulia mpaka kichwa kikaniuma na kumuona mzee Sambi ni muuaji asiye na huruma.

Nilijiuliza kama matatizo ya ugonjwa yaliyotaka kuchukua uhai wangu sababu ni mkewe. Baada ya kuamini siponi alinikimbia bila kujua hatma yangu. Nilishindwa nifanye nini kwani kichwa kiliniuma sana kama kinataka kupasuka.

Mama baada ya kugundua hali yangu alinifuata ndani na kutaka kujua nina tatizo gani.

Sikuwa na jinsi nilimueleza yote niliyokutana nayo siku ile, japokuwa alinikataza kufuatilia chochote kwa mzee Sambi.

“Mwaija mbona mwanangu umekuwa na masikio magumu, nimekueleza achana na kila kitu chake, Una shida gani toka alipokukimbia?”

“Sina mama lakini roho inaniuma ile ilikuwa tayari nyumba yangu.”
“Kama haki yako utaipata kwa njia nyingine mwache kama anajifanya mjanja.”

“Kwa hiyo nifanye nini?”
“Achana naye, jipange kwa maisha mapya.”
Nilikubaliana na mama japokuwa moyo ulikuwa ukiniuma sana kwa unyama alionifanyia mzee Sambi na kuamua kumuachia Mungu.

Siku iliyofuata niliamua kwenda kwa mama Amina ili kumuomba anieleze matatizo yangu kinagaubaga na kumuomba asinifiche hata kitu moja.

Kama kawaida nilipofika nilikuta wagonjwa wengi, baada ya kunisalimia aliendelea na kazi zake. Baada ya saa moja aliniita ndani, nilipoingia na kukaa kwenye mkeka kwanza aliniuliza hali yangu.

“Namshukuru Mungu naweza kusema sasa nimepona.”
“Kazi imebakia moja kuhakikisha nasafisha ndoa yako, kwa vile nyota yako bado ipo juu nina hakika kwa uwezo wa Mungu mambo yako yatakuwa vizuri muda si mrefu.”

“Nashukuru sana mama Amina, ila nilikuwa na ombi moja.”
“Lipi hilo?”
“Kuhusu kufanana kwa matukio yangu.”
“Matukio gani?”

“Ya kuondokewa na wapenzi wangu bila kuelezwa tatizo, naomba leo unieleze kinagaubaga hata kama mama yangu anahusika naomba uniweke wazi nifahamu kisha tujue tufanye nini.”

“Mwaija mambo mengine hayatakiwi kuchambuliwa, kwa vile tatizo lako limekwisha angalia maisha yako yaliyopita achana nayo.”
“Hapana mama Amina huu utakuwa mchezo wa kuigiza, Naweza kupata mwanaume mwingine mambo yakawa yaleyale.”

“Nakuhakikishia matatizo yaliyo tokea hayatatokea tena.”
“Kivipi?”
“Tatizo lililokuwepo nimeishalimaliza japokuwa ilikuwa kazi nzito.”

“Unaweza kuniambia nani aliyefanya mchezo huu?”
“Wapo wawili, mmoja mke wa huyu mzee, na mwingine nina imani naye ameachana na mchezo huu,” mama Amina alinificha.

“Nani mama?”
“Hapana.”
“Sasa nani?”
“Shida yako kupona au kumjua huyo mtu?”
“Vyote.”

“Naomba basi nisikilize, acha kuchimbua vilivyopita. Mshukuru Mungu kukuponya.”
Sikutaka kumchimbua sana na kujikuta mawazo yangu nikihamishia kwa mama. Lakini wazo hilo nilipingana nalo kutokana jinsi mama alivyopigania maisha yangu.

Nilijiuliza atakuwa nani au dada mkubwa niliyemchukulia mpenzi wake. Lakini kama dada angekuwa amefanya vile alikuwa ananionea kwa vile tulikubaliana.

Hata wazo hilo bado sikukubaliana nalo kutokana na matatizo ya awali kunitokea nikiwa ndani ya ndoa yangu. Swali likabakia ni nani aliyenifanyia vile, kwa nini mama Amina hakuniambia kama alivyonieleza ya mke wa mzee Sambi?

Swali lile liliniumiza kichwa, sikutaka kumuuliza sana kwani ningemuuzdhi na kuonesha sina adabu kama makosa niliyofanya mwanzo. Wasiwasi wangu kutokea tatizo lingine na mama Amina kugoma kunisaidia kwa vile si msikivu.

Mama Amina alinipatia dawa za kuoga na makombe ya kunywa. Baada ya zoezi la mwisho alinieleza nifanye chochote bila tatizo. Nilirudi zangu nyumbani kichwa kikiwa kizito cha kujiuliza kwa nini mtu huyo hatakiwi kutajwa, ni nani?

Nilipanda gari la Mbande Tandika na kuteremkia Tandika. Kwa vile kulikuwa na njia ya mkato sikutaka kupanda usafiri wowote nilikatiza kwenda nyumbani.
Nilikuwa navuka barabara ya Devis Kona, nilisikia jina langu linaitwa.

“Mwaija.”
Sikuitika mpaka nilipogeuka na kumuona aliyekuwa akiniita. Alikuwa kaka mmoja tuliyekuwa tukikaa mtaa mmoja siku za nyuma, alikuwa kwenye gari.
“Abee,” niliitika na kugeuka kumsikiliza.
“Unatoka wapi?”

“Mbagala.”
“Kwema?”
“Kwema.”
“Kwa vile naelekea maeneo ya kwenu naomba nikusogeze.”

“Acha tu nitafika.”
“Hapana Mwaija nafika karibia na kwenu ingia twende.”

Sikutaka kuwa mbishi nilifungua mlango wa gari na kuingia. Baada ya kuondoka na tuliporibia Transfoma alinisemesha.
“Leo nina bahati ya kuonana na wewe.”
“Bahati ipi Juma?” nilimuuliza huku nikimtazama.

“Kwanza pole.”
“Asante,” nilimjibu kwa mkato.
“Nimekufuatilia muda mrefu.”
“Kuhusu nini?” nilimkata kauli.

“Subiri basi.”
“Haya endelea.”
“Mwaija kama usingeolewa na Beka ningekuoa mimi.”

“Kivipi?”
“Nilikupenda muda mrefu, huwezi kuamini kila hatua yako niliifuatilia mpaka mlipoachana na Beka. Wakati najiandaa kuja kwenu nilipata safari ya ghafla.
“Niliporudi nilikuta unaumwa sana, bado nikakufuatilia. Leo hii ninaweza kusema hii ni nafasi yangu.”

“Nafasi gani?”
“Ya kutuma maombi ya kukuoa.”
“Juma naomba sasa hivi suala ya mapenzi tuachane nalo.”

“Kwa sababu gani?”
“Nahitaji kupumzika, mapenzi yamesababisha nichungulie kaburi.”
“Bila matatizo hayo ungekuwa tayari?”
“Ndiyo kwa vile heshima ya mwanamke ni ndoa.”

“Kwa nini usinipe nafasi hiyo?”
“Labda baadaye, lakini sasa hivi nahitaji mapumziko ya muda mrefu, kwa sasa nayachukia mapenzi kuliko kitu chochote.”
“Kwa hiyo utakuwa tayari lini?”
“Niache kwanza.”

Juma alinifikisha nyumbani na kuniacha huku akiniomba awe sehemu ya mawazo yangu ya kila siku. Nilimkubalia ili aniache nipumzike kwa vile bado mbaya wangu aliendelea kuwa siri iliyonitesa sana.

Baada ya kufika nyumbani niliendelea kutumia dawa nilizopewa na mama Amina huku ombi la Juma likiwa halipo akilini mwangu.

Lakini kumbe mwenzangu ilikuwa tofauti, kumbe aliendelea kunifuatilia kwa karibu. Baada ya wiki mbili kukatika, mama aliniita na kunipa taarifa ya kujitokeza mtu wa kutaka kunioa ambaye ni Juma.

“Mama naomba suala hilo tuachane nalo kwa sasa.”
“Hapana mwanangu nakuomba ukubaliane nalo.”

“Mama nimechoka kila siku miye tu.”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Mapenzi yamekuwa mateso na kutishia uhai wangu kila siku.”

“Sasa hivi hayatatokea tena.”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Mimi najua, naomba unisikilize mimi mama yako.”

“Mmh! Sawa mama kwa vile nakupenda sana pia umenipigania maisha yangu kwa nguvu zako zote.”
“Nimefurahi mwanangu kunisikiliza mama yako.”

Nilikubaliana na mama kukubali kuolewa, huku nikishangaa mama yangu kuwa mbele katika kukubali kuolewa kwangu tofauti na siku za nyuma.

Majibu yalirudi kuwa nimekubali, mipango ya ndoa ilianza mara moja. Taarifa ile nilimweleza mama Amina na da’ Suzy wote waliniunga mkono uamuzi wa kukubali kuolewa tena.

Namshukuru Mungu nilipata ushirikiano wa hali na mali kwa familia, muda wote mpaka wakati wa ndoa yangu.
Niliolewa na Juma
 
Asante shunie..mwaija mwenye bahati yake ya ndoa
Sehemu ya 25

Niliingia ndani, nilipotupa macho kwa mbele nilishtuka kumuona mzee Sambi na mkewe wa mwanaume mwingine akiwa na mkewe wakizungumza.

Sikujua walikuwa wakizungumza nini na wale watu. Nilirudi nje haraka ili wasinione, wakati huo nao walionekana wanatoka, niliwachungulia kupitia kwenye tundu la mlangoni na kuona wote wakiingia kwenye gari zao ili waondoke.

Nilimuona mlinzi akisogea mlangoni kufungua geti, nilijificha nyuma ya mti uliokuwepo pale. Baada ya muda gari zilitoka na kuelekea mjini. Pamoja na kuyaona yale yote bado sikujua nini kinaendelea.

Magari yalipotoka na geti kufungwa nilisogea getini ili kutaka kujua zaidi ya ile nyumba yangu. Niligonga geti na mlinzi alitoka na kuniuliza:

“Nikusaidie nini dada, kama kazi sasa hivi hakuna nyumba imemalizika. “
“Sina shida hiyo.”

“Una shida gani?”
“Samahani kaka una muda gani hapa?”
“Una maanisha kuwepo hapa kivipi?”
“Kikazi.”

“Huu mwezi wa pili, kwani vipi?” mlinzi alionesha kunishangaa.

“Ndiyo maana unifahamu.”
“Kwani wewe nani?”
“Mimi...”
Nilianza kujitambulisha kwa kifupi.
“Sasa mbona sijawahi kukuona pia nyumba hii ni ya mkewe mzee Sambi.”

“Ndiyo wanavyosema?” niliuliza macho yamenitoka pima.
“Ndiyo, muda wote ulikuwa wapi?”
“Nilikuwa naumwa.”

“Mmh! Pole sana, kwa kweli siwezi kuchangia chochote labda muonane na mzee.”
“Sawa, na wale watu wamekuja kufanya nini?”
“Ni wapangaji ambao nielezwa wanaingia wiki ijayo.”

“Mmh! Asante.”
“Pole sana dada yangu kama unayosema ni kweli, siamini kama mzee yule anaweza kukufanyia ubaya huo. Basi hata ugonjwa wako naamini mkewe anahusika.”

“Kaka yangu wacha niende.”
“Lakini kama una hati za kiwanja utapata haki yako.”
“Aliichukua.”

“Basi nenda mahakamani nina imani utetezi wako utakusaidia kupata haki yako.”
Japokuwa maneno ya yule kaka yalikuwa yana ushauri mzuri, lakini muda ule yalikuwa yakinivuruga. Niliondoka bila kumuaga na kuelekea zangu barabara ambako nilichukua daladala hadi Mwenge kisha nilipanda za Tandika mpaka nyumbani.

Njia nzima sikupata jibu kuhusu mzee Sambi kwenda na mkewe kwenye nyumba yangu. Kilichonishtua zaidi kusikia ile nyumba ni ya mke wa mzee Sambi. Moyo uliniuma na kutokwa machozi njia nzima mtandio haukucheza mbali na uso wangu kwa ajili ya kufuta machozi.

Nilipofika nyumba nilikwenda chumbani kwangu na kuendelea kulia mpaka kichwa kikaniuma na kumuona mzee Sambi ni muuaji asiye na huruma.

Nilijiuliza kama matatizo ya ugonjwa yaliyotaka kuchukua uhai wangu sababu ni mkewe. Baada ya kuamini siponi alinikimbia bila kujua hatma yangu. Nilishindwa nifanye nini kwani kichwa kiliniuma sana kama kinataka kupasuka.

Mama baada ya kugundua hali yangu alinifuata ndani na kutaka kujua nina tatizo gani.

Sikuwa na jinsi nilimueleza yote niliyokutana nayo siku ile, japokuwa alinikataza kufuatilia chochote kwa mzee Sambi.

“Mwaija mbona mwanangu umekuwa na masikio magumu, nimekueleza achana na kila kitu chake, Una shida gani toka alipokukimbia?”

“Sina mama lakini roho inaniuma ile ilikuwa tayari nyumba yangu.”
“Kama haki yako utaipata kwa njia nyingine mwache kama anajifanya mjanja.”

“Kwa hiyo nifanye nini?”
“Achana naye, jipange kwa maisha mapya.”
Nilikubaliana na mama japokuwa moyo ulikuwa ukiniuma sana kwa unyama alionifanyia mzee Sambi na kuamua kumuachia Mungu.

Siku iliyofuata niliamua kwenda kwa mama Amina ili kumuomba anieleze matatizo yangu kinagaubaga na kumuomba asinifiche hata kitu moja.

Kama kawaida nilipofika nilikuta wagonjwa wengi, baada ya kunisalimia aliendelea na kazi zake. Baada ya saa moja aliniita ndani, nilipoingia na kukaa kwenye mkeka kwanza aliniuliza hali yangu.

“Namshukuru Mungu naweza kusema sasa nimepona.”
“Kazi imebakia moja kuhakikisha nasafisha ndoa yako, kwa vile nyota yako bado ipo juu nina hakika kwa uwezo wa Mungu mambo yako yatakuwa vizuri muda si mrefu.”

“Nashukuru sana mama Amina, ila nilikuwa na ombi moja.”
“Lipi hilo?”
“Kuhusu kufanana kwa matukio yangu.”
“Matukio gani?”

“Ya kuondokewa na wapenzi wangu bila kuelezwa tatizo, naomba leo unieleze kinagaubaga hata kama mama yangu anahusika naomba uniweke wazi nifahamu kisha tujue tufanye nini.”

“Mwaija mambo mengine hayatakiwi kuchambuliwa, kwa vile tatizo lako limekwisha angalia maisha yako yaliyopita achana nayo.”
“Hapana mama Amina huu utakuwa mchezo wa kuigiza, Naweza kupata mwanaume mwingine mambo yakawa yaleyale.”

“Nakuhakikishia matatizo yaliyo tokea hayatatokea tena.”
“Kivipi?”
“Tatizo lililokuwepo nimeishalimaliza japokuwa ilikuwa kazi nzito.”

“Unaweza kuniambia nani aliyefanya mchezo huu?”
“Wapo wawili, mmoja mke wa huyu mzee, na mwingine nina imani naye ameachana na mchezo huu,” mama Amina alinificha.

“Nani mama?”
“Hapana.”
“Sasa nani?”
“Shida yako kupona au kumjua huyo mtu?”
“Vyote.”

“Naomba basi nisikilize, acha kuchimbua vilivyopita. Mshukuru Mungu kukuponya.”
Sikutaka kumchimbua sana na kujikuta mawazo yangu nikihamishia kwa mama. Lakini wazo hilo nilipingana nalo kutokana jinsi mama alivyopigania maisha yangu.

Nilijiuliza atakuwa nani au dada mkubwa niliyemchukulia mpenzi wake. Lakini kama dada angekuwa amefanya vile alikuwa ananionea kwa vile tulikubaliana.

Hata wazo hilo bado sikukubaliana nalo kutokana na matatizo ya awali kunitokea nikiwa ndani ya ndoa yangu. Swali likabakia ni nani aliyenifanyia vile, kwa nini mama Amina hakuniambia kama alivyonieleza ya mke wa mzee Sambi?

Swali lile liliniumiza kichwa, sikutaka kumuuliza sana kwani ningemuuzdhi na kuonesha sina adabu kama makosa niliyofanya mwanzo. Wasiwasi wangu kutokea tatizo lingine na mama Amina kugoma kunisaidia kwa vile si msikivu.

Mama Amina alinipatia dawa za kuoga na makombe ya kunywa. Baada ya zoezi la mwisho alinieleza nifanye chochote bila tatizo. Nilirudi zangu nyumbani kichwa kikiwa kizito cha kujiuliza kwa nini mtu huyo hatakiwi kutajwa, ni nani?

Nilipanda gari la Mbande Tandika na kuteremkia Tandika. Kwa vile kulikuwa na njia ya mkato sikutaka kupanda usafiri wowote nilikatiza kwenda nyumbani.
Nilikuwa navuka barabara ya Devis Kona, nilisikia jina langu linaitwa.

“Mwaija.”
Sikuitika mpaka nilipogeuka na kumuona aliyekuwa akiniita. Alikuwa kaka mmoja tuliyekuwa tukikaa mtaa mmoja siku za nyuma, alikuwa kwenye gari.
“Abee,” niliitika na kugeuka kumsikiliza.
“Unatoka wapi?”

“Mbagala.”
“Kwema?”
“Kwema.”
“Kwa vile naelekea maeneo ya kwenu naomba nikusogeze.”

“Acha tu nitafika.”
“Hapana Mwaija nafika karibia na kwenu ingia twende.”

Sikutaka kuwa mbishi nilifungua mlango wa gari na kuingia. Baada ya kuondoka na tuliporibia Transfoma alinisemesha.
“Leo nina bahati ya kuonana na wewe.”
“Bahati ipi Juma?” nilimuuliza huku nikimtazama.

“Kwanza pole.”
“Asante,” nilimjibu kwa mkato.
“Nimekufuatilia muda mrefu.”
“Kuhusu nini?” nilimkata kauli.

“Subiri basi.”
“Haya endelea.”
“Mwaija kama usingeolewa na Beka ningekuoa mimi.”

“Kivipi?”
“Nilikupenda muda mrefu, huwezi kuamini kila hatua yako niliifuatilia mpaka mlipoachana na Beka. Wakati najiandaa kuja kwenu nilipata safari ya ghafla.
“Niliporudi nilikuta unaumwa sana, bado nikakufuatilia. Leo hii ninaweza kusema hii ni nafasi yangu.”

“Nafasi gani?”
“Ya kutuma maombi ya kukuoa.”
“Juma naomba sasa hivi suala ya mapenzi tuachane nalo.”

“Kwa sababu gani?”
“Nahitaji kupumzika, mapenzi yamesababisha nichungulie kaburi.”
“Bila matatizo hayo ungekuwa tayari?”
“Ndiyo kwa vile heshima ya mwanamke ni ndoa.”

“Kwa nini usinipe nafasi hiyo?”
“Labda baadaye, lakini sasa hivi nahitaji mapumziko ya muda mrefu, kwa sasa nayachukia mapenzi kuliko kitu chochote.”
“Kwa hiyo utakuwa tayari lini?”
“Niache kwanza.”

Juma alinifikisha nyumbani na kuniacha huku akiniomba awe sehemu ya mawazo yangu ya kila siku. Nilimkubalia ili aniache nipumzike kwa vile bado mbaya wangu aliendelea kuwa siri iliyonitesa sana.

Baada ya kufika nyumbani niliendelea kutumia dawa nilizopewa na mama Amina huku ombi la Juma likiwa halipo akilini mwangu.

Lakini kumbe mwenzangu ilikuwa tofauti, kumbe aliendelea kunifuatilia kwa karibu. Baada ya wiki mbili kukatika, mama aliniita na kunipa taarifa ya kujitokeza mtu wa kutaka kunioa ambaye ni Juma.

“Mama naomba suala hilo tuachane nalo kwa sasa.”
“Hapana mwanangu nakuomba ukubaliane nalo.”

“Mama nimechoka kila siku miye tu.”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Mapenzi yamekuwa mateso na kutishia uhai wangu kila siku.”

“Sasa hivi hayatatokea tena.”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Mimi najua, naomba unisikilize mimi mama yako.”

“Mmh! Sawa mama kwa vile nakupenda sana pia umenipigania maisha yangu kwa nguvu zako zote.”
“Nimefurahi mwanangu kunisikiliza mama yako.”

Nilikubaliana na mama kukubali kuolewa, huku nikishangaa mama yangu kuwa mbele katika kukubali kuolewa kwangu tofauti na siku za nyuma.

Majibu yalirudi kuwa nimekubali, mipango ya ndoa ilianza mara moja. Taarifa ile nilimweleza mama Amina na da’ Suzy wote waliniunga mkono uamuzi wa kukubali kuolewa tena.

Namshukuru Mungu nilipata ushirikiano wa hali na mali kwa familia, muda wote mpaka wakati wa ndoa yangu.
Niliolewa na Juma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sehemu ya 26

Namshukuru Mungu nilipata ushirikiano wa hali na mali kwa familia, muda wote mpaka wakati wa ndoa yangu.
Niliolewa na Juma, mfanyabiashara wa maduka ya nguo na vyombo vya umeme Kariakoo aliyekuwa amejenga Kibamba.

Namshukuru Mungu baada ya ndoa nilimuweka wazi mume wangu juu maisha yangu niliyopitia na umuhimu na mama Amina kwangu.

Hakuwa na tatizo alinipa ushirikiano ikiwa pamoja na kumualika mama Amina kwetu japokuwa kwenye harusi yangu alihudhuria na kunipa ushirikiano mkubwa sana.

Kuna kitu kimoja kilinifurahisha mama Amina japo mganga wa jadi alikuwa alikuwa wamo.
Akiamua kujilipua na pamba huwezi kuamini kama ni yeye anayevaa kaniki wakati wa kutibu.

Siku ya harusi nilimsahau nilivyolipuka na migold iliyomchafua kichwani mpaka mikononi. Alikuwa mganga wa kileo anayekwenda na wakati.

Namshukuru Mungu maisha ya ndoa yalikwenda vizuri baada ya muda nilishika ujauzito. Mama Amina aliufunga ili nisiupoteze tena.

Mungu alijalia nilijifungua salama mtoto wa kike mwenye afya njema. Kwa kweli maisha niliyoishi na mume wangu yalinikumbusha mbali huku wasiwasi wangu ukiwa ni kutokea yaliyotokea mwanzo.

Nilikuwa na furaha na malezi mazuri ya mume wangu pamoja na familia yangu kwa ujumla ilikuwa karibu. Lakini nilipokumbuka maisha ya zamani na misukosuko moyo ulikosa raha.
Nakumbuka vizuri siku moja nikiwa Kariakoo karibu na kituo cha Msimbazi Big Bon kituo cha mafuta niliguswa bega na mtu.

Nilipogeuka nilikutana na mtalaka wangu Beka.
“Mwaija,” aliniita akionesha kunishangaa.
“Abee.”

Japokuwa nilimpenda kuliko mwanaume yeyote lakini kitendo alichonifanyia sikumchangamkia nilimuona mtu wa kawaida.
“Za siku?”

“Nzuri.”
“Umeolewa?” aliniuliza baada ya kuona pete ya ndoa kidoleni.

“Uliponiacha ulitegemea siolewi tena?” nilijikuta nikizungumza huku nimebinua midomo japokuwa sikukipenda kitu kile katika maisha yangu.

“Mwaija bila vile ningebakia jina,” Beka alisema kwa sauti ya majonzi.
“Si nilikuuliza nani anataka kukubakiza jina huniambii ikabakia siri yako na familia yako huku ukitaka kunigombanisha na mama yangu.”

“Samahani naomba tutafute sehemu nzuri tuzungumze vizuri.”
“Leo ndiyo unaweza kumsema?” nilimuuliza nimemkazia macho.

“Kama mpaka leo hujui tatizo lazima nikueleze huenda likaiokoa ndoa yako ya sasa.”

Kauli ile ilinifanya niwe na hamu ya kumsikiliza. Tulisogea kwenye mgahawa uliokuwa karibu na kutafuta meza ya pembeni.

Baada ya kukaa tuliagiza vinywaji, nilitulia kumsikiliza Beka mtalaka wangu bwana na mwanaume wa usichana wangu ambaye alionekana maisha si mabaya.

“Mwaija najua unaweza kunichukia na kuniona adui yako kutokana na kushindwa kusema ukweli. Lakini nilifanya hivyo kulinda amani iliyo ndani ya familia yenu.

“Nina imani mama yako unampenda sana na unamuamini kwa kila kitu?”

“Ndiyo.”
“Ni vigumu kuamini mama yako ndiye aliyekuwa adui yako namba moja.”
“Etiii!?” nilishtuka kusikia vile.

“Ndiyo maana sikutaka kuyasema hayo kipindi kile kwa vile tungeweza kupotea wote kabla siri haijatoka nje.”
“Una maana gani?” sikumuelewa alimaanisha nini.

“Mwaija nina imani unanijua vizuri kuliko mtu yeyote?”
“Ndiyo.”
“Na maisha yangu unayajua vizuri?”
“Ndiyo.”

“Baada ya ndoa yetu kupigwa mizengwe na wewe kusimama kidete, mwisho tulifanikiwa kuoana. Namshukuru baada ya ndoa maisha yalikuwa mazuri sana, mpaka tukanunua kiwanja na kuanza ujenzi.”

“Ni kweli.”
“Tatizo lilianza baada ya kubeba ujauzito uongo kweli?”
“Ni kweli.”

“Na ujauzito wako ulitoka katika mazingira ya utatanishi?”
“Ni kweli kabisa.”
“Na baada ya hapo ndipo mikosi na mabalaa yalipoanza mpaka nikakosa hata kazi na wewe ni shahidi ulifuata fedha kwenu.”
“Ndiyo.”

“Kwa kweli sikujua chochote kuhusiana na matatizo yale kwa kuamini ni mipango ya Mungu. Lakini nilishikwa mkono na rafiki yangu aliyeshangazwa na anguko langu la ghafla na kunipelekwa kwa mtaalamu Handeni Tanga.

“Nilipofika huko niliyosikia kwanza sikuamini, niliamini mganga ni muongo. Alinieleza mambo mengi kuhusiana na matatizo yangu mpaka ya ndani ya familia yako.”

“Eeh!” nilishtuka kusikia vile.
“Eeh! Ndiyo, alisema chanzo ni mama yenu ndiye aliyefanya mambo ya kishirikina ikiwa ni kukutega mlangoni uliporuka ujauzito ukatoka kisha akaanza kuniwangia mpaka mambo yangu yakawa hayaeleweki.

“Alikwenda kwenye kiwanja na kuifunga nyumba yetu iliyokuwa kwenye hali nzuri ili tusiendelee huku akifunga riziki kila kona. Baada ya kuona pamoja na hali ya maisha kuwa mbaya lakini hutaki kuachana na mimi. Alianza kuitafuta roho yangu kuhakikisha ananitenganisha na wewe.

“Ilionesha hata kama ningekueleza usingekubali kitu ambacho kingefanya nipoteze maisha kwa vile alikuwa na nafasi ya kuja kwetu angenimaliza kwa urahisi.

“Japokuwa maneno ya mganga yalikuwa yakifanana na kweli, bado sikukubaliana naye kwa kuamini kauli ile ni ya uchonganishi ambayo ndicho chanzo cha vitabu vya dini kuikataa ramli.

“Ukweli kuamini moja kwa moja nilishindwa wala kukueleza jambo zito kama lile ambalo lazima lingeleta mpasuko. Nilimueleza mganga jinsi mama mkwe alivyonisaidia mpaka hata kupata nauli ya kwenda kule.

“Alinieleza kama siwezi kukueleza basi niachane na wewe. Ilikuwa vigumu kukubali kuachana na wewe mke wangu kipenzi ambaye naamini mpaka nakufa sitapata mwingine kama wewe.

“Mwaija hata sijui kwa nini nilichukua uamuzi huo heri ningesema mapema kwa jinsi ulivyokuwa ukinipenda ungeweza kunisikiliza, lakini wasiwasi wangu ndiyo ulionifanya nilie kila siku kukumbuka mke wangu mpenzi.

“Basi mganga alinieleza nichague moja katika matatu. Nikueleze ubaya wa mama yako, kama nikishindwa nikuache huku nikikueleza kila kitu anajua mama yako na kama ungemwambia angeujua ubaya wake au vyote vikishindikana nikubali kufa.”

Maneno ya Beka yalinisisimua mwili na kuanza kuamini yote aliyosema hasa baada ya mama Amina kukataa kunitajia mbaya wangu. Niliendelea kumsikiliza mtalaka wangu huku mapigo ya moyo yakinienda kasi.

“Kwa kweli bado sikuwa tayari lakini
alinichambulia moja baada ya lingine kama ameniumba yeye, hata sababu ya dada zako kuachika na kutokuwa na wazo la kuolewa tena.

Kama mtu akitokea anataka kuoa basi hugeuka ugomvi na kumfukuza kama mbwa.”
Maneno yale yalikuwa na ukweli kwa sababu dada alimfukuza mzee Sambi baada ya kumtaka kumuoa.

“Basi alinipa mtihani mmoja ili kuhakikisha anachosema ni kweli, aliniambia angenipa kitu ambacho ningekuja nacho kwenu. Mama yako angeniona angeanguka.

Alinieleza baada ya tukio lile nilitakiwa nikuache na kuondoka haraka kama ningeendelea kuwepo kwenu mama yako angekufa.”

“Ni kwa nini?” niliuliza mkono shavuni.
“Kwa sababu ya ubaya wake.”
“Unafikiri kwa nini amekuwa na tabia hiyo?” nilimuuliza swali ambalo nilitakiwa nilijibu mimi mwenyewe.

“Ni roho mbaya na kupenda kushiriki mambo ya kishirikina yamempelekea kupenda kucheza michezo ya kichawi.”

“Ehe, nini kuliendelea?”
“Kwanza nilikataa na kuamua kuachana na wazo hilo. Baada ya kubahatika kupata kazi katika mradi ya ujenzi barabara njia ya Tanga.

Nilifanya kazi kule kwa muda huku nikiwa na wazo la kutafuta njia mbadala tofauti na maelezo ya mganga.

“Lakini mganga alinieleza kama sijipendi nifanye kinyume na alivyonieleza. Baada ya kufanya kazi kwa muda nilipata nafasi ya kurudi nyumbani.

“Kabla ya kuja Dar nilirudi kwa mtaalamu ambaye alinieleza nifanye kama alivyonielekeza na kunieleza mambo nitakayoyakuta siku nitakayo kuja kwenu na hali itakayojitokeza.

Niliporudi Dar sikukaa nilikuja kwenu kila nilichoelezwa na mganga kilitokea ikiwa pamoja na mama yako kuanguka alipokuwa amekaa baada ya kushtuka kuniona.

“Kwa kweli tukio lile linifanya nichukue uamuzi mgumu wa kukupa talaka na kukuacha na fumbo kuhusiana na talaka yako.

“Niliamini mama yako angekueleza lakini hakukueleza, nilipo ondoka kwa kweli sikutaka kujua habari za nyuma. Leo unaponiona nina siku mbili na kesho naondoka kurudi nilipo, kwa yaliyonitokea nimejikuta sipendi tena kukaa jiji hili.”

Beka mpaka anamaliza kunielezea chanzo cha talaka yangu, macho yake yalikuwa yamejaa machozi. Si yeye hata mimi muda wote nilikuwa nalia huku nikitumia mtandio kujifuta machozi.

Nilijitahidi kuzungumza japokuwa moyo wangu ulikuwa kama umechubuliwa kovu lililoanza kupona na maumivu yake kuwa mara mbili.

“Beka nakubaliana na wewe kwa asilimia mia kuwa mama yangu anahusika, lakini bado hukutakiwa kuutesa moyo wangu kwa maswali yasiyo na majibu.

“Najua pengine mimi ndiye niliyesababisha kwa kutoa siri ya kipato chetu kwa mama. Lakini kwa vile ni mkeo ulitakiwa kuniweka wazi. Siamini kama kuna mwanadamu anaweza kuua bali kwa idhini ya Mungu.

Hata kwenye riziki anaweza kuichelewesha si kuizuia kabisa.

“Beka ungekuwa wazi ningejua nifanye nini, pengine ukimya wako umenifanya nichungulie kaburi au ningezikwa ningali hai.”
“Kwa nini?” Beka aliuliza macho yamemtoka pima.

Nilimueleza yote yaliyotokea baada ya kunipa talaka, maisha niliyoishi nakufika kuugua ugonjwa wa ajabu.
“Dah! Pole sana Mwaija, nina imani hata huyo bwana kuondoka kwake inawezekana mama yako kachangia.”

“Inawekana,” nilimkubalia.
“Lazima ujiulize kwa nini mtu akukimbie wakati wa matatizo?” aliniuliza.
“Beka nashukuru kwa maelezo yako ambayo naamini yamechelewa kunifikia nina imani leo hii tungekuwa pamoja.”

“Ni kweli lakini sina wa kumlaumu bali wasiwasi wa nafsi yangu.”
“Beka naomba nikapumzike kwa vile sijisikii vizuri, pia mwanangu nimemwacha muda mrefu.”
“Ha! Mwaija una mtoto?” Beka alishtuka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom