Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Mimi macho kodo! Akitia unyayo wake, na Mimi nimo.
 
Ohoooo unaweka kambi, mkuu wa kikosi kasha sepa

Humu nishagundua ntavuna pressure, hafu vitu vyenyewe ni stori cha kushangaza roho inauma kam vilr ni kweli.

Naomba kama mh. Paul Makonda yumo humu JF aje ajifunze kwa wenzie hapa,
Pressure huukoooo! Si hapa.

Hii ni simulizi yangu mwenyewe, nimeandika na kuighani kwa akili yangu. Na kwa akili zangu timamu naituma mpaka mwisho hapa hapa.

☆Steve
 
Pressure huukoooo! Si hapa.

Hii ni simulizi yangu mwenyewe, nimeandika na kuighani kwa akili yangu. Na kwa akili zangu timamu naituma mpaka mwisho hapa hapa.

☆Steve
Kiukweli umenipi tumai, najihisi kama naishi rasi ya tumaini jema
 
***SURA YA AROBAINI NA TANO***





(MSIMU WA 02)





Njemba mwenye bunduki akatikisa kichwa kukataa.
“Hakuna haja ya kwenda hospitali wakati utakufa tu. Nashukuru sana kwa ushirikiano wako, kwa sasa unaweza ukapumzika kwa amani.” Alisema njemba mwenye bunduki alafu akahitimisha uhai wa bwana Isaac kwa kumdidimizia risasi kwenye paji lake la uso.
Video ya kila kitu kilichotokea ndani ya nyumba ya bwana Isaack ikasambazwa kwenye mitandao ya jamii, watu wakatumiana kama bidhaa. Hatimaye ikachukua nafasi mpaka kwenye vyombo vikubwa vya habari. Mwisho wa video maandishi mekundu yalijiandika yakiuliza: Who’s next?
Baada ya siku mbili:
Uso wa bwana Wyne ulikuwa mwekundu. Alikuwa ameketi ndani ya nyumba yake kubwa maeneo ya Masaki akiwa kabebelea sigara kubwa. Saa yake kubwa ya ukutani yenye rangi ya kijivu na urembo wa maua ilikuwa inasema ni saa tisa huku mshale wa dakika ukiwa katikati ya namba tano na nne. Palikuwa patulivu sana kiasi kwamba hata nzi akikatiza inakuwa ni kelele kubwa. Ila punde sauti ya honi ya gari ikaharibu utulivu huo. Ndani ya dakika chache wakaingia watoto wawili wa kike waliovalia sare za shule, kwa makadirio ya miaka saba kwa kila mmoja, walimparamia bwana Wyne wakipayuka:
“Daaaddyyy!”
Bwana Wyne akawatizama kwa sura kavu isiyo na mapokezi.
“Go change your clothes, faster!”
Watoto wakanywea. Wakiwa wameelekeza sura zao chini waliondoka kuelekea chumbani. Bwana Wyne akaendelea kuvuta sigara yake kubwa kwa hisia. Alitoa simu yake akaipachika namba na kuita.
“Borg, for how long should I wait for the number? … Send me the number immediately!” Wyne alifoka akakata simu. Baada tu ya muda mfupi, ujumbe ukaingia kwenye simu ya Wyne, namba za mawasiliano zikiwa na jina la ‘White Mask’. Wyne akapiga hiyo namba.
“Hey Whitey! … Please I need your help … You know what has been happening to our crew at this time, we are at risk, please protect me and my family, I need your assistance … Okay, thanks.”
Wyne alipokata simu akatabasamu. Alitegemea sasa kuanzia muda ule kikosi cha ulinzi kitakuja na kumuhakikishia usalama. Aliweka sigara yake kubwa kwenye ki-sahani maalum alafu akajilaza kwenye kochi. Bakari alitua simu mezani akawatizama Kaguta, Vitalis, Jombi na Miraji, akawaambia:
“Mnaweza mkaenda sasa. Anahitaji ulinzi toka kwa wenzake.”
Baada ya dakika kadhaa wanaume wakavalia suti kali, wakajiweka kwenye defender moja kwa moja mpaka getini kwa Bwana Wyne.Walipofika mlinzi akataka maelezo.
“We are here for the sake of protecting Mr Wyne.” Miraji alieleza kifupi. Mlinzi akapiga simu ndani kumuuliza mkuu wake kama ana miadi, Bwana Wyne akamtaka awaruhusu, WAGENI wakaingia ndani.
“Karibuni sana. Karibuni!” Bwana Wyne aliongea kwa lafudhi ya kimarekani.
“Ahsante sana.” Vitalis akasema huku wakiketi.
“Nilikuwa navategemea kujha.” Wyne aliongelea puani. “Lakini sikujua kama mtawahi. Mpo njema kweli.”
“Yah! Tupo njema kweli. Hii ni kazi yetu na tunaipenda.”
“Nafurahi kusikia.” Wyne akajibu, “Natumai mtahakikisha nakuwa salama na family yangu. Hali imekuwa very worse nowadays. I wonder nani anafanya haya.”
Hakuna aliyemuongelesha. Kaguta alinyanyuka akapanda juu ya meza na kufunga kamba yenye kitanzi hapo. Vitalis akatoa bunduki nyuma ya kiuno chake akamnyooshea bwana Wyne. Miraji akatoa vinyago akawakabidhi wenzake. Miraji akatoka nje kwenda kumalizana na mlinzi na kuteka kamera.
“What’s happening?” Wyne alitahamaki. Kaguta, Vitalis na Jombi wakamtazama wakiwa tayari wamefichama sura zao kwenye vinyago. Miraji aliporudi akawasha kamera na kuanza kurekodi.
“Leo ni zamu yako kutembelewa na wageni, bwana Wyne.”
“What the *** is this? Nyie ni nani? Mnataka nini?” Wyne aliuliza kwa mkupuo na sauti yake inayopitia kwenye tundu za pua.
“Sisi ni WAGENI. Ulidhani unaweza kutukwepa? … Pole sana, sisi hatuhitaji mualiko.”
Vitalis alisema alafu akamtizama Kaguta. Kaguta akaenda vyumbani kufunga milango yote na komeo ikiwemo na chumba walichopo watoto.
“Tell me what you want. Nitawapa. Msiniuwe!” Wyne aliongea kwa huruma.
“Tunataka tu taarifa.” Vitalis alisema kwa ufupi. “We need only information from you.”
“Nitawaambia everything. But don’t kill me as you did kwa Mr Isaack.”
“Isaack tulimuua kwasababu alijifanya mjanja. Hakuweka wazi kila taarifa na alithubutu kutaka kutudanganya. So if you don’t wanna die, be honest.”
“I will! Kweli kabisa.”
“Wewe ni nani kwa Mr Kim Salvatore?”
“Just agent. Nipo kama kiongozi wa white people wote ndani ya Tanzania.”
“Najua mbali na agency, kuna kazi mnakuwa mnafanya. Wewe majukumu yako mengine ni yapi?”
Wyne akasita kidogo kujibu. Kaguta akamnyanyua na kumsimamisha juu ya meza, akamvesha kitanzi.
“I will answer.”
“Then do it before it’s too late.” Vitalis alitishia. Bwana Wyne akafungua mdomo wake kusema:
“Apart for being agent. Pia nafanya kazi ya porching, ujangili. Natafuta meno ya tembo, vifaru na ngozi za wanyama then I transport kwenda kwenye ghala ya Kim.”
“Kampuni yako inaitwaje?”
“Deep Africa wildlife.”
“Na huwa unashirikiana na nani kufanya your deals successful?”
“Katibu ya wizara ya maliasili.”
“Okay. Thanks for your information.”
Vitalis alinyanyuka akamtizama Kaguta na kumpa ishara ya kumtikisia kichwa. Kaguta akatengua meza iliyombeba bwana Wyne. Kitanzi kikadaka koo la mzungu huyo na kuling’ang’ania mpaka pumzi ikakata. Wakafanya msako ndani ya chumba cha bwana Wyne wakabeba baadhi ya nyaraka, wakaondoka.
Baadae video ikaanza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii mpaka kwenye luninga zikiwa zimeambatana na picha za nyaraka za bwana Wyne. Ndani ya muda mfupi katibu wa maliasili akakamatwa, kampuni ya Deep Africa ikafungiwa kwa uchunguzi, wahusika wa ulinzi bandarini na kwenye uwanja wa ndege wakasimamishwa kazi na kusekwa ndani kwa upelelezi zaidi.
Swali likazuka: nani atakayefuata kutembelewa na WAGENI? Hakuna yeyote aliyejua nani atafuata, mitandao ya kijamii ilikuwa inatizamwa mara kwa mara. Matumbo ya wafanyakazi wa serikali yalipashwa joto. Polisi walitangaza donge nono kwa yeyote atakayetoa taarifa ya upatikanaji wa WAGENI kwa kigezo cha kuvunja sheria kwa kufanya mauaji.
Japokuwa hakuna mwananchi aliyebashiri nani atakuwa mhanga ajaye wa WAGENI, bwana Rajesh Deepti yeye aliona ndiye atakayefuata pasi na shaka. Kila kitu chake alichokihitaji kiliwekwa ndani ya mabegi. Akiwa na miadi ya kupaa na ndege ya jioni na muda ukiwa umebakia masaa manne, alishasimama mbele ya geti lake kungojea taksi. Muda tu mfupi taksi ikafika, akaweka mabegi yake na kumuamuru dereva aelekee Mwalimu Nyerere Airport haraka sana. Wakati dereva anaendesha akawa anaongea na simu.
“Yes, I’m on my way to Airport now. I’m heading directly to New Delhi, India. Okay see you!”
Alikata simu akairejesha mkobani. Alitoa tiketi yake ya ndege akaitizama kisha akairudisha mkobani. Akashusha pumzi ndefu. Baada ya mwendo wa dakika kadhaa taksi ikakunja kona na kuacha barabara kuu. Rajesh akawaka:
“Hey! Nimekuambia twende Airport. Wapi unaenda huko?”
Mwendo kasi ukazidi kuongezwa kuelekea maporini. Rajesh akatoa simu yake mfukoni, taksi ikapiga breki kali simu ikadondoka chini, Rajesh akajigonga kwenye kiti cha mbele kwanguvu. Dereva taksi akashuka akaenda viti vya nyuma, kumbe alikuwa ni Kaguta, alimpiga Rajeshi kichwani na kitako cha bunduki, Rajesh akazirai.
Baada ya masaa mawili Rajesh alirejewa na fahamu akajikuta yupo kwenye kiti kilichozungushiwa nyaya uchi za umeme. Alikuwa amebanwa haswa kufurukuta hawezi. Mbali yake hatua kama tano, kulikuwepo na kebo ya umeme. Bernadetha pamoja na Vitalis walitokea wakajongea karibu yake. Bernadetha akamuuliza:
“Nadhani unakumbuka hii sura.”
Rajesh akabinua mdomo wake kwa dharau pasipo kusema kitu.
“Leo utakuwa mwisho wako. Kama wageni ni wako, ni wako tu. Huwezi kuwakimbia.” Alisema Bernadetha alafu akaondoka zake akimuacha Vitalis ambaye aliungana na Miraji baada ya muda mfupi akiwa amebebelea kamera.
Siku ikaenda. Kesho yake ikakaribishwa kwa kusambaa kwa video za mauaji ya Rajesh kwenye kiti cha umeme. Huku taarifa zake za uwakala wa watu wa Asia na kuwa kwenye kitengo cha sayansi na tiba zikitapakaa. Akiwa mshiriki mkubwa wa kuua watu makusudi kwa dhumuni la kufanyia tafiti madawa yao na huku maiti zikisafirishwa kwenda nchi mbalimbali zikiwa zimepandikizwa madawa ya kulevya.




MAHAYAWANI WAKAWA WAMEENDA NA MAJI.


***

☆Steve
 
***SURA YA AROBAINI NA SITA***




(MSIMU WA PILI)







*** SHETANI MPYA ***


Ilikuwa usiku wa saa mbili wakati Vitalis akiwa sebuleni anatizama taarifa ya habari runingani. Baada ya taarifa moja kukatiza ikiwa inaongelea ziara ya raisi wa Tanzania nchini China, ilifuatia taarifa iliyogutusha uso wa Vitalis. Aliona picha yake kwenye kioo cha runinga huku maelezo yakielezwa kama mshutumiwa nambari moja wa mauaji yaliyotukia ndani ya muda mfupi, waziri wa mambo ya nje na uhusiano wa kimataifa ameuwawa kwa kudidimiziwa kisu shingoni.
La haula!
Kitambulisho cha kazi cha Vitalis kilionyeshwa na kamanda wa kanda maalum akisema kwamba kimepatikana eneo la tukio. Na mtuhumiwa anashukiwa anaweza kuwa mhusika wa kundi linalotafutwa kwa udi na uvumba, WAGENI.
Vitalis alisimama akiwa ameshika kiuno na macho yake yakiwa yametoka nje. Alizunguka sebuleni kwa hatua kadhaa akienda na kurudi. Taarifa ya habari ilikuwa imepita na zingine zaendelea lakini kichwani kwake bado alikuwa anasikia jina lake kama mtuhumiwa wa kwanza kwenye mauaji ya mtu mkubwa serikalini.
“Nani kaniset kwenye haya mauaji? … Wametoa wapi kitambulisho changu? Ila si alikichukua OCD? …Kwanini waziri wa mambo ya nje?” Maswali yalimtafuna Vitalis.
Wakiwa kwenye kikao juu ya jambo hilo la mauaji, Bakari alitoa maono:
“Itatulazimu twende eneo la tukio, tunaweza tukapata jambo huko likatusaidia kusafisha jina lako kwa watu.”
“Ila unadhani itakuwa ni rahisi?” Jombi aliuliza, “Hilo eneo bila shaka litakuwa kwenye uangalizi mkubwa.”
“Si lazima tuingie eneoni.” Bakari alisema na kuongezea kwa kuuliza, “Kwani makazi ya marehemu ni wapi?”
“Msasani, ama tunaweza sema mpakani mwa Msasani na Oysterbay.” Vitalis alijibu. Bakari akavuta tanakilishi yake na kwenda kwenye ramani moja kwa moja, Vitalis akamuonyeshea makazi ya marehemu kwa kidole.
“Hapa!”
Bakari akatikisa kichwa, akavuta picha kwa ukaribu na kuitizama kwa umakini huku wenzake wakiwa wanamngojea aseme kitu.
“Tunaweza tukapata data.” Bakari alisema huku akihamisha macho yake toka kwenye tanakilishi mpaka usoni mwa Vitalis. “Pembeni kidogo ya jengo la makazi ya marehemu kuna duka kubwa la vifaa vya kisasa vya kompyuta.”
“Kwahiyo?” Miraji alidakia.
“Kwahiyo jengo kama hilo ni lazima tu litakuwa na kamera za ndani na nje. Tutatumia kamera za nje kutizama juu ya hilo tukio kwa kuzingatia muda wa tukio tuone kuna wageni gani walitembelea hapo muda mfupi kabla ya tukio.”
“Ni wazo zuri.” Sandra alichangia, “ila inabidi pia tufanye juhudi ya kuingia ndani, kuna mambo ambayo hatuweza kuyapata kwa kamera pekee.”
“Nitafanya hiyo kazi.” Vitalis alihakikisha, “Kazi hiyo kamera nitakuachia Bakari, Miraji na Jombi, najua hamtoniangusha.”
Saa nane mchana gari lililowabebelea Jombi, Bakari na Miraji lilitua kwenye kiwanja cha duka kubwa la vifaa vya tanakilishi. Wanaume walishuka wakiwa wamevalia ovaroli na kapero za bluu. Ndani ya dakika chache wakafika eneo la ulinzi, wakaketi kwenye viti nyuma ya tanakilishi zote za kamera baada ya kuwafunga wahusika midomo, mikono na miguu.
Bakari alirudisha video nyuma akaanza kuangalia yaliyotukia jana mida ya saa kumi ya jioni kwa mujibu wa kamera za nje zilizokuwa zinatizama jengo la marehemu waziri. Katika wasaa huo kwenye dakika za ishirini, wakaona gari aina ya Mark X nyeusi ikiwa inaingia ndani. Bakari alisimamisha video alafu akaivuta kwa ukaribu zaidi taratibu taratibu, akaandika chini namba za usajili na tarakimu: 25119-20, zilizokuwa zimeandikwa kwenye stika upande wa kushoto wa kibao cha usajili. Alijaribu kuvuta picha zaidi na zaidi lakini hakuona nyuso za waliomo ndani.
Baadae wakiwa ndani ya nyumba ya Vitalis, Bakari akaonyesha yale waliyoyapata. Vitalis aliweka karatasi ya nailoni mezani ndani yake kukiwa na risasi mbili na sigara kubwa.
“Haya ndiyo ambayo nimeweza kuyaokoteza ndani ya uzio wa nyumba ya marehemu.”
Bakari alishika karatasi ya nailoni akaipeleka machoni kwake kwa ukaribu. Aliitizama riboni kubwa nyeupe iliyoizunguka sigara ile kubwa, akasoma maandishi yaliyoandikwa hapo.
“Lugha gani hii?”
Kaguta alichukua huo ushahidi akausoma.
“Ni kiitaliano.” Alisema na kuongezea, “Imetengenezwa Italy, ni sigara ya watu wa daraja la juu.”
Bakari alipokea tena ushahidi huo akaupiga picha kisha akasogelea tanakilishi yake na kuiunganisha na kamera. Akatafuta majibu ya sigara mtandaoni.
“Hiyo sigara uliikuta wapi Vitalis?” Bernadetha aliuliza.
“Mlango wa kuingilia sebule ya marehemu.” Vitalis akajibu.
“Kwanini unadhani inaweza ikatusaidia?”
“Kwasababu naamini ni lazima itakuwa imeachwa na wauaji. Sidhani kama mwenye nyumba anaweza akavuta sigara na kuitupia mlangoni kwake.”
“Ni kutoka Italy!” Sauti ya Bakari ilipasua anga, wote wakamtizama. “Inatengenezwa Italy na inasafirishwa kwenda nchi chache sana Afrika. Wateja wake wengi wapo Ulaya na Marekani. Ni ghali mno, na ndio mana inachukuliwa kama ni ya watu wa tabaka la juu.”
“Kwahiyo kwa Tanzania inapatikana wapi?” Vitalis alidadisi.
“Kuna wakala mawili tu wanaouza hizo sigara kwa Dar es Salaam. Wote wapo Posta, wanauza pia na vinywaji vikali kama vile spirits, wines na whisky.”
“Nataka hayo maduka yafuatiliwe. Tupate majina ya wateja na makazi yao. Bakari, Jombi na Miraji, hiyo kazi naacha mikononi mwenu. Sandra na Kaguta nitawataka kesho muende msibani, Sandra, nitataka uwe karibu mno na mtoto mkubwa wa kiume wa marehemu, mchimbe unavyoweza. Najua tutapata kitu toka kwake. Naamini unaweza.”
Baada ya kupeana majukumu, walikula na kunywa. Kaguta na Sandra wakaondoka. Vitalis alitoka nje kuvuta hewa safi, Jombi akamfuata huko.
“Hatujapata muda wa kuongea tokea nimetoka maeneoni, mkuu.” Jombi alisema huku akitizama tizama mazingira. Vitalis alitabasamu akasema:
“Ni kweli.” Alivuta pumzi ndefu na matundu yake ya pua, akamgeukia Jombi.
“Naomba unipe mrejesho wa miradi. Inaendeleaje?”
“Inaendelea vyema tu. Baada ya kuwekeza pesa ile tuliyoikwapua kwa Isaac na Mr Wyne, imefufua na kuipa nguvu kubwa. Kwa sasa faida ni kubwa. Tunaweza tukafanya mambo yetu pasipo na shida kabisa.”
Vitalis akatabasamu.
“Hongera sana! Sasa tuna kazi moja tu ya kuusogeza huu mlima mbele yetu, baada ya hapo kila mtu akaishi maisha yake.”
“Tutaweza tu. Dhamira safi siku zote hushinda.” Jombi alikazia uzi.
Gari safi Toyota Rav4 modeli mpya rangi ya kijivu ilisimama kando kando ya uzio mkubwa wa nyumba ya marehemu waziri. Magari yalikuwa mengi mno watu pia. Sandra na Kaguta walishuka toka kwenye Rav4 wakiwa wamevalia nguo nyeusi na miwani ya rangi hiyo hiyo. Wakiwa wanaongozana wakaingia ndani na kuketi kwenye mojawapo ya viti vilivyokuwa vimetandazwa uwanja mzima. Shingo zao zilizungusha vichwa wakitizama kule na kule, Kaguta akamgusa Sandra.
“Yule pale.”
Alionyeshea kwa kutumia kichwa chake. Sandra akaelezea uso wake kule alipoonyeshewa, akamuona mwanaume mmoja mwenye uso mchanga wenye ndevu zilizojaa kidevuni.
“Anaitwa Morris. Ndiye tageti yetu.” Kaguta alieleza. Sandra akataka kunyanyuka, Kaguta akamzuia.
“Ngoja kwanza tusome mazingira.”
Waliendelea kutizama huku na kule. Kaguta akawaona wanaume wanne waliovalia suti na miwani zenye vioo vyeusi. Masikioni mwao walikuwa na viwaya vyeupe vilvyokuja mpaka mdomoni. Kazi yao ilikuwa kuperuzi peruzi huku na huko. Kaguta aliingiza mkono wake mfukoni akatoa miwani. Aliibinua akawatizama wanaume wale kwenye kioo akawaona kwa ukaribu zaidi, shingoni mwao walikuwa na tarakimu 25119-20.
“Utakapoenda, hakikisha unakuwa makini kuwatizama wale watu. Inaonekana wapo hapa kwa malengo fulani kinyume na ya kwetu.”
“Sawa.”
Sandra alinyanyuka akasogea mbele kidogo. Akasogea tena na tena kila alipoona walinzi hawamjali, mwishowe akamfikia Morris. Alimpa mkono wa kuume akisema:
“Pole sana, Morris.”
“Ahsante, nishapoa.” Morris aliitikia huku uso wake ukiwa umebebelea ka-wasiwasi.
“Samahani. Nakujua?” Morris aliuliza.
“Sidhani kama unanijua.” Sandra alijibu. “Ila mimi nakujua, wewe ni mtoto wa kwanza wa Mheshimiwa Johnson Machibya, aliyekuwa mfanyakazi mwenzangu kipindi tunafanya kazi pamoja ubalozini Australia. Ndani ya ofisi yake alikuwa ana picha kubwa ya familia yake, na huko ndipo nikaona uso wako, hata nilipokuona hapa nikakutambua.”


***

☆Steve
 
***SURA YA AROBAINI NA SABA***




(MSIMU WA 02)







Morris alitabasamu kidogo, akauliza:
“Na wewe je, unaitwa nani?”
“Dakota.” Sandra akajibu, “Dakota Sean.”
“Okay. Karibu Tanzania.”
“Nipo Tanzania kwa miaka mitatu sasa, sistahili kukaribishwa. Ila sasa naona mahitaji makubwa ya kurudi Australia.” Sandra alieleza.
“Mahitaji gani?” Morris akauliza.
“Upungufu wa amani nchini kwetu - inantisha sasa. Kama mfanyakazi mwenzangu ameuwawa kiukatili hivyo nani anajua atakayefuata? Kama ni mimi?”
“Unadhani suluhisho ni kukimbia tatizo?” Morris aliuliza huku akimtizama Sandra. Wakati wanaendelea kuongea, Kaguta akaona walinzi ndani ya suti wakimtizama Sandra. Punde wakapeana habari na kuanza kuchukua hatua kuelekea alipo mlengwa wao kwa hatua kubwa kubwa. Kaguta alimuita Sandra kwa kunong’oneza lakini haikusaidia. Ilibidi atumie njia mbadala. Alidondoka chini akaanza kujirusha rusha kama mtu mwenye kifafa huku akitoa sauti ya kugugumia. Watu wote walitekwa na hilo tukio. Walinzi wakamsahau Sandra kwa dakika na kumkimbilia Kaguta.
Baada ya dakika kama mbili Kaguta alitulizana na kuwaomba radhi walinzi kwa usumbufu, walinzi walimuacha wakaenenda kwa mlengwa wao, Sandra, ila walipofika walimkuta mtoto wa marehemu pekee, Sandra hakujulikana wapi alienda. Walinzi walipomrudia Kaguta naye hawakumkuta, alishayoyoma. Wakabaki kwenye mduwazo.
Ndani ya Rav4 Kaguta na Sandra walijiweka wakatoka eneo la msiba. Wakiwa njiani wakawa wanateta:
“Vipi umefanikiwa?” Kaguta aliuliza.
“Ndio. Nimempatia namba yangu. Anaonekana ana kiu ya kutaka kufanya kitu juu ya kifo cha baba yake.”
“Safi sana.”
Walinzi walitoka nje kutizama kwenye paki ya magari, napo hawakuona gari lolote lililotoka, Kaguta na Sandra walikuwa tayari wameshapotea. Walinzi walitizama kushoto na kulia wasione kitu, wakaamua kurudi ndani ya uzio.
“Tumepata orodha ya wateja toka kwenye duka moja la sigara.” Bakari alimwambia Vitalis wakiwa wameketi sebuleni pamoja na wahusika wote wa kundi la WAGENI.
“Katika orodha hiyo wateja wa Dar wapo wawili tu, waliobakia wote ni kutoka Arusha wateja wengi wakiwa ni watalii.”
“Na vipi kuhusu duka la pili?” Vitalis aliuliza.
“Hatukuangaika nalo maana wao ni wakala tu wa kupokea sigara hizo na kuzipeleka Zambia na Uganda. Hawasambazi hapa Tanzania.”
“Sawa. Hao wateja wawili nahitaji uwafuatilie zaidi na tufahamu nani anahusika na hayo mauaji. Sawa?”
“Sawa. Hesabia kama tayari.”
Siku iliyofuata wasaa wa mchana Sandra alikuwa na Kaguta mgahawani wakipata chakula cha mchana huku wakilonga hili na lile. Haikuchukua muda mrefu kabla ya simu ya Sandra kuita, namba mpya kiooni. Sandra akapokea:
“Haloo! … Okay okay, nakuja.”
Alipokata simu akamtizama Kaguta.
“Morris anataka tukutane sasa hivi, acha niende.”
“Poa, see you!”
Muda mfupi tu baadae Sandra akawa ameketi na Morris kwenye uwanda wa nyasi kijani kibichi.Mkononi mwa kila mmoja wao kulikuwa kuna kinywaji kilaini rangi ya maji ya machungwa.
“Sijui nani wa kumuamini, kuna baadhi ya mambo nakinzana kabisa na jeshi la polisi.”
“Unaweza ukaniamini mimi. Tunaweza tukawatumia Interpol kama polisi hauwaamini. Ni mambo yapi unayokinzana na polisi?”
“Wanadai aliyefanya tukio ni mtu aliyeacha kitambulisho eneo la tukio. Sidhani kama ndiye.”
“Unadhani ni nani?”
“Mida ya saa kumi ya jioni tulivamiwa na watu watatu wakiwa wamevalia suti na vinyago usoni. Mmoja wao alikuwa anavuta sigara kubwa. Walimuua mlinzi na kumuweka baba chini ya ulinzi, wakamuuliza kama kuna mtu yeyote ndani, akajibu hapana. Walifanya msako lakini hawakunipata nilikuwa nimejificha nyuma ya kabati. Hawakuchukua chochote zaidi ya kumuua baba kwa kumchoma kisu shingoni - nilipata kushuhudia kwa macho yangu mwenyewe. Walipomaliza wakaondoka zao, mmoja wao akatupa kitambulisho kwa makusudi kabisa.Nadhani lengo lao lilikuwa ni kum-frame huyo anayetafutwa sasa.”
“Unaweza ukaniambia muonekano wa hao majambazi watatu?”
“Walikuwa wanaume warefu, mmoja wao alikuwa mrefu zaidi na mwenye mwili mpana, kinyago chake cha usoni kilipoishia ilitokezea alama ya kovu la kisu pembeni ya sikio. Ndiye aliyekuwa anavuta sigara na ndiye huyo aliyemchoma baba kisu cha shingoni, na ni yeye ndiye aliyewaamuru wenzake waondoke.”
Morris alinyamaza kimya huku macho yake yakiwa yanalenga machozi. Alitoa simu mfukoni akamkabidhi Sandra.
“Hii ni simu ya baba - password yake ni 18821. Kabla hatujavamiwa nilimsikia anaongea na mtu dakika chache tu nyuma. Inaweza ikasaidia kwenye upelelezi.”
Sandra aliitizama ile simu akaiweka mkobani.
“Ahsante. Ila sasa nahitaji namba yako.”
Morris alimpa namba Sandra, Sandra akainakili kwenye simu yake kisha wakaagana.
“Nitakutaarifu kila nyendo.”
Sandra alimtoa shaka Morris.
“Naamini itakuwa hivyo. Hakikisha inakuwa siri, nahisi kuna watu wananifuatilia.”
“Sawa, Morris.”



***

☆Steve
 
Pressure huukoooo! Si hapa.

Hii ni simulizi yangu mwenyewe, nimeandika na kuighani kwa akili yangu. Na kwa akili zangu timamu naituma mpaka mwisho hapa hapa.

☆Steve
Swahiba punguza Munkari yakhee!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom