Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Molel, achana na kujiamini na viswahili vya mitaani, kama unabishia nenda BAKITA ukawaulize maana ya BARADHULI wata kupa jibu.
na bila shaka kwa kiswahili chako cha mitaani MCHIZI WANGU, unaweza ukaitafsiri RAFIKI YANGU kumbe maana halisi ni MWENDAWAZIMU WANGU
Bwana MPHINGU, naomba uchukue wasaa wako kidogo upitie kamusi ya TUKI. Baradhuli ina maana ngapi.
 
hapo mtani wangu Mmasai Molel, kidogo naanza kukuelewa kuwa BARADHULI ina maana zaidi ya moja
 
Tafsiri jina langu la MPHINGU kama mim nilivyo tafsiri la kwako MOLEL, nikajua wewe ni MMASAI
 
Simulizi ni nzuri na inavutia sana sasa Bakari cjui ndiyo kafa ivyo au laah
 
Cc: Kaburungu , zinginary , nancy1983 , compact , matobholo , alphaking mahena , juma chief , fakalava , ArchAngel
Kumbe na huku upo wacha nifanye marejeo ambaye hajui hii Simulizi ataiona ya kawaida lakini mimi sitachoka kuisoma.
 
Mkuu SteveMollel hongera kwa kazi nzuri nilianza kuipitia hii kitu "BARADHULI MWENYE MIKONO YA CHUMA" jana mida ya saa 3 usiku yaan kila nilipomaliza sehemu moja ndipo nilizidi kushawishika kuendelea na sehemu iliyofuata mpaka saa 9 usiku ndipo nikamaliza na kulala
*Mtiririko wa matukio ukopoa
Ila matukio ya mauaji na uchawi wa kutisha i real enjoy it!
*Wahusika umewachora vizuri but huyu Jombi rafiki wa Miraji ilikuwaje asifunguliwe mashtaka dhidi ya mauaji aliyoyafanya
*Pia hongera kuhusu mauzauza ya kile kisiwa cha Bagamoyo inasemekani si pahala pa mchezomchezo
Aysee endelea kutupia mzigo mkuu
 
***SURA YA KUMI NA NANE***





(MSIMU WA 02)






Mvuvi mmoja alipaza sauti, mara wenzake nao wakamuunga mkono kwa kuita. Punde, watu waliokuwa maeneo yale wakarusha macho yao kule sauti ilipotokea. Jombi kwa woga akaanza kukimbia. Amah! Watu wakaanza kutiririka kuwafuata wakina inspekta wakiwa wamebebelea silaha. Hakukuwa na jinsi, inspekta na Kaguta wakaanza kukimbia kwa kasi, nyuma yao rundo la wananchi likiwafukuza.




Mawe yalirushwa kama risasi, moja likambonda inspekta mgongoni kwanguvu na lingine likamtwanga Kaguta maeneo ya shingoni, ila hawakukoma kukimbia. Waliziba vichwa vyao na mikono, miguu ikafanya kazi yake ya kuwatoa hatarini.




Baada ya dakika tatu wakalifikia gari, walifungua milango na kuingia kwa pupa gari likahepa milango ikiwa wazi. Kabla gari halijatokomea wananchi walirusha mawe, kioo cha nyuma cha gari na shepu ya gari vikawa nyang’a. Milango ya gari ikafungwa huko mbele ya safari, wakina inspekta wakawa wameokoka.



“Aisee! Ilikuwa bado kidogo tu.” Kaguta alisema huku akitikisa kichwa chake.
“Tatizo Jombi ulikimbia.” Inspekta alisema na kuongezea, “Ungetulia tu, ulipokimbia ndio ukawa umewasha moto sasa.”
“Mimi niliogopa ndugu yangu” Jombi alijinasibu, “kusikia tunaitiwa majambazi utulivu ukanitoka kabisa.”
“Unapokimbia ndio unakuwa umethibitisha kwamba wewe ni jambazi. Ila tushukuru maana ni Mungu tu,kama tungetiwa mikononi sijui ingekuwaje?” Inspekta alieleza.
“Yani sipati picha. Yani leo lazima niende kupiga kinywaji kwanza kujipongeza, maana si kwa ile shughuli.” Kaguta naye akaeleza.
“Ila jamani, Bakari atakuwepo wapi?” Jombi alirush swali.
“Hakuna anayejua, ila nadhani atakuwa kauwawa kwenye kile kisiwa. Kuna majaribu mengi sana mule.” Inspekta alitoa maoni yake, Kaguta akamuunga mkono;
“Hauko mbali na mimi kabisa. Huo ndio ukweli.”



Walipofika Dar, wakaenda kumpitia Marietta shuleni na kwenda nae nyumbani. Walimkuta mama Miraji akiwa amejaa tele sebuleni macho yake yakiwa yapo bize kuangalia runinga.





“Karibuni jamani.” Mama Miraji alisema kwa tabasamu pana. Wakina inspekta wakaingia pamoja na mtoto wakaketi na kupeana salamu.
“Inaelekea huko mlipotoka ilikuwa purukushani eenh, naona mmebadili rangi za mavazi kabisa.” Mama Miraji alitumbuiza.
“Yani we acha tu. Kutuona hapa hai ni kama miujiza!”Inspekta alisema huku aktikisa kichwa chake. Mama Miraji akaona jeraha la Kaguta shingoni.
“Mmmh … Kaguta, upo sawa?”
“Nipo sawa tu!”
“Mbona una jeraha shingoni latoa damu?”



Kaguta akajishika kwenye jeraha na kutizama vidole vyake, akaona damu. Akatabasamu kiuongo.




“Kidogo tu si saana. Ni pakuosha tu na kutia spirit.”
“Pole sana.”
“Hapana shida hapa dada.”




Inspekta alinyanyuka na kuwatakawenzake waende chumbani wakajiweke safi, wote wakanyanyuka na kwenda, mama Miraji akaona alama ya damu mgongoni mwa inspekta, akaishia kutikisa kichwa na kusema;




“Kuna kitu.”




Alimvua mwanae nguo za shule akampa chakula. Baada ya hapo, akapakua chakula na kukiweka mezani kwenye hotpot tayari kwa ajili ya wanaume watatu waliojileta nyumbani. Baada ya kula, Kaguta akaaga na kuahidi kurudi baadae. Nyumbani akabaki Jombi, mama Miraji na Marieta.





Baada ya muda kidogo, Jombi akaenda kupumzika kwenye chumba cha wageni, naye Marieta akaenda kujipumzisha kwenye chumba cha pili cha wageni alalamo yeye na mamaye, sasa akabaki inspekta na mama Miraji sebuleni, peke yao. Walipiga soga ila baada ya muda zikakata. Inspekta naye alijinyanyua akajinasibu anaenda pumzika, ila kabla hajaondoka mama Miraji akamuuliza;





“Inspekta, naweza nikakuhudumia?”




Inspekta akawa mkanganyikoni. “Kunihudumia kivipi yani?”
“Mgongoni kwako bado unavuja damu. Naomba nikuhudumie.”




Inspekta kwa sura ya haya akatabasamu. Hakuwa ametegemea kama mama Miraji aliona jeraha lake. Na labda kwa haya yake hiyo akawa hana budi kuvua shati lake na kujilaza kwenye kochi apate huduma.




Mama Miraji akaelekea ndani na kutoka na kiboksi kidogo chenye msalaba mwekundu, akakifungua na kutoa pamba na dawa fulani ya buluu kwenye kachupa kadogo kisha akajivika glovu na kuanza kutizama jeraha la inspekta.




“Mmmh umechimbika. Ulipigwa na nini hapa?”
“Jiwe.”
“Ilikuaje mpaka ukapigwa hivi?”
“Kuna wapumbavu walituitia mwizi.”
“Aisee! … Poleni. Vipi mmempata huyo mzee?”
“Hapana. Huwezi amini tumemtafuta bila ya mafanikio, zaidi kuona mauza uza tu.”
“Poleni. Si kazi ndogo kabisa.”



Wakati hayo maongezi yanachukua nafasi, mama Miraji taratibu alikuwa akisafisha jeraha kwa dawa. Inspekta alikuwa amefumba macho akisikilizia kila hatua.




“Ulishawahi kuwa nesi nini?” Inpekta aliuliza huku akitabasamu kwa mbali.
“Hapana, ila nina diploma ya nursing. Kabla sijaenda kazini niliolewa na mume wangu hakutaka niendelee na hiyo taaluma tena.”
“Pole.”
“Nishapoa kitambo mpaka naona n’shasahau kabisa hayo mambo.”
“Hujasahau bana, mbona bado una hiko kitu kabisa mikononi?”
“Kweli?”
“Kweli.”
“Ahsante. Ni kitu ambacho nilikuwa nakipenda tangu utotoni.”




Baada ya hayo maneno, kaukimya kakatawala anga. Ni sauti tu ya mikono ya mama Miraji ndiyo ikawa inasikika ikichua eneo la maumivu. Baada ya dakika moja, mama Miraji akasema;





“Inatakiwa ushonwe hapa. Pamechimbika.”
“Si unishone wewe nesi?”
“Mimi?”
“Ndio!”
“Ila sijawahi.”
“Si ulisomea?”
“Ndio.”
“Fanya basi.”





Mama Miraji alivuta na kushusha pumzi ndefu, akatoa uzi ndani ya kiboksi chake pamoja na kakipini akaanza kushona jeraha la inspekta kwa taratibu na kwa uangalifu mkubwa. Bila ya ganzi tendo likafanyika, inspekta aking’ata tu meno kwa maumivu.





Tendo lilipokamilika, mama Miraji akashusha pumzi tena kama mtu aliyetoka kufanya shughuli pevu mno. Akampongeza inspekta na kumuambia amemaliza.




“Hongera.” Inspekta alitoa pongezi huku akijigeuza na kuulalia mgongo.
“Ahsante. Natumai sijakuumiza sana.”
“Hujaniumiza, nashukuru sana kwa huduma yako.”
“Karibu muda wowote.”




Inspekta alinyanyuka akaketi kitako wakawa wanatizamana na mama Miraji bila ya kuongea kitu. Kwa muda wa dakika moja waliacha macho yao yatizamane, kisha taratibu wakaanza kusogezeana usokama watu wanaotaka kubadilishana mabusu. Kabla hawajafikiana, sauti ya Marieta ikasikika;




“Mama!”




Haraka inspekta na mama Miraji wakatengua pozi lao na kukaa kama vile hawakuwa pamoja.




“Nini mwanangu?”
“Nasikia kiu.”





Marieta alisema huku akifikicha fikicha macho yake kwa usingizi. Mama Miraji akanyanyuka na kwenda kumchotea mwana maji. Inspekta akaegeshea shati lake mwilini naye akaaga anaenda chumbani.




***

☆Steve
 
***SURA YA KUMI NA TISA***





(MSIMU WA 02)






Akiwa ameketi juu ya kiti kirefu mikono yake kaigemeza kwenye meza ya glocery, Kaguta alikuwa akipata kinywaji kigumu aina ya spirit tena kwa tarumbeta huku taratibu akitingiha tingisha kichwa chake kuonyesha kuvutiwa na muziki upigwao.



Baada ya kumaliza kinywaji chake akaagiza tena kingine kama kile kile akaendelea na starehe zake. Ila baada ya muda kama dakika tano tangu aagize kinywaji kipya, akamuita muhudumu na kumuuliza;
“Bhoke yupo wapi?”



Muhudumu akabinua mdomo na kurembua macho.




“Bhoke hayupo zamu leo, ila mimi nipo sema tu shida yako.”



Kaguta akatabasamu.




“Wewe utaniweza?”
“Kwanini nisikuweze? … Ngoma kubwa hii!”
Hapo Kaguta akacheka na kutikisa kichwa chake.
“Hapana! Hapana kwa kweli. Am sorry. Mi namtaka Bhoke, mtoto mashaalah sana yule, mie ndio type zangu zile!”
“Haya, ndio hayupo sasa!”
“Niitie basi, n’takutoa kidogo.”
“Shing’api?”
“Aaaah we niitie bwana hatuwezi shindwana.”



Mhudumu akampigia simu Bhoke. Baada ya dakika zisizozidi dakika kumi na tano Bhoke akaingizana eneoni na bodaboda. Alikuwa amevalia kimini kuntu chekundu akiacha mapaja yake makubwa rangi ya chocolate yabarizi. Kwa furaha walikumbatiana na Kaguta wakajuliana hali.





“Mbona umen’tupa hivyo, Benson?”



Bhoke alisema kwa tabasamu pana.




“Kazi zinanibana, Bhoke.”
“Kazi wapi wewe sema kama umepata uchi mwingine.”
“Aaaah Bhoke, nani kasema tena hayo?”
“Tatizo lako hata namba zako hukunipa nashindwa hata kukutafuta kwa njia yoyote ile.”
“Hata kama nikikupa namba yatakuwa yaleyale maana nabadili mara kwa mara. We tulia tu n’takuwa nakutafuta kama hivi.”
“Haya bana. Mie sina neno.”
“Nichum basi mtoto.”



Bhoke akambusu Kaguta shavuni.




“Utanibusuje shavuni bana kama mama yako?” Kaguta alilalamika. Bhoke akampa ulimi kabisa.
“Sasa je, mambo si ndio hayo. Kaa hapo unywe mrembo.”




Bhoke akaketi kwenye kiti cha pembezoni na Kaguta akaagiza safari, taratibu akaanza kuisuuza nafsi kwa kinywaji hiko huku wakipiga soga.




“Sasa mtoto, leo si unaenda kulala kwangu?”
“Unavyotaka wewe, mi sawa tu. Ila utanileta kazini kesho maana zamu yangu mchana.”
“Hilo tu, kuna kingine?”
“Walaah sema tu nimemis shoo zako za kibabe.”




Wakacheka na kugongeshana viganja. Kaguta akanyanyuka akalipia vinywaji na kumtoa muhudumu ngalawa kadhaa kisha wakaaga wakaondoka wakiwa wameshikana viuno. Wakati wanatoka kwenye geti la baa, wakapishana na Sandra. Kaguta hakuamini macho yake alidhani labda ni ulevi, alitikisa kichwa akatizama vizuri, akamuona kweli Sandra.




“Si unajua gari langu? Shika funguo, tangulia naja.” Kaguta alimpa maelekezo Bhoke.
“Unaenda wapi tena?”
“We tangulia, naja.”
Kaguta alisema kisha akashika njia kurudi ndani ya bar. Alimtizama Sandra anaelekea wapi, akamuona amemfuata mwanaume mmoja hivi mzee, yule aliyemtoa Robson polisi kipindi kile alivyokamatwa barabarani. Sandra akakumbatiana na huyo mzee na kupeana mabusu kisha wakaketi. Kaguta alitoa simu yake ya mkononi akaanza kuwarekodi kwa tahadhari asionekane.




Ali zoom na kuhakikisha amewajaza wahusika wake kwenye kioo barabara. Hapo akapoteza dakika kama tatu kabla ya honi ya gari haijamshtua na kukumbuka kuna mtu anamsubiria.



“Muda wote huo? Au ulikuwa na kademu kengine huko?”
“Wala! Kuna mtu nilipotezana naye muda sasa nikamuona leo, si unajua tena.”



Kaguta alijitetea, akawasha gari wakaondoka eneo lile.



Asubuhi palipokucha, Kaguta aliamka mapema akamuacha Bhoke kitandani amelala, akavaa nguoze za mazoezi na kutoka nje akaanza kupasha viungo vyake kwenye uwanja wa nyumba yake. Alipiga push up kadhaa, akaruka kamba. Alijog na kukimbia. Alipomaliza akarudi ndani na kumuamsha Bhoke waende kuoga.




Wakaenda kukoga na wakapata kifungua kinywa. Baadae Kaguta akampeleka Bhoke kazini kwake kisha yeye akaelekea Rosemath stationary. Alipaki gari lake upande wa pili wa barabara akawa anatizama eneo la stationary kwa mbali.




Muda ukayoyoma kama masaa mawili hivi likaja gari jeusi Suzuki Escudo likapaki nje ya stationary. Honi ilipigwa akatoka Sandra huku akiwapungia wenzake mkono wa kwaheri, akaingia ndani ya Escudo na gari likaondoka. Taratibu Kaguta akaanza kulifuatilia lile gari kwa nyuma.





Baada ya dakika kadhaa Escudo likapaki mbele ya duka kubwa la nguo maeneo ya Sinza, mzee akashuka na Sandra wakaingia ndani ya duka. Kaguta akawachukua video bila ya wao kujua. Baada ya kama lisaa yule mzee na Sandra wakatoka dukani na kurudi garini kisha Sandra akarejeshwa stationary na gari likaondoka.




Kaguta alipaki palepale alipokuwa amepaki awali. Alifungua video zake akawa anazitizama kwa makini. Alipomaliza aliweka simu yake kando, akalaza kiti na kutulia. Jioni iliposonga, stationary ikafungwa. Wadada wakatoka ofisini mwao na kutawanyika kwenda majumbani. Sandra akaja kuchukuliwa tena na gari lile lile, Escudo nyeusi, akapelekwa mpaka nyumbani kwake kisha gari likaondoka. Lilipotokomea, Kaguta akashuka na kuanza kuisogelea nyumba ya Sandra.




Akiwa ndani ya chumba chake, Sandra alivua nguo akavaa taulo jepesi kisha akaelekea bafuni kukoga. Alipotoka bafuni akamkuta Kaguta kajilaza kitandani. Akapigwa na butwaa.




“Wewe unafanya nini hapa?”
Kaguta akatabasamu.
“Vipi, kwani Roby anakuja?”
“Umeingiaje humu?”
“Kupitia mlangoni.”
“Mlango mbona nimefunga?”
“Haukufunga vya kutosha kunizuia nisiingie. Ila tuachane na hayo, njoo basi.”
“Wapi?”
“Aaah aah! Kwani kuna shida gani, Sandra?”
“Hujui? Mimi sina urafiki na maaskari.”
“Ndio mana ukanchoma siku zile ili bwana’ako afanye tukio?”




Kimya. Kaguta akasimama na kumsogelea Sandra akamshika kalio. Sandra akausukumizia pembeni mkono wa Kaguta.




“Usinishike!”



Kaguta akacheka kisha akawa serious ghafla.




“Kwanza mimi si askari. Si umeona hii?” Kaguta alionyeshea tattoo yake mkononi baada ya kukunja shati lake.
“Pili, siku zile ulinichomea na kunifanya nionekane mpumbavu, bwana’ako akafanya uhalifu. Leo ni zamu yako. Umeona hii?”



Kaguta akaanza kuonyeshea video za Sandra alizorekodi.




“Lazima zimfikie Roby. Kwahiyo jiandae.”



Kaguta alisema kisha akageuka na kuufuata mlango atoke. Ghafla Sandra akamshika mkono. Kaguta alipogeuka akamuona mwanamke kama alivyozaliwa.




“Tafadhali Kaguta, usifanye hivyo. Hujui ni kwa kiasi gani utafanya mambo yawe magumu kwangu na kwa Roby pia. Utasababisha vita kubwa. Please.”



Kaguta akatabasamu na kusema;
“Nitafanya utakavyo, endapo tu utanipa maelezo yote ninayoyahitaji. Upo tayari?”




Sandra alitizama chini na macho yaonyeshayo njia panda. Ni kama vile alikuwa ng’ombe mwembamba aliyelazimishwa ale majani ya shamba nzima ili kesho awe mnene mnadani. Mwishowe aliamua aketi kitandani na kumtizama Kaguta, akafungua mdomo kwa sauti iliyo karibu na mashaka;



“Unataka kujua nini toka kwangu?”




Kaguta akatabasamu. “Hayo ndio mambo sasa! … Kwanza, yule mzee uliyekuwa naye ni nani?”
“Anaitwa Isaac Makongo. Ni mkuu wetu.”
“Mkuu wenu kivipi?”
“Yeye ndiye coordinator. Kila kitu kutoka kwa mkuu hupitia kwake. Kuanzia pesa mpaka vifaa.”
“Kwahiyo ndio upo naye kimahusiano?”



Hapo Sandra alitulia kwanza na kupunguza kasi yake ya kujibu. Alitizama chini, Kaguta akarudia kuuliza swali.



“Si kwamba nipo naye kimahusiano.”
“Bali?”
“Ananitaka na sijui njia ya kumkatalia.”
“Hujui? Kwani wengine unawakataliaje?”
“Kumbuka nimekuambia yule ni mtu mkubwa. Kumkatalia maana yake ni kujiweka kwenye mazingira magumu mno hata kufa pia!”
“Kwahiyo kila mwanamke akitaka kuwa naye anampata, sio?”
“Nadhani.”
“Na vipi kumhusu Roby?”
“Kaguta, hakuna yeyote ninayempenda kati ya hao. Ni mazingira tu yananibana na kuniacha bila ya jinsi.”
“Na utakuwa mtumwa hivyo mpaka lini, Sandra?”



Sandra alidondosha chozi kusikia hilo swali. Alijifuta na vidole vyake vitatu lakini bado hakujibu, alikuwa anatizama tu chini mithili ya mtu anayejutia.




“Nani alikuingiza katika huu mtandao, Sandra?”




Kaguta aliuliza kwa sura ya huruma. Sandra hakujibu, bado alikuwa ameinamisha uso wake akitiririsha machozi. Baada ya dakika kama tano, Sandra ndipo akatia neno kwa sauti ya kukoroma tena huku akivuta makamasi ya kilio.




“Tokea nikiwa na miaka mitano, nilikuwa tayari nina chapa mwilini mwangu. Baba yangu alikuwa mtumishi mkubwa wa bwana Kim kiasi kwamba aliahidi familia yake yote kumtumikia mungu mtu huyo, Kim. Hata mama yangu pia akapigwa chapa na kuwa mfuasi, bahati mbaya yeye na mumewe hawakudumu. Waliuwawa wakiwa kazini na kuniacha yatima asiye na baba wala mama isipokuwa tu chapa niliyo nayo ya bwana Kim.”





Machozi yakawa kama mto kwenye mashavu ya Sandra. Alishindwa tena kuongea, akawa analia tu. Kaguta alimvuta na kumkumbata.




“Usilie, Sandra. Yatakwisha.”
“Hayawezi kwisha Kaguta, kamwe.” Sandra alisema kama mtu mwenye uhakika haswa na jambo analolitema. Kaguta alimbembeleza kama mwanaye, Sandra alipopoa ndio maelezo yakaendelea;
“Tokea hapo, nilichokuwa nakula, nakunywa na navaa ilikuwa ni juu ya taasisi ya bwana Kim. Nilikulia katika mikono hiyo mpaka leo hii najitambua japo siwezi kufanya lolote lile.”
“Hakuna jaribu lisilo na njia ya kutokea.”
“Hapana, Kaguta. Lipo na hili ni mojawapo. Ni ngumu mno kumshikia bwana Kim chini, nchi nzima ipo mikononi mwake. Serikali na mitaa yote ni ya kwake. Unaanzia wapi?”
“Amini mlango upo. Ila tu umepakwa rangi inayofanana na ukuta. Hatuna budi kuutafuta, kwa pamoja tutaweza.”
“Kwa pamoja?”
“Ndio, wewe na sisi.”




Sandra akatabasamu kidogo kisha akatikisa kichwa chake kwa mbali.




“Huwezi ukafanya lolote kwa sasa. Wewe ni mfuasi wa bwana Kim, hiyo chapa uliyo nayo haitokuruhusu ufanye jambo.”
“Hapana. Chapa hii itanizuia tu kutoa siri na si kufanya mengine.”
“Nani kakudanganya? … Ukishawekwa hiyo chapa, huyo aliyechorwa hapo mkononi mwako anaona kila unachokifanya. Kila hatua unayochukua. Kila utakachokuwa unakifanya atakutangulia kwa hatua tatu mbele. Weka hilo akilini mwako. Na hakuna lolote utakalofanya dhidi ya Mr Kim ukafanikiwa.”





Kaguta alitizama tattoo yake mkononi kwa uso wenye ndita. Aling’ta lips akashusha pumzi ndefu. Kwa muda kama wa kasoro dakika kukawa kimya. Kaguta alikumbuka yake yaliyokuwa yanatukia kule kisiwani akijaribu kulinganisha na kile akisemacho Sandra. Ni kweli walikuwa wanatanguliwa hatua tatu mbele? Alijiuliza hilo swali, sidhani kama alipata majibu, akamgeukia Sandra.



“Wapi naweza kumpata Isaac?”
“Wa nini, Kaguta? … Nimeshakuambia haiwezekani.”
“Nijibu maswali yangu.”
“Anaishi kurasini, nyumba namba 898.”
“Unaweza nambia anapendelea kitu gani, ama kutembelea maeneo gani … au ni mtu wa aina gani?”
“Anapenda sana mpira. Huwa hakosi kwenda kutizama mpira hasa Samaki Samaki ya maeneo ya Mbezi beach.”
“Ok.”





Kaguta akachukua simu toka mfukoni mwake akapakua application ya mpira na kuangalia ratiba ya mechi kubwa iliyo karibu, akaona mojawapo iliyopo kesho tena ikiwa ya ubingwa wa ulaya. Alitabasamu, akaenda kwenye reminder ya simu na kuweka tarehe ya mechi hiyo. Alipomaliza, alinyanyuka akamtizama Sandra na macho ya ahadi.





“Naomba niende nikuache upumzike. Tutaonana karibuni.”
“Okay. Take care.”
“You too!”




Kaguta akauendea mlango na kutoka nje. Sandra alivaa nguoze akajilaza kitandani. Hakuoneana yupo sawa. Si kingine itakuwa ni mawazo yalikuwa yanambana. Ila baada ya muda mafuriko ya usingizi yalimsomba na kumpeleka ng’ambo.





****

☆Steve
 
Wewe mama miraji. Mie Inspector Vitalis. Khaaah. Kumbe ndoto. Ndoto zingine za kiffala!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom