Simulizi: Muhanga Wa Mapenzi

Simulizi: Muhanga Wa Mapenzi

Sehemu ya 44

Kinyonge nikamshukuru babu huyo na kuondoka zangu. Nilikuwa nimeghafirika vibaya sana. Nilikiri nilikuwa nimeangukia kimapenzi kwa tapeli wa mjini, Victor.

Niliendesha gari langu huku donge kavu likiwa limenikaba kooni, nilijsikia vibaya sana, kuharakisha kumvulia nguo mwanaume huyo. Nilijiona kama kiumbe niliyejidhalilisha mbele ya handsome boy huyo.

Mara mbili almanusra nipate ajali barabarani nikiwa naendesha gari langu, mawazo juu ya uhuni niliofanyiwa na Victor ulinifanya nikose umakini njiani, kichwa changu kilikuwa kimevurugwa.

Nilikuwa katika mgogoro wa ndani kwa ndani, sauti moja iliniambia nimtafute Victor, kisha nimhoji kisa cha kuniongopea, lakini kuna sauti nyingine iliniambia nikae mbali na mwanaume huyo.

Ukweli ni kwamba nilikuwa na hasira juu ya uongo wa Victor, lakini hilo halikufuta shauku ya kumwona mwanaume yule. Nilitamani nimpate nizungumze naye, labda alikuwa na sababu za msingi za kuniongopea. Nilikuwa nampenda mno. Hilo halikuwa na kificho.

Dakika 40 tangu nitoke kule Magomeni Mwembe chai, nilikuwa ndio naingia Posta mtaa wa Kisutu. Niliingiza gari katika maegesho ya Maktaba ya taifa na kulipaki.

Pale ndipo ilikuwa sehemu yangu ya mwisho, ya kumpata Victor wangu. Ni sehemu ya kwanza niliyokutana naye, nilimtambua kama mfanyakazi wa Maktaba, lau kama nisingempata hapo, kusingekuwa na mahali pengine pakumpatia.

Niliwafuata walinzi wa getini na kumuulizia. Walinzi hakuna walilokuwa wakifahamu, ila walichofanya ni kunipelekakwa jamaa mmoja mbaye ndiye alikuwa akihusika na utuzaji wa maktaba.

“Namuulizia jamaa mmoja anaitwa Victor, nadhani anafanya kazi hapa kama ‘Cleaner.”
“Victor!!” jamaa akauliza uso wake ukijawa mshangao.

“Ndio”
“Sijawahi kupata rekodi ya mtu mwenye jina hilo hapa. Halafu watu wa ‘Cleaner’ hakuna ambaye ni mfanyakazi wa kudumu hapa, kila siku tunachukua vijana wapya.”

“Mungu wangu!!”
“Kwani vipi dada?”
“Kuna mkaka mmoja mweupe kidogo, akicheka anavishimo mashavuni, niliwahi kukutana naye hapa akanieleza anaitwa Victor.”

“Oky fine, amefanya nini?” ofisa yule wa maktaba aliniuliza.
“Nina mdai” nilidamdanya.
“Pole sana dada, hapa sina taarifa za mtu mwenye jina hilo.” Nilinyong’onyea.
 
Sehemu ya 45

Niliondoka nikiwa na hasira, nilitambua hata majina yake alikuwa akibadili badili kila wakati, hili la Victor kama utakumbuka vizuri hakuniambia yeye, ila nilisikia akiitwa na mwanamke mmoja huko msasani loung beez Hotel jina.

“Victor mbwa wewe, ulaniwe milele huko uliko.” Nilinong’ona.
Niliondoka na kurudi nyumbani, kwa mara nyingine mapenzi yakanichapa.

Tukio la kufanya mapenzi kwenye gari langu lilikuwa likijirudia kila siku, kuna wakati niliumia kila kumbukumbu hiyo ilipojitengeneza akilini mwangu, na kuna wakati nilifurahia na kumisi mno Victor.

Hata hivyo kuna jambo nilijifunza, kitendo cha mwanamke kutoa mwili wake sadakalawe kwa mwanaume unaye kutana naye ndani ya muda mchache sio jambo zuri.

Kwa muda mfupi nilikuwa nimetokea kumpenda mno Victor, moyo wangu ulikuwa umekufa umeoza kwake, lakini mpumbavu yule hakuliona hilo. Naye kwa muda mfupi akaniumiza na kwenda zake.

Siku zilikwenda, miezi ikakatika, Victor sikumwona tena machoni mwangu, nikabakia na kidonda moyoni mwangu, kila wakati sura yake nzuri ilijitengeneza kichwani.

Niliishi kwa machungu nikiwa nimezingirwa na picha ya mwanaume huyo kichwani mwangu, ilikuwa hivyo kwa mwaka mzima, hadi siku moja ulipoibuka mkasa mwingine uliozifutuilia mbali kumbukumbu zote za Victor, mbwa yule.

****
Ilikuwa ni asubuhi Moja, nilikuwa katika kumalizia usingizi wangu wa asubuhi, usingizi ulioambatana na uchovu. Hii ni kutokana na usiku wa kuamkia siku hiyo, nilichelewa sana kulala baada ya kukesha katika harusi ya mfanya kazi wangu mmoja aliyekuwa anaoa.

Nikiwa katika ‘hang over’ kutokana na konyagi nilizozifakamia usiku huo, kiasi cha kunifanya nilale kama mfu, ghafla, nilistushwa na sauti kali ya kengele ya getini.

Nafsi ilitaka nisimame, lakini mwili iligoma, kengele ikazidi kugongwa. “Nanii aaagh!!” nilimaka. Sikupenda kabisa mgongaji aendelee kunivurugia pumziko langu asubuhi ile.

Na kwa mara ya kwanza nikaona umuhimu wa kuishi na dada wa kazi ambaye angeweza kunisaidia kuikabiliana na ile kadhia.
Kengele ikalia tena.
 
Sehemu ya 46

Nilisimama nikiwa na hasira kali, kimoyomoyo nikasema ole wake nimkute ni yule muuza samaki majinuni apitaye mtaani akipiga piga kelele za kunadi bidhaa zake huku akigonga mageti ya watu kama juha.

“Nikifika cha kwanza namtukana, halafu namfukuzia mbali ngedere huyu muuza samaki” Nilinong’ona.

Ilikuwa ni kabla sijapiga hatua tatu, mara nikapatwa na kichefuchefu na muda huo huo matapishi yakajaa mdomoni, nikakimbilia maliwato. Nikatapika hadi nikahisi utumbo unataka kutoka.

Nyagi si mchezo. Hii pombe huwa sijui naipendea nini kwa mateso yale. Kule getini mgongaji alizidi kubonyeza kengele. Hakuchoka.

Nilijisafisha, nikajiangalia kwenye kioo nywele zangu zilikuwa zimevurugika timtim, macho yameniiva kama mvuta bangi, nikasema ‘Yes’ hivi nilivyo natisha, hii inaafaa kukabiliana na huyu mpumbavu anisumbaye asubuhi hii.

Nilipolifikia geti nikafungua geti kwa pupa, macho ya hasira yamenitoka. Lahaulaa!! Sikuamini niliyemwona mbele yangu.

ALEX mchumba wangu na mwanaume wangu wa kwanza kuniingiza kwenye dunia ya mepenzi, alikuwa amesimama mbele ya mlango.

Mwanaume huyo ambaye nilikuwa na ndoto aje kuwa mume wangu, aliniacha siku moja kabla ya harusi yetu, ilikuwa ni baada ya kutumiwa picha zangu za chafu na mtu tusiyemjua, akaniacha nikiwa katika mkandamizo mkubwa wa penzi lake.

Nilikonda, dunia ikawa chungu, pombe ikawa kimbilio, nikawa kama katuni, nilichekesha machoni kwa watu. Ilikuwa almanusra niwe kichaa wa mapenzi.

Mungu si Athumani, usomaji wa vitabu, ukanirudishia haiba yangu, Alex nikamsahau. Nilipokutana na Victor, mwanaume mtamu ajuaye mapenzi, Alex nilimzika kabisa.

Ni kiasi kiasi cha mwaka mmoja na nusu tangu mambo hayo yote yapite. Leo Alex alikuwa mbele ya mlango wa nyumba yangu huku uso wake ukiwa umesawijika kwa mashaka na wasiwasi.

Tulibakia tunaangaliana kwa sekunde kadhaa bila yeyote kumsemesha mwenziye, kwa nukta chache nilijiuliza mambo mengi sana juu ya ujio wa mwanaume huyo.

Amefuata nini kwangu? Kuna kheri ama shari? Niliwaza.
“Kuna nini?” nilimuliza.
“Hunikaribishi?”
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom