SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,803
- 25,444
- Thread starter
- #821
***SURA YA SABINI NA TATU***
(MSIMU WA 02)
MTUNZI: Steve Mollel
No: 0685 758 123
“Ulifanya kile nilichokuagiza?” Mamba alimuuliza mwanaume mmoja chotara kwa kumkazia macho.
Walikuwa ndani ya chumba kikubwa cha kuvutia chenye kila aina ya vikolombwezo vya gharama. Kwa kukisia haraka kilikuwa ni chumba cha hoteli. Tena hoteli ya nyota nyingi tu.
Mwanaume huyo chotara alitikisa kichwa akajibu:
“Ndio nimefanya.”
“Umegundua hiyo simu yako ipo wapi?”
“Ndio. Ipo kwenye kisiwa fulani bahari ya Hindi.”
Mwanaume huyo alisema akimkabidhi Mamba simu yake kubwa rangi nyeusi.
Mamba alitizama simu hiyo akaona ramani iliyotoholewa mtandaoni. Katikati ya ramani hiyo palikuwapo na kidoti chekundu ‘kikimwekamweka’ kama taa ya ishara ya gari. Chini ya kidoti hicho palikuwapo na maelezo ya nyuzi za longitudo la latitudo ya mahali hapo.
“Ulipapataje?” Mamba aliuliza.
“Simu yangu ina program ya kujikinga dhidi ya virusi.” Chotara akajibu.
“Programu ya virusi imepelekeaje wewe kupata mahali hapa?” Mamba aliuliza.
“Ndani ya programu hiyo unaweza pia ukatenga mahesabu ya kupata simu yako iliyopotea kwa kuamrisha simu nyingine utakayoichagua iwe inakupa taarifa ya simu yako. Na simu yenyewe ndiyo hiyo hapo. Hata mwizi atakapotoa laini haitosaidia kumficha.”
Mamba akatabasamu.
“Nalijua hili eneo.”
“Ndio mana tukakutafuta kwa hali na mali.” Chotara akadakia, “Sasa tunaweza kwenda na kumaliza biashara yetu?”
“Ndio twaweza kwenda. Ila sio kwa haraka kiasi hiko.”
“Kivipi?”
“Yatupasa kujikamilisha kwa silaha na mipango. Kisiwa hiki kipo pweke hivyo ni rahisi kwa mgeni kuonekana akija tokea upande wowote. Na pia hatujajua wao wamejipangaje. Huwezi jua labda wanategemea ujio wetu.”
“Kwahiyo tunafanyaje?”
“Waite wenzako kwanza tuyajenge.”
Baada ya nusu saa, wote watano wakawapo ndani ya chumba hicho wakapata kupanga na kupangua, Mamba akiwa kiongozi.
Walipomaliza kuainisha mipango yao, Mamba akawaambia.
“Huyo Vitalis mumuache. Nataka nimshughulikie kwa mikono yangu mwenyewe.”
Wote wakaafiki kisha wakajipumzisha na mipango yao waliyokuwa wanaisuka kwa kuzoza na mengine ya dunia, huku wakishushia na vinywaji vikali vilivyotapakaza meza. Huenda mawazo yao ya sasa yalichombezwa na mwenendo mkali wa vileo vichwani. Walicheka hovyo na kupaza sauti pasipo na mahitaji.
“Mlienda wapi, mbona hamkutuaga?” Mamba aliuliza wanaume watatu ambao hawakuwepo hapo awali. Mmoja wao akacheka kidogo na kujibu:
“Tulikuwa huko mtaani tukionja ladha ya wanawake wa Tanzania.”
Wote wakajikuta wakicheka.
“Umeionaje ladha yao?” Mamba alichokoza huku wakiendelea kutandika vileo.
“Aaah! Kusema ukweli haielezeki.” Mwingine alijibu. “Unajua kule kwetu Bermuda, hamna wanawake wenye shepu nzuri kama huku. Wengi wao wanafanana tu na sisi pindi wakivua nguo, lakini hapa ni tofauti kabisa!”
Wakacheka.
“Ni kweli.” Mwingine akatia neno, “Waweza vunja shingo ukikatiza barabarani mana kila mmoja ana mvuto wake wa kushangaza. Mapaja yao ya moto na meupe. Matiti yao makubwa yakujaza. Makalio ndio doh …”
Wakacheka tena.
“Sasa mbona hata hamkunambia kama mlienda huko?” Chotara aliuliza kwa kulaumu. “Mbona ni wabinafsi sana nyie ndugu zangu?”
“Sasa hivi tutaenda sisi na nyie mbaki hapa.” Mamba akasema akioneshea kidole sakafuni.
“Kwanini tusiwaite hapa wakatufuata? Nilichukua namba zao za simu. Nitawaambia waje na wenzao, au mnasemaje?” Mwanaume mmoja miongoni mwa wale waliotoka huko nje alitoa wazo. Likaonekana kukonga nafsi zao.
Mamba akasema:
“Utanipa niongee nao. Wakijua nyie wageni watatupiga pesa ndefu sana.”
Simu ikanyanyuliwa na kupigwa, Mamba akatoa oda ya wanawake nane ambao alihadiwa kufika walipo kwenye majira ya saa nne usiku, ila hilo likifanyika baada ya malipo ya awali kutumwa.
Mamba alituma pesa hizo kisha wakakaa tenge sasa kungoja raha.
Raha toka kwa wanawake walionona haswa.
Raha toka kwa wanawake wa danguro ghali na maarufu jijini Dar lipatikanalo maeneo ya Mbezi beach.
***
Muda si barafu ukaganda.
Majira ya saa nne usiku yalijongea na kuwaleta wanawake warembo haswa ndani ya chumba namba 321 walimokuwemo Mamba na wenzake wakijiliwaza kwa kutizama televisheni na kunywa pombe kali.
Wanawake hao walipambwa na shepu barabara zikibanwa na nguo fupi. Nywele ndefu za kisasa isipokuwa mmoja tu mwenye nazo fupi. Nyuso zilizokozwa ‘make up’ za kulaghai. Michuchumio ya hatari ya kumetameta bila kusahau mapochi makubwa ya bei ghali.
Kila mwanamume alijichagulia wa kwake akanywa na kucheza naye. Mamba alitwaa wanawake wanne peke yake wenzake wakigawana mmoja kwa kila mmoja.
Baada ya kucheza na kuwehuka kwa muda, wakaanza ‘kuchojoana’ nguo na kufanya mapenzi mbele ya kila mmoja kana kwamba kuna mashindano.
Usipite muda mrefu, wanaume hao wakajikuta wazito mno. Waliamka majira ya saa nne asubuhi wakiwa peke yao ndani ya chumba.
Walikombwa pesa zote na vitu vya thamani: saa, viatu na nguo. Hata ramani waliyoikuwa wamepangia mambo yao haikuwapo.
Mamba alishika kichwa chake akapiga ukunga wa hasira.
“Uliwatoa wapi? Hawa wanawake sio wa danguro la Mbezi! Hawana tabia hizi za kishenzi!” Mamba alifoka.
“Ila walisema ni wa Mbezi!” Aliyetoa namba alijitetea.
“Lakini mbona kama kunywa tulikunywa wote. Walituwekea madawa sehemu gani?” Mwingine aliuliza.
“Hawa malaya huwezi ukashindana nao kwa kunywa.” Mamba aling’aka. “Wana vichwa vigumu sana kulewa … itakuwa kuna mahali tu walitupatia wakatuweza. Si kwasababu ya pombe. Tusingeweza kuzima vile.”
“Sasa tutafanyaje na pesa zote wameondoka nazo? Tuwasiliane na mkuu atuwezeshe?” Mmoja alitoa wazo.
“Hapana! Hapana!” Mwenzake akadakia haraka. “Hatuwezi tukaomba pesa nyingine wakati alizotupa zilikuwa ni nyingi mno, na tumezimaliza kabla hatujafanikisha alichotuagiza.”
“Kwahiyo unashaurije?”
“Tupambane kwanza kufanikisha hili jambo mbele yetu kwa njia yoyote ile. Hapo mkuu anaweza akatuelewa na kutupatia pesa. La sivyo hakuna tena njia.”
****
Masaa kadhaa nyuma …
“Wamepiga simu, wanataka wanawake nane. Sasa hilo dili vipi?” Aliuliza mwanamke mmoja mwenye nywele fupi na hereni kubwa za mviringo masikioni.
Ndani ya chumba hicho walikuwepo jumla ya wanawake watano waliojilaza na kuketi kwenye godoro lililolazwa chini. Wote walivalia nguo za ‘hasara hasara’, watatu miongoni mwao wakipasha mapafu kwa sigara.
“Huo sio mchongo wa kuuacha kabisa. Watakuwa ndio wale wale wageni tuliowapa namba za simu. Wana madola ya kumwaga. Kama vipi wash’tue wakina Shamira tukachukue pesa hizo.”
“Ila kabla ya kwenda umewaambia watoe pesa ya advansi?” Mmoja aliuliza.
“Sasa tutaendaje kichwa kichwa bila kuwaambia hivyo?” Aliyeongea na simu akajibu kwa swali. Mwingine akachangia:
“Na kama unavyojua walituonea maeneo ya Mbezi kwahiyo wanajua sisi mambo safi, sio wale wa mitaani. Kwahiyo kama tunaenda basi tuwaambie wakina Shamira waje na mitupio ya hatari.”
“Poa poa!”
Simu ikapigwa na kutoa maelekezo yote. Baada ya punde Shamira na wenzake wakafika chumbani hapo na mikoba ya gharama iliyobebelea nguo za maana.
Baada ya kujivesha na kujitathmini, wakasuka mipango yao.
“Kama mnavyoelewa, sie ni watoto wa mbwa. Hapa hatulazi damu wala hatuzubai. Inabidi tuwakombe kila kitu.” Alisema yule mwanamke mweye nywele fupi na hereni kubwa. “Kila mmoja ahakikishe anapaka dawa yake kama kawa. Au sio?”
“Poa.”
Wakati wanajiandaa kwenda kutoa huduma kwa wanaume waliowaita kwa kujikwatua na kujipulizia manukato ya Paris, walipakaa pia unga fulani mweupe kwenye chuchu za matiti yao kwa kuzungusha kidole.
Walipomaliza, mmoja wao akasema kwa kebehi:
“Wakinyonya tu imekula kwao.”
Wote wakacheka na kugongesha viganja vyao.
****
☆Steve
(MSIMU WA 02)
MTUNZI: Steve Mollel
No: 0685 758 123
“Ulifanya kile nilichokuagiza?” Mamba alimuuliza mwanaume mmoja chotara kwa kumkazia macho.
Walikuwa ndani ya chumba kikubwa cha kuvutia chenye kila aina ya vikolombwezo vya gharama. Kwa kukisia haraka kilikuwa ni chumba cha hoteli. Tena hoteli ya nyota nyingi tu.
Mwanaume huyo chotara alitikisa kichwa akajibu:
“Ndio nimefanya.”
“Umegundua hiyo simu yako ipo wapi?”
“Ndio. Ipo kwenye kisiwa fulani bahari ya Hindi.”
Mwanaume huyo alisema akimkabidhi Mamba simu yake kubwa rangi nyeusi.
Mamba alitizama simu hiyo akaona ramani iliyotoholewa mtandaoni. Katikati ya ramani hiyo palikuwapo na kidoti chekundu ‘kikimwekamweka’ kama taa ya ishara ya gari. Chini ya kidoti hicho palikuwapo na maelezo ya nyuzi za longitudo la latitudo ya mahali hapo.
“Ulipapataje?” Mamba aliuliza.
“Simu yangu ina program ya kujikinga dhidi ya virusi.” Chotara akajibu.
“Programu ya virusi imepelekeaje wewe kupata mahali hapa?” Mamba aliuliza.
“Ndani ya programu hiyo unaweza pia ukatenga mahesabu ya kupata simu yako iliyopotea kwa kuamrisha simu nyingine utakayoichagua iwe inakupa taarifa ya simu yako. Na simu yenyewe ndiyo hiyo hapo. Hata mwizi atakapotoa laini haitosaidia kumficha.”
Mamba akatabasamu.
“Nalijua hili eneo.”
“Ndio mana tukakutafuta kwa hali na mali.” Chotara akadakia, “Sasa tunaweza kwenda na kumaliza biashara yetu?”
“Ndio twaweza kwenda. Ila sio kwa haraka kiasi hiko.”
“Kivipi?”
“Yatupasa kujikamilisha kwa silaha na mipango. Kisiwa hiki kipo pweke hivyo ni rahisi kwa mgeni kuonekana akija tokea upande wowote. Na pia hatujajua wao wamejipangaje. Huwezi jua labda wanategemea ujio wetu.”
“Kwahiyo tunafanyaje?”
“Waite wenzako kwanza tuyajenge.”
Baada ya nusu saa, wote watano wakawapo ndani ya chumba hicho wakapata kupanga na kupangua, Mamba akiwa kiongozi.
Walipomaliza kuainisha mipango yao, Mamba akawaambia.
“Huyo Vitalis mumuache. Nataka nimshughulikie kwa mikono yangu mwenyewe.”
Wote wakaafiki kisha wakajipumzisha na mipango yao waliyokuwa wanaisuka kwa kuzoza na mengine ya dunia, huku wakishushia na vinywaji vikali vilivyotapakaza meza. Huenda mawazo yao ya sasa yalichombezwa na mwenendo mkali wa vileo vichwani. Walicheka hovyo na kupaza sauti pasipo na mahitaji.
“Mlienda wapi, mbona hamkutuaga?” Mamba aliuliza wanaume watatu ambao hawakuwepo hapo awali. Mmoja wao akacheka kidogo na kujibu:
“Tulikuwa huko mtaani tukionja ladha ya wanawake wa Tanzania.”
Wote wakajikuta wakicheka.
“Umeionaje ladha yao?” Mamba alichokoza huku wakiendelea kutandika vileo.
“Aaah! Kusema ukweli haielezeki.” Mwingine alijibu. “Unajua kule kwetu Bermuda, hamna wanawake wenye shepu nzuri kama huku. Wengi wao wanafanana tu na sisi pindi wakivua nguo, lakini hapa ni tofauti kabisa!”
Wakacheka.
“Ni kweli.” Mwingine akatia neno, “Waweza vunja shingo ukikatiza barabarani mana kila mmoja ana mvuto wake wa kushangaza. Mapaja yao ya moto na meupe. Matiti yao makubwa yakujaza. Makalio ndio doh …”
Wakacheka tena.
“Sasa mbona hata hamkunambia kama mlienda huko?” Chotara aliuliza kwa kulaumu. “Mbona ni wabinafsi sana nyie ndugu zangu?”
“Sasa hivi tutaenda sisi na nyie mbaki hapa.” Mamba akasema akioneshea kidole sakafuni.
“Kwanini tusiwaite hapa wakatufuata? Nilichukua namba zao za simu. Nitawaambia waje na wenzao, au mnasemaje?” Mwanaume mmoja miongoni mwa wale waliotoka huko nje alitoa wazo. Likaonekana kukonga nafsi zao.
Mamba akasema:
“Utanipa niongee nao. Wakijua nyie wageni watatupiga pesa ndefu sana.”
Simu ikanyanyuliwa na kupigwa, Mamba akatoa oda ya wanawake nane ambao alihadiwa kufika walipo kwenye majira ya saa nne usiku, ila hilo likifanyika baada ya malipo ya awali kutumwa.
Mamba alituma pesa hizo kisha wakakaa tenge sasa kungoja raha.
Raha toka kwa wanawake walionona haswa.
Raha toka kwa wanawake wa danguro ghali na maarufu jijini Dar lipatikanalo maeneo ya Mbezi beach.
***
Muda si barafu ukaganda.
Majira ya saa nne usiku yalijongea na kuwaleta wanawake warembo haswa ndani ya chumba namba 321 walimokuwemo Mamba na wenzake wakijiliwaza kwa kutizama televisheni na kunywa pombe kali.
Wanawake hao walipambwa na shepu barabara zikibanwa na nguo fupi. Nywele ndefu za kisasa isipokuwa mmoja tu mwenye nazo fupi. Nyuso zilizokozwa ‘make up’ za kulaghai. Michuchumio ya hatari ya kumetameta bila kusahau mapochi makubwa ya bei ghali.
Kila mwanamume alijichagulia wa kwake akanywa na kucheza naye. Mamba alitwaa wanawake wanne peke yake wenzake wakigawana mmoja kwa kila mmoja.
Baada ya kucheza na kuwehuka kwa muda, wakaanza ‘kuchojoana’ nguo na kufanya mapenzi mbele ya kila mmoja kana kwamba kuna mashindano.
Usipite muda mrefu, wanaume hao wakajikuta wazito mno. Waliamka majira ya saa nne asubuhi wakiwa peke yao ndani ya chumba.
Walikombwa pesa zote na vitu vya thamani: saa, viatu na nguo. Hata ramani waliyoikuwa wamepangia mambo yao haikuwapo.
Mamba alishika kichwa chake akapiga ukunga wa hasira.
“Uliwatoa wapi? Hawa wanawake sio wa danguro la Mbezi! Hawana tabia hizi za kishenzi!” Mamba alifoka.
“Ila walisema ni wa Mbezi!” Aliyetoa namba alijitetea.
“Lakini mbona kama kunywa tulikunywa wote. Walituwekea madawa sehemu gani?” Mwingine aliuliza.
“Hawa malaya huwezi ukashindana nao kwa kunywa.” Mamba aling’aka. “Wana vichwa vigumu sana kulewa … itakuwa kuna mahali tu walitupatia wakatuweza. Si kwasababu ya pombe. Tusingeweza kuzima vile.”
“Sasa tutafanyaje na pesa zote wameondoka nazo? Tuwasiliane na mkuu atuwezeshe?” Mmoja alitoa wazo.
“Hapana! Hapana!” Mwenzake akadakia haraka. “Hatuwezi tukaomba pesa nyingine wakati alizotupa zilikuwa ni nyingi mno, na tumezimaliza kabla hatujafanikisha alichotuagiza.”
“Kwahiyo unashaurije?”
“Tupambane kwanza kufanikisha hili jambo mbele yetu kwa njia yoyote ile. Hapo mkuu anaweza akatuelewa na kutupatia pesa. La sivyo hakuna tena njia.”
****
Masaa kadhaa nyuma …
“Wamepiga simu, wanataka wanawake nane. Sasa hilo dili vipi?” Aliuliza mwanamke mmoja mwenye nywele fupi na hereni kubwa za mviringo masikioni.
Ndani ya chumba hicho walikuwepo jumla ya wanawake watano waliojilaza na kuketi kwenye godoro lililolazwa chini. Wote walivalia nguo za ‘hasara hasara’, watatu miongoni mwao wakipasha mapafu kwa sigara.
“Huo sio mchongo wa kuuacha kabisa. Watakuwa ndio wale wale wageni tuliowapa namba za simu. Wana madola ya kumwaga. Kama vipi wash’tue wakina Shamira tukachukue pesa hizo.”
“Ila kabla ya kwenda umewaambia watoe pesa ya advansi?” Mmoja aliuliza.
“Sasa tutaendaje kichwa kichwa bila kuwaambia hivyo?” Aliyeongea na simu akajibu kwa swali. Mwingine akachangia:
“Na kama unavyojua walituonea maeneo ya Mbezi kwahiyo wanajua sisi mambo safi, sio wale wa mitaani. Kwahiyo kama tunaenda basi tuwaambie wakina Shamira waje na mitupio ya hatari.”
“Poa poa!”
Simu ikapigwa na kutoa maelekezo yote. Baada ya punde Shamira na wenzake wakafika chumbani hapo na mikoba ya gharama iliyobebelea nguo za maana.
Baada ya kujivesha na kujitathmini, wakasuka mipango yao.
“Kama mnavyoelewa, sie ni watoto wa mbwa. Hapa hatulazi damu wala hatuzubai. Inabidi tuwakombe kila kitu.” Alisema yule mwanamke mweye nywele fupi na hereni kubwa. “Kila mmoja ahakikishe anapaka dawa yake kama kawa. Au sio?”
“Poa.”
Wakati wanajiandaa kwenda kutoa huduma kwa wanaume waliowaita kwa kujikwatua na kujipulizia manukato ya Paris, walipakaa pia unga fulani mweupe kwenye chuchu za matiti yao kwa kuzungusha kidole.
Walipomaliza, mmoja wao akasema kwa kebehi:
“Wakinyonya tu imekula kwao.”
Wote wakacheka na kugongesha viganja vyao.
****
☆Steve