Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Mkuu SteveMolel tuachie kaborudani ka weekend mkuu pls ni ombi lakini samahani kama nitakuwa naingilia mipango ya ratiba zako
 
USHAHIDI WA HONGO una kesi mbili za kujibu hapo pamebipa raha sana maana huyu mkurugenzi alifikiri palaini kumbe ni mwamba wa bahari haulainishwi kwa maji
Kaikanyaga!
 
Ngoja nianze nikija kufika mlipo itakuwa ishaisha
 
***SURA YA THELATHINI NA MOJA***





(MSIMU WA 02)





Ikiwa ni asubuhi ya saa mbili watu walikuwa wamejazana kwenye kijiwe cha magazeti kilichokuwa kimejiweka pembezoni mwa barabara kuu ya lami. Walikuwa wanateta juu ya vichwa vya habari pasipo kuonekana hata mmoja akiwa amebebelea gazeti mkononi.



Kundi hilo lililokuwa na watu wanne liliongezeka baada ya Kaguta kusogea na kurusha macho yake kwenye vichwa vya habari, gazeti moja likakamata macho yake.



‘SIMANZI: KIJANA MMOJA AUWAWA KINYAMA KWA RISASI KUMI’




Kichwa cha habari kilijieleza kikiambatana na picha ya kijana huyo ambaye alikuwa amechafuka damu. Kaguta alitoa shilingi elfu moja mfukoni mwake akampatia muuzaji na kumnyooshea kidole gazeti atakalo, muuzaji akampatia.





Kaguta akalisogeza gazeti machoni na kuanza kuitizama ile picha ya muhusika aliyeuwawa kwa risasi kumi. Mara mmoja wa wale waliokuwa wanajadili vichwa vya habari akaanza kuhororoja:




“Unamtizama huyo jamaa? … Unaweza ukamuona huruma ila mshenzi kama nini!”
Mara mwenzake akauliza:
“Nani huyo?”
“Si Roby!” Jamaa akajibu. Basi majadiliano yote yakahamia kwenye lile gazeti alilonunua Kaguta.
“Muuaji kauwawa hatimaye. Ila nani atakuwa kamuua?”
“Watakuwa wameuana wenyewe hao. Si unajua hawa madili yao ya madawa?”
“Kweli, hata mimi nahisi hivyo. Unakumbuka siku ile huyu jamaa alipita na gari kwa kasi tulipokuwaga kule magomeni?”
“Alikuwa anaendesha Prado?”
“Ndio, nyeusi hivi.”
“Eeeh … nakumbuka!”
“Sasa pale si alikuwa anaenda kwa yule Niga c. He! Baadae nakuja kusikia Niga c kauwawa na risasi mwanangu!”
“Walimuua yule!”
“Ndio mana yake, cha kushangaza hata mshkaji hakufuatiliwa wala nini!”




Kaguta alifunga gazeti lake akaondoka lile eneo. Alielekea hospitalini kwenda kumjulia hali Vitalis, alipomkuta mlengwa wake kalala alifungua gazeti lake akawa anasoma habari ya Roby. Alizama gazetini mpaka pale alipokuja kushtuliwa na Bernadetha.





“Umekuja saa ngapi?”
“Muda si mrefu sana. Vipi unaendeleaje?”
“Safi tu. Mbona hujamuamsha Vitalis?”
“Sijataka kumsumbua, mwache tu apumzike.”
“Hapana. Anatakiwa aamke anywe chai saa hivi.”
“Iko wapi?”
“Namletea hivi punde.”





Bernadetha alimuamsha Vitalis akaketi kitako. Baada ya kujuliana hali, Kaguta alimuonyesha Vitalis gazeti aliloninunua, Vitalis akapitia yaliyomo, alipomaliza Bernadetha naye akalichukua na kulisoma.





“Nani atakuwa kamuua?” Vitalis alimuuliza Kaguta kwa mshangao.
“Watakuwa ni wakina Isaac Makongo.” Kaguta alijibu.
“Umejuaje?”
“Hujaona pale kwenye gazeti?”
“Sijaona sehemu iliyosema kauwawa na wakina Isaac.”
“Kauwawa maeneo Oysterbay na huo mtaa naujua. Pembezoni mwake mbele kidogo kuna nyumba kubwa ina namba 898.”
“Ila Isaac anaishi Kurasini.”
“Basi jua kati ya yule muhindi ama yule mzungu, Ford, atakuwa anahusika na kifo hiko.”
“Ila kwanini wamuue?”
“Hapo ndipo kuna la kutafuta. Inabidi tufanye utafiti.”
“Tufanye? … mmh mmh hapana! Sijihusishi tena na mambo ya hao watu. I am done, Kaguta.”
“You are done kivipi, Vitalis?”
“Sitaki tena kujihusisha na mambo yoyote ya upelelezi. Sasa hivi mimi ni mwananchi wa kawaida, acha iwe hivyo tu. Kama Mungu akinijalia nikatoka hapa, basi nitaenda kufanya biashara zangu basi.”




Kaguta alimtizama Bernadetha, Bernadetha akapandisha mabega. Kaguta alishusha pumzi ndefu kisha akanyanyuka.





“Nitakuja baadae mida ya jioni. Ila Vitalis, fikiria maamuzi yako mara mbili.”




Kaguta akatoka. Bernadetha akamtizama Vitalis na kutabasamu.





“Mbona unatabasamu?”
“Nimefurahi.”
“Umefurahishwa na nini?”
“Kujua kuanzia sasa utakuwa salama.”



Vitalis alitabasamu akaunyanyua mkono wa Bernadetha na kuuweka kifuani kwake.


****


Gari la Kaguta lilipaki pembezoni mwa baa iliyobebelea jina la Karunde. Ni mida ya saa mbili ya usiku. Kaguta alishuka akiwa kavalia suruali nyeusi ya kadeti, shati jeupe la kubana na koti single button rangi nyekundu aliyoifananisha na viatu vyake vya kuchomeka.




Alinyookea glocery akaagiza kinywaji, alibebelea glasi akapeleka mdomoni na kuria mafundo mawilikabla hajatoa simu yake mfukoni na kutuma ujumbe kwa Sandra.




‘Nipo hapa bar karibu na kwako njoo basi’




Alimaliza kinywaji chake lakini bado Sandra hakutokea. Alinyanyuka akalipa akatoka nje ya bar mpaka kwenye gari lake, akarusha macho yake barabarani pasipo kuomuona mtu. Alianza kutembea taratibu taratibu mpaka nyumbani kwa Sandra.





Aligonga mlango lakini hakuruhusiwa aingie ndani. Aligonga na kugonga lakini hakukuwa na majibu yoyote. Alizunguka nyuma ya nyumba akachungulia kupitia dirishani, akaona miguu ya Sandra ikiwa imelala chini. Alijitahidi auone mwili mzima lakini haikuwezekana, pazia la dirisha lilimkinga.




Haraka Kaguta alirudi mlangoni, alichomoa earphone ya simu mfukoni akaing’ata na kutengeneza waya mnene kiasi alioupenyeza kwenye kitasa akadondosha ufunguo uliokuwemo humo. Akautoa waya na kuupindisha alama ya saba, akaungiza ndani ya tundu ya kitasa na kuuchezesha, mara ikasikika sauti ‘tas!’ mlango ukafunguka.






Kaguta aliingia ndani akamkuta Sandra uchi wa mnyama, pembezoni mwake kulikuwa na pakti ya madawa ya vidonge, mashavu yake yalikuwa na alama nyekundu za vidole, uso umevimba na kuvijilia damu na mdomo wake ulikuwa una mabaki ya mapovu.





Kaguta alikimbilia kabatini akatoa gauni. Alimvika Sandra kisha akambeba na kumkimbizia garini kwake haraka. Aliondoa gari mpaka hospitalini ndani ya dakika mbili tu, alishuka akambeba Sandra na kumuingiza ndani. Alitolewa nje ya chumba cha wagonjwa akaambiwa angoje majibu nje.





Aliketi kwenye mabenchi, akawa amefungamana mikono yake na kuiweka mbele ya mdomo wake. Alikaa hapo kwa muda, hakuna dokta aliyekuja kumpa majibu. Mwishowe alilala kabisa. Alikuja kuamshwa na daktari usiku ukiwa mzito.




“Mgonjwa wako amekunywa madawa: alikuwa anafanya jaribio la kujiua. Na inaelekea alipta kipigo kabla hajachukua maamuzi hayo.”
“Anaendeleaje kwa sasa?”
“Anaendelea vizuri. Tumempa huduma ya kwanza tu. Tunaomba uende kituo cha polisi ukaripoti, hatuwezi mtibia bila hivyo.”




Kaguta alitoa kitambulisho chake cha kazi akamuonyesha daktari. Daktari akasema:
“Okay. Ameomba aonane na wewe.”




Daktari aliposema tu hivyo, Kaguta alianza kutembea. Daktari alimshika mkono akamwambia:





“Fanya haraka. Inabidi apumzike.”




Kaguta alitikisa kichwa akaendelea na safari yake. Alipoingia chumba cha Sandra alikutana macho kwa macho na mwanamke huyo. Sandra akaanza kulia. Kaguta alimsogelea akambembeleza anyamaze.





“Niambie nani kakufanyia hivi?”




Sandra akiwa amekabwa na kilio alisema:





“Isaac … Isaac Makongo. Amemuua Roby, amenipiga na kusema hatambui ujauzito nilio nao. Hataki kuniona tena! Sikudhani kama angekuja kunifanyia unyama kiasi hiki!”




Baada ya hayo maneno, Sandra aliangua kilio kama aliyefiwa. Kaguta alitikisa kichwa chake akamvuta Sandra na kumkumbata. Ila punde, Sandra alizirai. Kaguta alikimbia kwenda kumtafuta dokta akaja naye upesi, daktari alimtoa Kaguta nje afanye kazi yake, baada ya muda daktari alitoka chumbani akampasha Kaguta habari.





“Amezirai tu. Nadhani sasa ni muda wa kumuacha apumzike.”





Kaguta alitoka hospitali akaeleka bar. Alinunua chupa moja kubwa ya konyagi akaiweka mezani taratibu akawa anamiminia kooni kwake kwa pozi. Kabla ya chupa kufika nusu, Bhoke alisogea eneo alilopo Kaguta. Alitabasamu kisha akapaza sauti yake laini:




“Mambo handsome!”





Kaguta alimtizama Bhoke kisha akapandisha nyusi zake.




“Poa, karibu.”





Bhoke alivuta kiti akaketi.




“Niambie, handsome. Kitambo sijakuona.”




Kaguta alitabasamu tabasamu lililo kinyume na macho yake. Alikunywa fundo moja kisha akajibu:
“Mbona nipo tu. Mambo yamebana.”
“Nimekumisi sana. Nichukue kinywaji.”
“Chukua.”




Bhoke aligeuza shingo yake akatazama kaunta.




“We Mishiii naomba castle nyongaa!”





Haraka mhudumu alikuja na sahani inayobebelea castle, akaiweka mezani na kuifungua. Bhoke akaidaka castle akaipeleka mdomoni na kunywa mafundo manne kama vile maji.





“Sasa, leo twaenda wote ama?”
“Hapana!”
“Kwanini? … Umepata mwanamke mwingine baba?”
“Hapana. Nimechoka tu.”




Baada ya kusema hivyo, Kaguta alisimama akamiminia kinywaji chake mdomoni kama vile si konyagi bali juisi au energy drink, alafu akaaga:





“Sasa mi naenda. Tutaonana.” Alisema huku akitoa pesa kwenye pochi yake na kuilaza mezani. Bhoke akabaki akimtizama Kaguta kama mtu anayeshuhudia mtu akimla simba.




Kaguta akautoa mwili wake pale bar na kufuata gari lake, wakati yu njiani kwenye lami mara simu yake ikapokea ujumbe. Mkono moja ulibeba simu na kuipeleka usoni wakati mwingine ukiwa umeshikilia usukani, akausoma ujumbe:




“Hi Peltridge! ts me Rhoda from hospital.”




Kaguta alisonya akaitupia simu yake kwenye kiti cha kando.


****
☆Steve
 
***SURA YA THELATHINI NA MBILI***




(MSIMU WA 02)









Ilikuwa ni jioni, si tu saa ilisema hivyo bali hata nguvu ya jua ilikuwa imepungua na giza lilianza kusogelea uso wa ulimwengu. Mataa ya hospitali yalikuwa yameanza kuwashwa sehemu mbalimbali wakati huo Bernadetha alikuwa nje akimfanyisha mazoezi Vitalis wakitembea toka eneo moja kwenda lingine,Bernadetha alikuwa amemshikilia mkono Vitalis aliyekuwa anachechemea akitembea.




“Sasa hivi angalau sasa, napata moyo.”
“Kwanini?”
“Unajitahidi kutembea. Mara ya kwanza nilikuwa nahofia kweli, nikadhani unakuwa kilema sasa.”
“Kwahiyo tusema Mungu yu pamoja nami, sio?”
“Kabisa.”
“Nashukuru sana. Ila najisikia vibaya kwa kilichotokea leo.”
“Nini?”
“Marietta kuja na kunikuta nimelala. Kwanini hukuniamsha?”
“Sikutaka kukusumbua. Atakuja hata siku nyingine, usihofu.”
“Sijamuona kitambo. Umenikatili, mama.”
“Usifadhaike bwana, atakuja. By the way, umeona zawadi aliyokuletea?”
“Hapana.”
“Nimeiweka kwenye droo. Tukirudi nitakuonyesha.”
“Aisee! Sikupata hata muda wa kumshukuru.”




Vitalis alilalama. Wakati wanaongea, Bernadetha alijisahau akamuachia Vitalis mkono.





“Zawadi yenyewe pipi!”
“Ndio hiyo hiyo! Kwani nilikuwa nayo?”





Mara Vitalis akagonga jiwe na mguu wake wa kulia, alikosa balansi akataka kudondoka, upesi Bernadetha alimdaka na kumvuta kwanguvu akamkumbatia wakawa wanatizamana uso kwa uso, macho kwa macho. Kwa sekunde tano hakuna aliyesema kitu, macho yaliteta. Walikuja kurudishwa fahamuni kwa sauti ya mtu asafishaye koo. Walipokengeuka kutizama wakamuona Miraji.




“Umejuaje tupo huku?”
“Nimeelekezwa na wafanyakazi wenzako mpo mazoezini.”
“Karibu.”
“Ahsante! Sh’kamoo.”
“Marhaba!” Bernadetha na Vitalis waliitikia.
“Nimekuja kumjulia hali mgonjwa, naona anaendelea vyema sasa.”
“Mungu anasaidia. Naendelea vizuri sana tu.” Vitalis alijibu. Walitafuta eneo moja tulivu wakaketi na kuanza kuteta wakiwa wanapata vinywaji vilaini.
“Umesikia habari za mauaji ya yule mtu maeneo ya Oysterbay?” Miraji aliuliza.
“Ndio, nimesikia. Niliona kwenye gazeti.” Vitalis alijibu.
“Yani haijapita hata muda, wameuwawa wengine watatu kama huyo wa Oysterbay.”
“Wapi?”
“Inasemekana maeneo ya Bunju, nyumba namba mia tatu na mbili hivi kama sikosei. Wameshindiliwa risasi za kutosha. Na mashuhuda wanasema waliwaona watu watatu wameingia katika hiyo nyumba wakiwa wamevalia suti kabla ya mauaji hayo kutokea.”
“Umesema Bunju?”
“Ndio!”
“Nyumba namba mia tatu na mbili?”
“Yap! Kama kumbukumbu zangu ziko sawa.”





Vitalis akatulia kwa muda kidogo akiwaza. Picha ya nyumba aliyoingia Bakari kipindi kile wakiwa wanamfuatilia yeye na Kaguta, ilikuja kichwani. Ndio, ilikuwa ni nyumba namba mia tatu na mbili maeneo ya Bunju. Sasa nani kauliwa? Bakari? Vitalis alijiuliza nafsini, mara akakurupushwa na Miraji.






“Vipi? Kuna shida?”
“Hapana! Hamna shida.”
Vitalis alikurupuka. Alipitisha kiganja chake usoni akashusha pumzi ndefu.
“Embu tuachane na hizo habari. Tuongelee mengine.”



Vitalis aliomba.



****



Siku mbili zilipita. Ikiwa ni wasaa wa saa nane ya mchana ikishuhudiwa na jua lililosimama utosini, alikuja mgeni maeneo ya nyumba ya Vitalis. Aligonga hodi mara tatu, sauti toka ndani ikaitikia. Mlango ulipofunguliwa mgeni akaingia.




“Hah! Bakari!”





Jombi alipaza sauti akishangaa. Bakari aliingia ndani akauliza:
“Inspekta Vitalis yupo wapi?”
“Yupo hospitali.”
“Kaguta je?”
“Naye hayupo!”
“Tafadhali, naomba unisaidie. Nina shida nao kubwa sana.”
“Shida gani?”
“Tafadhali naomba unisaidie kuwapata.”
“Ok, karibu, ingia ndani.”




Bakari aliingia akaketi kwenye kochi. Alisalimiana na Miraji kisha akarudisha macho yake kwa Jombi.





“Tafadhali, nakuomba ufanye upesi.”



Jombi alitoa simu yake mfukoni akampigia Kaguta na kumtaka afike nyumbani kwa Vitalis haraka. Alipokata simu akamwambia Bakari.





“Kama dakika kumi na tano hivi, Kaguta atakuwepo hapa.”




Bakari akaridhika. Alilaza kichwa chake kwenye kochi, baada ya muda mfupi akapitiwa na usingizi. Miraji na Jombi wakamuacha apumzike, wao wakawa wanatizama runinga. Ila mara kwa mara Bakari alikuwa akishtuka toka usingizini pale sauti yoyote kubwa kiasi ya runinga ilipokuwa inamfikia.





Kila aliposhtuka alikuwa anakimbizia macho yake dirishani kuchungulia nje kisha anatulia na kulala tena. Hali hiyo ikawa inawatisha Jombi na Miraji. Baada ya muda wa dakika ishirini na tano, Kaguta aliwasili. Bakari aliamka akatoka na Kaguta nje.





“Bakari, umepajuaje hapa?”
“Tuachane na hayo, Kaguta. Nina shida.”
“Shida gani?”
“Wanataka kuniua! Naomba unisaidie.” Bakari alilia.
“Wakina nani wanataka kukuua?”
“Jeshi la Mr Kim. Wameshawaua wenzangu watatu. Wanan’tafuta na mimi waniue!”
“Kwanini wakuue?”
“Nimetoa siri yao kuhusu kisiwa cha Alwatan Kombo. Wanataka kutumaliza wote!”
“Usihofu, nitakusaida. Lakini, kwanini haukumwambia Jombi hizi habari, umeamua kunambia mie tu?”




Kabla Bakari hajajibu, alitizama kushoto na kulia kwake kwanza ndipo akasema:




“Najua Jombi ana tattoo. Ni hatari, kwani nikimuambia taarifa zitawafikia ninaowakimbia.”
“Umejuaje hizo habari za tattoo, Bakari? Umejuaje kama hao watu ni jeshi la Mr Kim?”
“Najua kwasababu namimi nilishawahi kuwepo huko. Nilishawahi kuwa mfuasi wa hilo genge. Nilishawahi kuwa na hiyo tattoo kabla sijaiondoa karibuni.”
“Kuiondoa?”
“Ndio!”
“Umeiondoaje? Pasi?”
“Hapana! Niliiondoa na chumvi.”
“Chumvi?”
“Ndio!”
“Chumvi?”
“Ndio! Mimi ni zaidi ya mnijuavyo, Kaguta.”
“Wow! Inaonekana.”
Kaguta alisema na kutabasamu.


****
☆Steve
 
***SURA YA THELATHINI NA TATU***



(MSIMU WA PILI)






Ikiwa ni saa tisa ya alasiri, Kaguta alikuwa yu njiani beneti na Bakari wakiwa wanaelekea hospitalini alipolazwa Sandra. Kaguta alikuwa kavalia koti la suti, jeans na moka nyeusi wakati Bakari alikuwa kavalia shati jeupe la Jombi na suruali ya kaki ya kadeti.




Walipoingia ndani ya geti Kaguta aliona gari moja jeusi aina ya range rover, alipolitizama vyema akaona ubavuni mwa gari limepachikwa stika ya tattoo, tattoo ya nyoka, nyoka aliyemuona kule kwenye kijumba cha Alwatan Kombo. Kaguta akamvuta Bakari na kulifuata lile gari. Aliuingiza mkono wake chini ya gari akasema:





“Bado lina joto, wamekuja muda si mrefu.”
“Wakina nani?”
“Bila shaka watakuwa jeshi la Kim.”
“My God! Wanafanya nini hapa?”
“Hiko ndicho nataka kujua.”





Kaguta alisema, alitoa peni mfukoni mwake akatobolea tairi moja la gari. Alimshika mkono Bakari wakaanza kutembea haraka kuelekea wodi ya Sandra. Wakiwa koridoni, Bakari aliona wanaume watatu waliovalia suti mbele yao hatua chache. Akamshtua Kaguta:





“Hao hapo mbele.”
“Umewajuaje?”
“Ndio hao. Wote hawana nywele na wanatembea pamoja. Ndio hao! Ndio hao!”
“Ssshh! ... Taratibu.”




Kaguta alitizama mikononi mwa wale wanaume watatu akaona wamefichilia bunduki. Alimtizama Bakari akamuambia:




“Tafuta batan ya hatari popote pale humu hospitalini, bonyeza. Hakikisha king’ora kinalia. Fanya haraka! Hatuna njia yoyote zaidi ya hiyo, hatuwezi kuanzisha vita hospitalini.”
“Sawa!”





Bakari aliachana na Kaguta akaenda kufanya alichoagizwa. Kaguta akabakia akitembea nyuma ya wale watu watatu ambao walikuwa wanaelekea wodi ya Sandra.





Dakika zikapita pasipo king’ora kulia na wale wanaume wakazidi kusogea zaidi na zaidi. Kaguta aliangalia huku na huko kwa hofu. Akaanza kujisemea:




“Bakari … Bakari … Bakari, please.”




Mara king’ora kikalia kwanguvu. Watu walipatwa na taharuki wakaanza kukimbia huku na huko, walinzi nao wakaanza kupandisha kwenye majengo kutizama usalama. Wanaume wale watatu ndani ya suti wakatizamana, walipeana ishara ya kichwa wakageuka na kuanza kurudi.





Hapo Kaguta akaona sura zao, loh! Walikuwa wamefanana kila kitu usoni.Walipopita, Kaguta alitoka alipokuwa amejificha akabaki anawatizama kwa kuduwaa.






Walinzi walipomfikia aliwaita akawaonyeshea kitambulisho chake cha kazi na kuwaelekeza wawakamate wale wanaume watatu mapacha wapo chini yalipopakiwa magari. Walinzi wakashuka upesi kwenda walipotumwa, bahati mbaya wakakuta wanaume wale wameshatoweka na gari lingine.





Bakari na Kaguta wakaendelea na safari yao kwenda chumba alicholazwa Sandra. Walimkuta wakamjulia hali yake, lakini pia wakampasha habari juu ya yaliyotokea. Bakari akasema:




“Ni kwasababu ya tattoo yako. Watakufuata popote utakapokuwa.”




Sandra akashangazwa na hizo habari.





“Umejuaje?” Alimuuliza Bakari.




Kaguta akatabasamu na kumjibu:




“Ni simulizi ndefu. Kwanza inabidi utoke hili eneo, si salama tena.”




****
☆Steve
 
Mkuu SteveMolel tuachie kaborudani ka weekend mkuu pls ni ombi lakini samahani kama nitakuwa naingilia mipango ya ratiba zako
Pasi na shaka mkuu. Ni bampa to bampa!

☆Steve
Leo muda unaruhusu sana.
Leo msicheze mbali. Weekend hii!

☆Steve
Hongera mkuu story bomba kweli
Ahsante mkuu. Pamoja sana.

☆Steve
Ngoja nianze nikija kufika mlipo itakuwa ishaisha
Ukianza hutoacha mkuu. Na hapa hamna longo longo.

☆Steve
Tuko pamoja
Ahsante mkuu. Natumai tutamaliza wote pia.

☆Steve
USHAHIDI WA HONGO una kesi mbili za kujibu hapo pamebipa raha sana maana huyu mkurugenzi alifikiri palaini kumbe ni mwamba wa bahari haulainishwi kwa maji
Mkuu yani ni moto juu ya moto!

☆Steve
Dooh..!!
Mkuu sijui kawaje siku hizi ,ngoja tumuulize,eti Mr Kim mbona wafupisha sana siku hizi..!!??
Hahahha mbona ya kawaida jamani. Nitume gazeti kabisa.

☆Steve
hahahhh ndio unavyowaza hivyo tukadiscuss jlw
Mnajuana nyie.

☆Steve
Steve unatoa fupi fupi Sana na wewe hutaki tumalize nn
Mkuu hata hii ikiisha zipo zingine. Siungi ungi. Mie sio tia maji tia maji.

☆Steve
hoyaa steve mbona fupi leo daah
Raha tu yakunogea Evarist.

☆Steve
Asante sana.sijui ndio kunogewa ila nahisi leo kama fupi
Umenogewa tu. Haya leo tuwe macho hapa hapa.

☆Steve
 
nataka kujua insp.vitallis anarudije kwenye game...
maana tumehama kabisa kutoka kwa kina mtenvu,k square,pius na wenzake......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom