mizambwa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2008
- 4,422
- 1,790
- Thread starter
- #41
MAPENZI YA DHATI
SEHEMU YA KUMI NA TANO:
SEHEMU YA KUMI NA TANO:
Nyumba tulivu kabisa ya mh.Manyama ililipuka kwa furaha kwa kurejea kwa Reshmail akiwa mwenye furaha tele umetuletea na mjukuu!! alitania mama Resh.
mtoto wa Eve huyu anamwita mama mdogo Resh naye akadanganya
kazuri kweli kama alisita kumalizia baba yake
ni kama Adam baba usiogope kufananisha wamefanana kweli alimtoa baba yake wasiwasi huku akimkumbatia baba yake kasha mama yake.
mh!! Tulikuwa wapweke kweli jamani dada msaidizi wa kazi za ndani aliyeitwa Fatuma alimwambia Reshmail huku akimkumbatia na kumbusu shavuni
na huyo mtoto kama mwanao vile hebu kaone aliendelea Fatuma
sio kama wa kwangu ila ni wa kwangu humwoni alivyonifanana? alijibu kimzaha na wote wakacheka kwa pamoja
** ***** *****
Hali ya sintofahamu iliwakumba wale wafanyakazi wa lile jumba (ngomeni) alipokuwa anatunzwa Adam. Mkuu wa ngome hiyo bwana Lwebe alikuwa na ghadhabu kubwa sana,kila mbua alikuwa na ghadhabu kubwa sana,kila kitu kilikuwa shaghala baghala kila mara aliongea kwenye simu hukuakitoa vitisho vikali sana na hata kutishia kuua.
Wafanyakazi hawakumwelewa lolote walizitambua hasira za bosi wao huyo ambaye mara chache anazokuwa katika hali kama hiyo humalizia hasira zake kwa kutoa roho ya mtu
mlete Adam hapa mara moja !! aliamrisha huku akijikuna ndevu zake kwa kutumia mdomo wa bunduki aliyokuwa nayo
maskini Adam sijui amekosa nini alijiuliza aliyekuwa anaenda kumwita. Bila wasiwasi wowote Adam akamfikia Lwebe D kwa ishara ya mkono akamwamrisha kumfuata,pamoja na mabaunsa wawili waliotinga suti nyeusi .
lwebe hakuongea neno lolote hadi walipofika kwa nje,tayari kigiza cha saa mbili kilikuwa kimetawala
mlete na yule mwingine wa nyumba ya chini alitoa amri nyingine tena baada ya tano walioagizwa wakarejea na mtu mwingine
we kinyamkera una bahati sana aliyekuleta hapa amesema haujasambaza taarifa zozote mbaya laiti kama ungethubutu ningeiondoa shingo yako sasa hivi.
Nakuacha uende tena lakini tambua mtandao wangu upo popote katika nchi hii sasa ole wako uthubutu kunyanyua mdomo wako kutangaza ujinga aliambiwa yule binti aliyeletwa pale huku akionyeshwa njia ya kutokea
we kidume kwa jeuri ya bosi wako kujaribu kunidhurumu pesa yangu wakati wewe unakula na kulala bure hapa;lazima nimwonyeshe mimi ni nani na ni wewe utakayeumia aliongea Lwebe huku akipuliza moshi wa sigara hewani.
**********
Ilikuwa ni mwezi mmoja tangu Bite arejeshwe kwenye ile ngome lakini katika chumba kingine,hakuwa msaidizi wa kazi tena bali mtuhumiwa na hakupata fursa ya kuonana na Adam hata siku moja .
siku alipotolewa nje usiku na kwa mahesabu ya miaka mitano ambayo Adam angekaa pale machale yalimcheza,alivyopewa uhuru wa kuondoka hakwenda mbali sana alifika eneo moja kwenye mtaro na kuanza kusubiria ni nini kitatokea japo hakusikia vizuri maneno lakini alisubiri hata vitendo
**********
Mkataba wa miaka mitano alioandikishana Bi.gaudensia na Lwebe wa Adam kuhifadhiwa pale ulikuwa umeisha tayari na miezi mitatu zaidi ilikuwa imepita,suala hilo la kuchelewesha pesa lilimkera sana Lwebe na pia ahadi za uongo kutoka kwa Gaudencia zilichochea sana hasira za Lwebe kufikia hatua ya kuamua kuzipooza kwa huyo Adam aliyehifadhiwa hapo.
Ni usiku huo alipoamua kwa mkono wake mwenyewe Adam duniani kama kisasi kwa Bi.Gaudensia
paa!! Paa!! mlio mkali wa risasi ulisikika na kumzindua Bite ambaye alikuwa amepitiwa na usingizi pale kwenye mtalo, kidogo apige kelele lakini viganja vya mkono wake vikawahi kuuziba haraka sana. Hakusikia hata chembe ya kilio na baada ya dakika kama saba akasikia milango imefungwa
Kwa ujasiri na tahadhari kubwa Bite akajisogeza hadi karibu kabisa na eneo ambalo aliamini hakika ndipo mlio wa risasi umetokea huku kichwani kwake akiwa ana jibu la nimesahau saa yangu iwapo atakutana au kushtukiwa na mlinzi, kwa hofu alizurura katika lile eneo dakika tatu bila kuona chochotenau wameingia nae ndani?? alijiuliza bila kupata jibu
koh!! Koh!! Alishtuliwa na sauti ya kikohozi nyuma yake, mawazo yake alidhania ni mlinzi eneo lile lakini alipogeukz hakuwa mlinzi tena ni mwili wa binadamu ukiwa chini,hakutambua mara moja yule ni nani hadi macho yake yalipolizoea giza la pale Adam!!!!!
we ni nani?? alijibiwa kwa sauti ya chini sana iliyokuwa inaunguruma kama mnyama anayechinjwa
Bite mimi jamani Adam
ondoka watakuua hao Bite ondoka niache mi nife hapa alijibu Adam
hapana Adam usife,usife Adam twende tukamtafute mwanetu Chrstian anatamani sana kukuona,usife Adam tafadhali Bite alibembeleza
**********
Risasi mbili zilizopenya katika paja lake la kulia zilikuwa zimemsababishia Adam kuvuja sana damu na mbele yake alichokitarajia ni kifo hakuna kingine lakini maneno ya Bite.
Nguvu zilirejea upya kabisa tena kwa kasiBite ulijifungua, mtoto wangu yuko wapi? Ni wa kiume au wa kike? alihoji maswali mfululizo Adam huku akijitutumua kusimama kwa nguvu alizokuwa amezipata
ni stori ndefu na hapa sio mahali pake tuondoke tafadhali jitahidi kuna hatari kubwa kama unampenda mwanao jitahidi tuondoke aliongea Bite huku akiuweka mkono wa Adam katika bega lake na kuanza kumkongoja kutoka eneo lile huku (Adam) akitumia mguu mmoja na ule uliojeruhiwa ukiwa juu juu.
Kutoka pale walipokuwa hadi barabarani haukuwa umbali mrefu sana na walifanikiwa kufika,kwa giza nene lililokuwepo hawakuweza kuonekana na mtu yeyote,nguvu zilikuwa zinamwishia Adam kutokana na kuvuja damu lakini alijikaza kijasiri sana na kuendelea mbele
********* ******* *******
ITAENDELEA...............