Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

***SURA YA AROBAINI NA TISA***



(MSIMU WA 02)






Mahali hapo kabla hapajageuka jehanamu ndogo palikuwa ni mali ya bwana Msolasa aliyetumia eneo hilo kama kiwanda cha tumbaku. Tamaa yake ya pesa ilimpelekea akauza eneo hilo kwa mwanaume mmoja mwenye asili ya Amerika ya kusini, Emilio Diego, kwa shilingi milioni mia tisa. Kabla ya pesa hiyo kutumiwa hata thumni, Msolasa akavamiwa na watu wasiojulikana wakamnyonga na kumtupia baharini pesa yote ikikombwa na kurudi mkononi mwa Emilio. Japokuwa kifo cha Msolasa kiliteka vyombo vya habari, hakuna lolote lililofanywa na polisi zaidi tu ya ahadi lukuki ambazo ziliishia kutotekelezwa. Sasa habari yake ilikuwa ni tungo ambayo ilipeperushwa na upepo, hakuna tena aliyemkumbuka bwana huyo isipokuwa familia yake iliyoachwa na ukata mkali, mjane na watoto wakibangaiza.
“Kabla hatujaenda inabidi tufahamu hilo eneo vizuri.” Jombi alitoa angalizo.
“Ni eneo ambalo limejitenga mbali na barabara. Hakuna jengo lingine lolote lililo karibu yake kwa kilomita si chini ya kumi ukiwa unatokea Dar, na kumi na tano ikiwa unaelekea mbele na barabara hiyo kuu.” Sandra alieleza.
“Kwahiyo Sandra, unataka kunambia haujui lolote juu ya yale yanayoendelea ndani ya jengo hilo japokuwa wote mpo chini ya Kim?” Miraji aliuliza.
“Kama alivyosema Bakari, huwezi jua yale yanayoendeshwa na makundi mengine isipokuwa tu la kwako. Kila kundi lina viongozi, miiko na taratibu zake japokuwa viongozi wote huwa wanakutana mara mbili kwa mwaka kuelezeana mafanikio na changamoto zao.” Sandra alitoa maelezo.
“Sasa unaweza ukatupa maelezo kidogo juu ya hilo eneo ili tupate kufahamu pa kuanzia?” Jombi aliuliza, mara hii Bakari akadakia:
“Tutatumia Google map kusoma hilo eneo. Nadhani ni njia nzuri zaidi ya kufahamu eneo lolote kinaga ubaga.”
Hilo halikuhitaji mzozo likapita. Walimuacha Bakari acheze na mashine yake kwa dakika kadhaa kisha akawapa jibu:
“Kuna njia tunaweza kutumia pasipo kugundulika kwa wepesi.”

****

Kulikuwa ni giza totoro hakuna kilichokuwa kinaonekana kwa macho ya kawaida. Ndani ya giza hilo kulikuwa kukisikika pumzi za watu zikihema taratibu mara zingine zikikatizwa na kwikwi. Kwa muda kidogo sauti ikanong’oneza:
“Kagutaa … Kagutaa.”
Hakukuwa na jibu. Ni giza kali tu ndilo lilijibu. Sauti ile ya kunong’oneza haikukata tamaa, ikaita tena:
“Kagutaa … Kagutaa.”
Kimya.
Mara mtu akaguna kama aliyezidiwa.
“Kaguta, upo sawa?” Sauti ya kunong’oneza iliwahi kuuliza baada tu ya kusikia mguno. Akajibiwa tena na mguno.
“Upo sawa? … Enh? … Kaguta?”
Hakuna jibu lolote zaidi tu ya mguno.
Mara taa zikawashwa ghafula, kiza chote kikapotea kufumba na kufumbua. Palikuwa peupe peh mithili ya mchana wa jua la utosi. Kaguta na Vitalis walikuwa wamekalishwa kwenye viti wakiwa wamefungwa mikono, miguu, kichwa na kiuno kwa kamba nene. Nyuso zao zilikuwa hazitamaniki kwa majeraha na kuvimba vimba. Midomo na pua ilikuwa inachuruza damu huku wakionekana kuchoka mno hasa Kaguta ambaye alikuwa amefumba macho na mdomo wake ukiwa wazi kama mtu aliye jangwani akibanwa na kiu kikali mno hamna hata tone la maji ya kunywa. Nguo zilikuwa zimechanwa chanwa hazitamaniki, hazikufaa tena kuitwa nguo bali matambara.
Wanaume watatu waliovalia suti nyeusi walionekana punde baada ya taa kuwaka wakiwa wamekaa kwenye viti virefu kidogo vilivyokuwa vinawatizama mateka wao. Kabla ya kunyanyuka na kuwasogelea mateka walitizamana alafu wote wakanyanyuka na kutembea taratibu mpaka karibu kabisa na Vitalis ambaye aliwapokea kwa macho ya kifedhuli. Hawakujali, badala yake walitabasamu mmoja akauliza:
“Unadhani mwenzako anaweza kuongea baada ya kile kipigo kitakatifu alichokula?”
Wote wakacheka kana kwamba wanatizama futuhi. Kwao kuua ilikuwa ni kama kunawa mikono – kitu wanachoweza kufanya bila ya kujifikiria mara mbili. Mmoja wao alikuwa mrefu zaidi mwenye uso wenye kovu la kisu pembeni kidogo ya sikio, mwingine alikuwa ana kipara kichwani kwake akiwa ana kumbukumbu kubwa ya alama ya mkato wa kitu cha ncha kali. Wa mwisho yeye alikuwa na mdomo wenye kovu la jeraha lililokula nyuzi za kutosha upande wake wa kulia – alishawahi kuchanwa mdomo, haliitaji akili nyingi kugundua hilo.
“Sasa mpo tayari kutuambia nani anawafadhili ama tuendelee kuwashibisha kipigo?” Alinguruma mwanaume mwenye kovu la kisu pembeni ya sikio. Hakuonyesha anatania bali anayemaanisha kile anachokisema. Uso wake ulikuwa unatisha haswa, kama ana mke ama mpenzi basi bila shaka atakuwa ni miongoni mwa wa wanawake wenye uvumilivu wa hali ya juu.
Vitalis alimtizama mwanaume huyo kwa macho yake yaliyovimba na kuchuruza damu akamwambia kibabe mdomo ukipinda kwa hasira na kebehi:
“Muda utakaoingia mikononi mwangu, ndio utakuwa muda wako wa mwisho juu ya uso wa dunia. Sitabakiza mfupa wako wowote mzima. Nitahakikisha hata mama yako mzazi hawezi kukutambua hata!”
Akamtemea mate yake ya damu usoni mwa mwanaume aliyemuuliza, mwanaume huyo akajipangusa huku akitabasamu.
“Naona somo halijakuingia kijana. Wacha nikufundishe kile ambacho mama yako ameshindwa.”
Alituma ngumi yake nzito kwenye uso wa Vitalis damu zikaruka kama maji yanayotoka kwa kasi bombani. Alimpiga Vitalis ngumi tano za tumbo, Vitalis akatapika damu huku puani nako kukichuruza. Kabla hajaendelea kushambulia, wenzake walimkamata na kumtaka aache, inatosha.
“Utamuua sasa. Si unajua mkuu anamtaka akiwa hai?” Mwanaume mwenye kovu kichwani alitahadharisha. Mwenzao akajibandua toka kwenye mikono yao kwanguvu.
“Hawezi akaniletea dharau za kijinga nikabaki namtizama!”
“Sasa ukimuua je, unadhani utamwambia nini mkuu?” Mwanaume mwenye kovu la kichwa aliendelea kunena huku mwenzake mwenye kovu la mdomo akitikisa tu kichwa.
“Mkuu! Mkuu naye mpumbavu tu. Aliwaamini sana wale triple badala yangu, mbona wamekufa sasa? Wako wapi sasa? Na anawatakia nini hawa mbwa wakiwa hai wakati tayari wameshaua triple power yake? Mkuu mwenyewe sasa hivi anaishi chini ya kivuli vya wenzake ambao bado wana power zao. *** off!”
“Unamaanisha nini kusema hivyo jembe?”
Kabla hajajibu aligeuka kwanza kumtizama Vitalis akamuona hajielewi mdono wazi anachuruza tu madamu.
“Kwani nyie hamjui kama triple yake imeshakufa? … Maana yake Emilio atalamba miguu ya Cruz na Santanna.” Alipomaliza kusema hivyo walisikia kelele kali ya mtu akilalamikia maumivu. Walitizamana, mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio akatoa ishara, mmoja akabakia na wakina Vitalis, wawili: mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio na kichwani, wakagawana muelekeo – kulia na kushoto. Baada ya muda wakajikuta wapo nje ya jengo upande wa kushoto sauti ilipokuwa inatokea, walikuwa wanaume wawili mmoja akiwa kamlalia mwenzake kwa juu, mwanaume wa chini akiwa analia kwa sauti ya maumivu. Mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio akajongea kwa tahadhari akamsogeza mwanaume aliyekuwa juu ilia pate kumtizama alalamikaye. Ajabu akamkuta amekufa, alipomgusa mwili wake alihisi ubaridi mkali kuonyesha ya kwamba amekufa kwa kitambo kidogo. Alipotizama pembeni akaona kirekodi sauti na kumbe hicho ndio kilikuwa kinapiga kelele kwa muda wote huo.
“Pumbavu!” Mwanaume amwenye kovu pembeni ya sikio alilalamika. “Bode tumevamiwa. Bonyeza alarm washtue wote!”


***

☆Steve
 
***SURA YA HAMSINI***




(MSIMU WA 02)







Kabla amri haijatimizwa wakasikia sauti ya mtu mwingine anapiga kelele. Mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio akaropoka:
“Huyo sio Gongo!”
“Ndiye yeye! Wavamizi watakuwa wanawaokoa mateka. Twende haraka!”
Jengo lao lilikuwa limegawanywa katika vipengele vikubwa vitatu kila kipengele kikiwa kimekaa mbali kidogo na chenzake na kutenganishwa na kuta pana refu. Kipengele cha kwanza kilikuwa ni kwa ajili ya mateso kwa mateka. Cha pili ambacho kilikuwa kikubwa kuliko vyote, ni kwa ajili ya kuchanganyia mabaki ya binadamu na makemikali, watu wa hapo walikuwa wanavaa makoti meupe marefu, wanabana nywele zao na kofia na kuziba midomo na pua zao kwa vinyago. Kipengele cha tatu kilikuwa cha uhifadhi wa mifuko ya mbolea ambazo tayari zilikuwa zimeshamalizika. Kile kipengele kilikuwa kina ulinzi wake ila kwa nje pia kulikuwa na ulinzi wa jengo zima kwa pamoja. Walinzi wote hao wa nje pamoja na wa kipengele cha mateso walikuwa wameshauwawa, walikuwa chini wakimiminika damu sehemu kadha wa kadha za miili yao. Ila ajabu ni kwamba hakuna yeyote aliyekuwa ndani aliyefahamu kwamba wamevamiwa. Tendo hilo lilifanyika kwa ukimya mno na utaalamu wa hali ya juu huku silaha zilizotumika zikiwa ni visu na kamba ambazo ziling’ang’ania shingo za walinzi na kuwaacha wakiwa wafu. Wavamizi walitembea kwa tahadhari na walionekana wanalijua jengo hilo vyema wakifahamu waingilie na kutokea wapi.
“Bonyeza alarm. Harakaaa!” Mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio alifoka baada ya kuona mateka wote hawapo, juu ya kiti kimoja akiwa amekaa mwenzao waliyemuacha awatizame meteka, damu zikiwa zinammiminika shingoni toka kwenye matundu mawili ya kisu. Wavamizi walitumia mlango huo huo ambao ulitumiwa na wanaume wale wawili baada ya kuuacha wazi wakifuata sauti.
Alarm ilibonyezwa sauti kubwa ikalia na kuwakusanya wanaume wote waliokuwepo hai ndani ya jengo. Walikuwa wanaume thelathini na saba kwa idadi. Miili yao ilikuwa mikubwa na wenye sura mbaya, wote walikuwa wamevalia suti nyeusi na tai nyembamba nyekundu. Mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio alisimama mbele yao akafoka:
“Kuna watu wamevamia ngome na kuwaokoa mateka. Najua hawajafika mbali, nawataka hapa ndani ya dakika tano tu!”
Wanaume wale walitapakaa kila upande kusaka.
***
Kaguta na Vitalis walikuwa wamebebelewa migongoni mwa wanaume wawili ambao walikuwa wamevalia kombati nyeusi wakiongozana na wanawake wawili waliokuwa kama walinzi wa wale wanaume waliobebelea wenzao. Walikuwa wanatembea haraka haraka wakiacha jengo la BEAST umbali wa nusu ,maili moja nyuma yao wakielekea upande wa magharibi.
Majani yalikuwa marefu mno kiasi cha kuleta ugumu kutembea. Lakini kwa njia moja ikawasaidia wavamizi kujificha mara tu walipoona mwanga mkali wa kurunzi unataka kuwamuliza. Mwanga huo mkali ulikuwa unatoka kwenye kibanda ambacho kilikuwa kipo juu kabisa kwenye jengo la BEAST, humo alikuwepo mwanaume aliyekuwa ameshikilia kurunzi kubwa akilepeleka huku na huko kutafuta walengwa wao.
Baada ya muda mfupi wana-BEAST walimaliza kusaka, hawakuona mtu yeyote. Walirejea wakamwambia mkuu wao – mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio – kwamba hawajamuona mtu yeyote kote kabisa.
“Wapumbavu nyie! Mnashindwaje kuwakamata watu ndani ya eneo kubwa kama hili?”
Mwanaume huyo alichomoa bunduki yake kwenye koti akalenga vichwa viwili vya wenzake, wakafa papo hapo.
“Nendeni mkawatafute! Mkirudi hapa bila ya watu hao, nasambaratisha bongo zenu!”
Wanaume walisambaratika kwenda kusaka tena, pamoja nao sasa nyuma yao wakaongozana na mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio. Ndani ya dakika chache walifika eneo moja lenye shimo ambalo lilikuwa limefunika funikwa na nyasi. Waliingia ndani ya shimo hilo wakagundua ni njia ambayo ilienda kuchomoza kando kando mwa barabara kuu. Walichokuta ni alama tu za matairi kabla hazijapotelea kwenye uso mweusi wa lami.
“Nataka hawa mbwa wapatikane ndani ya masaa ishirini na nne! Nimesema nawataka hawa mbwa ndani ya masaa ishirini na nneeee!” Aliwaka mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio.
***
Sauti ya ndege pori zilimfanya Vitalis ashtuke toka kwenye usingizi mzito wa maumivu. Alikuwa amelala kwenye kitanda kidogo chembamba ndani ya nyumba ndogo iliyofumwa fumwa na miti ya mianzi. Aligeuza uso wake huku na huko akajaribu kunyanyuka, ila mara akasikia sauti ya Bernadetha ikimkataza kufanya hivyo. Bernadetha alitokea akiwa anatabasamu akaketi karibu yake.
“Unaendeleaje?”
Kabla Vitalis hajajibu, aliuliza:
“Kaguta yupo wapi?”
Bernadetha akamtoa hofu: “Amempumzika. Anaendelea vizuri.”
“Na hapa tupo wapi?”
“Kisiwa kando ya Mafia. Nyumbani si salama tena.”
Kichwa kilimuuma Vitalis akashindwa kuendelea. Alilaza kichwa chake kilichokuwa kimefungwa bandeji kwenye godoro na kufumba macho kupumzika.
Ilikuwa ni siku ya pili tangu watoroke kwenye jengo la BEAST. Ndani ya muda huo Vitalis na Kaguta walikuwa wanatafutwa kwa hali na mali ndani ya jiji kwa gharama yeyote ile. Nyumba ya Vitalis ilichomwa moto na kuteketezwa mpaka kuwa majivu baada ya msako kufanyika. Huku Marietta akinusurika kutekwa kwenye bweni la shule yao kabla ya kuokolewa na Miraji punde tu baada ya wana-BEAST kuwasili eneo hilo. Jiji halikuwa salama tena kwa WAGENI, ilikuwa ni kisiwani tu ambapo walikuwa wanaishi wenyewe wakiwa wamejenga makazi ya muda.
Baada ya siku tatu, Vitalis na Kaguta walipata unafuu japokuwa si kuwa sawa kamili. Bado miili yao ilikuwa na maumivu ambayo yaliwapasua eidha wakiwa wanatembea, kuongea, kuruka ama kujihusisha na shughuli yoyote ya viungo. Lakini kazi lazima ifanyike hivyo hakukuwa na muda wa kubweteka. Wana-BEAST waligeuza mji na kuufanya uwanja wao kwa kufanya mauaji na kuwatesa watu kama salamu kwa Vitalis na Kaguta. Ndani ya muda huo watu nane waliuwawa ikiwemo majirani wa Vitalis, walimu wa Marietta na hata wafanyakazi wenzake na Bernadetha, wale aliofanya nao kazi kwa kipindi kifupi kule hospitalini. Haikujulikana wana-BEAST walipatia wapi taarifa zote hizo. Hayo yalizidi kuwapa hofu WAGENI juu ya BEAST.
Mwanaume mwenye kovu pembeni ya sikio, ajulikanae na wahalifu wenzake kwa jina Mamba, ni miongoni mwa watu hatari juu ya uso wa dunia. Anapotembea katikati ya jiji hakuna anayejua ya kwamba ndiye mwanaume yule yule aliyepata kutikisa Tanzania kwa ujambazi wake wa silaha za moto miaka ya 1980 mpaka 1990 akiwa kama mhusika wa kundi maarufu la kijambazi lililojipachika jina la WANYAMA, kila mhusika ndani akiwa amebebelea jina la mnyama anayempenda. Kwenye miaka ya 2000 kundi hilo lilisambaratishwa na jeshi la polisi, wahusika wote walikamatwa na kutupiwa jela kwa kifungo cha maisha isipokuwa Mamba ambaye alitorokea msitu wa Pangani, Tanga, huko akaishi kama mnyama kwa miaka kumi na tano kabla ya kurejea tena mjini akiwa amebadilika kabisa, uso wake ukiwa umefichwa na ndevu na nywele nyingi. Hata mwili wake ulikuwa mpana zaidi kutokana na mazoezi aliyokuwa anayafanya kutwa kucha. Mjaa asili haachi asili, Mamba alitafuta tena kundi la kijambazi na kujiunga nalo aendeleze kipaji chake. Kutokana na mahusiano makubwa na kundi la bwana Kim ambaye aliitawala serikali ya Tanzania kwa kiasi kikubwa, Mamba alifanikiwa kufuta rekodi yake ya ujambazi na kuwa raia kama wengine. Sasa yupo mtaani kuendeleza mkono wake damu. Amepewa nafasi kubwa na bwana Emilio Diego katika kundi lake la BEAST chini tu baada ya mapacha watatu ambao tayari wameshauwawa, hivyo sasa kumfanya awe juu kuliko wengineo. Na sasa anahaha kumthibitishia mkuu wake kuwa yeye ni bora kuliko hata wale mapacha watatu. Ingetakiwa ampe nafasi na kumuamini zaidi.

***

☆Steve
 
Kazi bado ipo,nguvu ya mamba ni kwenye maji hapa nitulie nione nje ya maji inakuaje
 
Steve pulizi natetemeka kwa hisia tuma hata mbili tatu ili nikidhi afya ya macho yanguu kwa usiku huu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom