Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Watu wenye majina ya Steven wanakuaga humbled sana ......
Tunakungoja .....mkuu utamu kolea........
 
Kweli nimeamini kuitwa mtumwa haihitaji ufungwe minyororo!
We steve mmasai yapaswa upigwe fine make si kwa kusubirishana kihivi aseee!
 
***SURA YA SITINI NA SABA***



(MSIMU WA 02)







Masaa matano mbele wote wakiwa wamedidimia ndani ya usingizi mzito, wanaume wasiopungua kumi na mbili wakiwa vifua wazi, wamebebelea mishale, mikuki na mapanga, waliwazingira katika hali ambayo hakuna sauti yoyote ilisikika – kama mizuka.
Wanaume hao walikuwa wamejichora chora michoro ya ajabu miilini mwao. Si kaptula wala suruali walivaa, bali ngozi zilizofungiwa vema viunoni mwao vipate kuwasitiri nyeti. Miguuni walikuwa peku. Kwenye mapaja ya mikono yao ya kushoto walifunga kamba isipokuwa mwanaume mmoja tu ambaye yeye pekee ndiye aliyevalia kofia kubwa la manyoya kichwani, shingoni akivalia cheni ya mifupa.
Mwanaume huyo alikuwa ana macho makubwa meupe yaliyokodoa. Aliwatizama wenzake akapandisha kichwa, wote wakasogea zaidi wakinyanyua mikono yao kana kwamba wanataka sasa kushambulia ndani muda mfupi ujao. Kabla hawajatimiza adhma, Vitalis alishituka usingizini mithili ya mtu aliyeona mzimu.
Alihema kama mbwa mwitu akitizama pande zake zote pasipo kuona kitu. Hakukuwa na lolote isipokuwa giza tu. Hakutosheka, alinyanyuka akatembea hatua kadhaa kila upande kabla hajarudi alipokuwa ameketi na kuanza kupekenyua mkoba mmoja uliokuwa kando, akatoa sindano.
Alishusha pumzi ndefu. Alipapasa papasa mkono wake wa kulia maeneo ya mkunjo akitafuta mshipa wa damu, taratibu akapeleka hapo sindano na kujidunga kwa uangalifu mkubwa wa vidole vyake kwenye uhakiki.
Alirudisha sindano mkobani, akajaribu kujilaza tena. Isichukue muda mrefu, akasikia sauti ya majani yakimwendo. Alikaa kitako akatizama tizama, mwishowe alipuuzia akaacha usingizi umbebe.
Watu wale waliokuwa wanataka kuvamia walikaa umbali wa mita kadhaa wakitizama yote anayofanya Vitalis. Japokuwa kulikuwa na giza totoro, kwao haikuonekana shida, walimuona vema Vitalis akihangaika hangaika mpaka pale alipoamua kujilaza.
Mwanaume yule mwenye shungi la manyoya alipiga kamluzi kadogo, wote wakaondoka eneo hilo wasijulikane hata wapi walielekea.
Masaa yalisonga, jua likachomoza. Kaguta alikuwa wa kwanza kuamka kabla ya yeyote. Alijikongoja akaenda baharini kupata maji, baada ya muda mfupi aliungana na Bakari na Miraji majini. Sandra naye na Bernadetha wasichukue muda wakaamka wakatengenezea kuni na kuwasha moto kwa ajili ya kuandaa chai. Muda wote huo, Vitalis alikuwa bado yu usingizini. Tena si usingizi mwepesi, bali ule wa kukoroma hoi bin taabani.
Sandra alimtizama Vitalis akamwambia Sandra:
“Sandra, unadhani ni kawaida?”
“Nini?” Sandra alijibu kwa kuuliza.
“Vitalis kulala mpaka saa hizi wakati yeye ndiyo huwa wa kwanza kuamka kila siku?”
“Labda kachoka. Kazi ya jana ilikuwa pevu.”
“Sidhani. Mbona wenzake wamekwisha amka? … huwa ikifika saa kumi na moja tu, Vitalis anaamka. Haijalishi amefanya kitu gani jana yake.”
“Kwahiyo wewe unahisi nini?”
Bernadetha alirusha macho yake vema akaona mkoba mmoja uliokuwa karibu na Vitalis ukiwa wazi. Alinyanyuka upesi akafuata mkoba huo alioutwaa na kutizama ndani. Akaona sindano tupu.
“Nilijua tu.” Alijisemea mwenyewe. Alichuchumaa akapachika kiganja chake kwenye paji la uso la Vitalis.
“Mmmh … wa moto.” Akasema tena. Alimtizama Vitalis kwa macho ya huruma, akatikisa kichwa.
“Nini kimetokea Vitalis? …” Alinong’oneza. Mara Vitalis akakurupuka. Bernadetha alimshika mabega akimtuliza.
“Tulia Vitalis … tulia, tupo hapa. Tupo wote.”
Vitalis alishusha pumzi akatizama chini. Bernadetha akamuuliza:
“Imekurudia jana, sio?”
Vitalis akatikisa kichwa kukubali.
“Ulijis’kiaje?”
“Nilihisi kuna watu wamekuja kutuvamia … nilisikia sauti za ajabu na vishindo vyao vikisogea tokea mbali. Nilipoamka sikukuta yeyote. Ila bado nilikuwa nasikia sauti … sauti kana kwamba wanatembea.”
“Haukuwaona kabisa?”
“Sikuwaona! Labda kwasababu sikugeuka mnyama kabisa. Niliwahi kujidunga sindano ndipo nikapata ahueni. Nikalala.”
“Pole sana. Ila upo sawa sasa.”
Alisema Bernadetha kwa tabasamu la matumaini. Vitalis alishika kichwa akalalama:
“Kichwa kinanipasua.”
Bernadetha akamlaza akimwambia:
“Pumzika. Mwili wako umetoka kwenye kazi kubwa ya kurudi kwenye hali yake.”
Vitalis akajilaza tena.
Bernadetha alinyanyuka akamrudia Sandra. Alimueleza yale yote aliyoyasikia toka kwa Vitalis, na kipindi wanapata chai akawaeleza na wanaume: Kaguta, Bakari na Miraji juu ya habari hizo.
Walipomaliza kunywa chai, Kaguta aliwaaga anaelekea bara kuleta mahitaji yaliyopungua, akilenga kwenda mapema hiyo ili awahi kurudi waendeleze zoezi lao la ujenzi lililokomea jana. Bakari alimpatia Kaguta tanakilishi pamoja na simu akazitie moto huko penye umeme.
Kaguta aliwasha boti akaondoka zake, baada ya nusu saa akakanyaga ardhi ya jiji la Dar es Salaam. Alipeleka simu na tanakilishi sehemu za kutia moto kisha akaelekea maeneo ya soko la kariakoo ambapo ndipo anachukulia mahitaji yake.
Hakuwa na papara, kwakuwa alilazimika kungoja vifaa vile vya umeme alivyovipeleka vipate moto, basi akaamua kutafuta mahali atulizane kidogo akinywa vitu vyake.
Akielekea kwenye mgahawa mmoja hapo hapo maeneo ya Kariakoo, alikatiza eneo la magazeti aoshe macho kwa kufahamu yanayoendelea ulimwenguni. Hapo vichwa viwili vya magazeti vikamteka fahamu:
MAJAMBAZI YATOROKA KIJASUSI!




MAJAMBAZI WAUA MAGEREZA NA KUTOKOMEA!




****


☆Steve
 
***SURA YA SITINI NA NANE***




(MSIMU WA 02)









Vichwa hivyo vya habari viliambatana na picha kadhaa za gari la wafungwa likiwa lina matundu kadhaa ya risasi – damu zimetapakaa zikifanya barabara nyekundu ya bendera. Kando kando ya picha hizo, kulikuwepo na picha ndogo ya wanaume watatu, mmojawapo Alphonce Mwamtembo, almaarufu Mamba.
Kaguta alitoa pesa mfukoni akanunua magazeti hayo. Alipoenda mgahawani akawa anayapitia taratibu akishushia na Tusker baridi.
Habari ni kwamba wafungwa watatu wakiwa njiani kuhamishwa gereza baada ya kutokea kwa vurugu kubwa gereza walilokuwepo hapo awali, walifanikiwa kuwapiku maaskari baada ya gari hilo kuvamiwa ghafula pale liliposimama ili maaskari watoe magogo kadhaa yaliyotandikwa barabarani.
Watu nane wakibebelea bunduki ‘SMG’ walichomoza vichakani wakawateka maaskari waliokuwemo ndani ya basi la wafungwa na wale wasindikizaji walikuwemo ndani ya defender. Wakawalaza barabarani na kuwamiminia risasi kisha wakawafungua watuhumiwa na kutokomea.
Maelezo hayo yalikuwa ni kwa mujibu wa askari aliyenusurika kufa, akiachwa na majeraha makubwa mwilini.
Kaguta aliyaweka magazeti hayo chini akanywa fundo moja la bia yake kisha akasema:
“Karibu tena mtaani Mamba. Ni kifo tu kinakuita.”

***

Hamilton, Bermuda: Saa kumi jioni.

Kim akiwa ameketi kwenye kiti chake cha kuzunguka, anaenda kushoto na kulia, aliwatizama wanaume wake wa kazi watano, wale ambao walinyweshwa damu ya mfalme wakiwa wamesimama kwa ukakamavu wanamtizama kwa makini, akatekenya ndevu zake za kidevuni akisema:
“Kwa siku tatu sasa namtafuta pasipo majibu. Kama mnavyojua, bado kuna kazi yangu ndogo sijamaliza naye alafu nimpotezee mbali. Nashindwa kuelewa wapi alipo na anafanya nini. Nataka mumtafute popote alipo, mji mdogo huu. Namuhitaji hapa kabla jua la kesho halijakucha. Mnaweza mkaenda.”
Waliitikia kwa kuinamisha vichwa vyao kisha wakashika njia kwenda nje. Kabla hawajatoka mlangoni, Kim aliita akauliza:
"Mmemuona Stanis leo?"
Walitazamana wakakanusha. Kim akawaruhusu waende.
Baada ya dakika ishirini wanaume hao wa kazi wakafika mbele ya tempo kubwa lenye rangi nyeupe.
Hapo wakaangaza angaza macho yao kabla ya mwanaume mmoja akivalia joho hajaja na kuwauliza:
"Naweza nikawasaidia?"
"Tunamtaka Rajul." Akajibiwa kiufupi pasipo babaisho.
"Samahani, hamuwezi kumpata huyo mtu kwa sasa." Alisema mwanaume yule pasipo kupepesa macho.
Hakujua kauli hiyo ingekuwa ya mwisho kwake kabla hajaiaga dunia. Alijikuta hewani baada ya kutandikwa teke kali la kifua. Alipotua chini hakusema hata 'mama!' pumzi haikuwa yake tena. Alitawanywa mbavu, kifua kikatengeneza shimo.
Mara kengele ikalia keng! Keng! Keng! Keng! Keng! Mwanaume mmoja aliyekuwa ameketi juu ghorofani aliiliza kwanguvu. Ndani ya dakika chache wakajaa wanaume sio chini ya hamsini. Wote walikuwa wamevalia sare za majoho ya kaki, vichwa vyao vikiwa vitupu kwa ukosefu wa nywele.
Walitapakaa uwanjani wakiwatizama wageni wao walioleta shari.
"Tunamtaka Rajul! Tupatieni na hamtopata kadhia yoyote. Kinyume na hapo tutabadili majina yenu muitwe marehemu ndani ya dakika!" Alitishia mwanaume mmoja wa kazi. Akajibiwa na mwanaume mlinzi:
"Hakuna chochote mtakachopata hapa! Unadhani tunawahofia?"
Mwanaume yule wa kazi alitabasamu kwanza kisha akawatizama wenzake. Kufumba na kufumbua macho yao yalibadilika yakawa ya simba.
Walinguruma kama simba mwituni. Walinzi walitazamana kwa hofu lakini hawakwenda popote, walisimama palepale wakiwazuia wageni kusonga ndani.
Hiko kikawa kifo chao. Ndani ya dakika tano tu walitenguliwa, wakavunjwa na kuchanwa chanwa, wakaachwa kwenye dimbwi la damu.
Wanaume wa kazi waliingia ndani wakamsaka Rajul mpaka wakapata chumba alimofungiwa. Walivunja mlango kwa teke moja tu, wakamkuta muhindi huyo akiwa hoi bin taaban ameng'ang'aniwa na minyororo. Mwili wake ulikuwa mwekundu kwa kuvujia damu. Alikuwa ana mashimo mashimo mwili mzima kwa kunyofolewa nyofolewa nyama na tai kila siku baada ya kuchapwa mijeledi hamsini kama dozi.
Ilikuwa ngumu kumtambua mpaka pale alipoitika kwa taabu sana alipoitwa jina lake.
"Tumekuja kukuokoa."
"Hapana. Hapana ... naomba mniache. Nataka ... kutumikia adhabu yangu..."
"Mkuu ametuagiza tukupeleke."
"Mmmh mmh ... siwezi kwenda. Mimi na ... mimi na yeye ... hatuna ... cha kufanya."
Wanaume wale wa kazi walivunja minyororo na mikono yao, mmoja akambeba Rajul begani wakaondoka zao.

***


☆Steve
 
***SURA YA SITINI NA TISA***






(MSIMU WA 02)







Majira ya saa nne usiku, pembezoni mwa bahari.

Stanis alichomoa sigara toka kwenye pakti, akaiwasha na kuiweka mdomoni. Alivuta mapafu matatu kabla hajawaona watu kadhaa wanakuja kwa mbali.
Watu hao waliposogea karibu alipata kuwahesabu na kugundua wapo kumi, akatabasamu. Alifahamu sasa kazi inaelekea kuwa nyepesi zaidi. Kwa watu wengi kama hao, hakuna kisiki kigumu.
Watu hao walikaribia, Gog akawatambulisha kwa Stanis kama wahusika wapya waliopendezwa na wazo lake la kuleta mabadiliko. Mmoja alisogea mbele akaongea kwa niaba:
"Tunatumai utafanya maisha yetu yawe bora zaidi kuliko afanyavyo Kim. Tumeamini hivyo na ndio maana tupo hapa."
Walipeana mkono na Stanis, Stanis akawapa pia neno lake:
"Naahidi hilo kwa moyo wangu wote. Ameshindwa kuthamini mchango wetu, basi hatuna budi kujilipa fadhila wenyewe..."
Akakatizwa:
"Unataka tufanye nini?" Mwanaume aliyeongea kwa niaba aliuliza.
Stanis akatabasamu kwanza.
"Nataka kuwapa kazi moja tu, vingine nitavimaliza mwenyewe."
“Kazi gani hiyo?”
“Msiwe na haraka. Ni moja ila kinataka uangalifu mkubwa sana. Endapo tukiwa na papara basi tutagundulikana na kuishia kwenye vitanzi.”
Wote walikaa kimya wakiskiza.
“Mbele yetu kuna mlima mmoja tu, kama tukiupanda huo basi kote ni tambarare. Mlima huo una vilele vitano, kila kilele kina ncha na baridi kali. Ila ndio njia yetu pekee. Lazima tuupande tuikute tambarare.”
“Sijaelewa, unamaanisha nini?” Mwanaume mmoja mgeni aliuliza.
“Namaanisha kwamba, ili tupate yale tunayoyahitaji basi lazima tuwamalize watu wale watano waliokunywa damu ya simba. Kim hana chochote wala lolote la kutuzuia, ni tambarare tu.”
“Kim ni tambarare?” Aliuliza tena mwanaume yule. Stanis akatikisa kichwa.
“Ndio, ni tambarare. Najua udhaifu wake upo wapi. Hana nguvu yeyote kama vile anavyotudanganya kila siku, hilo nina ushahidi nao wa kutosha. Juzi nilimsikia anaongea na wale watu wake aliowanywesha damu ya kwamba anangoja na yeye apate kutimizwa na mganga ili wawe familia kamili isiyozuilika. Ina mana Kim anapelea, kuna jambo bado hajatimizwa isipokuwa tu wale watano. Kwahiyo dhumuni letu ni kumshambulia haraka kabla hajaonana na Rajul.”
Fraud alikohoa kidogo, wote wakamtizama. Akasema:
“Kim atakuwa tayari ameonana na mganga wake. Leo nimeshuhudia akiletwa jengoni.”
Nun akadakia:
“Ila alikuwa na hali mbaya sana, hata kuongea shida. Sidhani kama watakuwa wamefanya lolote. Mwili wake wote umejaa majeraha na damu. Wanasema alikuwa matesoni huko walipomtoa.”
“Basi kesho itabidi tufanye tukio letu.” Stanis akapendekeza.
“Kazi yenu itakuwa moja tu ya kuwahadaa watu wale watano kwamba mmevamiwa. Mtafanya hayo kwa malengo ya kuwavutia ndani ya chumba cha mateso na kuwafungia humo. Tayari nimeshaandaa gesi ya sumu kwa ajili yao, mtapenyeza bomba chini ya mlango. Kwa dakika moja tu watakauka kama mabua. Mimi nitaenda kumalizana na Kim.”
Wakaridhia. Stanis akawageukia Gog, Nun, Fraud na Adrian.
“Nyie kazi yenu ni kukata viherehere wote wataokuwa kinyume na sisi. Hakikisheni hawaponi kwa njia yoyote ile.”
Nao wakaridhia.
“Tukutane kesho asubuhi ya saa kumi na mbili, hapahapa.” Stanis alitoa tamko, wakatawanyika kuondoka.
Juu ya meza ya Kim, ofisini, kifaa kimoja cha bluu mithili ya redio ndogo kilitoa sauti ya vishindo vya watu wakitembea. Baada ya muda sauti hizo zilififia, ikasikika sauti moja ikisema:
“Nadhani umesikia yote yaliyopangwa, mkuu.”
Kim akatikisa kichwa akisema:
“Nimeyasikia yote. Umefanya kazi njema, kapumzike sasa tukutane kesho.”


***


☆Steve
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom