Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Simulizi inapendeza na inamafundisho mazuri, ingawaje INA maudhui yasiyo chanya kwa viongozi wa Serikali.
 
***SURA YA HAMSINI NA SABA***





(MSIMU WA 02)







Giza lilitwaa jiji la Hamilton ambalo ukiachana tu na umaarufu wake wa kuwa na fukwe za bahari zinazovutia basi utakutana na bandari yake asili inayofanya kazi usiku mchana. Meli za makampuni makubwa kama DryShips Inc, Frontline Limited na Dockwise zilikuwa zinapishana kuingia makaoni mwake.
Sauti za mawimbi ya bahari, upepo mwanana na milio ya mabasi makubwa ya abiria ambayo bado yalikuwa yanatoa huduma ndio hasa zilikuwa zinasikika zikitumia utulivu wa usiku kwa faidaze. Mbali na hapo labda sauti za watu wachache hapa na pale.
Ndani ya jengo jeupe la ghorofa kwenye uwanja mkubwa walisimama wanaume wapatao themanini kwa idadi. Walichanganyikana wanaume weusi na wazungu. Vifua vyao vilivyojengeka kimazoezi vilikuwa wazi wakivalia suruali nyeusi za jeans. Migongoni mwao walibebelea mchoro mkubwa wa kichwa cha simba.
Mbele ya wanaume hao kulikuwapo na kiti kikubwa kirefu chenye rangi ya dhahabu. Hakikuwa na mtu lakini wanaume wote walikuwa wanakitizama kana kwamba kuna mtu asiyeonekana amekaa hapo.
Kim alitokea mlango wa kushoto wa uwanja, akanyookea kitini na kuketi. Wanaume wote nao wakaketi kitako chini wakimtizama.
“Nimewaita hapa kwa dhumuni la kuwataarifu kazi iliyopo mbele yetu. Ndani ya siku nne zijazo tunatakiwa tutengeneza msiba mkubwa. Msiba wa kifalme. Msiba utakaotikisa vichwa vya habari.”
Kim alisema kwa kujiamini akikaza macho yake.
“Nitawateua wanaume watano miongoni mwenu. Wanaume hao wataenda Oman. Wataenda huko kwa dhumuni moja tu: kummaliza Sultan Absaedy Omar ama mwanawe yeyote wa kiume. Nataka damu zao hapa kwa gharama yoyote ile … kwa gharama yoyote! … Wanaume hao watakaofanikisha hilo, watazawadiwa maradufu kwa ushujaa na ufanisi wao.”
Kim alinyanyuka akaweka mikono yake nyuma. Alitembea akipita katikati ya mistari ya wanaume waliokuwa wamejipanga akiendelea kumwaga maneno.
“Hakuna nafasi ya kufanya makosa katika hili. Ni eidha kufa ama kupona. Ni eidha wao wafe ama sisi tufe. Hatujawahi kushindwa vita yoyote ile na hii siyo ya kwanza na wala haitakuwa ya mwisho. Nawaamini.”
Baada ya maneno hayo aliwateua wanaume watano kwa kuwagusa mabegani. Wanaume hao wakasimama na kwenda mbele, wengine wakasimama na kutokomea.
Katikati ya wanaume hao watano walioachaguliwa, walikuwepo pia wanaume wale wawili waliokuwa na Kim wakati anatizama televisheni, walijulikana kwa majina ya Panther na Jaguar.
Kim aliwatizama akawapa ishara huku wengine akiwaambia kwa maneno:
“Nimewachagua nyie kwasababu naamini kwa dhati mnaweza mkafanya hii kazi. Nataka damu ya kifalme ije hapa ndani ya siku tatu tu. Siku tatu! Nataka mkajadili na kupanga usiku huu. Kesho asubuhi mnieleze nini mnahitaji kukamilisha hili zoezi.”
Wanaume hao wakaondoka wakimuacha Kim mwenyewe ameketi kwenye kiti chake kikubwa. Alifikira kwa muda kisha akatabasamu akitikisa kichwa.
“Nadhani hili litakuwa kisasi kizuri dhidi ya yule mshenzi aliyeninyima fursa ya kuwekeza kwenye biashara yake ya mafuta … Sultan, nipo njiani nakuja. Ulinihukumu kwa uchotara wangu, mimi nitakuhukumu kwa ncha ya upanga.”

***

Bakari akiwa pamoja na Miraji walitizama kioo cha tanakilishi mpakato kilichokuwa kinaonesha michoro ya simba na alama za maji kwa makini kana kwamba wanatafutia suluhisho hesabu ngumu.
Bakari alitikisa kichwa chake akauliza:
“Sijui hii michoro ina maanisha nini?”
Ukimya ulikatiza kwa sekunde kabla Bakari hajaendelea kunena:
“Ina mana kuna watu wengine wenye hii michoro, sio?”
“Nadhani.” Miraji alijibu.
“Sasa tutawapataje hao watu? Au tutawangoja mpaka watushambulie?”
“Inabidi tuwagundue mapema. Tofauti na ilivyokuwa kwa kundi la nyoka, wenyewe walitutafuta. Hatujajua hawa wenye hii michoro watatutafuta ama tutawatafuta. Ila tutakuwa salama zaidi endapo tutawatafuta kabla wao hawajafanya hivyo.”
Vitalis na Kaguta waliingia wakaungana na wakina Bakari. Waliendeleza mjadala wakijaribu kufumbua fumbo ambalo lilikuwa gumu kufumbuliwa.
Marietta aliingilia mjadala huo akamuiba Vitalis. Alitaka akacheze naye fukweni kwani alimkumbuka sana tokea yupo shuleni bweni. Vitalis alishindwa kukataa. Alimnyanyua Marietta akamuweka begani wakaenda zao kuchezea maji ya fukweni.
Walirushiana maji wakikimbizana. Walioga michanga. Waliogelea wakishindana kukaa muda mrefu majini. Mwishowe walilala kwenye mchanga mlaini wa fukwe wakitizama jua la saa mbili asubuhi. Hapo Bernadetha akajitokeza na kujiunga nao baada ya kukaa muda mrefu pembeni akiwatizama pasipo wao kujua.
Macho yake yalikuwa mekundu akitabasamu. Kwa muda wakati anamtizama Vitalis akicheza na mwanae, Marietta, alimkumbuka mume wake, Malale. Kila mwisho wa juma walikuwa wanaenda ufukweni kama familia. Huko walicheza na kufurahia kisha wanarudi nyumbani jua likizama.
“Karibu!” Vitalis alimkaribisha Bernadetha.
“Ahsante.” Bernadetha alijibu akimtizama mwanae.
“Vipi, kuna tatizo?” Vitalis aliuliza.
“Hapana. Hamna tatizo!” Bernadetha alijibu akilazimisha tabasamu. Alimbeba mwanae akamuuliza:
“Mlikuwa mnafanya nini?”
“Tunacheza! … Nilikuwa nacheza na anko!” Marietta alijibu kwa maajivuno.
“Alafu mama, nimemuambia anko anifundishe ngumi!”
“Ngumi?” Bernadetha alitabasamu. “Nani kakuambia anko anapigana ngumi?”
“Nilimuona! … siku moja nilimuona akipigana na anko Kaguta.”
Baada ya kucheka, Bernadetha akauliza:
“Wewe unataka ukampige nani?”
“Kule shuleni kuna mijitu migomvi!” Marietta alijibu. “Nataka niwapige mpaka wakome!”
Wote walicheka wakaondoka kurudi kwenye makazi yao.
Siku hiyo ilikuwa ni ya kupumzika. Hakuna kazi waliyofanya zaidi ya kupika na kula kisha kufurahia mandhari ya bahari. Waliogelea, walicheza mpira mpaka jua linatuama.
Kaguta akiwa pamoja na Sandra, Miraji, Jombi na Bakari waliaga wanatoka kwenda kujirusha nje ya kisiwa. Waliahidi kurudi siku inayofuata mapema, wanahitaji kupumzisha na kubadilisha mazingira mara moja.
Baada ya mvutano wa hapa na pale, walikubaliana waende.
“Kuweni makini.” Bernadetha aliwahasa.
“Usihofu. Wapo na mimi.” Kaguta akajibu akijinyooshea kidole.
Walitumia boti yao ndogo wakakata maji kwenda jiji la Dar, wakawaacha Bernadetha, Vitalis na Marietta kisiwani.
Haukupita muda mrefu baada ya kula chakula cha usiku, Marietta akapitiwa na usingizi. Vitalis alimbeba akampeleka chumbani alipomlaza na kumfunika na shuka.
Alirudi sebuleni akamkuta Berbadetha ametulia akijikunyata. Alikuwa anafikiria jambo ambalo halikuchukua muda mrefu akamshirikisha Vitalis:
“Samahani, Vitalis. Kuna muda naona picha ya mume wangu pale ninapokutizama. Sijui kwanini inakuwa hivyo. Haijalishi mara ngapi najitahidi kujizuia lakini haisaidii katu.”
Bernadetha aliweka kituo akitizama chini, mara chozi likaanza kumshuka.
“Leo wakati nakuona na mwanangu nili …”
“Sshh! …” Vitalis alimkatiza. Alimfuta chozi akamnyanyua uso.
“Usihofu. Haina haja ya kuomba samahani, Bernadetha. Naelewa. Naelewa unachojihisi … kuna mambo yakupasa uyaache yaende ili upate amani moyoni.”
Vitalis alimbusu Bernadetha shavuni kisha akambeba akimlaza mikononi mwake.
“Nataka uwe na furaha. Sipendi kukuona ukifadhaika.”
Bernadetha alipeleka mdomo wake kwa Vitalis wakanyonyana ndimi. Walielekea chumbani wakazima taa.

****


☆Steve
 
***SURA YA HAMSINI NA NANE***






(Msimu wa 02)






Muziki ulizidi kunoga ndani ya klabu. Huku mataa ya rangi mbali mbali yakimulika mulika hovyo, watu walikuwa wanajichengua kwa miondoko mbali mbali kutokana na midundo ya muziki iliyokuwa inaita muda huo kwenye vipaza. Walicheza kana kwamba kuna mtu anawalipa, ama labda kuna shindano la kumtafuta gwiji la miondoko.
Wadada walivalia nguo fupi na za kubana. Wanaume wengine nao walivalia nguo zilizobana miili yao hali iliyopelekea ugumu kuwatambua jinsia endapo ukiwatizama kwa nyuma.
Kila mtu alicheza na mtu wake, ikiwemo pia na wakina Kaguta waliokuwemo humo ndani. Wakati Kaguta anacheza na Sandra, Miraji, Bakari na Kaguta walishapata wenzi waliokuwa wakisakata nao rhumba.
Wakati hayo yanaendelea, mwanaume mmoja akiwa amevalia tisheti nyeusi yenye maandishi ya lugha ya kifaransa, Mon frere, alikuwa anawatizama wakina Kaguta na macho yasiyopepesuka. Mkono wake wa kulia alibebelea kinywaji cha BALTIKA ya kopo. Mkono wake wa kushoto alikuwa akiutumia kukunia ndevu zake kidevuni.
Baada ya dakika kadhaa, Miraji alitoka kwenye uwanja wa kucheza akaelekea chooni. Mwanaume yule aliyekuwa anawatizama akanyanyuka na kumfuata. Akitembea kuelekea huko, alichomoa kisu kidogo mfuko wa nyuma wa suruali, akakiweka vema mkononi.
Watu wengi walikuwa wanaelekea huko chooni. Haswa walevi ambao walikuwa wanaenda kupunguza wakapate kuongeza tena. Katikati ya nyomi hiyo iliyokuwa inaenda na kurudi, Miraji alipotelea asijulikana wapi alipo. Giza lilifanya ugumu kuonekana. Kwakuwa wengi wao waliokuwa wanaenda huko maliwatoni ni walevi na hawapendi mwanga, walizima taa.
Mwanaume yule alirudi sehemu yake alipokuwa ameketi awali akasubiri hapo. Muda ukazidi kuyoyoma. Alitizama saa yake mara kwa mara mwishowe akaamua kunyanyuka akafanye tukio vivyo hivyo.
Taratibu alitembea akiwapisha watu. Macho yake yalimtizama Jombi kwa umakini asimpoteze. Alipofika karibu na tageti yake akachomoa kisu chake, ila kabla hajafanya tukio, alishitukia mtu akimsukumiza tokea nyuma yake. Ulikuwa ni ugomvi wanaume wawili wakimgombea mwanamke.
Haraka mabaunsa walikuja kutuliza fujo. Mwanaume yule akarudisha kisu chake mfukoni upesi, akatoka na kurudi alipokuwa ameketi. Sasa aliwapoteza watu wake na hakujua wapi walipo. Alirusha macho yake huku na kule asione kitu. Alikunja sura. Alisaga meno kwa hasira. Aliminya kopo la kinywaji chake akakitupia chini.
Alitoka ndani akaenda nje, huko akawa anangoja walengwa wake watoke apate kuwashughulikia.
Haukupita muda mrefu, akawaona wanatoka wakicheka na kulonga. Taratibu akaanza kuwasogelea.
Kosa alilofanya ni kutopiga mahesabu. Walengwa wake walikuwa wanne badala ya watano. Kuna mmoja hakuwepo na hakujua wapi alipo.
Wakati akijongea kusogea zaidi alisikia mkono begani. Aligeuka akakutana uso kwa uso na ngumi moja nzito iliyompeleka chini kama mbuyu. Alinyanyuka upesi apambane ila akarudishwa chini na teke liliofyatukia hewani likimtengua taya na kumwacha hoi.
“Bado unataka tena?” Kaguta alimuuliza mwanaume yule aliyekuwa chini hajiwezi. Punde wakina Miraji na baadhi ya watu wengine wakajongea karibu.
Kabla hawajafanya lolote, mwanaume yule alijichoma kisu shingoni akafa.

****

“Kwahiyo hamkupata chochote toka kwake?” Vitalis aliuliza akimtizama Kaguta.
“Hatujapata kitu kutoka mdomoni mwake … zaidi alikuwa ana mchoro wa simba mgongoni.”
“Ina mana tayari hili kundi la simba limeshaanza kutufuatilia.” Alisema Bakari. “Inashangaza ni kwa namna gani wanapata taarifa zetu.”
Kaguta alinyanyua kikombe cha maji akanywa. Alizungusha macho yake kuwatizama wenzake wote waliokuwepo mezani kisha akashusha pumzi ndefu. Wote walimtizama kana kwamba wanategemea atie neno.
“Inabidi tuongeze umakini.” Alisema Kaguta akinyanyuka. Alitoka ndani akivua shati akaelekea baharini.
“Ok. Tutaendela kujadili baadae.” Vitalis aliwatawanyisha wenzake. Kila mmoja alitoka akaenda upande wake wakimuacha Vitalis na Bernadetha ndani peke yao.
“Sasa tunafanya nini, Vitalis?” Bernadetha aliuliza kwa sauti taratibu. Aligeuza shingo yake nyembamba akamtizama Vitalis aliyekuwa anawaza na kuwazua.
“Bado sijajua kwa sasa.” Vitalis alijibu. Aligeuza naye shingo yake akamtizama Bernadetha. Walitizamana machoni kwa dakika moja kana kwamba kuna vitu wanaona kwenye viini vyao vya macho. Walishituliwa na mtoto, Marietta, alipokuja akiwaita.
Vitalis alimkwapua Marietta akambeba mgongoni kwa furaha. Huku akimchezea mashavu mwana huyo akaenda naye nje baada ya kumuaga Bernadetha kwa kumkonyeza.
Mpaka jua lazama kuhitimisha hiyo siku hakuna lolote lililogundulikana isijalishe ni mara ngapi walijadili ama kwa muda gani Bakari alikaa karibu na tanakilishi yake kupembua na kuchambua.
Ngoma bado ilikuwa nzito …

***
Muscat, Oman.

Tangu karne ya kwanza jiji hili, Muscat, limekuwa ni jiji muhimu sana kama kitovu cha biashara kati ya ulimwengu wa mashariki na magharibi. Kwa mujibu wa historia kitambo huko nyuma, tunaelezwa ya kwamba waarabu hawa wa Oman walikuja mashariki ya Afrika wakaweka makazi yao katika mji wa Zanzibar wakiboresha mji huo kwa majengo na kuupa umilki wa dini ya kiislamu inayotawala mpaka sasa.
Uwepo wa mazao kama karafuu na majengo yenye asili ya mashariki ya mbali, uarabuni, yamesimama mpaka sasa kama kiashiria cha makazi ya watu hao hapo zamani.
Jiji la Muscat kwa kiasi kikubwa limetawaliwa na milima ya Al Hajar. Barabara na majengo yake yamezungukwa na milima hii ya wastani ambayo pia huwa ni kivutio cha utalii. Mbali na hapo ni mojawapo ya jiji lenye joto kubwa na pia vile vile kavu kama majiji mengi ya mashariki ya mbali, uarabuni, kwasababu ya ukosefu wa mvua za kutosha. Ila hilo si kigezo cha ukosefu wa maji katika jiji hilo, mabomba ya maji yametambaa kila kona yakimimina maji freshi masaa ishirini na manne.
Wageni wa jiji hili watumiao ndege, hupokelewa kwenye uwanja mkubwa wa ndege Muscat International Airport. Uwanja huo upo umbali wa kilometa takribani ishirini na tano kutoka kwenye wilaya ya biashara ndani ya jiji, Ruwi, huku uwanja huo ukiwa takribani kilometa kumi na tano mpaka kwenye makazi ya Sultan.
Jengo la Al Alam, makazi ya Sultan wa Oman, ni mojawapo ya jengo linalowavutia watali kwa muundo na muonekano wake wa kuvutia. Jengo hilo lililojengwa mwaka alfu tisa mia sabini na mbili ndilo ambalo limekuwa likisimama kama alama ya utawala wa Sultan, ambaye ni miongoni mwa viongozi walioshikilia madaraka kwa muda mrefu sana duniani.
Watumishi watano wa Kim Salvatore, wakivalia suti nadhifu, walishuka kwenye ndege kubwa Qatar Airways wakaongozana mpaka nje walipochukua taksi ikawapeleka moja kwa moja kwenye hoteli yenye hadhi ya nyota tatu.
Waliandikisha majina bandia hapo wakichukua vyumba viwili baada ya kukataliwa kurundikana kwenye chumba kimoja kwa mujibu wa idadi yao. Wakiwa ndani ya chumba kimoja walianza kupanga yale waliyodhamiria kuyafanya kama vile walivyoagizwa kutenda.
Wakiwa wana ramani ya jiji zima la Muscat, pamoja pia na ramani ya jengo la Al Alam, wakaanza kupanga wapi waingilie, wapi watokee, wapi wafanye hiki na wapi wafanye kile. Watatu walielekezana kwa maneno huku wale wenzao wawili, mabubu, wakielekezwa kwa ishara ya mikono. Ndani ya begi lao kubwa walitoa sura za bandia, shuka kubwa rangi ya dhahabu, tiketi za kurudi walipotoka pamoja na kifaa cha kukingia damu. Kifaa hicho kilikaa kama birika lakini lenye mdomo ulichongoka.
“Tutafanya kazi yetu ijumaa, yani kesho. Ni siku ambayo Sultan hutoka kwenda msikitini. Tutatumia nafasi hiyo kuingia ndani ya jengo lake kwakuwa ulinzi utakuwa hafifu. Na pale tu atakaporudi, tutatumia dakika ishirini tu kumaliza kazi yetu na kuondoka. Hatuna muda wa kupoteza!”
Walimaliza usiku wao kwa hayo maagano.

***


☆Steve
 
***SURA YA HAMSINI NA SABA***





(MSIMU WA 02)







Giza lilitwaa jiji la Hamilton ambalo ukiachana tu na umaarufu wake wa kuwa na fukwe za bahari zinazovutia basi utakutana na bandari yake asili inayofanya kazi usiku mchana. Meli za makampuni makubwa kama DryShips Inc, Frontline Limited na Dockwise zilikuwa zinapishana kuingia makaoni mwake.
Sauti za mawimbi ya bahari, upepo mwanana na milio ya mabasi makubwa ya abiria ambayo bado yalikuwa yanatoa huduma ndio hasa zilikuwa zinasikika zikitumia utulivu wa usiku kwa faidaze. Mbali na hapo labda sauti za watu wachache hapa na pale.
Ndani ya jengo jeupe la ghorofa kwenye uwanja mkubwa walisimama wanaume wapatao themanini kwa idadi. Walichanganyikana wanaume weusi na wazungu. Vifua vyao vilivyojengeka kimazoezi vilikuwa wazi wakivalia suruali nyeusi za jeans. Migongoni mwao walibebelea mchoro mkubwa wa kichwa cha simba.
Mbele ya wanaume hao kulikuwapo na kiti kikubwa kirefu chenye rangi ya dhahabu. Hakikuwa na mtu lakini wanaume wote walikuwa wanakitizama kana kwamba kuna mtu asiyeonekana amekaa hapo.
Kim alitokea mlango wa kushoto wa uwanja, akanyookea kitini na kuketi. Wanaume wote nao wakaketi kitako chini wakimtizama.
“Nimewaita hapa kwa dhumuni la kuwataarifu kazi iliyopo mbele yetu. Ndani ya siku nne zijazo tunatakiwa tutengeneza msiba mkubwa. Msiba wa kifalme. Msiba utakaotikisa vichwa vya habari.”
Kim alisema kwa kujiamini akikaza macho yake.
“Nitawateua wanaume watano miongoni mwenu. Wanaume hao wataenda Oman. Wataenda huko kwa dhumuni moja tu: kummaliza Sultan Absaedy Omar ama mwanawe yeyote wa kiume. Nataka damu zao hapa kwa gharama yoyote ile … kwa gharama yoyote! … Wanaume hao watakaofanikisha hilo, watazawadiwa maradufu kwa ushujaa na ufanisi wao.”
Kim alinyanyuka akaweka mikono yake nyuma. Alitembea akipita katikati ya mistari ya wanaume waliokuwa wamejipanga akiendelea kumwaga maneno.
“Hakuna nafasi ya kufanya makosa katika hili. Ni eidha kufa ama kupona. Ni eidha wao wafe ama sisi tufe. Hatujawahi kushindwa vita yoyote ile na hii siyo ya kwanza na wala haitakuwa ya mwisho. Nawaamini.”
Baada ya maneno hayo aliwateua wanaume watano kwa kuwagusa mabegani. Wanaume hao wakasimama na kwenda mbele, wengine wakasimama na kutokomea.
Katikati ya wanaume hao watano walioachaguliwa, walikuwepo pia wanaume wale wawili waliokuwa na Kim wakati anatizama televisheni, walijulikana kwa majina ya Panther na Jaguar.
Kim aliwatizama akawapa ishara huku wengine akiwaambia kwa maneno:
“Nimewachagua nyie kwasababu naamini kwa dhati mnaweza mkafanya hii kazi. Nataka damu ya kifalme ije hapa ndani ya siku tatu tu. Siku tatu! Nataka mkajadili na kupanga usiku huu. Kesho asubuhi mnieleze nini mnahitaji kukamilisha hili zoezi.”
Wanaume hao wakaondoka wakimuacha Kim mwenyewe ameketi kwenye kiti chake kikubwa. Alifikira kwa muda kisha akatabasamu akitikisa kichwa.
“Nadhani hili litakuwa kisasi kizuri dhidi ya yule mshenzi aliyeninyima fursa ya kuwekeza kwenye biashara yake ya mafuta … Sultan, nipo njiani nakuja. Ulinihukumu kwa uchotara wangu, mimi nitakuhukumu kwa ncha ya upanga.”

***

Bakari akiwa pamoja na Miraji walitizama kioo cha tanakilishi mpakato kilichokuwa kinaonesha michoro ya simba na alama za maji kwa makini kana kwamba wanatafutia suluhisho hesabu ngumu.
Bakari alitikisa kichwa chake akauliza:
“Sijui hii michoro ina maanisha nini?”
Ukimya ulikatiza kwa sekunde kabla Bakari hajaendelea kunena:
“Ina mana kuna watu wengine wenye hii michoro, sio?”
“Nadhani.” Miraji alijibu.
“Sasa tutawapataje hao watu? Au tutawangoja mpaka watushambulie?”
“Inabidi tuwagundue mapema. Tofauti na ilivyokuwa kwa kundi la nyoka, wenyewe walitutafuta. Hatujajua hawa wenye hii michoro watatutafuta ama tutawatafuta. Ila tutakuwa salama zaidi endapo tutawatafuta kabla wao hawajafanya hivyo.”
Vitalis na Kaguta waliingia wakaungana na wakina Bakari. Waliendeleza mjadala wakijaribu kufumbua fumbo ambalo lilikuwa gumu kufumbuliwa.
Marietta aliingilia mjadala huo akamuiba Vitalis. Alitaka akacheze naye fukweni kwani alimkumbuka sana tokea yupo shuleni bweni. Vitalis alishindwa kukataa. Alimnyanyua Marietta akamuweka begani wakaenda zao kuchezea maji ya fukweni.
Walirushiana maji wakikimbizana. Walioga michanga. Waliogelea wakishindana kukaa muda mrefu majini. Mwishowe walilala kwenye mchanga mlaini wa fukwe wakitizama jua la saa mbili asubuhi. Hapo Bernadetha akajitokeza na kujiunga nao baada ya kukaa muda mrefu pembeni akiwatizama pasipo wao kujua.
Macho yake yalikuwa mekundu akitabasamu. Kwa muda wakati anamtizama Vitalis akicheza na mwanae, Marietta, alimkumbuka mume wake, Malale. Kila mwisho wa juma walikuwa wanaenda ufukweni kama familia. Huko walicheza na kufurahia kisha wanarudi nyumbani jua likizama.
“Karibu!” Vitalis alimkaribisha Bernadetha.
“Ahsante.” Bernadetha alijibu akimtizama mwanae.
“Vipi, kuna tatizo?” Vitalis aliuliza.
“Hapana. Hamna tatizo!” Bernadetha alijibu akilazimisha tabasamu. Alimbeba mwanae akamuuliza:
“Mlikuwa mnafanya nini?”
“Tunacheza! … Nilikuwa nacheza na anko!” Marietta alijibu kwa maajivuno.
“Alafu mama, nimemuambia anko anifundishe ngumi!”
“Ngumi?” Bernadetha alitabasamu. “Nani kakuambia anko anapigana ngumi?”
“Nilimuona! … siku moja nilimuona akipigana na anko Kaguta.”
Baada ya kucheka, Bernadetha akauliza:
“Wewe unataka ukampige nani?”
“Kule shuleni kuna mijitu migomvi!” Marietta alijibu. “Nataka niwapige mpaka wakome!”
Wote walicheka wakaondoka kurudi kwenye makazi yao.
Siku hiyo ilikuwa ni ya kupumzika. Hakuna kazi waliyofanya zaidi ya kupika na kula kisha kufurahia mandhari ya bahari. Waliogelea, walicheza mpira mpaka jua linatuama.
Kaguta akiwa pamoja na Sandra, Miraji, Jombi na Bakari waliaga wanatoka kwenda kujirusha nje ya kisiwa. Waliahidi kurudi siku inayofuata mapema, wanahitaji kupumzisha na kubadilisha mazingira mara moja.
Baada ya mvutano wa hapa na pale, walikubaliana waende.
“Kuweni makini.” Bernadetha aliwahasa.
“Usihofu. Wapo na mimi.” Kaguta akajibu akijinyooshea kidole.
Walitumia boti yao ndogo wakakata maji kwenda jiji la Dar, wakawaacha Bernadetha, Vitalis na Marietta kisiwani.
Haukupita muda mrefu baada ya kula chakula cha usiku, Marietta akapitiwa na usingizi. Vitalis alimbeba akampeleka chumbani alipomlaza na kumfunika na shuka.
Alirudi sebuleni akamkuta Berbadetha ametulia akijikunyata. Alikuwa anafikiria jambo ambalo halikuchukua muda mrefu akamshirikisha Vitalis:
“Samahani, Vitalis. Kuna muda naona picha ya mume wangu pale ninapokutizama. Sijui kwanini inakuwa hivyo. Haijalishi mara ngapi najitahidi kujizuia lakini haisaidii katu.”
Bernadetha aliweka kituo akitizama chini, mara chozi likaanza kumshuka.
“Leo wakati nakuona na mwanangu nili …”
“Sshh! …” Vitalis alimkatiza. Alimfuta chozi akamnyanyua uso.
“Usihofu. Haina haja ya kuomba samahani, Bernadetha. Naelewa. Naelewa unachojihisi … kuna mambo yakupasa uyaache yaende ili upate amani moyoni.”
Vitalis alimbusu Bernadetha shavuni kisha akambeba akimlaza mikononi mwake.
“Nataka uwe na furaha. Sipendi kukuona ukifadhaika.”
Bernadetha alipeleka mdomo wake kwa Vitalis wakanyonyana ndimi. Walielekea chumbani wakazima taa.

****


☆Steve
Daaah kwa nini wadhime taa lkn ,eti wajameni..!!??
Good job mkuu ,hata wakina Dan Brown walianza kama hv
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom