Simulizi: Mchawi

Sehemu ya 50

Nilipanga baada msiba kwisha nisafiri kuchunguza kifo cha baba ambacho kwa upande wangu sikukubaliana nacho.

****
Siku ya pili tulimzika baba, msiba ulioudhuliwa na watu wengi sana, wafanyakazi wenzangu walikuwa miongoni mwa watu waliokuja kumzika baba yangu na kunipa faraja kubwa.

Msibani kulikuwa na minong’ono ya chinichini ikisema, msiba ule si bure lazima kutakuwa na mkono wa mtu. Mama hakukubaliana na minong’ono ile kwa kuamini kifo cha baba pamoja na vitu vya kushangaza kutokea bado aliamini ni amri ya Mungu.

Baada ya mazishi na kukaa siku mbili nilimuomba mama niondoke naye ili tukamalizie msiba nyumbani kwangu. Lakini mama alikataa na kusema msiba ataumalizia palepale nyumbani kwake. Sikuwa na jinsi kwa vile alikuwa ameamua ilibidi niiache familia yangu ikae na mama kipindi chote cha mama kumaliza msiba wa baba.

Wiki moja ilikatika na muda wa kurudi kazini ulifika. Nilirudi zangu kwangu na kumwacha mke wangu amtunze mama kwa kipindi chote cha kumalizia msiba wa baba. Nilirudi zangu nyumbani siku ya jumapili na jumatatu asubuhi nilikwenda kazini. Nilianza kazi nikiwa bado na kitendawili kizito kichwani mwangu kutokana na kifo cha baba. Pamoja na mama kusema kifo cha baba ni amri ya Mungu sikutaka kukubaliana naye japokuwa nilimkubalia ili kumlizisha.

Nilipanga siku ya Ijumaa niondoke na gari la kampuni kwenda Malalo. Niliamini hata kama nitalala Tewe siku ile na kesho yake lakini siku ya jumapili. Lazima niwe nimerudi kwa muda wowote ili mradi jumatatu inikute kazini.

Wiki nzima niliyokuwa kazini nilikuwa katika dimbwi la mawazo kuhusiana na mazingira ya kifo cha baba yangu. Wengi walijua kukosa kwangu raha kazini kulitokana na maumivu ya kifo cha baba yangu, ambaye siku zote alikuwa mtu wangu wa karibu. Japokuwa kifo cha baba kiliniuma sana kutokana na kipindi kile ndicho nilikuwa nikiwahitaji sana wazazi wangu kula jasho langu.

Kilichonichanganya zaidi na kuupa moyo wangu wasiwasi kilikuwa mazingira ya kifo cha baba. Niliamini utatuzi wake ningeupata kwa mtoto wa mzee Kidereko. Bado safari yangu ilibakia siri yangu sikutaka kumshirikisha mtu yeyote.

Mwisho wa wiki niliomba gari kama nakwenda kumuona mama. Kwa vile nilikuwa naivana na bosi, alinikubalia niondoke na gari. Siku ya ijumaa niliondoka kazini saa tano asubuhi, watu wote walijua nimekwenda kumuona mama.

Niliondoka kazini saa tano na nusu, nilitumia saa mbili na nusu kufika Chalinze kutoka na mwendo kasi niliokuwa nikitembea nao. Niliunganisha moja kwa moja kuelekea Lushoto. Kwa mwendo niliokuwa nakwenda nilifika Tewe saa kumi na mbili jioni. Nilikuta bado mwanga wa jua bado haujazama vizuri na kuamini mambo yangu kama yatafanikiwa yatakwenda vizuri ningeweza kurudi siku ileile na kuelekea kwa mama kisha ningerudi kazini.

Ugeni wangu wa ghafla uliwashtua, baada ya kunipokea walitaka kujua ujaji wangu wa siku ile.

Kwa vile muda ulikuwa bado nilipata muda wa kuzungumza na mtoto wa mzee Kidereko. Palepale nje chini ya mti, wote walitupisha kutuacha tuzungumze wawili.

“Ndiyo ndugu zangu za siku?” mtoto wa mzee Kidereko aliniuliza.
“Nzuri kiasi,” nilimjibu huku nikimtaza na kukutanisha macho yalionesha anashauku ya kujua kilichonipeleka pale.

“Hata mimi ujaji wako umenionesha kuna kitu, ehe, ndugu yangu tatizo nini?”
Nilimuelezea utata wa mazingira ya kifo cha baba yangu. Baada ya kunisikiliza alimwita msaidizi wake, alimwita kijana mmoja kati ya wasaidizi wa baba yake mzee Kidereko.

“Hamis njoo.”
“Naam.”
“Niletee unga wa kutazamia mbali.”
Juma alikwenda ndani na kurudi na chupa ndogo aliyomkabidhi. Baada ya kumkabidhi alifungua chupa na kujimiminia unga mweupe mkononi. Kisha aliumwaga kwa kuusambaza na kutulia kuutazama ule unga aliopeperuka kwa upepo.

Aliutazama ule unga uliokuwa ukipepea kwa upepo kama anaangalia kitu ambacho mimi sikukiona. Baada ya kutulia kwa muda alishusha pumzi ndefu na kusema:
“Kuna vita nzito sana.”
“Vita?” nilishtuka kusikia vile.
“Tena nzito, mmh! Kuna kazi!”
“Kazi?” nilizidi kushtuka na maneno ya mganga.

“Tena nzito, hii kwangu.mmh, sijui!” mganga alinikatisha tamaa bila kujua hiyo ni vita gani na uzito wake ni upi.
“Mbona unanitisha?”
“Sikutishi, ndiyo ukweli wenyewe, vita hii ingenoga mzee angekuwepo.”

“Una maana gani?”
“Kifo cha baba yako kina siri nzito.”
“Mganga hebu nieleze tatizo kuliko kunizungusha na kunitisha.”
“Inaonesha hapa kifo cha baba yako kimetokana kisasi.”

“Kisasi?” nilishtuka.
“Ndiyo.”
“Kisasi kipi tena?”
“Baada ya kifo cha mgoni wako wa pili, ndugu zake hawakukubali kama kile kifo cha amri ya Mungu. Kutokana na mazingira ya kifo chake, aliamua kukifanyia uchuguzi ndipo walipo kukuta. Hawakukubali kumpoteza ndugu yao, waliamua kulipa kisasi.

“Inavyoonekana waganga wengi wa nchini wamechemsha hivyo wakaamua kutoka nje ya nchi kuhakikisha wanakulambisha mchanga. Inaonesha uchawi waliotumia kukuroga umetoka mbali sana.

“Naweza kusema mshukuru sana mzee Kidereko kwa kinga aliyokupa. Uchawi waliotumia tungekuwa tumekwisha kukuzika muda mrefu. Unakumbuka siku moja ukiwa kazini uliumwa sana kichwa kisha ulitoka damu puani?”

“Ndiyo nakumbuka.”
Nilikumbuka siku moja ambayo nina imani katika kusimulia sikulisema hili. Ni kweli siku moja nikiwa kazini baada ya kazi ya kutoa vifaa ambayo vilikuwa vingi na kunifanya nisimame kwa muda mrefu.
“Nilipokaa kichwa kilianza kuniuma kama kinapasuka kikifuatiwa na kutokwa damu nyingi puani.

Nilikimbizwa hospitali ambako nilikutwa na maralia. Baada ya matibabu nilijisikia vizuri na kuruhusiwa kutoka hospitali. Hali ile haikujirudia tena na kuamini yale yalikuwa maralia tu.

“Basi yale hayakuwa maralia ilikuwa ndiyo safari, shukuru kupelekwa kwenye mizimu, uchawi uliofanyiwa mbaya sana. Kutoka damu puani ilikuwa safari isiyo na kwaheri. Lile lilikuwa jini la kutumwa, jini Makata lilikuwa likukate palepale.
“Baada ya kuona kwako ngoma nzito walibadilisha mashambulizi na kuyaelekeza kwenye familia yako.

Wameanza na baba yako baada ya hapo atatafutwa mtu mwingine.”
“He! Ina maana wamepanga kuiteketeza familia yangu yote?” nilishtuka kusikia vile.

“Ndiyo.”
“Wanatumia uchawi wa ndizi, wanaroga kwenye mkungu wa ndizi wenye ndizi mbichi, ikiiva ndizi moja na kundoka, basi katika familia yako anaondoka mtu mmoja.”
“Mungu wangu!” nilishika kichwa kwa mshtuko.

“Mtego wao haukuwasumbua kukunasa kwa vile kilikuwa kisasi cha kuuawa ndugu yao, hivyo ilikuwa rahisi kukupata.”
“Sasa utanisaidiaje?”
“Kazi hii kwa uwezo wangu nzito sana, ila nitakuelekeza kwa mzee mmoja ambaye alikuwa swahiba wa baba ambaye naye yupo vizuri kama mzee Kidereko.”

“Anakaa wapi?”
“Maeneo ya mbele kidogo japo kuna kamwendo kadogo.”
“Tunaweza kwenda leo?”
“Tunaweza kwa vile muda bado.”
 
Shunie mama unavyoweka part 1 unatuonea kabisa at least part 3 au 4 jitahid basi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sehemu ya 51

“Tunaweza kwenda leo?”
“Tunaweza kwa vile muda bado.”
“Tunaweza kutumia gari?”
“Hatuwezi kwenda na gari kutokana na eneo lenyewe, lazima tupande kilima na kushuka.”
“Usiku hakuna wanyama wakali?”
“Hakuna.”

Tulikubalia kwenda kwa mganga mwingine baada ya ngoma yangu kuwa nzito kwake. Tuliongozana wawili kuelekea kwa mganga, ilikuwa safari ya kupanda na kushuka milima mpaka kufika kwa mganga nikiwa nimechoka na kutokwa na jasho chapachapa.

Toka nilipouachia mwili nilikuwa mzembe, safari na nusu saa ilikuwa kama nimetembea zaidi ya saa sita. Tulipofika kwanza nilikaa chini kupumua, kwani hata kuongea nilishindwa kutokana na kifua kujaa pumzi.

Mtoto wa mzee Kidereko aliniacha nimepumzika kwenye gogo la mnazi na yeye kuingia ndani kwa mganga. Ilionesha pale ni mwenyeji kwa jinsi walivyo mpokea.

Nilitulia kwenye gogo huku giza likianza kuimeza nuru ya mchana. Baada ya muda alirudi na kunieleza jambo ambalo lilinishtua kidogo.

“Ndugu yangu tumefeli.”
“Una maana gani?”
“Mzee amekwenda mkoani, kuna watu wamemchukua jana.”

“Atarudi lini?”
“Mmh! Haijulikani.”
“Kwani ndiyo mara yake ya kwanza kusafiri kikazi?”
“Mara nyingi, huwa akiondoka kwenda kufanya kazi za watu mikoani, anaweza kumaliza hata mwezi mzima.”

“Mmh! Sasa itakuwaje, hana msaidizi?”
“Yupo, lakini kazi yako si ya kutumwa mtu mwepesi, unaweza kumpoteza kama mchezo.”

“Kwani ni nzito sana?”
“Hauna tofauti na uliyosababisha ugonjwa kwa baba uliopelekea sababu ya mauti yake.”

“Mmh! Sasa nitafanyaje, hakuna waganga wengine?”
“Kwa kweli mimi niliyekuleta kwake ndiye niliyekuwa naye karibu pia nina mahusiano mazuri. Hata kazi zao walikuwa wakisaidiana na marehemu baba.”

“Uliniambia uchawi wao ni wa ndizi, kwa hiyo kuna mkungu unaendelea kuiva?”
“Ndiyo, tena uchawi huu ni mbaya sana unaweza kumaliza ukoo wako kwa muda mfupi.”

“Mungu wangu sasa nitafanya nini ikiwa hakuna mtu wa kunisaidia?” nilijikuta nazidi kuchanganyikiwa.
“Mmh! Hebu turudi nyumbani nataka nikajaribu kutafuta ufumbuzi,” mtoto wa mzee Kidereko aliniambia.

“Ukishindwa?”
“Tumuombe Mungu nisishindwe, shida yangu ni kuzuia, kwani ukifanya mzaha wiki nzima unaweza kuzika familia nzima.”
“Eti?” kauli ile ilizidi kunitisha.
“Uchawi waliotumia ni mbaya sana, ule haubakizi ukoo.”

Tukiwa katika ya mazungumzo alitoka kijana mmoja aliyeonekana amevalia nguo za kiganga na kunisalimia.

“Za saizi kaka?”
“Nzuri.”
“Pole sana, nimefuatilia mazungumzo yako na maneno aliyoniambia Maghinde kwa kweli yamenishtua. Wakati nyinyi mkizungumza, niliangalia tatizo lako. Kwa kweli ni vita nzito sana.”

“Jamani badala ya kunisaidia mnazidi kunikata maini,” nilitamani kulia na kuiona kama dunia imeniinamia na hakuna wa kunipa msaada.

“Nia kubwa ni kukusaidia, kuna kitu nimekiona kimenitisha sana.”
“Mungu wangu kitu gani tena hicho?” kauli ya Bwaza ilizidi kunitia hofu.
“Hebu twendeni kwanza ndani, hili si jambo la kulizungumza hapa.”

Tuliongozana ndani huku nikihisi mwili kupoteza nguvu, moyoni nilijuta kujiingiza kwenye vita ya ushirikina. Moyo wangu uliingia hofu ya kupoteza familia yangu yote kutokana na maelezo ya uchawi wa ndizi unavyoua watu kwa mpigo.

Baada ya kuingia ndani alichukua unga kama alivyofanya Maghinde mtoto wa mzee Kidereko. Baada ya muda alisema:
“Kama ulivyoambiwa vita hii ni nzito, hali inavyojionesha ni mbaya sana upande wako. Inaonesha wiki hii na ijayo lazima upande watu watatu.”
“Watu watatu?”
“Ndiyo, hapa panaonesha ndizi tatu zimeiva tayari zinaweza kuanguka wakati wowote.”

“Ndiziii?”
“Ndiyo, inaonekana imedondoka moja ambayo ni baba yako. Zilizobaki zitadondoka wakati wowote ila moja itadondoka wakati wowote kuanzia sasa.”
“Mungu, sasa nitafanyaje jamani, ina maana na mama anakufa?”
“Hatujajua ila wakati wowote tegemea kupata taarifa za kukushtua.”

“Jamani mbona imekuwa hivi?”
“Mzee angekuwepo nina imani kila kitu kingekwenda vizuri.”
“Jamani mtanisaidiaje, Mungu wangu ina maana na mama nampoteza?” nilianza kulia kwa uchungu.

Mara simu yangu iliita, nilipoangalia ilionesha inatoka kwa mke wangu. Moyo ulinilipuka na jasho kunitoka, moyoni niliomba jisipokee habari mbaya. Niliipokea huku nikiuliza kwanza hali ya mama kabla ya salam.

“Haloo mke wangu, mama anaendeleaje?”
“Anaendelea vizuri, ndiye uliyemuacha peke yake huku nyumbani?”
“Nisamehe mke wangu, za huko watoto hawajambo?”
“Mwanao mdogo ndiye anaumwa hapa tupo hospitali tumepewa kitanda.”
“Nini zaidi?”

“Anachemka sana na kuhema kwa shida.”
“Hali hiyo imeanza lini?”
“Hebu subiri kwanza..” mke wangu alisema upande wa pili huku akikata simu.
Nilikata simu kusubiri maelezo ya mke wangu.

“Vipi?” Maghinde aliniuliza.
“Mke wangu anasema mtoto ameumwa ghafla ila mama hajambo.”
“Ameumwa ghafla yupo wapi?”
“Hospital.

Kauli yangu ilifanya wote watazamane kisha walishusha pumzi nzito. Kitendo kile kilinishtua sana na kujiuliza kulikoni kufanya vile.

“Kazala, hapa panaonesha ndizi tatu zimeiva ila moja tayari imedondoka.”
“Sijakuelewa si unasema zimeiva ndizi tatu na moja imedondoka?”
“Ndiyo, katika zile ndizi tatu kuna moja imedondoka na kufanya upoteze watu wawili mpaka sasa.”

“Mungu wangu mnataka kuniambia tofauti na baba kuna mtu amekufa?”
“Tena sasa hivi,” Bwaza alinijibu kwa sauti ya upole.

“U...u..nataka ku..kuni..”
Nilikatishwa kauli na sauti ya mlio wa simu yangu, nilinyamaza na kuangalia simu ilikuwa ya mke wangu. Huku mapigo ya moyo yakinienda mbio nilipokea.
“Haloo mke wangu.”

“Mume wangu...maskini mwanangu,” ilikuwa sauti ya kilio ya mke wangu kuonesha mambo yameharibika.
“Mtoto kafanya nini?” niliuliza pumzi zikiwa juu.
“Ame...me..fariki.”


ITAENDELEA KESHO.
 
Duh yaani kupenda penda kifala ndo kumemsababishia yote haya. Sema hii hadithi imenifundisha kitu kikubwa sana mpaka sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shunie unanifanya kila dakika niangalie kama umepost,weka story hilo usitukatili mama.
 
Kitachotokea hapa ni jamaa kugeuka mwanga kabisa na kuanza kulipa kisasi...
 
Sehemu ya 52

Nilikatishwa kauli na sauti ya mlio wa simu yangu, nilinyamaza na kuangalia simu ilikuwa ya mke wangu. Huku mapigo ya moyo yakinienda mbio nilipokea.
“Haloo mke wangu.”

“Mume wangu...maskini mwanangu,” ilikuwa sauti ya kilio ya mke wangu kuonesha mambo yameharibika.
“Mtoto kafanya nini?” niliuliza pumzi zikiwa juu.

“Ame...me..fariki.”
Nilipatwa na mshtuko na kujikuta napoteza fahamu, nilipozinduka nilijikuta nimelazwa nje kwenye mkeka huku nikipigwa na baridi kali. Muda huo kiza kilikuwa kimeingia ila mwezi ulikuwa ukiangaza. Pembeni yangu alikuwepo Maghinde na Bwaza.

“Kazala,” Maghinde aliniita.
“Naam,”
“Msikilize Bwaza kuna kitu anataka kukuambia cha muhimu sana.”
“Jamani naomba niondoke usiku huu nirudi nyumbani,” kwa kweli baada ya kupata fahamu sikutaka kitu kingine zaidi ya kurudi nyumbani usiku ule kuwahi msiba wa mwanangu.

“Sasa kama ulijua hivyo, huku umekuja kufanya nini?”
“Nilichokifuata sijakipata mnafikiri nifanye nini zaidi ya kurudi kusubiri tufe wote,” kwa kweli nilikuwa nimekata tamaa kwa kauli niliyoambiwa na kilichokuwa kikiendelea.
“Sikiliza Kazala ndiyo maana kikakwambia msikilize Bwaza kuna kitu anataka kukueleza.”

“Haya nieleze mbona mwaka huu nitakoma.”
“Ni hivi bwana Kazala, kweli kama tulivyokueleza hali ni mbaya na ndizi kweli zimeonesha zimeiva na moja imeisha dondoka muda mfupi na zingine mbili zitafuata. Katika kuangalia inaonesha nguvu zinazo kulinda wewe ni za mizimu na majini ya mti mkuu.

“Naamini kabisa majini na mizimu inakutambua, nina imani kilio chako mbele yao kitaweza kukulinda na balaa linalokuja mbele.”
“Sasa jamani, nitawezaje kwenda kwenye mizimu na kuwahi mazishi ya mwanangu?”

“Tulichokipanga tutaondoka usiku huuhuu hadi kwenye mti wa mizimu na mbuzi mwekundu na mweupe na vitu vingine tutakusaidia kuvitafuta ili kutoa sadaka itakayokusaidia kupata msaada wa haraka wa mizimu na majini.”
“Jamani hao mbuzi usiku huu nitawatoa wapi?”
“Wewe utatoa fedha kila kitu tumekipanga wakati tukikusughulikia ulipoanguka.”

“Kwa hiyo shilingi ngapi mbuzi wote?”
Walinitajia fedha ya mbuzi wote, kwa vile nilikuwa nayo niliwapa. Hatukupoteza muda tuliwachukua wale mbuzi wawili na baadhi ya vitu wanavyojua wao kwa kazi yangu na kuelekea porini. Tulitembea kwa saa mbili mpaka kufika kwenye mizimu.
Tilipofika pale Bwaza msaidizi wa mganga rafiki wa mzee Kidereko alifanya kama alivyofanya mzee Kidereko siku aliponipeleka pale enzi ya uhai wake.

Alichukua maji yaliyokuwa kwenye chupa na kuyaweka mdomoni kisha aliyapuliza kuelekea kwenye ule mti mkubwa. Baada ya kumaliza zoezi lile alichukua unga wa dawa na kuurusha sehemu nne za dunia na kusema kwa sauti.

“Hodi mizimu.. hodi majini yote kuanzia Kibwengo na majini yote katika mti huu..hodi tumekuja kutaka msaada wenu.. tunajua ninyi mna nguvu, mizimu yote na majini tupokeeni mtusaidie shida zetu,” Baada ya kusema maneno yale ulifuatia muungurumo ambao haukudumu muda mrefu ulinyamaza pia haukuwa na tofauti na mwanzo nilipokuja kwa mara ya kwanza Kidereko.
Baada ya hali ile kutulia nilimsikia Bwaza akisema:

“Asante mkuu wa mti huu, asante mizimu yote, asante majini yote.”
Alipomaliza kusema vile alinieleza nikae chini kwenye kichuguu ambacho nilikikumbuka nilikalishwa na mzee Kidereko, mambo mengi yalijirudia.
Baada ya kukaa nilinyoosha miguu kuelekea ule mti mkubwa na kutulia kusubiri maelekezo mengine.

Walichukuliwa wale mbuzi na kuanza kuwatembeza kunizunguka mara saba, kisha walisimama mbele yangu kila mmoja akiwa amemshikilia mbuzi wake kuuelekea ule mti mkubwa.

Bwaza kwa sauti kama anazungumza na mtu alisema:
“Mizimu, amekuja tena mwanadamu huyu ambaye mwanzo aliletwa na mkuu wetu na kumtambulisha kwenu.

Tunashukuru msaada wenu umesaidia, lakini umesahau walio mzunguka wazazi na watoto. Tunavyosema hivi tayari walimwengu wameisha chukua vichwa wawili kwenye zizi lake.

“Tumefundishwa wa wakuu kuwa tunapopata matatizo tukimbilie huku kuomba msaada wenu. Tunajua ninyi amshindwi na kitu tunaomba mumsaidie mwanadamu huyu na waliomzunguka. Wakuu ndizi zilizoiva zisidondoke bali wadondoke wao.”

Baada ya kusema vile ulizuka upepo mkali, ulivuma kwa muda kidogo. Safari ile sikushtuka kwani hakikuwa kitu kigeni kwangu. Baada upepo kutulia Bwaza aliniambia ninuie kwa kuwashika wale mbuzi wote kichwani.
“Ninuie nini?” niliuliza kwa vile nilikuwa sijui cha kunuia.

“Chochote kuhusiana matatizo yako ili kukuondolea mabalaa yanayokukabili.”
Nilitulia na kunuia kuiomba mizimu na majini kunilinda mimi na familia yangu.

Baada ya kunuia nilimweleza Bwaza nimemaliza. Waliwachukua wale mbuzi na kuwalaza, kisha waliwachinja wote na kuchukua mfuko uliokuwa na nafaka mchanganyiko na kuumimina kwenye ungo uliokuwa pembeni ya ule mtu mkubwa. Kisha Bwaza alipaza sauti na kusema:

“Mizimu na majini tumekuleteeni zawadi kubwa ambayo tuna imani mtaipenda. Tunakuahidini kuwaletea ng’ombe mzima kama mtatufanyia kazi nzuri.”

Baada ya kuzungumza vile alimwaga unga wa dawa kwenye damu ya mbuzi na kwenye nafaka kisha tulisimama wote nyuma ya wale mbuzi waliowachinja.
Baada ya kusimama nilishtuka kusikia sauti ukicheka mfurulizo kisha vigelegele ukifuatiwa na upepo uliovuma kwa muda kisha ulikoma.

Baada ya muda upepo ulitulia alinieleza nizunguke ule mti mkubwa mara kumi na nne huku nikinuia tena. Nilifanya vile kwa kuuzunguka mara kumi na nne, kisha nilirudi walipokuwa wamesimama. Baada ya muda palitokea mtikisiko wa ajabu kama mti ule mkubwa unataka kung’oka. Sikuwa tena na wasi wa kuangukiwa na mti ule mkubwa.

Baada ya zoezi lile Bwaza alinieleza:
“Nina imani mambo yamekwenda vizuri sana, inaoneka mizimu na majini imefurahi kwa hiyo tuna imani ndizi zilizobaki haziwezi kudondoka tena.”
“Nashukuru sana kwa msaada wetu,” niliwahukuru nikiwa siamini walichonieleza.

“Washukuru Mizimu na majini ndiyo yaliyokubali kukusaidia.”
Niliishukuru mizimu na majini kisha tulirudi nyumbani, kwa kumwaga dawa ya unga huku nikisema kwa sauti maneno niliyoelezwa niyaseme.

Baada ya zoezi lile nilielezwa shughuli imeisha hivyo tulitakiwa kuondoka kurudi nyumbani.
Nilielezwa sitapewa dawa nyingine kwa vile kazi iliishia kwenye mti mkubwa. Mpaka tunafika nyumbani ilikuwa saa nane za usiku.

Kwa vile nilikuwa nimechoka sana nilala kidogo na saa kumi za usiku niliamka na kuianza safari msiba wa mwanangu nyumbani. Japokuwa nililala kidogo, kitandani muda wote niligeuka moyo ukiniuma familia yangu ikiteketea huku naiona.

Mpaka muda niliopanga kuamka sikupata usingizi hata kidogo. Njia nzima kichwa kilikuwa kizito kutokana na uchovu na kutokulala.

Niliendesha gari macho yakiwa yamenivimba kwa kukosa usingizi na mwili uliniuma kama kidonda kutokana na kutopumzika kwa siku nzima.

Niliondoka kurudi nyumbani kwa kujilazimisha, mwili ulikuwa hautaki kabisa kwa uchovu wa mihangaiko na kukosa usingizi.

Kama isingekuwa msiba wa mwanangu ningelala na kuondoka jioni ya siku ile. Niliendesha gari huku moyo ukiniuma kuona napoteza ukoo kwa ajili ya ushirikina, kuna kuopindi nililia peke yangu. Lakini nilijua kulia si dawa zaidi ya kupambana.

Niliyakumbuka maneno ya rafiki yangu Simon kuhusu kumuacha mke wangu kama tabia zake hazibadiliki kuliko kwenda kwa mganga. Niliamini kama ningemsikiza yote yale yasingenikuta ya kumkufuru Mungu. Lakini bado nilikuwa na haki ya kumpigania mke wangu.

Niliamini kama ningekubali kumwacha, ningeendelea kuwa mnyonge, nilijiuliza ningeacha wanawake wangapi. Bado swali lililoniumiza kwa nini mtu amfuate mke wangu.

Nilikuwa tayari nimempoteza baba mzazi na mwanangu wa mwisho na kupewa imani kuwa wawili waliotakiwa kuondoka wiki ijayo kupitia tambiko lile, wote waliotakiwa kufa kwa uchawi wa ndizi wamepona.

Nilifika nyumbani majira ya saa tano asubuhi, ilikuwata watu wamesanyika nyumbani kuashiria kuna msibani kweli. Aliyenipokea alikuwa mzee Samweli rafiki wa marehemu baba. Baada ya kunipokea alinieleza taarifa iliyozidi kunichanganya na kutaka kunirusha akili.

Alinieleza mke wangu na mama yangu wapo hospitali baada ya kuugua ghafla usiku wa kuamkia siku ile na hali zao si nzuri sana. Nilijikuta nikichananyikiwa na kuamini zile ndizi mbili nilizoelezwa zimeiva ni mke wangu na mama yangu.

Nilimuomba Mungu awanusuru maisha yao, kwani ningekuwa mwenzawazimu kama ningezika watu watatu kwa mpigo.
Mwili wa mwanangu ulikuwa bado uko hospitali. Nilimshukuru mzee Samweli na familia yake kusimamia msiba na ugonjwa wa mama na mke wangu.

Nilipofika hospitali nilikuta hali za wagonjwa zimebadilika kwa kiasi kikubwa. Hata daktari alishangaa wagonjwa kupata nafuu ya haraka tofauti na walivyopelekwa usiku wa kuamkia siku ile.

Kauli ile ilinifanya nikumbuke maneno ya waganga kule kwenye mizimu alipoomba ndizi zilizoiva zisidondoke. Ilionesha wazi kama nisingekwenda kule ningewapoteza mama na mke wangu.

Baada ya matibabu walitoka jioni ya siku ile na kesho yake tulifanya mazishi ya mwanangu. Baada ya mazishi nilipumzika kwa wiki nyingine na kurudi kazini. Baada ya kurudi kazini, muda mwingi nilikuwa mtu mwenye mawazo kuhusiana na watu waliokaa na kupanga kuipukutisha familia yangu.

Moyoni sikukubali kuona naonewa vile, nilipanga kwenda popote koya yote ya dunia kuutafuta uchawi hata nchini Nigeria ili kuhakikisha naupukutisha ukoo wao wote.

Kwa uchungu wa kumpoteza baba yangu na mwanangu nilikuwa radhi kufilisika lakini nihakikishe nimelipa kisasi cha mla mbuzi kulipa ng’ombe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…