Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
Mtunzi Juma Hiza
Sehemu ya 01.
Huu ni mkasa ambao sitoweza kuusahau katika maisha yangu mpaka siku nitakayokufa.
Kwa jina naitwa Stella ni mtoto wa pili na mwisho kuzaliwa katika familia yetu. Kwa sasa ninapokusimulia mkasa huu nina umri wa miaka ishirini na saba.
Nakumbuka siku ya kwanza nilipoanza kuishi maisha yangu ya kujitegemea ilikuwa ni pale nilipohitimu elimu yangu ya chuo kikuu cha Dar es Salaam na kufanikiwa kupata kazi katika kampuni moja hapa mjini ambayo ilikuwa ikinilipa mshahara mzuri uliokidhi mahitaji yangu.
Katika kipindi hicho nilinunua vitu vyote vya umuhimu ambavyo vilihitajika wakati wa kuanza maisha. Nilipoona nimekamilisha kila kitu ndipo hapo nilipoanza kutafuta chumba.
Nilijitahidi kutafuta chumba sehemu tofauti tofauti bila mafanikio yoyote, nilipoona nimeshindwa ndipo hapo nilipoamua kumtafuta dalali mzoefu wa kazi hiyo aliyekuwa akiitwa Mbegu.
Nilipompata na kumwelezea shida yangu kwamba nilihitaji chumba cha aina gani aliweza kunielewa na haraka alianza mchakato wa kunitafutia chumba hicho.
Hazikupita siku nyingi hatimaye alifanikiwa kupata chumba hicho.
Nakumbuka siku hiyo nilikuwa ofisini nikiendelea kufanya kazi zangu kama ilivyokuwa kawaida. Ghafla! simu yangu ilianza kuita, nilipoangalia kwenye kioo cha simu na kuliona jina la dalali, Mbegu haraka sana nilipokea.
“Vipi Stella za kazi?” sauti ya dalali Mbegu ilinipokea simuni kwa kunisalimu.
“Nzuri tu sijui wewe,” nilimjibu.
“Kwangu pia ni nzuri.”
“Enhe niambie, umefikia wapi?”
“Nimefanikiwa kupata chumba.”
“Kipo maeneo gani?”
“Kulekule Sinza kwa Remi uliponiambia.”
“Ni kizuri?”
“Ndiyo naamini utakipenda sana, kimeendana na uzuri wako pia.”
“Hahaha! Sawa basi jioni nikitoka kazini nitakupitia hapo kijiweni ili niende nikakione.”
“Hakuna tatizo bosi wangu.”
“Sawa,” nilimwambia kisha nikakata simu.
Je nini kitaendelea.
Sehemu ya 01.
Huu ni mkasa ambao sitoweza kuusahau katika maisha yangu mpaka siku nitakayokufa.
Kwa jina naitwa Stella ni mtoto wa pili na mwisho kuzaliwa katika familia yetu. Kwa sasa ninapokusimulia mkasa huu nina umri wa miaka ishirini na saba.
Nakumbuka siku ya kwanza nilipoanza kuishi maisha yangu ya kujitegemea ilikuwa ni pale nilipohitimu elimu yangu ya chuo kikuu cha Dar es Salaam na kufanikiwa kupata kazi katika kampuni moja hapa mjini ambayo ilikuwa ikinilipa mshahara mzuri uliokidhi mahitaji yangu.
Katika kipindi hicho nilinunua vitu vyote vya umuhimu ambavyo vilihitajika wakati wa kuanza maisha. Nilipoona nimekamilisha kila kitu ndipo hapo nilipoanza kutafuta chumba.
Nilijitahidi kutafuta chumba sehemu tofauti tofauti bila mafanikio yoyote, nilipoona nimeshindwa ndipo hapo nilipoamua kumtafuta dalali mzoefu wa kazi hiyo aliyekuwa akiitwa Mbegu.
Nilipompata na kumwelezea shida yangu kwamba nilihitaji chumba cha aina gani aliweza kunielewa na haraka alianza mchakato wa kunitafutia chumba hicho.
Hazikupita siku nyingi hatimaye alifanikiwa kupata chumba hicho.
Nakumbuka siku hiyo nilikuwa ofisini nikiendelea kufanya kazi zangu kama ilivyokuwa kawaida. Ghafla! simu yangu ilianza kuita, nilipoangalia kwenye kioo cha simu na kuliona jina la dalali, Mbegu haraka sana nilipokea.
“Vipi Stella za kazi?” sauti ya dalali Mbegu ilinipokea simuni kwa kunisalimu.
“Nzuri tu sijui wewe,” nilimjibu.
“Kwangu pia ni nzuri.”
“Enhe niambie, umefikia wapi?”
“Nimefanikiwa kupata chumba.”
“Kipo maeneo gani?”
“Kulekule Sinza kwa Remi uliponiambia.”
“Ni kizuri?”
“Ndiyo naamini utakipenda sana, kimeendana na uzuri wako pia.”
“Hahaha! Sawa basi jioni nikitoka kazini nitakupitia hapo kijiweni ili niende nikakione.”
“Hakuna tatizo bosi wangu.”
“Sawa,” nilimwambia kisha nikakata simu.
Je nini kitaendelea.