SIMULIZI: JUMBA JEUSI

SIMULIZI: JUMBA JEUSI

STORY: JUMBA JEUSI
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
Storyteller: Bux the story teller
WhatsApp: 0621567672
Email: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UTANGULIZI.....
EPISODE 1.


BANZOKA
Pembezoni mwa barabara ndogo ya vumbi ambayo ilikuwa inaingia kwenye kichaka kilichokuwa kimemezwa na miti ya kutosha, mwanaume mmoja alikuwa akijikokota huku akiwa anavuja damu kwa wingi. Alikuwa anauburuza mguu wake ambao haukuwa kwenye hali nzuri kabisa, mguu wake ulikuwa una alama za kukatwa na makovu kadhaa ambayo hayakumfanya bwana huyo kuwa kwenye hali nzuri kiafya.
Hatua zake hazikuwa za kuridhisha kabisa kwa sababu alionekana kuwa mtu ambaye alitembea kwa muda mrefu bila kuwa na msaada. Alionyesha hofu usoni ambayo iliufanya hata moyo wake kwenda mbio kiasi cha kupiga mpaka kwenye kifua chake hata mtu ambaye angekuwa umbali kadhaa kutoka mahali ambapo alikuwepo basi angetambua kwamba bwana huyo alikuwa amemezwa na taharuki ambayo ilimnyima raha na amani kiasi cha kumpatia mawazo ya namna hiyo.

Sura yake haikuwa ikionekana vizuri huenda kwa sababu ya kiza ambacho kilikuwa kimelimeza lile eneo ukijumlisha na miti ambayo ilizungukia eneo hilo ndiyo kabisa ilizalisha kiza na kulifanya kuwa tulivu isipokuwa hatua za bwana huyo ambazo hazikuwa na umakini kwa sababu ya kukosa utaratibu maalumu kwani alikuwa akiumia. Kwa mwonekano wake wa mbali hakuwa mtu mwepesi, alionekana kuwa shupavu na shababi ambaye mwili wake ulikuwa umeshiba vilivyo kama sio kwa mazoezi makali basi bwana huyo alikuwa amezoea maisha magumu ama yale maisha ambayo hayana utulivu kabisa ndani yake.

Tafsiri ya maisha yake ilikuwa inakuja kwa namna alivyokuwa na hali ambayo alikuwa nayo kwa wakati huo, alikokuwa ametoka kwa nyakati hizo hakukuonekana kuwa na usalama wa kutosha ndiyo maana hali haikuwa inavutia kwa upande wake. Alisikika akiwa anahema kwa nguvu, ile sauti yenye kitetemeshi ndani yake mithili ya mtu ambaye alikuwa anautua mzigo mzito ambao aliubeba kwa muda mrefu kwenye mwili wake na moyo wake kwa ujumla. Mbalamwezi ilichanua nyakati hizo na kusababisha mwanga kwa mbali ambao ulifanya hata lile jasho lake kuchuruzika na kumpa nafasi ya kuona umbali mdogo ambao hata yeye mwenyewe hakuonyesha kama umbali huo ulikuwa unaenda kuwa na msaada kwa upande wake yeye.

Aligeuka nyuma mithili ya mtu ambaye alikuwa anahakiki jambo ama kuna kitu alikisahau huko ambako alitoka, aligundua kwamba hakukuwa na usalama wa kutosha kwani mwili wake haukuwa na utulivu, alikuwa anapata misisimko ambayo ilizidi kumpatia tahadhari juu ya eneo ambalo alikuwepo, mpaka wakati huo alitambua kabisa kwamba lilikuwa ni suala la muda tu kuweza kufikiwa mahali ambapo yeye alikuwepo. Mwili wake ulikuwa kama unashindana na nguvu zake za kutembea kwani alijihisi kama ana kizunguzungu kikali kwa nyakati hizo, kilikuja katikati ya hiyo safari yake na kwenye kumbukumbu za maisha yake hakuwahi kufikiria kama aliwahi kuwa na tatizo la namna hiyo kabla.

Alitikisa kichwa ili aweze kuwa sawa ila alihisi kama anaona nyota mbilimbili mbele yake, alishika kichwa huku akiwa anaguna kwa maumivu ambayo yalitosha kumfanya jicho lake kutoa chozi bila kupenda. Bwana huyo alijigeuza akiwa anazunguka hiyo sehemu na maumivu yake, hapo ndipo mwili wake ulionekana vyema. Upande wa ubavu mmoja ulikuwa na kisu ambacho kiligota hapo, kwenye mgongo wake kulikuwa na nondo fupi ambayo ilisalia kwenye huo mwili wake lakini pia upande wa nyuma wa shingo yake ulikuwa umetobolewa kidogo eneo ambalo lilikuwa linatoa damu taratibu. Mwili wake ulionekana kuchakaa vya kutosha kwa kipigo ukiacha upande wa mbele ambao alionekana aliulinda ipasavyo ndiyo maana ulionekana kuwa ngangali bado.

Bwana huyo ile hali ilionekana kabisa kumuelemea pale alipokuwepo, hakuweza kusimama tena kama mwanzo, aliyumba yumba na kujisogeza mpaka pembezoni eneo ambalo lilikuwa na mti mfupi na mnene. Alidondokea upande wa pili na kuegamia mti huo huku akiwa bado anahangaika na maumivu ya mwili, kichwa ambayo kwa pamoja yalikuwa yanashindana na mawazo yake.
“Zyra” alitamka jina ambalo lilionekana kuwa la kike kwa sauti yenye kitete lakini ambayo ilishiba vya kutosha, alilitamka neno hilo kwa sauti ndogo na nyepesi ila ule uzito wake ndio ambao uliifanya isikike kwa mbali. Haikueleweka sababu ya mtu huyo kuweza kulitaja jina hilo tena akiwa sehemu kama hiyo ambayo ilionekana kutokuwa salama kabisa kwa upande wake. Huenda lilikuwa ni jina ambalo ndiyo ilikuwa sababu ya yeye kuishia sehemu ama eneo hilo ama lilikuwa ni jina ambalo lilikuwa na maana kubwa kwenye maisha yake, kwa nyakati hizo ni yeye pekee ambaye alikuwa ana majibu ya sababu za kulitaja jina hilo eneo kama hiyo na wakati kama huo.

Aliketi kwa kuuegamia huo mti lakini akiwa anahangaika na maumivu makali ambayo yalimvaa huku akijua kabisa maisha yake yalikuwa kwenye hatari kubwa, akili yake ilimrudisha nyuma dakika kadhaa ambazo zilikuwa zimepita. Bwana huyo alikuwa anakimbia kwa spidi ambazo kama mtu ambaye alikuwa anamfukuza asingekuwa na kasi ya kutosha basi abadani asingempata kwenye maisha yake yote. Alionekana kukimbia ili kuiponya nafsi yake ambayo haikuwa na usalama wa kutosha kwa nyakati hizo, alitamani kama angekuwa anafukuzwa na mtu mmoja ama wawili lakini haikuwa hivyo, walikuwa ni wanaume wapatao sita ambao walikuwa wapo nyuma yake kula naye sahani moja.

Ile miondoko yake ambayo ilikuwa inakatisha tamaa kwa wakimbizaji, haikufua dafu kuweza kuwafanya wanaume hao kughairi safari ya kumpata bwana huyo. Akiwa anaendelea kukimbia ni kama mwili wake ulianza kuchoka mpaka akahisi ile hali haikuwa ya kawaida kwake, hakuwa mbovu namna ile kiasi kwamba kwa muda mfupi tu aweze kuwa na ule uchovu. Akiwa anaendelea kujiwazia huku akiwa anaendelea kuikata nyika ndipo alihisi hali isiyo ya kawaida, ni ile hali ya mvumo wa upepo, ni kama ilizidi kwa upande wake, alihisi kuja jambo zito nyuma yake hivyo alijivutia pembeni ambapo kulikuwa na mti. Kujivuta kwake kulimsaidia kuikwepa nondo moja ndefu kiasi na yenye makali ya kutosha ikaenda kukita kwenye mti mdogo ambao ulikuwa mbele yake kiasi kwamba nondo hiyo ilizama na kutokezea upande wa pili.

Kama ingefanikiwa kuingia kwenye mwili wake basi mpaka muda huo asingekuwa hai kwa namna yoyote ile. Alihema na kuendelea na safari yake kwani alikuwa ameshaanza kuvisikia vishindo vizito vikiwa vinakuja karibu na alipo tena wahusika wakionekana kuwa na usongo mkali na huyo bwana kama wangempata. Kila ambavyo alikuwa anajaribu kukimbia ndivyo ambavyo mwili wake ulizidi kuwa wa utofauti mpaka yeye mwenyewe akaanza kujitilia shaka na hizo harakati zake za kujiokoa. Kujiuliza uliza mara mbili mbili wakati ambao alitakiwa kuyapambania maisha yake kwanza likawa kosa lake la maisha ambalo kila dakika ilivyozidi kwenda mbele alianza kulijutia kwa maumivu makali.

Ule wakati ambao aliutumia kuwaza ni wakati ambao alikuwa amefikiwa, alichotwa kwa nguvu kubwa na kwa sababu hakuwa na balansi ya kutosha, bwana yule alibaki anaelea hewani huku akitoa sauti ile ya mshtuko wa kutoamini bado kama jambo hilo lilikuwa linamfika hizo nyakati eneo ambalo yeye mwenyewe alitambua kwamba hakuwa na msaada kutoka kwa mtu yeyote yule zaidi ya mikono yake na mbio zake tu pekee. Alitua kwa sarakasi nne ambazo zilimfanya kuyumba kwani hakutarajia, muda ambao alikuwa anaendelea kujipanga alihisi kama kuna kitu kimezama kwenye mwili wake hapo akaundua kwamba ni nondo fupi ilipita nyuma ya tumbo. Alipiga hesabu za kujivuta mbele zaidi ila huko ndiko kulioonekana kuwa na hatari kubwa zaidi ya nyuma.

Alikutana na mguu ambao ulitua kwenye shingo yake, ule mguu ulikuwa mithili ya mtu ambaye alikuwa anapiga mpira aina ya volley. Damu ilimtoka mdomoni bila kupenda huku akiwa anatokwa na jasho jingi na nondo ikiwa kwenye mwili wake. Alisogea pembeni akiwa anahema kama kuku ambaye aliwekwa kati kwa ajili ya kuliwa na wali, hapo ndipo akawaona hao mabwana ambao walikuwa wanayahitaji maisha yake kwa nyakati hizo. Walikuwa watatu, wawili mbele na mmoja nyuma, moyo wake ulipiga kite baada ya kugundua kwamba aliingizwa kwenye mtego mwingine uliohitaji muda wa kutosha kuweza kuutegua lakini kwa habati mbaya hata huo muda hakuwa nao. Aligundua kwamba wanaume hao walikuwa sita tangu mwanzo, sasa hao watatu walikuwa wapi? Haukuwa muda sahihi kwa yeye kuweza kulijibu hilo swali lake zaidi ya kuweza kuyapigania maisha yake.

“Ulitakiwa kulihama hili taifa wakati ambao ulikuwa na nafasi, unajua kabisa ambacho kimewatokea watangulizi wako ambao wamewahi kuwa kwenye hiyo nafasi yako lakini bado ukaleta jeuri. Maisha hayaendi hivyo ndugu yangu, ona sasa muda huu unaenda kufa tena kama mbwa bila msaada ndani ya kichaka kidogo kama hiki kisicho na sifa hata ya kuitwa msitu” alitamka bwana mmoja ambaye alikuwa amevaa nguo zilizokuwa nzito lakini kwa upande wake hata huo uzito haukuwepo kabisa, alikuwa anaongea na mtu aliyekuwa katikati yao akiwa hana mahali pakwenda. Walionekana kutambuana kwenye maisha mengine ambayo yalipita ila kwa wakati huo ni huyo mwanaume mmoja ambaye alitakiwa kuyapigania maisha yake kutoka kwa hao mabwana.

Hakuwapa nafasi ya kuwajibu maneno yake ya thamani kwani alijua kabisa kwamba hayakuwa na msaada wowote kwa upande wake. Alizikunja ngumi zake kwa ustadi na kuwanyooshea wanaume hao ambao walimfuata kwa pamoja pale kati. Alikimbilia mbele na kuinama akipiga goti ambapo alijilaza kabisa na kughala ghala huku akiwa makini ile nondo isizidi kuingia ndani kiasi kwamba wale mabwana wakapishana naye akaibukia upande wa pili, hakusimama, bali zilikuwa ni mbio ambazo zilitakiwa kumponya. Kwenye kukimbia kwake ndiko ambako kulimponza kwa sababu baada ya sekunde thalathini tu alirudi nyuma kwa hatua kama kumi baada ya kukutanishwa na kitu ambacho yeye alihisi ni kama nyundo nzito imetua kwenye kifua chake.

Ndiyo kwanza kabisa naifunua episode ya kwanza ya simulizi hii bora mno ya JUMBA JEUSI. Ni simulizi ambayo ina mengi ya kutupatia ndani yake, utaisoma siasa kwa undani zaidi na namna inavyofanya kazi hususani kwenye mataifa ya Afrika hivyo nakusihi ungana nami kuanzia mwanzo mpaka siku ambayo nitatua nukta ya mwisho na kusema nimeimaliza rasmi.

Nyuma ya kalamu ni mwandishi wako pendwa wa siku zote, FEBIANI BABUYA wao wanapenda kuniita Bux the storyteller.

Wasalaam.
Mimi masubiri ya jumba jeupe
 
STORY: JUMBA JEUSI
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

EPISODE 13.
ENDELEA.......

“Hayo yote yalifanyika mzee Magamba”
“Kama yalifanyika sasa kivipi huyu mtu bado haupo naye kwenye mikono yako?”
“Ndiyo maana nimewaambia hata mimi bado nafikiria kwamba ni kwa namna gani huyu mtu amefanikiwa kuishi mpaka wakati huu”
“Hili unalo lifanya ni utoto, kama hii kazi imekushinda tuachie sisi wenyewe tuifanye”
“Magamba” aliitwa na wenzake ili atulie lakini haikuonekana kufanya kazi njia ya kuweza kumtuliza.

“Hapana, lazima tuongee ukweli, huyu mtu kwetu ni hatari au niseme kwangu ni hatari kwa sababu nyie wote humu ndani hajui kuhusu uhusika wenu ila anajua kuhusu mimi, maana yake kama akipona mtu wake wa kwanza kumpigia hesabu ni mimi hapa na wala sio ninyi ndiyo maana naona hamjali lolote lile kuhusu hili kwa sababu mnajua mpo salama ila tambueni kwamba kama ikija kutokea siku hata moja akarudi kwangu basi nitawataja wote” mzee Magamba aliongea kwa jazba kali akionekana kabisa kuvurugwa. Wote walibaki wamemkodolea macho kwani alikiri wazi kwamba yupo tayari kuwasaliti wenzake.

“Wote nendeni makwenu, nitawaita tena nikiwahitaji” mheshimiwa alionekana kuchukizwa na zile kauli za mzee Magamba, walinyanyuka wote na kutoka lakini Eusebius alibakia hapo ambapo alisogelea kiti ambacho alikuwa ameketi raisi.
“Mheshimiwa vipi kama haya ambayo ameyasema hapa atayafanya kweli?”
“Ndiyo maana nina mpango wa kumuua pindi tu nikipata habari kwamba Bazoka amerudi ikitokea sijampata na kumuua huko aliko kwa sasa”
“Una uhakika na hili?”
“Nenda nyumbani Eusebius” hakuwa na namna zaidi ya kujizoa na kuondoka kwa sababu ilikuwa ni amri ya mkuu wa nchi.




***********
MWALIMU NYERERE MEMORIAL ACADEMY
Moja kati ya vyuo vya muda mrefu, chuo ambacho kimepewa jina la muasisi wa taifa la Tanzania Mwl. Nyerere. Kipo maeneo ya Kigamboni kikiwa kimegusana na bahari ya Hindi hivyo kukifanya kuwa eneo zuri kwa ajili ya kuweza kujisomea ama kupata utulivu wa akili.


Professor Gerald
Ndani ya chuo hicho, kulikuwa na profesa ambaye alikuwa maarufu mno, ukongwe wake na utendaji wake kazi ambao ulikuwa bora zaidi ya wengi ndio ambao ulimpatia jina kubwa na kumfanya kujulikana kila kona. Mbali na hilo na namna alivyokuwa bingwa wa kuweza kuyawasilisha mawazo yake kwa njia ambayo ni rahisi na kila mmoja akaelewa hali ambayo ilifanya darasa lake kuwa na ufaulu wa hali ya juu tofauti na madarasa mengine ambayo yalikuwa yakihadhiriwa na wakufunzi wengine, pia utulivu wake ulikuwa sehemu ya mhimu kwenye maisha ya watu wengine.

Majira ya saa mbili jioni alikuwa kwenye mhadhara akiwa anatoa elimu kuhusu rasilimali watu, ulikuwa ni uwanja wake wa nyumbani hivyo alikuwa akiwakumbusha vijana wake kuhusu umuhimu wa rasilimali watu kwenye maendeleo ya kampuni, jamii lakini hata taifa kwa ujumla. Rasilimali watu zilikuwa ni nguzo ya mhimu kwa sababu ili kila kitu kiende vizuri ni lazima kuwa na watu nyuma yake ambao wanayafanya mambo kwa weledi kuhakikisha wanapata matokeo ambayo ni chanya. Alikuwa anasisitiza namna ya watu kuutumia uwezo wao wote waliokuwa nao kuhakikisha wanafanikisha kutimiza malengo ambayo yanakuwa yapo mbele yao tena kwa ufanisi wa hali ya juu.

Profesa huyo alikuwa akipenda zaidi kufundisha majira ya usiku ambapo aliamini kwamba akili ilikuwa inapata utulivu wa kutosha ndiyo maana mihadhara yake mingi ilikuwa muda huo ila hilo lilikuja baada ya yeye kutoka kwenye likizo ya miezi miwili na kurudi. Mara ya kwanza kabla ya kwenda kwenye hiyo likizo yake, hakuwa mtu wa namna hiyo ila hayo mabadiliko yalikuja baadae tu. Wakati anaondoka, alikuwa mtu wa kawaida, mrefu kidogo na mwembamba kiasi lakini wakati anarudi alikuwa tofauti, mwili ulikuwa umenona na kumfanya kutuna kidogo na ndipo hapo ambapo alikuja na hayo mabadiliko.

Akiwa anaendelea na mhadhara wake ambapo darasa lilitulia vyema, ulisikika mlio wa risasi kwenye venue nyingine ambayo ilikuwa umbali wa mita ishirini kutoka hapo. Ule mlio ulileta raharuki kwani kila mtu alianza kugeuka kila upande ili kujua kulikuwa na tukio gani lakini kabla hawajakaa sawa tena kwa mara nyingine ulisikika mlio mwingine wa risasi ambapo wanafunzi hawakusubiri tena. Kuna ambao walitembea juu ya meza, kuna ambapo waliwasukuma wenzao na kuna ambao walisukumana ili kila mtu awahi kutoka na kuweza kukimbia kutoka eneo hilo. Hakuwa na nguvu ya kuweza kuwazuia hivyo aliwapisha waweze kuondoka na kukimbia watakako wao.

Kwenye ile venue ambako ndiko zilisikika risasi, kulikuwa na wanafunzi wengi ambao walikuwa wanajisomea kivyao tu, kuna ambao walikuwa wamejigawa kwenye makundi makundi na kuna ambao walikuwa wapo wenyewe tu bila msaada wa watu wengine. Wakiwa wanaendelea na mambo yao hali ambayo ilifanya kelele ziwepo ndipo aliingia mwanaume mmoja na mwanamke mmoja ambao walikuwa wamevalia mavazi ya kawaida tu, wawili wale waliangaza kila upande wakionekana kabisa kwamba walikuwa wakimtafuta mtu kama sio watu kadhaa.

Kwenye kona moja walikuwa wamekaa vijana wawili wa umri wa kawaida, kijana wa kwanza alikuwa wa kiume ambaye alikuwa na simu mkononi lakini kijana wa pili alikuwa ni wa kike. Watu wale wawili walisogelea mpaka kwenye ile kona na baada ya kufika, yule mwanamke aliitoa simu yake mfukoni akaisogeza kwenye uso wa kijana yule wa kike, alimwangalia mwenzake baada ya kuscan na sura ile ikasoma mpaka 100%, bila shaka mtu ambaye walikuwa wakimtafuta alikuwa ni yeye mwenyewe. Wale vijana wawili walibaki wamehamaki wasijue wale watu walikuwa pale kwa sababu zipi na walikuwa wakifanya nini.

Wakiwa wanaendelea kuhamaki, yule mwanamke alitoa bastola kwenye mkono wake na kutamka kwa nguvu
“Out” wakati anatamka hivyo, alipiga risasi moja hewani, risasi ambayo ilileta msisimko mle ndani na kuleta taharuki kubwa. Hakuna ambaye alisimama, kila mtu alianza kutoka nje kwa kasi ya ajabu na wakati ambao kelele zilianza kusikika ni wakati ambao alipiga risasi ya pili ila kwa sasa ile risasi haikuwa hewani tena bali ilienda kwa yule kijana wa kiume ambaye alikaa na yule binti. Risasi ilitua kwenye paji la uso na kumfanya afariki pale pale, yule kijana wa kike ni kama alikuwa amepigwa na ganzi nzito ila ndani ya sekunde kadhaa alianza kupiga yote lakini hakupewa hiyo nafasi kwa sababu yule mwanaume alimpiga na ngumi nzito shingoni akapoteza fahamu pale pale. Alimbeba begani na kuanza kutoka naye kuelekea upande wa bahari lakini wakati hayo yanatokea, kuna mwanamke aliwaona. Hakuonekana kuwa mgeni wa yale maeneo, hata yeye alionekana kuwa mmoja wa wanafunzi wa pale pale ila utofauti wake ni kwamba yeye hakuwa na uoga wa namna yoyote ile bali alianza kuwafuata watu wale wawili.

Profesa Gerald baada ya kuona wanafunzi wake wote wametoka na kila mmoja kutawanyika kuelekea akujuapo, aliitoa miwani yake akiwa hana wasiwasi kabisa kwenye uso wake. Aliangalia nje na kutabasamu, alijigusa kwenye shingo yake na kuitoa ile sura ya bandia ambayo ilikuwa kwenye uso wake. Hakuwa yule profesa Gerald ambaye wengi walikuwa wamemzoea tangu mwanzo, alikuwa ni kijana tena shupavu mwenye afya yake japo haikujulikana sababu za yeye kuwa kwenye hiyo venue na kuvaa sura ya mtu mwingine. Alitoka humo ndani na kuanza kuelekea mahali ambako kulikuwa na ofisi ambayo yeye alihitaji kuifikia na kuingia.

Akiwa anatembea nyakati hiyo, alipishana na walinzi ambao walikuwa wanakimbilia lile eneo ambalo mlio wa risasi ulisikika lakini mlinzi mmoja alishtuka na kugeuka, alimtaka bwana huyo asimame hali ambayo iliwashtua hata wenzake nao wakaamua kusimama na kumsogelea mtu huyo ambaye alikuwa amegeukia upande mwingine. Alimshtukia kwa sababu sura yake ilikuwa ngeni, wao walikuwa walinzi hapo, kama kungekuwa na sura mpya au ambayo wameizoea basi wangeitambua hivyo kuona sura ngeni majira ya usiku na hali ambayo ilikuwa inaendelea hapo ndiyo ambayo ilimpa wasiwasi na mashaka hivyo akataka kumjua bwana huyo.
Hizo harakati zake ndizo ambazo zilimponza yeye na wenzake, haukuwa wakati mwema kwake kuweza kufuatilia maisha ya watu wengine nyakati kama hizo

“Wewe ni nani na unatafuta nini hapa?” aliuliza kwa sauti yenye ukali akiwa anahitaji kuonekana kwamba alikuwa na mamlaka hayo ya kuweza kuuliza swali kama hilo lakini hakujibiwa. Aliona kama anadharauliwa ndipo akainyoosha silaha yake kumsogelea zaidi huyo bwana ila kusogea karibu zaidi mehesabu yake yalikuwa ya hovyo kwani kijana huyo aligeuka kwa kurudi nyuma kidogo na kuidaka silaha hiyo ambayo aliivutia kwake na kuidaka yeye kisha akaigeuzia kwa mlinzi yule na kumsokomezea nayo kwenye shingo yake. Ilikuwa ni ghafla wenzake walishtuka wakati mwenzao anaenda chini.

Episode ya 13 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: JUMBA JEUSI
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

EPISODE 14.
ENDELEA.......

Alitembea kama ananyata na kushika tumbo la mmoja wa wale wawili ambalo alilitoboa kwa vidole vyake kisha akaivuta shingo ya mwanaume huyo ambaye alikuwa anafurukuta na kuivunja mara moja. Baada ya kukamilisha hilo yule mwingine alikuwa anaikoki silaha yake ila muda wake haukuwa rafiki kihivyo kwahiyo wakati anakaa sawa alikutana na ngumi ambayo ilitua kwenye sehemu yake ya moyo, alibaki anahangaika akiwa anazunguka huku na huko na wakati huo yule kijana ambaye alikuwa ameuvaa uhusika wa profesa Gerald aliendelea na safari yake kwani alikuwa na uhakika kwamba bwana yule asingeweza kupona kwa ile ngumi yake. Alifika kwenye ile ofisi ambapo nje alikutana na walinzi wawili ambao walimtaka ageuze kwani nyakati zile hawakuwa wakiruhusu mgeni yeyote lakini wakati wanafanya hayo mazungumzo walikuwa karibu naye hali ambayo ilimfanya kuwaua wote wawili kwa bastola ambayo ilikuwa kwenye mkono wake alio uweka nyuma. Kwenye ile ofisi alikuwa amefuata mkanda wa video za marejeo ambazo alijua zingekuja kutumika kama ushahidi kwa baadae na baada ya kukamilisha jambo hilo alitoweka kuelekea kule ambako wale watekaji walikuwa wameenda.

Ule upande wa pili wale watu wawili walikuwa kwenye mwendo wa haraka kidogo kuelekea ile sehemu ambapo walionekana kabisa kwamba hawakuhitaji kupoteza muda wao. Hawakuwa wakijua kwamba nyuma yao kulikuwa na mtu ambaye anawafuata tena akiwa ni mwanamke, walitembea kwa muda kidogo mpaka wakafika ufukweni mwa bahari, taa zilikuwa zinalimulika jiji la Mzizima huku baharini kukiendelea na harakati zingine hususani za wavuvi ambao ndio kwanza walikuwa wanajiandaa lakini upande mwingine watu walikuwa wanaendelea kuvuka kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine.

Pembezoni mwa hilo eneo ambalo walifikia kulikuwa na boti moja ndogo binafsi, boti ambao ilionekana kuwa yao na ilikuwa ikiwasubiri ni wao tu. Mwanaume yule alimrushia yule binti kwenye boti kisha akapanda lakini kabla hajawasha alisikia sauti ikiwataka watulie kama walivyokuwa, ni yule mwanamke ambaye alikuwa anawafuatilia ndiye ambaye aliwataka watu wale watulie kama walinvyo, hali hiyo ilimfanya yule mrembo kugeuka ili kumjua mtu ambaye alikuwa amekuja hapo kuwapotezea muda. Ni binti ambaye hakuwa akimfahamu kabisa huenda kwa sababu hawakuwahi kuonana kabla.
“Unaitwa nani bibie?”
“Sipo hapa kufahamiana na wewe, mrudishe huyo binti mara moja”
“Hilo ndilo limekuleta hapa?” aliongea mwanamke huyo akiwa anamsogelea kwa sababu hawakuwa mbali na mahali ambapo walikuwa wamesimama.

Yule mwanamke ambaye alikuwa amefika eneo lile kuweza kuwazuia kuondoka na yule binti ambaye walimbeba chuo, akiwa anaendelea kutafakari jambo la kufanya aliona mchanga ukija upande wake wa uso hapo ndipo akagundua kwamba yule mrembo aliubeba kwenye fukwe ya bahari na kutaka kumpinga changa la macho. Aliyafumba macho yake ili usije ukamuingia, alihisi kitu kinamuwasha kwenye tumbo lake hivyo akafumbua macho haraka na kugundua kwamba alikuwa amepigwa na kiatu kirefu kwenye tumbo. Alipata ghadhabu na kuhitaji kurudisha hayo mapigo lakini hakuwa amejipanga vizuri bado, hivyo akajikuta anaguswa kwenye mkono wake japo hakuiachilia ile bastola yake.

Aligeuka nyuma na kumkosa yule mrembo, akaruka sarakasi ya nyuma kwa mkono mmoja na kuchana msamba wa hewani ambao ulitua kwenye kichwa cha yule mrembo ambaye alirudi nyuma hatua kadhaa akiwa anatoa sauti ya miguno kwa sababu hakuonekana kabisa kuwa levo yake. Hakumpa nafasi ya kupumua, alimtishia na ile bastola akainama, alizunguka na teke la nyuma ambalo lilimgusa kwenye kidevu mrembo yule wakati ambao mwenzake kwenye boti alikuwa ameiwasha boti na kumuita ili waondoke haraka kwani maeneo kama hayo hayakuwa rafiki kutumia bastola, askari hawakuwa mbali kutokana na kwamba bandari haikuwa mbali lakini hiyo nafasi hakupewa kabisa.

Alijitahidi kukumbana na huyo mwanamke ila alionekana kuwa zaidi yake, alipigwa ngumi tano za uso akawa anaona giza, alipokuja kukaa sawa alipigwa mtama na kukutanishwa na teke la uso kikatili. Mwanamke ambaye alikuwa anazuia tukio hilo alikuwa anahesabu hatua kumsogelea yule mrembo lakini kabla hajafanya jambo lolote alihisi ubaridi kwenye shingo yake ndipo akagundua kwamba kulikuwa na mtu mwingine nyuma ambaye yeye hakumuona.
“Usije ukafanya jambo lolote la kipuuzi kwa sababu sitahesabu hata moja nafyatua hii risasi” aliongea mwanaume huyo akijitokeza upande wa mbele na kumtaka mwanamke huyo aweze kumpatia ile bastola ambayo alikuwa nayo kwenye mkono wake. Alimpatia bwana huyo huku akiwa na mshangao mkubwa, alionekana kutomjua lakini mavazi yake hayakuwa mageni kwake.

“Profesa Gerald?” aliita kwa mshangao akiwa bado kama haamini.
“Huyo mtu amekufa muda mrefu kidogo ila hakuna anaye litambua hilo bibie”
“Who are you?”
“Ni mapema kuweza kunifahamu mimi ndiyo maana kwa leo sitaki kukuua Jessica, utafika wakati ambao mimi na wewe tutahitajika kujuana na ndio wakati ambao tutafahamiana na nitaona kama nitakupa nafasi nyingine ya kuweza kuishi”
“Umelifahamu vipi jina langu?”

“Sio kazi kubwa kwangu kumfahamu jasusi wa aina yako ambaye anaigiza kuwa mwanafunzi kwenye chuo kama hiki ila jambo moja ambalo sikufanikiwa kulifahamu kwako ni sababu ambayo ilikuleta hii sehemu. Sio mbaya kwa leo nakupa hii nafasi ya kutoka ukiwa hai ila wakati mwingine tutaona” wakati naongea hayo bwana huyo na kumshangaza mwanamke huyo ambaye yeye alimtambua kama Jessica, aliirusha shilingi moja kwa nguvu kubwa mno na kwa sababu yule mwanamke alikuwa amehamaki wakati anaambiwa hayo mambo alijikuta anairuhusu inatua kwenye shingo yake bila kuwa na uwezo wa kuizuia. Alidondoka na kupoteza fahamu wakati watu hao watatu wakiingia kwenye hiyo boti na kuweza kutoweka hilo eneo.

Jessica alishtuka baada ya dakika kumi kupita, shingo yake ilikuwa inauma mno hivyo ikamlazimu kuanza kujinyoosha ili akae sawa. Ni sekunde kumi tu zilipita mpaka alipoweza kukumbuka tukio ambalo lilikuwa limetokea, alijikuta anakurupuka na kushtuka wakati akianza kujikagua, alitambua kwamba bastola yake ilikuwa ipo kando yake lakini wale watu hawakuwepo hilo eneo. Alijaribu kuangaza kila upande lakini hakuona mtu hapo ndipo akatambua kwamba alikuwa amewapoteza watu wake japo kichwani alikuwa na maswali mengi ambayo majibu yake kwake yalikuwa ni magumu kuweza kuyapata akiwa mwenyewe. Yule mtu hakuwa Profesa maana yake ni yeye alimuua kisha akauvaa uhusika wake, kwa sababu zipi hasa mpaka alifanya yale yote? Ni kwa sababu ya yule binti ambaye alitekwa? Kwani yule binti alikuwa ni nani mpaka awe na umuhimu mkubwa kwao kiasi kile mpaka kuyatoa sadaka maisha ya mtu kama profesa Gerald? Hakuwa na uhakika na nadharia zake ila alianza kuyaunganisha hayo matukio lakini jibu la moja kwa moja halikuja upande wake.

Akaendelea kujiwazia tena, yule bwana alionekana kumfahamu yeye vyema mpaka akamtaja jina lake na kazi yake ya siri ambayo alikuwa anaifanya, alijuaje kuhusu kazi yake na jina lake? Kwamba naye alikuwa anafanya kazi kama yake? Hapana, lilikuwa ni jibu la haraka kwa sababu mtu wa kazi yake asingeweza kuteka mtu tena mwanafunzi namna ile pamoja na kusababisha hatari kwenye halaiki hivyo akatambua kwamba yule hakuwa mwenzake, sasa alikuwa nani? Kilikuwa kitendawili kingine kigumu. Jambo lingine ambalo lilimshangaza ni bwana yule kuweza kumuacha hai wakati alikuwa na nafasi ya kuweza kuyabeba maisha yake, aliwaza ni sababu zipi za msingi ambazo zimemfanya yule bwana ampe nafasi nyingine ya kuishi? Aligundua kwamba kwa muda ambao alikuwa nao haukuwa rafiki kuweza kumpatia majibu sahihi ya jambo ambalo alikuwa analifanya ndipo akakumbuka kwamba alitakiwa kurudi tena mazingira ya ndani ya chuo kujua kilichokuwa kikiendelea hususani baada ya kusikia mlio wa gari za polisi zikiwa zinaingia hilo eneo.

Baada ya kurudi tena ndipo aliduwaa, aliduwaa baada ya kusikia kwamba kuna watu sita walikuwa wameuawa, alitambua kabisa kwamba wale watekaji wawili waliua mtu mmoja tu pekee sasa hao wengine watano waliuawa na nani? Ndipo akamkumbuka yule bwana ambaye alikuwa kwenye mavazi ya profesa Gerald, yeye ndiye ambaye alibaki nyuma na bila shaka kulikuwa na muunganiko wa mauaji ya watu hao na yeye kwenda kubeba video za merejeo ili asiache ushahidi wowote nyuma. Uchunguzi ndani ya eneo hilo ulianza mara moja ukiwa unaongozwa na afisa wa polisi Jerry zopa.

Jessica alikuwa pembeni akiwa anawaangalia namna polisi walivyokuwa wanapambana na ile kesi, kwa wakati huo hakutaka kujiingiza moja kwa moja bila kuwa na uhakika na watu ambao walikuwa wanashughulika na jambo lile ndiyo sababu iliyo mfanya kukaa kando kwanza kuweza kuyasoma mazingira na mambo yote ambayo yalikuwa yanaendelea lile eneo.

Episode 14 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: JUMBA JEUSI
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

EPISODE 15.
ENDELEA.......


“Haya mauaji ni kwa mara ya kwanza kuyashuhudia kwenye vyuo vya hapa nyumbani, sijawahi kuona kabla likitokea jambo kama hili hususani la utekaji tangu taifa letu liweze kupata uhuru” aliongea askari mmoja ambaye alikuwa anaufunika mwili wa mlinzi aliyekuwa ametobolewa tumbo.
“Kwangu hainishangazi kutokea hivi kwani kama haijawahi kutokea basi lilikuwa ni suala la muda tu kabla na sisi hatujapitia kwenye nyakati kama hizi, kwangu jambo ambalo linanisumbua ni kwamba kwanini itokee hivi?” aliongea afisa wa polisi Jerry Zopa akiwa makini kuangalia shingo ya yule mlinzi ambaye alisokomezewa silaha eneo hilo na kumfanya kufa vibaya.
“Lengo hasa la hawa watu lilikuwa ni lipi?”

“Tito hilo jibu tungelipata kwa uharaka zaidi kama tungefanikiwa kupata kamera za marejeo hapa lakini kwa bahati mbaya ni kwamba mkanda wake umeibiwa na kamera mfumo wake umeharibiwa hivyo kwa yeyote ambaye amehusika na hili alikuwa anajua kile ambacho alikuwa anakifanya”
“Kama ni hivyo, maana yake ni tukio ambalo liliandaliwa kwa muda mrefu na sio kwa bahati mbaya, hawezi mtu kuja kiholela bila kujua utaratibu wa hapa ulivyo akafanya tukio kama hilo na kufanikiwa kuondoka bila kuweza kujulikana ama kupatikana”
“Maana yako ni ipi Tito?”

“Namaanisha kwamba kama tunahitaji kweli kuweza kumpata mhusika wa tukio hili tunatakiwa kuijua sababu ya msingi ya yeye au wao kufanya hivi na ili kuweza kulitambua hilo tunatakiwa kujua maisha ya binti ambaye ametekwa kabla ya hawa watu kuja. Mpaka wanaua watu wengi namna hii maana yake ni kwamba huyo binti alikuwa ni mhimu zaidi kwao na huenda ni mhimu akiwa hai ndiyo maana hawajamuua hapa hapa. Kama tukifanikiwa kutimiza hilo basi bila shaka nina imani kabisa kwamba tutawapata wahusika wa hili jambo ama hata kupata kitu kama mwanzo wa kuujua ukweli” Tito maelezo yake yalikuwa yameshiba na yalionekana kumshawishi Jerry japo jambo moja lilikuwa linausumbua ubongo wake bado.

“Upo sahihi Tito lakini kuna jambo moja ambalo linanishangaza hapa, ni kwanini haya matukio yote yaanze kutokea baada tu ya raisi aliyekuwa madarakani kuuawa na huyu mpya ndo kwanza anaingia Ikulu?”
“Huenda haya yote yana uhusiano wa moja kwa moja”
“Ina maana tunaweza kujikuta tunaichunguza ofisi kuu ya nchi?” Jerry aliuliza swali ambalo alilijua jibu lake na ndiyo sababu ambayo ilifanya wawili hao waishie kuangaliana tu kila mtu akiwa anawaza yake moyoni.
“Kwa maana hiyo ni kwamba hatuwezi kufika popote kwenye hili” aliongea Tito akionekana kama ni mtu ambaye amekata tamaa.

“Hapana, lazima tuujue ukweli ambao upo ndani yake na kama kweli Ikulu itakuwa inahusika lazima tuujue ukweli kwamba ni kwanini wafanye haya? Huyu binti anahusiana nini na Ikulu mpaka kutekwa kwake kusababishe mauaji?” wote walikubaliana kwa pamoja, hilo jambo walitakiwa kulifanyia kazi haraka iwezekanavyo na ili kuweza kufanikisha hilo walitakiwa kwanza kuipata historia ya maisha ya yule binti aliyekuwa ametekwa kwani ndiye alionekana kuwa sababu ya matatizo yote kutokea ndani ya hicho chuo. Wawili hao walianza kuondoka hapo ili waelekee kwenye ile venue ambayo kijana aliyekuwa na yule binti aliuliwa lengo likiwa ni kukusanya ushahidi wa pamoja ili kuweza kupata mwafaka wa hiyo kesi yao ambayo walikuwa wameivamia. Lakini wakati anaanza kuelekea huko, Jerry alishtuka, kwa sababu aliona kuna sura mpya kwake ambayo haikuwa maeneo ya mbali kutoka hapo ambapo walisimama na bila shaka mtu ambaye alikuwa aneo lile, alikuwa akiwasikia wakati wanaongea.

Alikuwa ni mwanamke mgeni kwake, lile eneo lilikuwa limewekwa kizuizi kiasi kwamba hakuna mtu wa kawaida ambaye alikuwa anaruhusiwa kuwepo sasa alishangaa kumuona mwanamke huyo akiwa hilo eneo na ndiyo sababu ambayo ilimvutia yeye kusogelea hapo ili aweze kutambua kwamba mwanamke huyo alikuwa ana shughuli ipi yale maeneo.
“Tunafahamiana kabla?” aliongea kwa sauti yake nzito kidogo ambayo iliambatana na vitisho huku akiiwasha sigara yake na kuivuta kwa mbwembwe.
“Haina umuhimu wa mimi kujibizana maswali hayo na mtu kama wewe”
“Unajua unaongea na nani?”
“Umevaa gwanda lako ambalo linaonyesha wewe ni nani, una haja ipi ya kuniuliza swali la kipuuzi namna hiyo?” majibu ya yule mwanamke kidogo yalimfanya ahamaki na kutuliza akili. Raia wa kawaida asingekuwa na ujasiri wa kumjibu namna ile lazima kulikuwa na jambo lingine ambalo tayari moyo wake ulikuwa umeanza kuhisi.
“Unatafuta nini hapa?” aliuliza akiwa siriasi kidogo
“Nataka nione jinsi mnavyo ipeleka hii kesi”
“Umetumwa kutoka Ikulu?”

“Kama ningekuwa nimetoka huko mpaka wakati huu ningekuwa nimewafukuza kwenye hii kesi”
“Kwahiyo wewe ni nani?”
“Hatuna haja ya kutambuana ila mpo mbali na ukweli kwa sababu hamjui lolote na kwa maelezo yenu ambayo nimeyasikia hata mkipewa mwaka mzima hakuna kitu mtakipata kwenye hiyo kesi yenu”
“Maana yako ni ipi?”
“Namjua binti ambaye ametekwa ila siwajui watu ambao wamemteka”
“Whaaaaaat?”
“Yeah, kwa sababu nimeshindwa kumsaidia”
“Kwamba umewaona hao watekaji?”
“Ndiyo, sio kuwaona tu bali nimekutana nao”
“Kivipi?”
“Mtu ambaye alikuwa anasimamia hili zoezi ni yule ambaye wengi walikuwa wanahisi ni Profesa Gerald”
“Baso sijakuelewa, profesa anaingiaje hapa?”
“Kwa sababu mtu ambaye amehusika kumteka yule binti ndiye aliigiza kuwa profesa”
“Kama aliigiza kuwa profesa na profesa mwenyewe yuko wapi?”
“Alishakufa”

“Profesa ni mzima wa afya na kwa taarifa za awali ni kwamba alikuwa anafundisha hapa siku ya leo hivyo nadhani wewe ndiye ambaye unatakiwa kuzitafuta taarifa sahihi kabla ya kuja kuropoka kwa kuuficha uhalisia wako”
“Nisikilize vizuri, majivuno na kiburi kwenye hii kazi hayatakusaidia lolote, mimi nipo tofauti na wewe kwa sababu huwa sishirikishi hisia zangu kwenye kufanya maamuzi. Huyu mtu amemuua profesa miezi miwili ambayo imepita kwa sababu alikuwa anaitafuta nafasi yake na kwa sababu profesa alikuwa likizo ndefu basi aliutumia muda huo kuweza kumuiga kwa kila kitu. Kwa maana hiyo ni kwamba ambaye alirudi hapa chuoni sio profesa bali ni huyo muuaji na wenzake”

“Hilo jambo haliingii akilini kabisa, hata tukisema ni yeye kama alitaka kumteka huyo binti kulikuwa na namna nyingi za kuweza kufanya sasa kwanini ahatarishe mambo yote hayo kwa ajili ya kumteka mtu mmoja tena mwanamke?”
“Kwa sababu alikuwa hamjui”
“Unataka kusema kwamba alikuja kufundisha hapa kwa sababu tu ya kutaka kumjua huyo binti ili amteke?”
“Nadhani umejijibu mwenyewe”
“Huyu binti ni nani mpaka awe na umuhimu kiasi hicho?”
“Hiyo ni kazi yako wewe kuweza kutafuta majibu ya hilo swali Jerry”
“Umelitambua vipi jina langu?”
“Wewe ni afisa wa polisi ambaye unapenda umaarufu hapa mjini, sasa kama unapenda umaarufu inawezekana vipi jina lako lisitambulike?”
“Na wewe umeyajuaje haya yote?”
“Kwa sababu nilitakiwa kumpata huyu binti kabla yao”
“Unamaanisha kwamba na wewe ulikuwa haumfahamu?”
“Ndiyo”
“Hili linawezekanaje?”
“Sina jibu la kukupa kwa wakati huu”
“Na kama ungempata?”
“Nilitakiwa kumlinda kwa maisha yangu yote”
“Inamaanisha kwamba unamfahamu huyu mwanamke”
“Nayafahamu maisha yake kidogo ila yeye sikuwa namfahamu bado”
“Ina maana wewe ndiye ulipaswa kuwa mlinzi wake?”
“Ndiyo”
“Hiyo kazi ulipewa na nani?”

Episode 15 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: JUMBA JEUSI
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

EPISODE 16.
ENDELEA.......

“Kafanye uchunguzi wako Jerry” Jessica baada ya kumpa taarifa za kushangaza afisa huyo wa polisi, alianza kutoweka kwenye lile eneo lakini alisikia bastola ikikokiwa taratibu hivyo akageuka.
“Huwezi kuondoka hapa mpaka nijue wewe ni nani na unipatie taarifa zote ambazo unazo kisha baada ya hapo ndipo nitafanya maamuzi kama unastahili kukamatwa au uendelee kutamba na porojo zako hapa” mwanamke huyo hakumkopesha yule afisa, alijongea mpaka pale ambapo alikuwepo bila hofu na uoga wowote ule.

“Kama kwenye maisha yako utakuja kuninyooshea hii bastola yako tena au hata kutishia basi nitakuua dakika hiyo hiyo bwana mdogo. Kupewa hiyo nafasi yako usije ukajiona kwamba unaweza kufanya lolote na mahali popote ambapo unapahitaji wewe. Kwa leo kwa sababu haunifahamu bado, nitahesabia kwamba ni kosa la bahati mbaya ila ukija kurudia kwa mara nyingine tena? Sitakuwa na hii huruma kama ya leo” aliongea kwa sauti ile ya taratibu lakini yenye ujumbe wa kutosha, wakati Jerry akiwa ametahamaki na vitisho vya mwanamke mrembo wa kuvutia ambaye alikuwa mbele yake, alijikuta anaipoteza bastola yake mkononi baada ya kuvutwa kwa nguvu na mwanamke yule kisha akazitoa risasi zote kwa nguvu ya ajabu na kuzimwaga zote chini, alimkabidhi bastola yake na kuanza kuondoka hilo eneo. Jerry alibaki ametulia huku moshi wa sigara ukiwa unapuliza taratibu bila shida, hakuelewa yule mwanamke alikuwa ni nani na kwanini aligoma kujitambulisha ila jambo moja ambalo alikuwa na uhakika nalo ni kwamba yule mwanamke hakuwa mwenye utani, alionekana kutoka sehemu ya juu zaidi yake ndiyo maana hakuwa na hofu naye kabisa licha ya kukijua cheo chake.


JESSICA
Pembezoni mwa Bahari eneo la Osterbay, kwenye apartment moja kubwa na nzuri ya kuvutia ambayo ilikuwa umbali kidogo kutoka ilipo bahari ya Hindi ndimo ambamo alikuwa anaishi mwanamke mrembo Jessica. Mrembo huyo wa miaka thelathini na sita alikuwa uchi kabisa bila nguo hata moja kwenye mwili wake, alikuwa ameshika cigar kwenye mkono wake huku akiwa amekikaribia kioo ambacho kilikuwa kinaonyesha mandhari nzuri ya bahari.

Wakati anaendelea kufanya hayo yote, alikuwa anaendelea kutoa sauti ambazo zilionyesha kwamba alikuwa anazifurahia nyakati zake ambazo zilikuwa bora. Mwanamke huyo alionekana kuzama kwenye dunia ya maraha, dunia ambayo ilikuwa inazikuna hisia zake kwa sababu upande wa nyuma kulikuwa na kijana mmoja wa kawaida ambaye alionekana aliyapenda mazoezi. Kijana huyo alikuwa akimpa huduma mwanamke huyo na kuhakikisha ababurudika vya kutosha. Kijana huyo alikuwa amemuinamisha mwanamke huyo kwa kumpa mhogo wake wa Jang’ombe kwa namna ambayo ilionekana kwamba alikuwa anatumia uwezo wake wote ili asije kuonekana haiwezi kazi.

Zoezi lao lilienda kwa saa zima mpaka pale wote walipofika ndipo mrembo huyo alipo sogea kwenye kabati ndogo huku sehemu zake za nyuma akiwa anazitingisha kiasi kwamba zikaanza kumtamanisha upya yule kijana ambaye mhogo wake ulianza kuvimba tena lakini muda haukuwa wake kabisa. Mrembo yule aliifungua ile kabati na kutoa dola kadhaa ambazo alimrushia kijana yule ambaye wakati huo alikuwa amesimama akisubiri tena kuweza kumsulubisha mrembo huyo lakini alimpa ishara aondoke kwani hakumtaka tena ndani mwake kwa sababu alikuwa ameshatimiza lengo ambalo yeye alikuwa analitaka.
Mwanamke huyo ilikuwa kawaida yake kuweza kuwanunua vijana kuweza kutimiza shida zake za ngono pale ambapo angewahitaji ndiyo maana hata muda huo alikuwa na huyo kijana ambaye alikuwa amemlipa ili amshughulikie. Hakuwa na muda wa kuwa na mwanaume mmoja kutokana na majukumu yake wala uwezo wa kuwa na familia, kwake lilikuwa jambo gumu mno hivyo hayo ndiyo yalikuwa maisha yake na kutokana na kwamba jiji lilikuwa na vijana wengi ambao hawakuwa na kazi lakini walikuwa wanapenda maisha mazuri haikumpa ugumu kuwapata.

Baada ya kijana huyo kuweza kuondoka, alibaki mwenyewe akiwa anatafakari mambo mengi kwenye ubongo wake ambapo mengi hakuelewa angeweza kuanzia wapi kuyatatua. Alitoa mpaka kweye balkoni akiwa bado yupo uchi kabisa kwenye mwili wake, mwili ambao ulikuwa una mvuto mkali mno, hakuna mwanaume angeweza kuutazama halafu mate yasimtoke labda kama hakuwa mwanaume kamili bali mwanaume jina tu. Aliutoa moshi taratibu huku akiwa anaangalia namna bahari ilivyokuwa na utulivu mkubwa wala usingeamini kwamba inamiliki viumbe vya kutisha ndani yake.
Mawazo yake wala hayakuwa hapo baharini japo alikuwa anaangalia hapo nyakati hizo, akili yake yote ilikuwa kwenye tukio ambalo lilitokea kwenye chuo cha mwalimu Nyerere. Lile tukio sio tu kwamba lilimgusa kwa namna lilivyo tokea bali lilikuwa linamhusu yeye moja kwa moja kwa sababu ni yeye ambaye alitakiwa kuhakikisha kwamba anamlinda yule binti kwa gharama yoyote ambayo ingekuja mbele yake lakini kwa bahati mbaya zaidi alipewa kazi ya kumlinda mtu ambaye hakuwa akimjua wala hakuwahi kukutana naye hata siku moja, kazi ambayo kwake ilionekana kuwa ngumu kwa wakati huo.

Mwanamke huyo sababu ya kwenda ndani ya kile chuo ilikuwa ni kujifanya anasoma pale ili aweze kumpata binti huyo kabla hajatua kwa watu wengine lakini kwa bahati mbaya siku ambayo alikuwa anamtambua binti huyo ndiyo siku ambayo alikuwa anatekwa na watu ambao bila shaka walikuwa wamemzidi kete za ulingoni. Mbali na yale maswali ambayo alikuwa anajiuliza kuhusu ule tambulisho wa mhusika ambaye alijifanya kuwa profesa Gerald, swali lake kubwa kwa wakati huo ambalo ndilo lilizibeba hisia zake na mawazo yake ni wapi ambapo alikuwepo binti huyo! Aliwaza ni kwa namna gani anaweza kumpata ikiwa watu ambao walimteka ni wazi kwamba alikuwa hawawezi kabisa na walikuwa wanamzidi mpaka uwezo ambao alikuwa nao. Jambo hilo lilimfana ajikute anataka kukata tamaa, kwa sababu hakuona mahali ambapo angeweza kutokea na kufanikisha kuimaliza hiyo kazi.

Wakati ambao mawazo yake yaliamua kukata tamaa, alijikuta anakutana na mambo mengine ambayo yalijihifadhi kwenye ubongo wake. Mambo hayo japo yalimshtua lakini yalionekana kuwa na maana kubwa kwake kwa wakati huo.
“Bazoka!” alijikuta analitamka hiyo jina, jina la mwanaume ambaye mpaka wakati huo hakuna ambaye alikuwa anajua yupo wapi. Alihamaki kwa muda baada ya kulitamka jina hilo ambalo lilikuwa kwenye mdomo wake bila hata kutarajia.

“Tayari amekufa? kama amekufa lazima ningesikia taarifa zake kwa namna yoyote hivyo kuna nafasi ndogo kwamba bado yupo hai! Huyu ndiye mtu pekee ambaye anaweza kunisaidia kufanikisha hili. Lakini kama yupo hai atakuwa wapi kwa sasa? au wamemuua na hawataki hili jambo lijulikane mahali popote? Lazima nilifanyie kwanza hili kazi nijue kama atakuwa hai au amekufa na kama yupo hai huyu ndiye ambaye nitatakiwa kumtafuta kwa gharama yoyote ambayo itakuja mbele yangu” mwanamke huyo alijikuta ana maswali mengi ambayo mengine yalianza kumuumiza kichwa kwani majibu yake ni kama yalikuwa yanakinzana.

Hisia zake zilimrudisha nyuma kidogo siku ambayo alikutana na mtu wa ajabu ambaye alimpatia hiyo kazi ya kumlinda huyo binti ambaye yeye hakuwa akimfahamu. Mwanamke huyo alikuwa ametoka kufanya mapenzi, mapenzi ilikuwa ndiyo starehe yake kubwa huenda kutokana na kwamba alikuwa ni mpweke muda mwingi. Siku hiyo alikuwa ametoka kwenye nyumba ya wageni na mwanaume mmoja shababi ambaye alitoka kumtelekeza na kuingia kwenye gari yake lakini wakati anaiwasha gari yake aligundua kwamba humo ndani ya gari kulikuwa na ongezeko la mtu mwingine ambaye hakuwa na taarifa naye. Jambo hilo alilishtukia akiwa amechelewa kwani wakati anataka kufanya maamuzi ya kujihami aligusana na kitu cha baridi hivyo ikamlazimu kuwa mpole ili asije kupoteza ubongo wake.

“Unataka nini kwangu kwa sababu mpaka umenipata hapa maana yake umenifuatilia na kama ungehitaji kuniua ungesha niua hivyo mpaka sasa unanitaka nikiwa hai! Hivyo nambie unataka nini haraka nataka nikapumzike!?”
“Upo sahihi, nimekuwa nikikufuatilia kwa muda mrefu, nina taarifa kwamba wewe ndiye ambaye ulienda Kenya na kuiba taarifa zao za siri kuhusu jeshi lao na mpango kazi wao wa miaka hamsini ijayo. Hii imekuwa ni siri kubwa kwa upande wako na tangu urudi ndipo umeanza kuutumia muda wako kutafuta vijana wa kukuridhisha kingono jambo ambalo hata sikulaumu kwani halinihusu kabisa” ilikuwa ni sauti ya kiutu uzima mno kutoka upande wa nyuma kwa mtu ambaye kwa taarifa ambayo alimpatia ni wazi alikuwa akimfuailia kwa muda mrefu.
“Wewe ni nani?”
“Huu sio muda rafiki wa mimi na wewe kujuana bibie”
“Kwahiyo unataka nini?”
“Kuna kazi kubwa sana nataka nikupatie na unatakiwa kuhakikisha unaifanya kwa uharaka mkubwa kwa sababu muda mfupi ujao mambo yanaenda kuharibika”

“Unahisi kwanini naweza kuifanya kazi yako?”
“Kwa sababu hauna namna”
“Unamaanisha kwamba utavujisha taarifa zangu juu ya mambo ambayo nimeyafanya Kenya?”

16 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: JUMBA JEUSI
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

EPISODE 17.
ENDELEA.......

“Nashukuru kwa kuniokolea muda kwa sababu unaonekana kuwa mwanamke muelewa tofauti na nilivyokuwa nakufikiria”
“Ni kazi gani unataka kunipatia?”
“Kuna binti unatakiwa umtafute kisha umlinde hata ikikulazimu kuyatoa maisha yako yote”
“Unamaanisha kitu gani?”
“Ni kwamba kuna binti anasoma ndani ya chuo cha mwalimu Nyerere, ni binti ambaye hata mimi simfahamu ila unatakiwa kumpata”
“Unanipa kazi ya kumtafuta mtu ambaye hata wewe mwenyewe haumjui?”
“Ndiyo”
“Siwezi kuifanya kazi kama hiyo kwa sababu haiwezekani”
“Wewe ndiye ambaye unatakiwa kutafuta njia ya kuhakikisha jambo hilo linawezekana”
“Kwanini unahisi naweza kuifanya kazi kama hiyo?”
“Kwa sababu ndiyo maisha yako Jessica”
“Sasa nitamjuaje?”
“Utamjua kwa sababu ni tofauti na mabinti wengine, huo utofauti wake ndio ambao unafanya awe wa mhimu kuliko hata maisha yako hivyo nakuomba sana hakikisha unampata huyu binti”
“Jina lake anaitwa nani?”
“Luana ndilo jina lake la kuzaliwa japo kwa sasa anaweza kuwa na jina tofauti kutokana na historia ya maisha yake ambayo sipo tayari kukupatia hapa”

“Baada ya kumpata natakiwa nimpeleke wapi?”
“Unatakiwa umlinde mpaka siku ambayo utakuwa na uhakika na usalama wake”
“Kuna jambo ambalo hautaki kuniambia si ndiyo?”
“Yapo mengi binti ila kwa bahati mbaya haupo kwenye nafasi ya kuweza kuyajua haya mambo kwa sasa”
“Kama ni hivyo unanipa kazi ngumu kuweza kukusaidia ombi lako”
“Kuna jambo baya linaenda kulikumba hili taifa ndiyo maana nimehitaji msaada wako”
“Jambo gani hilo?”
“Kama nikikwambia hali itakuwa mbaya zaidi”
“Mpaka unakuja kwangu maana yake kwenye hesabu yako uliona kwamba mimi unaweza ukaniamini kiasi kwamba ukanipa nafasi ya kumlinda mtu ambaye bila shaka kwako ni mhimu sana hivyo sioni kama kuna jambo kubwa zaidi ya huyo binti”

“Raisi anaenda kuuawa”
“Samahani umesema?”
“Muda sio mrefu taifa hili linaingia gizani, raisi anatakiwa kufa”
“Ni nani huyo mwenye hiyo jeuri ya kupanga njama za kuweza kumuua raisi?”
“Sio kila mtu ni mwema na sio kila mtu ni dhaifu kuliko raisi bibie”
“Mimi na wewe tunajua kabisa kwamba jambo hili haliwezekani kabisa kutokea”
“Mimi ninajua kwamba linawezekana na hakuna wa kuweza kulizuia ndiyo maana nimekuja hapa kwako”

“Bado sijakuelewa, ni nani ambaye anaweza kumuua raisi? Na jambo hata kama halipo, imekuwaje usalama wa taifa hawajui? Inakuwaje shirika letu halina taarifa hizi?”
“Nisikilize bibie, taifa hili linawatambua usalama wa taifa tu, hilo shirika lenu halitambuliki kama lipo kwa sababu ni kama wazo la kufikirika tu ndiyo maana hata wewe hakuna mtu anaye ijua kazi yako zaidi ya watu kadhaa tu hususani wakubwa zako. Hata kama wangejua hao usalama, una uhakika gani kwamba wao hawawezi kuwa sehemu ya huo mpango?”
“Kama unaweza naomba unipe nafasi ya kumsaidia raisi wangu”
“Nasikitika kusema kwamba hauwezi kufanya hivyo na hakuna namna unaweza kuzuia hili jambo zaidi utafanya mambo kuwa mabaya zaidi”
“Raisi anajua kuhusu hili?”
“Hapana”
“Unaonekana unajali kuhusu yeye sasa kwanini usimsaidie?”

“Mambo hayaendi hivyo bibie ndiyo maana nimekwambia kwamba siwezi kukupa taarifa zote ambazo unazitaka wewe. Ipo siku muda ukifika tunaweza kukutana ama kuna watu watakuja kukupa taarifa kamili na sababu za msingi za huyo binti kutakuwa kulindwa na wewe”
“Kwanini wanahitaji kumuua raisi?”
“Ni sababu nyingi ila kikubwa ni kwamba uzalendo wake ndio umekuwa shida kubwa”
“Uzelendo? Hilo ndilo jambo la msingi zaidi kwa taifa sasa kivipi raisi kuwa mzalendo iwe sababu ya yeye kufa?”
“Unahisi hao watu wenye pesa wanajali lolote kuhusu uzalendo? Unahisi wanajali lolote kuhusu raia wa taifa hili? Kama ulikuwa unawaza hivyo basi bado una mengi ya kujifunza. Siasa haipo hivyo bibie, siasa ni mlima mkubwa zaidi hata ya ule mlima pendwa wa Kilimanjaro, siasa ina mambo mengi ndani yake lakini pia ina watu wengi ambao wana malengo na maono tofauti lakini ono moja kubwa kuliko yote ni pesa. Hao watu wote ambao nimekutajia hapo lengo lao kuu ni pesa hivyo kama ukija na mlengo wa kutaka kuzuia jambo hilo kwao unakuwa hauna umuhimu wowote ukiwa hai hivyo ni bora ufe”
“Unamaanisha wanamuua kwa kazi nzuri ambayo anaifanya?”

“Kuanzia wakati huu hatutakiwi kulizungumzia jambo hili kwa mara nyingine tena na wala nisije kusikia unalitaja mahali popote kwa sababu itachukua dakika kumi tu mimi kupata habari hizi pindi ukiufungua mdomo wako. Kuanzia sasa unatakiwa kwenda kumlinda binti huyo na kama ukimpata basi hakikisha unaondoka naye hata ikiwezekana mbali na taifa hili mimi nitakutafuta” maelezo ya mzee huyo yalibaki yanamshangaza kwani hakuwa anamuelewa kwa sababu alikuwa anaongea mambo magumu na ya kutisha kwa lugha rahisi na ya kawaida kana kwamba alikuwa anaenda kuwinda ndege wa mwituni.
“Na chuo?”
“Chuo na maisha ya mtu kipi kina thamani kubwa? Huyo binti anaweza kusoma sehemu yoyote hapa duniani hivyo mtafute kwanza”
“Kwanini mimi?”
“Kwa sababu unafaa kwa hii kazi. Kumbuka tu huyo binti kuwa hai ni jukumu lako wewe na kama atapata tatizo lolote lile basi sitakusamehe maisha yako yote” mzee huyo alishuka akiwa amejifunika na kofia na wakati anashuka kuna gari ilifika hapo akaingia ikatoweka ikiwa na namba za Ikulu jambo ambalo lilimshangaza Jessica kwani bado alikuwa yupo njiapanda akihisi kama ni mtu ambaye alikuwa ndotoni na muda wowote ule angeshtuka lakini haikuwa hivyo.


Kazi ambayo alisisitizwa kuifanya mpaka wakati huo ilionekana kwamba ilikuwa imemshinda ndiyo maana alihitaji kujua ukweli kuhusu maisha ya Bazoka kama alikuwa hai aweze kumsaidia kwani ni yeye pekee ambaye aliamini kwamba angekuwa na uwezo wa kumsaidia. Sasa ngempatia wapi mwanaume huyo ambaye mpaka muda huo ilikuwa ni hamsini hamsini kwamba yupo hai au emekufa. Sehemu ilikuwa ni moja tu ya kuweza kupata dodoso za mwamba huyo, kwa mpenzi wake.
Baada ya kupewa taarifa ya kufa kwa raisi akiwa bado hai kabisa alianza kufuatilia taarifa za watu wa karibu zaidi na raisi ili aweze kumtambua ambaye alimpa kazi lakini alihitaji kuwa na uhakika kama yule mtu alikuwa sahihi au alitaka kumtumia kwa kazi zake binafsi kupitia Ikulu jambo ambalo alijua ni wengi huwa wanautumia huyo mwanya kuweza kukamilisha kazi zao binafsi. Hivyo moja ya watu ambao alianza kuyafuatilia maisha yao kwa ukaribu alikuwa ni mlinzi mkuu wa raisi. Mwanaume huyo aliipata historia yake ambayo haikuwa ndefu japo kwenye hiyo taarifa kulikuwa na habari moja ambayo ilimvutia kuweza kuifuatilia kwani ingemfunulia mengi kwenye hiyo safari.

Habari ambayo ilikuwa nzuri kwake ni baada ya kugundua kwamba bwana huyo alikuwa kwenye penzi la siri na mrembo mmoja ambaye alikuwa akifanya biashara ya vipodozi. Mwanamke huyo alikuwa maarufu mno nchini kwa sababu alikuwa ni Miss Tanzania kwa miaka mitatu mfululizo lakini pia mwaka huo alitoka kushinda tuzo ya Miss East Africa. Kutokana na mvuto tukuka wa huyo mwanamke, ni wanaume wengi walikuwa wanatamani kuweza kumpata lakini waliishia kugonga mwamba kwa sababu hakuwa tayari kuwa na mwanaume yeyote yule akidai kwamba alikuwa na mwanaume wake ambaye alimpenda mno na muda mfupi baadae wangeenda kufunga ndoa na kuishi pamoja kama mume na mke.

17 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
MIAKA 15 NYUMA YA UKUTA WA GEREZA!!!!!

Alan, anatokea kwenye umaskini ulipo pitiliza, dunia inamfunza kuwa mshenzi ili aweze kuishi ndipo anaingia kwenye ulingo wa MAUAJI ili aweze kupata mkate wake.... Huko anaanza kuua watu kwa miaka mitano ambapo anafanikiwa kutengeneza pesa za kitanzania Bilioni 5....

Baadae unagundulika ulingo huo ulikuwa kinyume cha utaratibu hivyo wahusika wote wanakamatwa na kuporwa kila kitu yeye anafanikiwa kuachwa hai ila akiwa maskini kama zamani....

Baadae anapata kazi ya kwenda kumuokoa mtoto wa tajiri mmoja ndani ya jiji la ABUJA, NIGERIA ambaye alitekwa na magaidi kwa malipo ya shilingi bilioni 10 za kitanzania lakini kazi hiyo inaishia pabaya baada ya binti huyo kuuawa na yeye mwenyewe kudungwa sindano yenye sumu kali sana....

Alan anapotea namna hiyo lakini miezi miwili baadae anakuja kuonekana mtu ambaye anafanana naye kwenye kamera za shirika la kijasusi la Tanzania yaani (TIA) TANZANIA INTELLIGENCE AGENCY ndani ya jiji la Dar es salaam jambo ambalo linawashangaza kwa sababu walijua alikufa na walikuwa na uhakika na hilo ......

Wakiwa wanajiuliza na kuanza kufuatilia mkasa huo ndipo Tanzania inavamiwa na magaidi kwa ajili ya kesi ile ile baada ya miaka mitano kwa madai ya kwamba walihisi bwana huyo bado alikuwa hai tena aliwaibia kiasi cha shilingi bilioni 20 za kitanzania.

Nchi inaingia sehemu mbaya huku wakimtafuta bwana huyo bila mafanikio kwa miaka 15.....

Wanapata uvumi wa kwamba bwana huyo alipotea kwenye mazingira ya ajabu bila kuacha taarifa nyuma ila kwa taarifa za kudhania zilidai kwamba mwanaume huyo alienda kujificha kwenye GEREZA Moja la Siri ambako aliishi kwa miaka 15 ....

Sasa ni kipi kilimpeleka huko? Ni kweli kwamba alikuwa ni yeye hakufa kule Nigeria? Kama sio yeye ni nani alikuwa anatumia sura yake? Kwanini apotee miaka 15 tena kwenda gerezani?

KAMA ULIKUWA UNATAMANI KUKUTANA NA SIMULIZI YA KIJASUSI YENYE WATU WENYE NGUVU ZA AJABU (SUPERNATURAL POWERS) Upo sehemu sahihi..... Karibu sana.

Hii ni simulizi ambayo ina mapigano, upelelezi wa hatari, mapenzi, siasa, supernatural powers ( nguvu za ajabu) na story ambayo imeshiba haswa...... FANTASY

Unaweza ukaipata kwa shilingi 5000 tu za kitanzania kwa namba hizi hapa chini 👇

0621567672 (HALOPESA).......WhatsApp

0745982347 (M-PESA)

0714581046 (TIGO-PESA)

0689440143 (AIRTEL MONEY)

36316279 (LIPA NAMBA (M-PESA) inapokea mitandao yote)

FEBIANI BABUYA
 

Attachments

  • Miaka 15.jpg
    Miaka 15.jpg
    379.1 KB · Views: 21
STORY: JUMBA JEUSI
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

EPISODE 17.
ENDELEA.......

“Nashukuru kwa kuniokolea muda kwa sababu unaonekana kuwa mwanamke muelewa tofauti na nilivyokuwa nakufikiria”
“Ni kazi gani unataka kunipatia?”
“Kuna binti unatakiwa umtafute kisha umlinde hata ikikulazimu kuyatoa maisha yako yote”
“Unamaanisha kitu gani?”
“Ni kwamba kuna binti anasoma ndani ya chuo cha mwalimu Nyerere, ni binti ambaye hata mimi simfahamu ila unatakiwa kumpata”
“Unanipa kazi ya kumtafuta mtu ambaye hata wewe mwenyewe haumjui?”
“Ndiyo”
“Siwezi kuifanya kazi kama hiyo kwa sababu haiwezekani”
“Wewe ndiye ambaye unatakiwa kutafuta njia ya kuhakikisha jambo hilo linawezekana”
“Kwanini unahisi naweza kuifanya kazi kama hiyo?”
“Kwa sababu ndiyo maisha yako Jessica”
“Sasa nitamjuaje?”
“Utamjua kwa sababu ni tofauti na mabinti wengine, huo utofauti wake ndio ambao unafanya awe wa mhimu kuliko hata maisha yako hivyo nakuomba sana hakikisha unampata huyu binti”
“Jina lake anaitwa nani?”
“Luana ndilo jina lake la kuzaliwa japo kwa sasa anaweza kuwa na jina tofauti kutokana na historia ya maisha yake ambayo sipo tayari kukupatia hapa”

“Baada ya kumpata natakiwa nimpeleke wapi?”
“Unatakiwa umlinde mpaka siku ambayo utakuwa na uhakika na usalama wake”
“Kuna jambo ambalo hautaki kuniambia si ndiyo?”
“Yapo mengi binti ila kwa bahati mbaya haupo kwenye nafasi ya kuweza kuyajua haya mambo kwa sasa”
“Kama ni hivyo unanipa kazi ngumu kuweza kukusaidia ombi lako”
“Kuna jambo baya linaenda kulikumba hili taifa ndiyo maana nimehitaji msaada wako”
“Jambo gani hilo?”
“Kama nikikwambia hali itakuwa mbaya zaidi”
“Mpaka unakuja kwangu maana yake kwenye hesabu yako uliona kwamba mimi unaweza ukaniamini kiasi kwamba ukanipa nafasi ya kumlinda mtu ambaye bila shaka kwako ni mhimu sana hivyo sioni kama kuna jambo kubwa zaidi ya huyo binti”

“Raisi anaenda kuuawa”
“Samahani umesema?”
“Muda sio mrefu taifa hili linaingia gizani, raisi anatakiwa kufa”
“Ni nani huyo mwenye hiyo jeuri ya kupanga njama za kuweza kumuua raisi?”
“Sio kila mtu ni mwema na sio kila mtu ni dhaifu kuliko raisi bibie”
“Mimi na wewe tunajua kabisa kwamba jambo hili haliwezekani kabisa kutokea”
“Mimi ninajua kwamba linawezekana na hakuna wa kuweza kulizuia ndiyo maana nimekuja hapa kwako”

“Bado sijakuelewa, ni nani ambaye anaweza kumuua raisi? Na jambo hata kama halipo, imekuwaje usalama wa taifa hawajui? Inakuwaje shirika letu halina taarifa hizi?”
“Nisikilize bibie, taifa hili linawatambua usalama wa taifa tu, hilo shirika lenu halitambuliki kama lipo kwa sababu ni kama wazo la kufikirika tu ndiyo maana hata wewe hakuna mtu anaye ijua kazi yako zaidi ya watu kadhaa tu hususani wakubwa zako. Hata kama wangejua hao usalama, una uhakika gani kwamba wao hawawezi kuwa sehemu ya huo mpango?”
“Kama unaweza naomba unipe nafasi ya kumsaidia raisi wangu”
“Nasikitika kusema kwamba hauwezi kufanya hivyo na hakuna namna unaweza kuzuia hili jambo zaidi utafanya mambo kuwa mabaya zaidi”
“Raisi anajua kuhusu hili?”
“Hapana”
“Unaonekana unajali kuhusu yeye sasa kwanini usimsaidie?”

“Mambo hayaendi hivyo bibie ndiyo maana nimekwambia kwamba siwezi kukupa taarifa zote ambazo unazitaka wewe. Ipo siku muda ukifika tunaweza kukutana ama kuna watu watakuja kukupa taarifa kamili na sababu za msingi za huyo binti kutakuwa kulindwa na wewe”
“Kwanini wanahitaji kumuua raisi?”
“Ni sababu nyingi ila kikubwa ni kwamba uzalendo wake ndio umekuwa shida kubwa”
“Uzelendo? Hilo ndilo jambo la msingi zaidi kwa taifa sasa kivipi raisi kuwa mzalendo iwe sababu ya yeye kufa?”
“Unahisi hao watu wenye pesa wanajali lolote kuhusu uzalendo? Unahisi wanajali lolote kuhusu raia wa taifa hili? Kama ulikuwa unawaza hivyo basi bado una mengi ya kujifunza. Siasa haipo hivyo bibie, siasa ni mlima mkubwa zaidi hata ya ule mlima pendwa wa Kilimanjaro, siasa ina mambo mengi ndani yake lakini pia ina watu wengi ambao wana malengo na maono tofauti lakini ono moja kubwa kuliko yote ni pesa. Hao watu wote ambao nimekutajia hapo lengo lao kuu ni pesa hivyo kama ukija na mlengo wa kutaka kuzuia jambo hilo kwao unakuwa hauna umuhimu wowote ukiwa hai hivyo ni bora ufe”
“Unamaanisha wanamuua kwa kazi nzuri ambayo anaifanya?”

“Kuanzia wakati huu hatutakiwi kulizungumzia jambo hili kwa mara nyingine tena na wala nisije kusikia unalitaja mahali popote kwa sababu itachukua dakika kumi tu mimi kupata habari hizi pindi ukiufungua mdomo wako. Kuanzia sasa unatakiwa kwenda kumlinda binti huyo na kama ukimpata basi hakikisha unaondoka naye hata ikiwezekana mbali na taifa hili mimi nitakutafuta” maelezo ya mzee huyo yalibaki yanamshangaza kwani hakuwa anamuelewa kwa sababu alikuwa anaongea mambo magumu na ya kutisha kwa lugha rahisi na ya kawaida kana kwamba alikuwa anaenda kuwinda ndege wa mwituni.
“Na chuo?”
“Chuo na maisha ya mtu kipi kina thamani kubwa? Huyo binti anaweza kusoma sehemu yoyote hapa duniani hivyo mtafute kwanza”
“Kwanini mimi?”
“Kwa sababu unafaa kwa hii kazi. Kumbuka tu huyo binti kuwa hai ni jukumu lako wewe na kama atapata tatizo lolote lile basi sitakusamehe maisha yako yote” mzee huyo alishuka akiwa amejifunika na kofia na wakati anashuka kuna gari ilifika hapo akaingia ikatoweka ikiwa na namba za Ikulu jambo ambalo lilimshangaza Jessica kwani bado alikuwa yupo njiapanda akihisi kama ni mtu ambaye alikuwa ndotoni na muda wowote ule angeshtuka lakini haikuwa hivyo.


Kazi ambayo alisisitizwa kuifanya mpaka wakati huo ilionekana kwamba ilikuwa imemshinda ndiyo maana alihitaji kujua ukweli kuhusu maisha ya Bazoka kama alikuwa hai aweze kumsaidia kwani ni yeye pekee ambaye aliamini kwamba angekuwa na uwezo wa kumsaidia. Sasa ngempatia wapi mwanaume huyo ambaye mpaka muda huo ilikuwa ni hamsini hamsini kwamba yupo hai au emekufa. Sehemu ilikuwa ni moja tu ya kuweza kupata dodoso za mwamba huyo, kwa mpenzi wake.
Baada ya kupewa taarifa ya kufa kwa raisi akiwa bado hai kabisa alianza kufuatilia taarifa za watu wa karibu zaidi na raisi ili aweze kumtambua ambaye alimpa kazi lakini alihitaji kuwa na uhakika kama yule mtu alikuwa sahihi au alitaka kumtumia kwa kazi zake binafsi kupitia Ikulu jambo ambalo alijua ni wengi huwa wanautumia huyo mwanya kuweza kukamilisha kazi zao binafsi. Hivyo moja ya watu ambao alianza kuyafuatilia maisha yao kwa ukaribu alikuwa ni mlinzi mkuu wa raisi. Mwanaume huyo aliipata historia yake ambayo haikuwa ndefu japo kwenye hiyo taarifa kulikuwa na habari moja ambayo ilimvutia kuweza kuifuatilia kwani ingemfunulia mengi kwenye hiyo safari.

Habari ambayo ilikuwa nzuri kwake ni baada ya kugundua kwamba bwana huyo alikuwa kwenye penzi la siri na mrembo mmoja ambaye alikuwa akifanya biashara ya vipodozi. Mwanamke huyo alikuwa maarufu mno nchini kwa sababu alikuwa ni Miss Tanzania kwa miaka mitatu mfululizo lakini pia mwaka huo alitoka kushinda tuzo ya Miss East Africa. Kutokana na mvuto tukuka wa huyo mwanamke, ni wanaume wengi walikuwa wanatamani kuweza kumpata lakini waliishia kugonga mwamba kwa sababu hakuwa tayari kuwa na mwanaume yeyote yule akidai kwamba alikuwa na mwanaume wake ambaye alimpenda mno na muda mfupi baadae wangeenda kufunga ndoa na kuishi pamoja kama mume na mke.

17 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
Shukrani mtaalam FEBIANI BABUYA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom