SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,803
- 25,444
- Thread starter
- #841
***SURA YA SABINI NA SITA***
(MSIMU WA 02)
MTUNZI: Stevie Mollel
No: 0685 758 123
Baada tu ya mlango wa chumba kufungwa, Rajul alijaribu tena kuita jina la Stanis mara tatu pasipo majibu. Alichungulia kwenye kitundu lakini hakuona kitu kwa sababu ya giza lililokuwepo kwenye chumba cha Stanis.
Alipiga piga tena ukuta, mara hii Stanis akashituka, ila hakutoa sauti yoyote.
“Stanis! … Stanis upo?” Rajul alinong’oneza baada ya kusikia sauti ya mtu akisogea.
“Eeeiiigh …” Stanis aliitikia kwa kukoroma. Rajul akatabasamu.
“Stanis, inabidi utoroke, la sivyo utauwawa. Unanisikia?”
“Eeeeiggh …”
“Inabidi uondoke humo kwa njia yoyote. Inabidi tutoroke la sivyo, Kim atafanikiwa adhma yake.”
“Eeeeiigghhh …”
“Ili Kim afanikiwe anahitaji damu. Na endapo nikimwambia hilo basi atakufanya sadaka. Akikufanya sadaka, atapata nguvu. Akipata nguvu, hakutokuwa na wa kumzuia tena.”
“Eeeigggh …”
“Una wazo lolote la kutoroka?”
“Eeeiigggh …”
“Stanis, huwezi kuongea neno lolote?”
“Eeeiiggh …”
“Mungu wangu!” Rajul alijibamiza kichwa akaegemea ukuta.
“Nifanye nini sasa? … Nifanye nini?”
Aliwaza na kuwazua kwa dakika kadhaa, mara akatikisa kichwa na kusema:
“Hii sasa ndio njia. Hii ndio njia pekee.”
Aligeukia kwenye kitundu, akamuita Stanis.
“Stanis, nina njia ya kututoa humu. Upo tayari?”
“Eeeiggh …” Stanis akaitikia kwa kukoroma kama ada.
***
Sauti kubwa ya mlio wa pembe la ng’ombe ililia na kumshitua Vitalis aliyekuwa amelala.
Ilikuwa ni asubuhi sasa ya saa kumi na mbili hata jua halijasimama. Vitalis alimtizama Kaguta aliyelala upande wake wa kushoto akamuona yu hoi usingizini. Asimsumbue hata, akanyanyuka na kutoka nje atizame kunani. Huko akakutana na Bernadetha, Bakari na Miraji, wote walikuwa wametoka nje kushangaa. Kama wehu, wenyeji wao walikuwa wanatoka kwenye makazi yao wakikimbia kuelekea msituni sauti inapotokea. Wakiwa wamebung’aa wasipate hata mtu wa kumuuliza, wakamuona kiongozi. Upesi, Vitalis alimkimbilia akamwambia:
“Unajua ni wewe tu ndiye unayeongea lugha tunayoielewa.”
Kiongozi akaitikia kwa kutikisa kichwa.
“Kuna nini?” Vitalis aliuliza. “Mbona watu wanakimbia?” Kiongozi akatabasamu.
“Kuna taarifa ya mateka wamekamatwa mtegoni.” Alisema. “Usiwe na hofu.”
Kauli yake hiyo ikafungwa kwa kuingizwa kwa mateka hao ndani ya kijiji wakiwa wamewekwa chini ya ulinzi mkali. Vitalis alimuona Mamba pamoja na wenzake, akajikuta anatabasamu na kusema:
“Mungu mkubwa. Amenipa nafasi ya kutimiza ahadi yangu.”
“Vitalis!” Mamba alishangaa kumuona adui yake. Alijikuta anacheka kwanza kisha ndiyo akaendelea kunena:
“Sikujua kama ulikuja kuomba msaada wa watu hawa washamba ... wa kale ... wasiojua ulimwengu unaendaje.”
Alicheka tena alafu akaendelea:
“Sikujua kama wewe ni muoga kiasi hiki. Sikujua kama wewe ni mwanamke kiasi hiki. Vitalis, watu wanavyokudhania huko nje ni tofauti na ulivyo. Hawajui jinsi gani ulivyo mtu wa kujificha na kukimbia kama panya."
Mamba aliongea kwa kejeli akiupindisha mdomo wake. Vitalis akamuuliza:
"Unakumbuka ahadi yangu niliyoiweka mbele yako kule kiwandani?"
"Ahadi gani wewe mwanamke?" Mamba akauliza pia. Vitalis akamsogelea karibu zaidi.
"Nilikuambia siku nikikutia mikononi nitahakikisha nakuharibu mpaka mama yako mzazi ashindwe kukutambua. Siku yenyewe ndiyo leo."
"Karibu!” Mamba alisema akimuita Vitalis kwa ishara ya ulimi. “… sasa nitapambanaje na nimefungwa kama mzigo wa msafiri?" Akauliza. Vitalis akamuomba kiongozi ampatie mtu huyo, kiongozi akaridhia. Mamba alifunguliwa kamba, wakapewa uwanja.
La haula, kabla Vitalis hajajiweka sawa, Mamba alijitosa hewani akamgawia teke zito lililomzoa na kumbwaga chini mwanaume huyo.
Upesi Vitalis aliamka kwa sarakasi akajiweka sawa kisha akatulia kungojea tena shambulizi.
Mamba akatuma tena teke, mara hii likadakwa na mkono wa kuume wa Vitalis. Teke hilo likavutwa karibu kisha Vitalis akaruka na kujigeuza akimtandika Mamba kisigino cha taya. Mithili ya mzigo, Mamba akarushiwa kando.
Aliponyanyuka kwa hasira aonyeshe ubabe wake, akaula tena wa chuya, kila ngumi na teke alilorusha zikakwepwa kisha akazawadiwa ngumi nzito chini ya kifua, akacheua damu.
Mamba alifuta damu yake kwa kiganja kisha akaguna. Alikimbia kumfuata Vitalis, ila Vitalis akamkwepa haraka na kumuwekea goti la mguu wa kushoto mwanaume huyo aliyegota hapo kama gari la mwendo kasi. Kama haitoshi, Vitalis akarusha mguu wake wa kulia na kumkita nao Mamba shingoni. Sasa Mamba akadondoka chini ila akiwa katikati ya miguu ya Vitalis. Miguu ikabanwa kwanguvu na kumnyima Mamba hewa. Alirusha ngumi kwa fujo ajiokoe, Vitalis akakamata mikono hiyo na kuivunja kisha akavuta jabali lililokuwa pembeni akaponda uso wa Mamba mpaka pale ulipokuwa chapati.
Damu zilimrukia Vitalis kwa fujo. Shati lake lote na hata suruali vilichafuka damu. Wakati anafanya tukio hilo la kuponda kila mtu alimshangaa. Ni kama vile alikuwa anaponda mawe kumbe kichwa cha mtu. Hakuwa na roho ya ubinadamu hata kidogo muda huo bali ya shetani, tena shetani mwekundu. Hakuacha hilo zoezi mpaka pale alipokuja kutolewa na Kiongozi aliyemvutia pembeni na kumtaka apunguze jazba.
Aliwatizama wenzake na Mamba akawaambia:
“Nyie ndio mnafuata!”
Watu hao, isipokuwa chotara, walimtizama Vitalis kana kwamba wanatizama pundamilia akimla simba. Chotara yeye alikuwa hoi asijali hata kinachoendelea. Alisimama kama mgomba ulioelemewa na mkungu wa ndizi. Alikuwa ametota jasho mdomo ukiwa mkavu mno. Macho yake yalikuwa yamelegea yakiwa mekundu ya kutisha.
Vitalis alijikwamua toka mikononi mwa Kiongozi akajiendea ndani asiwaone watu hao. Mateka walitundikwa mitini, watu wakaendelea na shughuli zingine kama ada. Baada ya muda mfupi, Bakari aliwafuata hao mateka waliotundikwa mitini akawapekua mifukoni. Miongoni mwa mmoja wao alikuta simu. Aliitia mfukoni mwake akawauliza:
“Mmetumwa na nani?”
Mateka wale watatu, walio wazima wa afya, wakatabasamu.
“Usitegemee kupata jibu lolote toka kwetu.” Mmoja alijibu.
Bakari alimfuata chotara akamtizama kwa karibu. Aliona mishipa ya shingoni ya mwanaume huyo imegeuka kuwa rangi ya kijani. Alimfungua macho akamtizama, napo akaona macho ya mwanaume huyo yakiwa na umbijani kwa mbali, akaishia kutikisa kichwa na kusema:
“Mwenzenu atakufa muda si mrefu.”
“Tunaomba umsaidie.” Mmoja akasema. “Tafadhali naomba umsaidie.”
Bakari akatabasamu.
“Usitegemee kupata msaada wowote toka kwangu.”
Alisema kisha akajigeuza aondoke. Akaitwa.
“Tafadhali msaidie. Tutakuambia unayoyataka.”
“Vipi kama mkiniambia alafu ndiyo niwasaidie?” Bakari alisema akisogea karibu kwa aliyemuita.
“Hapana! Tutajuaje kama unatulaghai?”
“Na mimi nitajuaje kama mtanilaghai?”
“Hatuwezi kufanya hivyo. Tukikulaghai, tutaondokaje na mmetufungia mtini?”
“Siwezi jua. Ila ingekuwa vema kama mngeniambia upesi ili mwenzenu apate tiba upesi, yupo kwenye hali mbaya. Si mnamuona?” Bakari alimtizama chotara.
Alikatizwa zoezi lake hilo na sauti ya Bernadetha iliyomuita. Aliaga akaahidi kurudi upesi kumalizana nao. Aliondoka, Kaguta akasogea karibu na mateka. Muda wote Bakari aliokuwepo hapo, Kaguta alikuwa akimtizama kwa karibu.
Sura yake ilikuwa imekunjamana. Macho yake yalikuwa yamevimba na mekundu. Mdomo wake ulibinuliwa kwa kebehi ama hasira. Nyuma ya mgongo wake alikuwa amefichama mkono uliobebelea kisu. Aliwatizama mateka akawaambia kwa sauti ya chini:
“Nimekuja kudai uhai wenu.”
Bakari aliporejea baadae kwa mateka hao, akawakuta wote wamekufa. Kila mmoja alikuwa anachuruza damu kifuani mwake akiwa na matundu ya visu si chini ya mawili.
“Samahani kwa kuingilia maongezi yako.” Sauti ya Kaguta ilimfikia Bakari na kumshitua. Aligeuka akamkuta Kaguta nyuma yake.
“Kwanini umewaua?” Bakari aliuliza. “Kuna taarifa muhimu walikuwa wanataka kunipa!”
“Unadhani wangekuambia kitu?” Kaguta aliuliza. “Kama ulitegemea kitu toka kwa watu waliokula viapo vya kutosema lolote, pole sana. Hawa watu hawastahili huruma yoyote.”
Baada ya kusema hivyo Kaguta aliondoka akaelekea ndani ya kijumba. Alinyofoa mtungi wa pombe uliokuwepo chini ya kitanda cha ngozi alaliacho, akamwagia kinywaji hicho ndani yake mpaka pale alipozima akalala. Hakutia tumboni kitu chochote isipokuwa pombe hiyo ya kienyeji. Hata pale jioni alipoamka, aliamkia na pombe hiyo. Ni Vitalis ndiye aliyekuja kumuokoa toka kwenye hiyo shughuli.
“Inatosha!” Vitalis alisema akimpokonya Kaguta mtungi wa pombe kwanguvu.
“Unadhani itasaidia?” Vitalis aliuliza. “Haitosaidia zaidi ya kutuongezea msiba mwingine, Kaguta!” Alifoka. Aliweka kituo akapunguza sauti.
“Tuna maongezi. Tunakungojea nje, fanya uje.”
Alitoka ndani ya chumba, Kaguta akamfuata baada ya muda mfupi.
Wakiwa watano, WAGENI, wamekaa kwenye benchi refu, waliteta:
“Sasa ni muda wa kwenda kumalizana na adui yetu mkubwa.” Vitalis alifungua maongezi. “Kila tunachokihitaji tunacho. Hatuna tena muda wa kungoja.” Alimtizama Bakari, Bakari akachukua zamu:
“Nilifanikiwa kwenda town kuchaji simu. Bahati nzuri baada ya simu kuwaka, barua pepe toka kwa Mr Kim ziliingia. Nilichat naye nikijifanya mimi ni mtumishi wake, nikapata taarifa muhimu za kutufikisha alipo.”
“Basi twende!” Kaguta aliropoka. “Tunangoja nini?”
“Tulia Kaguta.” Vitalis akasihi. “Si tu kwenda, tupange kwanza. Unajua tutafikia wapi? Unajua tutafanyaje kumpata Mr Kim?”
“Haya, tuendelee.”
Kaguta alisema kwa sauti ya chini isiyoridhia.
***
☆Steve
(MSIMU WA 02)
MTUNZI: Stevie Mollel
No: 0685 758 123
Baada tu ya mlango wa chumba kufungwa, Rajul alijaribu tena kuita jina la Stanis mara tatu pasipo majibu. Alichungulia kwenye kitundu lakini hakuona kitu kwa sababu ya giza lililokuwepo kwenye chumba cha Stanis.
Alipiga piga tena ukuta, mara hii Stanis akashituka, ila hakutoa sauti yoyote.
“Stanis! … Stanis upo?” Rajul alinong’oneza baada ya kusikia sauti ya mtu akisogea.
“Eeeiiigh …” Stanis aliitikia kwa kukoroma. Rajul akatabasamu.
“Stanis, inabidi utoroke, la sivyo utauwawa. Unanisikia?”
“Eeeeiggh …”
“Inabidi uondoke humo kwa njia yoyote. Inabidi tutoroke la sivyo, Kim atafanikiwa adhma yake.”
“Eeeeiigghhh …”
“Ili Kim afanikiwe anahitaji damu. Na endapo nikimwambia hilo basi atakufanya sadaka. Akikufanya sadaka, atapata nguvu. Akipata nguvu, hakutokuwa na wa kumzuia tena.”
“Eeeigggh …”
“Una wazo lolote la kutoroka?”
“Eeeiigggh …”
“Stanis, huwezi kuongea neno lolote?”
“Eeeiiggh …”
“Mungu wangu!” Rajul alijibamiza kichwa akaegemea ukuta.
“Nifanye nini sasa? … Nifanye nini?”
Aliwaza na kuwazua kwa dakika kadhaa, mara akatikisa kichwa na kusema:
“Hii sasa ndio njia. Hii ndio njia pekee.”
Aligeukia kwenye kitundu, akamuita Stanis.
“Stanis, nina njia ya kututoa humu. Upo tayari?”
“Eeeiggh …” Stanis akaitikia kwa kukoroma kama ada.
***
Sauti kubwa ya mlio wa pembe la ng’ombe ililia na kumshitua Vitalis aliyekuwa amelala.
Ilikuwa ni asubuhi sasa ya saa kumi na mbili hata jua halijasimama. Vitalis alimtizama Kaguta aliyelala upande wake wa kushoto akamuona yu hoi usingizini. Asimsumbue hata, akanyanyuka na kutoka nje atizame kunani. Huko akakutana na Bernadetha, Bakari na Miraji, wote walikuwa wametoka nje kushangaa. Kama wehu, wenyeji wao walikuwa wanatoka kwenye makazi yao wakikimbia kuelekea msituni sauti inapotokea. Wakiwa wamebung’aa wasipate hata mtu wa kumuuliza, wakamuona kiongozi. Upesi, Vitalis alimkimbilia akamwambia:
“Unajua ni wewe tu ndiye unayeongea lugha tunayoielewa.”
Kiongozi akaitikia kwa kutikisa kichwa.
“Kuna nini?” Vitalis aliuliza. “Mbona watu wanakimbia?” Kiongozi akatabasamu.
“Kuna taarifa ya mateka wamekamatwa mtegoni.” Alisema. “Usiwe na hofu.”
Kauli yake hiyo ikafungwa kwa kuingizwa kwa mateka hao ndani ya kijiji wakiwa wamewekwa chini ya ulinzi mkali. Vitalis alimuona Mamba pamoja na wenzake, akajikuta anatabasamu na kusema:
“Mungu mkubwa. Amenipa nafasi ya kutimiza ahadi yangu.”
“Vitalis!” Mamba alishangaa kumuona adui yake. Alijikuta anacheka kwanza kisha ndiyo akaendelea kunena:
“Sikujua kama ulikuja kuomba msaada wa watu hawa washamba ... wa kale ... wasiojua ulimwengu unaendaje.”
Alicheka tena alafu akaendelea:
“Sikujua kama wewe ni muoga kiasi hiki. Sikujua kama wewe ni mwanamke kiasi hiki. Vitalis, watu wanavyokudhania huko nje ni tofauti na ulivyo. Hawajui jinsi gani ulivyo mtu wa kujificha na kukimbia kama panya."
Mamba aliongea kwa kejeli akiupindisha mdomo wake. Vitalis akamuuliza:
"Unakumbuka ahadi yangu niliyoiweka mbele yako kule kiwandani?"
"Ahadi gani wewe mwanamke?" Mamba akauliza pia. Vitalis akamsogelea karibu zaidi.
"Nilikuambia siku nikikutia mikononi nitahakikisha nakuharibu mpaka mama yako mzazi ashindwe kukutambua. Siku yenyewe ndiyo leo."
"Karibu!” Mamba alisema akimuita Vitalis kwa ishara ya ulimi. “… sasa nitapambanaje na nimefungwa kama mzigo wa msafiri?" Akauliza. Vitalis akamuomba kiongozi ampatie mtu huyo, kiongozi akaridhia. Mamba alifunguliwa kamba, wakapewa uwanja.
La haula, kabla Vitalis hajajiweka sawa, Mamba alijitosa hewani akamgawia teke zito lililomzoa na kumbwaga chini mwanaume huyo.
Upesi Vitalis aliamka kwa sarakasi akajiweka sawa kisha akatulia kungojea tena shambulizi.
Mamba akatuma tena teke, mara hii likadakwa na mkono wa kuume wa Vitalis. Teke hilo likavutwa karibu kisha Vitalis akaruka na kujigeuza akimtandika Mamba kisigino cha taya. Mithili ya mzigo, Mamba akarushiwa kando.
Aliponyanyuka kwa hasira aonyeshe ubabe wake, akaula tena wa chuya, kila ngumi na teke alilorusha zikakwepwa kisha akazawadiwa ngumi nzito chini ya kifua, akacheua damu.
Mamba alifuta damu yake kwa kiganja kisha akaguna. Alikimbia kumfuata Vitalis, ila Vitalis akamkwepa haraka na kumuwekea goti la mguu wa kushoto mwanaume huyo aliyegota hapo kama gari la mwendo kasi. Kama haitoshi, Vitalis akarusha mguu wake wa kulia na kumkita nao Mamba shingoni. Sasa Mamba akadondoka chini ila akiwa katikati ya miguu ya Vitalis. Miguu ikabanwa kwanguvu na kumnyima Mamba hewa. Alirusha ngumi kwa fujo ajiokoe, Vitalis akakamata mikono hiyo na kuivunja kisha akavuta jabali lililokuwa pembeni akaponda uso wa Mamba mpaka pale ulipokuwa chapati.
Damu zilimrukia Vitalis kwa fujo. Shati lake lote na hata suruali vilichafuka damu. Wakati anafanya tukio hilo la kuponda kila mtu alimshangaa. Ni kama vile alikuwa anaponda mawe kumbe kichwa cha mtu. Hakuwa na roho ya ubinadamu hata kidogo muda huo bali ya shetani, tena shetani mwekundu. Hakuacha hilo zoezi mpaka pale alipokuja kutolewa na Kiongozi aliyemvutia pembeni na kumtaka apunguze jazba.
Aliwatizama wenzake na Mamba akawaambia:
“Nyie ndio mnafuata!”
Watu hao, isipokuwa chotara, walimtizama Vitalis kana kwamba wanatizama pundamilia akimla simba. Chotara yeye alikuwa hoi asijali hata kinachoendelea. Alisimama kama mgomba ulioelemewa na mkungu wa ndizi. Alikuwa ametota jasho mdomo ukiwa mkavu mno. Macho yake yalikuwa yamelegea yakiwa mekundu ya kutisha.
Vitalis alijikwamua toka mikononi mwa Kiongozi akajiendea ndani asiwaone watu hao. Mateka walitundikwa mitini, watu wakaendelea na shughuli zingine kama ada. Baada ya muda mfupi, Bakari aliwafuata hao mateka waliotundikwa mitini akawapekua mifukoni. Miongoni mwa mmoja wao alikuta simu. Aliitia mfukoni mwake akawauliza:
“Mmetumwa na nani?”
Mateka wale watatu, walio wazima wa afya, wakatabasamu.
“Usitegemee kupata jibu lolote toka kwetu.” Mmoja alijibu.
Bakari alimfuata chotara akamtizama kwa karibu. Aliona mishipa ya shingoni ya mwanaume huyo imegeuka kuwa rangi ya kijani. Alimfungua macho akamtizama, napo akaona macho ya mwanaume huyo yakiwa na umbijani kwa mbali, akaishia kutikisa kichwa na kusema:
“Mwenzenu atakufa muda si mrefu.”
“Tunaomba umsaidie.” Mmoja akasema. “Tafadhali naomba umsaidie.”
Bakari akatabasamu.
“Usitegemee kupata msaada wowote toka kwangu.”
Alisema kisha akajigeuza aondoke. Akaitwa.
“Tafadhali msaidie. Tutakuambia unayoyataka.”
“Vipi kama mkiniambia alafu ndiyo niwasaidie?” Bakari alisema akisogea karibu kwa aliyemuita.
“Hapana! Tutajuaje kama unatulaghai?”
“Na mimi nitajuaje kama mtanilaghai?”
“Hatuwezi kufanya hivyo. Tukikulaghai, tutaondokaje na mmetufungia mtini?”
“Siwezi jua. Ila ingekuwa vema kama mngeniambia upesi ili mwenzenu apate tiba upesi, yupo kwenye hali mbaya. Si mnamuona?” Bakari alimtizama chotara.
Alikatizwa zoezi lake hilo na sauti ya Bernadetha iliyomuita. Aliaga akaahidi kurudi upesi kumalizana nao. Aliondoka, Kaguta akasogea karibu na mateka. Muda wote Bakari aliokuwepo hapo, Kaguta alikuwa akimtizama kwa karibu.
Sura yake ilikuwa imekunjamana. Macho yake yalikuwa yamevimba na mekundu. Mdomo wake ulibinuliwa kwa kebehi ama hasira. Nyuma ya mgongo wake alikuwa amefichama mkono uliobebelea kisu. Aliwatizama mateka akawaambia kwa sauti ya chini:
“Nimekuja kudai uhai wenu.”
Bakari aliporejea baadae kwa mateka hao, akawakuta wote wamekufa. Kila mmoja alikuwa anachuruza damu kifuani mwake akiwa na matundu ya visu si chini ya mawili.
“Samahani kwa kuingilia maongezi yako.” Sauti ya Kaguta ilimfikia Bakari na kumshitua. Aligeuka akamkuta Kaguta nyuma yake.
“Kwanini umewaua?” Bakari aliuliza. “Kuna taarifa muhimu walikuwa wanataka kunipa!”
“Unadhani wangekuambia kitu?” Kaguta aliuliza. “Kama ulitegemea kitu toka kwa watu waliokula viapo vya kutosema lolote, pole sana. Hawa watu hawastahili huruma yoyote.”
Baada ya kusema hivyo Kaguta aliondoka akaelekea ndani ya kijumba. Alinyofoa mtungi wa pombe uliokuwepo chini ya kitanda cha ngozi alaliacho, akamwagia kinywaji hicho ndani yake mpaka pale alipozima akalala. Hakutia tumboni kitu chochote isipokuwa pombe hiyo ya kienyeji. Hata pale jioni alipoamka, aliamkia na pombe hiyo. Ni Vitalis ndiye aliyekuja kumuokoa toka kwenye hiyo shughuli.
“Inatosha!” Vitalis alisema akimpokonya Kaguta mtungi wa pombe kwanguvu.
“Unadhani itasaidia?” Vitalis aliuliza. “Haitosaidia zaidi ya kutuongezea msiba mwingine, Kaguta!” Alifoka. Aliweka kituo akapunguza sauti.
“Tuna maongezi. Tunakungojea nje, fanya uje.”
Alitoka ndani ya chumba, Kaguta akamfuata baada ya muda mfupi.
Wakiwa watano, WAGENI, wamekaa kwenye benchi refu, waliteta:
“Sasa ni muda wa kwenda kumalizana na adui yetu mkubwa.” Vitalis alifungua maongezi. “Kila tunachokihitaji tunacho. Hatuna tena muda wa kungoja.” Alimtizama Bakari, Bakari akachukua zamu:
“Nilifanikiwa kwenda town kuchaji simu. Bahati nzuri baada ya simu kuwaka, barua pepe toka kwa Mr Kim ziliingia. Nilichat naye nikijifanya mimi ni mtumishi wake, nikapata taarifa muhimu za kutufikisha alipo.”
“Basi twende!” Kaguta aliropoka. “Tunangoja nini?”
“Tulia Kaguta.” Vitalis akasihi. “Si tu kwenda, tupange kwanza. Unajua tutafikia wapi? Unajua tutafanyaje kumpata Mr Kim?”
“Haya, tuendelee.”
Kaguta alisema kwa sauti ya chini isiyoridhia.
***
☆Steve
