SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,803
- 25,444
- Thread starter
- #521
**SURA YA AROBAINI NA MOJA**
(MSIMU WA 02)
Kesho yake ndani ya asubuhi Tahid akiwa amevaa suti yake nyeusi alikutana na bwana Isaac Makongo kwenye mgahawa mmoja uliokuwa na watu wachache. Walikuwa wanapata kifungua kinywa huku wakipeta soga. Kila walichokuwa wanakiongea kilikuwa kinasikika na Vitalis, Kaguta, Jombi na Miraji waliokuwa wapo ndani ya gari aina ya van iliyosimama umbali wa kama mita mbili toka eneo la mgahawa.
Uso wa Tahid haukuonyesha woga wala tafakuri tatanishi yoyote lakini mikono yake ilikuwa inatetemeka. Hakuweza kubeba kikombe cha chai, kila alipojaribu aliishia katikati na kukirejesha mezani. Isaac akagundua hilo.
“Vipi kuna tatizo?”
“Ndio.”
Tahid akatoa bunduki yake na kumuonyeshea Isaac huku akiwa ameificha na koti, akamuamuru afuate gari aina ya van iliyoko kando, Isaac akatii, wakasogea mpaka garini. Gari likafunguliwa Isaac akaingia ndani. Tahid akasema:
“Nimemaliza kazi yenu sasa, naomba video na remote ya bomu niende.”
Mara ghafla gari likatokea kwa nyuma, Tahid aligeuka kushangaa akakutana na risasi tatu zilizokita kifuani mwake, akadondoka chini kama gogo. Vitalis akafunga milango ya gari, mafuta yakakanyagwa kwanguvu. Barabarani ikawa mfukuzano, gari la wakina Vitalis mbele, nyuma yao wakiwa wanakimbizwa na Range rover nyeusi, risasi zikirushwa kama njugu. Magari yalipelekwa kwa kasi mno kama vile game. Kaguta aliyekamatia van alihakikisha habandui mguu wake sehemu ya kukanyagia mafuta, hata pale konani. Lakini hata waliokuwa wanawakimbiza walifanya vivyo hivyo.
Kaguta akatoka barabara kubwa ya njia nne, akaingia ya njia moja. Ila punde kwa mbele yakatokea magari mawili makubwa, yakaziba njia. Kaguta alipotaka kurudisha nyuma akashindwa, alibanwa na Range rover hatua kadhaa nyuma. Wanaume watano: mapacha watatu na wengine wawili wakashuka toka kwenye magari yao wakiwa wamebebelea bunduki wakawaamuru wote waliokuwepo ndani ya van washuke chini haraka kabla namba zinazohesabiwa hazijafika kumi.
Wakiwa katika mahesabu hayo, Vitalis akawaambia wenzake:
“Muda wa plan B sasa.”
Jombi akachomoa solo tape mfukoni akamfunika mdomo Isaac alafu wakashuka watu wanne tu: Vitalis, Kaguta, Jombi na Isaac. Miraji akabakizwa ndani. Mapacha wale watatu na wenzao wawili wote wakajongea sehemu moja, nyuma ya van, kumpokea Isaac. Vitalis na wenzake walikuwa wamenyoosha mikono juu, lakini muda huo huo wote walikuwa wanahesabu namba kwa kunong’oneza tokea wametoka ndani ya van. Ilipofika namba tano, wote wakarukia pembeni, ghafla van ikarudi nyuma haraka na kuwasukuma maadui wote kwanguvu wakarukia huko, wakina Vitalis wakawahi silaha za maadui na kuwaweka chini ya ulinzi. Wakawaamuru wote wapande ndani ya van. Wakapanda na kuondoka.
Wakiwa wametembea kwa dakika moja barabarani, mapacha watatu wakatizamana kwa macho yanayowasiliana. Mmoja akasema kwa kunong’oneza:
“Plan b.”
Wote wakapeleka mikono kwenye saa zao za mikononi na kuzibofya, moshi ukaanza kutoka taratibu. Wao wakabana pumzi huku wakiwatizama wengine ambao haikuchukua muda wakalewa na kulala. Baada ya lisaa limoja, macho ya Kaguta yakafunguka. Mapacha watatu, Isaac na wenzao wawili hawakuwepo, walibakia wahusika wanne wa kundi la WAGENI tu. Van ilikuwa imesimama kandokando ya barabara ikiwa wazi.
“Amkeni!” Kaguta aliwaamsha wenzake. Vitalis akapepesa macho kisha akauliza:
“Wapo wapi?”
“Hawapo. Wameondoka.” Kaguta alijibu huku akiwa amekunja sura. Vitalis akapiga ngumi gari.
“Shit! … Shit!”
Alishia tu kutikisa kichwa na kushika tama. Gari liliwashwa wakaondoka. Walipofika nyumbani, Bakari akawahabarisha.
“Nilifunga kamera ndani ya gari, nadhani inaweza kutusaidia kutupa baadhi ya taarifa.”
Wakaketi na kuanza kusoma matukio yote yaliyotukia ndani ya gari kwa kupitia tanakilishi ya Bakari. Wakaona jinsi mapacha wale watatu walivyopeana taarifa na kubofya saa zao. Wakaona pia jinsi walivyonusurika kufa baada ya jaribio la kupigwa risasi kushindikana pindi wakiwa wamelala kilevi baada ya mapacha wale watatu kukosa risasi za kufanyia tukio. Video ilipoisha, Kaguta akasema:
“Nadhani tulikosea target. Kumpata Isaac yatupasa kwanza kuwauwa hawa mbwa watatu. Wao ndio kila kitu. Na inawezekana Isaac ana chip ndani ya mwili wake, popote atakapokuwepo, hawa mbwa watatu watafahamu.”
“Kweli.” Vitalis akaunga mkono hoja.
“Ila kati ya hao watu watatu wanaofanana kuna ambaye anaongoza wenzake.” Miraji alichangia, “Wote hawa ni mtu mmoja tu ambaye amegawanywa, inaitwa Human Plurality Modification, ama HPM. Ukitizama vema video utaona kuna ambaye anatangulia kufanya kitu alafu wengine ndio wanafuata. Hata pale kwenye kunong’oneza huyo anayetangulia yeye ndiye aliyefanya hilo tukio, wengine wakafuata, huyo kiongozi anaitwa ‘the brain’ama ubongo. Kama tunataka kuwamaliza hawa watatu inabidi kwanza tumjue kiongozi wao, na huyo ndio awe primary target.”
“Miraji, Umejulia wapi haya mambo?” Kaguta aliuliza, Miraji akatabasamu kisha akamtizama Vitalis huku akitabasamu. Vitalis naye akarejesha tabasamu kisha akasema:
“Tuna bahati sana kuwa na wewe kwenye kundi letu. Sasa umetupa matumaini mapya. Naamini ukikaa na Bakari mnaweza mkafanya kazi nzuri tukakamilisha misheni yetu kwa ufanisi.”
Miraji akamtizama Bakari alafu wote wakatabasamu na kutikisa vichwa.
“Okay jamani. Naomba nitoe udhuru.” Kaguta akasema huku akisimama. “Leo nina mtoko na bibie Sandra usiku huu, naomba nikajiandae wandugu, si unajua tena?”
“Unaweza tu ukaenda, take care!” Vitalis akamsabahi rafiki yake. Kaguta akampa mkono kila mtu na kuwatakia kazi njema. Kaguta alipotoka ndani Miraji na Bakari wakamtizama Vitalis kwa macho yenye mshumbusi wa tafakuri.
“Vipi? … Mbona mnanitizama hivyo?” Vitalis aliuliza.
“Wewe hautoki na mwenzako?” Miraji akasema. Vitalis akaigiza.
“Nitoke na nani?”
“Kwani hujui nani?”
“Sijui nini mnaongelea.”
Bakari na Miraji wakatabasamu.
“Tunadhani na wewe ni muda muafaka wa kwenda mtoko na Miss Bernadetha.” Bakari akapasua jibu.
“Tafadhali mfanye mama yangu afurahi.” Miraji akashindilia msumari. Vitalis akakosa cha kusema, alibakia tu akitabasamu. Alinyanyuka akaenda chumbani kwake. Miraji na Bakari wakagongesha viganja vyao.
Baada mida ya saa mbili ya usiku gari la Kaguta likatua kwenye uwanja wa nyumba ya Vitalis. Ndani yake alikuwemo Kaguta na Sandra wakiwa wamependeza haswa. Honi ilipigwa na punde wakatoka Vitalis akiwa ameongozana na Bernadetha. Vitalis alivalia suti nyeusi wakati Bernadetha akiwa amevalia gauni refu jeupe lenye maua mekundu shingoni na mabegani. Walikuwa wanang’aa. Kaguta alitabasamu akamwambia Sandra:
“Yeyote aliyewapa hawa watu wazo la kufanya hivi, abarikiwe na mwenyezi Mungu mwenye enzi.”
Vitalis na Bernadetha wakapanda garini wakaondoka kwenda moja kwa moja KACHIKA BEACH HOTEL. Waliketi meza moja kila mtu akiwa karibu na mwenza wake. Vinywaji vikaletwa na kuchafua meza, mhudumu akamimina kinywaji kwenye kila glasi kisha akaondoka na kurudi na sahani zenye chakula laini.
Bakari na Miraji bado hawakuwa wamelala. Wote walikuwa wameketi karibu na tanakilishi wakiperuzi mambo. Miraji alishikilia usukani kwa kuweka vidole vyake juu ya vibofyeo akiweka maneno na kuyatafuta mtandaoni. Alama za fomula za kisayansi zilikuwa zinawekwa na kutafutwa mara kwa mara, mara zingine vitabu vya mambo ya uzalishaji na uzazi vikitafutwa na kusomwa na Miraji huku akiwa anaandika baadhi ya taarifa kando. Bakari alipiga mhayo akauliza:
“Uliyajulia wapi hayo mambo, Miraji?”
Miraji akaandika kwanza kitu kando alafu akamtizama Bakari aliyekuwa anarembua kiusingizi akamwambia:
“Haya ndiyo mambo niliyoyasomea India. Kabla sijaacha shule na kurudi nyumbani nilikuwa kwenye utafiti juu ya hii sayansi ya kugawanya watu na wakafanana vilevile.”
Bakari akapiga mhayo tena. Miraji akarejesha macho na vidole vyake kwenye tanakilishi akaendelea. Baada ya muda akasikia mtu anakoroma, aligeuza shingo kutizama akamkuta Bakari ameweka kichwa chake juu ya meza, amelala. Akanyanyuka akambeba akamlazia kwenye kochi kisha akarudi kuendelea na kazi yake.
Vicheko vilitawala meza ya wakina Vitalis. Nyuso za furaha zilitawala huku hakuna aliyeonekana kama anafikiria ulimwengu mwingine mbali na ule waliokuwemo. Kaguta na Vitalis walikuwa wanashindana kuimba huku wanawake wakiwa mahakimu kwa kutoa point. Kwakuwa hakuna aliyekuwa na sauti nzuri ya kuimba, basi lile tendo likawa kama mchezo wa futuhi, wote wakawa wanacheka na kusemana hapa na pale. Tafrija ilikuja kukatishwa pale alipokuja mwanamke mmoja akiwa kavalia nguo za wahudumu. Mwili wake ulikuwa umejaa kwa shepu ya kibantu, alitembea kwa madaha yote akasimama nyuma ya Kaguta kisha akainama na kumnong’oneza.
“Helo mpenzi!”
Kaguta akashtuka na kutizama sauti ilipotokea.
“Bhoke!” Kaguta akatahamaki. “Unafanya nini hapa?”
“Kwani vipi, hukutegemea kuniona, mpenzi?”
“Mpenzi wako nani? … Embu tafadhali nenda, hivi ndivyo mlivyofundishwa kuhudumia wateja?”
Bhoke akaguna.
“Leo unaniona takataka enh? Leo sina maana kwako, sio?”
“Kaguta, huyo nani?” Sandra akaingilia.
“Usihofu, mpenzi. Nitakuelezea.” Kaguta alijitetea.
“Utaeleza nini?” Bhoke akauliza, “Kumbe hata jina ulin’danganya ukanambia unaitwa Benson? Mwanaume wewe!”
Kaguta alinyanyuka akamtoa Bhoke lile eneo. Alimvutia mbali kabisa na eneo walilopo wenzake, akashusha pumzi ndefu na kutikisa kichwa chake.
“Unafanya nini, Bhoke? Tangu lini mimi na wewe tulikuwa wapenzi? Si tulikuwa tunamalizana tu kila mtu anaenda na zake?”
“Nilikudai pesa mara ngapi? Nilikudai pesa mara moja tu ile siku ya kwanza, siku zingine nilikuwa nakupa penzi bure kabisa. Unavyosema tulikuwa tunamalizana unamaanisha nini?”
Kaguta akatoa pochi yake mfukoni.
“Unanidai shilingi ngapi?”
Bhoke akasonya.
“Unadhani kama nilikuwa nataka pesa nisingekuambia muda wote huo? … Nakutaka wewe Benson, sijui Kaguta, vyovyote vile.”
“Unan’taka mimi?”
“Ndio. Nataka penzi ulilonipa liwe la kwangu tu.”
“Una wazimu wewe enh?”
“Ndio. Penzi lako lanipa wazimu.”
“Bhoke, tafadhali naomba uende. Unajua wale ni watu wa heshima sana. Unaniharibia picha yangu kwa kabisa.”
“Kwahiyo?”
“Nenda, tutayamaliza baadae.”
“Ole wako usinitafute.”
Bhoke akaondoka. Kaguta akashika kiuno.
“Aisee! Yani nimekimbia kule nije huku kumbe ndiyo nimeyakuta huku huku.”
Alitikisa kicha chake akang’ata lips.
“Kaja lini huku huyu mwanamke? … Mungu wangu!”
Aligeuza akawarudia wenzake akakuta kiti cha Sandra kitupu. Vitalis akamwambia:
“Ameondoka. Pole kwa maswahibu.” Kisha akatabasamu.
Hawakuchukua tena muda mrefu hapo, wakalipia bili na kuondoka zao. Kaguta aliwarudisha Vitalis na Bernadetha nyumbani yeye akaenda zake kwa madai ya kumfuata Sandra. Vitalis na Bernadetha wakaingia ndani wakawakuta Miraji amelala pembeni ya tanakilishi huku Bakari akiwa hajielewi usingizini kwenye kochi. Vitalis alimnyanyua mmoja mmoja akawapeleka chumbani na kuwafunika na shuka. Bernadetha alisimama mlangoni akimtizama Vitalis akiwafunika shuka wanausingizi. Vitalis alitoka chumban akamtizama Bernadetha kwa sekunde kadhaa, Bernadetha akasema:
“Una nguvu kweli. Umewabeba watu wazima hivyo.”
Vitalis akainama na kumnyanyua Bernadetha.
“Hata wewe naweza kukubeba.”
Alimpeleka chumbani akamlaza.
“Nakutakia usiku mwema. Nimefurahi sana kuwa na wewe usiku huu.” Kaguta alisema kisha akatoka chumbani. Bernadetha akavuta mto na kuukumbatia kwanguvu. Alitabasamu mwenyewe akajisemea:
“Ahsante kwa kurudisha furaha yangu.”
Masaa yakakimbia usiku ukakata. Asubuhi ya saa tatu, Miraji na Bakari walikuwa pamoja na Vitalis kwenye meza ya tanakilishi. Miraji akachukua karatasi yake aliyokuwa anaiandikia, akasema:
“Kuna habari nzuri na mbaya. Nianze na ipi?”
“Mbaya.” Vitalis akajibu.
“Habari mbaya ni kwamba, hatujapata njia ya kuwakamata mapacha watatu.”
“Na nzuri?”
“Habari nzuri, tumepata watu ambao kwa njia moja ama nyingine wanahusika na tendo hili la kisanyansi.”
***
☆Steve
(MSIMU WA 02)
Kesho yake ndani ya asubuhi Tahid akiwa amevaa suti yake nyeusi alikutana na bwana Isaac Makongo kwenye mgahawa mmoja uliokuwa na watu wachache. Walikuwa wanapata kifungua kinywa huku wakipeta soga. Kila walichokuwa wanakiongea kilikuwa kinasikika na Vitalis, Kaguta, Jombi na Miraji waliokuwa wapo ndani ya gari aina ya van iliyosimama umbali wa kama mita mbili toka eneo la mgahawa.
Uso wa Tahid haukuonyesha woga wala tafakuri tatanishi yoyote lakini mikono yake ilikuwa inatetemeka. Hakuweza kubeba kikombe cha chai, kila alipojaribu aliishia katikati na kukirejesha mezani. Isaac akagundua hilo.
“Vipi kuna tatizo?”
“Ndio.”
Tahid akatoa bunduki yake na kumuonyeshea Isaac huku akiwa ameificha na koti, akamuamuru afuate gari aina ya van iliyoko kando, Isaac akatii, wakasogea mpaka garini. Gari likafunguliwa Isaac akaingia ndani. Tahid akasema:
“Nimemaliza kazi yenu sasa, naomba video na remote ya bomu niende.”
Mara ghafla gari likatokea kwa nyuma, Tahid aligeuka kushangaa akakutana na risasi tatu zilizokita kifuani mwake, akadondoka chini kama gogo. Vitalis akafunga milango ya gari, mafuta yakakanyagwa kwanguvu. Barabarani ikawa mfukuzano, gari la wakina Vitalis mbele, nyuma yao wakiwa wanakimbizwa na Range rover nyeusi, risasi zikirushwa kama njugu. Magari yalipelekwa kwa kasi mno kama vile game. Kaguta aliyekamatia van alihakikisha habandui mguu wake sehemu ya kukanyagia mafuta, hata pale konani. Lakini hata waliokuwa wanawakimbiza walifanya vivyo hivyo.
Kaguta akatoka barabara kubwa ya njia nne, akaingia ya njia moja. Ila punde kwa mbele yakatokea magari mawili makubwa, yakaziba njia. Kaguta alipotaka kurudisha nyuma akashindwa, alibanwa na Range rover hatua kadhaa nyuma. Wanaume watano: mapacha watatu na wengine wawili wakashuka toka kwenye magari yao wakiwa wamebebelea bunduki wakawaamuru wote waliokuwepo ndani ya van washuke chini haraka kabla namba zinazohesabiwa hazijafika kumi.
Wakiwa katika mahesabu hayo, Vitalis akawaambia wenzake:
“Muda wa plan B sasa.”
Jombi akachomoa solo tape mfukoni akamfunika mdomo Isaac alafu wakashuka watu wanne tu: Vitalis, Kaguta, Jombi na Isaac. Miraji akabakizwa ndani. Mapacha wale watatu na wenzao wawili wote wakajongea sehemu moja, nyuma ya van, kumpokea Isaac. Vitalis na wenzake walikuwa wamenyoosha mikono juu, lakini muda huo huo wote walikuwa wanahesabu namba kwa kunong’oneza tokea wametoka ndani ya van. Ilipofika namba tano, wote wakarukia pembeni, ghafla van ikarudi nyuma haraka na kuwasukuma maadui wote kwanguvu wakarukia huko, wakina Vitalis wakawahi silaha za maadui na kuwaweka chini ya ulinzi. Wakawaamuru wote wapande ndani ya van. Wakapanda na kuondoka.
Wakiwa wametembea kwa dakika moja barabarani, mapacha watatu wakatizamana kwa macho yanayowasiliana. Mmoja akasema kwa kunong’oneza:
“Plan b.”
Wote wakapeleka mikono kwenye saa zao za mikononi na kuzibofya, moshi ukaanza kutoka taratibu. Wao wakabana pumzi huku wakiwatizama wengine ambao haikuchukua muda wakalewa na kulala. Baada ya lisaa limoja, macho ya Kaguta yakafunguka. Mapacha watatu, Isaac na wenzao wawili hawakuwepo, walibakia wahusika wanne wa kundi la WAGENI tu. Van ilikuwa imesimama kandokando ya barabara ikiwa wazi.
“Amkeni!” Kaguta aliwaamsha wenzake. Vitalis akapepesa macho kisha akauliza:
“Wapo wapi?”
“Hawapo. Wameondoka.” Kaguta alijibu huku akiwa amekunja sura. Vitalis akapiga ngumi gari.
“Shit! … Shit!”
Alishia tu kutikisa kichwa na kushika tama. Gari liliwashwa wakaondoka. Walipofika nyumbani, Bakari akawahabarisha.
“Nilifunga kamera ndani ya gari, nadhani inaweza kutusaidia kutupa baadhi ya taarifa.”
Wakaketi na kuanza kusoma matukio yote yaliyotukia ndani ya gari kwa kupitia tanakilishi ya Bakari. Wakaona jinsi mapacha wale watatu walivyopeana taarifa na kubofya saa zao. Wakaona pia jinsi walivyonusurika kufa baada ya jaribio la kupigwa risasi kushindikana pindi wakiwa wamelala kilevi baada ya mapacha wale watatu kukosa risasi za kufanyia tukio. Video ilipoisha, Kaguta akasema:
“Nadhani tulikosea target. Kumpata Isaac yatupasa kwanza kuwauwa hawa mbwa watatu. Wao ndio kila kitu. Na inawezekana Isaac ana chip ndani ya mwili wake, popote atakapokuwepo, hawa mbwa watatu watafahamu.”
“Kweli.” Vitalis akaunga mkono hoja.
“Ila kati ya hao watu watatu wanaofanana kuna ambaye anaongoza wenzake.” Miraji alichangia, “Wote hawa ni mtu mmoja tu ambaye amegawanywa, inaitwa Human Plurality Modification, ama HPM. Ukitizama vema video utaona kuna ambaye anatangulia kufanya kitu alafu wengine ndio wanafuata. Hata pale kwenye kunong’oneza huyo anayetangulia yeye ndiye aliyefanya hilo tukio, wengine wakafuata, huyo kiongozi anaitwa ‘the brain’ama ubongo. Kama tunataka kuwamaliza hawa watatu inabidi kwanza tumjue kiongozi wao, na huyo ndio awe primary target.”
“Miraji, Umejulia wapi haya mambo?” Kaguta aliuliza, Miraji akatabasamu kisha akamtizama Vitalis huku akitabasamu. Vitalis naye akarejesha tabasamu kisha akasema:
“Tuna bahati sana kuwa na wewe kwenye kundi letu. Sasa umetupa matumaini mapya. Naamini ukikaa na Bakari mnaweza mkafanya kazi nzuri tukakamilisha misheni yetu kwa ufanisi.”
Miraji akamtizama Bakari alafu wote wakatabasamu na kutikisa vichwa.
“Okay jamani. Naomba nitoe udhuru.” Kaguta akasema huku akisimama. “Leo nina mtoko na bibie Sandra usiku huu, naomba nikajiandae wandugu, si unajua tena?”
“Unaweza tu ukaenda, take care!” Vitalis akamsabahi rafiki yake. Kaguta akampa mkono kila mtu na kuwatakia kazi njema. Kaguta alipotoka ndani Miraji na Bakari wakamtizama Vitalis kwa macho yenye mshumbusi wa tafakuri.
“Vipi? … Mbona mnanitizama hivyo?” Vitalis aliuliza.
“Wewe hautoki na mwenzako?” Miraji akasema. Vitalis akaigiza.
“Nitoke na nani?”
“Kwani hujui nani?”
“Sijui nini mnaongelea.”
Bakari na Miraji wakatabasamu.
“Tunadhani na wewe ni muda muafaka wa kwenda mtoko na Miss Bernadetha.” Bakari akapasua jibu.
“Tafadhali mfanye mama yangu afurahi.” Miraji akashindilia msumari. Vitalis akakosa cha kusema, alibakia tu akitabasamu. Alinyanyuka akaenda chumbani kwake. Miraji na Bakari wakagongesha viganja vyao.
Baada mida ya saa mbili ya usiku gari la Kaguta likatua kwenye uwanja wa nyumba ya Vitalis. Ndani yake alikuwemo Kaguta na Sandra wakiwa wamependeza haswa. Honi ilipigwa na punde wakatoka Vitalis akiwa ameongozana na Bernadetha. Vitalis alivalia suti nyeusi wakati Bernadetha akiwa amevalia gauni refu jeupe lenye maua mekundu shingoni na mabegani. Walikuwa wanang’aa. Kaguta alitabasamu akamwambia Sandra:
“Yeyote aliyewapa hawa watu wazo la kufanya hivi, abarikiwe na mwenyezi Mungu mwenye enzi.”
Vitalis na Bernadetha wakapanda garini wakaondoka kwenda moja kwa moja KACHIKA BEACH HOTEL. Waliketi meza moja kila mtu akiwa karibu na mwenza wake. Vinywaji vikaletwa na kuchafua meza, mhudumu akamimina kinywaji kwenye kila glasi kisha akaondoka na kurudi na sahani zenye chakula laini.
Bakari na Miraji bado hawakuwa wamelala. Wote walikuwa wameketi karibu na tanakilishi wakiperuzi mambo. Miraji alishikilia usukani kwa kuweka vidole vyake juu ya vibofyeo akiweka maneno na kuyatafuta mtandaoni. Alama za fomula za kisayansi zilikuwa zinawekwa na kutafutwa mara kwa mara, mara zingine vitabu vya mambo ya uzalishaji na uzazi vikitafutwa na kusomwa na Miraji huku akiwa anaandika baadhi ya taarifa kando. Bakari alipiga mhayo akauliza:
“Uliyajulia wapi hayo mambo, Miraji?”
Miraji akaandika kwanza kitu kando alafu akamtizama Bakari aliyekuwa anarembua kiusingizi akamwambia:
“Haya ndiyo mambo niliyoyasomea India. Kabla sijaacha shule na kurudi nyumbani nilikuwa kwenye utafiti juu ya hii sayansi ya kugawanya watu na wakafanana vilevile.”
Bakari akapiga mhayo tena. Miraji akarejesha macho na vidole vyake kwenye tanakilishi akaendelea. Baada ya muda akasikia mtu anakoroma, aligeuza shingo kutizama akamkuta Bakari ameweka kichwa chake juu ya meza, amelala. Akanyanyuka akambeba akamlazia kwenye kochi kisha akarudi kuendelea na kazi yake.
Vicheko vilitawala meza ya wakina Vitalis. Nyuso za furaha zilitawala huku hakuna aliyeonekana kama anafikiria ulimwengu mwingine mbali na ule waliokuwemo. Kaguta na Vitalis walikuwa wanashindana kuimba huku wanawake wakiwa mahakimu kwa kutoa point. Kwakuwa hakuna aliyekuwa na sauti nzuri ya kuimba, basi lile tendo likawa kama mchezo wa futuhi, wote wakawa wanacheka na kusemana hapa na pale. Tafrija ilikuja kukatishwa pale alipokuja mwanamke mmoja akiwa kavalia nguo za wahudumu. Mwili wake ulikuwa umejaa kwa shepu ya kibantu, alitembea kwa madaha yote akasimama nyuma ya Kaguta kisha akainama na kumnong’oneza.
“Helo mpenzi!”
Kaguta akashtuka na kutizama sauti ilipotokea.
“Bhoke!” Kaguta akatahamaki. “Unafanya nini hapa?”
“Kwani vipi, hukutegemea kuniona, mpenzi?”
“Mpenzi wako nani? … Embu tafadhali nenda, hivi ndivyo mlivyofundishwa kuhudumia wateja?”
Bhoke akaguna.
“Leo unaniona takataka enh? Leo sina maana kwako, sio?”
“Kaguta, huyo nani?” Sandra akaingilia.
“Usihofu, mpenzi. Nitakuelezea.” Kaguta alijitetea.
“Utaeleza nini?” Bhoke akauliza, “Kumbe hata jina ulin’danganya ukanambia unaitwa Benson? Mwanaume wewe!”
Kaguta alinyanyuka akamtoa Bhoke lile eneo. Alimvutia mbali kabisa na eneo walilopo wenzake, akashusha pumzi ndefu na kutikisa kichwa chake.
“Unafanya nini, Bhoke? Tangu lini mimi na wewe tulikuwa wapenzi? Si tulikuwa tunamalizana tu kila mtu anaenda na zake?”
“Nilikudai pesa mara ngapi? Nilikudai pesa mara moja tu ile siku ya kwanza, siku zingine nilikuwa nakupa penzi bure kabisa. Unavyosema tulikuwa tunamalizana unamaanisha nini?”
Kaguta akatoa pochi yake mfukoni.
“Unanidai shilingi ngapi?”
Bhoke akasonya.
“Unadhani kama nilikuwa nataka pesa nisingekuambia muda wote huo? … Nakutaka wewe Benson, sijui Kaguta, vyovyote vile.”
“Unan’taka mimi?”
“Ndio. Nataka penzi ulilonipa liwe la kwangu tu.”
“Una wazimu wewe enh?”
“Ndio. Penzi lako lanipa wazimu.”
“Bhoke, tafadhali naomba uende. Unajua wale ni watu wa heshima sana. Unaniharibia picha yangu kwa kabisa.”
“Kwahiyo?”
“Nenda, tutayamaliza baadae.”
“Ole wako usinitafute.”
Bhoke akaondoka. Kaguta akashika kiuno.
“Aisee! Yani nimekimbia kule nije huku kumbe ndiyo nimeyakuta huku huku.”
Alitikisa kicha chake akang’ata lips.
“Kaja lini huku huyu mwanamke? … Mungu wangu!”
Aligeuza akawarudia wenzake akakuta kiti cha Sandra kitupu. Vitalis akamwambia:
“Ameondoka. Pole kwa maswahibu.” Kisha akatabasamu.
Hawakuchukua tena muda mrefu hapo, wakalipia bili na kuondoka zao. Kaguta aliwarudisha Vitalis na Bernadetha nyumbani yeye akaenda zake kwa madai ya kumfuata Sandra. Vitalis na Bernadetha wakaingia ndani wakawakuta Miraji amelala pembeni ya tanakilishi huku Bakari akiwa hajielewi usingizini kwenye kochi. Vitalis alimnyanyua mmoja mmoja akawapeleka chumbani na kuwafunika na shuka. Bernadetha alisimama mlangoni akimtizama Vitalis akiwafunika shuka wanausingizi. Vitalis alitoka chumban akamtizama Bernadetha kwa sekunde kadhaa, Bernadetha akasema:
“Una nguvu kweli. Umewabeba watu wazima hivyo.”
Vitalis akainama na kumnyanyua Bernadetha.
“Hata wewe naweza kukubeba.”
Alimpeleka chumbani akamlaza.
“Nakutakia usiku mwema. Nimefurahi sana kuwa na wewe usiku huu.” Kaguta alisema kisha akatoka chumbani. Bernadetha akavuta mto na kuukumbatia kwanguvu. Alitabasamu mwenyewe akajisemea:
“Ahsante kwa kurudisha furaha yangu.”
Masaa yakakimbia usiku ukakata. Asubuhi ya saa tatu, Miraji na Bakari walikuwa pamoja na Vitalis kwenye meza ya tanakilishi. Miraji akachukua karatasi yake aliyokuwa anaiandikia, akasema:
“Kuna habari nzuri na mbaya. Nianze na ipi?”
“Mbaya.” Vitalis akajibu.
“Habari mbaya ni kwamba, hatujapata njia ya kuwakamata mapacha watatu.”
“Na nzuri?”
“Habari nzuri, tumepata watu ambao kwa njia moja ama nyingine wanahusika na tendo hili la kisanyansi.”
***
☆Steve