Simulizi: John ze mwizi

Simulizi: John ze mwizi

bioto

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2017
Posts
1,261
Reaction score
2,099
Simulizi:John ze Mwizi
Na: Humph Isack
Whatsapp: 0742817066


Sehemu ya Kwanza

Koooooh!! koooh!! koooh!!" ilikuwa ni sauti ya babuyake john akikohoa kwa nguvu wakati amejilazakitandani,kikohozi kilitoka kikavu kilichopolelekea mpaka mwili wake uruke ruke na kufanya kitandakilichochoka kilalamike kutokana na msoto kinaopitia"Amina naomba uniitie John haraka". Babu yake john alimuagiza Amina ambaye alikuwa ni mke wajohn na walikuwa wakiishi watatu tu katika nyumbayao ya tope,yote hayo ni baada ya wazazi wa johnkufariki kipindi akiwa kijana mdogo na kubakimikononi mwa mzee huyo aliyefahamika kijijini hapo kama Mzee Ndasi Mzee ndasi hakuwa na kipato cha kutosha kumuduMaisha yake na mjukuu wake hivyo hata masomoya john alishindwa kuyamudu kwani hakuwezakununua sare za shule wala madaftari kwaajili yamjukuu wake ispokuwa aliweza kupata chakula chakumtosha yeye na john pekee.

Baada ya kipindi kirefu kupita john alianzakujishughulisha na mazao ya chakula katika shambala babu yake na hivyo kuifanya familia iwezekujiendesha walau katika familia zenye hali yakawaida.Ilifikia kipindi john akabalehe na waswahili hupendakuziita kuwa ni balehe za kwanza kamatunavyoelewa balehe hizi za mwanzo zinavyokuwana msisimko wa hali ya juu kiasi kwamba mhusikaakijichanganya tuu basi anapotelea kwenye hubanzito yenye kina haswaa.

Ndivyo ilivyotokea kwa John bin Ndasi ambaye akiliyake haikutulia nyumbani,ikaanza kutafuta visichanavilivyochipukia kama yeye na kwa bahati akampata Amina kwa kusota mno lengo ikiwa atulizemihemko yake na mshawasha kisha atokomeee bilakujua kuwa amependa kusikopendeka na kadri siku zilivyoyoyoma alizidi kuzama zaidi na zaidi kwabinti yule wa rika lake na kusahau mipango yotealiyokiwekea kabla ya kujihusisha na mahusiano yakimapenzi na binti Amina.

Walianza penzi lao kwa siri na mwisho marafikiwakatambua,siri haikuwa siri tena ikafika kwawazazi wa Amina ambao hawa hawakuwa na dogokijijini pale, waliamini mzee Ndasi ni kigagula yaanimchawi kutokana na itikadi zake zilivyokuwa.Kwakuwa walimfahamu vyema mzee huyo wakaanzamoja kwa moja kumuonya binti yao kuwa ile familiasi nzuri hata kidogo kwahiyo aachane nayo maramoja,lakini binti Amina alisikia kushoto yakatokeakulia usishangae ni kwanini ila sababu ni moja Johnalikuwa ni chaguo la kwanza na mwanaume wakwanza kwa Amina.

Siku zilikatika na penzi likazidi kunoga haswaa nahatimaye likamfikia Mzee wa Wazee yaani kiboko yaWazee wengine ambaye ni Mzee Ndasi,kamakawaida yake alipitia kwanza machozi ya simbaama waswahili wanaita majisafi au pyua na kamahujanielewa naamanisha nini nd'o nakupa jibu kuwani ile pombe iliyopigwa marufuku na serikali nakuwa vita kubwa kati ya wauzaji na Polisi kilakukicha.Hauwezi kuamini kama katika kijiji cha akina john bin Ndasi hakuna aliyelifuatilia suala lile zaidi nazaidi walijumuika wote kupata machozi yasimba.Basi Mzee Ndasi akahakikisha amejaza kwelikatika tumbo lake lisilokuwa na hata dalili yakitambi kisha akaanza taratibu kuifuata njiainayoelekea nyumbani kwake.Kwa mwendo aliokuwa nao mzee Ndasi si rahisikumtilia shaka kuwa amelewa kwani hakuyumbayumba hata kidogo hii ikionesha wazi ni jinsi gani alivyo mzoefu katika matumizi ya pombe kwa mudamrefu.

Hayawi hayawi sasa yalikuwa Mzee Ndasi alifikanyumbani kwake mapema licha ya kuwa ulikuwa niumbali kiasi mpaka kufikia nyumbani kwake lakininyimbo alizokuwa akiimba njiani zilimsindikizaipasavyo."John! john! john! amka weee pumbavu,nasemaamkaaa shenzi weeee!" alianza kutupa maneno Yaleakiwa uwanjaniKwakuwa John alikuwa amelala fofofo hakuwezakusikia chochote kutoka kwa babu yake"Leo utanitambua si unajifanya umekua kidumengoja" Mzee Ndasi alijiongelea huku akiufuatia mtiwa mifolo wengine wanaiita miti ya zabibu japohaitoi zabibuAkakata fimbo ndefu iliyonyooka vyema na kuelekeanayo ndani,alipoingia tu akanyoosha moja kwa mojakatika chumba cha john na kumkuta akiwa amelalahoi hajielewi.

Mzee Ndasi alisimama kwanza akimuangalia johnkupitia mwanga hafifu wa tàa aina ya chemliitumiayo mafuta ya taa,Akatikisa kichwa akisikitikana kujisemea moyoni "Maskini John,unalala fofofokama si mwanaume vile sasa hata wezi wakivamiahumu ndani si wanaweza kukuhamisha kishawakaiba godoro wewe ukalala chin I au ukimuoahuyo binti utamlinda kweli? loooh!! maskini Johnngoja Leo nikufunze wanaume wanavyolala".kwa nguvu zote mzee Ndasi alishusha fimbo usawawa makalio ya john ambaye alikuwa amepoteleausingiziñi huku amejifunika shuka laini mno.Hamadi!! John alikurupuka huku akipiga yowe kali"Babu nakufaaaaaaaaa"
 
Sehemu ya Pili

★★★Ilipoishia★★★

Hamadi!! John alikurupuka huku akipiga yowe kali"Babu nakufaaaaaaaaa"

★★★Teremka Nayo ★★★

Mzee Ndasi hakukosea alizidisha bakola kwa johnkila sehemu ya mwili wake,usingizi ukampaa Johnalipotazama vizuri bakola zinapotokea akakumbanana babu yake aliyekuwa amekunja matuta kadhaausoni huku akitukana matusi mengi yaliyokuwayanamfikia john barabara.

Fimbo yote iliishia katika mwili wa John kisha mzeeNdasi akamsogelea john"Hauna akili wewe kale katoto ka mzee Maziumekapendea nini? eeeh! si nakuuliza?""Tulia sasa babu kumbe nd'o kisa cha kunipiga'' alijibu john "Nitolee ujinga wewee! huna adabu kabisa we ni wakunidhalilisha Mimi wewe laaaah!""Hapana babu haujanielewa tu Mimi nampenda yulebinti babu tena siongopei kabisa"Mzee Ndasi baada ya kusikia maneno yale kiliokikaanza kumtoka huku akiongea kwa uchungu nakama ungekuwepo ungetambua kuwa kumbepombe sio chai"Yaani na taabu zote nilizopitia kukulea wewe mpaka umekua unataka uniongezee mzigo mwingine tena na uzee huu" Alilalamika mzee Ndasi"Hapana babu kama sisi tunaweza kula Milo mitatukwa siku sembuse huyo mmoja atakayeongezeka?"alijibu Humph kiurahisi"Nadhani haujui gharama ya Mke wewe afadhalihata ungeuliza kwanza ni vitu gani unavyotakiwakuwa navyo na si kukurupuka""Babuuuu, aaah! mbona bado sijachelewa maanasijamuoa bado kwahiyo utanielekeza si etibabuu,basi nyamaza babu yangu yaani unachukiavitu vidogo vidogo vya kuviweka sawa dakika sifuribwana." John alimpoza babu yake "We mtoto umezidi kwakweli ni bora hata wazaziwako wangekuwepo huenda ningepataa unafuu wakukulea."

Mzee Ndasi aliongea huku akifuta machozi"Babu naye ni maneno gani sasa hayo,inuka ukalalebasi."John akamshika mkono mzee Ndasi na kumsaidiakumuinua, kwa mwendo wa taratibu walielekeachumbani kwa mzee Ndasi na kufanikiwa kumlazamzee yule kitandani.Mzee Ndasi alianza kukoroma punde baada yakuulaza ubavu wake.John alirudi chumbani mwakena kuanza kujikagua alama za fimbo,alikuwaamevimba sehemu zote alizokuwa amechapwa nababu yake.John alishindwa kulala kabisa,alikuwa akiwaziamaneno ya babu yake kuhusu Amina,hakujilaumukumpenda binti yule kwani tayari alishazama vilivyomoyoni mwake ila alilaani Maisha ya umaskinikwani hayo pekee nd'o yanataka kumkosesha penzilake.

Hatimaye asubuhi iliwadia ikiwa na anga linalong'aalikiashiria ni siku njema,lakini usisahau kuwa johnaliianza siku hii vibaya toka alipochapwa na babuyake.★★★★★★★★★★★Mzee Mazi hakuwa na raha tangu alipoamka,alikuwaakimfikiria binti yake ambaye hakuwa na umriunaompasa kuolewa hata kidogo ila kutokana naufinyu wake wa akili na uelewa mdogo alikimbiliavitu vinavyomzidi uwezo.

Mbaya zaidi binti yake Amina along'ang'ania familiaisiyokuwa na chochote kitu,familia inayosadikikaimejaa vimbwanga vya uchawi usio eleweka.Kiukweli ilimuuuma haswaa hadi.ikafikia mahali akili yakeikagota kufikiria njia sahihi ya kumtoa Amina katikajanga lile akabaki akilaani tu kwanini amezaa mtotokama yule asiyeshaurika wala kuambilika.Mzee Mazi alikuwa amejishika shavu akiwaza nakuwazua yanayomsibu na wakati huo huo bi Mazinaye alikuwa amesimama mlangoni akimtazamamzee Mazi anavyotingisha kichwa kwa masikitikona majuto mazito."Mme wangu,mme wangu,Mme wangu si nakuitajamani?" aliiita bi Mazi lakini wapi, mzee Mazialikuwa katika dimbwi zito mno la mawazo ni kamaanaangalia tamthilia inayokonga moyo wakekutokana na.matukio yalivyopangiliwa.Sasa bi Mazi akasogea taratibu pale alipo Mmewake, alipofika mbele yake bado mzee Mazi hakuwana hili wala lile, Bi Mazi akastajaabishwa sana nahali ya mumewe ikambidi apunge mkono mbele yamacho ya mzee Mazi lakini haikusaidia,akaupitishajirani na macho ya mzee Mazi wala mzee huyohakustuka.

Bi Mazi alihuzunika mno ndipo kwa hasiraakamshika mzee Mazi kwa nguvu "We mzeeMazi",kwa spidi ya ajabu mzee Mazi aliruka kwamstuko alioupata"Tutauana kwa presha bureeee!" aliongea mzee Mazihuku akihema mno"Looooh!! we mwanaume unatatizo gani mbonawanitisha mno?" Aliuliza Bi Mazi"Mwanao,mwanao ananipa mawazo mno sijuinifanye kitu gani ili aachane na huyu john." aliongeamzee Mazi kwa mfadhaiko mkubwa"John, john, john, ni nani mpaka akukoseshe rahakiasi hicho au kisa Yule babu yake.kigagula nd'ounamuogopa?""Hapana sio huyo Mzee tatizo ananiharibia mwanangu angali mbichi kabisaaa."

"Sasa unashauri tufanye nini?" Aliuliza bi Mazi"Sielewi kwakweli nahisi kuchanganyikiwa.""Mwanaume akichanganyikiwa na mwanamkeafanye nini?" Alisema bi Mazi"Unaanza kunikoroga sio, nitahamishia hasira zangukwako sasa hivi au umenisahau eeeh!""Samahani mme wangu nimekosea."alijishusha biMazi"Eti samahani Mme wangu nimekosea,kama haunala kusema unitokee hapa" alirudia kauli ya ni Mazihuku amebana pua"Sawa Mme wangu, Nina wazo hapo ili tumkomeshehuyo John"Mzee Mazi akakodoa macho akimtazama bi Mazi"Atii umesema!!! hebu nidokeze kidogo"Bi Mazi akamsogelea Mme wake na kumuuma sikio(kumnong'oneza)"Nd'o maaana nakupenda mke wangu una akili mnokama yule paka wangu wa zamani." aliongea mzeeMazi akiongeza na utani kwa mkewe"Mmmh! lione mfyuuuu!!!" alisema bi Mazi nakumfyonza hali iliyosababisha Mzee Mazi ainuke nakuanza kumkimbiza bi Mazi aliyekuwa akikimbiliandani,walionekanà kama watoto ama vijana ambaond'o kwanza penzi lao limeanza kuchanua hakikawalifaana.

John matatani, nini kitamkuta? Usikose sehemuzinazofuata.
 
Sehemu ya tatu

★★★Ilipoishia★★★

"Mmmh! lione mfyuuuu!!!" alisema bi Mazi nakumfyonza hali iliyosababisha Mzee Mazi ainuke nakuanza kumkimbiza bi Mazi aliyekuwa akikimbiliandani,walionekanà kama watoto ama vijana ambaond'o kwanza penzi lao limeanza kuchanua hakikawalifaana.

★★★Endelea Nayo★★★

Mzee Mazi alipoingia ndani akafunga mlango ilimke wake asimpige chenga na kutoka nje.★★★★★★★★★★Upande mwingine wa asubuhi hii Mzee Ndasialiamka akiwa mchovu kuliko kawaida nadhani nikwasababu alipata machozi ya simba Jana yake,alikuwa akipiga miayo hovyo kila alipokuwa akipigahatua kadhaa.Kama ilivyo ada ya pombe kali, Mzee Ndasi alisurubiwa haswaa na njaa iliyotokana na.pombehali kadhalika kwa walevi wengine ambao wakiamkacha kwanza ni kutafuta supu iliko.

Hii ilikuwa tofauti kwa mzee Ndasi ambayealielekea moja kwa moja katika jiko lake la kuni nakuanza kutafuta tafuta mwenye vyombo akiwa nalengo la kupata walau kiporo atulizie njaa ile yaasubuhi. Hakuwa na jipya tena baada ya kukosa kiporoalichoamua ni kukusanya kuni na kuwasha moto nataratibu za kupika ugali zikaanza Mara moja bilakujali kama ni asubuhi au la! Muda wote huo John alikuwa ameelekea shambanikusafisha safisha kwaajili ya kilimo cha msimuhuo.John akiwa shambani akili yake yote ilikuwaikiwazia jinsi ya kumdhibiti Amina katika mikonoyake bila kujua kama usipo uwahi muda basi mudautakuwahi weweJohn alipohakikisha amemaliza kazi zake akarudinyumbani mapema na kumkuta babu yake akiwaametulia kwenye kiti chake cha "Laza mgongoupumzike" nafikiri wengi wenu mnavifahamu viti hivivinavyotumiwa mara nyingi na wazee.

John alimsabahi babu yake ambaye hakuoneshachuki yoyote wala uwepo wa hasira alizokuwa nazoJana yake mpaka akamchapa John.Kama kawaida na desturi za nyumbani kwa kinaJohn mtu yeyote kati ya john na babu yakeasipokuwepo wakati chakula kinaandaliwa basi hanachake hii ilifananishwa na kale kamsemo ka"usicheze mbali unga robo" hivyo John aliporudihakuhangaika kumuuliza babu yake kuhusu chakulaalichokifanya ni kuingia jikoni nakuanza kupika.

"Amina mama njoo" aliita bi Mazi"abeee! mama nakuja" alijibu Amina"Niliongea na baba yako kuhusu huyo john wako natukafikia muafaka kuwa una haki ya kuwa nayewakati wowote ule unapohitaji""Asante mama sijui nikupe nini mama yangu"Aliruka kwa furaha Amina akimshukuru mama yake"Usijali wewe ni mwanangu wa pekee sipaswikukuona ukipata tabu ya aina yoyote ile,ilanimekupa ruksa kufanya hivyo kwa sharti moja tu""Lipi hilo mama yangu?""Leo hii unatakiwa kwenda kwa john usiku nasitutakuja huko kwaajili ya kuidhinisha muwe pamojasawa mwanangu""Nitashukuru sana mama yangu mkifanya hivyongoja nijiandae mapema kabisaa"Bi Mazi alitoka ndani na kumfuata mume wakealiyekuwa ameketi katika kivuli akipunga upepo"Baba Amina ule mpango umefanikiwa, sasa wejiandae mapema umpe na taarifa mjomba wakeAmina ili tukawakomeshe hawa watu usimsahaumwenyekiti eeeeeh!" alisisitiza Bi Mazi"Palipo na hela hamnaga msahaulifu bwana lazimanikumbuke kila kitu."★★★★★★★★★John akiwa amepumzika ndani Mara mlangounagongwa kwa mtindo wa kipekee sanauliomfanya John atambue kuwa mgongaji niAmina.

Kwa haraka akakimbia kwenda kufungua nakukumbana na kumbatio la aina yake"We Amina ni nini kimekuleta usiku huu""John hata bila salamu kwa mpenzi wako nimambo gani haya unayonifanyia lakini""Tatizo hatukuwa na miadi ya kukutana tena usikuunadhani wazazi wako wataniacha kweli?""Nawe nae umezidi uoga loooh!! janaume zima""Sio uoga Amina baba yako namfahamu fika nimkorofi""Hebu njoo huku kwanza" Amina alimvuta Johnwakizama ndani kabisa ya chumba cha john

Je, unafikiri ni kwanini Amina alitangulizwa, au unahisi ni kamchezo gani ambako John anachezewaYote hayo utayapata katika sehemu inayofuata.
 
Sehemu ya Nne

★★★ilipoishia★★★

"Hebu njoo huku kwanza" Amina alimvuta Johnwakizama ndani kabisa ya chumba cha John

★★★Endelea nayo★★★

John hakuwa mbishi tena kwa madai ya kuwa yuleni msichana na ndipo udhaifu wake ulipo piaalifuata kale kamsemo ka "fuata nyuki ule asali"Amina alikuwa amejilaza kitandani kwa John tenapembeni kabisa na john,kwakuwa siku hiyo alikuwana furaha alizipunguza nguo zake (kuziondoa) baadhi na kuwa huru kwa john "Amina una nini kimekuingia Leo mbona sikuelewi?"aliuliza John"Utaelewa tu, kwanza Leo Nina bonge lafuraha,wazazi wangu wamebali niwe na wewe namuda si mrefu watafika hapa" Aliongea Amina nakuinuka kitandani Kisha akaanza kujigeuza geuza na kunesa nesa kama wasichana wanaogombea umisi."weeeeeee!! unasema nini?,aaaah!! Nimekwisha Mimi" aliongea John kwa huzuni na mshangao mkubwa.

"Mbona sikuelewi john jamani,ina maana wewe haujafurahia wazazi kukubali mshusiano yetu" Safarihii Amina aliongea akiwa hajiamini na furahaaliyokuwa nayo ilisambaratika ghafla"Hataa!! si hivyo unavyofikiri Amina Mimi nakupendasana lakini unafikiri wazazi wako wanakuja kufanyanini huku na inawezekanaje wakubali kirahisi hivyomahusiano yetu ikiwa wao nd'o walikuwa watu wamstari wa mbele kutupinga,eeeh!! hebu fikiri"alifafanua john hisia zake"Hapana john mama hawezi kunihadaa, haiwezekani""Ohoooo!! kumbe haunipendi eti, mi najipenda sanasasa hatuna muda vaa nguo twende nikutoe hapakabla wazazi wako hawajafika" alizungumza johnakiwa tayari ameivaa sura ya kaziLakini kabla hata john hajatimiza alilokusudiamlango ukagongwa, akatazamana na Aminaikionesha kila mtu anaogopa sasa huku wakitupiana macho yale ya nenda wewe ukafungue Mlango ulizidi kugongwa tena kwa fujo kulikomwanzo,akili ya john ikaanza kuzunguka kamasekunde zinavyokimbia kwenye saa.

John aliufuata mlango kwa ujasiri wote kishaakauliza "we nani usiku huu""Mzee Mazi hapa" ilisikika sauti ikijibu kutokea njeMoyo wa John ulipiga paaaaaaaa!!! nguvuzikamuishia akajua tayari amefumaniwa sikuhiyo,john hakukubali kirahisi vile akaufuata ukuta wachumba chake lakini hakukuwa na dirisha lakusema atatokea hapo kwani dirisha lililokuwepo nindogo mno nalo lilikuwa karibu na mlangomuda wote huo Amina alikuwa amesimamaanashangaa anachotaka kufanya John,Johnaliuchunguza ukuta na kufanikiwa kuona mwanya mdogo maeneo yenye mbao ila hizi nyumba zamajani ziliwekwa miti wanaiita fito ambayo ilitumikakama kenchi,Akajirusha kidogo na kuukamata ukutabarabara.

Amina akabaki tatu bila juu ya kitendo cha johnikambidi apige kelele "John anataka kutoroka baba"John alivyosikia vile akashuka chini na kumnasakibao Amina na kumtolea vitisho asipige kelelekisha akarudi na kupanda tena ukuta na kufanikiwakujivuta juu ambapo alipitisha kichwa kwenye ulemwanya,mkono mmoja akashika fito akainua juu nailikuwa rahisi kwasababu fito hazikushikana na ukuta Kwa nguvu zote john akafanikiwa kupata nafasi yakupita,alipopitisha mgongo na kufika kiunonimikono ikashindwa kuhimili uzito uliopo ikaachiafito zile na kusababisha paa la nyasi limbane kiunoJohn akaanza kupiga kelele "Nisaidieninakufaaa,jamani msaada nakufaa"Mzee Mazi na shemeji yake wakazunguka nyuma yanyumba na walipomulika wakamuona ni john,ndiposhemeji yake mzee Mazi akarudi mbiomlangoni,Huwezi amini Amina alikuwaamechanganyikiwa Mara afunue kitanda mara arudimlangoni mpaka pale aliposikia sauti ya mjombawake akimwambia "Amina, Amina, fungua mlango "Unafikiri John atapona kweli? Fumanizi si mchezo.
 
Sehemu ya Tano

★★★Ilipoishia★★★

Mzee Mazi na shemeji yake wakazunguka nyuma yanyumba na walipomulika wakamuona ni john, ndipo shemeji yake mzee Mazi akarudi mbio mlangoni, Huwezi amini Amina alikuwaamechanganyikiwa Mara afunue kitanda mara arudimlangoni mpaka pale aliposikia sauti ya mjombawake akimwambia "Amina,Amina,fungua mlango"

★★★Endelea nayo★★★

Amina akakimbilia mlangoni na kufungua mlangotahamaki!! mjomba mtu akabaki amebung'aaa(kupigwa na bumbuwazi) baada ya kuona Amina yukonusu uchi"Mmmh! " ilisikika sauti ya mguno kutoka kwamjomba wake Amina huku akimtaza vizuri Aminabila kukwepesha macho na hapo ndipo Aminaakagundua kuwa hajavaa, kwa haraka akarudi ndanimbio na kuchukua kipande cha kanga alichokujanacho na kujifunga,ikawa ahueni kwa mjombaaliyeamua kupotezea lile suala na kumfuata johnambaye bado alikuwa akining'inia ukutani hukuamebanwa.

Cha kwanza alichokifanya mjomba wa Amina nikumuonja john kwa makofi ya makalio yaliyomfanyajohn azidi kupiga makelele ya kuomba msaadaMpaka bi Mazi na mzee Mazi wafike John alikuwaamekiona cha mtemakuni,Amina alikuwaamesimama pembeni ya kitanda akitetemeka.Mzee Mazi na shemeji yake walianza jitihada zakumnasua john mpaka wakafanikiwa kumshushapale alipokuwa amening'inia.Muda huo huo mwenyekiti wa kijiji aliwasili akiwana kidaftari kidogo na biki mkononi Mjomba wa Amina alizidi kula sahani moja na Johnalimkarisha chini kwa makofi,japo john alikuwa nimbishi ila siku hii alimkuta mbishi zaidi yake nakatika siku ambazo john aliwahi kuambulia vibaovingi ilikuwa ni siku hiyo.

Mwenyekiti kwa mbwembwe zote akatoa simu yakeya Nokia zile za tochi akaanza kummulika johnusoni"Bwana mdogo naona ulikuwa ukifaidi matunda yamwenye shamba kiwizi wizi na mwisho wa sikuukanogewa ukasahau kuwa za mwizi arobaini"alisema mwenyekiti"Mbona maneno mengi mwenyekiti mpe asainikama tumemfumania na binti yetu ili tujue mipangoya kesho bwana" aliongea bi Mazi kwa uvivuuliotawaliwa na usingizi"Kijana nafikiri mkamatwa na ngozi ndiye mlanyama na sidhani kama una la kujitetea ikiwa bintimwenyewe tumemkuta katika hali hiyo hiiikiamanisha ni mtu wako hivyo kwa usalama wakoinatakiwa ufuate kile nitakachokwambia kishamengine tutamaliza kesho" aliongea Mwenyekiti kwamsisitizo"Sawa" aliitikia john kwa sauti ya mtetemesho"Andika hapo Mimi john nakiri kukutwa na Aminabinti wa mzee Mazi na kama kuna lolotelitakalotokea au kuhusiana na binti huyu nitahusika"alisema mwenyekiti"Jamani twendeni hatuna la ziada hapa". alisemamzee MaziWaliinuka na kuondoka wakimuacha john naAmina,John hakuwa na hamu ya kumtazama Aminaaliinuka pale chini alipokuwa amekaa na kwendakujilaza kitandani .

Amina naye alijua kuwa amemuudhi john wakehivyo hakuwa na jipya zaidi ya kujilaza miguuni mwaJohn ikawa ni kulala mzungu wa nne.Asubuhi na mapema Amina aliamka na kuanzakufanya usafi ili tu kumridhisha john,huwezi aminikwamba john hakupata hata lepe la usingizi tokakindumbwe ndumbwe kimkute.Mzee Ndasi alipoamka akapokelewa na ugeni wabinti Amina ambaye alikuwa akiendelea na usafi,hiiikampa wasiwasi mzee Ndasi maana hakuzoeakumuona binti Amina akiwa.

Nyumbani kwakeakijaribu kufanya kitu kama kile.Wasiwasi ukamjaa mzee ndasi machalr yakamchezakuwa tayari kuna kitu kisicho cha kawaidakinaendelea,taratibu akamfuata Amina nakumsemesha"Hujambo binti"Amina alistuka kuisikia ile sauti na kwa uogaakajikakamua kujibu"Sijambo shikamoo babu""Marhaba,mwenzio yuko wapi?""John!,aaah! John bado amelala""Aya endelea na kazi".

Mzee Ndasi alijitahidi kuzificha hasira zake kwanilengo alilokuwa nalo ni kumfukuza binti yule ilanafsi yake ikagoma akaona bora amfuate john iliajue kuna kitu gani kinachoendeleaMzee Ndasi alipoingia chumbani kwa john,johnalikuwa ameshaupata usingizi alioutafuta kwamuda.mrefuKwa busara zote mzee Ndasi akaanza kumuamshamjukuu wake kistaarabu kabisa kwa kumtikisakidogo kidogo ili aamke lakini balaa alilokutananalo alistaajabu mnoJohn alifikiri ni Amina.anajaribu kumuamsha ilihaliameshamsababishia matatizo kama Yale yasiyotarajiwa,akaanza kuropoka"Hebu niache nilale we mjinga wewe, uliyonifanyia yakuwaleta wazazi wako wanifumanie na wewehaijatosha unataka na usingizi niliouhangaikianikupatie nao eeeh!! huoni haya wewe hebu niachebwana inatosha kwa uliyonifanyia...?"mzee Ndasi akaelewa ni kitu gani kinachoendeleampaka pale sasa hakutaka tena kumuamsha johnkwa ustaarabu akaanzisha vibao ili John aamke kwalazima na sio kwamba aliamua kumuamsha kwamtindo.ule la! bali ni hasira zilizokuwa zikimfurukutakifuani mwake ndizo zilipelekea aanze kumpiga vibao.

"Amka mbuzi wewe, pamoja na kukuimbia wimbokila siku kuhusu huyo binti lakini haukusikia sijuiuna masikio ya kenge we mtoto ambayo kusikiampaka yavuje damu eti,kwanini lakini eeee! sinakuuliza una masikio ya kenge?"John akakurupuka akiwa ametoa macho baada yakugundua kuwa Yale maneno yote aliyoyaongeaamemwambia babu yake.Wakiwa wanaangaliana kama majogooyanayopambana kwa hasira huku kila mmojaakitaka kumuotea mwenzake wakasikia watuwakibisha hodi nje, ikabidi wote watazame nje kishawakageukiana na kuangaliana kila mmoja akiwa na mshangao kuhusu wageni wale.
 
Sehemu ya Sita

★★Ilipoishia★★

Wakiwa wanaangaliana kama majogooyanayopambana kwa hasira huku kila mmojaakitaka kumuotea mwenzake wakasikia watuwakibisha hodi nje,ikabidi wote watazame nje kishawakageukiana na kuangaliana kila.mmoja akiwa namshangao kuhusu wageni wale.

★★Shuka nayo★★

John alikuwa akitambua kinachoendelea lakiniakakauka kimya,mzee Ndasi akatoka nje kwendakuwasikiliza wageniLoooh!! alistuka baada ya kukuta ni familia yaAmina pamoja na mwenyekiti,alichoka akijua kiamakimefika na kwa sauti iliyoonyesha kupoozeaakawakaribisha na bila kuchelewa Amina alikujaharaka akiwa na kirago cha kukalia wageni wake."Aisee!! naona umekuwa mwenyeji kabisa wamazingira haya" alisema mwenyekiti Amina kwa aibu akainamisha kichwa bila kujibu"Karibuni wageni sijui kuna tatizo gani?" aliongeamzee Ndasi akiwa.mwingi wa mashaka"Asante,binafsi sina muda wakupoteza ni kwambakijana wako alifumaniwa usiku wa Jana akiwa nabinti wa mzee mazi na ndiyo maana umemkutaasubuhi hapa kwako sasa baada ya kumfumaniab

Wazazi wanahitaji haki yao maana kila kitu kikowazi" alifafanua mwenyekiti"Mmh!" aliguna mzee Ndasi"Sikia mzee mwenzangu ukiwa na kijana wa kiumetegemea uharibifu kama huo maana ni vijana wotena imeshatokea" alizidi.kupigilia msumari mzeeMazi"Nafikiri tuanze mjadala ili tufikie muafaka,naombaumuite kijana hapa" Mwenyekiti alitoa wazo lake"Sio mbaya kama Amina akamfuata,Amina hebumfuate mwenzio uje naye hapa" aliongea bi Mazikwa Mara ya kwanza Amina aliinuka pale alipokuwa ameketi na kuelekeachumbani kwa john,muda wote ule mamboyanaendelea john alikuwa anachungulia dirishani kilakinachofanyika pale nje mpaka mazungumzo yaoyalivyoenda huku akizidi kutetemeka kama mgonjwawa malaria.

Alipoona Amina anakuja akarudi kitandani haraka nakujifunika gubigubi akisikilizia matokeo"John,John amka unaitwa nje kuna kikao" aliongeaAmina kwa adabu"Tangulia nakuja" alisema john"Hapana john wamesema twende wote""Mbona msumbufu wewe alaaa!,nisubiri basi"alifoka john.

John akainuka na kufuatana na Amina,walipotoka tuwakakumbana na macho ya watu wotewakiwatazamajohn kwa Aibu akainamisha kichwa na kusogeampaka kikao kinapofanyika akatoa rai zake nakuketi pembeni"Kumbe kijana mwenyewe ana umri mzuri tu wakuoa" alisema mwenyekiti akiwa na tabasamu"Sasa kama tulivyoongea awali kijana ana makosahivyo sheria inasema mtu wa aina hii hulipa hela yamama mtu pamoja na Mali atakazopangiwa kamaatahitaji kuoa na Kama hana muda wa kuoa inabidialipie hizo hela za mama mtu" aliongezeamwenyekiti"Sawa lakini kabla sijajibu hilo suala naombanimuulize mjukuu wangu kama anamuoa huyu binti"Mzee Ndasi akatoka na john pembeni ili wajadili"John utamuoa huyu binti au""Kiukweli babu sitaki kusikia habari zake tena"

"Acha ujinga wewe hela zetu haziendi buree alafuukisema hauoi watataja hela nyingi kwa kutukomoakwahiyo wewe la msingi kubali kuoa tu maanahatuna jinsi""Aya babu Mimi nakusikiliza wewe tu""Mwenyekiti, kijana wangu anaoa hivyo fanyenitaratibu nyingine tumalize hili suala""Sawa tumsikilize mama Amina hapa" alijibumwenyekiti"Mimi sihitaji hela nyingi nataka laki saba tu"alisema bi Mazi aliangalia pembeni"Mmmmmh!! we mama unataka kununua ndegeau? hebu angalia na watu unaowatajia hicho kiasiama unamuuza binti yako" alisema mzee Ndasi"Mke wangu hebu punguza hasira kwanza" aliongeamzee Mazi"Hata mimi kama mwenyekiti siafikiani kabisa nakiasi hicho jaribu kuangalia hali iliyopo hapa kijijinina isitoshe mzee kama huyu atatoa wapi hizo helazote hizo".

"Kwani alipokuwa ananiharibia mwanangu hakujuakuwa nimemtunza kwa gharama mkubwa,basiwaseme wana kiasi gani?" alisema bi Mazi"Sisi tuna laki moja" alijibu mzee.Ndasi."Heeeeheeeheee!! unaona eeeeh!! si utani huumnaoufanya wee mzee nasema sitaki hela yenusasa na mwanangu nawaaachia ili tuonekama.mtafaidika kitu gani,mnaujua uchungu wakuzaa nyie etii laki moja,laki moja nayo ni hela hebujiheshimie we mzee"..
 
Sehemu ya Saba

*****ilipoishia******

"Heeeeheeeheee!! unaona eeeeh!! si utani huumnaoufanya wee mzee nasema sitaki hela yenusasa na mwanangu nawaaachia ili tuonekama.mtafaidika kitu gani,mnaujua uchungu wakuzaa nyie etii laki moja,laki moja nayo ni hela hebujiheshimie we mzee"........

★★Endelea nayo★★

"Mke wangu hebu punguza jazba,ni mambo ganihayo unayoyafanya mbele za.watu. tuliakwanza,tuliza hasira zako"Mzee Mazi alimtuliza mkewe."Huko ni kudhalilishana sasa tena mbele yamwenyekiti,tafadhali sana bi Mazi iheshimu serikalitena chonde Mimi nimeacha kazi zangu kule nakujahapa kuwasikiliza".

Mwenyekiti aliongea kwakukasirika"Si unaona sasa mke wangu tulizana basi ebooo!!"mzee Mazi alizidi kumtuliza mke wake"Mimi naona hapo mzee mwenzangu kwasababutunaunga undugu eeeh! tunakuwa ukoo mmoja siombaya kama mkajitahidi walau muongezee mpakakiasi cha laki tatu" mzee Mazi alishauri"Mimi sina neno hapo ila Kwakuwa sina helanaomba lile shamba langu nilikabidhi kwenu kwakiasi hicho mlichosema na pia hata mahali naombanikabidhi lile shamba langu la kule bondeni nalombaki nalo.na huyu mjukuu wangu Amina atabakihapa kuanzia Leo" Mzee.Ndasi alijitetea"Hilo halina shaka tuwape nafasi tu ya kujadili hawawazazi wa binti". alisema mwenyekit

Mzee Mazi na mke wake wakasogea pembenina kujadili"Umeona kiherehere chako,unapandisha dau nakuleta jazba mpaka mwanao ameombwa kubaki""Sio hivyo Mme wangu ila uchungu ulinishika kuonawatu wenyewe wanavyojipangia hela ndogo vile bilakujali magumu niliyopitia kwa yule mtoto,wemwenyewe ni shahidi si unaona alivyotusumbuampaka amekua""Aaaah! achana na hayo,huyo mzee kaingia kwenyemtego mwenyewe,tuchukue mashamba hayo""Mme wangu mtoto bado ni mdogo yule hawezikumudu nyumba kwanini tusiondoke nae""Hebu na wewe nikose utajiri kisa ujinga wenunipishe huko na ole wako.uongee"Mzee Mazi alirudi na kuketi kwaajili ya kutoahitimisho"Mimi na Mzazi mwenzangu tumeafikiana tuchukuehivyo vitu yaani tumuozeshe binti yetu kwahiyotuandikiane tu'' Mzee.Mazi aliongea kwa kuchekacheka huku mke wake akiwa anamkata kijicho hukuakisonya"Sawa nadhani hakuna haja ya malumbano kwasasa nyie ni ndugu""We mwenyekiti uniwie radhi sawa Mimi sinaundugu na hao watu,kwaherini" bi Mazi aliinukakama chizi na kuondoka eneo hilo akisonya Sonyaovyo.

"Achaneni naye huyo hapa mpo na baba mtuhakiharibiki kitu" mzee.Mazi alijitapaBaada ya mambo yote kuisha mzee Ndasi aliwekakikao.kidogo.na wajukuu zake wakijadili hali yaMaisha watakayoishi siku zote"Jamani ushirikiano ni kitu cha msingi,kwendashambani ni jadi hilo mliweke kichwani na kila mtuaitumie nafasi yake vyema,John umepata msaidiziyeye atapika wewe utatafuta chakula na malazi uvivuweka kando sawa""Nimekuelewa babu""Amina jisikie huru hapa ndipo nyumbani kwasasa""Sawa babu tupo pamoja"Huo ndiyo ilikuwa mwanzo wa John kumuoa Amina.

Zilipita siku na hatimaye mwaka Maisha yakazidikwenda mzee Ndasi akaugua ugonjwa usioelewekachanzo chair,john akajitahidi kwa hali na Mali lakinind'o kwanza ugonjwa ulizidi kupamba moto kilakukichaIlifika mahali hata wazazi wa Amina wakaacha kutoamsaada mdogo mdogo na mwisho wakawatengakabisa familia ya john kisa maneno mane noyakuwa eti mzee Ndasi ni mshirikina(kigagula)John hakuwa na jinsi alipitisha mchango kwawanakijiji lakini hawakumsaidia waliishia kumtengana kuinyanyapaa familia yake.Ikambidi john auze mashamba kumtibia babu yakelakini wapi hsikusaidia lolote,akabaki na shambamoja ambalo katu hakutaka kuliuza kwa vyovyotevile.Wakati wote huo Amina ndiye alikuwa tumaini lapekee kwa john kwa kumtia moyo kilakukicha.

Muda mwingine john alishinda akiliakutokana na changamoto anazopitia Maisha yalianza kuwa magumu kwa upande waomaana kila kitu hapo mwanzo walitegemeamashamba na babu yao katika mahitaji mbalimbali.na baada ya babu yao kuugua hali ikaanzakuwa korofi.Binti Amina alikuwa si mpole tu balimsikivu, muelewa na mtiifu kwa john vile vilehakuwa kama wasichana wengine yeye alimvumiliajohn kwa kila jambo.
 
Sehemu ya Nane

★★★Ilipoishia★★★

Binti Amina alikuwa si mpole tu balimsikivu,muelewa na mtiifu kwa john vile vilehakuwa kama wasichana wengine yeye alimvumiliajohn kwa kila jambo...

★★Teremka nayo★★

Haikuwa jambo rahisi kwa Amina lakini yotealichukulia ni mapito ambayo si ajabu watayashindamuda wowote na john wake.

★★Tulipoanzia★★
Baada ya Amina kumuita john ndani kamaalivyoagiza mzee Ndasi,Amina aliombwa atoke njeili wanaume wazungumze."John nafikiri umeteseka sana kwaajili ya babu yakona sasa ni muda wako wa kupumzika,hebu niinuekidogo"

Alianzisha mazungumzo mzee Ndasi John akamuinua babu yake na kumuweka aegemeemto wa kulalia"Utashangaa sana kwanini nasema haya yote,nahisiwakati wangu umefika wa kwenda kunakostahili""Usiseme hivyo babu bado una wakati mzuri tuwakupona""Hahahaha!! nashukuru Kwakuwa nimepata mjukuujasiri kama wewe, kuna baadhi ya vitu nilikuwanavyo humu ndani na sijawahi kukuonesha, koooh! koooh! kuna koti moja hapo kwenye kamba nimahususi kwa kufanyia lolote lile nilipewa na babuyangu enzi hizo, hilo koti linaweza kukubadilish amuonekano wako kwa mfano ukawa mtoto ghafla kwa mtu anayekuona au ukawa majani kama upo kwenye majani mengi, najua utashangaa lakini hata Mimi niliwahi kushangaa hivyo hivyo ila hii nisayansi ya zamani mno waliyotumia babu zetu""Sasa babu Mimi nitalitumiaje hilo koti katika Maisha yetu haya maana yamebadilika si kama Yale Maisha yenu ya zamani""Swadakta, una akili sana,hilo koti litumie kupatachochote katika milki ya mtu yoyote mpaka paleutakapokuwa na uwezo wa kujimudu na mkeo""kama ni hivyo haina shida babu sijui kama kuna kingine"

"Ndiyo kipo ni..ni...Ku...na....ki....tu.....ki....Me...ni....ka....ba" mzee Ndasi alianza kubabaika na mwishoakaanza kutoa macho"Babu,babu,babu sema basi ni kitu gani kilichobakiababu"kwa taabu mzee Ndasi akawa anakitahidi kuongealakini haikuwezekana ikabidi aoneshe kwa mkononao haukufika mbali ukalegea na kujiangukia ukawand'o mwisho wa mzee Ndasi.

John alibaki akipiga ukunga tu na kulia sana kwanimsaada pekee aliokuwa nao sasa umepoteleakusiko julikana hakika ilikuwa ni pigo moja kubwakwa john.Amina alivyosikia kilio akajua tayari kimeeleweka,taratibu akamfuata mumewe na kuanza kulia naye kwawakati huo ambao.ulihesabika kama kipindi kigumumno kwa johnWanakijiji ambao ni majirani walikuwa wakisubirisana tukio hilo kwa hamu kubwa hivyo waliposikiavilio walitoka mbio kwenda kujihakikishia kama nikweli kimetokea kile walichokingoja.

Taratibu za msiba zilifanyika na kama tunavyoelewahata kama marehemu alikuwa ni jambazi watuhusahau kwa muda mabaya yake na kumsemeamema tu huenda huwa wanafanya hivi ilikumsindikiza marehemu kule aendako.John alikuwa akitia huruma wakati wote akitafakarini jinsi gani basi anaweza kumtunza amina,kilamuda alikuwa akitokwa na machozi,watu walifikirihuenda anamkumbuka babu yake kumbe hakuwa nadira maalumu ya kuyaendesha maisha Yale ikiwahata mashamba yalishauzwa na kubaki na shambamoja tu na kilichomliza zaidi ni hicho kipindiambacho nd'o kwanza kiangazi kilikuwa kimeanzakukolea.Hakika john alikamatika,njia rahisi aliyoiona nikwenda kwa wazazi wa Amina kuomba msaadawalau wa fedha ama chakula cha kuwasukuma sikukadhaa"John,karibu sana mwanangu karibu" Alikaribishamzee Mazi"As ante baba,habari za muda huu" Johnalisalimia.kwa heshima"Safi tu sijui.huko ulikotoka""Ni salama mzee wangu""Eee! Sisi tupo tupo bwana,alafu mbona ni kamauna mawazo sana unajua ile ni kazi ya Mungukwahiyo haupaswi kuwa na majonzi kiasi hicho lamsingi piga moyo konde sawa""Ni kweli kabisa baba yote nimemuachia Mungu piakuna jambo lililonileta mzee wangu,hapa niliponaumiza kichwa nitaishije maana pesa zote mazaona akiba ya chakula tuliuza ili kumtibia babu hivyotafadhali naomba unisaidie walau katika hizi sikungapi niweze kupata pa kuanzia au nimrudisheAmina asije kudhurika ikiwa..wazazi wake mpo"John aliongea huku akipiga magoti"Hapana mzee haustahili kufanya hivyo kwangu piasamahani maana Mimi na mama yako tumepangatuuze mazao haya tununue bati si unaelewa hapakijijini ukiwa na nyumba ya bati unaonekana tajiriFulani hivi ila nitakusaidia kiasi kidogo cha fedhakikusukume siku mbili tatu wakati unajipangamwanangu asife na njaa""Asante baba nashukuru kwa msaada wako"

Johnalisema huku akiangusha machozi na kujisemeamoyoni ama kweli wanasema "kua uyaone" yaanikisa bati sisi tukose msaada hata wa gunia moja lamahindi"hiki kiasi kitakusaidia kidogo mzee na piaukumbuke kuwa wewe ni mwanaume pambanaamaana hata sisi kipindi tunaoa hatukuwa na msaadawa kulishiwa wake zetu tulipambana kufa na kuponasawa,we ni mwanaume usisahau hilo" Aliongeamzee Mazi kwa mbwembwe akiwa anamkabidhijohn shilingi elfu tano ambayo ilimfanya john azidikulia huku akisema asante.
 
Sehemu ya Tisa

★★Ilipoishia★★

Aliongea mzee Mazi kwa mbwembwe akiwaanamkabidhi john shilingi elfu tano ambayoilimfanya john azidi kulia huku akisema asante.

★★Shuka nayo★★

Mzee Mazi aliishia kutabasamu akiamini johnameufurahia msaada wake ambao.kwa johnulimpandishia mbegu mbaya ambayo kamwe.mzeehuyo hakuitambuaJohn alifika nyumbani kwake akiwa na huzuniambayo hata mkewe Amina aliitambua wazi waziikiwa si kawaida ya john kuwa vileKila.Amina alipojaribu kuuliza kinachoendelea johnalikatisha mada na kumfanya Amina atumie njiambadala ya kumtuliza mumewe mawazo.

Asubuhi na mapema john aliondoka nyumbanikwake na kumuachia Amina ile pesa anunue vileanavyoona vitafaa kwaajili yao siku hiyo.John alibeba koti kubwa aliloachiwa na babu yakena moja kwa moja akaingia nalo shambanikuangalia Kama litaendana na kile alichokiwazakichwani.

John alianza kazi akidhani koti lile litamsaidia walaukuongeza nguvu,alikuwa amejidanganya mno, mpakainafikia jioni hakuna alichokifanya zaidi ya kuchokakuliko kawaidaJohn akarudi nyumbani na kupokelewa naAmina,wakiwa ndani chakula kinaandaliwa loooh!!Amina alikuwa amepika wali john akashangazwa namapishi yale"Mke wangu nini hii mbona sielewi" aliuliza john"Aaaah!! Mme wangu si wali huu jamani".alijibuAmina akiwa na tabasamu pana"Asubuhi ulikula ni ni?""Nilipika chai na vitumbua,ndivyo nilivyoshindia"alijibu Amina kwa ujasiri"Mungu wangu nimekwisha Mimi" John alijisemeahuku akiegemeza kichwa chake ukutani"Ukioa mwanamke ambaye akili bado.haijakomaahapo ndipo utajua kwanini wanapiga marufuku ndoaza utotoni"John alichoka Mara tatu zaidi kuliko alivyotokashambani kwani hela aliyokuwa.nayo nd'o hiyoilinunua vitumbua na mchele,Hakuwa na jinsimwanaume huyu akajikakamua kula ule wali tenakidogo ili walau na asubuhi mkewe apate kidogoatelemshie na maji wakati anapiga hesabu za kipiafanye.

Cha ajabu John alipoinuka mke wake aliendela kulampaka akaumaliza wali wote hii ikionesha ni jinsigani Amina alivyoukosa wali kwa kipindi kirefu tenahakuishia hapo akachukua na sufuria lililobaki nawali kiasi akala wote na ukoko akaushambuliakama mtu mwenye njaa ya siku nyingi.

John alizidi kutoa macho kwa alichokiona,hakuamini Kama Amina anaweza kumaliza wali woteule,hapo ndipo john alikumbuka kamsemo ka akinamama eti "utakula ulikopeleka unga"Mawazo yalipandiana kichwani mwa John akainukataratibu akielekea chumbani ili kukwepa hasiraaliyokuwa nayo isimuishie Amina kipennzi chake.Hatimaye kulikucha tena john aliamka mapema sanana kuketi nje akipiga hesabu pakuanzia Maisha yasiku hiyo,wazo lake likaangukia katika duka la tajirimmoja wa kijiji chao,akaona bora akakope maanamuuzaji anamfahamu kwa sura.

Taratibu john akajongea katika duka lile akiaminilazima akopeshwe,alipofika mambo yalikuwa.tofautialikutana na askari mlangoni(kufuri) likimtazamakwa zamu ndipo akagundua kuwa ilikuwa bado niasubuhi sana hivyo akarudi tena nyumbani kwake iliavute muda.

John alimkuta Amina akiwa anafanya usafi kamailivyo ada,john akazama ndani na kujipumzishaakiwa anawaza na kuwazua hili na lile.Amina alikaa nje kwa muda mrefu mpaka mida yasaa nne nne hivi asubuhi akaanza kupigapiga.miayo ya hapa na pale mwisho akadhamiriakumfuata mume wake ajue hatma ya siku hiyo.Amina alipoingia ndani John alikuwa akimuona tubila kujishughulisha hata kumsemesha,Aminaakaketi pembeni ya John na baada ya kutazamanakwa.kipindi kirefu Amina akaanza tena kupigamiayo akiashiria njaa inamsakama.John aliligundua hilo ndipo na akili yakeikamrudisha dukani kwa tajiri kuwa atakuwaamefungua,john hakuona vyema kwenda vile vileakachukua koti lake kuu.kuu.na kulivaa akimuahidimkewe kuwa atarejea punde.

Duka la tajiri lilikuwa wazi mida hiyo john akasogeana kwasabahi wote waliokuwa palewakihudumiwa,baada ya wateja kuisha johnakajaribu bahati yake siku hiyo"Samahani bro naomba unikopeshe unga wa ugalikilo mbili na mafuta ya kupikia ya mia tano" Johnalijieleza"Unasema nini wewe unadhani naweza kukukopeshamtu Kama wewe kwanza sura ngeni alafu utalipa liniwewe kama sio kwenda jumla,hebu tutolee mikosiya asubuhi asubuhi wewe" alijibu muuzaji"Bro niamini nitaleta kesho isitoshe sisi ni wanaumeleo kwangu kesho kwako tafadhali nisaidie kwa Leotu"John alizidi kujitetea"Sina mdogo wangu kama wewe.potea sawa kablasijafanya maajabu hapa" alizidi kufoka muuzajiJohn hakuona haja ya kuendelea kukaa akageukaalipotokea na kuianza safari ya kinyonge ghaflaakasikia muuzaji wa duka akiitika na kuingiakwenye kamlango kadogo mle dukani.

Kwa wepesi wa ajabu bila kufikiri Mara mbili johnakaingia haraka mle dukani macho yakatua kwenyekisanduku chenye hela za noti tupu na pembenikulikuwa na sanduku lenye hela za vicheleJohn akainua sanduku lenye hela.za noti na kutokanje,wakati anatoka akapishana na mtu anaingiadukani na wakati huo huo muuzaji alikuwa akiingiadukani.
 
Sehemu ya Kumi

★★Ilipoishia★★

John akainua sanduku lenye hela.za noti na kutokanje,wakati anatoka akapishana na mtu anaingiadukani na wakati huo huo muuzaji alikuwa akiingiadukani.

★★Endelea nayo★★

Yule mtu alikuwa ni mteja akaomba anavyohitajihuku kila Mara akiangalia nyuma alikopoteleaJohn,Muuzaji alipotaka kuweka hela akatahamakikuona hakuna kisanduku cha kutunzia zile fedha."Nimeibiwa,nimeibiwa,nimeibiwa jamani" alianzakuongea ovyo ovyo yule muuzaji"Tulia kwanza wewe umeibiwa nini?" aliuliza mteja"Sanduku la kuwekea fedha na zipo nyingi mle""Yawezekana ni yule kijana niliyepishana naye hapa"alijibu mteja"Yuko wapi,yuko wapi huyoo tumfuate""Twende huku"Wakatoka na kuanza kukimbia kuelekea upande ulealiopita John, John alikuwa anatembea mwendo waharaka huku akigeuka Mara kwa Maranyuma,alipoona watu wanakuja mbio akapatwa nawasiwasi akaongeza mwendo mara dufuMuuzaji wa duka na mteja wake wakafanikiwakumuona john wakaanza.kupiga kelele "Mwizihuyooo,mwiziiii,mwiziiiii,mwiziii"John aliposikia vile akaanzisha kukimbia,watu wakaribu na eneo lile nao wakaanza kumkimbiza johnhuku wakipiga kelele "Kamata mwizii huyooo"John alikimbia kadri ya uwezo wake lakini kitukilichomsumbua ni kwamba hakuwahi kufanya tukiokama lile na hakuwa mzoefu kabisa wa kaziile.Alikimbia sana mpaka akahisi ulimi unatakakuanguka kwajinsi ulivyotokeza nje kama mbwaJohn alifika mahali akasimama apumzike,akiwaamesimama ghafla akakoswa na kipande cha tofalikilichopiga jirani yake ukutani,akaanzisha tenakukimbia aokoe Maisha yakeAkiwa anakimbia akakumbuka kuwa babu yakealisema koti lile linaweza kumbadili mvaajimuonekano,pale pale akabadili muelekeo nakuufuata uchochoro wa nyumba za pembezoni mwaBarabara.

John alipofika kwenye kona akakunja ghafla kishakwa haraka akafunga vishikizo vya koti lake kubwana kuanza kurudi alipotokea akiwa anatetemekamnoWatu wote waliokuwa wanamfukuzia john walifikana kupishana na john aliyekuwa akiendelea na safariya kurudi kwake.

Mtu wa mwisho kukutana na john alimuuliza "wemtoto watu wanaomfukuzia mwizi wamepita wapi?"John alishangaa kuitwa mtoto,hakutaka kuongeaakanyoosha mkono wake kuonesha sehemuwalipoelekea naye akazidi kutokomea.John alipofika nyumbani kwake alimkuta Aminaakiwa amekaa kivulini,john akanyata mpaka ndanina kuficha sanduku lile kisha akatundika koti lakehuku akijipongeza kwa kazi nzuri aliyoifanyaijapokuwa.muda.wote huo alikuwa akitetemeka kwauoga.John alitoka na hela mkononi akamfuata mkeweAmina"Totooo!! mambo?". John alisalimia kwa bashasha"Poa tu vipi mbona unafuraha hivyo kulikoni?" Aminaaliuliza"Aaaah!! ni kawaida tu shika hii,kanunuevinavyohitajika Leo hakikisha unanunua vitamuvitamu alafu kesho utaenda kusaga sawa" johnalisema akiwa na tabasamu lile lile"Mmmh!! John umezipata wazi hela zote hizi" Aminaaliuliza akiwa ameshika shilingi elfu thelathinimkononi"Shhhhhh!! Fanya niliyokuagiza" Alijibu johnAmina hakuwa mbishi kwa hilo alibarikiwa na walahakujihangaisha kumuuliza tena John yeye alifanyavile alivyoambiwa.

Siku hiyo nyumba ya john ilichangamka vilivyo hatapanya nao walilishuhudia hilo kwani waliwezakupata ahueni ya makombo yaliyoachwa ikiwa sikawaida ya watu hao kufanya vile.Hatimaye furaha ya siku chache ikaanza kufifia yotehiyo ikiwa ni kutokana na pesa kuanza kuisha,Johnalikuwa tayari amepiga hesabu ndefu kuhusuupatikanaji wa hela nyingine.Kwakuwa alifahamu vyema kuwa baba Amina ndiyealiyesababisha Maisha yao kuanza kwenda kombobasi lazima ahakikishe anamkomoa.Siku hiyo Amina akiwa hana hili wala lile Johnaliingia ndani mwake na kutoa lile sanduku lafedha,akaanza kuzihesabu mpaka alipofanikiwakuipata idadi kamili ya fedha alizonazo.

Cha kwanza akafikiria kujenga nyumba ya vyumbaviwili lakini hakuona Kama ni sawa kwani watuwataanza kumfuatilia ni wapi alikotoa hela kijanamdogo kama yeye asiye na kazi maalumu.John akachukua maamuzi magumu akatafutamakazi kijiji kinachofuata ambacho kilikuwa nauafadhali kuliko kijiji chao akanunua nyumba ya batiyenye vyumba viwili kisha akarejea kijijini kwao.

Amina hakuwa na hili wala lile kuhusu John yeyealifikiri kuwa john amepata kazi na ndiyo maanaalikuwa akipata hela inayowatosha kiasi kile.John alianza kumfuatilia mzee Mazi ili wamalizanedeni lao,kwa bahati john alifanikiwa kumuona mzeeMazi akiwa na wageni kadhaa,bila kupoteza mudaakawafuata pale walipo na kuanza kujipendekezakwa mzee Mazi ili ajue kipi kinachoendelea katiyao.
 
Sehemu ya Kumi na moja

★★★Ilipoishia★★★

John alianza kumfuatilia mzee Mazi ili wamalizanedeni lao,kwa bahati john alifanikiwa kumuona mzeeMazi akiwa na wageni kadhaa,bila kupoteza mudaakawafuata pale walipo na kuanza kujipendekezakwa mzee Mazi ili ajue kipi kinachoendelea katiyao.

★★★Shuka nayo★★★

Mzee Mazi hakuwa na hili wala lile nd'o kwanzaalimtambulisha john kama mkwewe na piaakamuelezea john siri ambayo ilikuwa ikitendekakati yao,Mzee Mazi alikuwa amelinadi shamba lakemoja ili apate hela ya kununua jenereta kwani kijijichao hakikuwa na umeme na tayari mzee Mazialishanunua runninga kwaajili ya kupata mambomotomoto ulimwenguni.

John alimpongeza tu huku akijitahidi kujua sikuwanayokabudhiana pesa hizo,haikuwa mbali balikesho yake mchana shambani kule kule ndipoilitakiwa wakakabidhianeJohn alimeza mate kweli kweli akiomba sikuzikimbie kama mvua ili awahi mechi ile adimu,Hakuchi! hakuchi! sasa kulikucha john akiwaamejiandaa vilivyo kumpora baba mkwe wake,Mzee Mazi zee lenye roho ngumu,alikuwa amewasilishambani na wanunuzi wake,kwa Mara nyingineakatembea nao kuwaonesha mipaka ya shambalake,wakafanikiwa kuandikianaMuda wote huo John alikuwa amejibanza kwenyekichaka akiangalia mambo yanavyokwenda. Mzesmazi alipozipata hela mkononi akaaga pale paleakiwaacha wanunuzi shambani bado wanakaguakagua.John alijihesabia ushindi wazi wazi akaanzakumfuatilia mzee mazi ambaye toka ametokashambani kwake hakugeuka hata robo kuona naniyupo nyuma yake.

Hatimaye John alipata upenyo wa kumpora mzesMazi alichokifanya ni kumuwahi mzee Mazi kwakabali ya mbao na mkono ukawahi mapemakuchomoa bahasha aliyokuwa ameihifadhi mzeeMazi mfukoni na kuitia katika koti lake kishaakamuongeza mzee Mazi kabali kwa nguvu zotempaka mzee yule alipoanza kutapa tapa kwakukosa hewa.

Lengo la john halikuwa kumuua baba mkwe wakeau kumuumiza bali alitaka kumkomesha kwakumrudisha nyuma kimaendeleo.John alimtanguliza mzee Mazi kwa teke mubasharalililomuangusha mbele na kumpatia john nafasi yakukimbia.Mzee Mazi aliwahi kuinuka na kuanza kupigaukunga huku akimfuata john kwa mbio za kiutuuzima "Mwizi,mwizi huyoo,kamata mwizijamani,mwizi huyoo"John alizidi kukimbia na kwa bahati mbayaalipokimbilia kulikuwa na watu wanakuja upandewake,wakagongana uso kwa.uso john akageuza nakukatisha sehemu nyingine,wale watu walivyosikiamzee Mazi akisema "mwiziiii" wakajua ni john wotewakaanza kumkimbiza john anapoelekea.John hakutaka kupumzika alikimbia vile awezavyoilimradi asinase kwa watu wale walioonekana kuwana hasira kali.

John alikimbia mno mpaka sehemu moja iliyokuwana bonde kwa chini lenye nyasi nyingi kiasi,walewaliokuwa wakimfukuzia wakadhani atasimama kwakuhofia ataumia.John alisita kuruka lakini alipoona wanaomfukuziawamekaribia kufika akajikusanya na kurukiabondeni.

Raia waliokuwa wakimfukuzia john waliishia palejuu na cha ajabu zaidi hawakufanikiwa kumuonajohn zaidi ya zile nyasi.John alifuarahi mno kukamilisha zoezi lake lakinikatu hakujua kama amefahamika kwa mmoja katiya wanakijiji wale.Alifika nyumbani kwake na kujipumzisha,Aminaalipofika alipokelewa kwa tabasamu mwanana lajohn.Mzee Mazi alikutana na wale watu waliokuwawakimfukuzia john alipowauliza kama wamefanikiwakumkamata wote walitikisa vichwa kuashiria kuwaimeshindikana lakini mmoja wao alimuona yulemwizi kuwa ni john"Samahani mzee Mazi Yule kijana anafanana namkweo john vile vile nina wasiwasi ni yeye""We tena shika adabu yako unataka kunikorogaeti,yule ni mume wa binti yangu na kamwe hawezikufanya upuuzi kama huo" alifoka mzee Mazi"Samahani mzee wangu nitakuwa nimemfananishatu" kijana alijitetea"Sisi tunaenda mzee pole sana kwa kuibiwa"alisema kijana mmoja"sawa nashukuru kwa ushirikiano wenu" mzee MazialijibuMzee Mazi alifuata njia yake akiwa amejiinamiakichwa kilikuwa kizito mno asiamini kilekilichotokea,alia mini sana kuwa huenda wanunuziwamemchezea keusi na kuirudisha hela yao.Mzee Mazi alipofika kwake alimkuta bi Mazi akiwaametulia tuli akisubiria majibu toka kwa Mmewake.

Cha kwanza alichokiona ilikuwa ni huzunialiyonayo mzee Mazi akatambua kuwa labda dililimekuwa dirishaHaraka bi Mazi akamfuata Mme wake na kuanzakumsaili kabla hata ya salamu"Kulikoni we Mazi mbona umepoa hivyo,una tatizogani,wamekataa au hawajafika""Afadhali hata ingekuwa hivyo mke wangu,haliniliyokutana nayo inatisha kweli kweli sielewi hatailikuwaje""Mmmmh!! Makubwa haya,enheee!! hebu niambievizuri una tatizo gani au nini haswa kimekupata nasio.kunipa ngonjera zako zisizo na maana hapa"
 
Sehemu ya Kumi na mbili

★★ilipoishia★★

"Mmmmh!! Makubwa haya,enheee!! hebu niambievizuri una tatizo gani au nini haswa kimekupata nasio.kunipa ngonjera zako zisizo na maana hapa"...

★★Teremka nayo★★

"Basi tukae mke wangu wima wima hivi kamawapiga kareti jamani eeeh!". alilalamika mzee Mazi"Hebu kaa hapa usiniletee viswahili vyako mpigakareti mpiga kareti unamjua wewe" Alisema bi Mazikwa kuudhika"Nisikilize kwa makini na usinihoji". Mzee Mazialitamka"kwahiyo hata nisipopaelewa nisiulize?""Weee mwanamke tuheshimiane sawa kwanza hapanimeshachanganyikiwa alafu unazidi kunichanganyatu""Etekeee!! mtu gani ambaye umewahi kumuonaamechanganyikiwa huku anajitambua kuwaamechanganyikiwa hebu acha masihara elezeakilichotokea""Nilikuwa nimeenda kule nilipokwambia naendakukamilisha ule muamala na Wale jamaa sasatulipomaliza kila kitu Mimi nikaaga narudi nyumbaniyalaweee!! ni kama nilijiroga Yule shetani sijuialitokea wapi akanikaba kabali ya nguvu" Mzee Mazialikuwa tayari amesimama anaongea kwa vitendona pale pale aliposema "akanikaba" basi akaiwahishingo ya mke wake na kumpiga kabaliBi Mazi alipoona vile akaanza kung'ang'ana aachiwelakini mzee Mazi akazidi kukazia.

"Enheee!! hata Mimi nilifanya hivyo hivyounavyofanya lile jamaa halikuniacha likaingizamkono mfukoni na kutoka na hela zote kishalikanisindikiza kwa teke,hiviii" mzee Mazi akampigamke wake teke akaanguka chini"Hivyo ndivyo ilivyokuwa" alisema mzee Mazi hukuakiketi"Mwanaume mpumbavu wewe nusu uniue hapahapa najiona" bi Mazi alilalamika"Si umetaka kuhadithiwa nikaona si mbayanikuonjeshe radha yake niliyoipata kidogo" mzeeMazi alijibu"Kwahiyo na kutuna kote huko umenyang'anywa helakama mtoto mdogo" alisema bi Mazi"Sasa maneno gani hayo mke wangu badala yakunipa pole au mpaka angeniua nd'o ungepata raha""Afadhali hata ingekuwa hivyo maana ulinifanyaMimi Kama ngoma yako Leo vidume wenziowamekufunza adabu" bi Mazi alisema kwa jeuri"We mama wewe chunga kauli zako nitakubomoasasa hivi ohooo!""Hiiiii!! ushindwe kumbomoa aliyekuibia ujeunibomoe Mimi thubutu!" bi Mazi aliendeleakumtingisha mmewe"Kweli Leo nimepatikana,basi mke wangu yaishe tutumeshapotelewa haviwezi kurudi" mzee Mazialijishusha"Mambo si hayo babu weeee!! pole mwaya kwakupigwa kizinga siku nyingine uwe makini hivyoeheeeee! shauri yako utaja poteza roho buree" biMazi alisema huku akimvutia mmewe ndani.

John hakuwa na shaka tena kuhusu Maisha yakealia mini kila kitu kinakwenda vile anavyohitaji hukuMara chache akimshukuru babu yake kwa urithialiomuachia na wakati mwingine aliamini ile kaulikuwa babu yake ni kigagula.

Amina hakujua siri ya vitu vyote vile yeyealichoamini ni kwamba bwana yake johnanajishughulisha mno ilikuyafikia mafanikio mpakawakati mwingine alihisi babu yake na john kuna vituvya thamani alivyomuachia john kama urithi nandiyo maana haangaiki kwa lolote wala kutetereka."John Mme wangu karibu chakula" Aminaalimkaribisha john kwa heshima mno"Asante mtoto mzuri,umewahi kweli jamani""Lazima niwahi Mme wangu ili upate nafasi yakufanya vitu vingine""Kweli etii""ndiyo kwanini isiwe kweli,inuka basi na wewechakula kinapoa" Amina alimhimiza john"Usijali mama watoto twende mezani"Wakainuka wote na kwenda kupata kilichoandaliwa,wakiwa mezani walikuwa wakizungumza mawilimatatu kuhusu Maisha yao"Hivi john unafanya kazi gani haswaa maana kilaukitoka huwa unarudi Mara na majani mwilini nawakati mwingine umejaa vumbi mwili mzima"aliuliza Amina"Usiwe na shaka ni vibarua vya hapa na pale, kulimakupalia na kufyeka ndiyo kazi inayotuweka hapa"john aliongopea"Mmmh!! pole ila ni nani anayeweza kukupa kazi yakulima kiangazi chote hiki isitoshe ardhi imekaukamno""mke mwenye pesa si mwenzako anaweza hatakusema uchimbe shimo na ulifukie hapo hapo naakakulipa kuchimba na kufukia kwahiyo mambonduvyo yalivyo" john alijaribu kutilia mkazo sentensiyake ya mwanzo.

"Ni kweli ukiwa na pesa utahamisha hadi mito naMilima""Nd'o hivyo bwana yote ni Maisha""Mmmh!! hapo sikubali john hata wewe haujaridhikana haya Maisha na endapo Kama yote ni Maishausingekuwa ukitafuta usiku na mchana""Ni kweli uyasemayo lakini mmh!! sijui wenginewanasemaje kuhusu hilo""Wahi basi kumaliza kula tukalale maana Ninausingizi balaa" Amina alimwambia john.
 
Sehemu ya Kumi na Tatu

★★Ilipoishia★★

"Wahi basi kumaliza kula tukalale maana Ninausingizi balaa" Amina alimwambia john

★★Endelea nayo★★

"Alafu hapo tu nd'o Mimi huwa sipendi na linitumeanza kuharakishana hata wakati wa kula""Atiii!! hupendi kuharakishwa aya ni sawa natukiingia humo ndani usinisemeshe""Mmmh!! kwahiyo wasusa au""kha! kumbe hukuelewa wenzio walivyosemaukisusa wenzio wala,we maliza kula nakusubiri nitoevyombo hivyo" Alijibu Amina huku kakunja surautadhani wale wakaanga sumu wa mtaa wa kati"Makubwaaaa" john alishangaa"Na bado madogo yananafuu" Amina alimjibu john"Basi mke wangu hutaniwi na wewe" john akaamuakunyenyekea"Alaaa!! utani,kuna utani wa namna hiyosikuhizi,kama ni hivyo tutalala mzungu wa nne Leotuone nini kitatokea" Amina alizidi kukazia"Daaah! ya leo kali" john alizidi kuongea"Mmmmmmm!! umeona eeeh!!""Aya mke wangu,hebu angalia ninavyopakiamatonge makubwa makubwa yaaani namaliza sasahivi ehee! ehee! si unaona mwenyewe" John alikuwaakijitetea kwa Amina huku akijaribu kujichekesha ilikuua soo ikawa ni vituko tu ndani mwao"Hahaaaaaaa!! kweli nina Mme basi maliza twende"

Asubuhi iliyofuata john aliwahi mapema kutembeleamitaa mbalimbali ili walau apate kitakachomfaamaana ile tabia yake ya wizi ilianza kushika hatamusasa kwani kila alichokiona kwa watu alitamani kiwechake.Alizurura mitaa kadhaa akiwa anadadisi nyumbakadhaa ambazo wamiliki wake walionekana niwenye nazo kidogo,lakini hakuvutiwa na chochotemaeneo yale.John akiwa katika mitaa hiyo akijidai anawahimahali jua tayari lilikuwa limepanda juu hii ikioneshani mida ya saa nne asubuhi.

John alifanikiwa kuiona nyumba moja iliyojengwakwa mtindo kama madarasa ya shule wengi wetutunaita 'I' kama wanavyoziita nyumba nyingine kwamfano mtindo kama 'u' nyingine 'L'Si kwamba ule mtindo ulimvutia john la! ila jeneretailiyokuwa inaunguruma maeneo hayo pamoja nawatoto waliokuwa wamejazana wakichunguliakwenye matundu mbalimbali ya nyumba ile pamojana nafasi zilizpo kwenye mlango"mwanya"Kipindi hicho runinga ilikuwa kitu adimu kiasikwamba wenye nazo ndiyo walikuwa wanamudu vitukama vile, na ndiyo maana watoto wengi walikuwawakijazana sehemu ambayo video zinapatikana iliwalau wasafishe macho.

Wakati john amehamishia mawazo yake kwenyenyumba ile na kuanza kuisogelea taratibuakapishana na Kijana mmoja ambaye alisimama nakuanza kumtazama john mpaka anakoelekea lakinijohn hakustukia tukio lile.Yule Kijana alisimama akiwa anajiongelea ni kamaanajishauri kitu na mwisho akaamua amfuate johnalikoelekea.

John alipoifikia ile nyumba akatafuta upenyo mzuripale mlangoni na kulipata tundu kubwa lililotoshajicho lake akaanza kutalii mle ndani jinsi mlivyo.Yule Kijana naye alifanikiwa kuupata upenyoakaanza kuchungulia,John na yule Kijanawalinogewa haswaa.kwa kile kilichokuwakinaoneshwa mle ndani.

Mama mwenye nyumba alikuwa amefura kwa hasirakutokana na wingu Fulani la Giza lililojitengenezapale mlangoni akapania kuwakomeshawachunguliaji.Jicho la john lilitua kwenye runinga ndogo aina yaHitachi inchi 14 chini yake alifanikiwa kuiona dekiya matofali kama wengi wanavyopenda kuiita amaVhs.

Mama mwenye nyumba hakuridhika na kile kitendoakatoka nje haraka haraka wale watoto wotewakatimua mbio hii yote ni kutoka na nakukifahamu kitimu timu cha mama mwenye nyumbaile.John na jamaa yake hawakuwa na habariwalinogewa haswaa na mkanda(muvi) iliyowekwamle ndani.

Mama mwenye nyumba akasimama akiwaangalialakini hawakustuka,ikambidi arudi ndani mpaka paleanapochungulia john naye akaanza kumchunguliawakakutanisha jicho kwa jichoJohn alivyokauzu akapaza sauti "Wewe toka hapounaniziba bhana" lakini mama mwenye nyumbaakazidi kumtazama john ili atoke pale.John akajiona ni mjinga akaamua atumie ubabekwa akili za haraka akainua mdomo wake nakupuliza jicho la mama mwenye nyumba."Mwanaha**mu wewe hivi hauna mshipa wa aibu etikubwa zima kazi kuchungulia milangoni kwa watuwakiwamwagia maji ya moto,mweee! hata hayamwanaume mzima" mama mwenye nyumba alianzakujilalamisha"ohoooooo!!" John alitoka mlangoni na kuanzakuondoka eneo lile.Yule Kijana baada ya kusikia yale matusi akatoka nakumfuata john"Samahani kaka,vipi hali" Kijana alisalimu"Safi tu kulikoni?" john aliuliza"Ni kama nakufananisha ila hapana ni wewe kabisawewe si ndiy....nani....nani...nani vile""John au?" john aliuliza"Haswaaa! john Mme wa Amina yule mtoto wamzee Mazi" Kijana alifafanua"Ndiyo Mimi kwani vipi""Nilitaka kukusalimu tu Mimi ni jirani yake mzeeMazi naitwa juma". Kijana alijitambulisha"aya asante karibu nyumbani kwangu" John alijibu"Nashukuru kaka msalimie sana Amina"John na juma wakaachana pale kila mtu akapita njiayake.

John alikuwa akiiwazia ile deki huku akijisemea"Tuna nyanyasika kwasababu yaruninga yao sasanitaiba deki ili tuone mtajidai na nini ngoja"akazidi kutembea kuelekea kwake hukuakitabasamu na alipogeuka nyuma akashangaakumuona juma akijiongelea Kama mtu mwenyematatizo ya kiakili suala lile likampa shauku yakwenda kumuuliza mkewe kuhusu JumaMuda huo juma alizidi kujiongelea tu mpaka wakatimwingine alikuwa akirusha mikono"Unaona haiwezekani kabisa,haiwezekaninawaambia,Mimi nilisema yule Kijana aliyemuibiamzee Mazi ni john wakakataa lakini Mimi nilimuonasi umeona sasa ni huyu huyu tena ngoja lazimanifikishe hili kwa Mzee mazi".
 
Sehemu ya Kumi na nne

★★Ilipoishia★★

"Unaona haiwezekani kabisa,haiwezekaninawaambia,Mimi nilisema yule Kijana aliyemuibiamzee Mazi ni john wakakataa lakini Mimi nilimuonasi umeona sasa ni huyu huyu tena ngoja lazimanifikishe hili kwa Mzee mazi".

★★Endelea★★

John alipogeuka nyuma alimuona juma akijiongeleakama chizi na hakufahamu bayana kuwa kisa ni niniila alichofahamu katika akili yake ni kwambahuenda yule mtu anamatatizo ya kiakili japohakujipa aslimia mia moja akatazamia kuwa nivyema akamuulize mkewe Amina.

Juma alizidi kukata mitaa dhamira yake kuu ikiwa nikumfikia mzee Mazi na kumpasha habari,Hatimayeekihere here kilichomtoa mbali kilimfikisha kwa mzeeMazi na kwa bahati alikuta mzee Mazi akiwaameketi chini ya mti kama ilivyo kawaida yakeakipunga upepo wa eneo hilo huku akitafakarimambo anayoyajua yeye.

"Babu,babu,babu naona umetulia sana leo,naaminibado unaziwaza hela zako kweli au si kweli?" jumaalimuanza mzee Mazi kwa mbwembwe"Tatizo lako huwa mpaka unichimbe mkwara alafukitu chenyewe kiwe hakina kichwa wala miguu""Umeona,aaaaah!! umeona,umeudharau mwiba sasasubiri huo mguu ulete balaa nd'o utanitafuta nikupemambo si unanielewa lakini kwamba mi ni kamayule malaika mpasha habari aya,shauri yako miminaenda" Juma aliamua kuzuga Kama anaondoka"Aaaah!! babu sasa unaenda wapi bwana hutaniwina wewe" Mzee Mazi aliona atulize boli ili apatemawili matatu kwa malaika mpasha habari kamaanavyojiita juma"Mimi nilijua tu kwamba utaniita si unayajua mamboyangu sibahatishi" Juma alijitapa"Umeanza ujinga wako hebu sema kilichokuleta"Mzee Mazi aliamua kufoka sasa akiwa anaigizakukasirika"Daaah! tatizo lako ni hapo tu huwa hauchelewikukasirika"

John alifika nyumbani kwake na kumkutakipenzi chake anaandaa mlo wa asubuhi kamaunavyojua kijijini,Amina alikuwa amepika uji wa ulezina viazi utamu ama viazi ukimwi wanavyoitawengine,John akaketi pembeni ya mkewe na kuanza ukorofiwake wa hapa na pale na mwisho akaanzisha hadihiya juma"Hivi unamfahamu jamaa mmoja hivi anaishi jiranina nyumbani kwenu wanamuita Juma" Johnalimuuliza mkewe"Yule muongeaji au?" na Amina aliuliza"Sina hakika ila anavyoonekana nimuongeaji mno"john alijibu"Ni mrefu mrefu hivi mweusi kama chungu alafuanapenda kucheka Cheka hivi,vimeno vyake vidogodogo na vineungua ungua ""Haujakosea kabisa ndiyo huyo huyo""Eeeeeh!! mwanaume simpendi Yule weee kwanzaulimjuaje?" aliuliza Amina akiwa amekereka"Nimekutana naye tu barabarani kwani vipi mpakauseme haumpendi au nd'o alikutongozaga""Thubutuuu!! ataanzia wapi kwanza hiki chuma babuwewe! alafu nisikilize yule mwanaume mpeke pekeyule kha!! utadhani ni wa kike""Maajabu!!" John alishangaa"Yaani kila kitu anajifanya anajua sasa kihereherekiko pale Kama sumaku ya treni""Alaaaaaa!! kumbee sikujua mie""Nini tena au ndiyo umeanza naye urafiki?,chungatena heeee! sipatii picha huo urafiki utakavyokuwa"Amina alizidi kuuchochea moto"Hapana bwana kawaida tu,Mimi Niko ndaninapumzika" john aliaga baada ya kugundua kuwaamealika majanga nyumbani kwake,alikuwaakiomba kimoyo moyo juma asifike nyumbanikwake hata siku moja

Juma alia za kujieleza kile kilichompeleka kwamzee Mazi"Yaani babu huwezi amini Yule mwizi aliyekuibiasiku ile zile pesa nimemuona Leo" alisema johnkwa msisitizo"Kweli? hebu twende sasa hivi Fanya haraka" mzeeMazi alikurupuka na kuanza kuongoza njia"Sasa mbona unaondoka unamfahamu huyo mwiziwako" juma aliuliza akiwa amesimama"Si unamfahamu wewe nd'o nakwambia twendetutajua huko huko nadhani hanifahamu vizuri Mimini nani hapa kijijini" Mzee Mazi alizidi kuchanjambuga na alipogeuka akamuona juma badoamesimama"Sio huko babu hiyo njia umepotea kabisaaa rudihuku kwanza nikwambie tunaenda wapi". alisemajuma"We mtoto wewe sipendi utani ujue ohoo!!nitakuanzia bakora hapa hapa alafu afuate huyomjinga mwenzio aliyeniibia" Mzee Mazi alisemakwa hasira"Kwahiyo na Mimi unanikasirikia,njoo kwanzanikujuze babu sio unakurupuka maana yule mtu nimzito" juma alizidi kumchanganya mzee Mazi .
 
Sehemu ya Kumi na sita

★★Ilipoishia★★

"Si unaona hata Mimi nilisema sio bure atakuwa anamatatizo binafsi na kama sio hivyo basianamatatizo ya akili,mkwe wangu Mimi aaaah! walahainipi kabisa kichwani mwangu,huyu mtoto huyu aukatumwa kuchonganisha ili mwanangu aachikeabaki kama dada yake yule msimbe anayekaakwao,mmmh!" Mzee Mazi alizidi kujisemea tu.

★★Endelea★★

John aliamka mapema na kuvaa nguo zake za kazina kumuaga mkewe kuwa atarudi baadae kidogoana kazi,siku hii akabeba kibegi cha mgongonikinachoweza kumtosha kwenye matumizi yake hukoaendako.

Breki ya kwanza ilikuwa ule mtaa ambao unanyumba ile ambayo aliiiona deki na runingaalipofika akatulia akiangaza angazaa mahali pakuanzia kwani ile nyumba ilikuwa wazi moja kwamojaMama mwenye nyumba alitoka na kandoo kadogoakaweka pembeni ya mlango,akatoa shatilililochakaa mlangoni pa kuingilia (kikanyagio) nakuanza kulikung'uta ili kuondoa vumbi.John alizidi kumtazama mama yule ambayehakuonekana kutambua lolote,Mama mwenyenyumba akachukua ndoo yake na kuelekea mahalikulipokuwa na nyumba ya peke yake yenye milangomiwili ikionesha ni maliwatoni, Alipoingia tu john hakufanya kosa akaangaliakushoto na kulia hakuna mtu akanyoosha moja kwamoja mpaka mlangoni akachungulia lakini hakuonamtu ndani,akaingia na kuifuata deki na runinga yakepale ilipo,akaanza kuhangaika na nyaya za dekiambazo hakujua kama zimechomekwa kwenyeruningaJohn alipoona atakutwa ikabidi achungulie nyuma yaruninga akakutana na nyaya zimechomekwa palekwa haraka akaanza kazi ya kuzichomoa naalipofanikiwa akatoa begi lake na kuiweka ile dekiakaanza kutoka nje huku anaweka nyaya zilezilizokuwa zikining'inia kwenye begiJohn alipotoka nje akakutana uso kwa uso namama.mwenye nyumba akiwa anatokamaliwatoni,john akarudisha macho kwenye nyaya nayule mama mwenye nyumba macho yake yakatuapale pale kwenye nyaya akaachia yowe la nguvu"Mwiziiiiiiiiiiii!!!!"John bila kupoteza muda akazisukumia nyaya zotemwenye begi na kuanzisha kukimbia,mama mwenyenyumba naye akamfuata john anakoelekea lakinihakufika mbali kutokana na unene alionao japoaliendelea kupaza sauti.

John hakuwa na jinsi zaidi ya kukimbilia barabarakuu na kuanza kuifuata.Watu walitoka mbio kumfuata mama.mwenyenyumba badala ya john walipofika tu akawaelekezeamkono "ameenda kule amebeba begi mgongoni""Nd'o yule tuliyepishana naye twendeni"mmoja wa watu wale alisemaRaia na hasira kali na wezi hivyo mwendowaliokimbia ulikuwa ni afadhali hata na gari yawagonjwa.Walifika barabara kuu wakanyoosha mojakwa.moja na kwa bahati wakaona kama mtuanakimbia wakajua ni yule mwizi wamaemkimbizawakazidi kuongeza mwendo.

Ukitaka kuona au kupata wanariadha wazuri basiitokee sehemu kuna mwizi hapo ndipo utawaonawatu wenye mbio nyingi duniani.John alipogeuka nyuma akawaona wananchi wengiwanamfuata kwa nyuma wakiwa na mwendo wahatari alafu John alikuwa tayari amechoka kukimbiazile.mbio ndefu."Sasa ni wakati wa kufanya maajabu" alijisemeajohn na pale pale akafunga koti lake vizurianavyojua yeye.

Wale wananchi wenye viherehere vya kupiga mwiziwalokaribia kumfikia John lakini cha ajabu zaidi yulewaliyemuona mwanzo ni mtu hakuwa vile tena balisokwe mkubwa akiwa anatembea kimaringoPale pale walirudi mbio walikotokea nawalipowakuta wenzao wakawapita bilakuwasemesha.

John alizidi kukimbia alipoona amewazidi mbaliakasimama kwa mbwembwe ili awasubiri mpakawatakapomfikiaWananchi wakiwa na mawe,marungu na mapangawakasimama kwanza mbele ya sokwe waliyemkutana kwa hofu wakaanza kurudi kinyume nyumeJohn kwa kutaka kujionesha zaidi naye akaanzakuwasogelea akiwa anataka Sifa na kweli kama Sifatu pale alijizolea za kumwaga kwani alipiwakaribiaakatoa ngurumo "Arrrrrrrrrrrrrrrrr"Wananchi wote wakakimbia mbio wakirudiwalikotoka.

John naye akakunja kona kuingia kwenye kamsitukadogo akielekea nyumbani kwake. Kwawaliomuona akiingia mle msituni walijua huend andiyo makazi yake.
 
Sehemu ya Kumi na sita

★★Ilipoishia★★

"Si unaona hata Mimi nilisema sio bure atakuwa anamatatizo binafsi na kama sio hivyo basianamatatizo ya akili,mkwe wangu Mimi aaaah! walahainipi kabisa kichwani mwangu,huyu mtoto huyu aukatumwa kuchonganisha ili mwanangu aachikeabaki kama dada yake yule msimbe anayekaakwao,mmmh!" Mzee Mazi alizidi kujisemea tu.

★★Endelea★★

John aliamka mapema na kuvaa nguo zake za kazina kumuaga mkewe kuwa atarudi baadae kidogoana kazi,siku hii akabeba kibegi cha mgongonikinachoweza kumtosha kwenye matumizi yake hukoaendako.

Breki ya kwanza ilikuwa ule mtaa ambao unanyumba ile ambayo aliiiona deki na runingaalipofika akatulia akiangaza angazaa mahali pakuanzia kwani ile nyumba ilikuwa wazi moja kwamojaMama mwenye nyumba alitoka na kandoo kadogoakaweka pembeni ya mlango,akatoa shatilililochakaa mlangoni pa kuingilia (kikanyagio) nakuanza kulikung'uta ili kuondoa vumbi.John alizidi kumtazama mama yule ambayehakuonekana kutambua lolote,Mama mwenyenyumba akachukua ndoo yake na kuelekea mahalikulipokuwa na nyumba ya peke yake yenye milangomiwili ikionesha ni maliwatoni, Alipoingia tu john hakufanya kosa akaangaliakushoto na kulia hakuna mtu akanyoosha moja kwamoja mpaka mlangoni akachungulia lakini hakuonamtu ndani,akaingia na kuifuata deki na runinga yakepale ilipo,akaanza kuhangaika na nyaya za dekiambazo hakujua kama zimechomekwa kwenyeruningaJohn alipoona atakutwa ikabidi achungulie nyuma yaruninga akakutana na nyaya zimechomekwa palekwa haraka akaanza kazi ya kuzichomoa naalipofanikiwa akatoa begi lake na kuiweka ile dekiakaanza kutoka nje huku anaweka nyaya zilezilizokuwa zikining'inia kwenye begiJohn alipotoka nje akakutana uso kwa uso namama.mwenye nyumba akiwa anatokamaliwatoni,john akarudisha macho kwenye nyaya nayule mama mwenye nyumba macho yake yakatuapale pale kwenye nyaya akaachia yowe la nguvu"Mwiziiiiiiiiiiii!!!!"John bila kupoteza muda akazisukumia nyaya zotemwenye begi na kuanzisha kukimbia,mama mwenyenyumba naye akamfuata john anakoelekea lakinihakufika mbali kutokana na unene alionao japoaliendelea kupaza sauti.

John hakuwa na jinsi zaidi ya kukimbilia barabarakuu na kuanza kuifuata.Watu walitoka mbio kumfuata mama.mwenyenyumba badala ya john walipofika tu akawaelekezeamkono "ameenda kule amebeba begi mgongoni""Nd'o yule tuliyepishana naye twendeni"mmoja wa watu wale alisemaRaia na hasira kali na wezi hivyo mwendowaliokimbia ulikuwa ni afadhali hata na gari yawagonjwa.Walifika barabara kuu wakanyoosha mojakwa.moja na kwa bahati wakaona kama mtuanakimbia wakajua ni yule mwizi wamaemkimbizawakazidi kuongeza mwendo.

Ukitaka kuona au kupata wanariadha wazuri basiitokee sehemu kuna mwizi hapo ndipo utawaonawatu wenye mbio nyingi duniani.John alipogeuka nyuma akawaona wananchi wengiwanamfuata kwa nyuma wakiwa na mwendo wahatari alafu John alikuwa tayari amechoka kukimbiazile.mbio ndefu."Sasa ni wakati wa kufanya maajabu" alijisemeajohn na pale pale akafunga koti lake vizurianavyojua yeye.

Wale wananchi wenye viherehere vya kupiga mwiziwalokaribia kumfikia John lakini cha ajabu zaidi yulewaliyemuona mwanzo ni mtu hakuwa vile tena balisokwe mkubwa akiwa anatembea kimaringoPale pale walirudi mbio walikotokea nawalipowakuta wenzao wakawapita bilakuwasemesha.

John alizidi kukimbia alipoona amewazidi mbaliakasimama kwa mbwembwe ili awasubiri mpakawatakapomfikiaWananchi wakiwa na mawe,marungu na mapangawakasimama kwanza mbele ya sokwe waliyemkutana kwa hofu wakaanza kurudi kinyume nyumeJohn kwa kutaka kujionesha zaidi naye akaanzakuwasogelea akiwa anataka Sifa na kweli kama Sifatu pale alijizolea za kumwaga kwani alipiwakaribiaakatoa ngurumo "Arrrrrrrrrrrrrrrrr"Wananchi wote wakakimbia mbio wakirudiwalikotoka.

John naye akakunja kona kuingia kwenye kamsitukadogo akielekea nyumbani kwake. Kwawaliomuona akiingia mle msituni walijua huend andiyo makazi yake.
 
Sehemu ya Kumi na saba

★★★Ilipoishia★★★

John naye akakunja kona kuingia kwenye kamsitukadogo akielekea nyumbani kwake. Kwawaliomuona akiingia mle msituni walijua huendandiyo makazi yake.

★★Endelea nayo★★

Wananchi walikimbia mno mpaka walipofika mahaliFulani wakasimama wakitweta,"Jamani Mimi siamini nilichokiona" alisema mmojawao.

"Hata Mimi kwa kile nilichokiona hapana sio kweli"alidakia mwingine"Nilijua tu kuna wengine hapa ni vichwa maji,yaanipamoja na kutishiwa na lile sokwe badohamjakubali kuwa mmeliona" Alisema mtumwingine"Daaah!! mimi nahisi hili dude sio la kijiji hiki lakinimbona yule mama alisema ni kijana ndiye ameibatena alisema amebeba begi mgongoni na yulesokwe naye amevaa begi vilevile" Kijana mwinginealitoa wazo lake."Mimi naona kuna kitu hapo sio bure inabidi tufanyekitu" Kijana wa Mara ya kwanza akatoa kauli"Mmh! mtaingia kwenye matatizo yasiyo wahusu lamsingi yaoneni kama yalivyo hayo mambo""Mimi nitalifuatilia hili hatua kwa hatua" Alisistizakijana mwingine"Sawa utatupatia majibu" walijibu wote kwa pamoja"Alafu jichunge" mmoja wao alisistiza.

John alifika nyumbani kwake na kupitiliza moja kwamoja ndani lakini amina alikuwa amemuonaanavyoingia na begi lake mgongoni na mbaya zaidiAmina aliliona lile koti alilovaa john,lilimpamashaka kwasababu ni mara ya kwanza anamuonanalo john ila haikuwa mara ya kwanza kusikiakuhusu mwizi anayevaa koti lefu ikiwa si kawaidakwa wanakijiji wa hapo kuvaa makoti marefu.Amina hakujali sana wala hakutaka kuumiza kichwachake akaendelea kupika.John akiwa ndani alivuazana zake za kazi na kushusha pumzi ndefu nikama mtu aliyefanikisha kuupanda mlimaKilimanjaro katika kilele chake.

John alihisi ameutua mzigo mzito aliokuwaamejibebesha toka siku iliyopita na aliazimiakwenda kupita mtaa ule ili awaone waathirika watukio wanavyoomboleza kimya kimya.

Wakati john akiwaza hayo yote Amina alitoka jikonina kumfuata mmewe ili walau ampe pole yamihangaiko ya hapa na pale kama ilivyokawaidayake kila Mme wake anapowasili kiukweli ilikuwa nizaidi ya mapenzi ya kihindi kati ya john na Amina.Amina alimkuta Mme wake akiwa amejilazakitandani macho juu akifikiria mambokedekede,Amina alimtazama mme wake huyo waujana anavyong'aa ngozi yake angavu na uzuri waasili akaishia kutabasamu huku moyoni akijipongezakwa kupata chaguo lililo bora kwake.

Amina akasogea mpaka alipo john na kukaapembeni,kwa heshima na taadhima akamshikataratibu John na kumsemesha lengo ikiwa sikumstua John.

"Habari za kazi Mme wangu" Alianzishamazungumzo Amina"Safi tu za mida mama watoto wangu" Johnalirudishia salam"Nzuri kiasi" alijibu Amina"Mmmh!! kuna tatizo gani mpaka iwe kiasi""Nilikuwa mpweke ujue,umechelewa kurudi mno"Alijibu Amina akiwa anadeka"Hahahaha!! kazi unayo, yaani masaa machache tuunasema umebaki mpweke je nikiondoka sikukadhaa si utakufa kwa kunikosa wewe" Alisemajohn kwa utani"Ukifanya hivyo sijui kama nitapona" Alijibu Amina"Sikuachi peke yako kipenzi,vipi kuhusu chakulamaana nahisi kuna jamaa wanakwangua na vijikotumboni""Heee! we mwanaume una njaa ya karibu sijui Sikuukishinda bila kula itakuwaje?""Nakwambia nitashinda nimelala kutokana na homaya njaa""Basi bwana twende sebuleni nikakuandalie.

Kijana aliyesema atafuatilia kuhusu mwizi ambaye nijohn alinyoosha moja kwa moja kwa juma akiaminikuwa kwasababu juma ni shushushu wa kuaminikabasi anaweza kukusanya taarifa kamili na mwishowamfahamu mhusikaBaada ya kumkuta Juma akiwa ametulia nyumbanikwao akaanza kumtafutia njia ya kumuingia kiakiliili juma aanze kazi ya kumsaka huyo mwizi ambayeanatishia kijiji muda huo"Kijana,mbona umeinamia sana rafiki yangu au nd'ounatunga sheria""Daaah! Ali karibu sana rafiki,ni mawazo tu nduguyangu ya hapa na pale yananisumbua" alijibu juma"Wacha weee! kitu gani hicho kinacho hangaishaubongo wako hivyo mzee wa kuumbua" Aliuliza Alihuku akimjaza Sifa rafiki yake"Au nd'o yule mwizi wa deki kwa mama mgenianakusumbua akili" aliongezea Ali"Anhaaaa! umenikumbusha eti na Leo yule jamaaameiba kwa mama mgeni?" Juma aliuliza"ohoooo! ulikuwa wapi rafiki yangu,sisi tumefukuzakama paka anayemfatia panya juu ya dari lakinitulichokutana nacho we acha tu" alielezea Ali"Mlikutana na nini eeeh!! hebu niambie" Humanalikaa sawa kusikiliza kilichotokea"Alikuwa ni mtu amevaa koti refu lakinitulipomkaribia tukakutana na bonge la sokweee"alijibu Ali.akiwa amenyong'onyea
 
Sehemu ya Kumi na nane

★★Ilipoishia★★

"Alikuwa ni mtu amevaa koti refu lakinitulipomkaribia tukakutana na bonge la sokweee"alijibu Ali.akiwa amenyong'onyea

★★Endelea nayo★★

"Alaaaa! si maajabu hayo inawezekanaje kwanza"Aliuliza juma akiwa ametoa macho"Hata Mimi sijui nd'o hivi nimekufuata ili tuangalietunafanyaje ili tumuumbue huyo jamaa maananilidhani unamfahamu""Hapana kwa kweli sifahamu, anhaaa! ndiyo maanatulipofika pale bondeni hatukumuona tena aaaah!kumbe" Juma alikuwa akijisemea"We juma ni nani huyo hamkumuona" aliluliza Ali"Ngoja nikwambie alipoibiwa mzee Mazi sisitulimkimbiza mwizi ila cha ajabu ni kwambaalipotea katika bonde moja hivi lenye kichaka"Alieleza juma"Kwani nd'o huyo aliyeiba deki au" aliuliza Ali"Ni huyo huyo na nina wasi wasi na john hebutumfuatilie tuone" Alijibu John."Sawa tuanze kazi"

John akiwa nyumbani kwake alikuwa anafikiriabaadhi ya maneno ya mke wake Amina hasa palealiposema kuwa john akikaa mbali naye atakufaSasa kila john akifikiria zile sentensi anashindwakuelewa ni kitu gani afanye kwa wakati huo maanakazi anayoifanya imejaa hatari tupu na licha yahatari kuna aidha kupoteza Maisha au kuangukiakatika mikono ya polisi ikawa taabu moja kwamoja.

John alikosa raha mpaka akaanza kuukumbukawosia wa babu yake na pia akakumbuka chanzocha yeye kuanza kuiba ni mzee Mazi kwasababualimnyima msaada wa kuanzia MaishaJohn hakuishia hapo alimlaani sana mzee Mazi kwakumfanyia kitendo Kama kile na kumharibia dira yaMaisha na katu hakuwaza kuwa alianza kujiharibiamwenyewe tangu awali babu yake alipomkanya amuache Amina.

John alifikia hatua ya kuanza kulia na akiwa katikatiya kilio akakumbuka babu yake alivyokuwaakimkabidhi koti lakini alimuasa kuwa atafutewepesi wa kuishi na si vinginevyo pia alijihisimwenye hatia kuendelea kuiba vitu vidogo vidogoKichwa cha john hakikuwa sawa hata kidogo,ghaflaakakumbuka kuwa babu yake hakumalizia kauli yamwisho kuhusu kitu ambacho hakijulikani.John akakurupuka na kwenda katika chumba chababu yake maana toka.alipokufa john alikifungachumba kile na hakutaka kusogea wala kukifunguatena

John aliingia mkuku mkuku akiwa.na papara yakutosha kufahamu siri ambayo babu yakehakuiweka bayana.Alipofika ndani akaduwaa kwanichumba kilikuwa cheupe kama alivyokiacha awaliJohn akaanza kupiga hatua taratibu mpaka katikakitanda cha babu yake akiangaza huku na kule bilamafanikio na mwisho akaamua akae kitandani paleghafla chini ya uvungu ikakisika sauti ya panyawakitafuna tafuna vituJohn akawahi kuchungulia kilichopo humo chini yauvungu na kukutana na sanduku moja ambalo kwaharaka alilivuta mpaka nje.

Lilikuwa ni sanduku lililosheheni vumbi nyingikuonesha halijaguswa siku nyingi,kwa uangalifumkubwa john akaanza kulifungua na kusababishamende zitoke mle ndani kwa wingi.Bado john hakujali wingi wa mende wale shaukuyake ilikuwa ni kutazama kilichomo mle ndanimaana alihisi sanduku lile ndilo litakuwa limebebasiri yote ambayo babu yake alitamani kumwambiakabla ya kifo chake.

Tahamaki!! john aliambulia peupe yaani sandukulilikuwa tupu isipokuwa kilichoonekana ni panyamdogo aliyetulia akiwa anachezesha nyusi zake nakaratasi moja chakavu iliyoonekana imekaa miakamingi sehemu hiyo huku mavi na mkojo wa panysukisaidia kuichakaza zaidi na zaidi kiasi kwambaiilionekana imechoka mno.

John alikasirika kutokana na muda na uangalifualioutumia kulifungua lile sanduku akatamani hatamuda ule angeutumia hata kutafuta vitu vinginehuenda angepata kitu cha thamani kuliko hichoalichokutana nacho muda ule.John aliamua kufunga sanduku lakini machaleyakamcheza na kujiuliza "kwanini yule panyahakimbii bali katulia pale pale??" Likawa fumbokwake ambalo alihitaji kulifumbuaJohn akafungua tena lile sanduku,akajaribu kumstuapanya yule lakini panya hakujali hata uwepo wakeikambidi john aingize mkono katika lile sanduku iliamkamate yule panya lakini panya hakuthubutu hatakujongea mbele.

John akafanikiwa kumshika yule panya ambayealitoa mlio punde tu alipokamatwaJohn alistuka baada ya yule panya kugeuka noti yashillingi elfu kumi,akaitupa chini na kusogeapembeni akishangaa ule muujizakwa hatua za taratibu akaanza kuifuata ile pesampaka akaifikia,akiwa anatetemeka akaiinua nakuishika vizuri mkononi akiitazama bila kuimalizahuku kichwani mwake akiwa na maswali lukuki juuya yule panya alivyobadilika kutoka katika umbilelake mpaka kuwa ile noti ya shillingi elfu kumi.Akili ya john ikazidi kupatwa.na kiwewe akatamaniatoke nje akamuulize Amina lakini bado hakuonasababu ya kumshirikisha mke wake huyoo.

John akachungulia ndani ya sanduku na kukumbanana ile karatasi iliyochakaaa,kwa taratibu mnoakaiinua na kuanza kuuangalia mwandiko uleulioonyesha dhahiri kuwa mwandishi alitumiakalamu ya wino katika uandishi japo haikujulikanahuyo mwandishi aliandika hiyo karatasi wakati gani.John akajivuta mpaka katika kitanda cha babu yakena kuanza kuisoma ile karatsi iliyoandikwa kiustadina usafi wa hali ya juu uliodhihirisha ni namna ganikaratasi ile ilikuwa ya thamani kupita maelezo
 
Sehemu ya Kumi na tisa

★★Ilipoishia★★

John akajivuta mpaka katika kitanda cha babu yakena kuanza kuisoma ile karatsi iliyoandikwa kiustadina usafi wa hali ya juu uliodhihirisha ni namna ganikaratasi ile ilikuwa ya thamani kupita maelezo.

★★Endelea★★

Macho ya john yalitua katika kichwa cha habarikilichopo katika.ile karatasi yenye manenomachache"Kwa yeyote atakayeipata karatasi hii,Panya huyo nimahsusi kwaajili ya kujiingizia kipato kwa njia yaharaka ikiwa tu mlengwa ataipeleka mahali ambapokuna mkusanyiko mkubwa wa pesa yaani pesanyingi,endapo nayo ikichanganywa nazo basi pesazote zitahamia kwako zikiwa ndani ya sandukulililohifadhi panya huyo kwa kipindi chote. Matumizimema,Mzee Ndasi"John alilipuka kwa furaha na kuanza kuruka rukamle ndani akiwa anaamini kuwa ile kazi ya wizikatika nyumba za watu itakuwa imefikiakikomo,John alinyanyua sanduku lake na kuongozanalo njeAmina alishangazwa na lile sanduku alilobeba johnmaana hakuwahi kuliona pale.nyumbani kwao pialilikuwa na vumbi mnoJohn akaomba maji kwa mke wake,Alipopewaakaanza kulisafisha sanduku lake lakini karatasi naile noti alivitia mfukoni.Amina alimuomba johnamsaidie kuliosha lile sanduku lakini john aligomakatakata ili Amina asifahamu kinachoendelea.Baada ya john kusafisha kila kitu akaingia ndanikuanza kupanga mikakati mipya kwaajili ya kazimpya ambayo alihitaji kuifanya Mara moja amambili kisha aachane na kila kitu aanze kufanyashughuli zake za kawaida.

Maandalizi yalitimia kwa upande wa john na sasailibakia suala la makubaliano na Amina ili awezekwenda kwenye kazi ya Mara ya kwanza kabisaambayo ilibeba sintofahamu kichwani mwakekutoka na na uoga aliokuwa nao pamoja nakuhakikishiwa kote katika ile ksratasi kuwa kila kituni salama kabisa.Hii ilikuwa ni jumamosi ambayo ni tulivu kulikojumamosi ambayo john aliipanga safari yake lakinilengo ikiwa ni kuifanya kazi yake siku ya jumapilikama alivyopangilia.Amina alikubali kishingo upande kwani yeye na johnwalishazoeana na wanautani kila Mara hasawanapokuwa pamoja,John alimpa matumaini Aminakuwa atawahi kurudi.Siku hiyo Amina alirudi kwa wazazi wake mpakapale.john atakapowasili.

Mzee Mazi hakupenda mwanaye alivyorudinyumbani kihasara hasara namna ile eti johnameenda mjini kikazi ndani ya siku mbili."Bi Mazi hebu njoo na huyo mwanao" Aliitamzee.Mazi"Bi Mazi kwa haraka alikwenda na Amina mpakaalipoketi mzee Mazi"rabeka! mume wangu" aliitika bi Mazi"Nataka maelezo.kamili yaliyonyooka,ni kwaniniAmina amerudi hapa nyumbani,hana kwake au?"Aliuliza mzee Mazi"Sio hivyo Mme wangu,mkwe wako ameelekea mjinikikazi anarudi kesho nd'o maana mtoto akaamuaaje hapa kututembelea mpaka hiyo kesho"bi.mazi.alieleza"Sitakagi ujinga Mimi huo ni mzigo wake na kilaanakoenda inapaswa awe nao,alafu hivi huyu Aminaalitia guu lake kwa amri ya nani?" Mzee mazialiuliza"Itikiiiii!!! umeanza hizo mbwembwe zakonitakuchambua buree!""Eeeeh!! unajifanya kidume wakati we ni kiuno tuhumu ndani""Mzee tuheshimiane sawa nina binti mmoja tu humundani,alafu hayo maneno yako ya shombo pelekahuko jalalani" Bi mazi aliwaka"Anhaaa!! mnateteana etii sasa nitawacharaza woteeohoooo!!" mzee mazi alijigamba huku akiinuka kwauoga na kuanza kuondoka."Sasa mbona unakimbia,ungesubiri niinuke wachanikupe tamu yako si umenisahau" Bi mazi alimtishamume wake"Sawa kwani mimi ni mjinga nikae hapo,unikaushedamu bureee" Alijibu mzee mazi ambaye alionekanawazi anamupgopa mke wake ambaye anaonekanani mcheza masumbwi mzuri tu"Amina mwanangu usimsikilize huyo mzee nimfumo dume tu unsomsumbua kutwa kuwazakuwanyanyasa wanawake" Bi mazi alimpoza bintiye"Usijali mama nilishamzoea japo wakati mwingineanakera mno yaani sijui mtu ufanyaje" alijibu Amina"Sema ni baba yako utamfanya nini zaidi yakumuangalia tu""kweli mama wala haina shida sana tumchukuliealivyo" Alijibu Amina."Andaa chakula mapema alafu usizime moto maananina shauku mno ya kufahamu maisha yenumnavyoyaendesha" Bi mazi alisema"Sawaa mama yangu" Amina alijibu
 
Sehemu ya ishirini

★★Ilipoishia★★

"Sawa mama yangu" Amina alijibu. John alifikia katika nyumba ya kulala wageni akiwachumbani mwake alijihasa sana kuhusu tukioanaloenda kulifanyakichwani mwake aliiamini kuwa.ile kazi inafafananakabisa na wizi wa benki kwa asilimia kadhaaAsubuhi yake John.alikwenda mapokezi na kuuliziahoteli kubwa maeneo hayo ambayo inaweza kumfaakwa natumizi yake ya siku hiyoAlielekezwa mahali ambapo ni jirani kabisa nanyumba hiyo ya kulala wageni japo mhudumu yulewa mapokezi alikuwa bado anashangazwa na johnambaye alihitaji kuelekea katika hoteli ambayohaiendani na hadhi yakeJohn,alifika na kukaa meza ya peke yake namuhudumu akamfuata na kumuuliza anachotumiakwa kiburi john akaomba chai na maandazi yakutoshaMhudumu aligundua kuwa john ni,mwanakijiji kwanimpaka rafudhi yake ilijiionesha, wazi.

Mhudumu alicheka sana mpaka akajisahaukama,,yupo kazini. John alivyoona hivyo akajuakaribia mpango wake ufeli kwasababu za ovyo ovyoikichangiwa na ushamba,wake.

"Samahani dada mi ni mgeni hapa kwahiyo sijuitaratibu zenu,hebu nisaidie " john akapenyezamfukoni na kutoa ile noti ya shillingi elfu kumi."kama kitabaki kiasi chochote hapo ni chako sawadada" John alijaribu kumuomba yule mhudumu"usijali ni kazi yangu kuhakikisha kila mtu anapatahuduma safi inayomstahili" Mhudumu alijibu"Ahsante sana" John alimaliziaJohn alisubiri kifungua kinywa mpaka kilipoletwa,ukisikia hoteli yaani ni hoteli kweli sio kama hizi zauswahilini kwetu kitafunio tu nd'o unaletewa na chaiyako lakini kwa hizi hoteli kubwa wanakuwekeamisosi na vikolombwezo kibao ukila unatoka mzitohasa.

John alitumbua macho kwa muda"Nitamaliza kweli maana mmenijazia mno""Ndivyo hivyo ilivyo kula uwezavyo ikishindikanautakiacha kama kilivyo" Mhudumu alijibuJohn akaanzisha kula mpaka alipohakikishaamejaza kibubu chakeTaratibu akaanza kuliacha eneo lile na kwendakutafuta usafiri wa kumrudisha kijijini kwao.Masaa machache baadae mhudumu ambayealikuwa anakusanya hela (kaunta) alionekanakuchanganyikiwa mno,Akaanza kupiga kelele za bilamaana huku akifungua,droo kila mara na kuangaliandaniWahudumu wengine waliojirani walikuja mbio mbiowakihitaji kufahamu kile kilichotokea na walipofikawalimkuta yule mhudumu amejivuruga nywele zakena kila muda alikuwa akifungua droo nakuitazama,waliofika mapema walibaki vinywa wazitu bila kutoa msaada wowote Mhudumu mmoja mstaarabu akamchukuamwenzake na kutoka naye nje akaanza kazi yakumfariji mpaka alipotulia kisha akaenda naye kwabosi wake kwaajili ya kumtaarifu kuhusu tukio lililotokea.

Bosi hakuwa na wasi wasi alihoji kwa utaratibu mno"Ni kiasi gani kilichoibiwa?" Bosi alihoji"Ni millioni kumi na tano mapato ya wiki nzima"Alijibu mhudumu"Aiseeeee!! ni njia ipi iliyotumiwa na huyo mwizi"Bosi alizidi kuhoji"Nililetewa hela shillingi elfu kumi ndiyo ilikuwa yamwisho kupokea ili zitimie millioni kumi na tano nabaada ya kutenga pamoja nikafunga ili nikuleteehesabu yote cha ajabu wakati nimefungua droonizichukue nikakumbana na mbao za droo tu badalaya hela" Alieleza yule mhudumu"Ni nani aliyekuletea hiyo hela ya mteja?" bosi alihoji"Ni ni Margaret" Alijibu mhudumu aliyeibiwa"Naomba mniitie margaret haraka" bosi alitoa amriMargaret akaitwa upesi akajibu mashtaka"Naam bosi"Margareta aliitika kwa hofu"Unaweza kuniambia mteja ambaye alikupa helaanafananaje,maana ni wewe pekee uliyepeleka hiyohela kwa mwenzio" Bosi alizidi kuhoji"Ni mwanakijiji mmoja hivi kuanzia lafudhiyake ni ya kijijini kabisa" Alijibu mhudumu"Je? akirudi tena unaweza kumfahamu".Aliuliza bosi"Ndiyo nitaikumbuka sura yake maana nimeikariri"Alijibu margareta"Unaweza kuendelea na kazi na pia nyie wote habarihizi msizisambaze sawa""Sawa bosi" Wahudumu wote waliitikia.

John alifika nyumbani kwake akiwa na hamu yakuziona hela alizozipata baada ya ile kazi isiyotoajasho kuishaAkaingia ndani kwa pupa mpaka kitandani kishaakainama chini ya uvungu na kuvuta sanduku lakealilolitoa chumbani kwa babu yake.Akalifungua haraka haraka macho yake yakatuakwenye hela zilizopangika vizuri,akiwa haaminikinachotokea john akajikuta analipua kelele zashangweAkasimama na kuanza kuruka ruka akaona haitoshiakaanza kukata kiuno yote hiyo ni kuonesha ni jinsigani alivyofurahia kazi yake.

John alirudi kitandani na kuzimwaga hela hukuakitetemeka kutokana na woga aliokuwa naoisitoshe ilikuwa ni Mara yake ya kwanza kupata helakama zile.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom