Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Simulizi: Mimi na Boss Wangu

SEHEMU INAYOFUATA.....

Licha ya ESTA kunifumbua macho na masikio juu ya kile ambacho sikuwa nakifahamu kabla,
Nilipanga kutokubadili msimamo wangu.

Yule jamaa kaja mpaka hapa kwangu akiwa na kusudi moja la kufanya kazi na mimi.Na sidhani kama Nina hadhi ya kufuatwa Hadi nyumbani na yule jamaa anayeonekana pesa si tatizo kwake.Nilijisemea moyoni.

Mume wangu,
Naona Kuna mapya hapa Sasa sijui itakuwaje,maana tunaambiwa kumbe hizo ni kampuni za mtu mmoja,
Huoni kama pengine ni mtego mume wangu? alihoji mke wangu .

Hapana,ni lazima niende kwanza wale ni watu wakubwa na maarufu hapa mjini hawawezi kuhangaika na Mimi ambaye Sina hata kipato Cha kueleweka,hivyo ni lazima nifike tu hiyo kesho.nilijibu pasipo kusita.

Sawa mume wangu wote hapa tunakuombea.

Asubuhi ya saa tatu asubuhi tayari nilikuwa maeneo ya mjini huku nikisikia upepo wa fulani kuashiria nipo karibu na bahari nikiwa nimeshika njia kuelekea kwenye ofisi za kampuni mpya

Nilifika huku walinzi wakinihoji maswali mengi ambayo niligundua ni kwa sababu nipo kwa miguu.

Oyaaa we ngosha, hebu mkague kwanza huyo, chunga sana hawa wanaokuja kwa miguu wanakuwa wanetumwa kuja kupeleleza watu

Aliropoka mmoja wa wale walinzi huku mkoba wangu uliobeba CV Ukiwa wa kwanza kufunguliwa.

Kisha nikasachiwa kibabe kuasi Cha wale walinzi kuchafua kaunda suti yangu, sikumaindi sana, labda kwakuwa hawanijui lakini pia ni taratibu za kazi maeneo mengi.

Nikaingia mapokezi nikamkuta jamaa mmoja aliyenichangamkia vizuri sana huku akiniita kwa majina huku nikiwa simjui , lakini haikunipa shida, pengine kapewa maelekezo na wajihi wangu,

Niliruhusiwa kuonana na bosi huku nikipandisha ngazi, kuelekea kule juu ghorofani ilipo ofisi yake, nilikaribishwa kwa heshima zote huku akiwa mchangamfu sana.

Sikutaka kuonesha hofu yoyote nilijilazimisha kujenga tabasamu fake huku nikiwa makini kuliko umakini wenyewe huku nikijiandaa kama yatajitokeza maswali ya kimitego.

Karibu sana bwana, bwanaaaa nani vile,

Nikamtajia full name.

Eeh ok ok,

Bila kukuficha bwana Daniel nilizisikia taarifa zako juu ya upotevu wa chombo sijui, kitu gani vile.

Ni hydraulic separator na pini joint za excavator, nilimjibu huku nikiwa Sina uhakika kama zinaitwa hivyo.

Ahaaaa ulienda kuzichukua mkoani siyo?

Ndiyo bosi . Nilimjibu jamaa huku akiwa anatafuna tafuna vyakula fulani vya asili ya uarabuni huko.

Sawa,hata hivyo kipindi tupo Oman na mzee ,tulizipokea taarifa zile tukakufikiria vibaya kupita maelezo
Lakini licha ya yote mzee wangu alikuwa njia panda,

Yaani alikuwa akikusifia sana kuhusu uchapakazi wako.

Kwani wewe boss unamwitaje?

Swali ambalo lilitakiwa kuishia kufikirika kichwani nilijikuta nimeropoka

Akacheka sana,

Ndiyo Mimi ni mtoto wa kwanza wa mzee (jina kapuni).

Najua umeuliza hivyo kwakuwa nilikudanganya nilipokuja siku ya Kwanza

Nilimwangalia, huku nikimuona kafanana sana na na boss wangu. Tuliongea mengi sana muda ule.

Ujue Daniel yule boss wako ambaye Mimi ni mama yangu mdogo alituaminisha mambo mengi sana kiasi Cha sisi kutaka kukuchukua ili tukuhoji. Pengine ni umetumwa kuja kudhohofisha kampuni zetu.

Lakini baada ya kukuchunguza tuligundua huna unalolijua ndugu yangu pole sana,

Japo nikukumbushe kuwa makini sana ujue kitendo Cha wewe kuibiwa mzigo stendi umeonekana mzembe kuliko maelezo, hii inaleta tafsiri ya kwamba wewe ni mtu wa kuwaamini sana watu haraka haraka.

Sikupaswa kuyasema yote haya ila Mimi nasema kwa upendo tu kwa kuwa wewe ni kama ndugu yangu
Najua nilipokuja kwako siku ile ulishangaa nimefikaje, lakini ni kwamba baada ya wewe kuwekwa ndani Kuna watu walikupeleleza sana kujua unaishi wapi, una familia gani lakini pia nje ya kufanya kazi na sisi unajishughulisha na Nini.
Taarifa zote zililetwa huku tukiwa tunakuchukulia kwa uzito wa juu. Kabla hatujagundua kuwa wewe ni mwepesi tu.

Hata hivyo kazi ya hapa nayokupa ni kubwa zaidi tumeamua kufanya hivi kwakuwa unafiti kukaa hapa lakini pia mzee alikuhurumia wewe kuteseka kule mahabusu, Sasa tukaamua kukupa nafasi nzuri, ila nafasi yako ya Sasa nikwambie ukweli, inahitaki umakini wa hali ya juu,

Ni kwamba utashughulika kuidhinisha vyombo vyote vya site
Yaani Equipments kwahiyo, chombo gani kibovu, kinahitaji kufanyiwa service gani, kinataka kiwekwe spear gani we ndiyo utakaye shughulika ukishirikiana na fundi mkuu wa hii kampuni,

Najua huwa Kuna asili ya majungu sana Kati ya mafundi wadogo na wale ma operator hata hivyo wewe komaa kwenye eneo lako tu , mtu ambaye ataharibikiwa na chombo Chake atamuona fundi mkuu wa site ya kule ambako ulikuwa unatumwa zamani.

Halafu taarifa zitamfikia engineer mkuu ambaye wewe utashirikiana naye kuingiza taarifa kwenye computer na sehemu mbalimbali

Kwasababu huwa Kuna ufanyaji wa maghumashi kwa mafundi kuharibu vyombo kwa makusudi Kisha kutafuta mianya ya kupiga hela.
Hivyo nafasi yako itasaidie kampuni kujua vifaa vilivyoharibika kihalali.

Haya yote nimekwambia kwa upendo tu, sikuwa na haja ya kukuelekeza, kwahiyo nenda kule mapokezi kanisubiri Kuna watu watakuita mida ya mchana baada ya kutoka lunch.
Alimalizia bosi huku Mimi tumbo likiwa linanikoroga kwenye kazi ambayo niliona imekaa kifitini zaidi.

Nilikaa pale nje huku nikifikiria vitu vingi ambavyo hata kupoteza ule mzigo wa kwanza ndugu zangu walihesabu ni ushirikina,kutokana na bifu za mafundi na Mimi Leo hii hata huku wananiweka huku huku Tena mbona ule mtego aliokuwa anasema mke wangu ndiyo huu naouona

Wakati nikiwaza hayo, alikuja mwanamke umri Kati ya miaka 30_35 .

Mr Daniel nifuate ofisini kwangu,

Nikainuka nikamfuata Hadi kule ambapo niliwakuta wanawake wengine wawili , walinikaribisha kwa bashasha mno huku wakiwa na tabasamu na lugha rafiki,

Nikaanza kupigwa spana na wale mademu ambao nadhani nje ya taaluma zao nadhani wapo pale kwa kigezo Cha uzuri wa sura na maumbo yao, niliulizwa maswali kadhaa, nikawajibu vizuri kabisa.

Taratibu zingine zikaendelea huku nikishangaa baada ya kupewa kazi tofauti kabisa na ambayo boss aliniambia pindi tunapiga stori

Cha kuingizwa kwenye computer kiliingizwa Cha kuandikwa kiliandikwa pa kusaini nilisaini, nikimuona ni mkataba rafiki usiotisha .kisha nikaongozana na mwanamke mwingine ambaye ni kama waigizaji wa kimarekani ambao ni ndoto kuwapata,

Tukafika mpaka kwa boss,ambaye aliniangalia kwa kutabasamu baada ya kuona nimepewa kazi tofauti.

Alijaza baadhi ya documents huku kazi yangu ikiwa ni kuanguka signature tu,kisha akamwambia yule dada atoke tukabaki wawili tu.

Safari hii hakuwa na maneno ya kirafiki Bali Kila alichosema alimaanisha,nikajua tayari nishakuwa mfanyakazi wake rasmi,hapa Dani utatakiwa kuripoti kazini kuanzia keshokutwa ,lakini pia nimetoa maelekezo kutoka ile kampuni yako ya mwanzo kwamba wewe utakuwa huku kwangu na mzee anatambua upo huku.tuliagana nikaondoka kwa furaha huku nikipewa laki elfu hamsini ya nauli

Nilifurahi sana hasa baada ya kuambiwa mshahara bwanaaaa.

Asikwambie mtu maisha ni kazi,na utamu wa kazi ni pesa.
Kubwa zaidi kazi niliyokuwa naiota hatimaye ninayo rasmi.
Ni kazi ya ndoto zangu.yenye malipo sahihi na hatimaye Kila kitu kimetimia.

Maisha tunayoishi karne hii ni ya kisasa, na ukisasa umeitawala Dunia haichagua masikini Wala tajiri.

Kila kitu kinaongozwa kisasa,na Kila kitu Cha kisasa ili ukipate ni lazima uwe na PESA.
Maisha ya kumuoa mtoto wa mtu Kisha kumpa Mashamba ni vitu vimepitwa na wakati

Hata wale wanawake wazuri duniani kote Ukiwa na pesa ni rahisi kuwapata, tunaishi Karne ambayo miliki pesa kidogo ugundue tabia za wanadamu hata huyo unayemwita mama mkwe yaani mama wa mkeo Ukiwa na pesa anaweza kukwambia neno la kufuru. Ukaambiwa hicho ulichokiona kwa mwanae yeye anacho Mara mia yake.

Ndiyo, mbona ni mambo nayasikia sana,.

Pata hela halafu ingia klabu matata halafu ukaone wale vidume wanavyojigongesha kwako.

Kama ni mgeni wa mambo ya mjini huwezi kuelewa, lakini ni kwamba hao vijana ni wale ambao wameamua kutusaliti wanaume wenzao kwa sababu wanazozijua wao, ama kweli Dunia inaisha.

Niliwaza sana kabla ya kushtuliwa na konda wa daladala,

Oy jombii vipi unageuka nayo nini,

kuangalia nakuta wale abiria wote wameshuka, gari inajiandaa kugeuza nikagundua nimepitiliza zaidi ya vituo vitano, kuangalia saa no saa kumi na mbili pia simu missed calls ni nyingi sana, nikatulia kwenye siti tayari kwa kurudi, ili nikashuke karibu na kwangu

Yule kinda nilimpa nauli yake akauliza wapi tena kiongozi mbona ulipandia mjini, hujashuka naona unarudi vipi.

Hamna nilipitiliza kituo, nashukia kituo Cha (nikataja)

Kama ni hapo tu shika pesa yako.
Wakati nikiikagua simu nikagundua imepigwa na watu wanne, ila boss wangu wa kike pekee kapiga Mara kumi na tatu, zingatia ni zaidi ya Mara kumi.

Huyu naye anatafuta Nini, nimefanya miezi minne tu kwao Sina ninachowadai na wao hawanidai

Ina maana hawajawasiliana kwamba Mimi nimechukua mkataba mwingine kwenye kampuni kongwe?

Kama nistahiki zangu Mimi nilishasamehe, pale najua nitakanyaga kwa sababu hizi kampuni zina ushirikiano.

Lakini si kwaajili yake huyu, anataka nini kwangu?

Oy kiongozi unawaza Nini tayari ushafika,konda alinishtua pengine ningepitiliza tena

Sehemu ijayo Ina majibu,kisa kinaitwa MIMI NA BOSS WANGU unataka kujua ni boss gani, bado kisa kibichi.

Itaendelea.....
 
SEHEMU INAYOFUATA...

Nikishuka kwenye gari huku nikigundua kuwa sipo sawa nikatafuta grosery iliyojificha ili nipate walau mbili tatu nipunguze mawazo.

Ni desturi kwa watu wengi kuhisi pombe hupunguza mawazo kumbe ni chanzo Cha kuingia kwenye huo uraibu mbaya.

Lengo la kwenda pale ni kutafuta nafasi ya kuongea na simu .
Nikaagiza bia huku nikimpigia boss wa zamani yule mwanamke

Baada ya kupokea simu malalamiko yakawa mengi,

Mbona wewe nakutafuta hupokei simu yangu, Ina maana tayari unajiona matawi ya juu baada ya kuajiriwa huko, Sasa kwa taarifa yako Mimi bado ni bosi wako kwakuwa bado unafanya kazi na mume wangu,

Nina mamlaka ya kukuachisha kazi hata muda huu, aliongea kwa jazba sana.

Hapana madam, kwanza Mimi nakuheshimu sana tu, natambua wewe bado ni boss wangu,
Simu sikuwa nayo niliiacha nyumbani ndo narudi muda huu nikaona ulinitafuta, nilijitetea kwa upole hasa ukizingatia Huyu ni mwanamke ukijichanganya, unaweza pata matatizo.

Hapana Dani ujue niliwaza tofauti sana, nikafikiri unaniletea dharau, kama ni hivyo sawa, ila nakuomba tuonane panga ratiba zako, na utenge muda wakuonana na wewe Nina mazungumzo, aliongea kwa sauti ya upole sijawahi kumsikia tangu nimfahamu.

Alikata simu,

Nikacheka kivivu baada ya yeye kunikatia simu, nikamalizia kinywaji changu nikashika njia kuelekea home.

Tulisalimiana na familia yangu pale huku Kila mmoja akiwa na shauku ya kutaka kujua Nini kimejiri, nikiwaeleza Kila kitu huku wakimshukuru MUNGU wa mbinguni baada ya kufanikisha mipango yetu.

Usiku wa siku hiyo nilichukua PC yangu ili nifungue sehemu mpya kwaajli ya kuhifadhi vitu vyangu vinavyohusu kampuni mpya.

Niliwaza mambo mengi sana kubwa zaidi likiwa ni kuanzisha biashara

Lazima niwe na kazi au mradi wangu wa kuingiza kipato, hizi kazi za watu siyo za kuzitegemea moja kwa moja
Kazi gani , Bora hata ningeajiriwa serikalini lakini hizi za watu binafsi hizi bado haziwezi kukupa ajira ya kudumu , safari hii nitahakikisha namiliki biashara yangu.

Asubuhi ya saa mbili ilinikuta ofisini huku nikienjoy zaidi mandhari ya ofisi mpya,haiba yangu ofisi mpya vilinipa muonekano mpya nilijisikia sana,amani ya moyo huku Kila kifaa Cha kieletronic nachokiona,kikiwa ni kipya,kwakuwa ilikuwa ijumaa ni kama nilikuja tu kupangilia ofisi yangu,nilipangilia nikaweka muonekano ninao utaka huku aliitwa fundi kwaajili ya kurekebisha kiyoyozi ambacho inlet ilifungwa mpya kwahiyo ikawa haipo standard

Akaja mwanamke mmoja muongeaji kupita maelezo,

Aaaaah Mr Daniel, karibu kwenye kampuni mpya baba,aliongea kwa sauti ya kichochezi

Ahsante sana, hata hivyo najivunia kuwa karibu na nyinyi,tuwekane wazi pale napokosea,nilijibu nikimtega.

Wewe mr, wewe una ofisi yako na Mimi yangu Tena tunafanya kazi zenye taaluma tofauti yaani unachofanya
Wewe Mimi hata sikijui hivyo nitakusahihisha vipi .

Aliongea yule Binti akiwa kakaza macho.

Hamna unajua nililenga zaidi makosa ya nje kuliko ya ofisini,nilijitetea

Ahaaaa kumbe una maana hiyo kweli kwa mfano, Mimi ninapopaki gari langu panajulikana, kwahiyo nikikuta Kuna mtu kapaki ile sehemu huwa nakuwa very bored.

Halafu Mr Daniel wewe gari lako huwa unapaki wapi mbona hata Jana sikukuona Ukiwa kwa gari
Alihoji yule Binti.

Kwanza nilishajikuta kama nadharaulika, nikadhibiti hasira zangu kwakuwa nilimuona Kama vile katumwa

Pili niliona anachoongea ni ukweli, ila ukweli unauma.

Ikabidi nimjibu kikakamavu, bila hofu yoyote,

Mimi Sina gari na sijawahi kumiliki gari langu binafsi.

Heeeey haya Mr. Ila nikwambie ukweli hufananii kabisa na mtu asiyekuwa na usafiri.Aliongea kidharau.

Kila mtu Ana mipango na malengo yake.huwezi kumpangia mtu namna ya kuishi awe na Nini na amiliki nini.
Nilimjibu kibabe,

Binti wa watu akanyongea, kwakuwa huwa sipendi kuwaudhi wanawake nikajishusha,

Nikwambie kitu my friend Mimi similiki gari la kutembelea lakini namiliki vitu vingi sana vya gharama na pia Nina mpango wa kuwa na gari hivi karibuni hivyo usijali ushauri wako nimeupenda sana.
Vipi tunaweza pata Chakula pamoja mchana huu. Niliongea kwa kulazimisha tabasamu.

Ndiyo hakuna shida,alijibu huku nikimuona Binti wa watu kama ananiogopa.

Nilimaliza shughuli zangu, nikatoka na yeye akaenda kuzima vitu vyake tukaingia kwenye gari lake, ni haya magari ya kawaida tu ambapo ningekuwa chizi magari tayari ningekuwa nalo siku nyingi.

Alinipeleka hotel moja ikanigharimu kama elfu thelathini hivi kwa wote wawili. Iliniuma kiasi ila nikaona kawaida. Maana wakati naingia tayari nilishajua bei zao.ieleweke kuwa Mimi huwa naishi maisha haya ya kawaida hata leo maisha yangu naishi kulingana na mazingira, na hadhi za watu, ila nakula kwa Hawa Hawa mamantilie.

Basi nikawa nimefanikiwa kurejesha tabasamu la Binti wa watu, na huwa napenda hivyo sipendi bifu na wanawake. Tukaongea mengi ya hapa na pale tukaagana akaondoka namimi nikashika njia ya kurudi nyumbani

Huku nikikumbuka jambo kuhusu mganga wa kienyeji wengine wanapenda kuwaita wataalamu.
Wazazi wangu, mkewangu, na baadhi ya marafiki huwa wananishauri kuhusu Mimi kujilinda, kujiwekea kinga dhidi ya husda na vijicho, pengine ndiyo maana nakuwa napata mikosi ni kwasababu ya kudharau hizi mambo

Nikafika home sikukaa, Wala sikutaka kumwambia mtu kuwa naenda sehemu za namna hiyo maana niliona kama najisibisha, kwakuwa najua alipo si mbali na nyumbani nikafika mpaka kwake nikakuta watu wengi kiasi sikujali sana miwani na kapelo vilinifanya niwe na amani

Zamu yangu ilifika, nikamweleza shida yangu , akasema sawa nikatajiwa kiasi kitakachogharimu.
Nikaambiwa kwa siku hiyo muda umeenda nije kesho.

Nikaaga na kuondoka huku nikiwa na wazo moja kuwa safari hii lazima nijizatiti.

Itaendelea............
 
SEHEMU INAYOFUATA......

Asubuhi tulivu kabisa ya jumamosi, niliamka mapema sana kwakuwa ilikuwa ni siku pekee ya kukamilisha mambo yangu mengi.

Eeh asubuhi asubuhi tu, mwenzangu wapi hiyo maana Leo ni jumamosi pumzika, aliongeza mke wangu .

Hapana unajua nikwambie kitu, yaani katika kipindi ambacho nahitaji kuwa na nidhamu ni hiki sipaswi kufanya kosa hata kidogo, Tena niandalie chai mapema Leo hata muda sidhani kama unatosha. Nilimjibu

Huku simu ya boss wa kike nayo ikiwa inaita asubuhi tu. Nikaipokea,

Habari mwanangu, naona Sasa hivi upo bize kuliko maelezo haya niambie, Leo ni jumamosi ni muda mzuri wa kuongea, mambo yetu.
Alisisitiza kwa upole sana

Unajua madam Mimi niwe mkweli na muwazi, Nina hofu sana juu ya wito wako na pia sioni umuhimu wangu kwako hasa ukizingatia tayari Mimi sipo kwenye kampuni yako, nilimjibu

Hapana Dani kwanza ujue tu kuwa hizi ni kampuni zinazofanya kazi ya aina moja zote zinajihusisha na ujenzi kwahiyo naamini ipo siku unaweza kuletwa kwenye huku kwangu kwahiyo sioni sababu ya wewe kunigomea nikikuhitaji. Aliongea kwa kuamrisha.

Suala la Mimi kuja huko, naamini nitakuja lakini ni kwa maelekezo ya waajiri wangu, hata hivyo hata Kama siji hapo ofisini sidhani Mimi Kama napaswa kuonekana na wewe sehemu tofauti na kazini.
Nahofia usalama wangu. Na pia kuja kupoteza kazi ambapo nitaitesa familia yangu. Mimi naona madam Kama una la zaidi ongea tu kwenye simu, inatosha.

Niliongea nikiwa tayari nishachoshwa, ningeweza hata kumjibu vibaya lakini nilihofia usalama wa kibarua changu, maana cheo alichonacho sipaswi kumjibu nitakavyo anaweza kukuachisha kazi.

Daniel, Daniel nadhani acha mawazo mabaya Mimi nina mazungumzo tofauti na mawazo yako, we sema tuonane wapi,

Nilifikiria kidogo, nikaona Bora aje maeneo ya nyumbani kwangu, maana huko kwenye mahoteli makubwa mnaweza kuonekana na watu wanaowajua wakafikiri wanavyojua wao, ili wakuchafue ukajikuta unaishia pabaya.

Jamani Daniiiiih ah nije huko njia za shamba Tena, yaani unanitesa wewe, kwani usije huju mjini bwana Kuna sehemu hiyo ni salama kabisa.

Lakini msimamo wangu ulikuwa mmoja tu aje karibu na nyumbani kama kilomita mbili kutoka kwangu.
Akakubali kishingo upande.

Basi madam nafikiri Chakula Cha mchana tutapata hukuhuku. Niliongea nikijipanga kugharamia hiyo huduma.

Weweee yaani huku maeneo ya kwenu ndiyo nije kula?
Hapana Kila mtu ale anapopajua kwahiyo huko tutazungumza mambo mengine tu, nikakubali huku nikiwaza Ina maana hata nyumbani kwangu hawezi kula, ndiyo hawezi si kasema huku hakuna vyakula vya kula yeye moja kwa moja tunaonekana tunaoishi huku ni wachafu.
Ah kwanza afadhali mambo ya kula pamoja mnaweza kuwekeana sumu bure, nilijiwazia.

Nikaona ule ni muda muafaka wa kwenda kwa mtaalamu wa Jana sikumuaga yeyote kwakuwa sikutaka wajue kama tayari najihusisha sehemu hizo. Nilifika pale yule mtaalamu akaanza mambo mengine Mara ooh , inatakiwa kuku mweupe sijui rangi gani.

Nikaona yaani niingie mtaani nianze kutafuta kuku Tena mweupe, halafu Kila mtu ajue kabisa kuwa naenda kufanya nini, aaah mbona ishu kubwa
Niliwaza.

Sema Nini baba yangu hapa kuku wapo Tena unatakiwa upate kuku anayejifunza kuwika , nikiwa na maana anaye babaika hajanyoosha vizuri, halafu nitatengeneza dawa huku nikinuizia mambo mengi, yaani kifupi nakutengenezea heshima.

Utaheshimika na Rika zote, mke atakupenda na kukuogopa pia.
Hata wafanyakazi wenzio watakuwa wazito kufanya maamuzi juu yako hata Kama Wana mpango wa kukuchoma kwa bosi basi watajikuta wanaishia njiani.

Hata bosi wako unaweza kumkosea jambo kubwa lakini ukakuta limeyeyuka na wewe unadunda tu, ndugu yangu hii ni Dunia. Dunia Ina mambo mengi lazima ujue kuwa tunaishi kwenye ulimwengu wa ushindani.

Yaani unaweza kununua gari, mtu akasema kanunua gari si Bora angejenga, unaweza kujenga ukaambiwa ni Bora angenunua usafiri uwe unarahisisha mipango yake kujenga angejenga tu kwani analala nje, Hawa ni walimwengu

Unaweza kumiliki vyote kwa pamoja gari nzuri na nyumba nzuri, lakini ukaambiwa huo mtindo wake wa kuipakia familia yake ipo siku watapata ajali na tukawazika wote, sasa kwanini uombewe mabaya kaka.Aliongea yule mtaalamu.

Tukirudi upande wa nyumba utaambiwa Mara ooh kijumba chenyewe kidogo Bora angesubiri apate pesa nyingi zaidi ajenge nyumba ya maana.

Ukijenga kubwa zaidi utaambiwa kajenga jumba kuuubwa si Bora hata angejenga mbili nyingine akapangisha. Yaani jambo lako, bajeti zako, lakini mtu atakupangia yaani mtu anaweza kufanya jambo baya kabisa wakati hujamkosea lengo akurudishe nyuma

hao ndio wanadamu kaka Sasa lazima wakumbane na dhoruba yangu, nitakutengenezea dawa utakunywa na utachanja chale mbili tu kifuani ili Kila utakayemtunishia kifua ajikute ananyong'onyea, lakini kila atakaye jaribu kukuharibia ajikute anababaika kama kuku anayejifunza kuwika.Alimalizia mtaalamu huku nikiwa Sina hata chembe ya pingamizi.

Aliita vijana wake wamletee yule kuku ni kweli alikuwa hajakomaa nikaambiwa nitamke maneno fulani , nikafanya hivyo,nikawapa wakaenda kumchinja wakatengeza mchanganyiko fulani wa dawa,Kisha tukaingia kilingeni,

Aiseee hii Dunia Ina mambo hii,tukatoka baada ya kumaliza,nikalipa nikaruhusiwa huku nikisisitizwa kuwa na IMANI.
Kwakuwa niliambiwa kuoga si tatizo,nilirudi nilijimwagia maji huku nikitulia pale sebuleni nikijihesabu kuwa na Mimi ni mshirikina tayari,
Duh,kweli ukubwa jalala Bora utoto niliwaza kizembe.

Nikapokea simu ya madam akinieleza kuwa tayari anakaribia kufika, nikatoka pale home tayari kuelekea alipo,

Nikafika eneo lile sikupata taabu kujua alipo ni baada ya kuiona range imepaki karibu na zahanati fulani, ni gari ambayo si tu kwakuwa naifahamu Bali hakuna gari kama ile pale mtaani,

Tukasalimiana, mmmh Dani hivi huku ulikupendea Nini mwenzangu maana kulivyo halafu nyumba zinajengwa bila mpangilia Ina maana mamlaka hazioni, na pia ningependa kuona nyumba yako,

Aliongea bila breki,

Haaaa madamuuuu Mimi Nina nyumba Nina kibanda,?Nilijitetea

Hapana, kwako kwako tu Mimi mbona Sina nyumba naishi apartment?

Madam we nasikia ulipewa nyumba kule karibu ukakataa, kwahiyo usiseme hivyo,

Akacheka sana, hivi Dani yaani ungekuwa wewe ungeishi nyumba ambayo ni ya dhuluma?
Ile nyumba watu wamehenya mahakamani. Mwenye Mali akashindwa, yule aliyeshinda akaona aiuze, ndiyo mume wangu akainunua eti niishi Mimi nilimkatalia, nataka nianze kujenga mwenyewe kuanzia msingi, tulitaniana tukacheka.

Ila Dani hujanionesha nyumba yako,

Hapana madam Mimi nyumba yangu ipo kilomita mbili toka hapa nikionesha kwa kidole Cha shahada Yale maeneo,

Ni kule alikonunua Mh waziri(akitaja jina)

Nikamjibu, ndiyo madam.

Kama kule sawa kule viwanja vimepimwa.

Sasa Dani tunakaa wapi mbona huku hamna hata sehemu ya kukaa mtu ukatulia? Alihoji kwa kudeka..

Nikampeleka kwenye mgahawa fulani japo umekaa kiswahili, akaridhika, japo kwa shingo upande.

Itaendelea...................
 
SEHEMU INAYOFUATA.....

Licha ya ESTA kunifumbua macho na masikio juu ya kile ambacho sikuwa nakifahamu kabla,
Nilipanga kutokubadili msimamo wangu.

Yule jamaa kaja mpaka hapa kwangu akiwa na kusudi moja la kufanya kazi na mimi.Na sidhani kama Nina hadhi ya kufuatwa Hadi nyumbani na yule jamaa anayeonekana pesa si tatizo kwake.Nilijisemea moyoni.

Mume wangu,
Naona Kuna mapya hapa Sasa sijui itakuwaje,maana tunaambiwa kumbe hizo ni kampuni za mtu mmoja,
Huoni kama pengine ni mtego mume wangu? alihoji mke wangu .

Hapana,ni lazima niende kwanza wale ni watu wakubwa na maarufu hapa mjini hawawezi kuhangaika na Mimi ambaye Sina hata kipato Cha kueleweka,hivyo ni lazima nifike tu hiyo kesho.nilijibu pasipo kusita.

Sawa mume wangu wote hapa tunakuombea.

Asubuhi ya saa tatu asubuhi tayari nilikuwa maeneo ya mjini huku nikisikia upepo wa fulani kuashiria nipo karibu na bahari nikiwa nimeshika njia kuelekea kwenye ofisi za kampuni mpya

Nilifika huku walinzi wakinihoji maswali mengi ambayo niligundua ni kwa sababu nipo kwa miguu.

Oyaaa we ngosha, hebu mkague kwanza huyo, chunga sana hawa wanaokuja kwa miguu wanakuwa wanetumwa kuja kupeleleza watu

Aliropoka mmoja wa wale walinzi huku mkoba wangu uliobeba CV Ukiwa wa kwanza kufunguliwa.

Kisha nikasachiwa kibabe kuasi Cha wale walinzi kuchafua kaunda suti yangu, sikumaindi sana, labda kwakuwa hawanijui lakini pia ni taratibu za kazi maeneo mengi.

Nikaingia mapokezi nikamkuta jamaa mmoja aliyenichangamkia vizuri sana huku akiniita kwa majina huku nikiwa simjui , lakini haikunipa shida, pengine kapewa maelekezo na wajihi wangu,

Niliruhusiwa kuonana na bosi huku nikipandisha ngazi, kuelekea kule juu ghorofani ilipo ofisi yake, nilikaribishwa kwa heshima zote huku akiwa mchangamfu sana.

Sikutaka kuonesha hofu yoyote nilijilazimisha kujenga tabasamu fake huku nikiwa makini kuliko umakini wenyewe huku nikijiandaa kama yatajitokeza maswali ya kimitego.

Karibu sana bwana, bwanaaaa nani vile,

Nikamtajia full name.

Eeh ok ok,

Bila kukuficha bwana Daniel nilizisikia taarifa zako juu ya upotevu wa chombo sijui, kitu gani vile.

Ni hydraulic separator na pini joint za excavator, nilimjibu huku nikiwa Sina uhakika kama zinaitwa hivyo.

Ahaaaa ulienda kuzichukua mkoani siyo?

Ndiyo bosi . Nilimjibu jamaa huku akiwa anatafuna tafuna vyakula fulani vya asili ya uarabuni huko.

Sawa,hata hivyo kipindi tupo Oman na mzee ,tulizipokea taarifa zile tukakufikiria vibaya kupita maelezo
Lakini licha ya yote mzee wangu alikuwa njia panda,

Yaani alikuwa akikusifia sana kuhusu uchapakazi wako.

Kwani wewe boss unamwitaje?

Swali ambalo lilitakiwa kuishia kufikirika kichwani nilijikuta nimeropoka

Akacheka sana,

Ndiyo Mimi ni mtoto wa kwanza wa mzee (jina kapuni).

Najua umeuliza hivyo kwakuwa nilikudanganya nilipokuja siku ya Kwanza

Nilimwangalia, huku nikimuona kafanana sana na na boss wangu. Tuliongea mengi sana muda ule.

Ujue Daniel yule boss wako ambaye Mimi ni mama yangu mdogo alituaminisha mambo mengi sana kiasi Cha sisi kutaka kukuchukua ili tukuhoji. Pengine ni umetumwa kuja kudhohofisha kampuni zetu.

Lakini baada ya kukuchunguza tuligundua huna unalolijua ndugu yangu pole sana,

Japo nikukumbushe kuwa makini sana ujue kitendo Cha wewe kuibiwa mzigo stendi umeonekana mzembe kuliko maelezo, hii inaleta tafsiri ya kwamba wewe ni mtu wa kuwaamini sana watu haraka haraka.

Sikupaswa kuyasema yote haya ila Mimi nasema kwa upendo tu kwa kuwa wewe ni kama ndugu yangu
Najua nilipokuja kwako siku ile ulishangaa nimefikaje, lakini ni kwamba baada ya wewe kuwekwa ndani Kuna watu walikupeleleza sana kujua unaishi wapi, una familia gani lakini pia nje ya kufanya kazi na sisi unajishughulisha na Nini.
Taarifa zote zililetwa huku tukiwa tunakuchukulia kwa uzito wa juu. Kabla hatujagundua kuwa wewe ni mwepesi tu.

Hata hivyo kazi ya hapa nayokupa ni kubwa zaidi tumeamua kufanya hivi kwakuwa unafiti kukaa hapa lakini pia mzee alikuhurumia wewe kuteseka kule mahabusu, Sasa tukaamua kukupa nafasi nzuri, ila nafasi yako ya Sasa nikwambie ukweli, inahitaki umakini wa hali ya juu,

Ni kwamba utashughulika kuidhinisha vyombo vyote vya site
Yaani Equipments kwahiyo, chombo gani kibovu, kinahitaji kufanyiwa service gani, kinataka kiwekwe spear gani we ndiyo utakaye shughulika ukishirikiana na fundi mkuu wa hii kampuni,

Najua huwa Kuna asili ya majungu sana Kati ya mafundi wadogo na wale ma operator hata hivyo wewe komaa kwenye eneo lako tu , mtu ambaye ataharibikiwa na chombo Chake atamuona fundi mkuu wa site ya kule ambako ulikuwa unatumwa zamani.

Halafu taarifa zitamfikia engineer mkuu ambaye wewe utashirikiana naye kuingiza taarifa kwenye computer na sehemu mbalimbali

Kwasababu huwa Kuna ufanyaji wa maghumashi kwa mafundi kuharibu vyombo kwa makusudi Kisha kutafuta mianya ya kupiga hela.
Hivyo nafasi yako itasaidie kampuni kujua vifaa vilivyoharibika kihalali.

Haya yote nimekwambia kwa upendo tu, sikuwa na haja ya kukuelekeza, kwahiyo nenda kule mapokezi kanisubiri Kuna watu watakuita mida ya mchana baada ya kutoka lunch.
Alimalizia bosi huku Mimi tumbo likiwa linanikoroga kwenye kazi ambayo niliona imekaa kifitini zaidi.

Nilikaa pale nje huku nikifikiria vitu vingi ambavyo hata kupoteza ule mzigo wa kwanza ndugu zangu walihesabu ni ushirikina,kutokana na bifu za mafundi na Mimi Leo hii hata huku wananiweka huku huku Tena mbona ule mtego aliokuwa anasema mke wangu ndiyo huu naouona

Wakati nikiwaza hayo, alikuja mwanamke umri Kati ya miaka 30_35 .

Mr Daniel nifuate ofisini kwangu,

Nikainuka nikamfuata Hadi kule ambapo niliwakuta wanawake wengine wawili , walinikaribisha kwa bashasha mno huku wakiwa na tabasamu na lugha rafiki,

Nikaanza kupigwa spana na wale mademu ambao nadhani nje ya taaluma zao nadhani wapo pale kwa kigezo Cha uzuri wa sura na maumbo yao, niliulizwa maswali kadhaa, nikawajibu vizuri kabisa.

Taratibu zingine zikaendelea huku nikishangaa baada ya kupewa kazi tofauti kabisa na ambayo boss aliniambia pindi tunapiga stori

Cha kuingizwa kwenye computer kiliingizwa Cha kuandikwa kiliandikwa pa kusaini nilisaini, nikimuona ni mkataba rafiki usiotisha .kisha nikaongozana na mwanamke mwingine ambaye ni kama waigizaji wa kimarekani ambao ni ndoto kuwapata,

Tukafika mpaka kwa boss,ambaye aliniangalia kwa kutabasamu baada ya kuona nimepewa kazi tofauti.

Alijaza baadhi ya documents huku kazi yangu ikiwa ni kuanguka signature tu,kisha akamwambia yule dada atoke tukabaki wawili tu.

Safari hii hakuwa na maneno ya kirafiki Bali Kila alichosema alimaanisha,nikajua tayari nishakuwa mfanyakazi wake rasmi,hapa Dani utatakiwa kuripoti kazini kuanzia keshokutwa ,lakini pia nimetoa maelekezo kutoka ile kampuni yako ya mwanzo kwamba wewe utakuwa huku kwangu na mzee anatambua upo huku.tuliagana nikaondoka kwa furaha huku nikipewa laki elfu hamsini ya nauli

Nilifurahi sana hasa baada ya kuambiwa mshahara bwanaaaa.

Asikwambie mtu maisha ni kazi,na utamu wa kazi ni pesa.
Kubwa zaidi kazi niliyokuwa naiota hatimaye ninayo rasmi.
Ni kazi ya ndoto zangu.yenye malipo sahihi na hatimaye Kila kitu kimetimia.

Maisha tunayoishi karne hii ni ya kisasa, na ukisasa umeitawala Dunia haichagua masikini Wala tajiri.

Kila kitu kinaongozwa kisasa,na Kila kitu Cha kisasa ili ukipate ni lazima uwe na PESA.
Maisha ya kumuoa mtoto wa mtu Kisha kumpa Mashamba ni vitu vimepitwa na wakati

Hata wale wanawake wazuri duniani kote Ukiwa na pesa ni rahisi kuwapata, tunaishi Karne ambayo miliki pesa kidogo ugundue tabia za wanadamu hata huyo unayemwita mama mkwe yaani mama wa mkeo Ukiwa na pesa anaweza kukwambia neno la kufuru. Ukaambiwa hicho ulichokiona kwa mwanae yeye anacho Mara mia yake.

Ndiyo, mbona ni mambo nayasikia sana,.

Pata hela halafu ingia klabu matata halafu ukaone wale vidume wanavyojigongesha kwako.

Kama ni mgeni wa mambo ya mjini huwezi kuelewa, lakini ni kwamba hao vijana ni wale ambao wameamua kutusaliti wanaume wenzao kwa sababu wanazozijua wao, ama kweli Dunia inaisha.

Niliwaza sana kabla ya kushtuliwa na konda wa daladala,

Oy jombii vipi unageuka nayo nini,

kuangalia nakuta wale abiria wote wameshuka, gari inajiandaa kugeuza nikagundua nimepitiliza zaidi ya vituo vitano, kuangalia saa no saa kumi na mbili pia simu missed calls ni nyingi sana, nikatulia kwenye siti tayari kwa kurudi, ili nikashuke karibu na kwangu

Yule kinda nilimpa nauli yake akauliza wapi tena kiongozi mbona ulipandia mjini, hujashuka naona unarudi vipi.

Hamna nilipitiliza kituo, nashukia kituo Cha (nikataja)

Kama ni hapo tu shika pesa yako.
Wakati nikiikagua simu nikagundua imepigwa na watu wanne, ila boss wangu wa kike pekee kapiga Mara kumi na tatu, zingatia ni zaidi ya Mara kumi.

Huyu naye anatafuta Nini, nimefanya miezi minne tu kwao Sina ninachowadai na wao hawanidai

Ina maana hawajawasiliana kwamba Mimi nimechukua mkataba mwingine kwenye kampuni kongwe?

Kama nistahiki zangu Mimi nilishasamehe, pale najua nitakanyaga kwa sababu hizi kampuni zina ushirikiano.

Lakini si kwaajili yake huyu, anataka nini kwangu?

Oy kiongozi unawaza Nini tayari ushafika,konda alinishtua pengine ningepitiliza tena

Sehemu ijayo Ina majibu,kisa kinaitwa MIMI NA BOSS WANGU unataka kujua ni boss gani, bado kisa kibichi.

Itaendelea.....
Duuuuh chuma ya moto aseeeee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom