Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 153,066
- 454,199
- Thread starter
- #61
Sehemu ya 43
Akawa na uhakika wa kumuona kila siku, moyo wake ulikuwa na furaha tele, alijisogeza kwa msichana huyo kiasi kwamba wakawa karibu mno na kila siku muda wa kwenda nyumbani, ilikuwa ni lazima amchukue John na kumpeleka mpaka Mwanga na kurudi zake nyumbani kwani hapakuwa mbali na mahali alipokuwa akiishi.
“Ulifanyaje mpaka kufanikiwa hivi?” aliuliza John.
“Ni kufanya kazi kwa bidii tu ila nitahitaji kufanya biashara zangu pia,” alijibu msichana huyo.
“Biashara gani? Inamaanisha mshahara hautoshi?” aliuliza John.
“Mshahara hauwezi kutosha! Na huwezi kufanikiwa kwa kutegemea pesa ya mshahara tu!” alijibu msichana huyo.
“Unamaanisha nini?”
“Ushasikia mtu amekuwa tajiri kwa kulipwa mshahara tu?”
“Hapana!”
“Basi ni lazima tuwe na biashara zetu, yaani lazima uwe na vyanzo vingi vya kuingiza mapato!” alisema msichana huyo.
“Oh!”
“Ndiyo hivyo!”
“Nashukuru kwa kunifumbua macho!”
“Na kwa nini umeacha biashara yako?”
“Ni kwa sababu ninahitaji kuajiriwa!”
“Unahisi utaingiza pesa nyingi kuliko kuuza samaki?”
“Hapana! Ila sitokuwa nazurura sana, inachosha, mwisho nigongwe na gari nife!” alisema John, wote wakaanza kucheka.
“Ila ungebaki kwenye biashara ingekuwa safi sana!” alisema Deborah.
“Najua ila kuna jingine kubwa!”
“Lipi?”
“Nilihitaji kuwa karibu na wewe!”
“Kuwa karibu na mimi?” aliuliza Deborah huku akionekana kushtuka.
“Ndiyo!”
“Kwa sababu gani?”
“Nakupenda!”
“Umesemaje?” aliuliza Deborah huku akipunguza mwendo wa gari!
“Ninakupenda!”
“Mimi?”
“Ndiyo!” alijibu msichana huyo, akasimamisha gari kabisa na kumwangalia John.
Akawa na uhakika wa kumuona kila siku, moyo wake ulikuwa na furaha tele, alijisogeza kwa msichana huyo kiasi kwamba wakawa karibu mno na kila siku muda wa kwenda nyumbani, ilikuwa ni lazima amchukue John na kumpeleka mpaka Mwanga na kurudi zake nyumbani kwani hapakuwa mbali na mahali alipokuwa akiishi.
“Ulifanyaje mpaka kufanikiwa hivi?” aliuliza John.
“Ni kufanya kazi kwa bidii tu ila nitahitaji kufanya biashara zangu pia,” alijibu msichana huyo.
“Biashara gani? Inamaanisha mshahara hautoshi?” aliuliza John.
“Mshahara hauwezi kutosha! Na huwezi kufanikiwa kwa kutegemea pesa ya mshahara tu!” alijibu msichana huyo.
“Unamaanisha nini?”
“Ushasikia mtu amekuwa tajiri kwa kulipwa mshahara tu?”
“Hapana!”
“Basi ni lazima tuwe na biashara zetu, yaani lazima uwe na vyanzo vingi vya kuingiza mapato!” alisema msichana huyo.
“Oh!”
“Ndiyo hivyo!”
“Nashukuru kwa kunifumbua macho!”
“Na kwa nini umeacha biashara yako?”
“Ni kwa sababu ninahitaji kuajiriwa!”
“Unahisi utaingiza pesa nyingi kuliko kuuza samaki?”
“Hapana! Ila sitokuwa nazurura sana, inachosha, mwisho nigongwe na gari nife!” alisema John, wote wakaanza kucheka.
“Ila ungebaki kwenye biashara ingekuwa safi sana!” alisema Deborah.
“Najua ila kuna jingine kubwa!”
“Lipi?”
“Nilihitaji kuwa karibu na wewe!”
“Kuwa karibu na mimi?” aliuliza Deborah huku akionekana kushtuka.
“Ndiyo!”
“Kwa sababu gani?”
“Nakupenda!”
“Umesemaje?” aliuliza Deborah huku akipunguza mwendo wa gari!
“Ninakupenda!”
“Mimi?”
“Ndiyo!” alijibu msichana huyo, akasimamisha gari kabisa na kumwangalia John.