Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,998
- 453,945
- Thread starter
- #21
Sehemu ya 21.
John hakuwa mzoefu wa mitaa mingi ya Kigoma Mjini hivyo rafiki yake, Jumanne ndiye aliyekuwa akimchukua na kwenda naye huko mitaani kufanya biashara ya kuuza samaki na kurudi nyumbani.
Maisha hayakuwa ya kawaida hata kidogo, kulikuwa na ugumu mkubwa mbele yake, hakukata tamaa, aliamini kuna siku moja angefanikiwa kama watu wengine, na inawezekana kabisa angeweza hata kuagiza gari kutoka Japan na kuliendesha katika mitaa hiyo.
Alipenda kujifunza kwa watu waliokuwa wamefanikiwa zaidi yake, aliamini kwa kufanya hivyo kungemfanya kuwa tofauti na watu ambao hawakuwa wamefanikiwa au hata kutokuwa na ndoto zozote zile za kufanikiwa mbele ya safari.
Alikuwa akitoka nyumbani alfajiri sana na alipokuwa akichukua samaki na kwenda kuwauza, mpaka majira ya saa sita mchana alimaliza na hivyo kutafuta sehemu zilizokuwa na watu waliokuwa wakiweka mijadala mbalimbali na kuanza kusikiliza.
Moyo wake ulikuwa na kiu kubwa ya kufanikiwa, hakutaka kujiona akibaki hapo alipokuwa miaka yote na ndiyo maana alijaribu kuwafuata watu waliokuwa wamepiga hatua na kuwasikiliza kile walichokuwa wamekifanya mpaka kuwa hapo walipokuwa.
Hapo Mwanga, kulikuwa na mzee aliyeitwa Miraji, huyu alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakiishi maisha mazuri. Alikuwa na nyumba nzuri, magari ya kifahari na alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakiishi kama wafalme katika mtaa huo wa uswahilini.
Nyumbani kwa mzee huyo kulikuwa na bomba la maji, watu ambao hawakuwa na mabomba nyumbani kwao walipendelea kwenda hapo na kuchota maji hayo.
Kwa sababu ya umri wake kuwa mkubwa, mara nyingi alikuwa akikaa yeye na wakati mwingine walikuwa watoto wake.
Kila alipomwangalia mzee huyo, alipata picha ya mtu aliyekuwa amefanikiwa.
Kwa muonekano tu aliokuwanao hakuwa kama watu wengine, alionekana kuridhika na kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha yake.
Alihitaji kumsikia akizungumza naye kuhusu mafanikio, alitamani kuweka nae ukaribu ili apate kile alichokuwa akikihitaji wakati huo.
John hakuwa mzoefu wa mitaa mingi ya Kigoma Mjini hivyo rafiki yake, Jumanne ndiye aliyekuwa akimchukua na kwenda naye huko mitaani kufanya biashara ya kuuza samaki na kurudi nyumbani.
Maisha hayakuwa ya kawaida hata kidogo, kulikuwa na ugumu mkubwa mbele yake, hakukata tamaa, aliamini kuna siku moja angefanikiwa kama watu wengine, na inawezekana kabisa angeweza hata kuagiza gari kutoka Japan na kuliendesha katika mitaa hiyo.
Alipenda kujifunza kwa watu waliokuwa wamefanikiwa zaidi yake, aliamini kwa kufanya hivyo kungemfanya kuwa tofauti na watu ambao hawakuwa wamefanikiwa au hata kutokuwa na ndoto zozote zile za kufanikiwa mbele ya safari.
Alikuwa akitoka nyumbani alfajiri sana na alipokuwa akichukua samaki na kwenda kuwauza, mpaka majira ya saa sita mchana alimaliza na hivyo kutafuta sehemu zilizokuwa na watu waliokuwa wakiweka mijadala mbalimbali na kuanza kusikiliza.
Moyo wake ulikuwa na kiu kubwa ya kufanikiwa, hakutaka kujiona akibaki hapo alipokuwa miaka yote na ndiyo maana alijaribu kuwafuata watu waliokuwa wamepiga hatua na kuwasikiliza kile walichokuwa wamekifanya mpaka kuwa hapo walipokuwa.
Hapo Mwanga, kulikuwa na mzee aliyeitwa Miraji, huyu alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakiishi maisha mazuri. Alikuwa na nyumba nzuri, magari ya kifahari na alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakiishi kama wafalme katika mtaa huo wa uswahilini.
Nyumbani kwa mzee huyo kulikuwa na bomba la maji, watu ambao hawakuwa na mabomba nyumbani kwao walipendelea kwenda hapo na kuchota maji hayo.
Kwa sababu ya umri wake kuwa mkubwa, mara nyingi alikuwa akikaa yeye na wakati mwingine walikuwa watoto wake.
Kila alipomwangalia mzee huyo, alipata picha ya mtu aliyekuwa amefanikiwa.
Kwa muonekano tu aliokuwanao hakuwa kama watu wengine, alionekana kuridhika na kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha yake.
Alihitaji kumsikia akizungumza naye kuhusu mafanikio, alitamani kuweka nae ukaribu ili apate kile alichokuwa akikihitaji wakati huo.