Simulizi: Dada wa kazi

Simulizi: Dada wa kazi

JOTO LA MOTO

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2018
Posts
766
Reaction score
561
SCRIPT ZA IMA
KUTOKA:KWA MSANII JOTO LA MOTO.

SEHEMU YA KWANZA.

NYUMBANI KWA MR BEN-SEBULENI-USIKU.
Mama Esta, Mama,30, na Mr Beni, bwana, 35, wameketi sofani wakipata chakula huku wakipeana michapo ya hapa na pale, upande mwingine kwenye meza ya chakula wapo Meki, kijana barubaru, miaka 17, Esta, binti, miaka 7, na Sia, mdada, miaka 18 nao wakipata chakula, chini ya meza Meki ananyoosha mguu wake na kumgusa Sia, Sia anageuka na kumkata Meki jicho na kumnyooshea kidole huku akitoa tabasamu, na Meki anarudisha tabasamu pamoja na ishara zinazomsababisha Sia kucheka huku akijizuia sauti isitoke, Mr Beni na Mama Esta bado wakiendelea na michapo yao.

NYUMBANI KWA MR BENI-JIKONI-BAADAE.
Sia yupo kwenye sinki anaosha vyombo, “nikusaidie” Sia anashtushwa na sauti ya Meki nyuma yake, Sia anageuka kumuangalia Meki na kutabasamu kisha anasogea pembeni, Meki anasogea kwenye sinki na kuanza kuosha vile vyombo, “shauri yako Meki Mama yako akikukuta hapa tena leo mimi sipo” anasema Sia, “wamesha lala” anasema Meki, “wewe sema tu hivyo na unakumbuka juzi alikuja sebuleni saa tano” anaongeza Sia, “akija nitamwambia tu ukweli” anasema Meki, “ukweli gani?" anauliza Sia, “kwamba nakusaidia” anasema Meki, “mmh” anaguna Sia, kinapita kimya kifupi “kalale utachelewa shule kesho..shauri yako” anasema Sia, “sichelewi” anasema Meki huku akiendelea kuosha vile vyombo, kinapita kimya kifupi “Meki una roho nzuri” anasema Sia, Meki anageuka na kumuangalia Sia huku wote wakiachia tabasamu usoni.

NYUMBANI KWA MR BENI-MIEZI KADHAA BAADAE
Nyuma ya nyumba, Sia ameketi kwenye jiwe, akiwa amejiinamia, mlangoni anatoka Mama Esta na kwenda pale alipoketi Sia, “bado unajisikia vibaya?” anauliza Mama Esta, Sia anashtuka na kuinua kichwa, “kidogo afadhali dada” anasema Sia kwa sauti ya kichovu, “kesho asubuhi tunaenda hospitali ukapimwe” anasema Mama Esta huku Sia akibaki anatoa macho.
Kwenye kona anakuja Meki akiwa amevaa sare za shule, anasimama na kuwaangalia Sia na Mama Esta wakiongea, Mama Esta anaondoka, Meki anakwenda pale alipoketi Sia, “umemwambia?” Meki anamuuliza Sia kwa sauti yenye hofu, “sijamwambia” anajibu Sia, Meki anashusha pumzi kama Mtu aliyepata ahueni ya jambo “kuna Nesi rafiki yangu nimeongea nae..amesema kesho nikupeleke” anasema Meki, Sia anageuka kumuangalia Meki kwa jicho kali, “hivi niongee lugha gani uelewe Meki” anasema Sia kwa sauti ya chini lakini yenye msisitizo, “sitoi” anasema Sia, Meki anashusha pumzi, “sawa” anasema Meki kwa sauti ya chini huku anainuka, “sasa unitaje uone nitakachokufanya” anasema Meki, “utanifanya nini?” anasema Sia kwa sauti ya chini lakini yenye shari, “wewe niharibie tu uone” anasema Meki, “na usifikiri nacheza” anaongeza Meki kwa sauti iliyojaa vitisho huku akiondoka kuelekea ndani ya nyumba,na Sia akimsindikiza na jicho kali.

NYUMBANI KWA MR BEN-SIKU ILIYOFUATA-SEBULENI
Mama Esta ameketi kochini, “Sia” anaita Mama Esta, “bee” inasikika sauti ya Sia, sekunde chache baadae Sia anafika, “hebu keti hapo” Sia anaketi, Mama Esta anashusha pumzi nyepesi, “enhe..majibu yako nadhani umeyaona?” anasema Mama Esta, “sasa naomba uniambie ni nani muhusika” anasema Mama Esta kwa sauti ya chini na ya msisitizo, Sia anabaki kimya, Mama Esta anamuangalia Sia, “nasubiri jibu Sia?” anasema Mama Esta, Sia bado anabaki kimya akiangalia chini, inasikika honi ya gari, Mama Esta anashusha pumzi, “kesho nikitoka kazini nataka jibu” anasema Mama Esta, “andika hata kwenye karatasi unipe kama kuongea huwezi” anasema Mama Esta, Sia anabaki kimya, “hebu niondokee hapa”, Mama Esta anamkaripia Sia, Sia anainuka na kuondoka, mlango unafunguka, anaingia Mr Beni, “pole” Mama Esta anamwambia Mr Beni huku Mr Beni akiweka funguo za gari mezani na kuketi kwenye kochi.
 

Attachments

  • Dada.jpg
    Dada.jpg
    41.3 KB · Views: 848
SCRIPT ZA IMA.
DADA WA KAZI.
SEHEMU YA PILI
.
GENGENI-SIKU INAYOFUATA.
Sia anafika gengeni, “karibu switii” anasema Obo, kijana muuza genge, miaka 22, “vipi bebii wangu” anaongeza Obo kwa sauti ya bashasha huku akitoka gengeni na kuja upande alipo Sia, “naomba usinisumbue..nipe mboga mimi nirudi nyumbani” anasema Sia kwa sauti isiyo na mzaha, “mh” Obo anaguna na kurudi gengeni, “unataka nini leo maana naona upo vibaya” anasema Obo, “nipe nyanya za mia tano na karoti za mia mbili” anasema Sia, “alafu jibu langu utanipa lini Siaa?” anauliza Obo huku akimpatia Sia Nyanya na karoti, “jibu gani?” anauliza Sia kwa ukali, “acha kunizengua basi Siaa” anasema Obo, “unataka nianze tena upya?” anasema Obo, “kumbuka na mimi nina moyo eti Sia” anaendelea Obo, “achana na mimi bana” anasema Sia kwa ukali huku akimpatia Obo sarafu ya shilingi mia tano na ya mia mbili, “hiyo ya kwako” anasema Obo, Sia anabaki anamuangalia Obo kwa ukali kwa sekunde kadhaa kisha anaweka zile pesa pale mezani na kugeuka kuondoka “nasubiri jibu” anapayuka Obo huku Sia akitokomea.

NYUMBANI KWA MR BEN-JIONI.
Sia na Esta wameketi kochini wakiangalia TV, anaingia Meki akiwa kwenye sare za shule, Meki anaona Sia akiwa amefumbata kipande cha limao mkononi, anaketi na kushusha pumzi, “dingi na mama wako wapi?” anauliza Meki, “wameenda kanisani” anajibu Esta, Meki anamuangalia Sia kwa muda, Sia naye anageuka kumuangalia Meki, “siamini kama ungekuja kuwa katili hivi Meki?” anasema Sia, “ukatili gani?” anauliza Meki, Sia anashusha pumzi, “Mungu akusaidie tu huko uendako” anasema Sia, “wewe sema chochote tu unachojisikia..ila ujue sitaki mazoea” anasema Meki, “mazoea ya nini?” anauliza Esta, “wewe hayakuhusu angalia TV kule” Meki anambwatukia Esta, “usifikiri sina stori za Mpare Muuza genge” Meki anamwambia Sia, Sia anageuka kumuangalia Meki kwa mshangao, wanabaki wanaangaliana, Sia anashusha pumzi na kugeuka kuangalia kwenye TV, inasikika honi ya gari, “Daddy” anapayuka Esta huku yeye na Sia wakiinuka na kutoka,Meki anabaki ameketi akibofya bofya remote ya TV.

GENGENI KWA OBO-MCHANA.
Sia anafika gengeni, “karibu bebii” anasema Obo kwa bashasha huku akitoka gengeni na kuja alipo Sia, “upo tayari tukachukue zawadi yako?” anasema Obo, “kuichukua wapi?” anauliza Sia huku ameukunja uso, “si nyumbani?” anasema Obo, “ungetaka kunipa ungenipa wala usinisumbue mimi” anasema Sia, “ushaniona mimi ni wa kwenda kwenye nyumba za watu hovyo” anaongeza Sia, “nipe biringanya mbili nasubiriwa kupika” anasema Sia, Obo anarudi gengeni, anakuja Kibo, kijana wa miaka 21, anasimama pembeni, Obo anachukua biriganya mbili na kumpatia Sia, Sia anatoa noti ya shilingi elfu moja, Obo anatikisa mabega kuashiria hataki kuipokea, Sia anageuka na kuondoka, Kibo anasogea gengeni, “huyu Demu bado anakuzengua tu?” anauliza Kibo, “mambo mazuri hayataki haraka Kibo” anasema Obo.
 
DADA WA KAZI.
SEHEMU YA TATU


NYUMBANI KWA MR BENI-CHUMBANI KWA SIA-USIKU
Sia ameketi kitandani akiibofya simu yake huku Esta yupo kitandani amelala fo fo fo, mlio wa simu wa kuingia ujumbe unasikika, “hutaki kujibu meseji zangu ila najua ipo siku tu tutakuwa karibu Sia” Sia anasoma ujumbe ule ulioingia kwenye simu yake, mara mlango unafunguliwa, anaingia Mama Esta, Sia anashtuka na kuificha ile simu chini ya mto. Mama Esta anaketi juu ya kitanda pembeni ya Sia, “enhe..naona umeamua kukaa kimya tu” anasema Mama Esta, Sia anabaki amejiinamia, wanabaki kimya kwa muda, Sia anashusha pumzi, “Dada” Sia anasema, Mama Esta anatulia kumsikiliza, Sia anashusha pumzi ndefu, “mimba ni ya Meki” anasema Sia, Mama Esta anashtuka na kubaki ameduwaa kwa sekunde kadhaa, “hebu rudia tena?” anauliza Mama Esta kwa sauti ya chini, “huo ndio ukweli Dada” anasema Sia, Mama Esta anabaki kimya ameduwaa kwa sekunde kadhaa, “sikiliza Sia..tena naomba unisikilize vizuri” anasema Mama Esta, “leo iwe mwanzo na mwisho kukusikia unamtaja Mwanangu kwenye ujinga wako” anasema Mama Esta, “Meki ni mwanafunzi” anasema Mama Esta, “jiandae naenda kukata tiketi unarudi kwenu Singida” anasema Mama Esta, “nitarudi kwa nani dada na bibi yangu mlezi nilikwambia ameshafariki” anasema Sia kwa sauti ya upole na uoga, “hayo hayanihusu mimi” anasema Mama Esta huku akiinuka na kutoka, Sia anajiinamia na kutumia kanga yake kujifuta machozi yanayombubujika, mlio wa kuingia ujumbe kwenye simu unasikika, polepole Sia anainua mto na kuichukua simu yake, anaibofya na kusoma ujumbe ulioingia, “nitakusubiri bila kuchoka Sia..nitachoka siku nimekupata” Sia anamaliza kuusoma ujumbe na kuibofya simu off kuizima, anaiweka chini ya mto na kujilaza pale kitandani huku akiendelea kububujikwa machozi.

NYUMBANI KWA MR BENI-NJE-ASUBUHI.
Sia yupo kwenye kiti pembeni ya bomba la maji, chini kukiwa na nguo kadhaa ndoo na sabuni, ametulia akiwa na nguo na sabuni mkononi huku akionekana kama Mtu aliyezama kwenye mawazo mazito, “Sia” anashtushwa na sauti inayomuita upande wa pili, anatulia sekunde chache, “Shali” Sia naye anaita kwa sauti ya juu, “upo wapi wewe?” inauliza tena ile sauti, “njoo nipo huku uwani” anasema Sia, baada ya sekunde chache anafika Shali, dada, 20, akiwa na mfuko wenye vitu ndani “enhe” anasema Shali, “ndio unatoka dukani?” anauliza Sia, “ee” anaitikia Shali, “jana nilikuwa mbiombio tukashindwa kumalizia maongezi yetu” anasema Shali, “yaani Shali mwenzako nipo kwenye njia panda” anasema Sia, “Ni hiyo laki tatu ya mshahara ninayodai haijapatikana ungekuta nimeshaondoka tangu juzi” anaongeza Sia, wanabaki kimya kwa sekunde kadhaa, “ila ule ushauri wako ni mgumu sana Shali” anasema Sia, “Sia..huna namna nyingine besti” anasema Shali, “ukikubali kurudi kule kijijini hivyo umekwisha” anasema Shali, “vile nilivyokuambia ndio njia iliyobaki Siaa” anasema Shali, wanabaki kimya, Sia anashusha pumzi, “hivi hata nitaanzia wapi Shali?” anasema Sia, “simu yako iko wapi?” Shali anamuuliza Sia, “unataka kufanya nini?” anasema Sia huku akimpatia Shali ile simu kwa kusita, Shali anainyakua na kuanza kuibofya akiandika ujumbe na kuutuma, “wewe Shali..umeandika nini?” anauliza Sia baada ya kusikia mlio wa kutuma ujumbe ukitoka kwenye simu yake, “Nimemuuliza ile zawadi ipo tayari?” anasema Shali, “weee” anasema Sia kwa mshtuko, mara unasikika mlio wa kupokea ujumbe, Sia anainuka na kutaka kumpora Shali simu, Shali anakwepa na kusogea pembeni huku akibofya na kuusoma ujumbe, “siamini leo umenitumia ujumbe bebii..nimefurahi mpaka moyo umesimama kwa muda..niambie nikusubiri lini asali wa moyo wangu” Shali anausoma ujumbe kwa sauti huku Sia akiwa amesimama sambamba pembeni yake akimsikiliza, Shali anaangua kicheko, “yaani wewe” anasema Sia huku Shali akiandika tena ujumbe na kutuma, “kesho unipe mrejesho” anasema Shali huku akimpatia Sia ile simu, “umemuambiaje?” anauliza Sia huku akiipokea simu yake, “nimemwambia kesho” anasema Shali na kuondoka akimuacha Sia yupo na butwaa.

NYUMBANI KWA OBO-CHUMBANI-MCHANA.
Sia ameketi juu ya kitanda, kwenye chumba kidogo kilichosongamana kitanda, stuli, jiko la mchina, kiti cha plastiki na vikorokoro vingine kadhaa, Sia ametulia akiangalia huku na kule, mlango unafunguka, anaingia Obo akiwa na chupa ya soda na mfuko mdogo mweusi, “yaani leo siamini umekuja..mpaka nahisi kuchanganyikiwa” anasema Obo kwa bashasha huku akiwa amesimama na chupa ya soda mkononi akimshangaa Sia, Obo anaweka chupa na ule mfuko juu ya stuli, “sasa pale gengeni umemuacha nani?” anauliza Sia, “yupo Kibo yule rafiki yangu” anasema Obo huku akiifungua ile soda, “karibu” anasema Obo huku naye akiketi kwenye kiti, “siku ya leo nitaiandika kwenye kitabu changu” anasema Obo, Sia anamuangalia Obo akimshangaa, “kwa nini?” anauliza Sia, Obo anashusha pumzi, “hujui tu furaha niliyonayo moyoni kwa wewe kufika kwangu Sia” anasema Obo huku akiufungua ule mfuko wenye chips na kuku.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom