FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 2,229
- 4,345
- Thread starter
- #41
STORY: JUMBA JEUSI
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
EPISODE 18.
ENDELEA.......
Huyo mwanamke ndiye ulikuwa ubavu wa mlinzi mkuu wa raisi, wanaume wengi kushindwa kumpata mrembo huyo sifa zilizagaa kila kona hivyo ikapelekea kila mtu akawa anahitaji kuweza kumjua mwanaume ambaye alikuwa anampa kiburi mrembo huyo kiasi kwamba akawa anamkataa kila mwanaume ambaye alikuwa anakuja na kuonekana mbele yake lakini wote waligonga mwamba kwa sababu mahusiano yake yalikuwa yana usiri mkubwa mno. Wawili hao walikuwa na mapenzi ya kweli na ya dhati lakini ya siri kutokana na kazi zao kutohusiana moja kwa moja na kama yangekuwa wazi basi ingekuwa hatari kwao wote wawili.
Kwenye kuanza kuzifukua habari hizo ndipo Jessica alipo zipata kwenye mkono wake, alijaribu kufuatilia ili kuweza kuona kama mapenzi hayo yalikuwa na uhusiano wowote na raisi kwenda kuuawa lakini hakuona kasoro wala dosari yoyote ile hivyo akaona ni jambo ambalo halimhusu kwa wakati ule japo kiitifaki haikuwa sawa ila alivutiwa na simulizi ile ya yale mapenzi akajikuta anavutiwa na watu hao wawili hivyo akaamua kuwaacha na maisha yao kama yalivyo. Ila kwenye mazingira ambayo alikuwepo wakati huo akihitaji kuupata ukweli wa maisha ya Bazoka ndipo alimkumbuka mrembo huyo kwa sababu kama ni kujua wapi alipo basi huyo ndiye ambaye alikuwa anapaswa kuwa na taarifa za mwanaume wake ndipo akajikuta analitamka jina hilo
“Zyra” alitoa tabasamu hafifu wakati huo akiwa anavaa haraka haraka na kubeba funguo za gari kisha akatoka ili awahi kwenda kukutana naye ana kwa ana kwani alikuwa na mambo kadhaa ya kuweza kuongea naye.
ZYRA
Lilikuwa ni jina ambalo lilikuwa linatoa tafsiri sahihi ya nini maana ya urembo, jina ambalo lilikuwa linaelezea maana sahihi ya mwanamke ambaye ameumbwa kisha dunia ikamnakshi kwa uzuri wake na kila mtu akabariki jambo hilo. Alikuwa ni miss Tanzania kwa miaka mitatu mfululizo na mwaka huo wa tatu pia alifanikiwa kuwa Miss East Africa (Afrika ya Mashariki).
Ni miongoni mwa wanawake ambao hawakuwa na umri mkubwa lakini walikuwa na mafanikio makubwa, mafanikio yake yalikuja kutokana na nidhamu yake kwenye kazi ambayo alikuwa anaifanya jambo ambalo lilimsaidia kufika mbali lakini pia aliitumia chapa yake aliyo itengeneza kuweza kutengeneza na kukuza bidhaa zake za vipodozi ambazo zilikuwa zinapendwa kila kona na wadada wengi wa mjini ambao walikuwa wanahitaji kwenda na kasi ya maendeleo ya utandawazi. Zyra hakuwa mwanamke ambaye alipenda kuyaweka maisha yake binafsi kwenye mitandao wala kwenye jamii, alipenda maisha hayo kuwa binafsi baina yake mwenyewe na hao ambao walikuwa wanamhusu kwenye hayo maisha.
Jambo hilo ndilo lilifanya iwe vigumu yeye kutabirika au kujulikana nje ya kazi yake ya umiss ambapo watu walikuwa wakihangaika na kutamani kuweza kulijua hilo lakini haikuwezekana. Hayo maisha yake binafsi ndipo siri kubwa ya mafanikio yake ilipokuwa kwa sababu usiri wake ndio ambao ulifanya maadui zake na wale watu ambao walikuwa wakitamani kushindana naye wasijue ni sehemu gani walitakiwa kumbana ili waweze kumdondosha na kumshinda. Ilikuwa ni zaidi ya miaka mitatu imepita tangu aingie kwenye penzi ambalo lilikuwa limekusudiwa kuwa ndoa, penzi ambalo lilifikia sehemu likaaminiwa kwa ukubwa baina ya hao wawili ambao waliamua kulikubali kwa pamoja.
Oliver Jefferson ndilo lilikuwa jina la mwanaume ambaye yeye alikuwa anapendana naye, mwanaume ambaye alikuwa bado kijana shupavu lakini alipata bahati ya kuwa karibu na mkubwa wa nchi. Alikutana na bwana huyo mwaka mmoja tu baada ya raisi kuchaguliwa wakati ndo ikiwa mwaka wake wa kwanza kuweza kushiriki kwenye mashindano ya umiss. Mrembo huyo na wenzake walikuwa wamealikwa Ikulu na mheshimiwa siku hiyo ambapo sherehe ilichelewa kuisha na mheshimiwa raisi alimtaka mlinzi wake ahakikishe wanawake hao wote wanafika makwao salama kabisa na ndio ulikuwa mwanzo wa wawili hao kufahamiana ambapo matokeo yake ni kwamba walizama kwenye huba zito.
Safari yao ambayo ilianzia pasipo julikana iliishia sehemu ya wawili hao kuaminiana isivyo kawaida na hata yale mafanikio yote ambayo aliyapata Zyra yalifanywa na bwana Oliver ambaye aliamua kujitoa kwa mwanamke huyo kwa kumkutanisha na watu wakubwa ambao ndio waliirahisisha safari yake ambayo huenda asingeweza kuifikia akiwa mwenyewe naye hakufanya ajizi, aliitumia vizuri nafasi hiyo ya kuwa karibu na mlinzi mkuu wa raisi. Safari ilikuwa nzuri na yenye mfano bora mpaka pale ambapo yalitokea matatizo baada ya raisi kufa ndipo tatizo lilipokuwa limeanzia ikiwa ni siku kadhaa tu zimepita na siku hiyo Jessica aliamua kumtembea mrembo huyo kwa sababu alijua ndiyo ilikuwa sehemu pekee ya kuweza kuyapata majibu yake ambayo aliyakosa kwa sababu hiyo ingekuwa safari ya kumpata yule binti ambayo alimpoteza Luana.
Jessica baada ya kufuatilia kwa muda mrefu aligundua kwamba mwanamke huyo siku hiyo alikuwa kwenye moja ya makasino ya bei ghali hivyo ikamlazimu kumsubiri kwani hakutaka kumkurupukia na kumkosa kwa sababu kwake ilikuwa ni mhimu ampate usiku huo. alikuwa amesimama sehemu ya watu kuingilia akipata kinywaji huku akiwa ameegamia nguzo moja akijifanya kuwaangalia watu ambao walikuwa wanatafuta fursa kwenye kamari. Akiwa hapo alikaa kwa muda wa saa zima ndipo akaona mrembo huyo anatoka nje akiwa ana furaha tele lakini kwa nyuma yake kulikuwa na wanaume wanne ambapo mmoja alikuwa amemshikilia kiuno na wale wengine watatu walikuwa nyuma yake wakionekana kabisa kwamba walikuwa ni walinzi. Watu wale walikuwa wanatembea kwa furaha na ni wazi kwamba walikuwa ni watu ambao walijuana kwa muda mrefu jambo ambalo Jessica lilimshangaza kidogo kwani kulikuwa na sintofahamu ya uwepo wa mpenzi wake wa muda mrefu lakini mwenzake alikuwa anafurahia maisha? Kuna roho ilimtaka kuwa mpole kwani alihisi huenda bwana yule alikuwa salama, lakini huyu ambaye alikuwa naye alikuwa nani? Alipotezea kwani hakuona kama inamhusu sana.
Alitoka haraka nyuma yao na kukimbilia upande wa pili kuona tukio ambalo watu hao walikuwa wanaenda kulifanya, walizunguka mpaka sehemu ya nyuma ambako kulikuwa na gari ya kifahari imepaki hapo, walinzi walibaki umbali kadhaa na kugeuka, yule mwanaume alipo ikaribia gari ile alimuinamisha Zyra na kuifunua sketi yake ambapo ndani hakuvaa kitu chochote akaanza kufanya naye mapenzi huku wote wakifurahia hali hiyo na baada ya dakika tano walimaliza. Walinyonyana ndimi zao na mwanaume huyo akamtaka mrembo huyo aingie kwenye gari kisha mlinzi mmoja akaja na kuliwasha gari hilo akaondoka nalo taratibu.
Jessica alibaki ameduwaa kwa muda mpaka alipo ona ile gari inatoka nje kabisa ya eneo lile ndipo akashtuka. Kwa heshima ambayo alikuwa amejitengenezea Zyra kwenye jamii hata siku moja hakutarajia kwamba anaweza akamkuta akiwa anafanya tukio la namna ile ila aliamua kupotezea kwa kuhisi kwamba huenda ndiyo sababu kubwa ambayo ilimfanya mwanamke yule kuamua kutoyaweka maisha yake binafsi bayana na hadharani kwa kila mtu.
Aliingia kwenye gari yake na kuanza kuifuatilia ile gari ili ajue mahali ambako walikuwa wanaelekea majira yale. Jiji lilikuwa limetulia, usiku ulikuwa unazidi kuwa mzito na kila mtu alikuwa anapambana na hali yake kuhakikisha anamalizana na malengo yake ya siku hiyo kabla ya kuianza siku nyingine. Ile gari ilienda kusimama nje ya jumba moja safi ambalo lilikuwa la ghorofa moja, lilikuwa limepambwa vya kutosha na lilipendeza bila shaka bibie alikuwa anaishi maisha ya ndoto za wanawake wengi mjini. Alisimama umbali mrefu akiwa ameizima gari yake kabisa kusubiri kile ambacho kingefuata baada ya pale. Zilipita dakika tano tu ile gari ikatoka mle ndani na kutoka nje na wakati gari inatoka aliona kuna mlinzi mmoja alitoka nayo kisha akarudi ndani.
Ni jambo ambalo lilimfariji zaidi kwa sababu yule mlinzi alikuwa ametokea kwenye kampuni moja ya ulinzi ambayo aliamini haiwezi kuzalisha watu wa hatari hata kidogo, maana yake bibie alikuwa analindwa na watu wa kawaida tu ambao hakutakiwa hata kuwaua. Alivaa gloves kwenye mikono yake na kusogelea kwenye lile geti, aligonga taratibu akatoka yule bwana kwa mara nyingine. Alihitaji kuuliza jina la yule mwanamke ila aligushwa kwenye shingo yake akaenda chini, baada ya kuhakikisha amekamilisha hilo alirukia ndani kwa sarakasi ambapo alikutana na mlinzi mwingine ambaye alikuwa anasogea ili kuweza kuuliza juu ya hali ambayo ilikuwepo hapo ila naye hakuwa na bahati nzuri. Muda ambao aliutumia kutambua kwamba kulikuwa na adui ndani ya hilo eneo ni wakati ambao alikutana na ngumi ya shingo akadondoka na kupoteza fahamu.
Jessica alitambua kwamba eneo hilo lilikuwa na walinzi wawili tu pekee hivyo alikuwa amewamaliza. Aliangalia kwenye jumba hilo kwa umakini na kutambua kwamba usalama ulikuwa ni wa kutosha, sasa taratibu alielekea mlangoni kwani ulikuwa ni wakati wa kuweza kuongea na mwenyeji wake ambaye ndiye alimpeleka hilo eneo. Wakati anafika mlangoni alikigusa kitasa na kugundua kwamba kipo wazi, huenda ni kwa sababu ya uharaka wa mwenyeji au alikuwa anajiamini kwa sababu ana ulinzi ndiyo maana hakuwa makini. Baada ya kufungua alikutana na sebule kubwa ambayo ilikuwa imesheheni vitu vya bei ghali lakini hapakuwa na mtu, aliangaza kila sehemu ndipo akasikia sauti ya maji upande wa juu akagundua kwamba mwenyeji wake alikuwa kuoga.
18 inafika mwisho.
FEBIANI BABUYA.
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
EPISODE 18.
ENDELEA.......
Huyo mwanamke ndiye ulikuwa ubavu wa mlinzi mkuu wa raisi, wanaume wengi kushindwa kumpata mrembo huyo sifa zilizagaa kila kona hivyo ikapelekea kila mtu akawa anahitaji kuweza kumjua mwanaume ambaye alikuwa anampa kiburi mrembo huyo kiasi kwamba akawa anamkataa kila mwanaume ambaye alikuwa anakuja na kuonekana mbele yake lakini wote waligonga mwamba kwa sababu mahusiano yake yalikuwa yana usiri mkubwa mno. Wawili hao walikuwa na mapenzi ya kweli na ya dhati lakini ya siri kutokana na kazi zao kutohusiana moja kwa moja na kama yangekuwa wazi basi ingekuwa hatari kwao wote wawili.
Kwenye kuanza kuzifukua habari hizo ndipo Jessica alipo zipata kwenye mkono wake, alijaribu kufuatilia ili kuweza kuona kama mapenzi hayo yalikuwa na uhusiano wowote na raisi kwenda kuuawa lakini hakuona kasoro wala dosari yoyote ile hivyo akaona ni jambo ambalo halimhusu kwa wakati ule japo kiitifaki haikuwa sawa ila alivutiwa na simulizi ile ya yale mapenzi akajikuta anavutiwa na watu hao wawili hivyo akaamua kuwaacha na maisha yao kama yalivyo. Ila kwenye mazingira ambayo alikuwepo wakati huo akihitaji kuupata ukweli wa maisha ya Bazoka ndipo alimkumbuka mrembo huyo kwa sababu kama ni kujua wapi alipo basi huyo ndiye ambaye alikuwa anapaswa kuwa na taarifa za mwanaume wake ndipo akajikuta analitamka jina hilo
“Zyra” alitoa tabasamu hafifu wakati huo akiwa anavaa haraka haraka na kubeba funguo za gari kisha akatoka ili awahi kwenda kukutana naye ana kwa ana kwani alikuwa na mambo kadhaa ya kuweza kuongea naye.
ZYRA
Lilikuwa ni jina ambalo lilikuwa linatoa tafsiri sahihi ya nini maana ya urembo, jina ambalo lilikuwa linaelezea maana sahihi ya mwanamke ambaye ameumbwa kisha dunia ikamnakshi kwa uzuri wake na kila mtu akabariki jambo hilo. Alikuwa ni miss Tanzania kwa miaka mitatu mfululizo na mwaka huo wa tatu pia alifanikiwa kuwa Miss East Africa (Afrika ya Mashariki).
Ni miongoni mwa wanawake ambao hawakuwa na umri mkubwa lakini walikuwa na mafanikio makubwa, mafanikio yake yalikuja kutokana na nidhamu yake kwenye kazi ambayo alikuwa anaifanya jambo ambalo lilimsaidia kufika mbali lakini pia aliitumia chapa yake aliyo itengeneza kuweza kutengeneza na kukuza bidhaa zake za vipodozi ambazo zilikuwa zinapendwa kila kona na wadada wengi wa mjini ambao walikuwa wanahitaji kwenda na kasi ya maendeleo ya utandawazi. Zyra hakuwa mwanamke ambaye alipenda kuyaweka maisha yake binafsi kwenye mitandao wala kwenye jamii, alipenda maisha hayo kuwa binafsi baina yake mwenyewe na hao ambao walikuwa wanamhusu kwenye hayo maisha.
Jambo hilo ndilo lilifanya iwe vigumu yeye kutabirika au kujulikana nje ya kazi yake ya umiss ambapo watu walikuwa wakihangaika na kutamani kuweza kulijua hilo lakini haikuwezekana. Hayo maisha yake binafsi ndipo siri kubwa ya mafanikio yake ilipokuwa kwa sababu usiri wake ndio ambao ulifanya maadui zake na wale watu ambao walikuwa wakitamani kushindana naye wasijue ni sehemu gani walitakiwa kumbana ili waweze kumdondosha na kumshinda. Ilikuwa ni zaidi ya miaka mitatu imepita tangu aingie kwenye penzi ambalo lilikuwa limekusudiwa kuwa ndoa, penzi ambalo lilifikia sehemu likaaminiwa kwa ukubwa baina ya hao wawili ambao waliamua kulikubali kwa pamoja.
Oliver Jefferson ndilo lilikuwa jina la mwanaume ambaye yeye alikuwa anapendana naye, mwanaume ambaye alikuwa bado kijana shupavu lakini alipata bahati ya kuwa karibu na mkubwa wa nchi. Alikutana na bwana huyo mwaka mmoja tu baada ya raisi kuchaguliwa wakati ndo ikiwa mwaka wake wa kwanza kuweza kushiriki kwenye mashindano ya umiss. Mrembo huyo na wenzake walikuwa wamealikwa Ikulu na mheshimiwa siku hiyo ambapo sherehe ilichelewa kuisha na mheshimiwa raisi alimtaka mlinzi wake ahakikishe wanawake hao wote wanafika makwao salama kabisa na ndio ulikuwa mwanzo wa wawili hao kufahamiana ambapo matokeo yake ni kwamba walizama kwenye huba zito.
Safari yao ambayo ilianzia pasipo julikana iliishia sehemu ya wawili hao kuaminiana isivyo kawaida na hata yale mafanikio yote ambayo aliyapata Zyra yalifanywa na bwana Oliver ambaye aliamua kujitoa kwa mwanamke huyo kwa kumkutanisha na watu wakubwa ambao ndio waliirahisisha safari yake ambayo huenda asingeweza kuifikia akiwa mwenyewe naye hakufanya ajizi, aliitumia vizuri nafasi hiyo ya kuwa karibu na mlinzi mkuu wa raisi. Safari ilikuwa nzuri na yenye mfano bora mpaka pale ambapo yalitokea matatizo baada ya raisi kufa ndipo tatizo lilipokuwa limeanzia ikiwa ni siku kadhaa tu zimepita na siku hiyo Jessica aliamua kumtembea mrembo huyo kwa sababu alijua ndiyo ilikuwa sehemu pekee ya kuweza kuyapata majibu yake ambayo aliyakosa kwa sababu hiyo ingekuwa safari ya kumpata yule binti ambayo alimpoteza Luana.
Jessica baada ya kufuatilia kwa muda mrefu aligundua kwamba mwanamke huyo siku hiyo alikuwa kwenye moja ya makasino ya bei ghali hivyo ikamlazimu kumsubiri kwani hakutaka kumkurupukia na kumkosa kwa sababu kwake ilikuwa ni mhimu ampate usiku huo. alikuwa amesimama sehemu ya watu kuingilia akipata kinywaji huku akiwa ameegamia nguzo moja akijifanya kuwaangalia watu ambao walikuwa wanatafuta fursa kwenye kamari. Akiwa hapo alikaa kwa muda wa saa zima ndipo akaona mrembo huyo anatoka nje akiwa ana furaha tele lakini kwa nyuma yake kulikuwa na wanaume wanne ambapo mmoja alikuwa amemshikilia kiuno na wale wengine watatu walikuwa nyuma yake wakionekana kabisa kwamba walikuwa ni walinzi. Watu wale walikuwa wanatembea kwa furaha na ni wazi kwamba walikuwa ni watu ambao walijuana kwa muda mrefu jambo ambalo Jessica lilimshangaza kidogo kwani kulikuwa na sintofahamu ya uwepo wa mpenzi wake wa muda mrefu lakini mwenzake alikuwa anafurahia maisha? Kuna roho ilimtaka kuwa mpole kwani alihisi huenda bwana yule alikuwa salama, lakini huyu ambaye alikuwa naye alikuwa nani? Alipotezea kwani hakuona kama inamhusu sana.
Alitoka haraka nyuma yao na kukimbilia upande wa pili kuona tukio ambalo watu hao walikuwa wanaenda kulifanya, walizunguka mpaka sehemu ya nyuma ambako kulikuwa na gari ya kifahari imepaki hapo, walinzi walibaki umbali kadhaa na kugeuka, yule mwanaume alipo ikaribia gari ile alimuinamisha Zyra na kuifunua sketi yake ambapo ndani hakuvaa kitu chochote akaanza kufanya naye mapenzi huku wote wakifurahia hali hiyo na baada ya dakika tano walimaliza. Walinyonyana ndimi zao na mwanaume huyo akamtaka mrembo huyo aingie kwenye gari kisha mlinzi mmoja akaja na kuliwasha gari hilo akaondoka nalo taratibu.
Jessica alibaki ameduwaa kwa muda mpaka alipo ona ile gari inatoka nje kabisa ya eneo lile ndipo akashtuka. Kwa heshima ambayo alikuwa amejitengenezea Zyra kwenye jamii hata siku moja hakutarajia kwamba anaweza akamkuta akiwa anafanya tukio la namna ile ila aliamua kupotezea kwa kuhisi kwamba huenda ndiyo sababu kubwa ambayo ilimfanya mwanamke yule kuamua kutoyaweka maisha yake binafsi bayana na hadharani kwa kila mtu.
Aliingia kwenye gari yake na kuanza kuifuatilia ile gari ili ajue mahali ambako walikuwa wanaelekea majira yale. Jiji lilikuwa limetulia, usiku ulikuwa unazidi kuwa mzito na kila mtu alikuwa anapambana na hali yake kuhakikisha anamalizana na malengo yake ya siku hiyo kabla ya kuianza siku nyingine. Ile gari ilienda kusimama nje ya jumba moja safi ambalo lilikuwa la ghorofa moja, lilikuwa limepambwa vya kutosha na lilipendeza bila shaka bibie alikuwa anaishi maisha ya ndoto za wanawake wengi mjini. Alisimama umbali mrefu akiwa ameizima gari yake kabisa kusubiri kile ambacho kingefuata baada ya pale. Zilipita dakika tano tu ile gari ikatoka mle ndani na kutoka nje na wakati gari inatoka aliona kuna mlinzi mmoja alitoka nayo kisha akarudi ndani.
Ni jambo ambalo lilimfariji zaidi kwa sababu yule mlinzi alikuwa ametokea kwenye kampuni moja ya ulinzi ambayo aliamini haiwezi kuzalisha watu wa hatari hata kidogo, maana yake bibie alikuwa analindwa na watu wa kawaida tu ambao hakutakiwa hata kuwaua. Alivaa gloves kwenye mikono yake na kusogelea kwenye lile geti, aligonga taratibu akatoka yule bwana kwa mara nyingine. Alihitaji kuuliza jina la yule mwanamke ila aligushwa kwenye shingo yake akaenda chini, baada ya kuhakikisha amekamilisha hilo alirukia ndani kwa sarakasi ambapo alikutana na mlinzi mwingine ambaye alikuwa anasogea ili kuweza kuuliza juu ya hali ambayo ilikuwepo hapo ila naye hakuwa na bahati nzuri. Muda ambao aliutumia kutambua kwamba kulikuwa na adui ndani ya hilo eneo ni wakati ambao alikutana na ngumi ya shingo akadondoka na kupoteza fahamu.
Jessica alitambua kwamba eneo hilo lilikuwa na walinzi wawili tu pekee hivyo alikuwa amewamaliza. Aliangalia kwenye jumba hilo kwa umakini na kutambua kwamba usalama ulikuwa ni wa kutosha, sasa taratibu alielekea mlangoni kwani ulikuwa ni wakati wa kuweza kuongea na mwenyeji wake ambaye ndiye alimpeleka hilo eneo. Wakati anafika mlangoni alikigusa kitasa na kugundua kwamba kipo wazi, huenda ni kwa sababu ya uharaka wa mwenyeji au alikuwa anajiamini kwa sababu ana ulinzi ndiyo maana hakuwa makini. Baada ya kufungua alikutana na sebule kubwa ambayo ilikuwa imesheheni vitu vya bei ghali lakini hapakuwa na mtu, aliangaza kila sehemu ndipo akasikia sauti ya maji upande wa juu akagundua kwamba mwenyeji wake alikuwa kuoga.
18 inafika mwisho.
FEBIANI BABUYA.