Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

***SEHEMU YA THELATHINI NA NNE***




(MSIMU WA 02)






Ilichukua siku tatu tokea Sandra alipofuatwa na wanaume mapacha watatu ndani ya suti. Siku ya nne Vitalis akiwa kwenye kitanda chake cha hospitali, wageni watano walikuja kumuona: Jombi, Miraji, Sandra, Kaguta na Bakari, pamoja nao alikuwepo pia Bernadetha, jumla wakawa sita. Baada ya kujuliana hali, Kaguta alichukua fursa kumwambia Vitalis kile kilichowaleta:





“Vitalis, hawa unaowaona hapa mbele yako kwa njia moja ama nyingine wameathirika na Mr Kim. Wamepoteza wazazi wao na hata watu wao wa karibu kwasababu ya huyo mshenzi. Wamenifuata na kunieleza adhma yao, nami nikaona ni busara kuja kukueleza, kwamba wanataka kushiriki kuhakikisha wanampoteza Mr Kim. Wanataka kusaidia pia kuwaokoa wengine wasije wakawa kama wao. Tafadhali wape nafasi.”




Vitalis kimya.




“Kumbuka Vitalis, familia yako ipo wapi sasa? Mkeo, watoto wako? Je ni wangapi huko wanaendelea kupoteza wapendwa wao? Kama tusipochukua hatua leo, kesho itakuaje? Vilio vingapi vitaendelea huko mtaani? Wangapi watapoteza ndoto zao?”



Vitalis kimya. Bakari alisonga mbele akampokea Kaguta:
“Najua hunifahamu vyema, Vitalis, ila natumai hiki nitakachokuambia kitakugusa kwa njia moja ama nyingine.”




Bakari aliweka kituo kisha akaendelea:




“Miaka mitano nyuma ya hapa nilikuwa mfanyakazi wa kampuni kubwa ya mawasiliano Afrika ya mashariki. Kazi yangu ilikuwa ipo chini ya kitengo cha taarifa na teknolojia. Kipindi hiko, si tu niliweza kumudu maisha yangu bali pia ya wazaziwangu waliokuwa wananitegemea.Lakini baadae mambo yalikuja kubadilika baada ya Mr Kim kumuua bosi wetu kwa kile kilichosemekana ni kugeukana kwenye biashara.





Baada ya hapo maisha yakawa magumu, alikuja bosi mwingine lakini alishindwa kumudu kampuni mwishowe kampuni ikapata hasara na kulazimu kupunguza wafanyakazi, mmojawao kati ya waliofukuzwa ni mimi. Sikuja kupata kazi tena baada ya hapo haikujalisha mara ngapi nilizunguka na vyeti. Wazazi wangu nao je?





Maisha yalikuwa magumu kupita kiasi, mwishowe mama yangu alijiingiza kwenye biashara ya kujiuza tupate kula. Bahati mbaya alikuja akaukwaa ukimwi na kumuambukiza na baba pia, wote wakafa. Kwakuwa sikuwa na mbele wala nyuma, ikabidi nijiunge kwenye kundi la Mr Kim baada ya kushawishiwa na mwenzangu niliyefukuzwa naye kazi. Nikajiingiza humo, tukawa tunatumwa kuua watu mbalimbali.





Ila ilifikia muda nikachoka kufanya mauaji, nilifuta tattoo mwilini wangu pasipo yeyote kujua. Yote nilifanya ili niachane na matendo yao, lakini kabla sijakamilisha misheni yangu ndipo nikafanya kosa la kuwavujishia siri ya Alwatan Kombo. Mpaka sasa ninapoongea na nyie wenzangu watatu wameshauwawa na mimi natafutwa kwa udi na uvumba niuwawe. Najua nitakufa, ila basi nife nikiwa napigania dhamira safi, hata mara moja.”




Bakari alimaliza kueleza simulizi yake akakaa kando. Wote wakaamtizama Vitalis kwa macho yanayongoja jibu.




“Sawa. Naombeni nipate wasaa wa kufikiri.” Vitalis alisema kwa upole. Wageni wakaaga akabakia Bernadetha peke yake. Vitalis akamuuliza Bernadetha:
“Wewe unasemaje? Maoni yako ni yapi?”



Bernadetha akabanwa na kigugumizi.



******
☆Steve
 
***SEHEMU YA THELATHINI NA TANO***



(MSIMU WA 02)







Ilipita wiki moja, Vitalis akaruhusiwa kurudi nyumbani. Baada tu ya siku moja kikao kiliitishwa kati ya Vitalis, Kaguta, Miraji, Jombi, Bernadetha, Sandra na Bakari. Katika kikao Vitalis akatoa jibu lake kwamba ameridhia kurudi katika uwanja wa mapambano. Ila akatoa usia:



“Itatakiwa tutumie njia za kisasa zaidi kwa sasa.”




Kutimiza hilo, siku iliyofuata vifaa vilinunuliwa; vinyago, gloves, darubini, nguo nyeusi, mikasi, visu, kamba, vinasa sauti, radio call, tracker, mabuti na hata ramani kubwa ya Tanzania. Pia vikainishwa vipaumbele vya mapambano:




Kwenda kisiwani kukata mzizi wa fitna


Kutafuta na kuwakamata maaskari wanaoshirikiana na kundi la Mr Kim.


Kutafuta mawakala wote wa Kim. Wakianza na Isaac Makongo.


Kuwabana mawakala waeleze Kim alipo.


Kuwatafuta wanaume mapacha watatu.


Kukamata simu na vifaa vyovyote vya mawasiliano vya maadui kwa ajili ya kuwapa taarifa wazitakazo. Mtendaji akiwa Bakari.


Kumaliza na kufunga kila jengo linalotoa mafunzo ya kumtumikia bwana Kim.


Baada ya hapo kundi likapewa jina la THE GUESTS, yani kumaanisha ‘wageni.’




*** NDANI YA MDOMO WA MAUTI ***


Ilichukua juma moja kufuzu mafunzo ya kufyatua na kulenga risasi kwa wasio weza, Sandra na Bernadetha. Baada ya hapo, ikachukua tena majuma mawili kuwekana sawa kwa mazoezi mbalimbali kama vile kukimbia, kuruka, na hata kubana pumzi ndani ya maji, Vitalis na Kaguta wakiongoza wenzao. Walipomaliza hapo, sasa ikachukua tena juma moja kuelekezana jinsi ya kutumia kisu kama dhana pekee iliyo mkononi.






Kurusha kisu kwenye miti, kukata na kufunga na kuchimba kwa kutumia kisu. Hapo sasa ikawa imechukua mwezi mmoja rasmi kumaliza hayo. Siku iliyofuata wakiwa ndani, Bakari aliwafungia vifaa vya umeme mwilini kwa ajili ya mawasiliano. Kila mtu aliwekewa track na kupewa kisafirisha sauti kwa ajili ya kuwasiliana na wenzake.






Walivaa nguo nyeusi za kubana miili, gloves mikononi, na kofia za kufunika vichwa vyao, miguu yao ikaezekwa na viatu vikubwa vilivyobanwa vyema na kamba. Mabegi yao madogo yakajazwa kamba, risasi, mikasi, darubini, na chakula kidogo kilichofungwa kwenye kikontena kidogo cha kubana. Mikanda yao ikabebelea vifuko vya visu vikubwa. Kisha wakajiweka kwenye gari la Kaguta na kuanza safari ya kuelekea bwagamoyo.





Bakari pekee ndiye alibaki, alikaa na tanakilishi yake akiitumikisha satelaiti impe madadavuo ya maeneo yote ambayo wenzake wanakatiza, na hata kuwaelekeza pale panapohitajika. Kisafirisha sauti chake kilikuwa mdomoni, na pembeni yake aliweka kikombe cha kahawa alichokuwa anakipeleka mdomoni mwake kumpasha joto na kumfanya mchangamfu.




Kwakuwa gar aliendesha Kaguta, ndani ya muda mfupi ‘wageni’ walikanyaga ufukwe wa bwagamoyo. Walikodi boti ikawapeleka kisiwani na kuondoka zake. Hakukuwa na maajabu ya boti kupotea wala kuondoka yenyewe, labda kwakuwa jitu halikuwa na taarifa. Kabla ya kuenenda ndani ya kisiwa, Vitalis aliwasogeza wenzake karibu wakapeana maneno mawili matatu.





“Tunaweza tukapoteana humo ndani, hakikisha unawasiliana na wenzako kadiri inavyowezekana. Sawa?”
“Sawa!”
“Na pale utakapopotea, wasiliana na Bakari. Sisi tunamsikia lakini yeye anatuona pia. I know we can make it. Hii ndiyo hatua yetu ya kwanza, hatutakiwi kuipoteza kwa gharama yoyote.”




Waliweka mikono yao katikati wakigusana viganja. Wote wakasema:




“Sisi ni wageni wasio na mualiko. Mwenyeji umejiandaa?”





Walipeana matabasamu wakaifuata njia nyembamba iingiayo ndani. Baada ya hatua kadhaa, upepo ulitokea kusipojulikana ukawazoa na kumsambaratisha kila mtu sehemu yake. Baada ya kudondokea sehemu mpya, Vitalis alituma sauti yake kuuliza hali ya kila mmoja, wote wakasema wako sawa.




“Hakikisha unashikilia bunduki yako vyema. Focus!” Vitalis alisema kwa kujiamini. Wote wakafuata maelekezo. Macho yalitoka na mkono ukashikilia dhana kwanguvu.




“Kila mtu aende upande wake wa kaskazini, mtakutana baada ya kilometa mbili.” Taarifa ilitoka kwa Bakari, wote wakaipata na kuanza kuifuata.




Sandra alikuwa wa kwanza kujaribiwa. Akiwa anatembea kwa umakini, masikio yake yalimpa taarifa kuna kitu kinasogea. Alituma kichwa chake kila upande lakini hakuona kitu zaidi tu ya miti, miongoni mwao ukiwa wa mchungwa.





Basi akaendelea kutembea mbele akielekea kaskazini, ila hakupita muda mrefu, akasikia tena sauti na alipogeuka kutizama hakuona kitu, ila kuna jambo aligundua, mti wa mchungwa ulikuwa umesogea, haukuwepo pale alipouona mara ya kwanza. Kama vile hakugundua hilo, Sandra akaendelea kujongea kwenda mbele.





Punde sauti ya kitu kusogea iliita tena. Sandra aligeuka haraka kutizama na kuelekeza bunduki yake kwenye mti wa mchungwa, kabla hajafyatua risasi, mzizi wa mchungwa ulitambaa haraka ukakamata miguu ya Sandra na kuivuta, Sandra akadondoka, bunduki ikarukia kando. Mzizi ukaanza kumvuta Sandra karibu na mti. Sandra alitoa kisu haraka kiunoni mwake, akakata mzizi unaomvuta kisha akataarifu wenzake hali aliyopo.




“Hold on, nakuja muda si mrefu!” Sauti ya Kaguta ilimwambia Sandra.





Mzizi mwingine ulikuja haraka ukamchapa kibao Sandra na kumchana shavu. Ulimshika mkono wenye kisu ukaugongesha kwenye mti, Sandra akaachia kisu. Mzizi mwingine ukaja haraka ukakamata mguu wa Sandra na kuanza kumvuta tena kusogelea mti, wakati Sandra anavutwa alinyoosha mkono atwae bunduki yake iliyokuwa chini hatua kadhaa, mzizi mwingine ukasukumiza bunduki mbali.





Sandra akasogezwa karibu na mti, mizizi mingine ikachipuka na kumviringita kisha ikamnyanyua juu na kumtupia kwenye mti mwingine, Sandra akafikia mgongo na kudondoka kama mzigo. Alitoa sauti kali ya maumivu huku akiukunja mgongo wake.






“Nakuja Sandra, nipo karibu!” Sauti ya Kaguta ilisikika masikioni mwa Sandra.
“Kaguta fanya haraka!” Sauti ya Vitalis nayo ikasikika.
“Umekaribia kumfikia. Kimbilia upande huo huo.” Bakari naye alisikika akitoa maelezo.





Wakati Sandra akiwa anaugulia mgongo chini ya mti alikotupiwa, mzizi wa mchungwa ulikuja kwa kasi kama mkuki ukifuata kichwa chake, alikwepa mzizi ukachoma mti. Alitaka kunyanyuka, mzizi mwingine ukakamata mguu wake na kumdondosha kisha ukaanza kumburuza tena kufuata mti.




Wakati anasogezwa Sandra alipitishwa juu ya kisu chake, alikichukua kwa siri akaficha mkono nyuma, mzizi ulipomsogeza karibu na mti kama awali mizizi mingine ikaamka na kuanza kumpanda Sandra kuanzia miguuni huku ikimbinya kwanguvu. Ilipofika kiunoni, Sandra alipiga kelele kali ya maumivu, kabla ya mizizi kummalizia kumfunga tumboni na kifuani ilimsogeza karibu zaidi, Sandra akaona macho ya mti huo.






Yalikuwa makubwa na ya kijani mfumo wake ukiwa wa kenge.Hapo hapo Sandra akatoa kisu chake na kukikita kwenye macho hayo kwanguvu. Maji ya kijani yakaruka kama mafataki. Mti ukalalamika kwa kuyumba yumba huku na huko. Mizizi ikafunguka na kumuacha Sandra akadondoka chini, Sandra akiwa amebung’aa hapo, mti wa mchungwa ulidondoka na kumfunika. Alijitahidi achomoke lakini haikuwezekana, alibanwa.





Aliishia kupiga makelele ya kuomba msaada. Bahati njema Kaguta akawasili. Alimvuta akamchoropoa toka chini ya mti.
“Upo sawa?”
“Yah! Nipo okei.”
Kaguta aliutizama mti wa mchungwa kisha akamtizama Sandra.
“Upo vizuri, mama.”
“Ahsante.”





Sandra alichomoa kisu chake akakirejesha kiuoni. Mara sauti ya kelele ikawafikia masikioni kupitia earphone zao. Ilikuwa ni sauti ya Miraji ikiomba msaada. Ikafuatiwa na sauti ya Bakari.





“Miraji amebebwa. Anapelekwa upande wenu wa magharibi kwenu Bernadetha, Vitalis na Jombi, na kwa Kaguta na Sandra ni upande wa kaskazini magharibi. Fanyeni haraka!”





Haraka wote wakaanza kukimbia kuelekea kule walipoelekezwa.





Miraji alikuwa hewani akiwa amebebwa na ndege wa ajabu, alikuwa ni mweusi ti mwenye mdomo mrefu kama chuchunge. Mabawa yake yalikuwa mapana na yenye nguvu ingali macho yake ni mekundu yenye muundowa paka. Miraji hakuweza kufurukuta kwa ndege huyo aliyekuwa kamkamata mkono wake wa kuume na kucha zake zikiwa zimemtoboa.






Alijaribu kuutuma mkono wake wa kushoto kwenda kwenye mfuko wa suruali uliokaa upande wa kulia ili atoe kisu, lakini akashindwa. Upepo ulikuwa mkali na alihisi kupata maumivu zaidi. Hakukata tamaa, alijaribu tena akafanikiwa.





Alikata mguu wa ndege, ndege akamuachia akadondoka chini. Alifikia ubavu akalalamika kwa maumivu makali begani na kiunoni. Alitizama juu kumtizama ndege, ajabu akaona ndege watatu wakiwa wamefanana kama yule aliyembeba. Na mara wale ndege wakaanza kushuka kwa kasi wakimfuata Miraji. Miraji alinyanyuka akaanza kukimbia. Aliweka mkono wake sikioni akamuuliza Bakari:





“Nipo wapi?”
“Unaelekea kusini.” Bakari alijibu. “Nenda upande wako wa mashariki, wenzako wapo upande huo!”





Miraji aligeuza akaanza kuelekea upande wake wa mashariki. Hakufika mbali ndege mmoja alimsukuma na miguu akadondoka chini. Miraji kunyanyuka akakuta kazungukwa na ndege watatu.





Alivua begi lake akataka kuingiza mkono, ndege mmoja akatuma bawa lake likamzaba Miraji na kusogeza begi kando, kisha akamrukia Miraji na kumdonyoa shingoni kwanguvu huku miguu yake ikiwa juu ya kifua cha Miraji. Miraji alifurukuta kumtoa ndege juu yake lakini haikuwa rahisi kwani ndege aliweza kujibalansi na mbawa zake huku akimdonyoa maeneo mbalimbali.






Ilimchukua muda Miraji kuweka kisu chake vizuri mkononi na kukisokomeza kifuani mwa ndege aliyekuwa anamshambulia. Ndege akapiga kelele kali za kulalamikia maumivu aliyoyapata, Miraji akanyanyua mguu wake na kumsukumizia pembeni kisha akanyanyuka na kuanza kukimbia mbio za sakafuni ambazo hazimkufikisha mbali. Ndege wawili waliobakia walimuangusha chini, mmoja akakanyaga mikono ya Miraji na mwingine miguu, Miraji akabakia pasipo ujanja.





Ndege mmoja alipiga kelele za nguvu kwenye uso wa Miraji. Mate yalimtoka na kuingia mdomoni mwa Miraji aliyekuwa ameachama kwa mduwazo. Japokuwa Miraji alitema, lakini alikuwa kachelewa. Ndege alinyanyua shingo yake kwanguvu ammalize mhanga wake, ila mara sauti ya mlio wa bunduki ikavuma, kufumba na kufumbua ndege wote wakamdondokea Miraji wakiwa wafu.





****
☆Steve
 
Endelea tena steve

nataka kujua insp.vitallis anarudije kwenye game...
maana tumehama kabisa kutoka kwa kina mtenvu,k square,pius na wenzake......

mwaga vitu mkuu steve leo ndo leo

Tushamaliza, ongeza dozi Mkuu!

Nakaza macho vizurii sichezi mbali Steve

mkuu endelea basi

tupo pamoja mkuu
Nishafanya yangu. Tukitane tena saa tatu usiku.

☆Steve
 
Jamani saa tatu ya usiku kwa majira yapi mbona inaelekea saa nne!!?
Nasubiri mwendelezo wa ambush ya kisiwani make tayari mchungwa, madege3 wapo chini bado mtu wa mbao(sijui ndo jitu jeusi!), tik tok tik tok na wafuasi wenyewe!
Patamu hapo...!
 
***SURA YA THELATHINI NA SITA***



(MSIMU WA 02)






“Upo sawa?” Sauti ya Vitalis ilimuuliza Miraji aliyekuwa kabakizwa uso tu, mwili mzima ukiwa umefunikwa.
“Watoe hawa wadudu juu yangu!” Miraji aliropoka. Vitalis alitabasamu akamsaidia kuwaondoa ndege. Miraji alinyanyuka akamshukuru. Hawakukaa hapo muda, taarifa ikaingia toka Bakari:
“Bernadetha yupo matatizoni, Vitalis na Jombi rudini mashariki yenu mpo karibu naye!”
Vitalis alimtizama Miraji akamwambia;
“Acha niende!”
“Twende wote!” Miraji aliroroja.
“Hapana, umejeruhiwa. Niruhusu niende haraka. Utakuja nyuma yangu.”




Baada ya kusema tu hayo, Vitalis alifunguka haraka kurudi mashariki yake. Alikimbia kwa nguvu zake zote, mikono na miguu yake vikipishana kama treni ya umeme.





Baada tu ya punde alikuwa kamuacha Miraji mbali mno. Ila mara akasikia sauti ya Jombi, ikabidi asimame na kutizama pande zote kuona yupo wapi atoaye sauti. Punde akamuona Jombi anatokeza upande wake wa kushoto akikimbia kama mwehu.



“Kimbia, Vitalis. Kimbia!”




Kabla Vitalis hajachukua hatua yoyote, aliona mbwa mwitu wakubwa weusi wakimfuata Jombi kwa kasi. Vitalis aliwapiga risasi mbwa mwitu wawili na kuwaua akachelewa kumlenga mwingine ambaye alimrukia na kumdondosha chini, akamng’ata mkono wake wa kushoto.




Vitalis alimpiga ngumi mbwa mwitu kwa kutumia mkono wake wa kulia kisha akaishika shingo ya mbwa huyo na kujinyanyua akakaa juu ya mgongo wa mnyama huyo. Aliweka bunduki yake kiunoni. Alichomoa kisu chake akamchanja mbwa mwitu, mbwa mwitu akaanza kukimbia.





Vitalis akakamata masikio ya mbwa huyo na kuyatumia kama usukani akimuelekeza mbwa kuelekea upande wa mashariki. Mithili ya farasi, Vitalis alimtumia mbwa mwitu. Baada ya muda mfupi Vitalis akafika eneo alilopo Bernadetha, alichomoa kisu akamchoma mbwa mwitu mgongoni kisha akajirusha kando.





Mbwa mwitu alidondoka akafa. Vitalis akakimbia kumfuata Bernadetha aliyekuwa anakimbizwa na jitu lililofanania na mti mkavu. Lilikuwa na matawi na hata majani.




“Wewee!” Vitalis alipaza sauti. Mti ukageuka na kumtizama.
“Unanikumbuka? … Nimekuja tena. Unakumbuka nilichokufanya?”




Mti uligeuka ukaanza kumfuata Vitalis.





“Yeah! … Njoo kama una jiamini mti usio chimbwa dawa wewe!”




Mara mti ukaanza kukimbia. Vitalis aligeuka naye akaanza kukimbia.




“Bakari, nielekee wapi?” Vitalis aliuliza.
“Endelea kwenda mashariki yako, utakutana na Kaguta na Sandra.” Sauti ya Bakari ilijibu. Vitalis akaelekea upande huo.
“Kaguta!”
“Yeah!”
“Nakujaa na mti mkavu upande wako. Andaa moto, haraka!”
“Nitapatia wapi moto sasa?”
“Utajua. Andaa moto haraka!”



Kaguta alimtizama Sandra akamuuliza;



“Tunafanyaje sasa? Vitalis anakuja!”



Sandra alitizama kushoto na kulia kwake, akaanza kukusanya miti na majani makavu.



“Tunapata wapi moto sasa?” Kaguta alimuuliza Sandra. Sandra akamuonyeshea Kaguta saa yake ya mkononi.
“Tutatumia saa yako. Si ina lenzi?”




Kaguta aliitizama saa yake akajibu;




“Nadhani.”
“Chuchumaa, kioo cha saa yako kielekezee juani na kwenye majani haya makavu. Haraka!”




Kaguta alifanya kama alivyoelekezwa, mara moshi ukaanza kutoka baada ya dakika. Kabla moto haujakoza, Vitalis akatokeza.




“Tayari?”
“Bado kidogo!”
“Fanyeni haraka!”




Vitalis alisema huku akiendelea kukimbia kuwapita wenzake, nyuma yake mti ukiendelea kumfukuza. Baada ya muda akarudi tena.




“Kaguta, tayarii?!”
“Ndio!”
“Tumia kamba. Upesi!”




Kaguta alitoa kamba akafunga kitanzi kisha akairusha kwa mtu mti na kuanza kumvutia kwenye moto ambao ulikuwa umekoza sasa. Sandra naye alishika kamba akawa anamsaidia Kaguta, Vitalis naye akawaunga mkono wakamvuta mtu mti mpaka kwenye moto. Mti ukashika moto, ila nayo kamba ikakatika. Mtu mti ukaanza kukimbia hovyo hovyo ukielekea kaskazini.




“Kaskazini kuna kitu gani, Bakari?”




Vitalis aliuliza.




“Kuna mto!” Sauti ya Bakari ilijibu. Vitalis akawatizama Kaguta na Sandra akawaambia;
“Anaelekea mtoni kuzima moto. Inabidi tumzuie!”




Haraka wakaanza kukimbia kumfuata mtu mti. Vitalis alitoa kamba yake akatengeneza kitanzi. Aliirusha kwa mtu mti ikamkamata wakaanza kuivuta kwanguvu. Baada ya muda kidogo kamba ikakatika tena, mtu mti akaendelea kukimbia, ila hali yake ikiwa mbaya, matawi yalipukutika na moto ulizidi kumtafuna.





Mpaka anafika mtoni alikuwa tayari ameishakwisha. Vitalis alishusha pumzi akashika kiuno. Waliwasiliana na wenzao, wote wakakutana kwenye kingo ya mto kasoro Jombi.




“Upo wapi, Jombi?” Kaguta aliuliza kwenye kisafirisha sauti.



Kimya.



“Bakari, Jombi yupo wapi?”
“Yupo upande wenu wa magharibi.” Sauti ya Bakari ilijibu. Wote wakaanza kuelekea upande huo. Wakamkuta Jombi amelala chini hoi, pumzi tu ikionyesha yu hai.
“Jombi, kuna nini?” Kaguta aliuliza. Jombi akajibu;
“Saa … Saa imeanza kutoa majaribu yake.”
“Imetoa muda gani?”
“Dakika kumi kumi. Tayari jaribio la kwanza limeshapita, nimepambana nalo.”




Kaguta alitizama saa yake akaona haisemi majira. Vitalis alitizama na ya kwake pia, akaona haisemi majira sahihi.




“Inabidi tumtafute huyo mtu anayetoa hayo majaribu.” Vitalis aliwaambia wenzake.
“Tutampatia wapi?” Kaguta aliuliza.
“Lazima tu kuwe na njia.” Vitalis alijibu, “Tuifuatishe hii barabara.”




Kabla hawajachukua hatua, jaribio lengine la saa lilitokea. Upande wao wa kushoto walitokea watu wanane mbilikimo, nyuso zao zilikuwa zimepambwa na michoro ya ajabu, walikuwa wamevaa sketi za makuti, miongoni mwao wawili tu ndio walikuwa wameshikilia panga kila mkono.





“Nini hiki?” Sandra aliuliza. Bernadetha akaachama mdomo kwa mshangao.




Mara wale mbilikimo wakajitenga katika mafungu ya watu wanne wanne, wakabebana mabegani na kutengeneza watu wawili warefu, wale mbilikimo wenye mapanga wakawa ndio wapo juu. Vitalis na Miraji wakachukua kundi moja la mbilikimo, Kaguta na Jombi wakachukua kundi lililobakia.




Vitalis alirusha ngumi, mbilikimo wa kati akainama na kumfanya wa juu akwepe kisha panga likarushwa na kukata shati la Vitalis. Vitalis alipotizama pembeni yake akaona Kaguta na Jombi wamerushwa chini.




“Wow! Kumbe its serious.” Alisema Vitalis.




Miraji alirusha teke kumpiga mbilikimo wa juu, wa katikati akamrusha juu mwenzake, teke likapita, aliporejea mwenzake akamdaka mikono na kumrusha kwa Miraji, Miraji akasombwa na teke akarushwa huko. Vitalis akamnyanyua na kumnong’oneza;




“Focus na wa katikati, mimi nitadeal na wa chini. Wa juu hana kitu.”




Miraji aliitikia, wakaanza upya mchezo wakilenga mashambulizi kwa mtu wa chini na katikati, mbilikimo wa juu akawa mzigo kwa wenzake. Ndani ya muda mfupi wakawamaliza. Kaguta na Jombi wakatumia risasi kuwamaliza wa kwao baada ya kushindwa kuwamudu.






“Sasa tunafanyeje?” Miraji aliuliza.
“Unadhani tutafanikiwa?” Bernadetha naye akauliza.




Vitalis alitizama saa yake ya mkononi akaona mshale wa dakika unasogea tokea ilipokuwa namba tatu kwenda namba nne.Alimfuata Jombi akamuuliza;
“Jaribio la kwanza lilitokea upande gani?”




Jombi akanyooshea kaskazini. Vitalis akatabasamu.




“Yes! Sasa nimeelewa. Wakati unapata jaribu la kwanza mshale wa dakika ulikuwa juu, ndio maana jaribu likatokea kaskazini. Mshale ulipofika mashariki, yaani namba tatu, jaribu likatokea upande huo.”




“Kwahiyo?” Kaguta aliulza.



“Kwahiyo haya majaribu yanarandana na muelekeo wa mshale wa dakika. Sasa hivi jaribu linalokuja litatoka mashariki kusini kwakuwa dakika kumi zingine mshale wa dakika utakuwa kwenye namba tano. Kwahiyo ili tupate chanzo chake lazima tujue dakika zinaanzia wapi na kukomea wapi.”




“Kwenye kumi na mbili!” Sandra alilonga.



“Yap! Kwahiyo tuelekee kaskazini yetu haraka kabla mshale haujafika kwenye tano.” Vitalis alitema maneno. Upesi wakaanza kukimbia kwenda upande wa kaskazini. Ikiwa imebakia sekunde kadhaa mshale wa dakika ufike kwenye tano, wakawa wamefika sehemu moja walipokuta jicho kubwa la kijani. Vitalis akatabasamu na kusema;





“Here we are! Hapa ndipo majaribu yanapotokea. Hili ndilo jicho linaloona kila pande kwa ajili ya jitu jeusi.”




Walishindilia risasi kwenye hilo jicho likapasuka na kutoa ute wa kijani. Walikumbatiana na kupongezana. Hatimaye wakawa wametoka kwenye mdomo wa mauti.


***

☆Steve
 
Jamani saa tatu ya usiku kwa majira yapi mbona inaelekea saa nne!!?
Nasubiri mwendelezo wa ambush ya kisiwani make tayari mchungwa, madege3 wapo chini bado mtu wa mbao(sijui ndo jitu jeusi!), tik tok tik tok na wafuasi wenyewe!
Patamu hapo...!
Muendelezo tayar mkuu.

☆Steve
daah safi mkuu steve burdaani itaendelea saa tatu leo hakuna kulala
Bampa to bampa. Nitachelewa tu ila si kwamba situmi!

☆Steve
steve njoo bas
Nshakuja mama angu.

☆Steve
steve hujarudi tu kutoka kwa alwatan kombo?
Hahaha nsharudi!

☆Steve
Mia mkuu Steve ,good job.
Ila daaah,alwatan Kombo arobaini yake imefika ,sioni akichomoka hapa.
Mkuu soma kazi hiyo.

☆Steve
 
Muendelezo tayar mkuu.

☆Steve

Bampa to bampa. Nitachelewa tu ila si kwamba situmi!

☆Steve

Nshakuja mama angu.

☆Steve

Hahaha nsharudi!

☆Steve

Mkuu soma kazi hiyo.

☆Steve
weka bas steve tupate za kulalia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom