SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,803
- 25,444
- Thread starter
- #621
***SURA YA AROBAINI NA TISA***
(MSIMU WA 02)
Mahali hapo kabla hapajageuka jehanamu ndogo palikuwa ni mali ya bwana Msolasa aliyetumia eneo hilo kama kiwanda cha tumbaku. Tamaa yake ya pesa ilimpelekea akauza eneo hilo kwa mwanaume mmoja mwenye asili ya Amerika ya kusini, Emilio Diego, kwa shilingi milioni mia tisa. Kabla ya pesa hiyo kutumiwa hata thumni, Msolasa akavamiwa na watu wasiojulikana wakamnyonga na kumtupia baharini pesa yote ikikombwa na kurudi mkononi mwa Emilio. Japokuwa kifo cha Msolasa kiliteka vyombo vya habari, hakuna lolote lililofanywa na polisi zaidi tu ya ahadi lukuki ambazo ziliishia kutotekelezwa. Sasa habari yake ilikuwa ni tungo ambayo ilipeperushwa na upepo, hakuna tena aliyemkumbuka bwana huyo isipokuwa familia yake iliyoachwa na ukata mkali, mjane na watoto wakibangaiza.
“Kabla hatujaenda inabidi tufahamu hilo eneo vizuri.” Jombi alitoa angalizo.
“Ni eneo ambalo limejitenga mbali na barabara. Hakuna jengo lingine lolote lililo karibu yake kwa kilomita si chini ya kumi ukiwa unatokea Dar, na kumi na tano ikiwa unaelekea mbele na barabara hiyo kuu.” Sandra alieleza.
“Kwahiyo Sandra, unataka kunambia haujui lolote juu ya yale yanayoendelea ndani ya jengo hilo japokuwa wote mpo chini ya Kim?” Miraji aliuliza.
“Kama alivyosema Bakari, huwezi jua yale yanayoendeshwa na makundi mengine isipokuwa tu la kwako. Kila kundi lina viongozi, miiko na taratibu zake japokuwa viongozi wote huwa wanakutana mara mbili kwa mwaka kuelezeana mafanikio na changamoto zao.” Sandra alitoa maelezo.
“Sasa unaweza ukatupa maelezo kidogo juu ya hilo eneo ili tupate kufahamu pa kuanzia?” Jombi aliuliza, mara hii Bakari akadakia:
“Tutatumia Google map kusoma hilo eneo. Nadhani ni njia nzuri zaidi ya kufahamu eneo lolote kinaga ubaga.”
Hilo halikuhitaji mzozo likapita. Walimuacha Bakari acheze na mashine yake kwa dakika kadhaa kisha akawapa jibu:
“Kuna njia tunaweza kutumia pasipo kugundulika kwa wepesi.”
****
Kulikuwa ni giza totoro hakuna kilichokuwa kinaonekana kwa macho ya kawaida. Ndani ya giza hilo kulikuwa kukisikika pumzi za watu zikihema taratibu mara zingine zikikatizwa na kwikwi. Kwa muda kidogo sauti ikanong’oneza:
“Kagutaa … Kagutaa.”
Hakukuwa na jibu. Ni giza kali tu ndilo lilijibu. Sauti ile ya kunong’oneza haikukata tamaa, ikaita tena:
“Kagutaa … Kagutaa.”
Kimya.
Mara mtu akaguna kama aliyezidiwa.
“Kaguta, upo sawa?” Sauti ya kunong’oneza iliwahi kuuliza baada tu ya kusikia mguno. Akajibiwa tena na mguno.
“Upo sawa? … Enh? … Kaguta?”
Hakuna jibu lolote zaidi tu ya mguno.
Mara taa zikawashwa ghafula, kiza chote kikapotea kufumba na kufumbua. Palikuwa peupe peh mithili ya mchana wa jua la utosi. Kaguta na Vitalis walikuwa wamekalishwa kwenye viti wakiwa wamefungwa mikono, miguu, kichwa na kiuno kwa kamba nene. Nyuso zao zilikuwa hazitamaniki kwa majeraha na kuvimba vimba. Midomo na pua ilikuwa inachuruza damu huku wakionekana kuchoka mno hasa Kaguta ambaye alikuwa amefumba macho na mdomo wake ukiwa wazi kama mtu aliye jangwani akibanwa na kiu kikali mno hamna hata tone la maji ya kunywa. Nguo zilikuwa zimechanwa chanwa hazitamaniki, hazikufaa tena kuitwa nguo bali matambara.
Wanaume watatu waliovalia suti nyeusi walionekana punde baada ya taa kuwaka wakiwa wamekaa kwenye viti virefu kidogo vilivyokuwa vinawatizama mateka wao. Kabla ya kunyanyuka na kuwasogelea mateka walitizamana alafu wote wakanyanyuka na kutembea taratibu mpaka karibu kabisa na Vitalis ambaye aliwapokea kwa macho ya kifedhuli. Hawakujali, badala yake walitabasamu mmoja akauliza:
“Unadhani mwenzako anaweza kuongea baada ya kile kipigo kitakatifu alichokula?”
Wote wakacheka kana kwamba wanatizama futuhi. Kwao kuua ilikuwa ni kama kunawa mikono – kitu wanachoweza kufanya bila ya kujifikiria mara mbili. Mmoja wao alikuwa mrefu zaidi mwenye uso wenye kovu la kisu pembeni kidogo ya sikio, mwingine alikuwa ana kipara kichwani kwake akiwa ana kumbukumbu kubwa ya alama ya mkato wa kitu cha ncha kali. Wa mwisho yeye alikuwa na mdomo wenye kovu la jeraha lililokula nyuzi za kutosha upande wake wa kulia – alishawahi kuchanwa mdomo, haliitaji akili nyingi kugundua hilo.
“Sasa mpo tayari kutuambia nani anawafadhili ama tuendelee kuwashibisha kipigo?” Alinguruma mwanaume mwenye kovu la kisu pembeni ya sikio. Hakuonyesha anatania bali anayemaanisha kile anachokisema. Uso wake ulikuwa unatisha haswa, kama ana mke ama mpenzi basi bila shaka atakuwa ni miongoni mwa wa wanawake wenye uvumilivu wa hali ya juu.
Vitalis alimtizama mwanaume huyo kwa macho yake yaliyovimba na kuchuruza damu akamwambia kibabe mdomo ukipinda kwa hasira na kebehi:
“Muda utakaoingia mikononi mwangu, ndio utakuwa muda wako wa mwisho juu ya uso wa dunia. Sitabakiza mfupa wako wowote mzima. Nitahakikisha hata mama yako mzazi hawezi kukutambua hata!”
Akamtemea mate yake ya damu usoni mwa mwanaume aliyemuuliza, mwanaume huyo akajipangusa huku akitabasamu.
“Naona somo halijakuingia kijana. Wacha nikufundishe kile ambacho mama yako ameshindwa.”
Alituma ngumi yake nzito kwenye uso wa Vitalis damu zikaruka kama maji yanayotoka kwa kasi bombani. Alimpiga Vitalis ngumi tano za tumbo, Vitalis akatapika damu huku puani nako kukichuruza. Kabla hajaendelea kushambulia, wenzake walimkamata na kumtaka aache, inatosha.
“Utamuua sasa. Si unajua mkuu anamtaka akiwa hai?” Mwanaume mwenye kovu kichwani alitahadharisha. Mwenzao akajibandua toka kwenye mikono yao kwanguvu.
“Hawezi akaniletea dharau za kijinga nikabaki namtizama!”
“Sasa ukimuua je, unadhani utamwambia nini mkuu?” Mwanaume mwenye kovu la kichwa aliendelea kunena huku mwenzake mwenye kovu la mdomo akitikisa tu kichwa.
“Mkuu! Mkuu naye mpumbavu tu. Aliwaamini sana wale triple badala yangu, mbona wamekufa sasa? Wako wapi sasa? Na anawatakia nini hawa mbwa wakiwa hai wakati tayari wameshaua triple power yake? Mkuu mwenyewe sasa hivi anaishi chini ya kivuli vya wenzake ambao bado wana power zao. *** off!”
“Unamaanisha nini kusema hivyo jembe?”
Kabla hajajibu aligeuka kwanza kumtizama Vitalis akamuona hajielewi mdono wazi anachuruza tu madamu.
“Kwani nyie hamjui kama triple yake imeshakufa? … Maana yake Emilio atalamba miguu ya Cruz na Santanna.” Alipomaliza kusema hivyo walisikia kelele kali ya mtu akilalamikia maumivu. Walitizamana, mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio akatoa ishara, mmoja akabakia na wakina Vitalis, wawili: mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio na kichwani, wakagawana muelekeo – kulia na kushoto. Baada ya muda wakajikuta wapo nje ya jengo upande wa kushoto sauti ilipokuwa inatokea, walikuwa wanaume wawili mmoja akiwa kamlalia mwenzake kwa juu, mwanaume wa chini akiwa analia kwa sauti ya maumivu. Mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio akajongea kwa tahadhari akamsogeza mwanaume aliyekuwa juu ilia pate kumtizama alalamikaye. Ajabu akamkuta amekufa, alipomgusa mwili wake alihisi ubaridi mkali kuonyesha ya kwamba amekufa kwa kitambo kidogo. Alipotizama pembeni akaona kirekodi sauti na kumbe hicho ndio kilikuwa kinapiga kelele kwa muda wote huo.
“Pumbavu!” Mwanaume amwenye kovu pembeni ya sikio alilalamika. “Bode tumevamiwa. Bonyeza alarm washtue wote!”
***
☆Steve
(MSIMU WA 02)
Mahali hapo kabla hapajageuka jehanamu ndogo palikuwa ni mali ya bwana Msolasa aliyetumia eneo hilo kama kiwanda cha tumbaku. Tamaa yake ya pesa ilimpelekea akauza eneo hilo kwa mwanaume mmoja mwenye asili ya Amerika ya kusini, Emilio Diego, kwa shilingi milioni mia tisa. Kabla ya pesa hiyo kutumiwa hata thumni, Msolasa akavamiwa na watu wasiojulikana wakamnyonga na kumtupia baharini pesa yote ikikombwa na kurudi mkononi mwa Emilio. Japokuwa kifo cha Msolasa kiliteka vyombo vya habari, hakuna lolote lililofanywa na polisi zaidi tu ya ahadi lukuki ambazo ziliishia kutotekelezwa. Sasa habari yake ilikuwa ni tungo ambayo ilipeperushwa na upepo, hakuna tena aliyemkumbuka bwana huyo isipokuwa familia yake iliyoachwa na ukata mkali, mjane na watoto wakibangaiza.
“Kabla hatujaenda inabidi tufahamu hilo eneo vizuri.” Jombi alitoa angalizo.
“Ni eneo ambalo limejitenga mbali na barabara. Hakuna jengo lingine lolote lililo karibu yake kwa kilomita si chini ya kumi ukiwa unatokea Dar, na kumi na tano ikiwa unaelekea mbele na barabara hiyo kuu.” Sandra alieleza.
“Kwahiyo Sandra, unataka kunambia haujui lolote juu ya yale yanayoendelea ndani ya jengo hilo japokuwa wote mpo chini ya Kim?” Miraji aliuliza.
“Kama alivyosema Bakari, huwezi jua yale yanayoendeshwa na makundi mengine isipokuwa tu la kwako. Kila kundi lina viongozi, miiko na taratibu zake japokuwa viongozi wote huwa wanakutana mara mbili kwa mwaka kuelezeana mafanikio na changamoto zao.” Sandra alitoa maelezo.
“Sasa unaweza ukatupa maelezo kidogo juu ya hilo eneo ili tupate kufahamu pa kuanzia?” Jombi aliuliza, mara hii Bakari akadakia:
“Tutatumia Google map kusoma hilo eneo. Nadhani ni njia nzuri zaidi ya kufahamu eneo lolote kinaga ubaga.”
Hilo halikuhitaji mzozo likapita. Walimuacha Bakari acheze na mashine yake kwa dakika kadhaa kisha akawapa jibu:
“Kuna njia tunaweza kutumia pasipo kugundulika kwa wepesi.”
****
Kulikuwa ni giza totoro hakuna kilichokuwa kinaonekana kwa macho ya kawaida. Ndani ya giza hilo kulikuwa kukisikika pumzi za watu zikihema taratibu mara zingine zikikatizwa na kwikwi. Kwa muda kidogo sauti ikanong’oneza:
“Kagutaa … Kagutaa.”
Hakukuwa na jibu. Ni giza kali tu ndilo lilijibu. Sauti ile ya kunong’oneza haikukata tamaa, ikaita tena:
“Kagutaa … Kagutaa.”
Kimya.
Mara mtu akaguna kama aliyezidiwa.
“Kaguta, upo sawa?” Sauti ya kunong’oneza iliwahi kuuliza baada tu ya kusikia mguno. Akajibiwa tena na mguno.
“Upo sawa? … Enh? … Kaguta?”
Hakuna jibu lolote zaidi tu ya mguno.
Mara taa zikawashwa ghafula, kiza chote kikapotea kufumba na kufumbua. Palikuwa peupe peh mithili ya mchana wa jua la utosi. Kaguta na Vitalis walikuwa wamekalishwa kwenye viti wakiwa wamefungwa mikono, miguu, kichwa na kiuno kwa kamba nene. Nyuso zao zilikuwa hazitamaniki kwa majeraha na kuvimba vimba. Midomo na pua ilikuwa inachuruza damu huku wakionekana kuchoka mno hasa Kaguta ambaye alikuwa amefumba macho na mdomo wake ukiwa wazi kama mtu aliye jangwani akibanwa na kiu kikali mno hamna hata tone la maji ya kunywa. Nguo zilikuwa zimechanwa chanwa hazitamaniki, hazikufaa tena kuitwa nguo bali matambara.
Wanaume watatu waliovalia suti nyeusi walionekana punde baada ya taa kuwaka wakiwa wamekaa kwenye viti virefu kidogo vilivyokuwa vinawatizama mateka wao. Kabla ya kunyanyuka na kuwasogelea mateka walitizamana alafu wote wakanyanyuka na kutembea taratibu mpaka karibu kabisa na Vitalis ambaye aliwapokea kwa macho ya kifedhuli. Hawakujali, badala yake walitabasamu mmoja akauliza:
“Unadhani mwenzako anaweza kuongea baada ya kile kipigo kitakatifu alichokula?”
Wote wakacheka kana kwamba wanatizama futuhi. Kwao kuua ilikuwa ni kama kunawa mikono – kitu wanachoweza kufanya bila ya kujifikiria mara mbili. Mmoja wao alikuwa mrefu zaidi mwenye uso wenye kovu la kisu pembeni kidogo ya sikio, mwingine alikuwa ana kipara kichwani kwake akiwa ana kumbukumbu kubwa ya alama ya mkato wa kitu cha ncha kali. Wa mwisho yeye alikuwa na mdomo wenye kovu la jeraha lililokula nyuzi za kutosha upande wake wa kulia – alishawahi kuchanwa mdomo, haliitaji akili nyingi kugundua hilo.
“Sasa mpo tayari kutuambia nani anawafadhili ama tuendelee kuwashibisha kipigo?” Alinguruma mwanaume mwenye kovu la kisu pembeni ya sikio. Hakuonyesha anatania bali anayemaanisha kile anachokisema. Uso wake ulikuwa unatisha haswa, kama ana mke ama mpenzi basi bila shaka atakuwa ni miongoni mwa wa wanawake wenye uvumilivu wa hali ya juu.
Vitalis alimtizama mwanaume huyo kwa macho yake yaliyovimba na kuchuruza damu akamwambia kibabe mdomo ukipinda kwa hasira na kebehi:
“Muda utakaoingia mikononi mwangu, ndio utakuwa muda wako wa mwisho juu ya uso wa dunia. Sitabakiza mfupa wako wowote mzima. Nitahakikisha hata mama yako mzazi hawezi kukutambua hata!”
Akamtemea mate yake ya damu usoni mwa mwanaume aliyemuuliza, mwanaume huyo akajipangusa huku akitabasamu.
“Naona somo halijakuingia kijana. Wacha nikufundishe kile ambacho mama yako ameshindwa.”
Alituma ngumi yake nzito kwenye uso wa Vitalis damu zikaruka kama maji yanayotoka kwa kasi bombani. Alimpiga Vitalis ngumi tano za tumbo, Vitalis akatapika damu huku puani nako kukichuruza. Kabla hajaendelea kushambulia, wenzake walimkamata na kumtaka aache, inatosha.
“Utamuua sasa. Si unajua mkuu anamtaka akiwa hai?” Mwanaume mwenye kovu kichwani alitahadharisha. Mwenzao akajibandua toka kwenye mikono yao kwanguvu.
“Hawezi akaniletea dharau za kijinga nikabaki namtizama!”
“Sasa ukimuua je, unadhani utamwambia nini mkuu?” Mwanaume mwenye kovu la kichwa aliendelea kunena huku mwenzake mwenye kovu la mdomo akitikisa tu kichwa.
“Mkuu! Mkuu naye mpumbavu tu. Aliwaamini sana wale triple badala yangu, mbona wamekufa sasa? Wako wapi sasa? Na anawatakia nini hawa mbwa wakiwa hai wakati tayari wameshaua triple power yake? Mkuu mwenyewe sasa hivi anaishi chini ya kivuli vya wenzake ambao bado wana power zao. *** off!”
“Unamaanisha nini kusema hivyo jembe?”
Kabla hajajibu aligeuka kwanza kumtizama Vitalis akamuona hajielewi mdono wazi anachuruza tu madamu.
“Kwani nyie hamjui kama triple yake imeshakufa? … Maana yake Emilio atalamba miguu ya Cruz na Santanna.” Alipomaliza kusema hivyo walisikia kelele kali ya mtu akilalamikia maumivu. Walitizamana, mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio akatoa ishara, mmoja akabakia na wakina Vitalis, wawili: mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio na kichwani, wakagawana muelekeo – kulia na kushoto. Baada ya muda wakajikuta wapo nje ya jengo upande wa kushoto sauti ilipokuwa inatokea, walikuwa wanaume wawili mmoja akiwa kamlalia mwenzake kwa juu, mwanaume wa chini akiwa analia kwa sauti ya maumivu. Mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio akajongea kwa tahadhari akamsogeza mwanaume aliyekuwa juu ilia pate kumtizama alalamikaye. Ajabu akamkuta amekufa, alipomgusa mwili wake alihisi ubaridi mkali kuonyesha ya kwamba amekufa kwa kitambo kidogo. Alipotizama pembeni akaona kirekodi sauti na kumbe hicho ndio kilikuwa kinapiga kelele kwa muda wote huo.
“Pumbavu!” Mwanaume amwenye kovu pembeni ya sikio alilalamika. “Bode tumevamiwa. Bonyeza alarm washtue wote!”
***
☆Steve