Xav Emmanuel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2018
- 215
- 316
- Thread starter
- #61
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (23)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
--------------------------------------------------
“Naaaam!, japo sikufa na kuumia sana. Lakini nilizimia. Nilijikuta tu nipo sehemu ambayo kuna weupe weupe ule wa hospitali!. Nilipoteza tena kumbukumbu kwa mara ya pili. Jambo lingine la kumshukuru Mungu ni kuwa hakuna nilichokumbuka zaidi ya jina langu tu Rose!. Nilipozinduka hapakuwa na mtu yoyote sehemu hile.
Chumba kilikuwa vizuri lakini hakuna nilichokumbuka. Nilijichekea tu mwenyewe. Kwa hali niliyokuwa nayo nilipaswa kabisa kupitilizwa hospitali kuu ya taifa ya vichaa Dodoma inaitwa milembe sijui. Nilikuwa sijielewi.
ENDELEA SEHEMU YA ISHILINI NA TATU…
Nilikaa hapo kitandani hadi alipofika mtu kwa cheo cha nesi. Alinijulia hali na kuniuliza maswali kadhaa ambayo majibu yake yalikuwa yanafanana.
“Sikumbuki chochote nesi!” ilo ndio jibu la kila swali nililoulizwa. Nilikuwa mkali haswa.
Uwezi amina Kaka, nilikumbuka jina langu tu Rose! Basi. Na kila nikijaribu kuwaza na kufikilia mimi ni nani kichwa kinaniuma tu!. Sijui nililogwa tena kwa mara ya tatu?.! Lakini nisiseme hivyo ni mipango ya Mungu.
Basi nilipotoka hospitali sikuwa na sehemu wala mwelekeo wa kwenda. Nilipitia vipindi vigumu vigumu kiasi kwamba kila kazi ya mbele ilikuwa yangu!. Nilikuwa msaidizi wa Mama ntile: Nikafukuzwa!, nilikuwa mfanya kazi wa ndani: Nikafukuzwa, nilikuwa muuza mboga mtaani: Nikaachishwa, nikarudi kuwa Msadizi wa Mama ntilie sehemu nyingine.
Huko ndipo nilipokutana na wewe Abdul, Abdul ambaye ni mpenzi wangu niliempenda sana. Abdul niliyekubali kumtunza na kumlea kwa miaka yote. Abdul ambaye niliangaika naye kutafuta mtoto na nikakosa. Abdul ambaye alikuwa mwamba wa kugundua vichochoro na njia za kutafuta pesa. Kumbe Abdul ni we-we, we!, Denis!
Kaka toka hapo hadi nakutana na wewe!, sikuwai kumbuka historia ya maisha yangu!, lakini naamini Damu!, Damu Kaka!. Damu ni nzito kuliko maji!.khaa!, umewezaje kunirudisha tena Utotoni kaka!. Nakumbuka sasa, nakumbuka hata mapigo ya moyo ya kipindi hiko tunasakwa na Baba Mchafu Frank!. Kumbe ndio huyu mbwa ambaye anatufuatilia kututokomeza kila siku! Bustard!..
Kaka ni mimi mdogo wako kabisa Maria!, ona!, ona kovu hili! Ona Kaka.!” Maria alinyanyuka pale alipo bila woga na kuanza kupandisha gauni lake refu kuonyesha kovu aliloongelea. Hakumaliza kulionesha lote akafunika na kufumba macho, akavuta hewa ndefu iliyopitia puani.. Kilio cha maneno machache kikafuata!.
“Oh!! Kaka kumbe huoni e?!. nijibu Kaka! Huoni?!” alifunika nguo yake na kulia bila mpangilio. Nilipoangaza kwa Abdul!, nae alikuwa ameshachanganya kabisa kulia.
Alihakikisha analia polepole ili kila aliyeko mahali pale asijue kama analia. Anafichaje sasa? Ficha moyo sio machozi!. Tulishaligundua hilo. Abdul ambaye ndiye Denis alikuwa anabwabwaja tu midomo kabla ya kusikika anachoongea. Mwishoni akatoa sauti.
“Ma….. Mari…… Maria! Maria eh!, Itika mdogo wangu!. Napaswa adhabu ya kushindwa kukutunza mdogo wangu. Nimekuaribia maisha yako!. Laana ya mwenyezi mungu hakika ipo mbele yangu. Katu siwezi tena kuwa mchafu!, Kama nilivyokuwa mwanzo. Nisamehe wewe Maria jamani.. nimela-la na we-we ki-ta-nda kimoja bila kutambua wewe ni mdogo wangu. Tena sio mara moja. Tumelala zaidi ya neno kulala. Eh!! Mungu ni nini hiki!. Hii si aibu jamani? Oh jamani!. Lakini… lakini mimi nimelala na Rose sio Maria!. Aaaaagh!!” Denisi alikuwa anahangaika tu. Walishikana mikono kwa kila mtu kumjulisha mwenzake hali ya moyo wake. Mimi na mke wangu ni miduwazo tu kila mda!. Mara tunalia mara tunashangaaa, mara tuna… da. Jamani Denis na Maria!, tumewakutanishaje??. Vichwa vyetu vilijaa alama za mshangao tu.
“Kaka!, tungejuaje sasa?, Naona macho ya kila mtu yakiwa karibu. Hakuna budi kuandika yote haya katika kitabu kimoja. Mwandishi usijali utatumia karatasi ngapi!, kikubwa we andika tu. Usifiche chochote. Nimeikimbia dhambi ya kujulisha uma kuwa nimethubutu kutoa maisha yangu kafara kwa nia ya kutetea watu wengine. Sijali ni malipo gani Mungu atanipa lakini hakuna namna hata kama akiamua kuchukua pumzi yake. Hakika tumekosea sana Kaka. Nashindwa nikutazame vipi!. Ivi wewe ni Mume wangu Abdul au Kaka yangu Denis?. Nimekubali kufa, hata kufa kwa kunyongwa lakini lazima nilipe kisasi kwa baradhuri Fred na ukoo wake!. Baada ya hapo kifo chema kitakuwa juu yangu. Ni ta po te a, nitapotea kaka!.” Alikuwa ni Rose mikononi mwa Abdul. Mtu na mke wake wa zamani. Mtu na dada yake wa sasa! Wanayoyaongea wanajua wenyewe..
********
Naaaaam!, hatukuwa tena na muda wa kupotea tokea hapo. Kilichobaki ni kutetea matumbo yetu yasiteketee kwa njaa. Niliwapanga wote Denis na Dada yake Maria kuwa wawe watulivu, suala lao lipo katika mchakato wangu.
Nikawaambia kuwa simulizi yao itakuwako katika kila haina ya chombo cha habari Tanzania, Afrika na Duniani kwa ujumla. Nikawaahidi kuwa wahusika wote waliosababisha maangamizo hayo watatiwa nguvuni, na si vyema kufuata sheria za bongo zao maharufu kama Sheria mkononi. Kwani Sheria ina pande zote mbili.
Sikusita kupata ujasiri wa kuwaahidi kuwa mali zote zitarudi mikononi mwao, kwa kuwa tayari Denis alishadokeza sehemu ambayo hati za mali za Baba yake zilikuwepo. Alisema.
“Kila kitu kipo kwa mwanashiria, alikuwa ni mwanasheria wa kijitegemea wa Baba. Kama baba alijua hivi, alimkabidhi kila kitu Mwanasheria huyo kwa kuhisi kabisa ipo siku mali zake zitaingia mikononi mwa wanajangili. Kama alitabiri hivi Mzee Yohana. Lakini sijui kama huyo Mwanasheria bado yupo hai au la!. Na kama yupo hai basi yupo nje ya nchi au amejificha sehemu za maficho. Bila shaka naye amepitia wakati mgumu kama sisi!.
Ndio mwandishi anaitwa Mwanasheria Credo Mwanuta!.!, Ndio, Ndio siwezi sahau jina lake kwa kuwa alikuwa rafiki yangu sana. Alikuwa ni mtani wangu kila tunapokutana. Ndio… Ndio…. ni Credo Mwanauta!.” Denis alitaja jina ambalo sio ngeni sana kwangu. Alikuwa ni Mwanasheria wa kujitegemea kwa kipindi hicho, aliwika sana miaka ya tisini kwa kuitambua vizuri sheria. Baada ya hapo. Akapotea!. Jina lake likasahaulika.
Nilianza harakati za kumtafuta kwa kutumia mitandao ya kijamii. Sikumtapa, kwani akaunti zake zote zilionesha zimefungwa mda mrefu sana. Siku hiyo niliitumia kumaliza kila kitu kinachohusu historia hii. Kumaliza hii simulizi ya vijana wawili ambao bila shaka dunia inapaswa kujifunza mengi kutoka kwao.
Kwa vile nilikuwa na ruhusa kazini na taaluma yangu iliruhusu kuingia kila sehemu, nilifanikiwa kukutana na muweka kumbukumbu na historia za wanasheria wilayani Ndugu Kharimu bin Mussa. Huko nikakutana na taarifa nusunusu tu kuwa mwanasheria huyo aliamia mkoa wa jirani wa Mtwara, kwa kujishughulisha na shughuli za kilimo cha korosho. Sio Mtwara hii unayoijua wewe!, ni Mtwara ndani ndani huko.
Nikachukua anuani zake na siku hiyo hiyo kupanda gari. Nilikuwa mimi mwenyewe binafsi na ushawishi wa kumfanya mzee huyo akubali wito wangu. Denis na dada yake niliwaacha na mke wangu nyumbani.
Ruhusa kutoka kazini haikuwa kikwazo kwangu. Ni kuomba tu na kupewa barua ya kuruhusiwa, si mambo ya kikazi bhana!. Na mimi ndio Baba lao!. Hivyo nikaenda Mtwara na kumtafuta huyo mzee ambaye alikuwa anawasimamia tu vijana wake kufanya kazi kwa jitihada, alikuwa ni mzee ambaye bila shaka alioga na kunywa chumvi nyingi sana. Nilifanikiwa kukutana naye na tukakaa kitako na kumpa dukuduku langu la kumuhitaji.
Hilo ndio tukio ambalo alikuwa analisubiri na kuliota kila siku!. Lini Denis atakuja kuchukua mizigo yake!!!. Sikupata shida kabisa katika kumwaminisha tayari alikuwa na hekima za uwelewa.
“Kijana, sheria imepinda sasa!, haijawa wima kama ilivyo mwanzo. Sasaa! Yaani ni bunda, chai, kahawa, na majani tu!. Pesa mbele, vifungu nyuma. Hakuna sheria kabisa sikuhizi!.” Alinidokeza Mzee Mwanauta ambaye alikuwa mwanasheria nguli kwa kipindi hiko.
Alikuwa akinipa fununu za kukengeuka kwa sheria kutoka zama za utu hadi zama za pesa!. Kila kitu ni mshiko tu!. Alinipasha yote wakati tupo kwenye gari kuja Songea. Hakuacha kunipasha pia kuhusu hamu yake ya kumuona mtoto wake Denis ambaye alisema pia alikabidhiwa na baba yake Denis Mzee Yohana kwani alimsimamia katika mafundisho ya dini yote, kuanzia kupokea Ubatizo wake.
Tulifika Songea na kumpeleka hadi sehemu ya tukio. Sehemu ambayo dhana ya nyumba ilitoweka kabisa na kubaki kuwa sehemu ya kupokea vilio na kukutanisha watu wasiojulikana.
Uzee wa Credo Mwanauta haukuwa kikwazo katika kutambua Denis ni yupi kati yetu. Aisee!, Mzee alilia. Alilia haswa!, alilia sio tu kutomuona Denis kwa kipindi kirefu hapana!. Bali ni afya tu ya Denis iliyopotelea sehemu isiyojulikana.
Ukubwa dawa!, hatukumnyamazisha, alitulia mwenyewe!. Alitumia busara sana. Hakuacha kumtazama Denis na kusikitika. Cha kushangaza akaongea neno ambalo lilifanya mapigo yangu ya moyo yabadili mwelekeo wake, yalipoteana kabisa yani. Eti nini!..
ITAENDELEA..
Sent using Jamii Forums mobile app
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
--------------------------------------------------
“Naaaam!, japo sikufa na kuumia sana. Lakini nilizimia. Nilijikuta tu nipo sehemu ambayo kuna weupe weupe ule wa hospitali!. Nilipoteza tena kumbukumbu kwa mara ya pili. Jambo lingine la kumshukuru Mungu ni kuwa hakuna nilichokumbuka zaidi ya jina langu tu Rose!. Nilipozinduka hapakuwa na mtu yoyote sehemu hile.
Chumba kilikuwa vizuri lakini hakuna nilichokumbuka. Nilijichekea tu mwenyewe. Kwa hali niliyokuwa nayo nilipaswa kabisa kupitilizwa hospitali kuu ya taifa ya vichaa Dodoma inaitwa milembe sijui. Nilikuwa sijielewi.
ENDELEA SEHEMU YA ISHILINI NA TATU…
Nilikaa hapo kitandani hadi alipofika mtu kwa cheo cha nesi. Alinijulia hali na kuniuliza maswali kadhaa ambayo majibu yake yalikuwa yanafanana.
“Sikumbuki chochote nesi!” ilo ndio jibu la kila swali nililoulizwa. Nilikuwa mkali haswa.
Uwezi amina Kaka, nilikumbuka jina langu tu Rose! Basi. Na kila nikijaribu kuwaza na kufikilia mimi ni nani kichwa kinaniuma tu!. Sijui nililogwa tena kwa mara ya tatu?.! Lakini nisiseme hivyo ni mipango ya Mungu.
Basi nilipotoka hospitali sikuwa na sehemu wala mwelekeo wa kwenda. Nilipitia vipindi vigumu vigumu kiasi kwamba kila kazi ya mbele ilikuwa yangu!. Nilikuwa msaidizi wa Mama ntile: Nikafukuzwa!, nilikuwa mfanya kazi wa ndani: Nikafukuzwa, nilikuwa muuza mboga mtaani: Nikaachishwa, nikarudi kuwa Msadizi wa Mama ntilie sehemu nyingine.
Huko ndipo nilipokutana na wewe Abdul, Abdul ambaye ni mpenzi wangu niliempenda sana. Abdul niliyekubali kumtunza na kumlea kwa miaka yote. Abdul ambaye niliangaika naye kutafuta mtoto na nikakosa. Abdul ambaye alikuwa mwamba wa kugundua vichochoro na njia za kutafuta pesa. Kumbe Abdul ni we-we, we!, Denis!
Kaka toka hapo hadi nakutana na wewe!, sikuwai kumbuka historia ya maisha yangu!, lakini naamini Damu!, Damu Kaka!. Damu ni nzito kuliko maji!.khaa!, umewezaje kunirudisha tena Utotoni kaka!. Nakumbuka sasa, nakumbuka hata mapigo ya moyo ya kipindi hiko tunasakwa na Baba Mchafu Frank!. Kumbe ndio huyu mbwa ambaye anatufuatilia kututokomeza kila siku! Bustard!..
Kaka ni mimi mdogo wako kabisa Maria!, ona!, ona kovu hili! Ona Kaka.!” Maria alinyanyuka pale alipo bila woga na kuanza kupandisha gauni lake refu kuonyesha kovu aliloongelea. Hakumaliza kulionesha lote akafunika na kufumba macho, akavuta hewa ndefu iliyopitia puani.. Kilio cha maneno machache kikafuata!.
“Oh!! Kaka kumbe huoni e?!. nijibu Kaka! Huoni?!” alifunika nguo yake na kulia bila mpangilio. Nilipoangaza kwa Abdul!, nae alikuwa ameshachanganya kabisa kulia.
Alihakikisha analia polepole ili kila aliyeko mahali pale asijue kama analia. Anafichaje sasa? Ficha moyo sio machozi!. Tulishaligundua hilo. Abdul ambaye ndiye Denis alikuwa anabwabwaja tu midomo kabla ya kusikika anachoongea. Mwishoni akatoa sauti.
“Ma….. Mari…… Maria! Maria eh!, Itika mdogo wangu!. Napaswa adhabu ya kushindwa kukutunza mdogo wangu. Nimekuaribia maisha yako!. Laana ya mwenyezi mungu hakika ipo mbele yangu. Katu siwezi tena kuwa mchafu!, Kama nilivyokuwa mwanzo. Nisamehe wewe Maria jamani.. nimela-la na we-we ki-ta-nda kimoja bila kutambua wewe ni mdogo wangu. Tena sio mara moja. Tumelala zaidi ya neno kulala. Eh!! Mungu ni nini hiki!. Hii si aibu jamani? Oh jamani!. Lakini… lakini mimi nimelala na Rose sio Maria!. Aaaaagh!!” Denisi alikuwa anahangaika tu. Walishikana mikono kwa kila mtu kumjulisha mwenzake hali ya moyo wake. Mimi na mke wangu ni miduwazo tu kila mda!. Mara tunalia mara tunashangaaa, mara tuna… da. Jamani Denis na Maria!, tumewakutanishaje??. Vichwa vyetu vilijaa alama za mshangao tu.
“Kaka!, tungejuaje sasa?, Naona macho ya kila mtu yakiwa karibu. Hakuna budi kuandika yote haya katika kitabu kimoja. Mwandishi usijali utatumia karatasi ngapi!, kikubwa we andika tu. Usifiche chochote. Nimeikimbia dhambi ya kujulisha uma kuwa nimethubutu kutoa maisha yangu kafara kwa nia ya kutetea watu wengine. Sijali ni malipo gani Mungu atanipa lakini hakuna namna hata kama akiamua kuchukua pumzi yake. Hakika tumekosea sana Kaka. Nashindwa nikutazame vipi!. Ivi wewe ni Mume wangu Abdul au Kaka yangu Denis?. Nimekubali kufa, hata kufa kwa kunyongwa lakini lazima nilipe kisasi kwa baradhuri Fred na ukoo wake!. Baada ya hapo kifo chema kitakuwa juu yangu. Ni ta po te a, nitapotea kaka!.” Alikuwa ni Rose mikononi mwa Abdul. Mtu na mke wake wa zamani. Mtu na dada yake wa sasa! Wanayoyaongea wanajua wenyewe..
********
Naaaaam!, hatukuwa tena na muda wa kupotea tokea hapo. Kilichobaki ni kutetea matumbo yetu yasiteketee kwa njaa. Niliwapanga wote Denis na Dada yake Maria kuwa wawe watulivu, suala lao lipo katika mchakato wangu.
Nikawaambia kuwa simulizi yao itakuwako katika kila haina ya chombo cha habari Tanzania, Afrika na Duniani kwa ujumla. Nikawaahidi kuwa wahusika wote waliosababisha maangamizo hayo watatiwa nguvuni, na si vyema kufuata sheria za bongo zao maharufu kama Sheria mkononi. Kwani Sheria ina pande zote mbili.
Sikusita kupata ujasiri wa kuwaahidi kuwa mali zote zitarudi mikononi mwao, kwa kuwa tayari Denis alishadokeza sehemu ambayo hati za mali za Baba yake zilikuwepo. Alisema.
“Kila kitu kipo kwa mwanashiria, alikuwa ni mwanasheria wa kijitegemea wa Baba. Kama baba alijua hivi, alimkabidhi kila kitu Mwanasheria huyo kwa kuhisi kabisa ipo siku mali zake zitaingia mikononi mwa wanajangili. Kama alitabiri hivi Mzee Yohana. Lakini sijui kama huyo Mwanasheria bado yupo hai au la!. Na kama yupo hai basi yupo nje ya nchi au amejificha sehemu za maficho. Bila shaka naye amepitia wakati mgumu kama sisi!.
Ndio mwandishi anaitwa Mwanasheria Credo Mwanuta!.!, Ndio, Ndio siwezi sahau jina lake kwa kuwa alikuwa rafiki yangu sana. Alikuwa ni mtani wangu kila tunapokutana. Ndio… Ndio…. ni Credo Mwanauta!.” Denis alitaja jina ambalo sio ngeni sana kwangu. Alikuwa ni Mwanasheria wa kujitegemea kwa kipindi hicho, aliwika sana miaka ya tisini kwa kuitambua vizuri sheria. Baada ya hapo. Akapotea!. Jina lake likasahaulika.
Nilianza harakati za kumtafuta kwa kutumia mitandao ya kijamii. Sikumtapa, kwani akaunti zake zote zilionesha zimefungwa mda mrefu sana. Siku hiyo niliitumia kumaliza kila kitu kinachohusu historia hii. Kumaliza hii simulizi ya vijana wawili ambao bila shaka dunia inapaswa kujifunza mengi kutoka kwao.
Kwa vile nilikuwa na ruhusa kazini na taaluma yangu iliruhusu kuingia kila sehemu, nilifanikiwa kukutana na muweka kumbukumbu na historia za wanasheria wilayani Ndugu Kharimu bin Mussa. Huko nikakutana na taarifa nusunusu tu kuwa mwanasheria huyo aliamia mkoa wa jirani wa Mtwara, kwa kujishughulisha na shughuli za kilimo cha korosho. Sio Mtwara hii unayoijua wewe!, ni Mtwara ndani ndani huko.
Nikachukua anuani zake na siku hiyo hiyo kupanda gari. Nilikuwa mimi mwenyewe binafsi na ushawishi wa kumfanya mzee huyo akubali wito wangu. Denis na dada yake niliwaacha na mke wangu nyumbani.
Ruhusa kutoka kazini haikuwa kikwazo kwangu. Ni kuomba tu na kupewa barua ya kuruhusiwa, si mambo ya kikazi bhana!. Na mimi ndio Baba lao!. Hivyo nikaenda Mtwara na kumtafuta huyo mzee ambaye alikuwa anawasimamia tu vijana wake kufanya kazi kwa jitihada, alikuwa ni mzee ambaye bila shaka alioga na kunywa chumvi nyingi sana. Nilifanikiwa kukutana naye na tukakaa kitako na kumpa dukuduku langu la kumuhitaji.
Hilo ndio tukio ambalo alikuwa analisubiri na kuliota kila siku!. Lini Denis atakuja kuchukua mizigo yake!!!. Sikupata shida kabisa katika kumwaminisha tayari alikuwa na hekima za uwelewa.
“Kijana, sheria imepinda sasa!, haijawa wima kama ilivyo mwanzo. Sasaa! Yaani ni bunda, chai, kahawa, na majani tu!. Pesa mbele, vifungu nyuma. Hakuna sheria kabisa sikuhizi!.” Alinidokeza Mzee Mwanauta ambaye alikuwa mwanasheria nguli kwa kipindi hiko.
Alikuwa akinipa fununu za kukengeuka kwa sheria kutoka zama za utu hadi zama za pesa!. Kila kitu ni mshiko tu!. Alinipasha yote wakati tupo kwenye gari kuja Songea. Hakuacha kunipasha pia kuhusu hamu yake ya kumuona mtoto wake Denis ambaye alisema pia alikabidhiwa na baba yake Denis Mzee Yohana kwani alimsimamia katika mafundisho ya dini yote, kuanzia kupokea Ubatizo wake.
Tulifika Songea na kumpeleka hadi sehemu ya tukio. Sehemu ambayo dhana ya nyumba ilitoweka kabisa na kubaki kuwa sehemu ya kupokea vilio na kukutanisha watu wasiojulikana.
Uzee wa Credo Mwanauta haukuwa kikwazo katika kutambua Denis ni yupi kati yetu. Aisee!, Mzee alilia. Alilia haswa!, alilia sio tu kutomuona Denis kwa kipindi kirefu hapana!. Bali ni afya tu ya Denis iliyopotelea sehemu isiyojulikana.
Ukubwa dawa!, hatukumnyamazisha, alitulia mwenyewe!. Alitumia busara sana. Hakuacha kumtazama Denis na kusikitika. Cha kushangaza akaongea neno ambalo lilifanya mapigo yangu ya moyo yabadili mwelekeo wake, yalipoteana kabisa yani. Eti nini!..
ITAENDELEA..
Sent using Jamii Forums mobile app
..