Simulizi: John ze mwizi

Simulizi: John ze mwizi

Sehemu ya ishirini na moja


★★Ilipoishia★★

John alirudi kitandani na kuzimwaga hela hukuakitetemeka kutokana na woga aliokuwa naoisitoshe ilikuwa ni Mara yake ya kwanza kupata helakama zile.

★★Shuka Nayo ★★

Amina alirudi nyumbani jioni akiwa hana uhakikakama john amerudi, Alipofika akakumbana namwanga hafifu wa chemli ambayo iliwashwa naJohnAmina alipitiliza moja kwa moja ndani,kulikuwatulivu mno ni kama hamna.kiumbe chochotekinachoishi mahali hapoAmina akaingia kwa kunyata ili amfumanie john kwakile anachokifanya ama la amstukize kwa ujio wake Amina alipoingia ndani alibaki kaduwaa baada yakumuona John amelala kitandani chali ila yu macholakini alikuwa akijichekea peke yake alafu ananunakisha anaanza tena kucheka,akawa anarudia rudiakile kitukoAmina akajua tayari Mme wake ameanza kuwa chiziakashikwa na huzuni na kumsogelea mpaka palealipolala john.

John hakuwa na habari aliendelea.na.kamchezokake kale kale. Amina akamshika john viganja nakuanza kuvipapasa hapo ndipo John alipostuka nakumuangalia Amina kwa mshangao"umekuwaje John wangu mbona sikuelewi" Aminaalianzisha mazungumzo"Aminaa!!!,am! aaaah! samahani sikutambua kamaumefika mke wangu" John alijiuma uma"Haujajibu swali langu ni kwanini upo hivyo unamatatizo gani?" Amina aliuliza"Hamna kitu mke wangu nifuraha tu iliyonitawalakwahiyo usiwe na wasiwasi niko vizuri kabisa" Alijibijohn akiwa anaamanisha."Sawa nimekuelewa vipi kuhusu safari yakoilikuwaje""Safi kabisa tena yenye mafanikio kiasi" John alijibukwa bashasha"Mmh!! aya najua umechoka ngoja nikuchemshiemaji ya kuoga" Alisema Amina.

"Wala usijali mke wangu"John hakuthubutu kumuonyesha mke wake helamaana alijua wazi angekumbana na maswali lukukikuhusu kazi yake mbaya zaidi ni kazi ya siku mojahela zote zile wala asingeeleweka kwa Amina★★★★★★★★★★★★Ukitaka kumfahamu mwanakijiji si kwa ushamba tuhata mipango yake inaweza kukutambulisha pia silazima atokee kijijini hata mjini nako kunawanakijiji. .John alikaa wiki moja tu ya mapumziko na wikiiliyofuata akapanga safari ya kuelekea mjini namuda wote huo Juma alikuwa akimfuatilia Johnhatua kwa hatua na kwa bahati alifanikiwakumuuliza Amina kuhusu kazi ya Mme wakealichojibu ni kuwa hajui ila kila anapoenda kazinihuvaa koti refuPale pale juma akawa amethibitisha kuwa mhusikamkuu ni John hivyo akaanza kutafuta, namna yakumuweka hatianiJohn alienda mjini kwa Mara ya pili kichwanimwake alipania kuwa hiyo ni Mara ya mwishokufanya kazi ya namna ile.

Ali na juma waliwafuata baadhi ya wananchiwaliokuwa nao katika tukio alilolifanya john kipindicha nyumaWalieleza uchunguzi wao ulivyokuwa mpaka hatimayake,waliazimia kumkamata john sikuinayofuata.Lakini pia walionana na mwenyekiti wakijiji ambaye aliwapatia mgambo kwaajili ya kazihiyo japo aliwaonya kuwa endapo watakosakithibitisho kinachowafanya wamkamate John basi nilazima walipe fidia ya kumdhalilisha.

Kama ilivyokawaida john alifikia katika nyumba yanyumba wageni na ilipotimia asubuhi alienda katikamaduka ya nguo akachagua suti moja matataitakayonfaa.Cha ajabu ni kwamba john hakwenda katika hotelnyingine zaidi ya ile ile ya mwanzo aliyowahikwenda,Si kwasababu hakuona sehemu nyingine yakwenda hapana ila chakula alichopewa siku ilekilikuwa na radha adimu na nd'o kitukilichompelekaJohn alifika na kuketi,ni kama bahati kwani yulemhudumu aliyewahi kumhudumia john ndiyealiyefika eneo lile kumhudumia tena john"Habari yako kaka na karibu katika hoteli yetu sijuinikuhudumie kitu gani au kama hautojali nikupemenyu yetu"

Aliongea mhudumu kwa bashashaakiwa tayari amempotea john"Salama kwa upande wangu pia nashukuru kwaukarimu wako lakini sijui kama unanikumbuka" Johnaliongea kwa utulivu ila kiukweli ni kwambaalijipoteza mwenyewe kwa kumkumbusha mhudumuyule ambaye alionesha wazi hamkumbuki"Hapana kaka yangu sikumbuki chochote kuhusuwewe na kama kuna.lolote nitafute baada yakazi,samahani kwa hilo" Mhudumu akawa mkalikatika kazi yake"Bila samahani lakini wiki kama ngapi zimepitakuna mteja alifika hapa akaagiza chai maandazi sikuhiyo ulicheka sana sijui kama ni wewe ila kamanimekosea basi nipatie kifungua kinywa" Alisema John akiwa amekata tamaa ya kumkumbusha yulemhudumu

Moyo wa Margaret ambaye ni muhudumu ulilipukamno akakumbuka kuwa ni huyo mtejawanayemsubiri kwa hamu pia ni huyo huyo mtejaaliyetaka kumkosesha ugali wake kinywani,Ijapokuwa margaret hakukumbuka mara ya mwisho kusalisiku hii alishukuru Mungu kimoyo moyo"Nimekumbuka kaka yangu,karibu sana japoumebadilika mno,samahani nimetumia muda mrefuhapa naomba nikuhudumie" Margaret alizungumza
 
Sehemu ya ishirini na mbili

★★★Ilipoishia★★★

"Nimekumbuka kaka yangu,karibu sana japoumebadilika mno,samahani lakini nimetumia mudamrefu hapa naomba nikuhudumie" Margaretalizungumza.

★★Shuka nayo★★

"Haina tabu nipe kifungua kinywa" John alijibu"Mmmh!! sasa hivi umejitahidi,nakuletea muda simrefu" Margaret akaondoka eneo lileJohn hakuwa na shaka na wala hakutambua kuwaalishastukiwa mapema sana akaendelea kusubiriakifungua kinywa chake kiletwe.

Margareta hakuwa na papara alileta chakula nakumkaribisha john na bila kutegea john akampahela na kumwambia vile vile kiasi kinachobaki akaenacho Margaret aliondoka akiwa anabinua binua midomoalafu mwendo aliotembea alitamani apae ili amfikiebosi wake mapemaMargaret alifika kwa bosi na kuingia bila hodi "Bosi bosi bosi amekuja amekuja yule aliyeiba zilehela amekuja na hela yake ni hii " Margaret, aliongeahuku akiruka ruka akiwa mwenye furaha "Ahaaaa! nimemsubiri sana, leta hapa hiyo hela alafuameondoka au?" aliiuliza bosi" Bado yupo bosi anakula" alijibu Margaret "Hakikisha unamuita huku kabla hajaondoka" "Sawa bosi" Alijibu Margaret akiwa ameiacha, helakwa bosi wakeJohn alipomaliza kula tu Margaret alikuwa amefikakatika meza yake "Samahani kaka unahitajika kidogo kwa bosianataka azungumze kidogo na wewe" Margaert alisema"Twende maana nina safari muda si mrefu"

John alifikiri huenda ile suti imemfanya aonekane wamaana hata kwa bosi wa hotel ile hivyo bila kufikiriakakubali haraka haraka kwenda John alifikishwa kwa bosi wa hoteli kisha Margaretakaombwa atoke nje ya chumba hicho"Samahani kwa kukusumbua mteja wangu"alianzisha bosi"Bila shaka usijali" alijibu john"Kuna huu mzigo sijui ni wa kwako" Bosiakamuonesha john yule panya wakeJohn akapatwa na mstuko wazi wazi mbele ya bosi yule "Natambua kuwa wewe ni mtafutaji ila hii njiaunayotumia umekosea sana,nikimuua huyu panyautakuwa umepoteza kila kitu sasa naombaunirudishie pesa zangu zote ulizobeba bilakupunguza kabla jua halijatua vinginevyo nisikuonehapa" AliOngea bosi,wa hoteli "Naleta sasa hivi" john alijibu kwa kutetemeka John akaondoka hotelini hapo akiwa na mawazotele kuwa za mwizi zimemfikia lakinihakuchanganyikiwa sana kwasababu alipewa chaguo.

Ikiwa ni mchana amina anapokea wageni kibaoikiwemo mgambo wa kijiji wanamlazimisha atoekoti analotumia mme wake kazini naye bila shakaanaenda kulitoa na kuwapatiaJohn anarudi nyumbani kwake akiwa mwenye harakamno anapofika nyumbani kwake anakumbana namgambo,na baadhi ya wanakijiji wanamkamata iliakajibu shtaka analokabiliwa nalo .John kwa kujiamini anaomba muda aongee na mkewake ndani nao bila hiyana wanamuachia kwasababu, jeuri yake wanayo waoJohn ananyoosha moja kwa moja mpaka chumbanina kuanza kulitafuta koti lakini hakuliona akaamua kumuuliza Amina naye bila uoga anasema amewapamgambo pale nje John anaikumbuka ile kauli ya "siku ya kufa nyanimiti yote huteleza" anatamani kulia lakiniinashindikana ikabidi atoke nje na kukubali kukamatwa Amina alibaki na sintofahamu mpaka alipoambiwa yaliyomkuta john.

John alifikishwa kituoni na kuhukumiwa kifungo chamiaka,miwili na kabla hajapelekwa mahabusualiomba aongee na Amina"Usilie Amina haya yote niliyafanya kwaajili yakolakini baba yako ndiye aliyeyataka yote hayo" Johnalikuwa akiongea kwa huzuniAmina nd'o kwanza alizidisha kilio na kumfanyajohn azidi kupata wakati mgumu"Ukumbuke kuwa nakupenda Amina na sikutakauteseke kwaajili yangu nakupenda sana" Johnalimalizia na kuondolewa eneo lile.

Ilipita wiki Amina si wakula wala kufanya lolotezaidi ya kulia tu na kujifungia ndani na hataalipokuwa akipitiwa na usingizi alikuwa akilitaja jinala John kila MaraBi Mazi na mzee Mazi waliona kuna haja,yakumsaidia john na licha ya hayo bi,Mazi alimlaumumzee Mazi kwa kusababisha kadhia ile nakupelekea mwanaye kupoteza furaha ya maishayake.

Amina alifanikiwa kwenda kumtembelea Johnambaye kwa muda,mfupi tu alipoteza mpaka rangiyake aliyokuwa NayoAmina alimuonea john huruma pia johnalimuelekeza Amina kwenye sanduku lenye hela iliamfanyie mpango wa kutokaAmina hakungoja alienda mpaka katika nyumbaaliyokuwa akiishi na John kwa bahati alilipatasanduku lakini lilikuwa tupu, Amina hakuwa na jinsi akamuomba baba yakeatafute wanunuzi wa nyumba ambao aliwapataharaka haraka kutokana, na nyumba kuuzwa kimacha chini mnoJohn akafanikiwa kutoka kwa hela nyingi ambazo siza nyumba tu bali hata za mzee mazi zilitumika hiini kutokana na kesi zilivyojumuishwakitendawili kilibaki kuwa john ataishi wapi kwanihata wanakijiji hawakumuhitaji tena katika eneo laolakini jibu lake ni kwamba kipindi john alipoibapesa dukani zilikuwa kiasi kikubwa mno ambachoalikipeleka katika kijiji kinachofuata na kuanzishamakazi bila mtu yeyote kufahamu.

Mzee Mazi aliomba sana msamaha na kuahidi kuwayuko tayari kusaidia kwa lolote bila upendeleo.John na Amina wakaanzisha maisha mapya yafuraha na amani katika kijiji kile alichoanzishamakazi John.

★★Mwisho★★
 
Habari mambo naitwa Mr Equator Nimeandika ujumbe huu kuku omba swala moja tu!
Mimi nimetengeza website ya ku share story ambayo ni EquatorStory
Je umekuwa ukipata tabu kupost story zako hapa?
Hili ndo suluhisho lako.
Mimi nataka nkupe nafasi ya kuwa mmoja wapo wa kwanza kutumia hii website
unda account yako na uweze kupost story yako mpya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom