Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

***SURA YA SITINI NA TANO***



(MSIMU WA 02)








Mwanaume mmoja akiwa kifua wazi, amevalia tu bukta alitoka eneo la wazi la la bahari akitembea kuelekea ndani ya jengo la hoteli ya Whitesands.
Mgongoni mwake alikuwa ana mchoro mkubwa wa kichwa cha simba. Kichwa chake hakikuwa na nywele. Mwili wake ulijaza vya kutosha kufanywa mlinzi. Alikuwa mrefu akitembea kwa kudunda mithili ya kitenesi.
Alikata korido akinywa kinywaji chake cha kopo taratibu mpaka pale alipowadia mbele ya mlango uliopachikwa namba 609. Hapo akagonga mlango mara tatu.
Mwanaume aliyekuwa ndani alichungulia kwenye kitundu kilichokuwepo mlangoni kwanza kabla hajaufungua mlango. Aliporidhika na alichokiona aliufungua mlango kisha akasimama kando kumngoja mwenzake aingie.
Ajabu akashangaa kuona mwili wa mwenzake huyo unadondokea ndani kama zigo. Kufumba na kufumbua akaingia Vitalis. Mwanaume yule aliyekuwepo ndani asipate hata nafasi ya kufanya kitu, haraka kama mwanga wa radi alikitwa teke la shingo akarushwa mbali.
Alidondokea kwenye meza ya kioo akaivunja vipande milioni.
Alijifyatua na mikono yake akasimama tena wima. Aliruka hewani akituma teke lakini lilidakwa na mkono wa kuume wa Vitalis kisha akarushwa akibamiziwa ukutani.
Asikome, alinyanyuka tena akiwa anavuja damu puani akakunja ngumi.
Mara hii Vitalis alihakikisha mwanaume huyo hasimami tena kwa kumpachika teke ubavu wa uso akitumia mguu wa kushoto baada ya kumhadaa kama vile anatumia mguu wa kulia.
Mwanaume huyo alidondoka chini akicheua damu. Alirembua macho akiachama mdomo. Alionekana tayari amekubali sheria, hana madhara tena.
Vitalis alimsogelea karibu mwanaume huyo akamtizama. Mara mwanaume huyo akaupeleka mkono wake nyuma ya kiuno akatoa bunduki na kumnyooshea Vitalis.
Alitabasamu kujipongeza. Alijua sasa anamaliza habari iliyoonekana awali kumshinda.
"Vitalis?"
Aliuliza mwanaume huyo.
Kabla Vitalis hajasema neno, mlio wa risasi ulivuma mara tatu mwanaume yule akitobolewa fuvu la kichwa. Risasi ilitoka kwa Kaguta ambaye alikuwa amesimama mlangoni.
"Mara ya pili hiyo!"
Kaguta alimwambia Vitalis akitabasamu kisha akaongezea:
"Tumeshawamaliza wote. Tunaweza tukaondoka sasa upesi kabla hayajageuka mengine."
"Hamna chochote mlichopata?"
"Kipo."
Kaguta alipomaliza kusema hilo, sauti ya king'ora ilianza kulia ndani ya hoteli. Miraji aliyekuwa amesimama nje ya mlango aliingia chumbani akawaambia:
"Tuondokeni haraka!"
Kaguta alisogelea dirisha la chumba akachungulia nje. Aliona walinzi kadhaa wakijipanga na kuwatuliza wageni, aligeuka akawaambia wenzake:
"Hatuwezi tukatoka hapa kirahisi, watakagua kuponi kabla ya kumruhusu mtu atoke nje."
"Vipi na baharini?" Vitalis aliuliza.
"Hamna mtu baharini. Hatutaweza kutumia njia hiyo, tutakamatwa kiurahisi!"
"Kwahiyo?" Miraji aliuliza.
"Inabidi tuunde tukio!" Kaguta alijibu. "Tukio litakalotufanya tuondoke kwa urahisi!"
Dakika tano tu kupita baada ya hiyo kauli, moto ulizuka hotelini. Hapo sasa vurugu ikawa kubwa. Watu ambao walikuwa wamejifungia ndani ya vyumba vyao waliposikia habari za moto, walizuka wakakimbia kama wehu.
Katikati ya watu hao walojichopeka wakina Vitalis wakatoka getini kiurahisi. Nani angekagua kuponi ilhali watu wanakimbia huku na huko kuokoa roho zao?

***

Taa iliwashwa kummulika Rajul aliyeketi kwenye kiti akiwa amefungwa kamba nzito. Alifichama macho yake kwa mwanga huo mkali akitizama pembeni. Alitulia kwa sekunde tano asisikie majibu, akauliza:
"wewe nani ... unataka nini kwangu?"
Kimya.

Alisikia vishindo vya miguu vikimsogelea na mara taa zikawashwa. Alijaribu kufungua macho yake kutizama lakini mwanga mkali wa taa ulimuumiza. Alifunga na kufungua macho taratibu taratibu mpaka pale yalipozoea mwanga.
Hapo ndio akaona watu nane wamemzunguka. Wote walikuwa wamenyoa vipara kama yeye, wakivalia nguo ambazo na yeye huvaa na pia shingoni wakibebelea cheni za madunguli makubwa ya mbao.
Utofauti ni kwamba yeye alivalia nguo nyeupe wakati wenzake wakivalia nguo rangi za kahawia na michoro yao kichwani haikuwa zigzag bali iliyonyooka ikikomea utosini na nukta nyekundu.
"Rajul, umepungukiwa imani na hekima kiasi hiki?" Sauti moja ilisikika ikiuliza. Haikujulikana ilitokea wapi mpaka pale mzee mmoja mwenye asili ya India alipotokezea nyuma ya wale wengine nane. Alikuwa ni mzee mrefu mwenye ndevu nyingi nyeupe kama sufi.

"Kwanini umebadili adhma ya nguvu zako ukitekwa na tamaa za dunia dhalimu, katili na ovu?" Aliuliza yule mzee akijongea karibu zaidi.

"Unafahamu fika, malengo yetu ni kusaidia walio wanyonge, walio masikini, wasio na nguvu. Tulikula kiapo hiko nawe pia wajua tukiahidi kuacha maisha yote na anasa zake ili tukapande mbegu ambayo itazaa mema duniani. Umesahau kiapo kile?"

Rajul alitikisa kichwa akitizama chini.

"Umetusaliti. Umesaliti imani yako. Umesaliti kiapo chako. Umemsaliti muumba wako na tutamuachia yeye akuhukumu. Sisi si chochote mbele zake bali wanaohitaji msamaha na upendo wake."
Alihitimisha yule mzee. Rajul akapaza sauti:

"Naomba nitizamwe kwa jicho la huruma! ... mtamuacha kondoo huyu aliyepotea ingali maisha yake yote tokea ujana alimtumikia Mungu wake kwa nia ya dhati?"

Aliwatizama waliomzunguka akiendelea kuongea.

"Mimi naliumbwa na damu na nyama. Ni binadamu. Natenda makosa. Napitiwa. Naomba nipewe nafasi nyingine ya kufuta makosa yangu. Najutia nilichokifanya."

"Rajul!" Mzee aliita. "Hakuna msamaha kwa mtu anayekiuka kiapo chake. Uliweka maagano na Mungu wako, na umeyavunja maagano hayo ukiwa na akili zako timamu. Ulituficha sisi binadamu, hukujua Mungu anaona kila sehemu, kila eneo, kila tukio na kila mtu. Hatuna la kusema wala kuamua juu yako, bali Mungu pekee. Tunatimiza yale uliyoyaingia maagano."
Alisema mzee yule kisha akawatizama wanaume waliokuwepo pale na kuwapa amri:

"Mpelekeni anapostahili. Hakikisheni anapata anayostahili."
Baada ya maneno hayo mzee akaondoka. Rajul alifunguliwa kamba akabebwa akipiga makelele ya kuomba msamaha.

****


☆Steve
 
***SURA YA SITINI NA SITA***





(MSIMU WA 02)









Hamilton, Bermuda.

Mawimbi ya bahari yalichapa fukwe taratibu yakisukumwa na upepo.
Siku hiyo maji yalikuwa machache, kwa kuyatizama tu ungaligundua hilo. Yalisonga mbali tofauti na kawaida yake. Hiyo ikawa fursa nzuri kwa watoto kuchezea maji na hata pia kwa watu kutembea tembea fukweni wakanyage mchanga ambao huwa unamezwa na maji mara nyingi.
Miongoni mwa watu hao, alikuwapo Stanis. Suruali yake ya jeans aliyoivaa aliikunja vema mpaka magotini akivalia shati jeupe jepesi lililokuwa linapeperushwa na upepo wa bahari.
Asionekane na furaha aliranda randa huku na kule akiyapiga maji teke. Ila mara kadhaa alitizama kushoto na kulia kama anatafuta kitu kisha akaendelea na shughuli yake ya kuzurura.
Baada ya dakika kama nne mbele simu yake ilitetemeka mfukoni. Aliitoa akaitizama. Alitabasamu akajongea kutoka eneo la bahari akielekea upande wake wa kushoto.
Huko akakutana na mwanaume chotara ya mweupe na mweusi mwenye nywele ndefu nyeusi ti. Walikumbatiana wakasonga mbali zaidi wakiteta;
"Yuko wapi Fraud?" Stanis aliuliza.
"Wote wameshafika, wanakungoja." Alijibu mwanaume yule mwenye nywele ndefu, Gog.
Walifika mahali fulani palipoezekwa makuti mepesi, wakajumuika na wanaume wengine watatu, jumla wakawa watano: Stanis, Gog,Fraud, Nun na Adrian.
Baada ya kutizama kushoto na kulia, Stanis akasema:
"Nimewaita hapa kwasababu najua ninyi ni marafiki zangu, watu wangu ninaowaamini, na ninatumai hamtoniangusha kamwe."
Alitizama tena kushoto na kulia kisha akaendelea:
"Bila shaka wote mnakumbuka jinsi nilivyowaunganisha kwa Kim baada ya kuhangaika sana. Nisingependa tujadili sana mambo ya nyuma, ila nadhani sasa ni muda wa kunigawia kidogo fadhila. Si tu kwasababu ya urafiki, bali pia fadhila hiyo yenu itawarejeshea fadhila kubwa sana."
"Kipi unataka tufanye Stanis?" Nun aliuliza wakimkodolea macho Stanis kwa makini.
"Nataka tuchukue huu ufalme!" Stanis alisema akitumbua macho.
"Nataka tuukwapue, tuuweke mikononi mwetu!"
"Kivipi?" Fraud aliuliza na kuongezea, "Sidhani kama hilo jambo ni rahisi hivyo."
"Si rahisi ila inawezekana!" Stanis alijibu kimkazo. Akaongezea:
"Nina mipango yote. Kila kitu nimeshakianisha, ni utekelezaji tu ndio unaotakiwa."
Akanyamaza akiwatizama wenzake kwa macho ya ufahamu.
"Nani atakuwa na mimi?" Aliuliza.
"Tupo pamoja." Gog akajibu akitikisa kichwa.
"Na mimi pia." Fraud akadakia akimaliziwa na wengine wawili.
Stanis akatabasamu.
"Ahsanteni sana." Alisema kisha akachuchumaa chini, akachora ardhi na kidole.
"Tizameni hapa mniambie ..."

***

Hakukuwa salama tena kisiwani. Boti ilishatua karibu na fukwe Vitalis na wenzake wakijipakia wapate kuyeya.
Walifanya hivyo baada ya kutoa heshima zao za mwisho kwenye makaburi ya wenzao waliotangulia mbele za haki. Baada ya kila mmoja kusali kwa imani yake, walibeba walichokiona cha muhimu wakatia moto boti mpaka walipokutana na kisiwa ambacho hata jina hawakukifahamu.
Hakikuwa kikubwa kama cha hapo mwanzo. Kilifungwa na misitu mingi kikitengeneza giza hata wakati wa mchana.
Kwa kutizama haraka haraka, hakukuwepo na dalili yoyote ya viumbe kuishi hapo. Palikuwa kimya, kimya mno. Hata milio ya ndege haikuwepo. Labda tu sauti ya mawimbi yakichapa fukwe.
Kabla basi ya jua kuzama, wanaume wakachakarika kukata miti, kusafisha vichaka watengeneze mahali pa kupumzikia.
Kwa ugumu wa kazi, mpaka jua lazama hawakuwa wamefanikiwa. Ila walipiga angalau hatua. Walishapata eneo safi ambalo walichopeka mistimu ya miti hapo na paa la majani majani kuvutia muda.
Kupambana na giza na ubaridi wakawasha moto wakiketi kwa kuuzunguka.
"Nini kinachofuata sasa?" Sandra aliuliza. Kana kwamba wamepanga, wote wakajikuta wakimtazama Vitalis.
"Kuna wengine wapo nchini, itabidi tuwamalize mapema. Bahati nzuri kwa upatikanaji wa simu ya mmojawao kutatusaidia kuwatambua wapi walipo. Hatuna muda mwingi, lakini pia hatupo mbali sana na mkuu wao, Kim." Alisema Vitalis. Akaendelea kuhutubia:
"Tumepewa sababu nyingine ya kupambana - kuwapumzisha wenzetu mahali salama. Kama tusipofanikiwa basi hawatokuwa na amani huko walipo. Tumebakiza michoro miwili tu, mmoja kati yao tumeshaanza kuhangaika nao. Hatutakiwi kuchoka bali kuongeza nguvu zaidi. Tuwe waangalifu sana tunapotoka nje ya hili eneo kwasababu yoyote ile, iwe ni kwaajili ya kufuata vifaa vyetu vya umeme ama kufuata mahitaji. Keshokutwa tutatoka huku mafichoni twende bara. Na hatutorudi mpaka pale tutakapohakikisha hakuna yeyote kati yao anayevuta pumzi tena.
"Kwanini keshokutwa si kesho?" Bernadetha aliuliza.
"Kwasababu kesho tuna kazi kubwa ya kufanya hapa." Kaguta alimsaidia Vitalis kujibu kisha akaongeza:
"Vipi tukienda huko bara, tutapata vinywaji? Nina kiu sana aisee! Sijaonja kitambo."
Sandra akamzaba Kaguta kofi dogo mgongoni.
"Umeanza. Hakuna kunywa tena!"
"Kidogo tu nisafishe koo." Kaguta alijitetea wakaendelea kuzozana na Sandra kiutani.
Giza lilisonga mwishowe wakapitiwa na usingizi. Moto ulivuma mpaka ukatika pakawa giza kamili ambalo lilishinda mwanga wa mwezi kwa kishindo kikuu.



***


☆Steve
 
Ndio naianza sasa kuisoma

Natanguliza shukrani kwako uliyeileta hii story!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom