Sehemu ya 50
“Sofia nakupenda, nakuhitaji katika maisha yangu kuliko kitu chochote. Nakuomba nikuchumbie tena kisha nikuoe haraka iwezekanavyo.”
Maneno ya Alex yaliniingia, yakavuruga kabisa mwenendo wa uwazaji wangu. Alex aligusa udhaifu wangu maishani. Katika maisha ya ukubwa wangu nilitamani ndoa kuliko kitu chochote.
“Unanipenda Alex?” “Zaidi ya sana sofia, nakupenda.”
“Huwezi kuniacha tena?” “Hata iweje, siwezi kukuacha muhibu wangu.”
“Niko tayari unioe, nakukabidhi tena moyo wangu,” nilisema.
Tulikumbatiana kwa hisia kali. Kufumba na kufumbua tukajikuta tumeangukia katika uwanja unatoa vipaji vyote duniani, a.k.a kitandani.
Sikumpigia tena Victor. Namba yake nikaifutilia mbali. Sikujua tena habari zake. Naye hakunipiga kabisa mbwa yule.
****
NDOA yangu na Alex ilimstajabisha kila mtu aliyekuwa akifahamu historia ya maisha yetu. Tulifunga ndoa kwa siri kwenye kanisa moja liko nje kidogo ya jiji. Ilikuwa ni harusi ndogo iliyojumuisha watu wachache sana.
Niliyaanza maisha ya ndoa nikiwa mke wa bwana Alex. Mwanaume huyo alinipenda asikwambie mtu, maisha yetu yalitawaliwa na vicheko na tabasamu. Ile ndoto ya kuwa mke wa mtu ilitimia.
Zilikuwa ni nyakati nzuri maishani mwangu. Nyumba niliyokuwa naishi awali niliipangisha baada ya kufunga ndoa na Alex, nilihamia katika nyumba yake nzuri iliyokuwa Kijitonyama. Hapo ndipo nilikuwa nikiishi na muhibi wangu Alex.
Miezi ilipita, mwaka ukakatika. Ndoa iliyokuwa na furaha na vicheko mara ikaanza kukumbwa na dosari. Kwanza nilikuwa sishiki mimba, lakini jambo la pili, mume wangu Alex, alikuwa na tabia mpya. Tabia ya kutosikiliza shida zangu za usiku.
Hakuwa mwenye kujali hisia zangu, kama nisipomtaka mimi angeweza kukaa hata miezi miwili bila kugusa mwili wangu. Sababu yake kubwa ilikuwa ni kuchoka na kazi.
Mwanzoni nilikuwa namwamini kwa sababu alizokuwa akinipa, lakini baada ya kufanya uchunguzi nikabaini, hakuwa akichoshwa na kazi. Ni kwa nini sasa anakuwa hivyo?
Hilo ni swali ambalo kila kukicha nililitafutia majibu. Je simrizishi mume wangu? Au hana hisia nami? Aidha amekinaiwa na penzi langu ama mwanaume huyu anaye mwanamke mwingine anaye mzuzua? Niliamini katika maswali haya,