SEHEMU INAYOFUATA...........
Nilizubaa zubaa pale stand ya ubungo,huku simu ikiwa inaita kwa fujo, lakini bado akili yangu ilitaka nionane ESTA kwanza,nikamalize haja zangu maana ,kutokana na ratiba zangu kubana.
Sioni muda mwingine nitakaopata,
Jamani Dani,umeniambia umeshafika,mbona muda unazidi kwenda ,fanya haraka bwana nataka niwahi kurudi,alisema ESTA upande wapili
Uwahi kurudi? kurudi wapi, Mimi nilitegemea nachukua logde tunalala,mpaka asubuhi,hayo mambo ya short time hayo bwana mi siwezi,sisi ni watu wazima mamaa,
Niliongea kwa sauti ya kukata tamaa,
Hapana Dani,natambua hilo lakini jua kuwa hata Mimi ni ratiba zangu ambazo sitakiwi kuzivunja,hata hivyo kumbuka nilikukatalia muda mrefu sana kuwa kwa Leo ratiba zimebana ukaniambia unahitaji masaa mawili tu ya kuwa na Mimi, iweje unanibadilikia unataka tulale,aliongeza ESTA
Nikaona dah,ni kweli nikiwa nambembeleza alikataa hata hivyo nikamuomba masaa mawili, yaani ni Kama maneno ya kutongozea , kumbe kashikilia hapo hapo, siyo mbaya hata Kama nusu saa lazima nikamvue nguo yule,
Simu ya mke wa boss iliingia,
Naam boss,nilisema hivyo baada ya kupokea
,niambie Dani umefikia wapi,hujaingia Dar es salaam bado?
Ah samahani boss gari nililopanda nilitegemea niingie saa kumi,hata hivyo liliharibika njiani lakini pia Kuna jamu tuliipata njiani foleni imechukua muda kifupi ndiyo naingia muda huu,
Jamani Dani my friend,tumetumia muda mwingi sana kusubiri hicho kifaa,na imani yetu wote,ipo kwako lakini mbona ni kama unatoka nje ya mstari,kiufupi fanya mpango hiyo spare ifike,kesho ipelekwe site
,alisema mke wa boss safari hii akiwa anaamrisha,
Nikaona dah mbona ishu ishakuwa ngumu nirudi kule store nifate spare Mara kuipelekaaaaaa,
Ah sinitafika nyumbani saa usiku wa manane Mimi,wakati nikiwaza hayo nikapokea simu yenye code number ya South Africa, nilitetemeka kidogo kwakuwa nilishajua,
Halooo,sauti ya bosi wa kiume ilisikika Mara tu baada ya kupokea simu,
Daniel, Daniel, Daniel nimekuita Mara tatu,sihitaji maelezo mengi,kifupi mbona unatupa wasi wasi? Alisema yule boss wa kiume.
Nilijitetea sana ,Tena sana kwamba spare ninayo na kesho asubuhi amtume dereva aifuate,hakujibu kitu lakini baada ya dakika tano nikapokea sms toka kwa boss boss mwanamke ikiwa inasomeka
"HATUKUELEWI"
Nikaona ni wasiwasi wao tu mbona Kila kitu kipo ok.
Nikampigia ESTA nimfahamishe kuwa tayari nakuja,
Naomba uwahi yaani sitalala maana nahitaji nirudi kikajiandae maana kesho Nina safari Tena ni ya lazima kwahiyo nakwambia kabisa ili usije kunibadilikia maana wanaume ndivyo mlivyo nyinyi.
Nikaishika barabara ya Sam nujoma kuelekea alipo yule ESTA.
Lakini wakati huo nikaona nimpigie wife maana tangu nipo kwenye gari ya mkoa niliongea naye saa nne asubuhi,nimeshuka kwenye gari naongea na watu wengine tu,
Ngoja niongee naye nimwambie gari imeharibika njiani kwahiyo sitafika Leo,
Mke wangu akapokea simu tuliongea mengi ya hapa na pale huku akinitaka niwe makini,
Lakini mume wangu,naomba ruhusa kesho nataka nimsindikize rafiki yangu mahali fulani,
Ni wapi unaenda,niliuliza
Akataja ni maeneo ya njia ya kilwa road kuelekea Mkuranga huko,
Nikauliza ni nani unampeleka,huko
Akajibu,
Ni yule rafiki yangu aliyekuja siku ile akajitambulisha kwa jina la ESTA,
Unajua Nini mume wangu yule ile siku anakuja pale nyumbani alikuwa na mambo mengi ya kuongea hata hivyo,we ulikuwa una haraka tu,ni kwamba yule ni muathirika anaishi na virusi vya ukimwi mwaka wa tatu Sasa hata hivyo yeye dozi yake huwa anachukulia hospitali ya..........(akaitaja hiyo hospital)
Kwahiyo Kuna ulazima gani wa wewe kwenda huko,niliuliza huku nilitetemeka baada ya kusikia habari inayomuhusu ESTA,kumbe nimwathirika huyu,nikaanza kumchukua ghafla kana kwamba yeye ndiye aliyenitongoza.
Mke wangu akaendelea,,
Hapana mume wangu,siyo kwamba lengo ni yeye tu hapana nahitaji kwenda kuangalia/kukagua Mashamba yetu ambayo Kila siku unanilaumu kuwa umenunua rasilimali za wote lakini nashindwa kuzifuatilia,nilimpongeza sana,huku nikishuka kituo Cha karibu kabisa nikighairi safari ya kwenda kwa ESTA baada tu ya kusikia habari hiyo mpya kwangu, kwahiyo alitaka kuniua huyu malaya nilitukana kimoyo moyo,
Nikampigia simu kuwa nimepata dharula kwahiyo hakuna uwezekano wa kuja Tena,akalaumu kiasi japo alinielewa.
Nikatafuta logde nyingine nikalala,
Asubuhi nilishitushwa na simu ya dereva wa kampuni akiwa anataka tukutane ubungo tuchukue kifaa chetu,
Muda wa saa mbili nikafika pale ubungo terminal nikimkuta dereva fulani mwenye lafudhi ya kimakonde akiwa kachangamka huku nikicheka chinichini alivyojipigilia suti yake iliyopauka na tai paana,haoooooo
Tupo store na wahudumu wa pale waliangalia vyumba vyote hatukuiona store pekua pekua na wewe hakuna kipindi hicho shati langu lote limeloa kwa jasho,ikabidi niwashirikishe maaskari waliokuwa kituo kidogo Cha mule ndani ,licha ya wale vijana kuhojiwa bado walidai ilikuwa ndani mulemule,
Nikaona mtihani huu, lakini yule dereva aliwaambia maaskari kuwa niwekwe chini ya ulinzi ikiwa ni maelekezo toka kwa boss wake,
Maaskari wakataka simu ipigwe kwa boss wajiridhishe,wakidai wananiwekaje chini ya ulinzi,wakati Mimi niliwakabidhi watu hiyo spare na waliokabidhiwa wanakiri waliipokea,lakini
Upande wa pili bosi alisema kuwa Hana uhakika kama kweli hao niliwakabidhi maana usumbufu niliuonesha tangu jana,huenda hao vijana wa matoroli wanajichanganya tu lakini spare hawakuipokea,
Watu wakapata pointi kuanzia maaskari Hadi wale vijana wasukuma matoroli wakanigeuka nikawa chini ya ulinzi rasmi.
Inaendeleaa usichoke..............
.,,,,