Simulizi: Muhanga Wa Mapenzi

Simulizi: Muhanga Wa Mapenzi

Sehemu ya 38

“Sijambo.” Mtoto wa kike nilijibu nikiwa sijiwezi kabisa mbele ya mwanaume yule. Sauti yangu niliitolea puani ili kumvutia mwanaume yule.

Kwa kweli Mr macho makubwa alikuwa ni kiboko yangu. Siku hiyo likuwa amevaa vizuri tofauti na alivyokuwa jana yake.

Alikuwa amevaa suruali ya jinsi ya kisasa, T’shart nyeupe ya Von dutch iliyomkaa vizuri. Chini alikuwa na raba kali ya bei mbaya.
“Hivi jina lako huwa unaitwa nani?” Mr macho makubwa akaniuliza.

“Naitwa Sofia. Wewe je?”
“Mimi naitwa...” kabla hajajibu mara akatokeza mwanamke mmoja nyuma yake, akamshika bega.

“MAMBO Victor,”mwanamke yule alimsalimu huku akimwangalia usoni kwa macho malegevu mkono wake ukiwa begani kwa mvulana huyo.

Sasa kupitia yule mwanamke, nilitambua kumbe Mr Macho makubwa anaitwa Victor. Walisalimiana na mwanamke yule kwa uchangamfu mkubwa.

Kwa kumwangalia mara moja tu mwanamke yule, nikabaini ni moja ya wanawake waliokubuhu kwa ushangingi mjini.
Asije tu kunipora mwanaume wangu huyu. Niliwaza.

Nilikuwa na wivu na Victor japokuwa hatukuwa tumeingia kwenye uhusiano wa kimapenzi. Siku hiyo ilikuwa ni siku ya kufungua ukurasa mpya wa maisha yangu na handsome boy huyo.

Upendo wangu kwakwe nisingeweza tena kuuficha. Nilikuwa tayari kuonekana wa hovyo mbele yake, lakini tu atambue kwamba nampenda.

Mapenzi kikohozi. Kuficha huwezi.
Baada ya kumaliza kusalimiana na jana jike lile, Victor alirudisha macho kwangu.
“Nani yule?” nilihoji, nilishindwa kabisa kuficha wivu usoni mwangu. “Mshikaji tu.”alijibu.

Ukimya mfupi ulipita kati yetu. Nilinyanya glasi ya kinywaji na kupiga fundo moja refu, lile donge kavu lililotokana na wivu nikahisi linayeyuka na kupotelea tumboni.

“Kumbe wewe unaitwa Victor!” nilianzisha mazungumzo upya.
“Aagh! Yes naitwa Victor.”
“Mbona leo hujakwenda kazini Victor?”
“Leo ni siku yangu ya off.”

“Kumbe leo upo Off. Ndio maana sikukuona,” “Kwani ulikwenda Maktaba?”
“Ndio Victor. Nilikwenda kwa ajili ya kukuona wewe tu.” Nilimwambia.

Akatabasamu, tabasamu lake ndio huwa linanimaliza kabisa mtoto wa kike.
Nikamuuliza tena.
“Unaishi wapi Victor?”
 
Sehemu ya 39

“Magomeni Mwembe chai, mtaa wa shekh Yahaya Hussein.”
“Umekuja hapa kufanya nini?”
“Kuna mtu mmoja nilikuwa na miadi naye hapa, bahati mbaya amepata udhuru.” Alisema.

“Ni nani. Mpenzi wako?” niliuliza kwa shauku, sauti yangu ilishindwa kabisa kuficha wivu wangu kwakwe.

“Hapana sio mpenzi,” alinijibu, kimoyomoyo nikasema: Afadhali. “Kwani wewe unaishi wapi Mrembo?” Naye aliniuliza. Kule kuniita mrembo, kuliifurahisha roho yangu.
“Naishi Mbeze Beach.”

“Umeolewa?” swali hili, nililipenda mno, niliona kwa kuulizwa hivi, tunazidi kusogea kwenye hatua ya kuwa wapenzi.
“Sijabahatika.” Nilimjibu. “Mchumba je?”
“Sina hata wa kusingiziwa”nilijibu kwa kujiamini.

“Hata mtoto?”
“Nimtoe wapi.”
Wote tukacheka. “Wewe je?” na mimi nikamuuliza huku nikimwangalia kwa macho ya kurembulia.

“Mimi ni kama wewe Sofia, sina mtoto, mke wala mpenzi.” Alisema. Sote tukatabasamu tena.

Kwa pamoja tukanyanyua tena glasi na kunywa kinywaji. Wimbo wa heart break hotel wa Elvis Presley ulikuwa ukipigwa kwa sauti ya chini katika spika za mapokezi bila kuvuruga maongezi yetu. “Familia yako iko wapi Victor?” nilizidi kumuuliza
“Familia ipo hapa hapa Dar, wewe je?” “Na mimi pia, ndugu zangu wapo hapa hapa jijini.”

“Miaka yako?” ilikuwa ni mwendo wa maswali.
“Miaka 27. Wewe je?”naye akaniuliza
“Mimi ni 24”

Kwa kweli tuliongea na kuulizana mengi mno siku hiyo. Kila mmoja alikuwa na hamu ya kujua maisha ya mwenzake. Kwa kiasi fulani nilimfahamu Victor. “Twende kwenye maji kidogo.” Mwisho Victor aliniomba baada ya kuwa tumekaa sana katika viti.

“Hakuna kitu naogopa kama maji.” “Usiogope upo na mimi, halafu tutachukua life jacket za kuogolea. Huwezi kuzama.”

Sikuwa na ubavu wa kumkatalia Victor. Tulikwenda katika sehemu fulani ndani ya hoteli ile, ambapo walikuwa wanatoa huduma za nguo za kwenye maji na maboya. tulibadilisha nguo na kuvaa nguo maalumu za kuogelea.

Tuliingia baharini na kuchezea maji, miili yetu ikiwa sehemu kubwa ni watupu. Macho ya Victor yalikuwa yakiniangalia kwa uchu na njaa kali.

Alinifundisha namna ya kupiga mbizi kwa mitindo mbalimbali. Kila alipokuwa akinigusa, nilihisi misisimko mikali mno, kuna wakati nikatamani anipe mkomboti mule mule majini.
 
Sehemu ya 40

Kwa masaa machache niliyokutana na Victor, a.k.a Mr Macho makubwa, nilijikuta nikifurahia mno maisha, nilitamani mwanaume huyo awe wangu peke yangu maisha yangu yote.

Baada ya kuchoka kuchezea majini, tulitoka ndani ya bahari na kurudi chumbani kuvaa nguo zetu. Wakati huo ilikuwa yaelekea magharibi.

Jua la jioni lilikuwa linaishilizia na kuacha mwanga wa manjano katika bahari.Upepo na baridi ukawa unavuma kwa kasi kuja pwani, nikawa natetemeka hadi meno yanagongana.

Victor akanisogelea na kunikumbatia, joto la mwili wake likanipa raha ya aina yake, nikatamani anikumbatie muda wote bila kuniacha.

“Pole kwa baridi mrembo, nadhani tuondoke sasa.” Victor alisema.
Nilikosa raha, hadi wakati huo hatukuwa kwenye makabaliano au mazungumzo yoyote ya kuingia katika uhusiano wa kimapenzi.

Kauli ya kuondoka, ilininyima raha, bado kuna kitu nilikuwa nakihitaji kwa mwanaume huyo, kauli yake ya ‘tuondoke’ ilinikosesha amani ya roho.
“Vipi mbona umekosa raha.”
“Sitaki uniache Victor, nakupenda.”

nilijikuta naropoka.
Victor akaningalia usoni bila kusema kitu, angalia yake ikanitia haya, nikashindwa kabisa kumtizama usoni. Sijui alinifikiriaje kwa kujilipua kule.
“Umekuja na gari lako?” aliniuliza.


Nikashindwa kuelewa gari langu linaingiliana vipi na kauli niliyomwambia. Hata hivyo ningefanya nini? Nilikwisha kuwa sijiwezi mbele ya mwanaume huyo. Nilitikisa kichwa kumkubalia.

“Twende.”
Nilitembea nikiwa sijielewi, nilikuwa nimeghafirika vibaya sana, asikwambie mtu hakuna jambo gumu kwa mwanamke wa kiafrika kama kumtongoza mwanaume.

Nilikuwa kama kondoo kwa mwanaume huyo, nilitii kila asemacho, mapenzi yalizidi nguvu ya utashi wangu.
Tuliingia ndani ya gari langu. Bila kujua mwanaume huyo alilenga nini hasa kwa kutaka tuingie garini.

Baada ya kufunga milango tu. Ghafla. Victor alinirukia kama fisi mwenye njaa, akanivutia kwakwe kisha akaninyonya ulimi wangu a.k.a denda.

Kufumba na kufumbua akaanza kunivua nguo zangu.

“Victor kwenye gari!!” nilisema nikiwa sijui kama natakiwa nimkubalie ama nimkatalie.

VICTOR hakujibu, alikazana kuifungua zipu ya sketi yangu kwa pupa. Pumzi zilikuwa zikimtoka kwa kasi kama mwanariadha wa mbio za marathoni.
 
Sehemu ya 41

Alinivua sketi, akanivua na blauzi. Nikabakia na kiguo cha ndani na sidiria, naye akavua t’shert na suruali. Akabakia na boxer.

“Victor mpenzi kwenye gari?” nilimuliza tena. Ndugu msomaji, labda unaweza kudhani nilikuwa sitaki ‘tuduu’ kwenye gari. Nilikuwa nataka sana, ila tu nilikuwa nazuga kumwonesha sikuwa na haraka na penzi lake.

Victor alitikisa kichwa kunitikia. Akanisogelea karibu na kunikumbatia. Joto la mwili wake liliponigusa nilihisi raha sana, nilitamani asitoke mwilini mwangu. “Nakupenda Victor,” nilimwambia tena kwa sauti ya chini.

“Nakupenda pia.”naye alinijibu kwa kunong’ona karibu na sikioni.
“Nataka uwe wangu wa milele.”nilimwambia tena.

Hakunijibu, alichofanya ni kuifyatua sidiria yangu, akajitoa kifuani mwangu kisha akaindoa kabisa ile nguo ya ndani.
Akanikumbatia tena, safari hii ncha za embe dodo zangu zikagusa kifua chake.

Wote tukahisi misisimko ya ajabu asikwambie mtu.
Ghafla. Tukaanza kunyonyana ndimi, nilijisikia faraja na raha kubwa kufanya kitendo kile dhidi ya mwanaume ninaye mpenda.

Mtoto wa kike sikuwa nyuma, wakati jambo lile linafanyika, mkono wangu mmoja ukashika mkomboti wa Victor uliokuwa wima, umekakamaa kama mwanajeshi wa umoja wa mataifa. Nikawa nauchezea kwa kupekecha pekecha. Acha mtoto wa watu achachawe.

Akawa anagumia kwa raha, naye kwa kweli hakuwa nyuma. Alikuwa mjanja sana kwenye mambo yetu hayo. Alikuwa akipitisha vidole vyake kwenye mfereji wa wa mgongo wangu mkono mmoja akibinya binya taratibu embe dodo zangu.

Ikawa ni mwendo wa nipe nikupe. sijui Victor alinishikwa wapi bwana, nikajikuta napiga kelele za kutaka mkomboti wake haraka iwezekanvyo.

Nilipoona anakawia, nilimchojoa ile boxer yake iliyokuwa bado ipo maungoni mwake nikaitupilia mbalia. Kama mtu aliyepandwa na mapepo, nikamsukumia kitini kisha nikaukalia mkomboti kwa juu. Angalau nikahisi ahueni dhidi ya hali iliyonipa baada ya kuguswa ile sehemu.

Japo uwanja hakuwa mzuri ila Ile mechi ilikuwa tafu sana, mbilinge mbilige halikuwa la kitoto. Mwisho gemu iliishia kwa matokeo ya mabao moja kwa moja.

Kwa lugha rahisi unaweza kusema mchezo ulikuwa sare. “Umeonjoy Sofia?”aliniuliza baada ya kupiga bao la kusawazisha.
 
Sehemu ya 42

“Ndio Victor. Ahsante.”
“Ahsante na wewe pia.”
Mwanaume yule alinibusu shavuni, kisha tukaanza kuvaa nguo zetu.

“Baby boxer yangu siioni.” Victor alisema. “Usijali, vaa tu suruali yako kesho nitaitafuta na kukutunzia.”

Wote tulicheka. Kisha tukavaa nguo zetu. “Sasa unaonaje nikikupeleka nyumbani kwako kwanza mpenzi.”
“Utakuwa umenisaidia sana, maana kwa muda huu magari ya kwetu hapa ni shida.” Alisema.

Niliwasha gari langu na kuondoka katika maegesho ya magari ya hotel ya Breez Lounge Msasani. Dakika 45 zingine nilikuwa Magomeni mwembe chai.
Mbele yetu kulikuwa na Nyumaba iliyochoka. Victor alinimbia ndipo alipokuwa amepanga chumba chake.

Mwonekano wa nyumba ile pia ulinipa picha aina ya chumba ambacho mwanaume yule alikuwa nacho
Nilijisikia vibaya sana kuona mwanaume ninayempenda anaishi maisha ya hohehahe. “Ndio pale!” nilisema tena nikiwa naikodolea macho nyumba ambayo victor alikwisha niambia ndipo kwakwe.

“Ndio kwangu hapo, mpenzi, karibu basi ndani, ” Alisema huku akinipapasa mapajani.
“Hapana Victor. Nitakuja siku nyingine, kwa sasa nimechoka nahitaji kuoga pia kupumzika.”

Sikutaka siku hiyo kuingia chumbani kwa mvulana yule, niliamini kama ningeingia chumbani kwakwe angenigeuza mkewe kwa kunipa mkomboti bab kubwa.

Sikutaka kabisa kujidanganya dhahama nitakayokutana nayo kwa kujipeleka kwenye geto la mtoto wa kiswahili Victor.

Mbona mpaka kuna kucha ningesahau nguo ya ndani
“Siku nyingine.” nilimwambia
Akateremka garini na kuelekea kwenye nyumba ile. Nilimpigia honi akageuka. Nikampungia mkono. Akatabasamu.

Alipotokomea na mimi nikaondoka. Nilipofika kwangu, nilibadili nguo, nikava kanga, kisha nikaenda bafuni kuoga.
Mtoto wa kike nikajiweka safi.

Nikazifunga nywele zangu vizuri, nikavaa nguo ya kulalia nikenda zangu sebuleni. Wakati huo ilikuwa yapata saa tatu usiku. Nikaliendelea jokofu na kuchukua maziwa ya Yoghati. Mara nyingi huwa napenda kula vyakula laini hasa nyakati za usiku.

Badaa ya kujisevia maziwa, nikajibwaga sofani kwa ajili ya kuangalia movie huku nikishushia maziwa. Majira ya usiku nikiwa nyumbani napenda kuangalia filamu mbalimbali hususani ‘Season’ nikachagua CD moja inaitwa ‘Lost’ nikawa naangalia.
 
Sehemu ya 43

Pamoja na kwamba macho yangu yalikuwa kwenye ile tamthilia ya kizungu, ila akili yangu ilishindwa kabisa kutulia pale. Kila wakati tukio la kwenye gari lilikuwa likijitengeneza akilini mwangu.

Kile nilichofanya na Victor kilikuwa kikijirudia kichwani mwangu, nilitamani sana nipate fursa ya kuishi na Victor, moyo wangu ulitokea kumuhusudu mno kijana yule.

Nikachukua simu ili nimpigie angalua nimtakie usiku mwema. Ghafla!! Moyo wangu ukapiga kite baada ya kubaini kumbe sikuwa na namba ya Victor. Lilikuwa ni kosa kubwa kwa kutochukua mawasiliano yake.

**** Siku ya pili, baada ya kukabidhi majukumu ya kikazi kwa wafanyakazi ofisini kwangu, nilieendesha gari hadi Magomeni Mwembe chai. Nisingeweza kushinda bila kumwona Victor wangu.

Nilipofika mbele ya nyumba aliyonilekeza usiku wa jana, nikashuka na kuifuata. Bahati nzuri nilimkuta mzee moja mbaye kwa mwonekano tu, alikuwa ni mmliki wa nyumba ile.
“Samahani babu.” Nilianza kuzungumza naye.

“Bila samahani bibi. Ongea.”
“Namuulizia kaka mmoja anaitwa Victor.”
“Victor!!”
“Ndio...”
“Hapa hakuna mtu mwenye jina hilo.”
“Eeh!”nilishituka.

“Yukoje huyo Victor.”babu akaniuliza.
“Mweupe kidogo, mrefu, akicheka ana kama anadimpozi mashavuni kwake.”
“Hapa haishi kijana mwenye sifa hizo.” Babu alinieleza. Macho yake yalionesha ukweli wa kile anachonimbia. “INAAMAANA Victor amenidanganya!!” niliropoka mbele ya yule mzee.

“Amekudanganya nini huyo Victor? Na ni nani yako?” mzee akahoji. “Ni mtu niliyekuwa nakutana naye huko posta, nilimwamini nikamkopesha pesa, akanieleza anaishi hapa,” nilimdanganya yule babu.

“Ooh!. Bibi umeibiwa. Hapa hakuna kabisa mtu mwenye jina hilo. Mimi ndiye mjumbe eneo hili, nawajua wakazi wote hapa. Hakuna kijana mwenye kuitwa Victor,” maneno ya yule mzee yalinikata maini.
 
Shunie,shunie,shunie weweee...! Utawafanya wanawake waanze kutafuta njia hiyo ya biashara mtandaoni,ya kuuza picha za uchi. Kama inalipa kwa namna hiyo na huku mtu hakugusi mbona haina shida kabisaaaa.
 
Shunie,shunie,shunie weweee...! Utawafanya wanawake waanze kutafuta njia hiyo ya biashara mtandaoni,ya kuuza picha za uchi. Kama inalipa kwa namna hiyo na huku mtu hakugusi mbona haina shida kabisaaaa.
Mmh sio kirahisi hivyo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom