Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

***SURA YA SABINI NA TATU***




(MSIMU WA 02)



MTUNZI: Steve Mollel


No: 0685 758 123








“Ulifanya kile nilichokuagiza?” Mamba alimuuliza mwanaume mmoja chotara kwa kumkazia macho.
Walikuwa ndani ya chumba kikubwa cha kuvutia chenye kila aina ya vikolombwezo vya gharama. Kwa kukisia haraka kilikuwa ni chumba cha hoteli. Tena hoteli ya nyota nyingi tu.
Mwanaume huyo chotara alitikisa kichwa akajibu:
“Ndio nimefanya.”
“Umegundua hiyo simu yako ipo wapi?”
“Ndio. Ipo kwenye kisiwa fulani bahari ya Hindi.”
Mwanaume huyo alisema akimkabidhi Mamba simu yake kubwa rangi nyeusi.
Mamba alitizama simu hiyo akaona ramani iliyotoholewa mtandaoni. Katikati ya ramani hiyo palikuwapo na kidoti chekundu ‘kikimwekamweka’ kama taa ya ishara ya gari. Chini ya kidoti hicho palikuwapo na maelezo ya nyuzi za longitudo la latitudo ya mahali hapo.
“Ulipapataje?” Mamba aliuliza.
“Simu yangu ina program ya kujikinga dhidi ya virusi.” Chotara akajibu.
“Programu ya virusi imepelekeaje wewe kupata mahali hapa?” Mamba aliuliza.
“Ndani ya programu hiyo unaweza pia ukatenga mahesabu ya kupata simu yako iliyopotea kwa kuamrisha simu nyingine utakayoichagua iwe inakupa taarifa ya simu yako. Na simu yenyewe ndiyo hiyo hapo. Hata mwizi atakapotoa laini haitosaidia kumficha.”
Mamba akatabasamu.
“Nalijua hili eneo.”
“Ndio mana tukakutafuta kwa hali na mali.” Chotara akadakia, “Sasa tunaweza kwenda na kumaliza biashara yetu?”
“Ndio twaweza kwenda. Ila sio kwa haraka kiasi hiko.”
“Kivipi?”
“Yatupasa kujikamilisha kwa silaha na mipango. Kisiwa hiki kipo pweke hivyo ni rahisi kwa mgeni kuonekana akija tokea upande wowote. Na pia hatujajua wao wamejipangaje. Huwezi jua labda wanategemea ujio wetu.”
“Kwahiyo tunafanyaje?”
“Waite wenzako kwanza tuyajenge.”
Baada ya nusu saa, wote watano wakawapo ndani ya chumba hicho wakapata kupanga na kupangua, Mamba akiwa kiongozi.
Walipomaliza kuainisha mipango yao, Mamba akawaambia.
“Huyo Vitalis mumuache. Nataka nimshughulikie kwa mikono yangu mwenyewe.”
Wote wakaafiki kisha wakajipumzisha na mipango yao waliyokuwa wanaisuka kwa kuzoza na mengine ya dunia, huku wakishushia na vinywaji vikali vilivyotapakaza meza. Huenda mawazo yao ya sasa yalichombezwa na mwenendo mkali wa vileo vichwani. Walicheka hovyo na kupaza sauti pasipo na mahitaji.
“Mlienda wapi, mbona hamkutuaga?” Mamba aliuliza wanaume watatu ambao hawakuwepo hapo awali. Mmoja wao akacheka kidogo na kujibu:
“Tulikuwa huko mtaani tukionja ladha ya wanawake wa Tanzania.”
Wote wakajikuta wakicheka.
“Umeionaje ladha yao?” Mamba alichokoza huku wakiendelea kutandika vileo.
“Aaah! Kusema ukweli haielezeki.” Mwingine alijibu. “Unajua kule kwetu Bermuda, hamna wanawake wenye shepu nzuri kama huku. Wengi wao wanafanana tu na sisi pindi wakivua nguo, lakini hapa ni tofauti kabisa!”
Wakacheka.
“Ni kweli.” Mwingine akatia neno, “Waweza vunja shingo ukikatiza barabarani mana kila mmoja ana mvuto wake wa kushangaza. Mapaja yao ya moto na meupe. Matiti yao makubwa yakujaza. Makalio ndio doh …”
Wakacheka tena.
“Sasa mbona hata hamkunambia kama mlienda huko?” Chotara aliuliza kwa kulaumu. “Mbona ni wabinafsi sana nyie ndugu zangu?”
“Sasa hivi tutaenda sisi na nyie mbaki hapa.” Mamba akasema akioneshea kidole sakafuni.
“Kwanini tusiwaite hapa wakatufuata? Nilichukua namba zao za simu. Nitawaambia waje na wenzao, au mnasemaje?” Mwanaume mmoja miongoni mwa wale waliotoka huko nje alitoa wazo. Likaonekana kukonga nafsi zao.
Mamba akasema:
“Utanipa niongee nao. Wakijua nyie wageni watatupiga pesa ndefu sana.”
Simu ikanyanyuliwa na kupigwa, Mamba akatoa oda ya wanawake nane ambao alihadiwa kufika walipo kwenye majira ya saa nne usiku, ila hilo likifanyika baada ya malipo ya awali kutumwa.
Mamba alituma pesa hizo kisha wakakaa tenge sasa kungoja raha.
Raha toka kwa wanawake walionona haswa.
Raha toka kwa wanawake wa danguro ghali na maarufu jijini Dar lipatikanalo maeneo ya Mbezi beach.

***

Muda si barafu ukaganda.
Majira ya saa nne usiku yalijongea na kuwaleta wanawake warembo haswa ndani ya chumba namba 321 walimokuwemo Mamba na wenzake wakijiliwaza kwa kutizama televisheni na kunywa pombe kali.
Wanawake hao walipambwa na shepu barabara zikibanwa na nguo fupi. Nywele ndefu za kisasa isipokuwa mmoja tu mwenye nazo fupi. Nyuso zilizokozwa ‘make up’ za kulaghai. Michuchumio ya hatari ya kumetameta bila kusahau mapochi makubwa ya bei ghali.
Kila mwanamume alijichagulia wa kwake akanywa na kucheza naye. Mamba alitwaa wanawake wanne peke yake wenzake wakigawana mmoja kwa kila mmoja.
Baada ya kucheza na kuwehuka kwa muda, wakaanza ‘kuchojoana’ nguo na kufanya mapenzi mbele ya kila mmoja kana kwamba kuna mashindano.
Usipite muda mrefu, wanaume hao wakajikuta wazito mno. Waliamka majira ya saa nne asubuhi wakiwa peke yao ndani ya chumba.
Walikombwa pesa zote na vitu vya thamani: saa, viatu na nguo. Hata ramani waliyoikuwa wamepangia mambo yao haikuwapo.
Mamba alishika kichwa chake akapiga ukunga wa hasira.
“Uliwatoa wapi? Hawa wanawake sio wa danguro la Mbezi! Hawana tabia hizi za kishenzi!” Mamba alifoka.
“Ila walisema ni wa Mbezi!” Aliyetoa namba alijitetea.
“Lakini mbona kama kunywa tulikunywa wote. Walituwekea madawa sehemu gani?” Mwingine aliuliza.
“Hawa malaya huwezi ukashindana nao kwa kunywa.” Mamba aling’aka. “Wana vichwa vigumu sana kulewa … itakuwa kuna mahali tu walitupatia wakatuweza. Si kwasababu ya pombe. Tusingeweza kuzima vile.”
“Sasa tutafanyaje na pesa zote wameondoka nazo? Tuwasiliane na mkuu atuwezeshe?” Mmoja alitoa wazo.
“Hapana! Hapana!” Mwenzake akadakia haraka. “Hatuwezi tukaomba pesa nyingine wakati alizotupa zilikuwa ni nyingi mno, na tumezimaliza kabla hatujafanikisha alichotuagiza.”
“Kwahiyo unashaurije?”
“Tupambane kwanza kufanikisha hili jambo mbele yetu kwa njia yoyote ile. Hapo mkuu anaweza akatuelewa na kutupatia pesa. La sivyo hakuna tena njia.”

****

Masaa kadhaa nyuma …

“Wamepiga simu, wanataka wanawake nane. Sasa hilo dili vipi?” Aliuliza mwanamke mmoja mwenye nywele fupi na hereni kubwa za mviringo masikioni.
Ndani ya chumba hicho walikuwepo jumla ya wanawake watano waliojilaza na kuketi kwenye godoro lililolazwa chini. Wote walivalia nguo za ‘hasara hasara’, watatu miongoni mwao wakipasha mapafu kwa sigara.
“Huo sio mchongo wa kuuacha kabisa. Watakuwa ndio wale wale wageni tuliowapa namba za simu. Wana madola ya kumwaga. Kama vipi wash’tue wakina Shamira tukachukue pesa hizo.”
“Ila kabla ya kwenda umewaambia watoe pesa ya advansi?” Mmoja aliuliza.
“Sasa tutaendaje kichwa kichwa bila kuwaambia hivyo?” Aliyeongea na simu akajibu kwa swali. Mwingine akachangia:
“Na kama unavyojua walituonea maeneo ya Mbezi kwahiyo wanajua sisi mambo safi, sio wale wa mitaani. Kwahiyo kama tunaenda basi tuwaambie wakina Shamira waje na mitupio ya hatari.”
“Poa poa!”
Simu ikapigwa na kutoa maelekezo yote. Baada ya punde Shamira na wenzake wakafika chumbani hapo na mikoba ya gharama iliyobebelea nguo za maana.
Baada ya kujivesha na kujitathmini, wakasuka mipango yao.
“Kama mnavyoelewa, sie ni watoto wa mbwa. Hapa hatulazi damu wala hatuzubai. Inabidi tuwakombe kila kitu.” Alisema yule mwanamke mweye nywele fupi na hereni kubwa. “Kila mmoja ahakikishe anapaka dawa yake kama kawa. Au sio?”
“Poa.”
Wakati wanajiandaa kwenda kutoa huduma kwa wanaume waliowaita kwa kujikwatua na kujipulizia manukato ya Paris, walipakaa pia unga fulani mweupe kwenye chuchu za matiti yao kwa kuzungusha kidole.
Walipomaliza, mmoja wao akasema kwa kebehi:
“Wakinyonya tu imekula kwao.”
Wote wakacheka na kugongesha viganja vyao.

****


☆Steve
 
daahhh.... ...!!!..yaaaniii utamu umekujaaa halafu umekataa... ...!!!..poa lakini..... .......
 
mh steve vp mkuu leo hadi mida hii bado au nawe umenyonya chuchu zilizotiwa ile dawa!!?
 
Mamba mbinafsi sasa Totoz zote nne unapeleka wap..
 
**SURA YA SABINI NA NNE**




(MSIMU WA 02)



MTUNZI: Steve Mollel



No: 0685 758 123






Baada ya mwanaume aliyevalia kiremba cha manyoya kunyoosha juu mkono wake uliobebelea panga, ngoma zote ziliacha kupigwa, kukawa kimya. Sauti pekee ya moto mkubwa uliowashwa kando ndio ikawa inavuma kwanguvu.
Watu wote wale wa ajabu waliovalia ngozi na michoro ya ajabu miilini mwao wakawatizama wakina Vitalis waliokuwa wamening’inizwa kwenye miti, kila mmoja na mti wake wakifungwa kamba miguuni, viunoni na mikononi.
Mwanaume yule mwenye kiremba cha manyoya akasogea karibu na kuanza kuwatizama mateka wake mmoja baada ya mmoja. Alifika kwa Sandra aliyekuwa wa mwisho upande wake wa kulia, akamtizama mwanamke huyo kana kwamba kuna jambo analitilia shaka.
Mwanamke huyo alikuwa amedhoofu mno. Macho yake yalikuwa yameingia ndani huku yakitengeneza uzio wa kijani. Pua yake ilikuwa inachuruza damu ya kijani. Mdomo wake ulikuwa umekauka sana ukichuruza udenda. Mguu wake uliopata jeraha ulikuwa kana kwamba umeoza, ulikuwa wa kijani mpaka maeneo ya ‘enka’, tena uking’ong’wa na nzi wengi.
Mwanaume huyo aliyevalia kiremba cha manyoya akatikisa kichwa chake akibinua mdomo. Mara sauti ya Kaguta ikapaza na kumshitua:
“Tafadhali, naomba umsaidie. Anaumwa sana!”
Kitendo cha Kaguta kumaliza tu hiyo kauli, alipokelewa na fimbo nane alizotandikwa kwa fujo na kuamriwa anyamaze kimya kwa ishara.
“Utakapoongea tena hayo maneno yako, hautochapwa, bali utauwawa.” Aliongea mwanaume yule mwenye kiremba cha manyoya kwa lafudhi ya mithili ya mtu aongeaye kiarabu, kisha akawaita wanaume wawili kwa ishara wakaja, akawanyooshea kidole kwa Sandra.
Wakamfungua Sandra na kumbebelea mpaka karibu na moto. Ngoma zikaanza kupigwa tena watu wakicheza na kuimba nyimbo zao kwa lugha ngeni. Japokuwa Kaguta na wenzake walipiga kelele kuomba Sandra aachiwe, haikusaidia. Sauti zao zilimezwa na sauti ya ngoma na nyimbo zisisikike kabisa.
Sandra akiwa hajiwezi kwa lolote akafungiwa kwenye mti mwembamba ila mkomavu na mgumu, tayari kwa ajili ya kutundikwa kwenye vishikizo vilivyosimama pembeni ya moto ili abanikwe kwa ajili ya nyama.
Kabla zoezi hilo halijakamilika, Bernadetha akamgeukia Vitalis akimtizama kwa sura yenye macho matulivu. Akamuita:
“Vitalis.”
“Naam!” Vitalis akaitika.
“Huu ndio muda wako. Muokoe Sandra.”
“Nitamuokoaje?” Vitalis aliuliza. Bernadetha akamjibu:
“Najua unaweza. Unajua unaweza. Muokoe kabla hatujachelewa.”
Wakati wanaume wale wakinyanyua mti uliombebelea Sandra wapate kumuweka motoni, wakasikia sauti kali ya mngurumo iliyowashitua.
Wote walitizama sauti hiyo ilipotokea, wakakutana na mnyama mkubwa mweusi akiwa amevimba.
Mnyama mkubwa akiwa ameshajiandaa kwa kufanya shambulizi.
Mnyama mkubwa akionesha meno yake makubwa na makali.
Mnyama mkubwa mwenye macho mekundu kama damu.
Mnyama huyo akiwa ni mbwa mwitu. Ila asiwe mbwa mwitu tunayemjua, bali yule mpana na mrefu, anayeogofya hata kumtizama.
Mwanaume yule mwenye kiremba cha manyoya akiwa ametoa macho ya kuduwaa, akapaza sauti kwa lugha ngeni. Mara watu wake wote pamoja na yeye wakatupa silaha zao pembeni na kuinama haraka kusujudu.
Mnyama alibadilika taratibu akawa Vitalis. Alimkimbilia Sandra na kumfungua toka kwenye ule mti aliofungiwa. Akamuuliza:
“Sandra, upo sawa?”
Sandra akatabasamu akiwa amefumba macho. Akasema:
“Ahsante, Vitalis. Ila nahisi muda wangu umefika.”
Vitalis aliwageukia watu wale wa ajabu waliokuwa bado wameinama, akawapazia sauti:
“Msaidieni, ana hali mbaya!”
Mwanaume yule mwenye kiremba cha manyoya akasogea karibu na kumwambia Vitalis kwa lafudhi yake kana kwamba anameza maneno:
“Tumechelewa, hatuwezi tukafanya lolote likamsaidia. Alitobolewa na mti wa mfofo. Ukitobolewa na mti huo inabidi utibiwe kabla haijapita dakika moja. Ikipita tu hakuna tena namna.” Vitalis aliporudisha tena macho yake kwa Sandra akamkuta mwanamke huyo akiwa ametulia tuli, mdomo wake unamimina damu ya kijani.
Alimuita lakini hakupata majibu. Aliweka sikio lake kifuani lakini hakusikia mapigo ya moyo.
Aligeuka akamtizama Kaguta na kumwambia:
“Ameenda.”
Kaguta akatizama chini na kudondosha chozi. Hakutia neno zaidi ya kusaga meno yake kwa uchungu usiomithilika.

***

“Kila kitu kipo sawa. Tunaweza tukaenda sasa.” Mwanaume mwenye kiremba cha manyoya alimwambia Vitalis aliyekuwa ameketi na Kaguta kwenye kitanda cha ngozi.
Macho ya Kaguta yalikuwa mekundu lakini pia uso wake ukiwa haba na furaha. Alinyanyuka akaongozana na Kaguta mpaka huko nje walipokutana na wanaume kadhaa wakaanza kusonga nao kuelekea upande wa mashariki.
“Kwanini umenikarimu ghafla hivi?” Vitalis alimuuliza mwanaume mwenye kiremba cha manyoya. Mwanaume huyo akatabasamu na kuuweka mkono wake begani mwa Vitalis. Akajibu:
“Kwasababu wewe ni kiongozi.”
“Kiongozi wa nini?”
“Katika mila na desturi zetu, mbwa mwitu ni mnyama mtakatifu anayeabudiwa. Huko nyuma, mababu zetu walipata kuwa kama wewe. Uwezo wao wa kugeuka na kuwa mbwa mwitu uliwafanya waheshimike na kulinda jamii yetu dhidi ya maadui.”
“Kwahiyo kwa sasa hakuna tena mtu anayegeuka na kuwa hivyo?”
“Hamna tena. Wote wameenda na kile kizazi cha mababu zetu. Hali hiyo imesababisha tuishi kwa mashaka lakini pia tukose mifano halisi ya kuwaelezea wajukuu zetu juu ya mambo hayo.”
“Lakini kwanini watu hao wamepotea na hakuna wengine? Ilikuwaje wakawepo?”
“Walituambia ni kwasababu walikuwa na mawasiliano na wanyama hao kipindi hiko cha zamani. Watu pekee waliopata uwezo huo ni wale tu waliokuwa shupavu na majasiri, wale waliojitolea kupambana na hao wanyama kwa ajili ya kulinda jamii zao. Hao wanyama ndio wakawapa huo uwezo. Ndivyo tulivyohadithiwa.”
Wakiwa wanamalizia maongezi hayo, wakawa tayari wameshakaribia eneo lililokuwa na watu wengi wakijikusanya, watu hao wakiwa ni wakazi wale wa kisiwa ila miongoni mwao wakiwapo pia Bernadetha, Bakari na Miraji.
Mwili wa Sandra ukiwa umefunikwa na majani mithili ya sanda ulishushwa na kufukiwa shimoni ngoma zikipigwa na nyimbo zikiimbwa. Juu ya kaburi hilo yakawekwa majani pamoja na nyoya moja lililotoka kwenye kiremba cha kiongozi. Baada ya hapo, watu wote wakarudi kwenye makazi yao na kuliacha kaburi nyuma.
Huko nyumbani siku ikajazwa na shughuli nyingi. Wakina mama wakawasha majiko yao na kuinjika vyungu motoni. Wanaume wakafyagia uwanja, wakaleta matunda mbalimbali nyumbani pamoja na kutengeneza uwanja mpana kwa ajili ya shughuli.
Wakati jua laelekea kuzama, sherehe kubwa ikazuka eneo hilo. Ngoma na nyimbo zikarindima kila eneo. Vitalis na wenzake walitengewa eneo maalumu la kuketi, karibu kabisa na kiongozi, hapo ndio wakaelekezwa dhumuni la tafrija hiyo.
“Ni mila na desturi zetu kushehereka pale ambapo mmoja wa familia ya kifalme anapofariki, kwasababu tunaamini anaenda mahali bora kuliko hapa. Marehemu ni miongoni mwa familia yenu, miongoni mwa kiongonzi wenu, anastahili heshima hii.”
Alisema kiongozi akimtizama Vitalis na kumuonesha kidole.
Walipewa chakula wakala, vinywaji wakanywa. Watu waliimba na kucheza kwa furaha.
Siku hiyo Kaguta akanywa pombe kupita kiasi asimsikie yeyote aliyemwambia aache hilo zoezi. Kwake aliona hiyo ndio njia mbadala ya kumtoa Sandra aliyeng’ang’ania kichwa chake haswa.
Alikunywa na kunywa mwishowe ‘akazima’. Akabebwa kama mtoto na kupelekwa ndani kulazwa.

***


☆Steve
 
***SURA YA SABINI NA TANO***




(MSIMU WA 02)




MTUNZI: Stevie Mollel



No: 0685 758 123





“Upesi! Hatuna muda wa kupoteza.” Mamba alifoka akiwaambia wenzake wanaoshuka kwenye boti ndogo nyeupe. Wote walivalia sare za wahudumu walizozipatia hotelini huku mikononi wasiwe hata na silaha yoyote.
Baada ya wote kushuka wakiwa wamekanyaga maji na moka zao, Mamba aliwaamuru:
“Nifuateni.”
Wakatembea hatua kadhaa kufuata nchi kavu. Macho yao yaliranda randa huku na huko lakini hawakuona kitu. Walisimama, Mamba akashusha pumzi ndefu akibinua mdomo wake.
“Hii ndio kazi ya kupoteza ramani. Hatujui tunaelekea wapi.”
Waling’aa ng’aa macho hapo kwa sekunde kadhaa, Mamba akasema:
“Twende mbele kwa mbele kabla tuliowaibia boti hawajatukuta hapa.”
Walisonga mbele kidogo wakaona ‘kijumba’ walichokuwa wanatumia wakina Vitalis. Waligawana pande wakavamia kijumba hicho ambamo ndani hawakukuta yeyote. Zaidi kwenye upekuzi huo walikuta simu na tanakilishi, bahati mbaya kwao, vyote navyo vilikuwa vimezima moto.
“Inabidi tusake kisiwa kizima. Haitotuchukua muda mrefu kutimiza hilo.” Mamba aliwaambia wenzake. Pasipo kubisha wakaanza kutimiza agizo hilo kwa kutembea huku na huko macho yao yakiwajibika haswa kutoa salamu kila pande ya dunia.
Baada ya mwendo wa dakika kumi na tano, chotara alipata ajali. Mguu wake wa kushoto ulichanwa pajani na mwiba. Pasipo kujua, ama kupuuzia madhara ya mwiba huo wakaendelea kutembea kutafuta wahusika wao.
Punde tu ilipopita dakika moja, chotara akaanza kuona kizungu na joto kupanda mwilini. Mwili mzima ulimvuja jasho kana kwamba amemwagiwa maji. Jeraha lilimimina damu haswa na kuchafua suruali, ila ajabu ni kwamba, damu ilikuwa ya kijani.
Mwishowe chotara akashindwa kutembea na kudondoka chini. Macho yake yalilegea mithili ya mtu anatekenywa na upamba sikioni, huku mwili ukifuka jasho kweli.
Haraka wenzake wakamsogelea kumjulia hali.
“Najisikia joto kali. Kizunguzungu, na macho hayaoni vizuri.” Alisema chotara kwa shida.
“Inabidi tumuache twende. Hatuna muda wa kupoteza.” Mamba akawaambia wenzake.
“Hapana. Hatuwezi tukamuacha hapa mtu tuliyekuja naye.”
Wengine wakamkatalia katu juu ya hilo.
“Nimesema tunamuacha hapa. Atakuwa tu mzigo kwetu huko mbele ukizingatia tuna kazi nzito.”
“Hapa tunamuacha na nani? Ingelikuwa wewe ungelitaka tukuache?”
Kishingo upande Mamba akaridhia waende naye. Wanaume wawili wakambebelea mwenzao safari ikajongea kuzidi kuzama ndani ya kisiwa ila sasa mwendo ukipungua kutokana na mzigo wa mgonjwa huyo.
Wanaume hao wasitembee muda mrefu, wakafika eneo dogo lililokuwa wazi lakini likizingirwa na miti mirefu kama sehemu zingine za kisiwa. Walikatiza eneo hilo, ghafla udongo ukatitia na kutengeneza shimo kubwa, wote wakazamia humo asiwepo hata wa kuwaokoa.
Kulikuwa ni giza na joto humo ndani. Mwanga wa jua uliokuwa unaangaza muda huo haukutosha kupenya shimoni na kuwamulika. Wakawa wanapapasa.
“Tupo wapi humu?”
Mmoja aliuliza. Badala yake sauti ya mwangwi ikamjibu:
“Tupo wapi humu?”

***

Mlango wa chumba afungiwacho Stanis ulifunguliwa wakaingia wanaume wawili. Wanaume hao walimfuata Stanis wakambebelea mithili ya kuku mwenye mdondo na kumburuzia nje mpaka eneo la mateso.
Walimfunga mikono na miguu kwenye mti kisha wakampisha mwenzao aliyeyebelea mjeledi apate kufanya kazi yake.
Sehemu zile zile zilizokuwa zina ‘madonda’ ya mijeledi ya jana, ndipo hapo pakafumuliwa na mijeledi mipya, damu zikamwagika kama maji.
Tofauti na siku iliyopita, Stanis hakupiga kelele kabisa siku hiyo. Macho yake yalikuwa yamechoka, mwili wake ukisukumwa na nguvu ya mijeledi mbele na nyuma. Mdomo wake mkavu ulinyamaza kimya usifunguke mpaka zoezi linakoma.
Watu wote wakiwa wanashuhudia, Stanis akabanduliwa toka kwenye mti aliofungiwa kisha akaburuzwa kama kiroba cha viazi kwenda kwenye makazi yake ya giza.
Huko, kama ada, akatupiwa ndani na mlango kufungwa.
Chumba kizima kilikuwa kinanuka damu kana kwamba ni machinjioni. Stanis akiwa kama mtu asiyejielewa, alilala humo kana kwamba hakusikia wala kujali harufu hiyo. Labda haikuwa inamkifu na kumbugudhi tena kama hapo awali. Aidha aliizoea sasa maana hakuwa na jinsi nyingine.
“Stanis! … Stanis!”
Sauti iliita. Stanis hata hakushituka wala kujisogeza.
Kwenye ukuta tunduni, Rajul akaendelea kuita jina hilo pasipo kukoma. Aliita mara kumi ila majibu yakiwa ni yale yale tu, kimya.
“Tafadhali Stanis, amka! … utakufa humu! Amka!”
Kimya.
Rajul alipiga piga ukuta mwishowe akachoka. Aliegemea ukuta akashusha pumzi.
“Lazima nifanye jambo kumuokoa huyu kiumbe. Hii inaweza ikawa sehemu yangu ya kwanza kutafuta rehema za Mungu wangu niliyemkosea.”
Alipenyeza kidole ndani ya shati aliyoivaa akatoboa mojawapo ya jeraha lake na kulichuruzisha damu. Alikinga damu hiyo na kuiweka kwenye kiganja cha mkono wake wa kushoto. Alinyanyua mkono wake wa kulia akaupeleka utosini na kufuta unga wa mchoro wake kwa kutumia kidole. Kisha kidole hicho akakidumbukiza kwenye damu kiganjani.
Kabla hajaendelea na kingine, akasikia mlango wa chumba chake unafunguliwa. Haraka akamwaga damu na kujifutia ukutani.
Waliingia wanaume wawili chumbani wakasimama mbele yake.
“Mkuu anataka kuonana na wewe.” Alisema mwanaume mmoja. Kabla Rajul hajasema lolote, alikwapuliwa na kubebwa mpaka ofisini kwa Kim alipokalishwa kwenye kiti kinachomtizama ‘Mkuu’, kisha wanaume hao wakatoka ndani na kusimama nje ya ofisi.
“Karibu, Rajul.” Kim alisema kwa tabasamu, Rajul asitie neno lolote.
“Bila kupoteza muda ningependa kwenda kwenye mada niliyokuitia. Na najua unaifahamu … Nadhani sasa ni muda wa kutimiza yale tuliyoyabakiza.”
Rajul alimtizama Kim kwa macho yaliyochoka, akasema:
“Siwezi. Sina nguvu ya kutimiza hayo. Unaj … hali yangu … si nzuri.”
“Bwana Rajul! Siwezi nikasubiri milele! Inabidi tumalize kazi yetu!” Kim alifoka.
“Najua … najua kitu ninachotakiwa kufanya. Ila kwa sasa … kwa sasa, sina ngu … vu hiyo.”
Rajul alijibu kisha akanyanyua sehemu yake ya shati yenye damu na kuipeleka puani. Harufu hiyo ikamchefua na kumtapisha.
Kim akakunja sura kwa kinyaa. Alimuita mfanyakazi wake aje kusafisha upesi. Akawaita na walinzi pia wamtoe Rajul na kumrudisha kwenye chumba chake.
Aligonga meza kwa hasira, akafoka:
“Ushenzi gani huu!”
Alishika kiuno akazunguka ofisi nzima huku na kule.

***


☆Steve
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom