Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
- Thread starter
- #101
SEHEMU YA 55
“Kwa hiyo akaja kwako?” aliuliza mchungaji.
“Ndiyo!”
“Unaye?”
“Ndiyo! Nilimwambia arudi nyumbani lakini alikataa katakata!” alisema John.
Polisi waliagizwa kwa ajili ya kumchukua mwanaume huyo na kuondoka naye hivyo hicho ndicho walichokifanya, wakamfunga pingu na kuondoka mahali hapo.
Hakuwa na hofu, alipofikishwa huko, macho yake yakatua kwa wazazi wa Deborah ambao walionekana kuwa na hasira naye, hakujali, akachukuliwa na kuingizwa selo.
“Huyu muacheni akae humo hata siku tatu ili ashike adabu. Bila shaka Deborah atakuwa nyumbani kwake, naomba twende huko,” alisema baba yake Deborah.
“Unapafahamu anapoishi?”
“Sipafahamu ila kuna mshirika mmoja anaweza kutupeleka,” alisema mzee Abraham.
“Basi tumfuate huyo mshirika kanisani atupeleke kumchukua binti yako,” alisema polisi, hapohapo wakaingia ndani ya gari na kuanza kwenda kanisani kwa lengo la kumchukua mtu na kumpeleka nyumbani kwa John.
|
|
Je, nini kitaendelea?
Tukutane tena week ijayo jumatano au alhamisi.....
“Kwa hiyo akaja kwako?” aliuliza mchungaji.
“Ndiyo!”
“Unaye?”
“Ndiyo! Nilimwambia arudi nyumbani lakini alikataa katakata!” alisema John.
Polisi waliagizwa kwa ajili ya kumchukua mwanaume huyo na kuondoka naye hivyo hicho ndicho walichokifanya, wakamfunga pingu na kuondoka mahali hapo.
Hakuwa na hofu, alipofikishwa huko, macho yake yakatua kwa wazazi wa Deborah ambao walionekana kuwa na hasira naye, hakujali, akachukuliwa na kuingizwa selo.
“Huyu muacheni akae humo hata siku tatu ili ashike adabu. Bila shaka Deborah atakuwa nyumbani kwake, naomba twende huko,” alisema baba yake Deborah.
“Unapafahamu anapoishi?”
“Sipafahamu ila kuna mshirika mmoja anaweza kutupeleka,” alisema mzee Abraham.
“Basi tumfuate huyo mshirika kanisani atupeleke kumchukua binti yako,” alisema polisi, hapohapo wakaingia ndani ya gari na kuanza kwenda kanisani kwa lengo la kumchukua mtu na kumpeleka nyumbani kwa John.
|
|
Je, nini kitaendelea?
Tukutane tena week ijayo jumatano au alhamisi.....

