Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Dah! Mkuu steve mi nimekaa siti ya mbele nasubiria bhanaaa....
Mkuu Leo tumelala dolooo,nahisi mkuu Steve kaalikwa na Sandra akaangalie tattoo yq jitu moshi.
Hahaaaaah,kikikikiiiiiiiihhh...!!
Cc Alwatan Kombo ,wapi kaguta na bhoke wake.
 
Mkuu Leo tumelala dolooo,nahisi mkuu Steve kaalikwa na Sandra akaangalie tattoo yq jitu moshi.
Hahaaaaah,kikikikiiiiiiiihhh...!!
Cc Alwatan Kombo ,wapi kaguta na bhoke wake.
Nakuja weeee!
 
***SURA YA ISHIRINI NA TATU***




(MSIMU WA 02)








Kilomita nne zilitafunwa barabarani mpaka kufikia eneo ambalo Suzuki Vitara iliingia. Ilikuwa ni nyumba kubwa mno yenye geti pana la mbao. Inspekta Vitalis alisogea hilo eneo akasoma namba ya nyumba … 898. Akakumbuka maneno ya Kaguta ya kwamba bwana Isaac Makongo anaishi kurasini nyumba namba 898. Inspekta Vitalis alishuka kwenye pikipiki, akasogelea geti na kugonga. Mlinzi akafungua kitundu kilichokuwepo kwenye geti na kuuliza;
“Wewe ni nani?”



Inspekta Vitalis akaonyesha kitambulisho chake cha kazi. Mlinzi hakuuliza tena, akafungua geti na kumruhusu inspekta aingie. Ajabu inspekta alipoingia alimkuta mlinzi mwenye mapembe. Inspekta alistaajabu mno, mlinzi alitabasamu na kumwambia;
“Karibu. Wakati mkuu anapita alinambia kuna mgeni atakuja muda si mrefu. Kumbe ni wewe. Umekuja muda muafaka.”




Inspekta hakusema jambo, bado alikuwa kwenye butwaa kwani kadiri mlinzi yule alivyokuwa anaongea alikuwa anaongezeka kimo na kuwa mrefu, mrefu na mrefu zaidi.



“Leo ni mwisho wako, Vitalis Byabata.”




Mlinzi alisema kwa sauti nzito, haikuwa tena kama ya mwanzoni. Macho yake yalibadilika na kuwa ya simba. Mkia ulichomoza na makucha yakaamka, mwili wake ukawa mkubwa mithili ya mbuyu wa kale. Inspekta Vitalis alitumbua macho kuona yasiyoaminika. Alifungua miguu yake kufuata geti ila alishikwa na kubamizwa kwa nguvu ukutani. Alikabwa koo akatoa macho kama ngumi. Jasho lilimtiririka, alijitahidi kuvuta pumzi ila hakuipata. Alijitahidi kufurukuta ila hakuweza.




Mishipa ya kichwa ilimsimama. Alirusha miguu kwa kutapatapa. Macho yalianza kupanda juu ishara ya mwili kuwa tayari kupokea kifo kwa sasa. Zikiwa zimebakia sekunde kadhaa tu inspekta aende na maji, jitu lilimwachia kwa kumtupa chini. Inspekta akadaka hewa na kuivuta kama vile yupo mashindanoni.





Alishika shingo yake huku akikohoa. Mapafu yalipanda na kushuka kama vile puto. Taratibu mlinzi alirudi kwenye hali yake kama mwanzoni, japokuwa mapembe yalibakia palepale. Alifungua geti, akanyooshea mkono wake nje;
“Toka upesi!”




Alifoka. Inspekta alijikusanya taratibu akatoka nje. Mlinzi akafungua kisehemu cha wazi cha geti na kusema kwa tabasamu;
“Karibu tena.”




Inspekta alijikokota akaendea pikipiki yake akapanda. Kabla hajaondoka alitumia dakika mbili kutizama lile eneo kama vile haamini kilichotokea mule ndani. Alikohoa akajiuliza;
“Kwanini ameniacha hai?”





Aliwasha pikipiki akarudi ofisini. Nguo zake zilikuwa zimechafuka. Alipaki pikipiki akaelekea nyumbani moja kwa moja. Aliketi kwenye kochi sebuleni akawa anafikiria. Kwa muda wa dakika kumi na tano alikaa pale na kutafakuri. Mwishowe alinyanyuka na kuchomeka pasi kwenye umeme, pasi ilipopata moto wa kutosha alikunja mkono wa shati lake akabandika pasi eneo lenye tattoo. Alipiga kelele kali mno.





Alibandua pasi ikatoka na ngozi, ikabakia jeraha kubwa hapo. Jombi alikuja sebuleni akamkuta inspekta ana alama kubwa nyekundu ya kuiva mkono wake wa kushoto huku akiwa amekunja sura kwa ukali wa maumivu anayoyahisi.




“Inspekta, umefanya nini?” Jombi aliuliza. Inspekta hakujibu, alikuwa tu anaugulia. Jombi alihisi harufu, alipepesa macho yake kutizama akaona pasi ipo kwenye moto, na tena ina mabaki ya damu. Jombi alichomoa waya wa pasi toka kwenye umeme kisha akamgeukia inspekta Vitalis.




“Inspekta inabidi twende hospitali!”
“Hapana! .. Mpigie Bernadetha, mwambie aje upesi.” Inspekta aliingiza mkono wake mfukoni akatoa simu. Jombi akaipokea na kumpigia mama Miraji. Ndani ya muda mfupi mama Miraji akawasili maeneo





. Bila kupoteza muda alianza kumuhudumia inspekta Vitalis kwa kumpakaa mafuta ya bunduki na asali kwa mbali kwenye jeraha. Zaidi ya hapo akampatia dawa ya kukabili maumivu na kumjuza utaratibu wa kupaka mafuta ya bunduki na asali kama tiba.




Inspekta alimtizama Bernadeta akatabasamu. Bernadetha naye akatabasamu na kuuliza;
“Mbona wafurahi?”
“Kwasababu mbili.” Vitalis alijibu.
“Zipi?”
“Moja, nimekuwa huru kuanzia sasa, sina tena chapa ya wadhalimu. Pili, nimekuona.”




Bernadetha alimwaga tabasamu pana, akasema;
“Nashukuru. Nimefurahi kukuona pia. Leo Marietta hajaenda shule kwa ajili yako.”
“Kwa ajili yangu?”
“Ndio. Anakungoja umpeleke shule.”
Inspekta alicheka kidogo akatia neno;
“Mwambie nakuja kumpeleka kesho. Naahidi.”
“Sawa.”
“Vipi Miraji anaendeleaje?”
“Anaendelea vyema tu. Yupo. Miraji ana hasira na ninyi, anaamini mpo upande ule ule na wale waliomuua baba yake.”
“Umemuambia chochote kuhusu mimi na Kaguta?”
“Hataki kusikia kitu kuhusu nyie. Ilibidi niongope ndio nipate kuja huku.”
“Pole sana. Atakuja kuelewa tu.”




Baada ya maongezi, mama Miraji aliingia jikoni akapika chakula kwa ajili ya majeruhi, Vitalis, kisha akaaga. Jombi akataka kwenda na Bernadetha akamjulie hali Miraji.




“Sasa mgonjwa unamuacha na nani?” Bernadetha aliuliza.
“Hapana. Mwache aende tu, mimi nipo sawa tu.” Inspekta Vitalis aliruhusu. Jombi na Bernadetha wakaondoka.



Jua likazama na kuchomoza.




Ingawa mkono wake ulikuwa unamuuma, inspekta Vitalis hakutaka kubakia nyumbani mwenyewe. Angeboreka. Alijinyanyua akajiandaa na kwenda kazini kama kawaida huku mkono wake akiwa kaufichama kwenye mkono mrefu wa shati lake jeusi. Ilikuwa ngumu kujua kama ana jeraha mpaka umtizame kwa makini jinsi anavyoulinda mkono wake huo na kutoupa kashkash za hapa na pale.





Kwa kuwa alingoja mpaka apate daladala lenye siti tena isiyo na bugdha, alichelewa kufika ofisini. Ilikuwa ni mida ya saa tatu tofauti na mida yake aingiayo ofisini ya saa moja. Alinyookea mlango wa ofisi yake, ajabu alipoushika ukafunguka bila ya kwazo.




“Alaah! Ina mana sikuufunga huu mlango?” Alijiuliza. Aliingia ndani akaanza kupekua mafaili yake, akakuta faili la MTEMVU’S CASE halipo. Haraka aliwasha tanakilishi yake akatizama faili la MTEMVU’S CASE lililopo humo, nalo halikuwepo.





Macho yalimtoka inspekta Vitalis. Alitoka kwa jazba akafuata ofisi ya OCD, aliposhika kitasa akasita. Alirudi ofisini kwake akafunga na kuamua arudi nyumbani. Aliketi sebuleni akawa anawaza. Alitikisa kichwa chake mara kwa mara huku akisonya. Mwishowe mawazo yake hayo yalimbeba kwa njia ya usingizi. Ni Kaguta ndiye alikuja kumuamsha na kumtoa akarefresh akili bar. Huko wakapiga soga, inspekta akamueleza Kaguta yote yaliyojiri.




Inspekta alikuwa anakunywa Heineken, Kaguta alikuwa anasukuma chupa kubwa ya Jack Daniels.



***

☆Steve
 
***SURA YA ISHIRINI NA NNE***






(MSIMU WA 02)






“Pole aisee. Inabidi uwe makini sana na OCD huyo.”
“Mshenzi sana huyo! Yani amenivunja moyo kabisa. Faili la ile kesi ina taarifa nyingi mno na za maana, kupotea kwake kumenirudisha nyuma mnooo.”
“Kabisaa.” Kaguta aliitikia kisha akapeleka fundo mbili za kinywaji chake. “Sasa kaka, kazi iliyokuwepo mbele yetu ni …” Kabla Kaguta hajamalizia, inspekta Vitalis alimzuia na kumuonyeshea alama ya tattoo mkononi mwake.
“Unakumbuka? … Hakuna litakalofanikiwa. Hatuwezi kupanga lolote ukiwa nayo.”




Kaguta aliitikia lakini macho yake yalionekana kutekwa na kitu nyuma ya inspekta Vitalis. Kaguta alifikicha macho yake kama mtu ambaye haamini anachokiona kisha akapiga fundo moja na kusema;





“Vitalis, yule ni Bakari au pombe zangu?” huku akionyeshea ishara kwa kichwa. Inspekta akajigeuza na kutizama.
“Eh! … Ndio yeye. Yupo na nani pale?”
“Sio Roby yule?”
“Ndio! Yule ni Roby!”
“Ina maana Bakari, hakufa?”
“Ndio mana tunamuona pale. Ila anaongea nini na Roby? Wanaongea kama watu wanaojuana kabisa. Ina maana Bakari …”




Kaguta alinyanyuka akataka kwenda, Vitalis akamshika mkono.




“Tuliza mihemko. Ngoja.”




Kaguta akakaa wakawa wanatizama huku wakishushia na vinywaji vyao. Roby na Kaguta waliongea kwa dakika kumi na tano tokea wakina Vitalis walipowaona, walipomaliza walilipa wakanyanyuka na kutoka nje ya bar, inspekta na Kaguta wakawafuata. Huko nje Roby na Bakari waliingia kwenye gari moja wakaondoka.





Vitalis na Kaguta wakazama kwenye gari lao na kuanza kuwafuata. Baada ya muda wa dakika tano za matembezi, gari la wakina Roby lilisimama, Bakari akashuka na kuaga. Vitalis na Kaguta nao wakashuka na kuanza kumfuatilia Bakari kwa nyuma mpaka sehemu fulani ambapo Bakari alikutana na wenzake ambao Kaguta na inspekta walivyotizama vizuri wakagundua hao watu ni wale wavuvi waliowakuta siku zile walipokwenda kisiwani.





Kwa umakini, inspekta na Kaguta wakawa wanawatizama wale wavuvi. Wavuvi waliongea kwa muda kidogo kisha Bakari akaingiza mkono wake mfukoni akatoa mifuko ya kaki aliyomkabidhi kila mmoja wao pale kisha kila mmoja akaenenda na njia yake.




Kaguta na inspekta walimfuata Bakari kwa kumnyatia mpaka alipofikia kwenye nyumba fulani ya saizi ya kati, hapo Bakari akagonga na kuingia ndani. Kaguta na inspekta Vitalis wakasogea mpaka dirishani wakachungulia ndani, wakamuona Bakari akiwa anaongea na simu ya mkononi. Mara ghafla Bakari alikunja sura akiwa anaongea, alirusha macho yake dirishani Kaguta na inspekta wakawahi kujificha.





Haraka Bakari akakimbia kuufuata mlango wa nyuma, inspekta Vitalis na Kaguta wakashtuka, haraka waliupiga teke mlango wakaingia ndani, haraka walikimbia kumfuata Bakari, Bakari akaufungua mlango akatoka nje na kuanza kukimbia. Inspekta na Kaguta walimkimbiza kwa kasi, Bakari akajikwaa akadondoka chini. Inspekta na Vitalis wakamkamata na kumuweka chini ya ulinzi.





“Shenzi sana wewe!” Inspekta alifoka. “Kumbe ulikuwa unatu-enjoy sio? … Sasa mwisho wako umefika!”





Inspekta na Kaguta walimbebelea Bakari msobe msobe mpaka kwenye ile nyumba Bakari alipotorokea. Walimkalisha chini wakaketi kitako na kumtazama kwa nyuso kavu.




“Anza kueleza mwenyewe nini ulitufanyia siku zile ... Na usitupotezee muda.” Inspekta Vitalis alieleleza. Bakari akajifanya hatambui muamala anaoulizwa. Alisema hajui lolote kuhusu wao: Vitalis wala Kaguta. Ilibidi inspekta Vitalis atumie nguvu ya ziada kupata majibu wanayoyataka toka kwa mtuhumiwa wao: ngumi kadhaa ziliajiriwa na baada ya muda Bakari akakiri kusema:
“Tulitumwa kufanya ile kazi. Tuliahidiwa pesa nzuri endapo kama tutafanikisha hiyo kazi.”
“Kazi ipi?” Kaguta aliuliza.
“Kazi ya kuwapoteza muelekeo, kazi ya kuwafanya mpotee na hata kwenda kufa huko!”
“Kwahiyo unataka kunambia kwamba yale yote mliyokuwa mnafanya kabla ya kutupeleka huko ilikuwa ni maigizo?” Inspekta Vitalis aliuliza.
“Ndio. Si kingine. Ni maigizo tu kuwaleta kwenye uhalisia.”
“Na nyie mlijuaje kama tunakuja?” Inspekta Vitalis aliuliza.
“Tulipewa taarifa juu ya ujio wenu.”
“Na nani?” Inspekta Vitalis aliuliza.
“Na bwana Roby. Alituambia mu njiani mwaja.”



Inspekta Vitalis alimtizama Kaguta, Kaguta akamuonyeshea tattoo aliyonayo mkononi.




“Kwahiyo ukweli ni upi? Wapi tulipokuwa tunatakiwa kwenda kukutana na yule tuliyemuhitaji?” Inspekta aliuliza. Ila kabla ya Bakari kujibu, Kaguta alionyeshea ishara ya kukaa kimya kwa kuweka kidole chake kwenye lips kisha akamtizama inspekta na kumuonyeshea tattoo aliyo nayo mkononi.




Inspekta alitikisa kichwa chake kisha wakamnyanyua Bakari na kumpeleka garini, wakaenda kwenye jumba lao bovu na kumfungia Bakari huko. Walimrudia siku inayofuata Kaguta akiwa hana tattoo mkononi mwake bali alama ya kuungua kwa pasi.





“Wapi tunaweza kumpata tunayemuhitaji?” Inspekta alirudia swali.
“Kule baharini kuna visiwa viwili: kimoja wapo ndicho anachokalia Alwatan Kombo.”
“Unaweza ukatupeleka?” Kaguta aliuliza. Bakari akasita kwa muda kidogo kutoa majibu ila kwanguvu ya msisitizo, akatoa majibu:
“Ndio naweza kuwapeleka.”




Inspekta Vitalis na Kaguta wakatizamana na kutabasamu. Kesho yake walijiweka kwenye gari pamoja na Bakari wakaenda bagamoyo. Walipanda mtumbwi wakafika kisiwani.




Huku Bakari akiwa mbele, safari ilielekea mpaka kwenye nyumba fulani kubwa na ya kisasa. Walibisha hodi wakafunguliwa na mmama mmoja mnene mwenye mvi. Aliwakaribu ndani, wakaingia na kuketi kwenye makochi yaliyojaa sebuleni.





“Tumemkuta bwana Alwatan Kombo?” Inspekta Vitalis aliuliza.
“Ndio. Ametoka tu kidogo, anakuja. Mna shida gani?”
“Tunataka tu kuonana naye kuna mambo tunataka atunyooshee.”





Punde mlango ulifunguliwa akaingia mzee mfupi mweusi akajitambulisha kwa jina la Alwatan Kombo.Aliwachukua wakina inspekta akaongozana nao kwenda nje ya nyumba mpaka kwenye kijumba kidogo walichoingia kwa kuinama. Humo ndani Alwatan Kombo akaketi kwenye kiti chake na kuuliza:




“Naweza nikawasaidia?”




Bakari aliwatizama inspekta Vitalis na Kaguta akawaona wanatizama ukutani mwa kile kijumba. Kwenye ukuta kulikuwa na mchoro kadhaa, mojawapo ulikuwa ni wa jitu, pembeni ya jitu kulikuwa na vitu vinne: mti wa mchungwa, mtu wa mbao, ndege wa ajabu na saa.





Pembeni ya hiyo michoro kulikuwa na michoro mingine: Nyoka mkubwa mwenye vichwa vitatu, Simba, alama za maji na namba 898. Wakati wakina inspekta wakibung’aa, Alwatan Kombo aliwashtua kwa kuwamwagia matone ya maji toka kwenye kikombe chake kilichokuwa kimekaa kando.





“Elezeni shida zenu vijana.”
“Mzee, sisi tumekuja hapa kwa ajili ya kupata ufumbuzi wa baadhi ya mambo tu toka kwako.” Inspekta Vitalis alisema kisha akatoa kitambulisho chake na kumuonyeshea mzee Alwatan Kombo.
“Tuna maswali machache tu toka kwako,tunaomba utupatie majibu. Mosi, bwana Kim Salvatore ni nani kwako?”
Alwatan Kombo alitabasamu kwa kejeli akatizama chini kwa muda kisha akaurudisha uso wake kwa inspekta.
“Hiko ndicho kimewaleta?”
“Ndio!” Inspekta Vitalis alijibu kwa kujiamini. Alwatan Kombo aligeuza uso wake akatizama ukuta wake. Alichovya kiganja chake kwenye maji kisha akapiga ukuta wake mara tatu … pah pah pah.




Mara kukaanza kutokea mtikisiko. Mchoro wa jitu ulianza kutokota na kukua. Inspekta Vitalis na Kaguta walitizamana kwa macho ya mshangao. Mchoro ulikua na hatimaye ukawazidi hata kimo. Alwatan Kombo alisimama akaamuru;
“Ondokeni kwa usalama wenu!”




Uso wa Bakari ulikuwa umelowana hofu, aliwataka wenzake aliokuja nao waondoke upesi. Kaguta alimtizama inspekta Vitalis na kumpa ishara ya kuafiki walichoamriwa. Walitoka ndani ya kijumba cha Alwatan Kombo wakasimama umbali wa hatua thelathini.





“Sasa tunafanyaje?” Kaguta aliuliza.
“Tuondokeni hapa jamani! … Tuondokeni tutakufa!” Bakari aliropoka. Inspekta Vitalis alikuwa kama mtu anayewaza jambo: hakusema kitu kwa muda kama wa sekunde tano. Alishusha pumzi ndefu akasema:
“Tuondoke!”




Hatua tatu mbele magari mawili aina ya defender yalitokeza yakiwa yamebebelea waliobebelea bunduki. Haraka inspekta Vitalis na Kaguta wakahisi kuna hatari.





Inspekta alimshika mkono Bakari wakaacha njia kuu na kukimbilia kando kujibanza kwenye jengo, wakiwa wanakimbia risasi ziliporomoshwa kuwafuata kwa fujo. Wanaume saba walishuka toka kwenye defender wakiwa wamebebelea SMG, mmoja wao akawaambia;
“Hatuna muda hapa. Dakika mbili tu!”




Haraka wanaume wale wakagawanyika wakielekea eneo walilokimbilia wakina inspekta. Walitafuta maeneo hayo wakapekua kwa macho yao makali lakini hawakuona kitu. Mpaka dakika mbili zatimba hakuna kitu walichopata. Walirudi kwenye magari yao wakarudisha ripoti:





“Hatujaona kitu, mkuu!”
“Hamjaona kitu?” Robson aliuliza: alikuwa ameketi kwenye kiti cha mbele kabisa cha dereva.
“Ndio! Hatujaona kitu.”
“Tuondoke. Pandeni haraka! Watu watajazana muda si mrefu.”




Wanaume wale saba haraka walipanda kwenye magari yao wakaondoka eneo lile ambalo watu walianza kujazana ndani ya muda mfupi tu wakiwa wanazoza juu ya lile tukio. Ndani ya watu hao waliosogea eneoni walikuwepo wakina inspekta.





Walikuwa wamechafuka mno kwa udongo, walinyooka na barabara mpaka eneo la mitumbwi wakapanda mtumbwi kwenda ng’ambo. Walijiweka kwenye gari lao wakaanza safari ya kurudi Dar es salaam. Mara hii alikuwa anaendesha inspekta Vitalis na kasi yake ilikuwa kubwa mno.





“Wanaweza wakaenda kumjeruhi Bernadetha. Inabidi tuwahi!” Inspekta Vitalis alisema kwa mjazo.
“Sidhani kama wana haja ya kufanya hivyo.” Kaguta alisema.
“Vita haina macho, Kaguta. Huwezi jua.”
“Kweli, tahadhari inabidi ichukuliwe. Ila Vitalis, kuna jambo lolote umeligundua pale kwa Alwatan Kombo?”
“Kuna mambo nimeyaona yananitatiza akilini.”
“Kama yapi?”
“Ile michoro.”
“Exactly. Ila ina maana gani? … Pembeni ya mchoro wa yule jitu kuna mchoro nimeuona wa mti wa mchungwa.”
“Una nini?”
“Huo mti ndio ambao nilipambana nao kule kisiwani?”
“Really?”
“Ndio!”
“Alafu hata mimi nimeona mtu wa mbao pembezoni ya mchoro huo huo wa jitu. Na huyo mtu ndiye niliyepambana naye pia kule kisiwani!”
“Je yule ndege, ulimuona?”
“Nilimuona!”
“Ndiye yule aliyekuwa kambeba Jombi kule kisiwani!”
“Sasa naanza kupata picha kamili. Hata ile saa tuliyoiona pembeni ya yule jitu maana yake ndio ule muda tuliokuwa tunapewa kule kisiwani na kila baada ya huo muda kukawa kunatokea majanga!”
“Haswaa!”
“Kwahiyo … Kwahiyo sasa … ina mana ile michoro kwanini ilikuwa pembezoni mwa yule jitu?”
“Hapo ndipo kuna la kupambazua.”
“Nadhani hivyo ndivyo vitu vinavyomtimiza huyo jitu. Ama ndivyo vitakavyokuwa power yake.”
“Labda. Kwahiyo ina maanisha tukitaka kumkabili yule jitu ni lazima tupitie hayo majaribu?”
“Bila kipingamizi, hivyo ndivyo. Lakini kuna jambo lanipa mashaka.”
“Lipi?”
“Kwanini huyo jitu haruhusiwi kutumaliza badala ya kuhangaika nasi kwa bunduki?”



****

☆Steve
 
utamu kunoga

mkuu asante sana ungetupia hata moja basi ya kulalia

Sante mkuu nalala roho safii

mambo ni burdaaani..big up mkuu steve

Safi. Imekaa Poa sana.

Dah! Mkuu steve mi nimekaa siti ya mbele nasubiria bhanaaa....

Dah nahisi sandra kama anakuja kufaa hv maana hyo tattoo dah
Karibuni wapendwa.
 
***SURA YA ISHIRINI NA TANO***






(MSIMU WA 02)






“Sijajua mpaka sasa. Kuna jambo lipo nyuma ya pazia.”
“Na inatulazimu kuling’amua. Pia umeona namba 898?”
“Nimeiona.”
“Itakuwa ina maanisha nini?”
“Sijajua. Ila si unajua nyumba ya bwana Isaac Makongo ina namba 898?”
“Ndio. Kuna kitu pia katika hiyo namba.”




Baada ya dakika ishirini na tano wakawa tayari wameshawasili jiji la Dar es salaam. Bakari alishushwa wakina inspekta wakaelekea mpaka nyumbani kwa Bernadetha.




“Karibuni!” Bernadetha aliwakaribisha kwa tabasamu pana.
“Ahsante!”




Waliketi kwenye viti inspekta Vitalis akamueleza Bernadetha yaliyotokea. Zaidi inspekta Vitalis akamtaka Bernadetha ahamie kwake kwa usalama. Jambo hilo likawa gumu.




“Mwanangu Miraji hataki kabisa hata uongelewe humu ndani. Inakuwa ugomvi kabisa, sembuse kuja kukaa kwako.”
“Mueleze hali halisi. Muambie mpo hatarini.”
“Sidhani kama itaweka mabadiliko yoyote. Anawahesabu nyie kama wauaji wa baba yake, hapo ndipo ugumu unakuja. Ila nitajitahidi sana kumueleza.”
“Sawa. Itakuwa vyema.”
“Vipi Kaguta, mbona mkono wako una bandeji?”




Kaguta akaeleza yaliyotukia. Bernadetha akachukua wasaa wake kumpa huduma ya kwanza kama ile aliyompa inspekta Vitalis kisha akamtaka Kaguta asifunge hilo jeraha. Baada ya hapo, wakina inspekta waliaga. Bernadetha aliwatoa mpaka nje, akamkumbatia inspekta Vitalis na kumbusu shavuni.




“Utakapohisi tatizo, nipigie immediately. Na usisahau kumsalimia Marietta akirudi.” Inspekta Vitalis alimwambia Bernadetha. Bernadetha akatikisa kichwa kukubali alichoambiwa. Mpaka wanaume wanatokomea na gari lao, Bernadetha akawa yu kibarazani anawatizama. Chozi lilimshuka akalipangusa na kiganja chake.




Alitizama chini akajigeuza na kurudi ndani. Kumbe wakati yupo hapo kibarazani Miraji alikuwa anamchungulia dirishani. Baada ya mama kuingia ndani, Miraji alifunga dirisha lake akajilaza kitandani akarusha macho yake darini kama mtu anayewaza jambo.





Katikati ya mida ya saa mbili za usiku, Bernadetha alikuwa na wanawe: Marietta na Miraji wakiwa wanapata chakula kwa pamoja. Kulikuwa ni kimya kati yao kwa muda wa dakika kadhaa, vijiko tu na sahani ndivyo vilikuwa vinapiga makelele. Miraji alimtizama mama yake, akamtizama na mdogo wake, Marietta, kisha akaamua kuufungua mdomo kwa kuuliza:




“Mama, mbona siku hizi hauna raha?”




Bernadetha alimtizama Miraji akatabasamu kiuongo.




“Kwanini unasema hivyo mwanangu? … Nipo sawa tu.”
“Hapana. Mara kwa mara nimekuwa nikikuona unaketi nje peke yako, unadondosha chozi. Umekuwa ni mtu wa kuketi kiupweke. Umekuwa ukichelewa kulala na hata mara nyingine kulala sebuleni. Nini tatizo, mama?”





Bernadetha aliyafichama yote yaliyosemwa na Miraji kwa tabasamu pana lililojaza uso wake. Akasema:
“Mwanangu, hakuna lolote. Labda kwa kuwa hujaniona kwa muda.”
“Mama, kwani uncle Vitalis amesema anakuja lini?” Marietta aliingilia kwa kuuliza.
“Atakuja tu.”
“Lini? Mi nimemkumbuka. Basi twende kwake.”




Marietta alizidi kusisitiza. Bernadetha akamtizama Miraji kwa jicho la tahadhari, Miraji hakusema jambo, aliendelea tu kula kama mtu ambaye hajasikia lolote.




‘Tutaenda tu, usihofu mwanangu.” Bernadetha alimwambia Marietta, Marietta akatabasamu na kuendelea kula. Miraji alipomaliza alinyanyuka akaondoka zake kwenda chumbani.





Baada ya muda mfupi, Marietta naye alinyanyuka akaenda kuoga na kulala, alibakia Bernadetha peke yake sebuleni akiwa anatizama runinga. Mara simu yake ya mkononi iliita na kutetemeka, akainyakua toka mezani na kuitizama, akaona ujumbe toka kwa inspekta.




“Helo … Umelala?”
Bernadetha akatabasamu na kubonyeza vitufe vya simu kujibu.
“Hapana, nipo tu natizama televisheni.”
“Upo salama?”
“Am ok. Wewe?”
“Nipo salama. Jus missin yu.”
Bernadetha alitabasamu tena, kisha akajibu:
“Me too.”
“Unakuja lini kuniona?”
“Nadhani wknd hii. Marietta pia anataka kukuona.”
“Nimemmis sana. Karibuni.”
“Ahsante. Mkono wako unaendeleaje?”
“Naendelea vyema tu. Upo na nani hapo?”
“Mwenyewe. Wewe je?”
“Nipo mwenyewe pia.”
“Wapi?”
“Chumbani. Naona nyumba imekuwa kubwa mno. Nakumiss kweli.”
“Sana?”




Marietta alituma ujumbe huku aking’ata lips zake. Bahati mbaya hakujibiwa. Alikaa dakika kama tano bila ya majibu. Simu ilikuwa imekata mtandao. Alitoka nje akanyanyua mkono wake kutafuta mtandao bila ya mafanikio.





Hata pale mtandao uliporudi hakuona ujumbe mwingine, alienda chumbani kwake akalala ila kila muda akawa anahisi sauti ya ujumbe kuingia ila alipotizama hakuona kitu, mwishowe usingizi ulimpitia akajikuta asubuhi simu yake ikiwa imejaa jumbe nyingi toka kwa inspekta Vitalis. Akatabasamu na kuanza kuzijibu kabla ya kufanya kitu kingine chochote.





****
☆Steve
 
***SURA YA ISHIRINI NA TANO***






(MSIMU WA 02)






“Sijajua mpaka sasa. Kuna jambo lipo nyuma ya pazia.”
“Na inatulazimu kuling’amua. Pia umeona namba 898?”
“Nimeiona.”
“Itakuwa ina maanisha nini?”
“Sijajua. Ila si unajua nyumba ya bwana Isaac Makongo ina namba 898?”
“Ndio. Kuna kitu pia katika hiyo namba.”




Baada ya dakika ishirini na tano wakawa tayari wameshawasili jiji la Dar es salaam. Bakari alishushwa wakina inspekta wakaelekea mpaka nyumbani kwa Bernadetha.




“Karibuni!” Bernadetha aliwakaribisha kwa tabasamu pana.
“Ahsante!”




Waliketi kwenye viti inspekta Vitalis akamueleza Bernadetha yaliyotokea. Zaidi inspekta Vitalis akamtaka Bernadetha ahamie kwake kwa usalama. Jambo hilo likawa gumu.




“Mwanangu Miraji hataki kabisa hata uongelewe humu ndani. Inakuwa ugomvi kabisa, sembuse kuja kukaa kwako.”
“Mueleze hali halisi. Muambie mpo hatarini.”
“Sidhani kama itaweka mabadiliko yoyote. Anawahesabu nyie kama wauaji wa baba yake, hapo ndipo ugumu unakuja. Ila nitajitahidi sana kumueleza.”
“Sawa. Itakuwa vyema.”
“Vipi Kaguta, mbona mkono wako una bandeji?”




Kaguta akaeleza yaliyotukia. Bernadetha akachukua wasaa wake kumpa huduma ya kwanza kama ile aliyompa inspekta Vitalis kisha akamtaka Kaguta asifunge hilo jeraha. Baada ya hapo, wakina inspekta waliaga. Bernadetha aliwatoa mpaka nje, akamkumbatia inspekta Vitalis na kumbusu shavuni.




“Utakapohisi tatizo, nipigie immediately. Na usisahau kumsalimia Marietta akirudi.” Inspekta Vitalis alimwambia Bernadetha. Bernadetha akatikisa kichwa kukubali alichoambiwa. Mpaka wanaume wanatokomea na gari lao, Bernadetha akawa yu kibarazani anawatizama. Chozi lilimshuka akalipangusa na kiganja chake.




Alitizama chini akajigeuza na kurudi ndani. Kumbe wakati yupo hapo kibarazani Miraji alikuwa anamchungulia dirishani. Baada ya mama kuingia ndani, Miraji alifunga dirisha lake akajilaza kitandani akarusha macho yake darini kama mtu anayewaza jambo.





Katikati ya mida ya saa mbili za usiku, Bernadetha alikuwa na wanawe: Marietta na Miraji wakiwa wanapata chakula kwa pamoja. Kulikuwa ni kimya kati yao kwa muda wa dakika kadhaa, vijiko tu na sahani ndivyo vilikuwa vinapiga makelele. Miraji alimtizama mama yake, akamtizama na mdogo wake, Marietta, kisha akaamua kuufungua mdomo kwa kuuliza:




“Mama, mbona siku hizi hauna raha?”




Bernadetha alimtizama Miraji akatabasamu kiuongo.




“Kwanini unasema hivyo mwanangu? … Nipo sawa tu.”
“Hapana. Mara kwa mara nimekuwa nikikuona unaketi nje peke yako, unadondosha chozi. Umekuwa ni mtu wa kuketi kiupweke. Umekuwa ukichelewa kulala na hata mara nyingine kulala sebuleni. Nini tatizo, mama?”





Bernadetha aliyafichama yote yaliyosemwa na Miraji kwa tabasamu pana lililojaza uso wake. Akasema:
“Mwanangu, hakuna lolote. Labda kwa kuwa hujaniona kwa muda.”
“Mama, kwani uncle Vitalis amesema anakuja lini?” Marietta aliingilia kwa kuuliza.
“Atakuja tu.”
“Lini? Mi nimemkumbuka. Basi twende kwake.”




Marietta alizidi kusisitiza. Bernadetha akamtizama Miraji kwa jicho la tahadhari, Miraji hakusema jambo, aliendelea tu kula kama mtu ambaye hajasikia lolote.




‘Tutaenda tu, usihofu mwanangu.” Bernadetha alimwambia Marietta, Marietta akatabasamu na kuendelea kula. Miraji alipomaliza alinyanyuka akaondoka zake kwenda chumbani.





Baada ya muda mfupi, Marietta naye alinyanyuka akaenda kuoga na kulala, alibakia Bernadetha peke yake sebuleni akiwa anatizama runinga. Mara simu yake ya mkononi iliita na kutetemeka, akainyakua toka mezani na kuitizama, akaona ujumbe toka kwa inspekta.




“Helo … Umelala?”
Bernadetha akatabasamu na kubonyeza vitufe vya simu kujibu.
“Hapana, nipo tu natizama televisheni.”
“Upo salama?”
“Am ok. Wewe?”
“Nipo salama. Jus missin yu.”
Bernadetha alitabasamu tena, kisha akajibu:
“Me too.”
“Unakuja lini kuniona?”
“Nadhani wknd hii. Marietta pia anataka kukuona.”
“Nimemmis sana. Karibuni.”
“Ahsante. Mkono wako unaendeleaje?”
“Naendelea vyema tu. Upo na nani hapo?”
“Mwenyewe. Wewe je?”
“Nipo mwenyewe pia.”
“Wapi?”
“Chumbani. Naona nyumba imekuwa kubwa mno. Nakumiss kweli.”
“Sana?”




Marietta alituma ujumbe huku aking’ata lips zake. Bahati mbaya hakujibiwa. Alikaa dakika kama tano bila ya majibu. Simu ilikuwa imekata mtandao. Alitoka nje akanyanyua mkono wake kutafuta mtandao bila ya mafanikio.





Hata pale mtandao uliporudi hakuona ujumbe mwingine, alienda chumbani kwake akalala ila kila muda akawa anahisi sauti ya ujumbe kuingia ila alipotizama hakuona kitu, mwishowe usingizi ulimpitia akajikuta asubuhi simu yake ikiwa imejaa jumbe nyingi toka kwa inspekta Vitalis. Akatabasamu na kuanza kuzijibu kabla ya kufanya kitu kingine chochote.





****
☆Steve
burdaaan mkuu steve
 
Mkuu naenda sambamba na wewe kwa burudani murua kabisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom