Mfyuuu ashindweHata sielewi kwakweli anataka niwawekee arosto
Kesho sasa.....!Sehemu ya 27.
Hapa sio mimi tu, naamini kwa asilimia zote mia moja hata kama ungekuwa ni wewe ndugu msomaji lazima ungechanganyikiwa.
Kwa vyovyote vile niliamini kama sio mama mwenye nyumba wangu alihusika katika hilo basi alifahamu kila kitu kilichokuwa
kimetokea kwa sababu katika mazingira ya kawaida ni jambo lisilowezekana hata kidogo.
Hebu fikiria umefunga mlango wa chumba chako vizuri halafu anakuja mtu kukubaka usiku, asivunje mlango wala kuonyesha dalili zozote kwamba alipitia dirishani. Ungewaza nini kama sio uchawi?
Nilichokifanya niliamka kitandani hapo nikavaa nguo zangu kisha nikatoka kuelekea kwa mama mwenye nyumba wangu, muda huo hasira zilikuwa zimenipanda kwa sababu kitendo nilichokuwa nimefanyiwa hakikuwa kizuri.
“Stella kulikoni mbona asubuhi asubuhi yote hii?” aliniuliza, nilimkuta akiwa anafagia.
“Mama unaweza kuniambia ni nani aliyenibaka?”
“Mwanangu hiyo ndiyo salamu kweli au ndivyo ulivyofundishwa huko nyumbani kwenu kutowasalimia wakubwa zako?” aliniuliza lakini kutokana na hasira nilizokuwa nazo sikutaka kumsalimia, nilichokifanya nikarudia kumuuliza tena kwa mara ya pili aniambie ukweli ni nani aliyenibaka.
Hapo ndipo nilipomkwaza zaidi.
“Stella hivi umechanganyikiwa? Ina maana unataka kuniambia kwamba mimi ndiye niliyekubaka? Mbona unanivunjia heshima wewe mtoto?”
“Sijasema kwamba wewe ndiye uliyenibaka ila utakuwa unafahamu kila kitu.”
“Mimi nafahamu kila kitu?”
“Ndiyo kwa sababu haiwezekani.”
“Kivipi?”
“Mama usijitoe ufahamu, najua unajua kila kitu kwa sababu mazingira niliobakwa ni ya ajabu na humu ndani tunaishi wawili tu.”
Nilipomwambia hivyo alinyamaza kwa muda kidogo, nikamwona kama vile kuna jambo fulani ambalo alikuwa akilitafari na baada ya kumaliza ndipo hapo aliniambia;
“Stella mwanangu mimi siwezi kukufanyia kitu kama hicho, kwanza nawezaje kukubaka wakati mimi ni mwanamke mwenzio?”
aliniuliza sauti ya upole swali hilo ambalo lilikuwa na mantiki kubwa sana lakini kwa sababu alikuwa mchawi niliamini yote hayo yanawezekana. Mchawi ni mchawi tu siku zote, anaweza kufanya kitu kisichowezekana kikawezekana.
“Mimi sijui kama ni wewe ama ni nani anayehusika, nataka kujua,” nilimwambia maneno yaliyozidi kumkwaza.
“Unataka kujua ukweli?” aliniuliza.
“Ndiyo,” nilimjibu.
“Sawa aliyekubaka ni msukule.”
“Msukule?”
“Ndiyo umefanya naye mapenzi usiku kucha bila wewe kujua,” aliniambia, nilipigwa na butwaa.
Sikutaka kuamini hata kidogo, japokuwa nilitaka kuujua ukweli kwa wakati huo lakini baada ya kuambiwa kwamba nilifanya mapenzi na msukule usiku kucha kiukweli hilo liliniogopesha sana na kunifanya niingiwe na simanzi nzito moyoni mwangu.
“Nimefanya mapenzi na msukule?”
“Ndiyo sasa unaogopa nini, si ulitaka kuujua ukweli?” aliniambia huku akiniuliza swali hilo kana kwamba lilikuwa ni jambo la kawaida kufanya mapenzi na msukule.
Moyo wangu ulilipuka kwa maumivu makali na kila nilipokuwa nikiifikiria kauli hiyo nilihisi kuchanganyikiwa.
Hapa najua kuna watu wanaweza wakajiuliza msukule uliweza vipi kufanya mapenzi na mimi? Swali hili ndilo ambalo hata mimi muda huo nilijiuliza bila kupata jibu.
Hakika lilikuwa ni jambo la kushangaza sana, wakati mwingine nilitamani iwe ni ndoto kama zilivyokuwa ndoto nyingine lakini huo ndiyo ulikuwa ukweli wenyewe. Nilifanyishwa mapenzi na msukule bila kujijua.
Labda nikwambie tu, huo haukuwa ni mwisho wangu wa kufanyishwa mapenzi na msukule bali ndiyo ulikuwa mwanzo.
Kila siku nilipokuwa nikiamka asubuhi na kujiangalia sehemu zangu za siri nilikuta tayari nimeshaingiliwa kimwili bila kujijua. Ukiachana na hilo pia nilihisi uchovu wa mwili usiokuwa wa kawaida.
Kiukweli niliumia sana, kuna wakati nilitamani kwenda polisi kushtaki kutokana na ukatili niliokuwa nafanyiwa na mama mwenye nyumba wangu lakini sikujua ningeanzia wapi?
Kwanza hivi kuna kesi gani ya ubakaji inaweza ikafunguliwa mahakamani kwa madai kwamba nimebakwa na msukule?
Hilo ni jambo lisilowezekana hata kidogo na hiyo ndiyo sababu ambayo naweza kusema ilinifanya nisifikirie kwenda polisi kwa wakati huo.
***
Siku ziliendelea kukatika, katika kipindi hicho sikujua kama nilibeba ujauzito mpaka pale ambapo nilianza kuhisi dalili, nilipoenda hospitalini kupima ndipo hapo majibu yalionyesha kwamba kweli nilikuwa nina ujauzito.
Mpaka kufikia hapo ilimaanisha kuwa nilibeba ujauzito wa msukule. Huo ndiyo ulikuwa ukweli ambao sikutaka kukubaliana nao kabisa.
“Hapana dokta haiwezekani,” nilimwambia daktari wakati akinipa majibu hayo.
“Haiwezekani kivipi na wakati vipimo vinaonyesha kwamba una ujauzito tena wa mwezi mmoja na nusu,” aliniambia daktari huku akiendelea kunisisitiza ukweli wa majibu ya vipimo.
“Ina maana nimebeba mimba ya msukule?” niliropoka.
“Mimba ya msukule? Kivipi? Una maanisha nini?” aliniuliza maswali matatu kwa mpigo, muda huo hata yeye mwenyewe alishangaa.
“Aa..ah..hakuna kitu,” nilimjibu kwa kigugumizi huku nikipotezea mada muda huo, sikutaka kumwambia kitu kilichokuwa kikiendelea lakini kwa kufanya hivyo moja kwa moja ilipelekea ahisi kuna kitu nilichokuwa nikimficha ambacho ndicho kilichokuwa kikiendelea nyuma ya pazia.
“Nimekusikia lakini ukisema kwamba umebeba mimba ya msukule?” aliniuliza huku akionekana kutoamini hicho alichokisikia.
“Ni kweli dokta huu ujauzito ni wa msukule,” nilimjibu, jibu hilo lilizidi kumchanganya sana.
“Kivipi? inawezekanaje binadamu akazaa na msukule?”
“Dokta najua huwezi kunielewa lakini wewe fahamu hivyo kuwa nimebeba ujauzito wa msukule,” nilimjibu.
Japokuwa nilimwambia ukweli daktari huyo lakini kile nilichomweleza kwa wakati huo alikiona kuwa kama maigizo.
Hakutaka kuamini hata kidogo, hata hivyo sikuwa na muda wa kumwelewesha zaidi na zaidi, nilichokifanya niliondoka zangu kuelekea nyumbani huku kichwa changu kikiwa kimetawaliwa na mawazo lukuki.
***
Kwa mambo yote hayo yaliyokuwa yakiendelea kunitokea katika maisha yangu najua unaweza ukahisi kwamba labda nilifukuzwa nyumbani kwetu ama sikuwa na ndugu yeyote hapa mjini na hiyo ndiyo sababu ambayo ilinifanya nishindwe kwenda kuomba msaada.
Haikuwa hivyo, ndugu nilikuwa nao na hata wazazi wangu pia walikuwepo ila sijui ni nini kilitokea, katika kipindi hicho sikukumbuka kama nilikuwa nina ndugu, hata wazo la kuwapigia simu kiukweli sikuwa nalo kichwani mwangu, ajabu sasa hata wao pia hawakunikumbuka jambo lililonifanya nizidi kusahau kama nilikuwa nina ndugu.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa, naweza kusema nilirogwa kwa sababu kwa akili ya haraka haraka ni jambo lisilowezekana mtu kusahau nyumbani kwao ama ndugu zake.
Je nini kiliendelea?
Tukutane kesho.....
Upuuzwe tuNatamani haya mauza uza yangemkumba marehemu màgufool kipindi cha mwisho mwisho cha uhai wake
Mfyuu me unaniudhi na hizo kesho zakoSehemu ya 27.
Hapa sio mimi tu, naamini kwa asilimia zote mia moja hata kama ungekuwa ni wewe ndugu msomaji lazima ungechanganyikiwa.
Kwa vyovyote vile niliamini kama sio mama mwenye nyumba wangu alihusika katika hilo basi alifahamu kila kitu kilichokuwa
kimetokea kwa sababu katika mazingira ya kawaida ni jambo lisilowezekana hata kidogo.
Hebu fikiria umefunga mlango wa chumba chako vizuri halafu anakuja mtu kukubaka usiku, asivunje mlango wala kuonyesha dalili zozote kwamba alipitia dirishani. Ungewaza nini kama sio uchawi?
Nilichokifanya niliamka kitandani hapo nikavaa nguo zangu kisha nikatoka kuelekea kwa mama mwenye nyumba wangu, muda huo hasira zilikuwa zimenipanda kwa sababu kitendo nilichokuwa nimefanyiwa hakikuwa kizuri.
“Stella kulikoni mbona asubuhi asubuhi yote hii?” aliniuliza, nilimkuta akiwa anafagia.
“Mama unaweza kuniambia ni nani aliyenibaka?”
“Mwanangu hiyo ndiyo salamu kweli au ndivyo ulivyofundishwa huko nyumbani kwenu kutowasalimia wakubwa zako?” aliniuliza lakini kutokana na hasira nilizokuwa nazo sikutaka kumsalimia, nilichokifanya nikarudia kumuuliza tena kwa mara ya pili aniambie ukweli ni nani aliyenibaka.
Hapo ndipo nilipomkwaza zaidi.
“Stella hivi umechanganyikiwa? Ina maana unataka kuniambia kwamba mimi ndiye niliyekubaka? Mbona unanivunjia heshima wewe mtoto?”
“Sijasema kwamba wewe ndiye uliyenibaka ila utakuwa unafahamu kila kitu.”
“Mimi nafahamu kila kitu?”
“Ndiyo kwa sababu haiwezekani.”
“Kivipi?”
“Mama usijitoe ufahamu, najua unajua kila kitu kwa sababu mazingira niliobakwa ni ya ajabu na humu ndani tunaishi wawili tu.”
Nilipomwambia hivyo alinyamaza kwa muda kidogo, nikamwona kama vile kuna jambo fulani ambalo alikuwa akilitafari na baada ya kumaliza ndipo hapo aliniambia;
“Stella mwanangu mimi siwezi kukufanyia kitu kama hicho, kwanza nawezaje kukubaka wakati mimi ni mwanamke mwenzio?”
aliniuliza sauti ya upole swali hilo ambalo lilikuwa na mantiki kubwa sana lakini kwa sababu alikuwa mchawi niliamini yote hayo yanawezekana. Mchawi ni mchawi tu siku zote, anaweza kufanya kitu kisichowezekana kikawezekana.
“Mimi sijui kama ni wewe ama ni nani anayehusika, nataka kujua,” nilimwambia maneno yaliyozidi kumkwaza.
“Unataka kujua ukweli?” aliniuliza.
“Ndiyo,” nilimjibu.
“Sawa aliyekubaka ni msukule.”
“Msukule?”
“Ndiyo umefanya naye mapenzi usiku kucha bila wewe kujua,” aliniambia, nilipigwa na butwaa.
Sikutaka kuamini hata kidogo, japokuwa nilitaka kuujua ukweli kwa wakati huo lakini baada ya kuambiwa kwamba nilifanya mapenzi na msukule usiku kucha kiukweli hilo liliniogopesha sana na kunifanya niingiwe na simanzi nzito moyoni mwangu.
“Nimefanya mapenzi na msukule?”
“Ndiyo sasa unaogopa nini, si ulitaka kuujua ukweli?” aliniambia huku akiniuliza swali hilo kana kwamba lilikuwa ni jambo la kawaida kufanya mapenzi na msukule.
Moyo wangu ulilipuka kwa maumivu makali na kila nilipokuwa nikiifikiria kauli hiyo nilihisi kuchanganyikiwa.
Hapa najua kuna watu wanaweza wakajiuliza msukule uliweza vipi kufanya mapenzi na mimi? Swali hili ndilo ambalo hata mimi muda huo nilijiuliza bila kupata jibu.
Hakika lilikuwa ni jambo la kushangaza sana, wakati mwingine nilitamani iwe ni ndoto kama zilivyokuwa ndoto nyingine lakini huo ndiyo ulikuwa ukweli wenyewe. Nilifanyishwa mapenzi na msukule bila kujijua.
Labda nikwambie tu, huo haukuwa ni mwisho wangu wa kufanyishwa mapenzi na msukule bali ndiyo ulikuwa mwanzo.
Kila siku nilipokuwa nikiamka asubuhi na kujiangalia sehemu zangu za siri nilikuta tayari nimeshaingiliwa kimwili bila kujijua. Ukiachana na hilo pia nilihisi uchovu wa mwili usiokuwa wa kawaida.
Kiukweli niliumia sana, kuna wakati nilitamani kwenda polisi kushtaki kutokana na ukatili niliokuwa nafanyiwa na mama mwenye nyumba wangu lakini sikujua ningeanzia wapi?
Kwanza hivi kuna kesi gani ya ubakaji inaweza ikafunguliwa mahakamani kwa madai kwamba nimebakwa na msukule?
Hilo ni jambo lisilowezekana hata kidogo na hiyo ndiyo sababu ambayo naweza kusema ilinifanya nisifikirie kwenda polisi kwa wakati huo.
***
Siku ziliendelea kukatika, katika kipindi hicho sikujua kama nilibeba ujauzito mpaka pale ambapo nilianza kuhisi dalili, nilipoenda hospitalini kupima ndipo hapo majibu yalionyesha kwamba kweli nilikuwa nina ujauzito.
Mpaka kufikia hapo ilimaanisha kuwa nilibeba ujauzito wa msukule. Huo ndiyo ulikuwa ukweli ambao sikutaka kukubaliana nao kabisa.
“Hapana dokta haiwezekani,” nilimwambia daktari wakati akinipa majibu hayo.
“Haiwezekani kivipi na wakati vipimo vinaonyesha kwamba una ujauzito tena wa mwezi mmoja na nusu,” aliniambia daktari huku akiendelea kunisisitiza ukweli wa majibu ya vipimo.
“Ina maana nimebeba mimba ya msukule?” niliropoka.
“Mimba ya msukule? Kivipi? Una maanisha nini?” aliniuliza maswali matatu kwa mpigo, muda huo hata yeye mwenyewe alishangaa.
“Aa..ah..hakuna kitu,” nilimjibu kwa kigugumizi huku nikipotezea mada muda huo, sikutaka kumwambia kitu kilichokuwa kikiendelea lakini kwa kufanya hivyo moja kwa moja ilipelekea ahisi kuna kitu nilichokuwa nikimficha ambacho ndicho kilichokuwa kikiendelea nyuma ya pazia.
“Nimekusikia lakini ukisema kwamba umebeba mimba ya msukule?” aliniuliza huku akionekana kutoamini hicho alichokisikia.
“Ni kweli dokta huu ujauzito ni wa msukule,” nilimjibu, jibu hilo lilizidi kumchanganya sana.
“Kivipi? inawezekanaje binadamu akazaa na msukule?”
“Dokta najua huwezi kunielewa lakini wewe fahamu hivyo kuwa nimebeba ujauzito wa msukule,” nilimjibu.
Japokuwa nilimwambia ukweli daktari huyo lakini kile nilichomweleza kwa wakati huo alikiona kuwa kama maigizo.
Hakutaka kuamini hata kidogo, hata hivyo sikuwa na muda wa kumwelewesha zaidi na zaidi, nilichokifanya niliondoka zangu kuelekea nyumbani huku kichwa changu kikiwa kimetawaliwa na mawazo lukuki.
***
Kwa mambo yote hayo yaliyokuwa yakiendelea kunitokea katika maisha yangu najua unaweza ukahisi kwamba labda nilifukuzwa nyumbani kwetu ama sikuwa na ndugu yeyote hapa mjini na hiyo ndiyo sababu ambayo ilinifanya nishindwe kwenda kuomba msaada.
Haikuwa hivyo, ndugu nilikuwa nao na hata wazazi wangu pia walikuwepo ila sijui ni nini kilitokea, katika kipindi hicho sikukumbuka kama nilikuwa nina ndugu, hata wazo la kuwapigia simu kiukweli sikuwa nalo kichwani mwangu, ajabu sasa hata wao pia hawakunikumbuka jambo lililonifanya nizidi kusahau kama nilikuwa nina ndugu.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa, naweza kusema nilirogwa kwa sababu kwa akili ya haraka haraka ni jambo lisilowezekana mtu kusahau nyumbani kwao ama ndugu zake.
Je nini kiliendelea?
Tukutane kesho.....
saint annaShukrani ya punda
Mwaaah mwaaah barikiwa kipenziSehemu ya 29.
Nilishtuka kutoka usingizi, jasho lilinitiririka mno, mapigo ya moyo wangu yalikuwa yakidunda kupita kawaida huku mwili wangu ukisisimka sana.
Niliangalia saa ya ukutani, ilionyesha muda huo ilikuwa ni saa nane usiku, nilipochungulia nje, giza totoro lilikuwa limetawala kwa wakati huo.
Nilikaa kitandani huku picha kamili ya ndoto hiyo nilioiota ikianza kunijia kichwani mwangu.
Nilikumbuka kila kitu kilichokuwa kimetokea kuanzia nilipokufa mpaka pale nilipokuwa nikipelekwa makaburini kuzikwa.
Huku nikiwa sifahamu kitu kilichokuwa kimetokea, mara macho yangu yakaanza kuwa mazito, muda huo sikuweza kufahamu ni nini kilitokea mpaka kusababisha hali hiyo lakini ghafla! nikajikuta nipo ndani ya chumba kimoja.
Huku nikiwa najiuliza maswali kwamba mahali hapo nilifikaje, mbele yangu alisimama mama mwenye nyumba wangu.
“Stella nilikwambia ninakudai kiumbe changu ukajifanya mjanja ukanikimbia, ona sasa mbio zako zimeishia ukingoni,” aliniambia huku akinicheka, sauti ya kicheko chake kilikuwa kikijirudia masikioni mwangu kama vile sauti ya mwang’wi.
“Naomba unisamehe,” nilimwambia huku nikiogopa sana.
“Siwezi kukusamehe.”
Aliponiambia hivyo katika hali ya kushangaza nikashikwa na uchungu. Nilipiga kelele nyingi za kuomba msaada lakini mama mwenye nyumba wangu alibaki akiniangalia huku akicheka mpaka pale ambapo nilikumbwa na usingizi mzito. Sikujua ni kitu gani kiliendelea.
***
Nilipata fahamu nikajikuta nikiwa ndani ya chumba changu kile nilichopanga Sinza. Ndani humo sikuwa peke yangu, tulikuwa wengi sana.
Ile kutazama huku na kule ndipo hapo nilishangaa kumwona Glory. Nilimuita lakini hakusikia wala kuonyesha ishara yoyote kwamba alinisikia kwa wakati huo.
Wakati niking’ang’ana kumuita mara mama mwenye nyumba wangu aliingia.
“Usijisumbue kumuita, huyo ni msukule hawezi kukusikia,” aliniambia kisha akaendelea.
“Nasubiria muda wako ufike na wewe nikufanye msukule kama wenzako.”
“Muda wangu ufike?”
“Ndiyo.”
“Kivipi?”
“Nasubiria uzikwe kwanza,” aliniambia huku akimaanisha kwamba kwa wakati huo nilikuwa nimekufa. Sikutaka kuamini.
Huo ndiyo ulikuwa ukweli kwamba nilikuwa nimekufa kwa wakati huo lakini katika hali ya kustaajabisha kumbe kulikuwa kuna nguvu mbili zilizokuwa zinashindana.
Sikufahamu lolote lile mpaka pale ambapo nilizinduka na kujikuta nipo kanisani, muda huo mchungaji alikuwa akiniombea.
Kiukweli nilishangaa sana, nilijiuliza maswali mengi ilikuwaje mpaka nikafika kanisani hapo na wakati mara ya mwisho nakumbuka nilikuwa katika kile chumba cha misukule?
“Pole sana binti, Mungu ametenda muujiza mkubwa sana katika maisha yako,” aliniambia mchungaji kisha akanyamaza kwa muda kiasi cha kumeza fundo moja la mate halafu akaendelea kuniambia.
“Ulikuwa umelala usingizi wa kifo na kama sio huyu rafiki yako kukuleta kwenye maombi sidhani kama ungekuwa hai.”
Aliponiambia hivyo ndipo hapo kumbukumbu zikaanza kurejea kichwani mwangu na nikawakumbuka wazazi wangu pamoja na ndugu zangu.
Kwa uwezo wa Mungu mama mwenye nyumba wangu alikuja kanisani hapo, akatubu dhambi zake. Lilikuwa ni jambo la kushangaza sana ambalo lilimuacha kila muumini wa kanisa hilo mdomo wazi. Hakukuwa kuna mtu ambaye alitaka kuamini hilo hata kidogo.
Huo ndiyo mkasa ulionisibu kipindi nilipopanga chumba cha misukule bila kujua. Hapa nilichokuwa najaribu kukwambia muda wote huo ni kwamba uchawi upo, unachotakiwa kukifanya ni kumtanguliza Mungu mahali popote pale.
Laiti kama ningemtanguliza Mungu sidhani kama yote haya yangenitokea. Japokuwa kwa sasa imebakia kuwa simulizi tu! ambayo ningependa isimuliwe kizazi hadi kizazi, naomba ujifunze kitu kupitia mkasa huu.
MWISHO.
Hahahaa ndo nimeamia kwenye hiyo baada ya robertson kunifanyia matusiHahahahhaah chizi wewe halafu inaonekana unaipenda sana saint anna