Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Kuna Billionaire mmoja mwanza.yaani huo utajiri wake ulitokana kuwa na mchepuko mwaminifu ujue jamani.
Yaani mwanamke Kama anakupenda utakula mema ya nchi ,mwanamke akipenda huwa haoni Ila Sasa ukikutana na Hawa sijui nitumie nauli nije.yaani Kuna mchepuko ukimsimulia wife anakuona mmewe Ni mjanja na wapo wake wanaposema chukua mchepuko anayenizidi hadhi sio unabeba beba tu baba akajaa vumbi.
Mie nazidi kuamini kweli. Hapa Rose inatakiwa aolewe mke wa Pili ama awe family friend inabidi wife ampende tu.
Kuna jamaa mmoja Ni chinga alitoka kwao akaoa Ana watt Sasa hapa alipo akapata mchepuko injinia. Sasa bana huo mchepuko ukawa unatunza kijana mpaka na familia yake ,yaani watt wanatumiwa Ada na mke anatumiwa hela ya matumizi na huyuhuyu mchepuko. Yaani hapa ndio akili yangu imetekwa na umuhimu wa kuwa na mchepuko. Ila rozi alikupenda tolu sema alipgopa kukuambia Mana asingependa kukuona unaumia mbele yake.
 
Kuna Billionaire mmoja mwanza.yaani huo utajiri wake ulitokana kuwa na mchepuko mwaminifu ujue jamani.
Yaani mwanamke Kama anakupenda utakula mema ya nchi ,mwanamke akipenda huwa haoni Ila Sasa ukikutana na Hawa sijui nitumie nauli nije.yaani Kuna mchepuko ukimsimulia wife anakuona mmewe Ni mjanja na wapo wake wanaposema chukua mchepuko anayenizidi hadhi sio unabeba beba tu baba akajaa vumbi.
Mie nazidi kuamini kweli. Hapa Rose inatakiwa aolewe mke wa Pili ama awe family friend inabidi wife ampende tu.
Kuna jamaa mmoja Ni chinga alitoka kwao akaoa Ana watt Sasa hapa alipo akapata mchepuko injinia. Sasa bana huo mchepuko ukawa unatunza kijana mpaka na familia yake ,yaani watt wanatumiwa Ada na mke anatumiwa hela ya matumizi na huyuhuyu mchepuko. Yaani hapa ndio akili yangu imetekwa na umuhimu wa kuwa na mchepuko. Ila rozi alikupenda tolu sema alipgopa kukuambia Mana asingependa kukuona unaumia mbele yake.
mkuu mwanaume hajaumbiwa hayo huko ni kukosea heshma umoja na amani hadhi ya kiume
 
SEHEMU INAYOFUATA.. .. ... ..

Baada ya kuongea na yule mzee, ambaye alionesha upendo wa dhati kabisa kwangu, walianza kukonyeza Kati ya yeye na mkewe, nikagundua ni masuala ya Chakula, ikabidi niwazuie. Kisha nikaaga ili niondoke.

Kwanza kijana wangu nakupongeza kwa kuwa imara na msimamo wa kweli hivyo nakukaribisha sana, karibu tena kwa Mara nyingine alisisitiza yule mzee huku na yule mama wakionesha furaha zao.

Nilishika njia ya nyumbani huku nikisikia njaa, yaani ile njaa ambayo ilikuwa hainisumbui sababu ya mawazo Sasa ikawa , inauma barabara. Tena haswaa,
Baada ya kufika nyumbani niliamrisha Chakula kiwahi kidogo maana nilikuwa na njaa sana.

Nilitulia sebuleni huku nikiwa napoteza muda kwenye TV hususani matangazo ya mwisho wa mwaka yaani punguzo la bei za bidhaa mbalimbali, Kila channel ukiweka matangazo ya bidhaa kwa msimu wa Christmas na mwaka mpya yalikithiri. Huku nikiwa nayachukia Yale matangazo,. Labda kwakuwa sikuwa na hela. Maana bidhaa zipo chini lakini bado huwezi kuharibu bajeti zako, nilichukia sana.

Mume wangu, Kuna tamthilia yangu imeshaanza hivyo naomba hiyo remote, Mke wangu alisema huku nikiwa Sina namna maana Hawa ndiyo wenye TV. nikainuka na kwenda chumbani huku, hali ya kusimamishwa kazi Kila wakati nikigundua sipo kwenye hali nzuri, huu ni mkosi, nikijikumbusha washkaji zangu kibao ambao, huwa wanazingua sana kwenye mishe zao lakini bado huwezi Kuta wakiwa na stori mbaya kama hii yangu, hii kwangu ni nuksi. nilijisemea

Unajua kuremba nako si kuzuri, yaani Kuna muda nilikuwa karibu na yule Boss wangu, Bora hata ningetembea naye ili haya yanayoongelewa nione labda nimekosea.
Tena alivyomaarufu ingekuwa poa maana huenda angenisaidia kwenye hii kadhia maana si ingekuwa kweli?
lakini ni ujinga tu, mbona Kuna watoto wabichi sana mtaani kumshinda yeye.

Niliendelea kuwaza yale mambo
ya kijinga huku nikiwa nachati na Rose kule chumbani.

Mume wangu Kuna wageni tunakuomba uje. ilikuwa sauti ya mke wangu ikiita.

Nilitoka huku nikikutana na wanawake wawili na mwanaume mmoja, huku mwanamke mmoja akiwa ni mke wa rafiki yangu Shedy, na wengine ni wageni huku mwanamke mwingine alijitambulisha kama rafiki yake na yule mke wa Shedy. na yule mwanaume alijitambulisha kivyake huku akisema yeye ni dereva wa Bajaj.

Karibuni sana jamani, lakini mbona muda huu vipi Kuna nini, halafu mbona shemeji yangu
Kama una majonzi vipi, niliuliza Huku nijiset vizuri kwenye kiti.

Shemu kwanza samahani sana kwa usumbufu, Hawa unaowana wamenisindikiza Mimi kuja hapa, suala ni kwamba mume wangu leo ni siku ya nne haonekani nyumbani, mwanzo niliingiwa na wivu kuwa huenda kafungiwa na mwanamke. Lakini baada ya kutimia siku ya nne
Ndipo, niliposhtuka kuwa huenda kapatwa na matatizo, hivyo nisharipoti kituo Cha polisi, na nimezunguka kwenye vituo vingi tu, bado maaskari wananieleza kuwa wapo kwenye mchakato kuhakikisha anapatikana.

Hivyo kwa Imani yangu, japokuwa mimi na nyie hatuna uhusiano mzuri ninakuomba au niwaombe wote wewe na mdogo wangu (akimaanisha mke wangu) naomba mnisaidie ndugu zangu, shemu wewe ni wa nyumbani kabisa, naomba waache hao naomba nisaidie mwenzio(huku akiongea kwa kilugha)hali iliyopelekea mke wangu atake kumaindi

Sawa nimekuelewa, na wote tunashukuru kwa taarifa hiyo maana jambo hilo ni zito sana,. Kwani gari lake liko wapi. niliuliza.

Gari lipo tu nyumbani maana lilishaharibika kitambo, hivyo shughuli zake za udalali alikuwa akitumia gari la rafiki yake. alijibu

Sawa, wewe Dada Mimi sikuchukii, kupotea, au kutoonekana kwa mumeo najua ni jambo linaumiza, ila naomba uwe unaongea kiswahili ili wote tujue, kuongea kilugha na mume wangu , jua kuwa huyu hawezi toa msaada wowote kama sijamruhusu.
aliongea kwa hasira mke wangu,.

Jamani eeh, Mimi shemu nimekuelewa sana, ila simu si tunazo? Kila kitakachojiri tutafahishana. Nilijibu kifupi kwani mke wangu na familia ya Shedy ni kama mbwa na paka. lengo nilitaka waondoke.

Kaka, kakaeee naomba tuongee kidogo hapa nje, samahani lakini mzee mwenzangu. aliongea yule jamaa aliyejitambulisha kama dereva Bajaj.

Kwanza nimekuita chemba lengo nikwambie ukweli,

Huyo rafiki yako sijui ndugu yakoooo,
Nisikufiche alijiingiza kwenye ujambazi baada ya shughuli za udalali kuwa haziendi kihivyo, lakini pia baa yake Alishafunga, baada ya wa kuwa hakuna wateja, na alikuwa malimbikizo ya madeni kwa wafanyakazi wake, wapo waliosamehe na wapo walioufungua kesi ya madai mahakamani. Upo kaka,
aliongea yule jamaa huku nikimsikiliza kwa umakini.

Akaendelea..........

Mtaani kwake pale Hana dhamana, kwanza ni tabia yake ya kutembea na wake za watu, tabia ambayo imewafanya watu wakose Imani naye.

Pili, Kuna tetesi jamaa, kajiingiza kwenye unyang'anyi wa kutumia silaha hivyo tayari baadhi ya watu hawataki kushirikana naye.

Lakiniiii, mke mtu yeye hajui hata kidogo yeye kwanza aliingiza wivu akijua mumewe labda yupo kwa mchepuko, Sasa basi za ndani kabisa inasemekana Shedy, washirika wake walimgeuka lengo na kumpiga risasi, ila mkewe hajui, hivyo basi wewe kama wewe leo tunaomba kushirikiana na wewe tujifanye kama tunamtafuta. aliweka kituo.

Wakati tunamtafuta tunashirikiana na nani na wewe umesema kwamba, baadhi ya majirani.,hawataki na pia tunamtafutia wapi, niliuliza.

Mbona inajulikana watu wa Bajaj na boda boda wote tayari wameshajipanga huku tukiongozwa na polisi, Kila kitu kinajulikana mbona. aliongea yule jamaa.

Kwanza wewe ni nani na kwanini uwe karibu na huyu shemej yangu?

Hii Bajaj unayoiona ni ya huyu mwanamke alinipa Mimi, na hata huyu marehemu mume wake alikuwa hajui kuwa mke wake ana miliki hii Bajaj. alijibu yule jamaa mwenye asili ya pwani ni muongeaji mzuri utasema tunafahamiana kitambo.

Tulirudi ndani huku nikijiona Sina matatizo kumbe Kuna watu Wana matatizo, niliwaruhusu watangulie wale wageni Kisha nikawaahidi kuwa nawafuata punde.

Mke wangu, naomba niruhusu niende kwa Hawa jamaa nahisi Kuna matatizo. nilishauriana na mke wangu.

Mmmh Hawa nao wamekosa watu woooote wameona waje huku, mtaa wa ishirini,mume wangu nenda ila kuwa makini maana wewe mwenyewe una yako tena yanakushinda.

Nilitoka huku nikijikoki vyema, huku tayari huruma na moyo wa kibinadamu vikinitesa , nikimuwaza Shedy huku nikilaumu shetani, kwanini alijiingiza kwenye ujambazi na kazi za hatari?

Nikikumbuka kuanzia utoto wetu, ujana, na mengine mengi nilijikuta naumia sana, wakati nikiikaribia nyumba ya Shedy niliwakuta maaskari wakimtukana mke wa Shedy.

Sikiliza wewe mwanamke, umekuja kuripoti kupotea kwa jambazi lako kumbe unatuchoresha tu, Sasa mumeo aliua, na yupo kituoni na wewe ingia kwenye gari.

Jeshi lipo imara, tutahakikisha watu kama mumeo na washirika wake wote wanaingia kwenye mkono wa Sheria, walimchukua yule mwanamke huku huruma ikiniingia sana , japo kusogea niliogopa, maana usijekuta unasombwa na maaskari wenye jazba.

Jamani mwacheni MUNGU aitwe MUNGU huyu , inasemekana kaua mwenzake Kisha akawa anatoroka hata hivyo kakatiwa mbali kabisa na maskini mke wake Wala hakuwa anajua, alisikika jirani mmoja.

Taarifa zilikuwa nyingi huku nikishindwa niiamini ipi, nikaona hapa hakuna Nini wala Nini maana niliambiwa amekufa, saizi nasikia kaua, ikabidi nichukue Bajaj hadi central moja kubwa.

Nilifika pale huku mke wa jamaa akiwa analia kama mtoto pale nje ni kweli niliambiwa na maaskari kuwa jamaa aliua, huku nikiambiwa uchunguzi unaendelea ili wajue sababu ya kuua ni Nini. Huku tulionywa kutokusambaza taarifa zisizo za kweli badala yake tuliachie jeshi lifanye kazi yake.

Nilimchukua yule shemeji yangu kwa nguvu maana alikuwa yupo nje analia tu huku maaskari walimkejeli na kumzidishia maumivu.

Nilifika nyumbani kwa Shedy,nikawakuta watoto nao wanalia sana , jamani Yale ndiyo yanaitwa matatizo sisi wengine tunapitia changamoto tu.

Niliwaita majirani na tukaungana huku nikiwashauri majirani kuwa ule si wakati wa vinyongo na visasi tusahau na tumsaidie mwenzetu, wengi walinielewa huku wanawake wawili wakikubali kulala pale pale, nilifurahi huku tukiagana ule muda wa saa Saba za usiku, nikiwaambia ngoja nikapunguze usingizi, na tutajua Cha kufanya kukipambazuka.

Inaendeleaa...........
 
Huwa naamini yaani Nina beliefs zangj kuwa kila Jambo Lina mana yake sema huwezi jua at that instant jamani. Yaani unaweza ukanifukuza kazi kumbe ndio naenda pazuri zaidi mno yaani mno Kama Ni chuki zako zinazidi kukuumiza na utakonda bure.
Yaani Ulimwengu ama universe Kuna namna inavyo operate.
Kuna jamaa alipata ajali katika boti akaogelea mpaka kisiwa hakina watu. Akajenga kibanda akajihifadhi hajui lini atapata Msaada. Usiku kibanda kikaungua akashtuka ,akaanza kutukana Mungu. Kumbe ule Moto ulifanya kapteni wa meli moja ilikuwa inapita mbali akauona so akasogea mpaka pale akampa Msaada akamuokoa. Yaani hata wabaya kwenye maisha huwa ndio walimu wetu ama kutufanya twende mbali zaidi kimaisha. Enemies,haters, mistakes, errors/losses are to be loved like friends. Ukifanya mistakes unajua kuwa hiyo beliefs ama wazo halifanyi kazi so utaanza Tena na wazo jingine unafanya experiments mpaka unapata products unayoitaka
 
Huwa naamini yaani Nina beliefs zangj kuwa kila Jambo Lina mana yake sema huwezi jua at that instant jamani. Yaani unaweza ukanifukuza kazi kumbe ndio naenda pazuri zaidi mno yaani mno Kama Ni chuki zako zinazidi kukuumiza na utakonda bure.
Yaani Ulimwengu ama universe Kuna namna inavyo operate.
Kuna jamaa alipata ajali katika boti akaogelea mpaka kisiwa hakina watu. Akajenga kibanda akajihifadhi hajui lini atapata Msaada. Usiku kibanda kikaungua akashtuka ,akaanza kutukana Mungu. Kumbe ule Moto ulifanya kapteni wa meli moja ilikuwa inapita mbali akauona so akasogea mpaka pale akampa Msaada akamuokoa. Yaani hata wabaya kwenye maisha huwa ndio walimu wetu ama kutufanya twende mbali zaidi kimaisha. Enemies,haters, mistakes, errors/losses are to be loved like friends. Ukifanya mistakes unajua kuwa hiyo beliefs ama wazo halifanyi kazi so utaanza Tena na wazo jingine unafanya experiments mpaka unapata products unayoitaka
Hahahah..mkuu ni kwel...baada ya kufukuzwa kazi mimi (kama nilivyoeleza huko juu) nikapitia msoto kama miez 6 hiv sijui nalipaje ada za watoto na mambo mengine.yan hata mshahara wa laki 3 nikawa nautamani 😂😂 kumbuka hapo niliondolewa kazin nilikua nalipwa laki 8 tuu.... Aisee ghafla akatokea mshkaji wangu tulisoma olevel katika maongez nikamwambia mwanangu kwasasa niko bench sina issue..akashangaa sana na kunambia mbona umekaa kimya muda wote huu jamaa angu...? Nitumie CV yako...ikapita mwez mmoja tu nikaitwa interview ya kizushi tu then huyoo nikaanza kazi......aisee nikawa nalamba mshahara wa 2,500,000 /= kwa mwezi kama take home... nilifanya kazi miezi 9... kwakua nyumba tayar nilikua nayo basi nikalipa madeni ikiwemo ada za watoto kisha nikanunua gari yangu second hand ....pesa ilibaki nikawekeza kwenye project yangu ya software development....kwakifupi nikaanza rasmi maisha ya kujiajir kwenye IT kwakwel mpaka leo japo Sijafika napokwenda ila safar yangu imejaa matumain tele...


Hivyo nakubaliana na wewe mkuu na hakika stori hii inatugusa wengi sanaa
 
Jamani Kuna michepuko una faida mno mjue yaani mno. Ila sio Hawa hàwaeleweki hawajasoma,mpaka vocha ya buku wanaomba. Kutana na mtu ambaye anakuomba milioni kwenda juu jamani.
Mapovu ruksa
Ahahahahah Dah haya mambo yananirudisha mbali sana...

Ila nakubaliana na wewe chief...kuna kipindi nilipitia msoto mkali kishenzi...nilikua na mtoto mmoja yuko grade 3. Sasa kwakua hali iliniyumbia nikashauriana na wife acha nimtoe mtoto shule nimhamishie ya gharama ya chini kidogo ..kimbembe kule nakotaka kumtoa nadaiwa hivyo uhamisho wakanigomea mpaka nimalize deni..

Basi siku nikiwa sina hil wala lile nikapigiwa simu na girlfriend angu mmoja tulikua wapenz nikiwa chuo.Huyu dada alinipendaga sana sana ila ndio hivyo hatukua na future na kila mtu alikubaliana na hilo..mimi nikaoa na yy akaolewa na nikajiweka nae kando kuepusha kuharib ndoa za watu ila tulibaki washkaji tu..


Bas siku nikiwa kwenye lindi la mawazo kuhusu dogo kuhama shule ndio simu yake inaingia..sikua na mood nzur sana a akaligundua hilo kwenye maongez ...akaniuliza shida nini nikamwambia hakuna tabu ..ni mambo ya kawaida .. akanidadis mpaka nikamwambia kinachonichanganya...

Kipindi hicho (mpaka sasa) yeye ni mfanyakazi kwenye moja ya benk kubwa tu hapa town...
Akanambia usimtoe mtoto shule mwache asome tu mpaka utakapokaa sawa..Nitalipa hizo gharama...naamin haitapita mwaka utapata kazi....

BWana bwana weeee...fasta akanitumia laki 5 nikapunguze deni shule mtoto aendelee na masomo...

Aisee na haikupita miez 3 kweli nikarud kazin (ambapo nilikua nimefukuzwa kwa mara ya kwanza kama nilivyokwisha eleza kwenye coment huko juu) wakanirudisha 😂.

Ila nilimrudishia pesa zake japo hakutaka but nili force nikamrudishia pesa yake yoote aliyonifadhil kipindi chote cha mpito wa mtikisiko wa uchumi 😎
 
Narudia kusema kuwa Kuna Billionaire mmoja mza Ni kutokana na michepuko,mwenzake waliyekuwa naye iyo hatua ya kuokolewa na mchepuko ilimpita kushoto akawa ameangukia pabaya akapotea. Na alikuwa anasukuma toroli huyo billionaire mpaka saivi Ana viwanda amepumzika zake watu wanampigia kazi anatumia leverage ya watu ama Ana trade money with time.
Ahahahahah Dah haya mambo yananirudisha mbali sana...

Ila nakubaliana na wewe chief...kuna kipindi nilipitia msoto mkali kishenzi...nilikua na mtoto mmoja yuko grade 3. Sasa kwakua hali iliniyumbia nikashauriana na wife acha nimtoe mtoto shule nimhamishie ya gharama ya chini kidogo ..kimbembe kule nakotaka kumtoa nadaiwa hivyo uhamisho wakanigomea mpaka nimalize deni..

Basi siku nikiwa sina hil wala lile nikapigiwa simu na girlfriend angu mmoja tulikua wapenz nikiwa chuo.Huyu dada alinipendaga sana sana ila ndio hivyo hatukua na future na kila mtu alikubaliana na hilo..mimi nikaoa na yy akaolewa na nikajiweka nae kando kuepusha kuharib ndoa za watu ila tulibaki washkaji tu..


Bas siku nikiwa kwenye lindi la mawazo kuhusu dogo kuhama shule ndio simu yake inaingia..sikua na mood nzur sana a akaligundua hilo kwenye maongez ...akaniuliza shida nini nikamwambia hakuna tabu ..ni mambo ya kawaida .. akanidadis mpaka nikamwambia kinachonichanganya...

Kipindi hicho (mpaka sasa) yeye ni mfanyakazi kwenye moja ya benk kubwa tu hapa town...
Akanambia usimtoe mtoto shule mwache asome tu mpaka utakapokaa sawa..Nitalipa hizo gharama...naamin haitapita mwaka utapata kazi....

BWana bwana weeee...fasta akanitumia laki 5 nikapunguze deni shule mtoto aendelee na masomo...

Aisee na haikupita miez 3 kweli nikarud kazin (ambapo nilikua nimefukuzwa kwa mara ya kwanza kama nilivyokwisha eleza kwenye coment huko juu) wakanirudisha 😂.

Ila nilimrudishia pesa zake japo hakutaka but nili force nikamrudishia pesa yake yoote aliyonifadhil kipindi chote cha mpito wa mtikisiko wa uchumi 😎A
 
Ila kwenye hii simulizi,nimepata kitu Tena,unapopata deal au kitu ambacho bado hujakushikilia mkononi usimwambie mtu yeyote.
Watu wengine wako kuhakikisha kuwa unakwamba .
Nakumbuka 2008 nikiwa Kampuni moja kubwa Sana ya Kigeni nilichaguliwa kwenda soma Nchi moja kusini mwa jangwa la Sahara, Nikajiandaa hadi passport na makorokoro mengine kwani ilikuwa ni Kozi ya Miaka 3.

Mambo yakatangazika Kampuni nzima na akatokea Mkuda mmoja kule Utawala eti akashauri Idara nifanyiayo Kazi itapata upungufu wa ufanisi pale niondokapo hivyo akashauri nisome online.

Hakika yule Mzee siwezi msahau kamwe japo nilishamsamehe.
 
Nakumbuka 2008 nikiwa Kampuni moja kubwa Sana ya Kigeni nilichaguliwa kwenda soma Nchi moja kusini mwa jangwa la Sahara, Nikajiandaa hadi passport na makorokoro mengine kwani ilikuwa ni Kozi ya Miaka 3.

Mambo yakatangazika Kampuni nzima na akatokea Mkuda mmoja kule Utawala eti akashauri Idara nifanyiayo Kazi itapata upungufu wa ufanisi pale niondokapo hivyo akashauri nisome online.

Hakika yule Mzee siwezi msahau kamwe japo nilishamsamehe.
Daaaaa,huko ni kuzibiana
 
Ila kwenye hii simulizi,nimepata kitu Tena,unapopata deal au kitu ambacho bado hujakushikilia mkononi usimwambie mtu yeyote.
Watu wengine wako kuhakikisha kuwa unakwamba .
Hii wazungu wanasema kuwa don't count chickens before hatching finished. Hata kihomehome na sie huwa haitakiwi uongee kitu ambacho hujakiweka mikononi nikiwa mdogo utasikia unakoromewa.
Hata iyo ya kuhesabu mayai unajua kuwa una vifaranga vingapi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom