Simulizi: "Angamizo"

Simulizi: "Angamizo"

SIMULIZI: “ANGAMIZO” (06)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: Xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
Social Net: @star_xav

Baba alikuwa mtu mkubwa amabaye, hata akiomba sehemu awe kiongozi basi wapinzani wote wanarudi nyuma kwa kuogopa ushindani; pesa zilitupa kiburi mno. Nadhani huu ndio mshahara wa dhambi zetu, umenitesa sana Baba!, umemtesa Mama, Umemtesa Maria, Umenitesa mimi na kizazi chako kijacho!, ziko wapi pesa zako Baba!!”. Abdul aliishia hapo na kuanza tena kulia, kilio chake hakikuwa cha sauti, nyumba yote ilikuwa kimya sana.

Mke wangu alikuwa ameduwaa kwa utamu na uchachu wa machungu wa maneno alikuwa anautoa Abdul, Abdul alikuwa fundi wa lugha kweli kweli, kwa hatua hii hakuna asiyeamini kuwa mtaa ulimfunza. Baada ya kufuta chozi mwanaume akaendelea…

ENDELEA SEHEMU YA SITA…

“Mwandishi, si unajuwa kuwa Akipangacho Mungu, binadamu katu hawezi pangua?. Usiangaike kujibu, ni kweli kabisa Mwandishi, Mungu alipanga na ikatokea.

Ilikuwa siku ya jumapili ya mwaka 2000 Jioni ya saa kumi na mbili kasoro, Nilikuwa nyuma ya kochi alilokaa Mama akiwa anaangalia televisheni ya Taifa, ulikuwa muda wa taarifa ya habari. Mimi nilikuwa naendelea kujisomea na kujiandaa na mambo yangu ya kishule kwani ndio ulikuwa mwaka wangu wa mwisho kumaliza elimu yangu ya msingi.

Lakini ghafla nilisikia kishindo cha ghafla nyuma yangu kama kitu kizito kimeanguka. Haraka nikakimbilia eneo ambalo kishindo kimesikika. Nilimwona Mama yangu mzazi akiwa chini, nilipigwa na bumbuwazi la maana kwa kushitushwa na hali hiyo. Nilianza kumwita kwa kumwamsha nikitumia sauti kubwa huku mikono yangu ikikazana kumtikisa nimwamshe. Katika kuangaza angaza nilikumbana na mwisho wa taarifa ya habari kutoka runingani. Nikatulia tuli kuimalizia..

“...Afisa wa polisi mkoa wa Morogoro amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo mnamo majira ya saa kumi na mbili jioni. Afisa ametoa angalizo kwa madereva ya magari binafsi kufuata taratibu na sheria za barabarani kuepusha ajali kama hizo. Roho ya marehemu Mzee Yohana Ephrehem ilazwe mahali pema peponi… Amina” Mwisho wa habari hiyo iliandamana na baadhi ya picha za gari lililochakaa kwa kujimega upande mmoja wa mbele, wahudumu wa kwanza wakifunika maiti na kupakia katika mifuko maalum ya kuhifadhia, kisha kuweka katika gari tayari kwa kuutoa mahali pale..

Picha ambazo zilionekana runingani ni picha ya ajali ya gari. Gari la Baba! Nilishituka na mikono yote kujikuta ipo juu ya kichwa changu kwa sekunde tu.. nikaja kujuwa kuwa Mama amepoteza fahamu kutokana na mshituko wa taarifa hiyo.

Nikapiga ukunga wa maana uliomwamsha hadi mdogo wangu usingizini, tuliungana kujitahidi kumwamsha Mama lakini mdogo wangu hakujua sababu na chanzo cha mama kupoteza fahamu. Sikuweza kumwambia. Mikono na sauti vilikazana kumwamsha Mama; ila akili ilikuwa mkoa wa morogoro kwenye maiti ya Baba. Tulishaachwa na kiongozi wa familia tayari.

Hakuna jilani yeyote aliyesikia kilio chetu. Hata kama wangesikia ni dhairi kuwa hakuna hata mmoja ambaye angethubutu kukanyaga kwetu. Hatukuwa na ushirikiano mzuri na majirani wenzetu, kwani tulijua pesa ndio kila kitu.

Tulilalama mimi na mdogo wangu hadi mashangazi wa karibu walipofika mkuku baada ya kupata habari kupitia televisheni zao makwao. Walitutoa pale na kutupeleka chumbani na wao wakaendelea na taratibu za kumpa Mama huduma ya kwanza. Kutokana na kushindwa vumilia hali nilikuwanayo nilianza kugombana na mtu ambaye tulikabidhiwa chumbani humo ili awe mwangalifu kwetu, nilikuwa mbishi kwa kutaka kumwona Mama yangu yu katika hali salama.

Ubishi wangu ulipelekea kumshinda nguvu mwanamama yule wa rika, nilimtoka mikononi mwake na kupitiliza moja kwa moja katika mlango wa kutokea chumbani humo. Sikufika mbali hata, nilipiga mweleka wa nguvu katika marumaru ambazo kila siku tulimsifia fundi kuwa katumia kipaji chake kwa kuzinakshi vyema.

Siku hiyo zilinisaliti, nilianguka kama jiwe na kupoteza fahamu hapohapo…” Ndugu Mwandishi. Nakupa onyo! Katu usilingie mali! Mali si kitu kwa kweli, ona sasa. Hadi marumaru nilizozizoea kuchezea na kukimbia nazo kila siku niendapo shule zimenisaliti kwa kunizimisha kabisa. Nilizimia mimi mwandishi…

ITAENDELEA…

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (07)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: Xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994

Ubishi wangu ulipelekea kumshinda nguvu mwanamama yule wa rika, nilimtoka mikononi mwake na kupitiliza moja kwa moja katika mlango wa kutokea chumbani humo. Sikufika mbali hata, nilipiga mweleka wa nguvu katika marumaru ambazo kila siku tulimsifia fundi kuwa katumia kipaji chake kwa kuzinakshi vyema.

Siku hiyo zilinisaliti, nilianguka kama jiwe na kupoteza fahamu hapohapo…” Ndugu Mwandishi. Nakupa onyo! Katu usilingie mali! Mali si kitu kwa kweli, ona sasa. Hadi marumaru nilizozizoea kuchezea na kukimbia nazo kila siku niendapo shule zimenisaliti kwa kunizimisha kabisa. Nilizimia mimi mwandishi…

ENDELEA SEHEMU YA SABA…

Hazina hata chembe ya huruma marumaru, zinajua kabisa nimefiwa, tena msiba mkubwa; haya ona naenda kumwona Mama yangu nazo zinanikataza, tena zinanizuia kwa kuniumiza. Mwandishi hadi Marumaru?. Lo! Kweli ‘Mbio za sakafuni huishia ukingoni’. Abdul akaongea kwa machungu na masikitiko makubwa kisha kuendelea.

“Nilipokuja kuzinduka, ilikuwa ni siku ya mazishi, Msiba haukuwa na watu niliowazoea, majirani walikuwa wachache wenye roho ya kusamehe. Rangi nyeusi ilitapakaa kuzishinda rangi nyingine. Wanaume wakiwaka kwa suti kutoka bara la jirani, huku tai zikiwa kama kikorombwezo cha kupima kasi na uelekeo wa upepo. Zilikuwa zinapeperuka tu. Macho yangu yalikutana na Mama ambaye alionekana amevimba macho huku bado akizidi kuendeleza kilio cha polepole bila machozi kuonekana. Sikuwa na uelewa wowote ule kuhusu msiba wala mazishi. Niliungana tu na mama kulia hadi tulipoelekea makaburini na kupumzisha mwili wa Baba yangu mzazi. Baada ya mazishi, watu wote wakapotea na kutuacha tukiwa mimi, Mama na mdogo wangu Maria. Hatukuwa na ndugu wa karibu.

Tulianza maisha mapya ya uyatima wa upande mmoja, Baba alikua ndiye kichwa na mshughulikaji wa familia, kupotea kwake kulisababisha mambo mengi sana kukwama. Mama alikuwa ni mwingi wa mawazo kwa kuwaza mustakabali wa kikao cha familia kitakacho fanyika siku ya ishirini na tisa baada ya mazishi. Tarehe maalum kabisa iliyopangwa na ndugu wa marehemu. Lengo ni kujadili masuala mbalimbali ya familia.

“Mwanangu, we ndio mkubwa hapa, we ndio Baba!, mtunze mdogo wako Baba eh! Sawa!” Mama aliongea kwa upole sana akionesha wasiwasi machoni kwake. Nilitumia kila fursa kumrudisha katika hali yake ya kawaida hadi tukaweza, nafasi kubwa na mpango huo aliufanikisha mdogo wangu Maria.
---
Maria alikuwa ni mchekeshaji mkubwa sana sijawai kuona, kama hutacheka basi lazima ufurahi. Licha rangi nzuri ya kuvutia kwake, Maria alikuwa kiboko ya wanaume wanaopenda mambo ya kuchipukia, kifuani kwake alibeba mzigo mwepesi uliotuna kwa ugumu wake kama makande ya wanafunzi katika shule za serikali. Hali hiyo ilifanya kila nguo nyepesi aliyovaa kutanuka kidogo hadi kutaka kutoboka kwa jinsi chuchu zake zilivyochongeka, hilo lilionekana kwa macho tu, alikuwa mzuri dada yangu sijui ni sababu ya pesa au ni malezi tu, au ndio kazi ya Mungu kama wasemavyo Manabii na Mitume!.
----
Basi siku ya hitimisho la mazishi lilifika, ilikuwa siku ya kikao cha familia. Kwanza likapigwa sebene la kufa mtu. Watu walikula nyama za aina tatu tofauti, ukianza na Ng’ombe mkubwa basi unamaliza na Mbuzi au supu ya kuku. Ni taratibu za familia na koo hiyo. Hakuna aliyethubutu kupinga kati yetu.

Mama hakupendezwa na mambo hayo lakini hana usemi wowote mbele ya wakubwa. Kitu cha kushangaza zaidi ni kutokumwona ndugu yoyote yule wa upande wa Mama, walijaa wote wa upande wa Baba na wengi nilikuwa siwafahamu, ila kuna sura ya Baba mdogo ambayo niliizoea sana kuliko ndugu wote pale.

Kikubwa ni kuwa hakukuwa na ushirikiano mzuri kati ya familia yetu na ndugu wa pande wengine, walikuwa kama wametutenga hivi. Baba mdogo tu ndiye niliyemfahamu haswa, yeye alikuwa akiletwa na Baba mara nyingi nyumbani. Ndiyo walikuwa karibu kuliko wengine. Hivyo nikapata sana kumkumbuka yeye.
Nakumbuka pesa nyingi niliziona kwa macho yangu kutoka kwa Baba na zikimiminika kwa kumpa mtaji Baba mdogo, na alikuwa anakuja mara moja baada ya miezi kama mitatu hivi. Mtu na mdogo wake walishibana kwelikweli.

Walipohakikisha kila mhusika wao amehudhuria kwenye kikao kile, Mzee mmoja mwenye mvi alinyanyuka na kutoa utambulisho.
“….. Binti, kiko wapi mlichokuwa mnajivunia?, mkakimbia wazazi kwa kutaka laana, mkafunga ndoa wawili tu wenyewe. Ndoa ya shetani wewe na baladhuri wako!, hukujua kuna siku mtatengana?. Vione na vitoto mlivyozaa… jamani!! mtoto wetu katutia aibu sana. Mwanamke tuliyemtafutia sisi ndio alikuwa bora mno. Yule alikuwa mcheshi, mkarimu!, eh!, mwanamke anashepu jamani sa yeye kaenda kwa dangulo na pesa zake kuokota huyu Malaya. Lo!..” Mzee aliyesimama alianza kuongea bila shida baada ya kutambulisha ndugu zake wote. Nilishangaa mno kwa matusi mazito kama yale kutua kifuani kwa Mama yangu. Kama nilivyohisi, nilimwona Mama anaanza kunyanyuka kwa nguvu na kuanza kuingilia kati suala hilo lakini kabla hajafanya lolote sauti nzito nyingine ilisikika.

“Kaa chini Alaah! Huna adabu?”, ilikuwa ni sauti ya Mzee mwingine ambaye alitambulishwa mwanzoni kuwa ni babu yangu. Yaani baba yake baba.

“Yale yalee… tulisema sisi, Mtoto… wakubwa wanaongea afu….. Mwee!”, Mwingine akachangia mada kuendeleza wimbi la ushindi, huyu alikuwa ni wa kike. Kama kikao hicho kilikuwa ni mchezo wa mpira wa miguu, basi mpaka sasa tulishwa fungwa goli tatu kwa sifuri katika uwanja wetu wa nyumbani.

“Hahahaha, sasa wakubwa!, hakuna namna hapo, msameheni tu. Hajui mila na taratibu tu za koo yetu, si kashaolewa!!, hakuna haja..” Baba mdogo nae alionesha dhahiri kuwa hakuwa upande wetu. Licha ya misaada yote ile lakini bado alitukana, Roho iliniuma sana kwakweli. Bado Mama hasira hazikumshuka. Alitaka usawa.

“Taratibu ni zilezile zinajulikana, sema tukumbushane tu,…” aliongea mzee yuleyule wa mwanzao, akafungua makatasi na kuendelea.

“..aah!! marehemu ameacha mali nyingi sana. Ambazo zooooote zitakuwa chini ya usimamizi wa Mdogo wake. Namaanisha zooote. hahaahaha” yule Mzee aliendelea kuzungumza.

Mama akaonekana kutaka kutoa neno lakini kigugumizi kilimshika na bado hali yake haikuwa nzuri sana kutokana na majanga ambayo ameshindwa kuyahimili. Bado kidonda cha kifo cha mume wake kilikuwa kibichi kabisa, sasa hawa nao wanamtia pilipili kwa kutaka apone mapema, jamani binadamu hawana huruma asee. Tayari waligusia urithi wa Mali.

“Na kwa taratibu za mila na tamaduni zetu pia, Bwana Furedi utarithi mke na mali nyingine zilizopo!.” Akaendelea.

“What????!” Mama aling’aka na kuinuka kwa nguvu huku mikono ikisaidia kuifunga vyema kanga yake na kufanya mdomo kuongea bila ruhusa. Tayari alisharuhusu hasira zake kuonekana hadharani, katu sikuwahi kumwona Mama katika hali kama hii. Mama alipatwa na hasira za ajabu.

“Kurithi Mke! Nani? Mbwa huyu! Huyuuuu!....., Aahg! za wapi hizi jamni. kwanini mnapenda kushindilia matuta ambayo yanamalengo ya kuzalisha miche mingi?, Nini nimekosa eh baba!” Mama aliongea kwa nguvu sana na baadae kupunguza sauti kwani kilio kilichukua nafasi. Alianza kulia Mama yangu.

“Mwanangu!, Ukipenda boga penda na ua lake!” Babu nae alishindilia nyundo ya maumivu kwa makini bila kupepesa macho…

ITAENDELEA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (08)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: Xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994

“What????!” Mama aling’aka na kuinuka kwa nguvu huku mikono ikisaidia kuifunga vyema kanga yake na kufanya mdomo kuongea bila ruhusa. Tayari alisharuhusu hasira zake kuonekana hadharani, katu sikuwahi kumwona Mama katika hali kama hii. Mama alipatwa na hasira za ajabu.

“Kurithi Mke! Nani? Mbwa huyu! Huyuuuu!....., Aahg! za wapi hizi jamni. kwanini mnapenda kushindilia matuta ambayo yanamalengo ya kuzalisha miche mingi?, Nini nimekosa eh baba!” Mama aliongea kwa nguvu sana na baadae kupunguza sauti kwani kilio kilichukua nafasi. Alianza kulia Mama yangu.

“Mwanangu!, Ukipenda boga penda na ua lake!” Babu nae alishindilia nyundo ya maumivu kwa makini bila kupepesa macho…

ENDELEA SEHEMU YA NANE…

“Hiyo ni lazima, hutaki toka na hizo takataka zako mbili peleka kwenu uko wapi sijui!” Yule Mzee wa Kwanza kutufungulia kikao alikuwa mkali kwelikweli; kama pilipili kichaa. Nilipojaribu kuingilia nikavamiwa na familia nzima kwa kukosa adabu. Nikatulia tulii… Maamuzi yakapita wakashinda wao japo walitumia uwanja wa ugenini, idadi ya magoli tuliyofungwa ilitosha kabisha kufungiwa na shilikisho ya Maisha Duniani (SMD). Kwa kuwa wao ndio wenye nguvu, wakashinda.

Baada ya kutuzidi nguvu na kiongozi wa upande wetu alikuwa wa kike, tukasalimu amri!. wakatuacha nyumbani hapo na wote wakatawanyika. Ndugu wote walikuwa wanaishi mbali na sisi, wengine walivuka hadi mkoa. kwa taarifa za awali kuwa Mama na Baba waliishi mbali na familia yao kwa kuwa Baba alikanwa na wazazi wake kwa kumuoa Mama yangu. Wazazi wake hao walitaka aoe mtu wa tamaduni na kabila lao ambao wao walimteua.

Tukawa na kazi nyingine ya kumbembeleza Mama huku wote tukiendelea kuumia kwa vitendo hivo, si mimi wala Maria wote tulikuwa katika umri sahihi wa kujua lipi baya na lipi jema. Maisha ya wasiwasi yalianza, tuliishi hapohapo kwani hatukuwa na pa kwenda.

Kwa maelezo ya Mama alituambia kwamba yeye hana Mama wala Baba, wote walifariki wakati wa utoto wake. Tukabaki katika jumba kubwa ambalo kwa sasa lilikuwa kama Jumba la Vilio Tanzania, kila kukicha ni kudeki machozi tu. Tuliumia mno kwa hatua waliyofikiana wanandugu.

Siku ya tatu baada ya kikao alikuja Baba mdogo Frank, eti alikuja kumwona mke wake na kumwambia siku rasmi ya yeye kuja kuishi nae. Tulimwacha ajimwage na maneno yake ya kebehi na kisha kuondoka. Alikuwa amesahau kabisa misaada yote aliyoipata toka kwa baba yangu. Kweli Dunia hadaa! Namchukia Baba Mdogo.

Basi ndugu mwandishi japo kwa shida lakini maisha yaliendelea kama kawaida, shule ilikuwa inasonga vilevile tu kama kawaida kwani ndio ulikuwa mwaka wangu wa mwisho kuhitimu darasa la saba. Kitu kizuri ni kwamba baba alishalipa ada na michango yote ya shule. Siku zilizidi kwenda tu.
----

Ndugu Mwandishi, Baba mdogo aliamua kabisa kukata kuja nyumbani, ulipita zaidi ya mwezi mmoja sikuona pua yake mlangoni kwetu. Ndani ya mwezi huo mmoja tabasamu la mama likarudi tena kama awali, alianza kuzoea kabisa hali ya maisha iliyopo. Mambo yote yalienda vizuri japo si kama kipindi Baba yangu mzazi yupo.

Katika biashara hakuna aliyeleta chochote wala kuelezea habari ya biashara alizokuwa anafanya Baba, labda zilikuwa chini ya mamlaka ya Baba Mdogo Frank. Na wala hatukuthubutu kuulizia mambo hayo. Tukabaki na amani yetu changa.
----

“Hahahaha we maria wewe! Sidhani kama shule ipo hapa. We umekaa maksihara maksihara tu!... umesema unataka kuwa nani? Hahahahaha!!” Kilikuwa ni kicheko cha Mama cha mwisho cha kumalizia mwezi wa furaha. Baada ya hapo akanyanyuka na kwenda kufungua mlango kuna mtu alibisha hodi. Akatoka nje kufungua na kurudi ndani na bahasha. Alishika bahasha mkononi Mama.

“Nataka kuwa boooonge la Mchekeshaji huhuhuhu!!, kuna siku mtanishuhudia nipo kwenye masteji makubwa huko… ah kama najiona hivi, Cheka tu stage, Churchill Show stage,.. up to Amerikaaaa oyoooo” Jibu la mdogo wangu lilinikata mbavu kwa kweli, tulicheka sana jamani,

Maria alikuwa vizuri katika kuchekesha lakini kwa jitihada za masomo hapana, hakuwa na ushirikiano na kitu kinachoitwa Shule. Mbali na mdogo wangu na mimi nilikuwa na ndoto ya kuja kuwa mwandishi mhariri au mtangazaji mmoja mkubwa wa Tanzania na kufahamika dunia nzima kwa ujumla.

Mama alicheka lakini hakuonyesha hata jino lake moja, ‘Macho yalikuwa bize kufungua barua’ aliyeipokea punde. Alisoma taratibu hadi kuifikia katikati barua hiyo, tukamwona anasimama na kuelekea chumbani kwake, tulikaa hapo barazani tukiendelea tu kubishana kuhusu ndoto zetu za baadae. Hakuna aliyehisi hali tofauti ya Mama.

Hadi baadae Mama akarudi na kukaa tena karibu yetu, hakuwa tena na furaha kama mwanzo, swali la kulikoni lilimwangukia miguuni mwake lakini hakujibu zaidi ya kuendelea kupandisha kamasi zake kama zimelegea na kutaka kutoka bila ruhusa. Nilijua kabisa hakuna jema linaloendelea, hata macho yake yalionesha uvumbe wa machozi. Alikuwa ametoka kulia sana mda sio mrefu.

“Denis… Maria!...” Alituita kwa majina yetu halisi. Akasita kabla ya kuendelea

“Wanangu hamna chenu hapa!!” alianza kuongea kauli tusiyo elewa inamaana gani kwa upole huku akizichezea nywele za Maria, kisha akaendelea.

“Hata kama nisipokuwepo mbeleni, hakikisha mnasoma! Msikubali kuwa na rafiki mjinga hata siku moja. Bora muongozane na Shule atawapa zawadi ya elimu, vipi kwa mjinga?. Denisi wewe ni mkubwa eh!. Maria kama unavyomwona, usimwache mdogo wako..” Mama alimaliza na kutotaka mazungumzo tena, alitoka nje kabisa ya nyumba, tulimchungulia tu dirishani anavyo kata mbuga kufungua geti.
Tukabaki na mawazo mengi sana ambayo mengi yalikuwa ni maswali tu. Tupo mimi namdogo wangu, maswali yetu yalikuwa mapacha kwani yanafanana kwa asilimia zote, nani atatoa majibu?. Tukabaki na huzuni zetu hadi jioni ilipotia timu na uzuri Mama alirejea nyumbani.
Kila tulilomuuliza alitabasamu na kujibu “Hakuna tatizo mwanangu”. Hatukupata ufafanuzi wa kile kilichombadilisha kwa nyakati zile…..

ITAENDELEA….

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (09)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994

Tukabaki na mawazo mengi sana ambayo mengi yalikuwa ni maswali tu. Tupo mimi namdogo wangu, maswali yetu yalikuwa mapacha kwani yanafanana kwa asilimia zote, nani atatoa majibu?. Tukabaki na huzuni zetu hadi jioni ilipotia timu na uzuri Mama alirejea nyumbani.
Kila tulilomuuliza alitabasamu na kujibu “Hakuna tatizo mwanangu”. Hatukupata ufafanuzi wa kile kilichombadilisha kwa nyakati zile…..

ENDELEA SEHEMU YA TISA….

Miezi ilizidi kukatika, na shida zikawa zinaendelea kugonga mlango. Mama alikuwa ni mtu wa kumwaga machozi kila baada ya siku mbili, hatukuwa na uhakika na kilichomliza lakini machozi hayo yalisababishwa na barua anazopokea kila siku. Sikujua ni nani ambaye anatibua furaha yetu siku zote.

Kuna siku nilikuwa chumbani kama kawaida. Mlango ukagonga na mtu wa kuleta barua alikuwa mlangoni kama anavyofanya kila siku, akakabidhi barua kwa Mama na kuondoka zake.

Nikamwona Mama akiketi katika kochi na kuanza kuifungua barua hiyo. Alisoma taratibu hadi kuifikia mwisho, akanyanyua fito ya ukingo wa kanga yake, akapikicha macho kidogo kisha akaweka sawa nguo yake. Akanyanyuka na kuichana barua hiyo kisha vipande vya karatasi hiyo akaongozana navyo hadi chumbani kwake

Kipindi hicho bado nilikuwa nikimchungulia mlangoni kwangu, alichukua mda kutoka ndani, alipotoka alikuwa ameshavaa nguo nzuri. Nguo ambazo anapenda sana kuvaa anapoenda kanisani. Akaniita na kuniaga kuwa anatoka. Suala la anakoenda hakuligusia kabisa, nikamwacha aondoke namimi kama ilivyo ada nikamsindikiza hadi nje kwa macho hadi anapotea.

Magari yalikuwepo ndugu Mtangazaji lakini nani anaendesha?. Labda mimi ningekuwa mkubwa ningemsaidia kumpeleka mwanamke yule aendako. Baada ya kuhakikisha kuwa ameshaenda mbali kidogo nikaelekea chumbani kwa Mama kukagua kama nitakutana na vipande vya barua ile iliyomfikia mda mfupi.

Kwa kuwa Mama hakuwa na tamaduni ya kufunga mlango wake labda tuwe tumetoka wote, hivyo ikawa urahisi wa kufanya uchunguzi wangu. Ndugu mwandishi hawa watu wanofanya shughuli za upelelezi we wasikie tu. Wanakutana na makubwa sana katika kazi zao. Kazi hiyo lazima uwe mkubwa kwa umri na umbo, maana kila unachofanyia upepelezi ni siri ya mtu. Najuta kujiingiza kwenye taaluma hii feki ya upelelezi ambayo haikuwa chaguo langu.

Sasa nilipofungua tu mlango nikakutana na ndoo maalum la kuwekea makaratasi na mabaki ya nywele anapochana pamoja na uchafu mwingine mwepesi. Juu kabisa nikakutana na siri niliyoitaka!, Ni siri nzito maana ilichanwa na kufinyangwa finyangwa kama ule udongo ambao Mungu alitumia kutengenezea binadamu kama Samson wa derila. Nilichukua makaratisi hayo na kuiunganisha ipasavyo.

Mwandiko ulikuwa mbovu kabisa, tena maandishi yote yalikuwa kwa herufi kubwa tu. Inaonekana mwandishi wa barua hiyo nilimpita darasa. Basi nikaungaunga na kupata muunganiko na maana ya barua hiyo nzito. Ilisomeka vizuri sana japo kwa shida:

“MUKE WANGU MAMA DENISI KIPENDO CHANGU MAMA MARIYA
MUME WAKO NAKARIBIYA KUKUJA HIVYO KARIBUNI TU, KAMA NDIVYOSEMAGA KWENYE ILE BARUWA YANGU ILE YA MWAZO. NDO NAKUJA SASA KUONYA JAPO TAMU YA KAKA YANGU MALEEMU
MIMI NIYO MUME WAKO SASA NAKUJAGA SA KULISI MALI YANGU. ILA NIKIJA MIMI NATAKA TU PEZI LAKO NA MALI BASII. BADA YA HAPO UTAPOTELEA MBALI SITAKI KITU MIMI KIGINE ZAIDI YA MALI TU.
NI MIMIMI MUME WAKO FUREDI”

Mwisho wa barua hiyo ni mwanzo mwingine wa chozi la mtoto anayejuwa maana ya mapenzi na thamani ya mali. Machozi yalinitoka sana na kufanya karatasi ilo kuanza kulowa. Barua ilibeba maneno mazito mno kushindwa kuyabeba mtoto kama mimi. Jamni kuna watu wanakera duniani.

Nilikumbuka kuwa sipo katika chumba changu, nikafinyanga tena lile karatasi na kutupa mule mule nilipochukua. Nikaenda chumbani nikiwa na fungu la kisasi moyoni. Nilimchukia Baba Mdogo kwa kweli na koo nzima ya Baba. Nilimlaani na kuhakikisha iko siku itafika, ataingia katika kumi na nane zangu.
----

Naam hatimaye Mama akarejea jioni yake. Hakuna halilosema. Alificha kila alilifanya nyuma ya nyumba yake. Udogo wangu ulinifanya nisiweze kujua vitu vingi vya kikubwa. Naamini ndugu mwandishi kuwa angali ningekuwa mkubwa kwa kipindi hicho basi kila baya au zuri la Mama ningelijua au kuambiwa. Nilifichwa kutokana na udogo wangu. Sikuweza kubeba matatizo makubwa makubwa. Siku hiyo ikapita hivyo ndugu mwandishi.

Ndugu mwandishi, ikiwa imebaki wiki moja tu nimalize mtihani wangu wa darasa la saba. Likaja tukio la kushangaza kupita maelezo. Huo ndio ulikuwa mwanzo wa maisha haya mliyo nikuta nayo. Maisha ambayo si chaguo langu kwa kweli. Maisha ambayo nililazimishwa kuishi kutokana na hali halisi. Maisha ya kutanga na njia, bila msaada wala tumaini la uzima. Kila kitu kilienda kombo. Kama wasemavyo wataalam wa lugha kuwa; Uchawi wa mali ni wokovu wa uhai. Na kweli ikaja kutokea

Ilikuwa ni jumapili kamili yenye wingi wa amani ndani yake. Sikuweza kubishana na kijua cha asubuhi katika kuchomoza mbawa zake na kunishinikiza kuwa natakiwa kutoka kitandani. Kwa vile ilikuwa ni wiki ya lala salama katika kuelekea kipindi cha mwisho cha kufanya mtihani wangu wa mwisho, basi sikuwa na hiyana katika kujisogeza na sehemu tulivu ya kujisomea.

Nilichukua vifaa vyangu na kutoka nje. Nilikutana na uso wa bashasha wa Mama akiendelea kupapalika katika kuosha na kusuuza vyombo vilivyotumika jana yake. Kama yalivyo mapenzi ya mtoto kwa Mama, nikaweka daftari chini kwanza kwa kumsaidia kusuuza vyombo hivyo.

“Mwanangu…! Maisha siyo ya kuvaliwa kikoi!, utaumbuka”. Mama alitoa neno la mwisho ambalo halikuingia sawasawa akilini, kwani sikujua maana yake hata kidogo, lilishia tu katika ubongo wa mwanzoni na kutoweka, kwani nilishamzoea Mama kunipachika misemo mipya na ya ajabu kila kuchwao. Nitafanya nini zaidi ya kutabasamu. Nilitabasamu tu ili ajue nipo pamoja na yeye.
Kilichofuata ni kupakua daftari langu na kuelekea sebuleni, tena nililala sakafuni kwa kuanza kulipitia. Nakumbuka lilikuwa ni somo la Kiingeleza. Somo ambalo nililipenda kuliko yote. Hata ukiesabu idadi ya vitabu, vingi vilikuwa ni vya lugha ya kiingeleza. Hii ilitokana na hamasa kutoka Marehemu baba yangu katika kupigania ndoto yangu.

“Dogo!, lugha ni sanaa ya habari!” hiyo ndio kauli kutoka kwa baba ambayo niliishi sana katika maisha yangu ya kuendeleza ndoto zangu. Basi niliendelea kusoma taratibu somo langu pendwa.

“Krinlii! Krinliii, Krinliiiiii..” Alamu kutoka katika geti kubwa ilisikika, ilisumbua ngoma za masikio yangu lakini katu sikusogea kwenda kufungua. Nikajitwika kiburi cha kusoma nifahuru mtihani wangu. Nilijikausha kama sisikii chochote hadi pale Mama alipoitika wito kwa kwenda kufungua mlango.

Ndugu mwandishi, siwezi sema kuwa nilikuwa na kiburi cha kushindwa kufungua mlango. Hapana!. Ila ni mazoea tu. Mazoea!. Kwani tumelelewa mazingira ya uwepesi sana hadi kutofanya hata baadhi ya kazi rahisi kama hii ya kufungua mlango. Tulikuwa tunadeka sana. Mama ni mwelewa sana na tabia yetu. Kwahiyo hata kufungua mlango lilikuwa ni jukumu lake. Mwandishi mimi najuta kuzaliwa familia ya pesa kama hii. Imenilea katika misingi ya ajabu sana. Najuta.

Naam aliye bisha hodi akaingia ndani baada ya kufunguliwa. Alikuwa ni yule yule aliyepotea kwa zaidi ya mwezi na ushee. Mtu ambaye alichukiwa na maisha yangu. Mtu ambaye hakuthubutu katu kupenyeza sauti yake ya wema kwa Mama yangu. Alimuumiza haswa, sio kila siku tu bali ni kila mda. Mtu ambaye alimtumia Mama yangu barua zisizokuwa na Kichwa wala miguu.

Aliingia hadi ndani na kusimama karibu na mlango. Kwa jinsi alivyokuwa mweusi ashukuru Mungu siku hiyo alikuwa upande wake kwani aling’azwa na mwanga wa jua la asubuhi, na kuonekana kwaumbali japo meno tu. Alikuwa anatisha. Hakika nilimchukia mtu huyu. Ninamchukia mtu huyu na nitamchikia mtu huyu. Yeye na kaburi lake wote nitawachukia….

ITAENDELEA…

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (10)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994

Naam aliye bisha hodi akaingia ndani baada ya kufunguliwa. Alikuwa ni yule yule aliyepotea kwa zaidi ya mwezi na ushee. Mtu ambaye alichukiwa na maisha yangu. Mtu ambaye hakuthubutu katu kupenyeza sauti yake ya wema kwa Mama yangu. Alimuumiza haswa, sio kila siku tu bali ni kila mda. Mtu ambaye alimtumia Mama yangu barua zisizokuwa na Kichwa wala miguu.

Aliingia hadi ndani na kusimama karibu na mlango. Kwa jinsi alivyokuwa mweusi ashukuru Mungu siku hiyo alikuwa upande wake kwani aling’azwa na mwanga wa jua la asubuhi, na kuonekana kwaumbali japo meno tu. Alikuwa anatisha. Hakika nilimchukia mtu huyu. Ninamchukia mtu huyu na nitamchikia mtu huyu. Yeye na kaburi lake wote nitawachukia….

ENDELEA SEHEMU YA KUMI…

Aliganda tu mlangoni huku mikono yake ikishika vyema kiuno chake utazani wale wa Mama Wazaramo wanapopata habari ya kusutwa kwa mdai wao. Mimi niliacha kusoma na kukaa kitako, nikaruhusu jicho langu kumkagua kuanzia chini hadi juu. Hata mpangilio wake wa mavazi ulisadifu tu alikuja kwa shari.

Shati lake la maua maua utazani mfakazi wa bustani ya motoni, lilimsimama haswa na mikunjo yake, koti la suti lilifunika sehemu ya nyuma tu ya mwili wake mbele likiwa wazi. Staili hiyo ya kutoka kijijini kwao ushambani ilisindikizwa na kiatu kikubwa cheusi.

Kichwa changu kikakosa jina la kukiita kiatu hicho ila kinafanana kabisa na yale mabuti ambayo wanavaa wataalam wa kuchunga ngo’ombe kwenye nyasi kubwa ili kuzuia unyevu na wadudu wasumbufu kuathiri miguu yao. Mavazi yake yalikuwa ni ya kuchekesha sana lakini nani atapanua mdomo kucheka wakati sura yake na uwepo wake ulikuwa wa shari?.

Labda mdogo wangu ambaye alikuwa amelala angelikuwepo basi angeongoza vumbi la kucheka bila kujali hali na mahali alipo. Maana mdogo wangu na akili zake, wanajuana wenyewe..

Baba Mdogo alicheka kidogo akiwa palepale mlangoni na mwisho kuishia na kutabasamu, akatoa mikono yake kiunoni na mmoja kuingiza katika mfuko wa koti lake la suti. Akatoa sigara na kuiweka mdomoni. Akaingiza tena mkono mfukoni na kupapasa kama atatoka na kiberiti, lakini hora!. Akatoa na kuingiza mfuko mwingine lakini hakukua na kiberiti. Kukosa kwa kiberiti kukaibua taswira nyingine ya taharuki.

“Naam! Awali nilikuambia mke wangu ni njiani kuja…” aliongea kwa kejeri na hakuna aliyeangaika kumjibu. Mama alibaki amekunja tu mikono akiegema karibu na kabati la vyombo sebureni hapo.

“Ah! Kuchelewa kwangu ni sababu ileile tu. Hakuna nyingine..” Aliendelea kubwabwaja huku akisogea kwa hatua tatu na kisha kusimama tena. Bado mikono yake ikiwa katika mfuko wa koti na kipande cha sigara kikiwa mdomoni bila kuwaka.

“Nazani barua zangu zote ulizipata kwa hakika. Nilikujuza kila kitu mke wangu. Ilo moja, pili ni kwamba mimi najua kabisa siwezi ishi na wewe kwa amani!, naam kweli siwezi ishi kabisaa, hahahahah!” akacheka na kuendelea kutafuta kibiriti chake, na sasa aliamia katika suruali yake.

Kwa bahati alikuta alichokitafuta. Akapata kiberiti. Akawasha sigara yake ambayo ilisimama mdomoni kwa muda wote wa maongezi yake. Akaivuta kwa kasi sana na kutolea moshi puani, alirudia tena na tena mtindo huo. Alipofika fundo la sita akaizima sigara yake na kuiweka katika mfuko wa koti pamoja na kibiriti chake. Akahema kwa bashasha kama mtu ambaye hana wasiwasi kabisa na kuendelea.

“Najua tu!, ah we kwani nani aishi na wewe?. Utanitia kiwingu sana na hivi vitoto vyako. Mambo yangu yatakwama” Aliongea kwa ishara huku mkono wake ukionyesha ishara ya kuelekeza kwangu. Kipindi hicho mdogo wangu Maria aliamka na kutoka chumbani alipokuwa amelala na kuja sebureni tulipo. Baba yule asiye na haya alimwangalia tu na kutabasamu. Akamuunganisha katika tukio lile.

“Oh Mamaa, nawe umekuwa kabisa yani!. Mulemule! Uwiiii!... ani subirini niwaambie kitu jamani. Sikutaka nifanye haya mapema sababu nampenda sana kaka yangu, hivyo niliacha kwanza msiba uishe afu pia na.. na.. kingine ni wewe mke wangu ulikonda sana wakati wa msiba wa kaka yangu. Sasa mimi sikutaka upotee mapema bila hata kukuonja kidogo jamani mama watoto. Sasa nikawa nasema nakulaje mzigo mtu umekonda vile? Basi nikaingiwa na huruma ya kukuacha ujazieee ujazieee weee! Kama hivi yani mtoto unalipa sasa Lo!” Aliongea maneno ambayo hata mimi mtoto niliona aibu kusikiliza. Mama akaona wanakoelekea ni kutiana aibu sasa, amevuka mipaka. Akaingia kati.

“Frank!!!!” Mama aliita kwa sauti kubwa huku jicho likiwa tayari limemuiva kama moto wa tanuli.

“Oh! Jamanii niite Mumee!” Yaaniii baba mdogo alikuwa ni mtu wa kukera sana. Anakera anakera anakera!. Alikuwa ni kichefuchefu kwa mtu ambaye hana vipimo vya mimba.

Mdogo wangu alinikimbilia nilipo, tuliinuka wote pale chini na kupanda kukaa kwenye kochi. Mama alishaonyesha hasira za wazi kabisa kwa kutovumilia vitendo vinavyoendelea bila aibu katika nyumba yake. Yani Baba mdogo aliamua kuja kututukana nyumbani kwetu?.

“Afuu! Sikia we mwanamke. Usinichukulie poa hata kidogo. Huna sauti. kaa kimya!!” Baba mdogo nae akamkata kauli Mama na mzozo wa hisia kuibuka kati yetu. Mdogo wangu mwepesi wa roho tayari alijua tumevamiwa. Chozi lilianza kumtoka, tena chozi zito tu.

“Leo ndio nimekuja, bora hata umeongea hilo neno lako la mwisho. Nina mamlaka ya kukufanya chochote kile. Wewe na wanao mnanitia wingu nimekuambia!!!. Mambo yangu hayaendi kisa nyie.. alaaa mali za kaka hizi nyie nani. Naongoza hiki lakini nakuwa na wasiwasi kutokana na vizio vyenu. Mmekaa nuksi tu. Najua mtakuja kuniaribia mbeleni mishe zangu. Bora nimalize mchezo leo…” Baba mdogo alifuka kwa hasira na kuongea bila nukta.

“Lakinii..”

“Kimyaaa!!!” Mama alitaka kuongea kitu lakini Baba ni Baba tu. Mdogo ni neno la kutungwa. Baba mdogo Alifanikiwa kutawala maongezi. Alikuwa ni mwingi wa hasira. Alikuwa Tembo mtu.

“Leo ndio mwisho wenu. Kwisha wewe, kwisha vitoto vyako” aliendelea kung’aka.

“Ba mgodo si..” nilidakia maongezi kwa kujitetea.

“We!, We, We, We katoto. Kione, kipo kama yai hivi. Unaongea na Baba yako anaongea? Pumbavu. Mbuzi wewe!. Ntaanza na wewe!” aliongea Baba mdogo kwa kupaniki na kuacha sauti yake itwale nyumba nzima. Tulimwona anatoa simu yake na kubonyeza kisha kuweka sikioni.

“Ingieni!” Hiyo ndio kauli ambayo ilisikika ikitoka kuelekea katika simu aliyopiga. Tulipigwa na butwaa haswa la kujiuliza siku hiyo imeaanzaje. Waingie??, wakina nani?, na kwanini?!..

ITAENDELEA….

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (11)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994

“Ba mgodo si..” nilidakia maongezi kwa kujitetea.

“We!, We, We, We katoto. Kione, kipo kama yai hivi. Unaongea na Baba yako anaongea? Pumbavu. Mbuzi wewe!. Ntaanza na wewe!” aliongea Baba mdogo kwa kupaniki na kuacha sauti yake itwale nyumba nzima. Tulimwona anatoa simu yake na kubonyeza kisha kuweka sikioni.

“Ingieni!” Hiyo ndio kauli ambayo ilisikika ikitoka kuelekea katika simu aliyopiga. Tulipigwa na butwaa haswa la kujiuliza siku hiyo imeaanzaje. Waingie??, wakina nani?, na kwanini?!..

ITAENDELEA….

“Sasa sikia, wewe Mama na Vyie vifaranga. Hamna chenu hapa. Leo nawapa tiketi ya kwenda kwenu! Kwenu. Anapotea mmoja baada ya...” akumalizia kusema tayari ndani waliingia vijana wanne. Hakuna aliyejuwa mahali walipotokea.

Wawili walikua ni Mapandikizi ya Baba wale wenye miraba minne wote walivaa mavazi meusi na miwani yao machoni. Wawili waliobaki walikua ni vijana wa kawaida sana ila misuli yao ilishaongea na akili yangu kuwa nao sio watu wa mchezo kabisa. Vilio vikaanza ndani mule, mimi na mdogo wangu tukajikuta mikononi mwa Mama yetu bila kutarajia. Hata kama na yeye anaogopa sasa, yeye ndio mkubwa sisi watoto tukimbilie wapi?. Wote tukasongamana kwake kwa woga.

Wakanong’onezana kitu na wote kukubali na kuitikia kwa kutikisa vichwa. Wawili waliamuliwa kututoa sisi kwa Mama. Alikuwa yule mbavu na mwingine ni mwembamba wa kimo. Alitusogelea kwa nguvu na kututoa mikononi mwa Mama ambaye tayari alilowa kwa machozi huku akipata shida kufunga kanga yake iliyotaka kudondoka kila saa. Alishuka chini taratibu na kupiga magoti pale alipo. Kilio cha kuomba msamaha kikasikika. Alikuja kugundua kweli Baba Mdogo alidhamilia kufanya unyama siku hiyo.

“BaB..!, BaaB Nsamehee.. nsamehe mimi eh na watoto wangu!, turuhusu tuondoke tu… te.. te.. tena bila chochote, Tafadhali..” Mama alitokwa na sauti ya shida akijaribu tena kuomba japo robo ya msamaha, hakukuwa na haja ya kuomba msamaha bila kosa. Ila hadi kufikia hatua hiyo tayari hali ya hewa ilibadilika ghafla. Manyunyu yaliyoaanza yalitulowesha wote watatu. Tukawa tunasubili mvua kubwa ya radi inayoandamana na upepo.

Baba mdogo akatokwa na sura yake ngumu na kugeuka kuwa ya kicheko. Alicheka sana kisha kusogea hadi mahali pale alipo piga magoti Mama. Mguu moja akaweka kwenye kochi na kuinama kama anachungulia hivi kufikia kinywa cha Mama.

Akaacha kucheka na kupitisha mkono wake wa kushoto usoni kwa Mama huku akimpapasa kama mtu anayetafuta chunisi usoni kwa mlimbwende wa dunia. alipapasa hadi kufikia kidevuni kwa Mama na kumuinua uso wake wakitazamana. Baba Mdogo alikuwa tayari kusogea kunywa mate ambayo si sahihi kuyapata. Licha ya Mama kufunga mdomo na kujitikisa alishindwa kujichomoa.

“Mwachee.. Mama angu!..” Kidume nikakaza roho yangu dhaifu na kuibadili kuwa roho ngumu ya kwenye picha za sinema. Kauli yangu haikuwa na msaada wowote hule kwa Mama yangu. Kiukweli nilishindwa tu kuchomoka kwa mbavu ile iliyonishika. Alinibana haswa.

Kauli yangu ilimkera sana Baba Mdogo, aliacha anachokifanya na kunisogelea kwa jazba. Bila kukaa sawa na kujiandaa tayari kibao kizito kiliwaka mashavuni mwangu!. Uso niliuona mzito sana, nikahisi nimeongezewa kichwa cha pili ambacho napaswa kukihudimia tena chakula na mafuta ya kukipakaa. Maluweluwe yakawa nyumba yangu kwa muda. Nikajihifadhi humo kwa takribani sekunde kumi na kisha kutoka. Nikatema mate tu sakafuni yaliyochanganyika na damu nikiwa bado nimeshikiliwa mikoni kwa kamanda yule wa miraba minne. Niliziona hadi nyota zile ambazo mamajusi walizifukuzia kuonana na Yesu Kristo!.

“Umeleaje mtoto kama kuku hivi!, hana adabu?” aliongea akimrudia Mama alipo.

“Aaaah uwiiii!!, we unaona upo sahihi!. Mungu atakulipa tu… haaaa jamani!!!” Mama alilalama na kumfanya mdogo wangu naye kuibuka na neno. Angali naye alishikwa lakini hakuacha ubishi wa neno.

“Jamaniiiiii tuacheeee, Mamaaaaa..!” alilia. Alilia hadi nikaona aibu. Mimi ndio mwanaume nyumba ile lakini katu sijafanya chochote kile kulinda nyumba yangu. Vilikuwa ni vilio tu vya kuponea maumivi ya maovu yale.

“Anhaa! Kumbe wote jeuri eh!, wote mmekuwa si ndio. Mnataka kunijazia watu?, eh! Nauliza” Baba Mdogo sasa aliingiza mkono wake kwenye kingo ya suruali yake upande wa kufungia mkanda. Akapenyeza nje ya koti lake lile kubwa na kutoka na Bastora!, wote tukahamaki kwa mshangao. Ndani mule hakuna asiyejua ilikuwa ni nini. Niliziona kabisa kamasi za Mama zikishuka pamoja na machozi zote chini ‘Puuh!’.

Akawaonyesha ishara nyingine ya kichwa vijana wawili waliobaki. Tukaona wakimyanyua Mama na kumpeleka chumbani. Chumba ambacho Mama yangu mzazi alikua anakitumia na Baba yangu mzazi. Baba mdogo alifuata kwa nyuma.

Kwa kuwa chumba hicho kilitazamana na sehemu tulipo tulishudia tu baadhi ya matukio. Baba mdogo aliingia ndani baada ya vijana wawili kumfikisha Mama ndani kwa kumburuta. Baada ya wote watatu kuingia ndani, wale wawili wakatoka nje na kubaki mlangoni. Baba mdogo alikuwa bado ndani. Sisi tukiwa bado sebureni tumeshikiliwa tusilete fujo.

Mpenzi Mwandishi, kipi tusisikie jamani, yote ya ndani yalisikika. Hayakuwa siri katu. Sauti za aina mbili tu zilitoka ndani. Hakukuwa na zile sauti za panya wasumbufu waliokuwa wanaangaika na Mama kila siku, nadhani hata panya hao walikaa pembeni kuangalia unyanyasaji wa aina yake. Sauti hizo mbili zilikuwa ni za Mama yangu na Baba yangu mdogo.

“Ah!, Uh!, Ah!, Uh, Ooh!, Ah!..” hiyo ilikuwa ni mihemo ya Baba yangu kana kwamba kuna kazi kubwa kubwa ya kukata mti wa kuchomea tanuri kwa kutumia shoka alikuwa anafanya. Alikua anatoa sauti ngumu kuzitafakari.

“Haaaaaaaaaaah! Mamaaaaaaa! Mam! Aaih! Oh oh oh Mamaaaaa.. uwiiiiiiii!!” Mama naye hakuwa mbali kujibu mapigo ya sauti kwa kumjibu Baba kikamilifu. Ni dhairi kuwa Baba alikuwa anafanya mapenzi na Mama bila ridhaa. Alikuwa anabaka. Laulah!.

Ilikuwa ni purukushani ya hapa na pale barazani, sikutaka kuachia ukubwa wangu wa familia upotee kizembe, nilingangana hasa kutaka kuchomoka kwa mbavu yule. Sikutaka kuwa mayayi kama anavyosema Baba mdogo. Mungu sio Juma asee.

Nilifanikiwa kutoka mikoni mwa mbavu yule, hatua zangu tatu tu zilinirudisha tena kwa jamaa yule. Alinidaka kabla sijafika mbali na kunipa tena kibano cha nguvu kupita maelezo. Hiki kiliingia kisawasawa kwani nikua naumia viungo kama vyote vya mwili. Mdogo wangu alikuwa Amelia sana hadi kukatika machozi yake alikuwa kama mtu aliyepewa robo tatu lita ya pombe maharufu kama ‘Ngedule’. Alikuwa amelegea mno.

Tulilia hadi kuchoka, hakuna msaada wa aina yeyote ile uliopatikana, ukisikia Mungu yupo likizo ndio siku hiyo. Hata malaika walinzi hawakuwepo kabisa eneo la lindo. Kiufupi tuliteseka sana. Nilimuhurumia sana Mama yangu ambaye bado alikuwa anafanyiwa unyama na Baba yangu mdogo!. Tulizoea kushuhudia katika televisheni tu!...

ITAENDELEA…

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (11)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994

“Ba mgodo si..” nilidakia maongezi kwa kujitetea.

“We!, We, We, We katoto. Kione, kipo kama yai hivi. Unaongea na Baba yako anaongea? Pumbavu. Mbuzi wewe!. Ntaanza na wewe!” aliongea Baba mdogo kwa kupaniki na kuacha sauti yake itwale nyumba nzima. Tulimwona anatoa simu yake na kubonyeza kisha kuweka sikioni.

“Ingieni!” Hiyo ndio kauli ambayo ilisikika ikitoka kuelekea katika simu aliyopiga. Tulipigwa na butwaa haswa la kujiuliza siku hiyo imeaanzaje. Waingie??, wakina nani?, na kwanini?!..

ITAENDELEA….

“Sasa sikia, wewe Mama na Vyie vifaranga. Hamna chenu hapa. Leo nawapa tiketi ya kwenda kwenu! Kwenu. Anapotea mmoja baada ya...” akumalizia kusema tayari ndani waliingia vijana wanne. Hakuna aliyejuwa mahali walipotokea.

Wawili walikua ni Mapandikizi ya Baba wale wenye miraba minne wote walivaa mavazi meusi na miwani yao machoni. Wawili waliobaki walikua ni vijana wa kawaida sana ila misuli yao ilishaongea na akili yangu kuwa nao sio watu wa mchezo kabisa. Vilio vikaanza ndani mule, mimi na mdogo wangu tukajikuta mikononi mwa Mama yetu bila kutarajia. Hata kama na yeye anaogopa sasa, yeye ndio mkubwa sisi watoto tukimbilie wapi?. Wote tukasongamana kwake kwa woga.

Wakanong’onezana kitu na wote kukubali na kuitikia kwa kutikisa vichwa. Wawili waliamuliwa kututoa sisi kwa Mama. Alikuwa yule mbavu na mwingine ni mwembamba wa kimo. Alitusogelea kwa nguvu na kututoa mikononi mwa Mama ambaye tayari alilowa kwa machozi huku akipata shida kufunga kanga yake iliyotaka kudondoka kila saa. Alishuka chini taratibu na kupiga magoti pale alipo. Kilio cha kuomba msamaha kikasikika. Alikuja kugundua kweli Baba Mdogo alidhamilia kufanya unyama siku hiyo.

“BaB..!, BaaB Nsamehee.. nsamehe mimi eh na watoto wangu!, turuhusu tuondoke tu… te.. te.. tena bila chochote, Tafadhali..” Mama alitokwa na sauti ya shida akijaribu tena kuomba japo robo ya msamaha, hakukuwa na haja ya kuomba msamaha bila kosa. Ila hadi kufikia hatua hiyo tayari hali ya hewa ilibadilika ghafla. Manyunyu yaliyoaanza yalitulowesha wote watatu. Tukawa tunasubili mvua kubwa ya radi inayoandamana na upepo.

Baba mdogo akatokwa na sura yake ngumu na kugeuka kuwa ya kicheko. Alicheka sana kisha kusogea hadi mahali pale alipo piga magoti Mama. Mguu moja akaweka kwenye kochi na kuinama kama anachungulia hivi kufikia kinywa cha Mama.

Akaacha kucheka na kupitisha mkono wake wa kushoto usoni kwa Mama huku akimpapasa kama mtu anayetafuta chunisi usoni kwa mlimbwende wa dunia. alipapasa hadi kufikia kidevuni kwa Mama na kumuinua uso wake wakitazamana. Baba Mdogo alikuwa tayari kusogea kunywa mate ambayo si sahihi kuyapata. Licha ya Mama kufunga mdomo na kujitikisa alishindwa kujichomoa.

“Mwachee.. Mama angu!..” Kidume nikakaza roho yangu dhaifu na kuibadili kuwa roho ngumu ya kwenye picha za sinema. Kauli yangu haikuwa na msaada wowote hule kwa Mama yangu. Kiukweli nilishindwa tu kuchomoka kwa mbavu ile iliyonishika. Alinibana haswa.

Kauli yangu ilimkera sana Baba Mdogo, aliacha anachokifanya na kunisogelea kwa jazba. Bila kukaa sawa na kujiandaa tayari kibao kizito kiliwaka mashavuni mwangu!. Uso niliuona mzito sana, nikahisi nimeongezewa kichwa cha pili ambacho napaswa kukihudimia tena chakula na mafuta ya kukipakaa. Maluweluwe yakawa nyumba yangu kwa muda. Nikajihifadhi humo kwa takribani sekunde kumi na kisha kutoka. Nikatema mate tu sakafuni yaliyochanganyika na damu nikiwa bado nimeshikiliwa mikoni kwa kamanda yule wa miraba minne. Niliziona hadi nyota zile ambazo mamajusi walizifukuzia kuonana na Yesu Kristo!.

“Umeleaje mtoto kama kuku hivi!, hana adabu?” aliongea akimrudia Mama alipo.

“Aaaah uwiiii!!, we unaona upo sahihi!. Mungu atakulipa tu… haaaa jamani!!!” Mama alilalama na kumfanya mdogo wangu naye kuibuka na neno. Angali naye alishikwa lakini hakuacha ubishi wa neno.

“Jamaniiiiii tuacheeee, Mamaaaaa..!” alilia. Alilia hadi nikaona aibu. Mimi ndio mwanaume nyumba ile lakini katu sijafanya chochote kile kulinda nyumba yangu. Vilikuwa ni vilio tu vya kuponea maumivi ya maovu yale.

“Anhaa! Kumbe wote jeuri eh!, wote mmekuwa si ndio. Mnataka kunijazia watu?, eh! Nauliza” Baba Mdogo sasa aliingiza mkono wake kwenye kingo ya suruali yake upande wa kufungia mkanda. Akapenyeza nje ya koti lake lile kubwa na kutoka na Bastora!, wote tukahamaki kwa mshangao. Ndani mule hakuna asiyejua ilikuwa ni nini. Niliziona kabisa kamasi za Mama zikishuka pamoja na machozi zote chini ‘Puuh!’.

Akawaonyesha ishara nyingine ya kichwa vijana wawili waliobaki. Tukaona wakimyanyua Mama na kumpeleka chumbani. Chumba ambacho Mama yangu mzazi alikua anakitumia na Baba yangu mzazi. Baba mdogo alifuata kwa nyuma.

Kwa kuwa chumba hicho kilitazamana na sehemu tulipo tulishudia tu baadhi ya matukio. Baba mdogo aliingia ndani baada ya vijana wawili kumfikisha Mama ndani kwa kumburuta. Baada ya wote watatu kuingia ndani, wale wawili wakatoka nje na kubaki mlangoni. Baba mdogo alikuwa bado ndani. Sisi tukiwa bado sebureni tumeshikiliwa tusilete fujo.

Mpenzi Mwandishi, kipi tusisikie jamani, yote ya ndani yalisikika. Hayakuwa siri katu. Sauti za aina mbili tu zilitoka ndani. Hakukuwa na zile sauti za panya wasumbufu waliokuwa wanaangaika na Mama kila siku, nadhani hata panya hao walikaa pembeni kuangalia unyanyasaji wa aina yake. Sauti hizo mbili zilikuwa ni za Mama yangu na Baba yangu mdogo.

“Ah!, Uh!, Ah!, Uh, Ooh!, Ah!..” hiyo ilikuwa ni mihemo ya Baba yangu kana kwamba kuna kazi kubwa kubwa ya kukata mti wa kuchomea tanuri kwa kutumia shoka alikuwa anafanya. Alikua anatoa sauti ngumu kuzitafakari.

“Haaaaaaaaaaah! Mamaaaaaaa! Mam! Aaih! Oh oh oh Mamaaaaa.. uwiiiiiiii!!” Mama naye hakuwa mbali kujibu mapigo ya sauti kwa kumjibu Baba kikamilifu. Ni dhairi kuwa Baba alikuwa anafanya mapenzi na Mama bila ridhaa. Alikuwa anabaka. Laulah!.

Ilikuwa ni purukushani ya hapa na pale barazani, sikutaka kuachia ukubwa wangu wa familia upotee kizembe, nilingangana hasa kutaka kuchomoka kwa mbavu yule. Sikutaka kuwa mayayi kama anavyosema Baba mdogo. Mungu sio Juma asee.

Nilifanikiwa kutoka mikoni mwa mbavu yule, hatua zangu tatu tu zilinirudisha tena kwa jamaa yule. Alinidaka kabla sijafika mbali na kunipa tena kibano cha nguvu kupita maelezo. Hiki kiliingia kisawasawa kwani nikua naumia viungo kama vyote vya mwili. Mdogo wangu alikuwa Amelia sana hadi kukatika machozi yake alikuwa kama mtu aliyepewa robo tatu lita ya pombe maharufu kama ‘Ngedule’. Alikuwa amelegea mno.

Tulilia hadi kuchoka, hakuna msaada wa aina yeyote ile uliopatikana, ukisikia Mungu yupo likizo ndio siku hiyo. Hata malaika walinzi hawakuwepo kabisa eneo la lindo. Kiufupi tuliteseka sana. Nilimuhurumia sana Mama yangu ambaye bado alikuwa anafanyiwa unyama na Baba yangu mdogo!. Tulizoea kushuhudia katika televisheni tu!...

ITAENDELEA…

Sent using Jamii Forums mobile app
hatari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (12)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
---------------------------------------------------

Nilifanikiwa kutoka mikoni mwa mbavu yule, hatua zangu tatu tu zilinirudisha tena kwa jamaa yule. Alinidaka kabla sijafika mbali na kunipa tena kibano cha nguvu kupita maelezo. Hiki kiliingia kisawasawa kwani nikua naumia viungo kama vyote vya mwili. Mdogo wangu alikuwa Amelia sana hadi kukatika machozi yake alikuwa kama mtu aliyepewa robo tatu lita ya pombe maharufu kama ‘Ngedule’. Alikuwa amelegea mno.

Tulilia hadi kuchoka, hakuna msaada wa aina yeyote ile uliopatikana, ukisikia Mungu yupo likizo ndio siku hiyo. Hata malaika walinzi hawakuwepo kabisa eneo la lindo. Kiufupi tuliteseka sana. Nilimuhurumia sana Mama yangu ambaye bado alikuwa anafanyiwa unyama na Baba yangu mdogo!. Tulizoea kushuhudia katika televisheni tu!...

ENDELEA SEHEMU YA KUMI NA MBILI…

Hakuwa na muda mwingi ndani, mda alioutumia ulimtosha kabisha kuhitimisha, Baba mdogo akatoka nje. Akatoka kwa kumalizia kufunga zipu yake ya suruali, akaweka sawa koti lake na kupisha mwingine kuingia. Aliingia yule mbabe mwingine akiacha na huyu aliyenishika mimi.

Bila woga na huruma naye alimtenda unyama Mama yangu. Hatukusikia tena sauti ya kilio kile cha mahaba kutoka kwa Mama. Zaidi ya kelele za raha kutoka kwa mtu aliyeingia. Alipomaliza ukawa mwanzo mwingine wa yule mwisho naye kuingia kumalizia. baada ya kuhahakisha kuwa wamerizika Baba mdogo akajongea pale tulipo. Alinisogelea mimi na kuniachia tabasamu kabla ya kuongea.

“Pole sana kijana, nalinda mali za ndugu yangu zisipotee…” Kabla hajamaliza nilifumba macho na kuandaa bomu la mate, kinywa nacho kikaongeza na makoozi ambayo sikuyacheua kwa miaka yangu yote toka nizaliwe. Mdomo wote ulipojaa nikamlipua bila kuchelewa.

Bila shaka bomu lile liliitwa uozo. Mate, makohozi, machozi, ghazabu na hasira vyote vilikuwa ndani ya bomu hilo. Lilitua sehemu sahihi kabisa, uso wake ulikuwa hautamaniki. Aliinua uso wake kwa hasira kabla ya kunichapa kofi jingine zito lililotuwa katikati ya shavu la kushoto, sikio la kushoto jicho la kushoto na sehemu ya kushoto ya ubongo. Lilikuwa ni zito kuliko la mwanzo.

Lilinipa mawenge ya aina yake yaliyonifanya nikumbuke uchungu alioupata Mama wakati wa kujifungua. Kofi hilo lilininyima nguvu na kujikuta naachiwa chini kama mzigo. Pumzi zikakata kwa muda na kuruhusu mapigo ya moyo kudunda dunda bila mpangilio maalum. Nilizimia mimi ndugu mwandishi.
---------

Mwandishi simulizi hii andika kama unavyoisikia, si vyema kuacha hata neno moja. Sipo na lengo la kupotosha uma kwa maneno ya vichekesho ninayoyatoa. Jamani hii ni simulizi ambayo nimepitia mimi. Laiti kama mmoja wenu angekuwa moja kati mshiriki alaa!!. Mbona angeopa FOTI kwa kusimamisha maisha akapumzike mbinguni kwa Baba….
---------

Naam!, nilikuja kuzinduka bado nikiwa katika kipengele ambacho sikipendi, pale pale nilipo paacha mwanzo paliendelea kuwa tukio kuu. Nilikuja kuhamaki Bastora ya Baba Mdogo ikiwa usawa wa kichwa cha Mama. Mdogo wangu akiwa mwenyewe kwenye kochi hajiwezi kabisa. Vijana wote wanne walikuwa wamesimama wima nyuma ya Baba mdogo.

Mama alikuwa amepiga magoti mbele kabisa ya bastora ya Baba mdogo huku mdomoni hakiwa hana la kuongea. Alikuwa amelegea sana kiasi kwamba kuna mda alishindwa hata kufunga vizuri kanga yake kusitili mwili wake. Alikuwa anaangaika bila neno kutoka mdomoni. Alichoka na shuruba zilizotokea, alikuwa hawezi kuongea, hawezi kulia, rangi yake usoni ilikuwa ni ya uvimbe uliochanganyika na uwekundu kiasi.

Alikuwa hatamaniki. hali hiyo yote niliikuta baada ya kuzinduka, nikataka kuinuka, nikajiona mwepesi sana kuliko maelezo. Wakati huo nilikuwa nipo mwenyewe tu, sijashikiliwa na mtu yeyote. Nikanyanyuka bila kujua nini naenda kufanya.

Kunyanyuka kwangu kulikuwa kosa la jinai. Ulisikika mlio wa bastora mbele yangu. Nilitokwa na yowe la nguvu lililohamaki damu nzito zilizokuwa zinarukia sakafuni. Mwili wa Mama nao ukafuata chini bila mpangilio.

Baba mdogo alimpiga risasi Mama yangu mzazi mbele yangu. Nikajikuta nimekuwa chizi kabisa kwa kutoelewa nini kinaendelea. Mdogo wangu nae alikuwa kimya tu kwenye kochi, sikujua ni nini kimempata, nikanyanyuka kwa nguvu kumkimbilia Mama yangu.. lakini nilipiga mweleka sakafuni kwa kukosa nguvu kabisa. Nikazimia tena.”

---------
Abdul aliacha kabisa kusimulia na kuanza kulia kupita maelezo. Si mke wangu wala mimi mwenyewe ambaye hakutoa chozi. Rose alikuwa akilia kwa kila nukta ya mpenzi wake Abdul akisimulia. Hakuijua simulizi hiyo kabla, ilionesha ilikuwa mpya kabisa masikioni mwake. Angali tulikuwa tunalia wote lakini kila mtu alichukua nafasi yake kumfariji Abdul ambaye mpaka sasa alituambia jina lake halisi la Denis. Mazoea yana tabu Tulishazoea kuita Abdul.

Mda ulikuwa umeenda sana, tumbo la kila mtu lilikuwa linaunguruma kama simba aliyekosa kitoweo. Simulizi ya abdul ilitupelekesha kwa muda bila kukumbuka kula. Breki ya kumweka Abdul awe sawa ikaendelea, kwa maana toka aweke nukta alikua analia tu kama mtoto. Ilikua inasikitisha sana kwa kweli. Hakuna asiyelia kwa wakati ule.

Njaa ilimpeleka Mpenzi wangu hadi jikoni kurekebisha. Alikuwa mwingi wa mawazo sana mpenzi wangu. Alimuhurumia sana Abdul. Mtu ambaye amepata mateso mazito mno katika maisha yake pasipo msaada. Alituacha barazani tukiwa bado na Rose tukimbembeleza Abdul. Ilikuwa kazi ngumu sana kumfanya Abdul atulie.

“Daah! Mwandishi… haki hipo wapi sasa!, ona hadi sasa sioni, sioni mimi mwenzako kisa baba mdogo. Maisha yangu yote yalikuwa na mateso toka nipo na miaka kumi na nne hadi leo hii, Nimepoteza Baba; aliuliwa. Nimepoteza Mama; alibakwa na kuuliwa mbele yangu. Mdogo wangu naye. Haaaaaaah Jamani.

Hakuna jirani, hakuna ndugu. Hakuna hata mmoja aliyeitika wito wetu ule wa uzuni. Hata risasi ile hawakuisikia?. Kweli amini ndugu mwandishi. ‘Sikio la maskini husikia ndoto tu’. Najua yote hayo ni chuki zao juu ya utajili tuliokuwa nao. Lakini sio sababu katika utu. Huwezi. Huwezi mwandishi kuacha mwenzako anakufa kisa kisasi… jamani Baba hakika umenipoteza mimi Denis..”

Abdul aliendelea kulalamika pasi nukta. Alitoa maneno ya uchungu yaliyomgusa kila mtu. Rose alikuwa analia tu lakini bila kutoa sauti. Sauti yote ilikakamaa haswa. Ilikuwa haitoki. Nilikuja kugundua kua hada daftari langu nililokuwa naandika baadhi ya matukio lilikuwa limelowa machozi. Haikuwa shida sana kwani nilifunga vifaa vya kunasa sauti ili nisipitwe na kila tukio. Hali ilikuwa sio shwari kwa kweli.

Rose alikuwa karibu mno na kipenzi chake, alimfuta machozi na kumpa maji anywe. Abdul alionekana kutia huruma kweli. Nilitamani kumwachisha kuadithia simulizi yake lakini haikuwa hivyo bado alikuwa na mengi ya kusimulia. Wapi alimpoteza dada yake?!, kwanini alipata ukipofu na Baba yake mdogo yupo wapi kwa sasa!. Bado nikabaki ya shauku ya kuendelea kusikiliza na kuandika baadhi ya vitu.

“Naakika simulizi hii itavuka mipaka ya kimataifa. Haki ya Abdul kupata kila kilicho chake lazima kitimie. Nitamsaidia kupamba simulizi hii kwa kila aina ya mapambio, ifike kila kona Duniani., Nahakika!” nilijiongelea kimoyo moyo kwa kujipa nguvu na imani kuwa hipo siku Abdul atapata haki yake. Kweli nilizamilia….

ITAENDELEA...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (13)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
---------------------------------------------------------

Rose alikuwa karibu mno na kipenzi chake, alimfuta machozi na kumpa maji anywe. Abdul alionekana kutia huruma kweli. Nilitamani kumwachisha kuadithia simulizi yake lakini haikuwa hivyo, bado alikuwa na mengi ya kusimulia. Wapi alimpoteza dada yake?!, kwanini alipata upofu na Baba yake mdogo yupo wapi kwa sasa!. Bado nikabaki ya shauku ya kuendelea kusikiliza na kuandika baadhi ya vitu.

“Naakika simulizi hii itavuka mipaka ya kimataifa. Haki ya Abdul kupata kila kilicho chake lazima kitimie. Nitamsaidia kupamba simulizi hii kwa kila aina ya mapambio, ifike kila kona Duniani., Nahakika!” nilijiongelea kimoyo moyo kwa kujipa nguvu na imani kuwa hipo siku Abdul atapata haki yake. Kweli nilizamilia….

ENDELEA SEHEMU YA KUMI NA TATU…..

“Rose!” Nikaita

“Ah! Abee” Rose ambaye ndiye mpenzi wa Abdul aliitika akionesha aibu.

“Kila kitu kitakuwa sawa, usijali” Nilimtia moyo.

“Haaah!, Labda! Kwani nashangaa kwanini Mume wangu amewaamini sana nyinyi. Mana katu hakuwai kumwamini mtu zaidi ya mke wake!, na sijawai kujua wala kusikia hiki asimuliacho” Rosea aliongea kwa aibu akifuta machozi. Maneno yake yakanifanya japo nitabasamu.

“Kweli wanapendana!” Nilijisemea tena kimoyomoyo.
Nikaongea na Rose mawili matatu, tukiwa tunatuliza munkari ya Adbul na kusubiri chakula.

Rose alisimulia siku aliyomuona Abdul, alisema walikutana njiani, alimwona Abdul akipata tabu kuvuka njia iliyosheheni magari. Akamsaidia hadi kuvuka na kutokea upande wa pili. Wakaachana.

Akasema akaja kumsaidia tena siku nyingine ambapo alikua anashida na chakula. Kipindi hicho alikuwa muhudumu wa muda kwa Mama ntilie. Toka siku hiyo akampenda mno Abdul na kuanza kumfatilia hadi wakaingia katika mahusiano baada ya kuzoeana. Akuendelea kuelezea tukio hilo japo nilimwona machoni kabisa kuna baadhi ya matukio anaruka au anaficha kwa kutaka kutoyasema. Kwa maana hadi kuishi na mtu kama Abdul basi kuna mengi sana mnapitia.

Tuliendelea na maongezi ya kujuana vizuri kati yetu kujenga usahihi wa taarifa, tukiwa tunasubiri chakula. Niliwaza sana chakula kinaweza kuwa kibichi kutokana na mke wangu kukosa kabisa hata chembe ya furaha. Uso wake ulijaa simulizi nzima ya Abdul.

Mke wangu alikuwa mwepesi sana katika kupoteza furaha, hasa akimuona mtu karibu yake hana furaha. Nililiona hilo, nikanyanyuka na kwenda japo kumpoteza katika mawazo yake. Baada ya muda kila kitu kikawa sawa. Na maakuli yakawa mezani.

Meza nzima ilikuwa kimya sana kila mtu akitegea kula. Kila upande ulikuwa na mawazo sana na kuwaza nani ataanzisha maongezi. Kwasababu mimi nilikuwa mwenyeji nikataka kuanzisha neno. Lakini ghafla nikawahiwa

“Hahahahaha haha!” kilisikika kicheko cha Abdul na kufanya meza nzima kuacha kula na kumshangaa. Kabla hajaulizwa kwa nini anacheka, akajibu kwa ufasaha.

“Daa!, chakula hiki na mboga kama hii ndicho kilikuwa chakula amabacho anakipenda sana mdogo wangu... Maria! Popote ulipo uje hapa kula na kaka yako.!” Akaongea akiwa na mwingi wa tabasamu na kutuacha wote tukiwa vinywa wazi.

“Mhhh! Huyo Maria atakuwa anakusikia kweli?, na je akija hapa utamuona?! Au kumjua??” Mke wangu akamtwanga swali ambalo wote pale tukaweka vijiko chini kusubiri jibu. Tulijua kabisa swali lile ni ngumu kupatikana kwa jibu fasaha. Lakini lilikuwa rahisi kwa Abdul.

“Sautiii… hapana sikumbuki!, Suraa…. Yah! Sura nakumbuka ila sitaiona sababu siwezi kuona kabisa…, hata nikimshika, siwezi kumfahamu, nilimpoteza mda sana. Wakati sina hisia juu yake. Laiti angepotea wakati nimepoteza uwezo wa kuona aaagh! Ningemjua bhana.!! na hawezi kuja hapa. Amekufa Maria!. Amekufa” Abdul akatamka neno zito ambalo lilifanya kupindua meza ya chakula na kila mmoja kubaki na huzuni ya aina yake.

Lakini kwa Abdul ilikuwa poa tu. Alitabasamu na kuweka vijiko viwili vya chakula mdomoni. Akaangaza meza nzima utazani alikuwa anatuona kila mtu wapi amekaa. Alikuwa na hisia sana Abdul. Baada ya kuzungusha kichwa meza nzima, Abdul alimwita kila mmoja akianza na upande wa kushoto alipokaa mke wake. Alipatia kila mtu na sehemu aliyokaa. Abdul alikuwa mchawi kwa kweli.


“Rose mke wangu. Ndugu mwandishi. Shemeji!... Hisia ni kitu muhimu sana katika maisha. Angali ningeishi maisha ya kutafutwa na kuangamizwa kama wanavyofanya, na hayahaya macho yangu mabovu!. Basi hakika ningekuwa mtu mmoja mkubwa sana hapa nchini. Nina uwezo mkubwa sana wa kuishi kwa hisia” Abdul alimaliza maneno hayo na kuonyesha ishara kusogeza vyombo kuwa ametosheka. Baada ya hapo akendelea.

“Ahsante Shemeji yangu!. Ahsante kwa chakula kilicho….. kilicho nikumbusha enzi hizo. Enzi amabazo tulikuwa tukigombana sana na mdogo wangu kuhusu vipimo vya chakula hicho. Kila mtu alitaka kuwa kinara kula wali mwingi.” Abdul aliongea huku akitoka mezani taratibu na kwenda sehemu ileile alipokaa mwanzo.

Mimi na mke wangu tulishangaa sana. Amewezaje!?. Tukaangaliana kwa maswali bila majibu. Hakika Abdul alikuwa kama mchawi, huwezi amani kama alikuwa ni kipofu!. ‘Hakika Hujafa, hujapatwa na mengi!’ alikaa tayari kuendelea na simulizi. Tuliokuwa mezani wote tukamaliza kwa hamu ya kujua nini kiliendelea. Moyoni nilijiandaa kupokea tena simulizi ya huzuni. Baada ya kumaliza kila kitu Abdul akaendelea pale alipoishia…
-----------------

“Nilipozimia, nilizinduka na kukuta nipo katika hali ya kiza. Niliangaza huku na huko na kumwona mdogo wangu Maria akiwa pembeni yangu huku chozi likimtoka.

“Kaka!!. Amka. Amka tuondoke hapa. Si sehemu salama..” Maria alisisitiza huku mikono yake ikiniinua mimi pale nilipo.

“Hapa wapi?” Niliuliza pasipo chukua hatua yoyote juu ya kile nilichoambiwa.

“Tupo stoo, wametuweka humu kaka, tuondokeee aagh!, mimi naogopa” akasisitiza tena.

“Mama?” Wala sikuwa mchoyo wa maswali, nikamuuliza swali lingine.

“Mamaaa!, Wameua!, Mama amekufa kaka!!! Kaka mamaa!. Nimeona kabisa wamembeba na kwenda kumtupa. niliwasikia.. kaka tukimbie jamani, naogopa!” Kilio cha Maria kikaongezeka na kuingia haswaa katika ubongo wangu. Chozi lilinitoka na mimi.

Nikakumbuka tukio la mwisho kulipata kabla sijazimia, nakumbuka niliwaona tu wanaume wakiongozana kuingia katika chumba cha Mama yangu. Waliingia kumtendea umyama Mama yangu. Baadae wakamuua!. Walimpiga risasi. Hasira zikanishika sawasawa, lakini sikuwa na chakufanya. Nikanyanyuka kwa nguvu na kuelekea mlango ulipo kwani licha kuwa na giza bado mwanga ulionyesha vyema mlango.

Kitu kilichotusaidia ni kuwa, milango yetu ilikuwa na ufunguo wa ndani. Mtu akiwa ndani ata kama akifungiwa kwa nje basi anaweza toka bila wasiwasi. Kulikuwa na kitasa kwa ndani ambacho hakikutupa shida kufungua, nikafungua taratibu kwa kuchungulia nje.

“Kwanini hukufungua mapema?” Nilihoji huku nikichungulia nje kuona kama usalama upo au la!.

“Na wewe eh!. tutoke bhana, swali gani hilo?. Eti nifungue?, nitoke si ndio? Peke yangu eh?, wakati robo saa nzima nakuamsha upo kama umekufa hapa chini!. Khaa!!, Fungua!! Bhaana aaagh!” Muda huo Maria alikuwa mkali sijawai kuona. Nilimwangalia kwa aibu kwani kweli nilikua nimezimia. Roho yake nzuri tu ndio ilifanya iniamshe na kunisubiri la si hivyo angeniacha niuliwe na mimi mle ndani.

“Twendee..” Nilimwita mdogo wangu kwa sauti ya upole mara baada ya kuchungulia nje na kuona kupo kimya.

Nilimwita tayari kwa kuondoka. Tulikuwa tayari kwa kutoroka nyumba hile. Lakini kwa jinsi alivyo nyanyuka mdogo wangu Maria. Ikanipa shaka zito moyoni. Alinyanyuka kinyonge sana kwa kujishika mapaja yake mkono mmoja, na mwingine kushika ukuta, huku nikisikia baadhi ya miguno ya maumivu ikimtoka, nikahisi jambo. Haraka nikaenda kumnyanyua na kumsaidia kutoka mahali pale. Alionyesha anamaumivu mazito mwilini kwani alishindwa tembea kwa ufasaha.

“Wamembaka!” Nilijikuta natamka neno hilo moyoni huku nikijaribu kuzuia hisia zangu zisionekane kabisa kama nimejua. Maana baada ya kumshika tu, mkono wangu uligusa damu kadhaa ambazo zilianza kukauka katika mapaja ya dada yangu Maria. Nikakaza roho na kumwongoza dada yangu kutoka eneo lile. Hata yeye Maria hakutaka kuonyesha kabisa kama kuna kitu kibaya kimempata. Alijitahidi kukaza miguu kuonesha yupo sawa lakini hapana. Ni jasiri dada yangu. Anaroho kama ya Baba yake. Akaficha maovu kifuani….

ITAENDELEA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (14)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
---------------------------------------------------------

Nilimwita tayari kwa kuondoka. Tulikuwa tayari kwa kutoroka nyumba hile. Lakini kwa jinsi alivyo nyanyuka mdogo wangu Maria. Ikanipa shaka zito moyoni. Alinyanyuka kinyonge sana kwa kujishika mapaja yake mkono mmoja, na mwingine kushika ukuta, huku nikisikia baadhi ya miguno ya maumivu ikimtoka, nikahisi jambo. Haraka nikaenda kumnyanyua na kumsaidia kutoka mahali pale. Alionyesha anamaumivu mazito mwilini kwani alishindwa tembea kwa ufasaha.

“Wamembaka!” Nilijikuta natamka neno hilo moyoni huku nikijaribu kuzuia hisia zangu zisionekane kabisa kama nimejua. Maana baada ya kumshika tu, mkono wangu uligusa damu kadhaa ambazo zilianza kukauka katika mapaja ya dada yangu Maria.

Nikakaza roho na kumwongoza dada yangu kutoka eneo lile. Hata yeye Maria hakutaka kuonyesha kabisa kama kuna kitu kibaya kimempata. Alijitahidi kukaza miguu kuonesha yupo sawa lakini hapana. Ni jasiri dada yangu. Anaroho kama ya Baba yake. Akaficha maovu kifuani….

ENDELEA SEHEMU YA KUMI NA NNE…

Ndugu Mwandishi nililia. Nililia kimoyomoyo. Kila tukio akilini mwangu ni picha tu ya adui yangu mkuu Baba mdogo. Hakika Baba Mdogo anamengi ya kuujibu moyo wangu. Hakika kisasi chake kitadumu machoni kwangu mpaka nimuondoe katika dunia hii kwa jinsi alivyonipa tabu mimi kiumbe dhaifu.

Sikuwa na ndoto hii ya kutangatanga ndugu Mwandishi. Ona sasa Mwandishi; DADA! Eh! Kweli! Dada jamani wa miaka kumi tu. Wanabaka!!!. Lo! Hakika!!, Hakika Wamekufa angali wapo hai. Mungu hatawahukumu.”.. Abdul alikomea hapo kwa kuinama chini na kutafakari kile anachosimulia!, akainuka na kuomba maji ya kunywa.

Uso wake ulikuwa na lundo la maumivu ambayo yamepelea kuwa na wekundu utokanao na machozi yatokayo katika kila kipande cha simulizi. Pafu tatu tu za maji zilitosha kabisa kukata kiu yake ya mda na kuendeleza wimbi la matatizo katika simulizi yake ya kweli ya maisha….

--------------
“Basi Mwandishi tukakokotana na mdogo wangu hadi sebureni ambako kwa mara ya mwisho matukio yote yalitokea hadi nikazimia. Nikakutana na ushahidi wa michilizi ya damu kuelekea mlangoni.

Kwa bahati niliiona ile Bastora aliyotumika kumuua Mama. Niliiona imeketi katika kochi. Nilihapa kumuua kifo kinachofanana na wazazi wangu. Nikachukua na kuiweka silaha hiyo kiunoni mwangu na kuifukia na shati. Nilikuwa sijui jinsi ya kuitumia lakini ujasiri tu wa kuibeba kama kinga ulitosha kabisa kufariji nafsi yangu. Sikuwa na namna ndugu mwandishi.

Mlango wa kutokea uwani ulikuwa wazi lakini geti kubwa lilikuwa limefungwa, tukatumia eneo la nyuma ya nyumba kulipokuwa na tenki la maji, nikaanza kupanda mimi hadi juu, nikamshika na mdogo wangu kwa kumsaidia na wote tukatua chini upande wa pili wa nyumba. Tulikuwa salama tu kwa mwonekano lakini kimwili na kiafya anajuwa Mungu kwa kweli.

Hatukupata!, na wala kutaka msaada wa aina yeyote ile kutoka kwa majirani kwani majirani wote hawakuwa rafiki na familia yetu kutokana na kiburi cha pesa. Na tungeenda vipi kwa majirani wakati tumekuwa Nguruwe karibu na Msikiti?. Na wengi wa majirani walikuwa hawatujui kabisa kutokana na kuwepo ndani kwa muda mrefu, kama hatupo ndani, basi tupo shuleni, na kama sio shuleni basi kwenye gari kula bata sehemu za starehe na familia…. Tukakomaa kwa kukaza mwendo, kutafuta msaada mbele kwa mbele.

Naam tukaanza kutangatanga kila kona ya njia tuliyoiona, tukawa wenyeji wa dira ya dunia. Nyumbani kukawa Kaskazini kwa sekunde, Magharibi kwa Dakika; Kusini na Mashaliki kwa Lisaa tu. Ulikua ni mwendo wa kutembea bila mafanikio. Nikiwa nimebeba uzito wa mawazo kichwani mwangu, huruma ikawa pande nyingine ya kujidai. Nilimuhurumia sana mdogo wangu Maria, uso umemvimba kama yale matunda yenye manundu manundu, alikuwa amechoka kama mtu aliyepigana masumbwi kwa raundi zaidi ya kumi na mbili bila mafanikio na kufanikiwa kutoka suruhu.

Tulibaki kushangawa tu na watu waliotuona kwa huruma kama watoto waliokosa Mama na Baba. Wamekosa nyumba, wamekosa chakula. Nakumbuka tulitembea kuanzia saa sita ya ahsubuhi hadi saa tisa ya jioni. Bado tulisonga mbele kwa kutojua wapi tunaenda na wapi tutapata msaada. Kuchoka hakukuwa suruhisho la kupata msaada.

Ilituchukua nusu saa baada ya kuhitimu saa tisa katika saa za wapiti njia. Tumbo lilikuwa mchezoni kugombana na miguu pamoja na akili. Hakuna kilichoenda mbele hata kimoja. Kila hatua ilitabasamu kwa ghadhabu za kukosa lishe. Tukakaza mwendo.

“Liwalo na liwe!” Nikajisemea kwa nguvu na kumkokota mdogo wangu hadi sehemu ya mtaa mmoja ambapo kuna moja ya mgahawa uliozungushiwa na mabati. Palikuwa pachafu sana kiasi kwamba huwezi fikiria mara mbili kama kuna chakula anachokula binadamu kinatoka pale.
Mguu kwa mguu hadi mbele ya mgahawa huo.

“Shhikamo!” Nikatoa salamu Iliyosindikizwa na uso wa uzuni. Nikaona Mama yule amekunja sura kwa ghadabu.

Mama huyo akaweka mikono yake kiunoni kwa kukunja dera lake vizuri. Mkono wa kushoto ulikuwako na mwiko ambao umetoka kukorogea maharagwe muda mchache uliopita. Hakuchukua muda, tayari mwiko huo ulisharushwa kifuani kwangu. Kwa bahati alinikosa. Hakuna lililofuata pale zaidi ya mbio. Tulipata nguvu za kukimbia ghafla eneo lile huku tukisindikizwa na matusi ya hapa na pale kutoka kwa Mama yule.

“Mbwa koko nyie!!!, juzi tu mmenitia hasara hapa. Kuwapa chakula mbwa nyie mkaamua kuweka sabuni hadi kwenye mboga ya wateje. ***** nyinyi!.” Mama yule alipandwa kweli na ghadhabu na kufanya wadada wengine walioko pale wote kucheka kwa pamoja.

Tulikimbia bila kuangalia nyuma hadi tulipohisi kuwa maneno yake hayajatufuata malipo tuliposimama. Tulihema sana huku mikono yote ikiwa kwenye vifundo vya magoti. Nilimwona mdogo wangu amepata nguvu za ajabu ambazo zilimfanya kuachia kicheko.

“Hahahaha kaka!, Kumbe maisha ndivyo yalivyo huku nje!, Hahahaha” Alicheka sana mdogo wangu na kufanya na mimi nitabasamu na kuanza kuzoea hali ile, tukaweka kitako karibu na mgomba mmoja ulio amua kijiuotea karibu na njia ya kupita watu. Bado tulikuwa katika vichochoro vipya machoni mwetu.

“Kaka tumbo!” Maria alilalama tukiwa bado tupo chini kuvuta hewa ya hasara iliyotolewa na mgomba hule.

Tumbo hilo bila shaka lilikuwa ni la njaa tu, kwa maana hata mimi kwa upande wangu nililisikia likinyonga. Nikampa moyo kuwa tutakula sio mda kwa kudra za Mwenyezi Mungu. Tuka nyanyuka pale na kuanza kutembea. Vichochoro hivyo vilikuwa havina watu kabisa, labda kwa sababu vilikuwa ni nyuma ya nyumba za watu.

Tulitembea sana kama saa nzima bila kujua uelekeo wetu. Mimi na mdogo wangu begani. Nilikuwa nawaza njia ya kupata kitu cha kula. Mawazo ya kuiba yakagonga mwamba kichwani. Nikajisemea mwenyewe kuwa yeyote atayekuwa mbele yangu na anazo dalili za fedha basi ataimba Alleluya!. Tulianza kuuzoea uyatima kwa kuwa hakuna chochote tulichonacho mikonomi mwetu. Tayari ramani nzima ya maisha ilishapotea kichwani.

Mungu alivyo mwema, tukakutana na bomba la maji ambalo limepasuka. Kwa muda hapo pakawa nyumbani, tulifakamia maji hayo hadi tulipohisi yametukoa. Kidogo taswira ya kuendelea kuishi ikaja tena moyoni mwangu. Mdogo wangu toka tukimbizwe kwa yule mama ntilie basi alikuwa imara mno. Hakuonyesha doa lolote lile kama amebakwa na wale mabaunsa. Kila nikimwangalia nilimwonea huruma. Nikaapa kumlinda hadi mwisho wa maisha yangu. Bado kisasi kilikuwa kuchonga siraha ya kumhangamiza Baba mdogo. Tulitoka pale na kusonga mbale….

ITAENDELEA…

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (15)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
---------------------------------------------------------

Tulitembea sana kama saa nzima bila kujua uelekeo wetu. Mimi na mdogo wangu begani. Nilikuwa nawaza njia ya kupata kitu cha kula. Mawazo ya kuiba yakagonga mwamba kichwani. Nikajisemea mwenyewe kuwa yeyote atayekuwa mbele yangu na anazo dalili za fedha basi ataimba Alleluya!. Tulianza kuuzoea uyatima kwa kuwa hakuna chochote tulichonacho mikonomi mwetu. Tayari ramani nzima ya maisha ilishapotea kichwani.

Mungu alivyo mwema, tukakutana na bomba la maji ambalo limepasuka. Kwa muda hapo pakawa nyumbani, tulifakamia maji hayo hadi tulipohisi yametukoa. Kidogo taswira ya kuendelea kuishi ikaja tena moyoni mwangu. Mdogo wangu toka tukimbizwe kwa yule mama ntilie basi alikuwa imara mno. Hakuonyesha doa lolote lile kama amebakwa na wale mabaunsa. Kila nikimwangalia nilimwonea huruma. Nikaapa kumlinda hadi mwisho wa maisha yangu. Bado kisasi kilikuwa kuchonga siraha ya kumhangamiza Baba mdogo. Tulitoka pale na kusonga mbale….

ENDELEA SEHEMU YA KUMI NA TANO…

“Nimechoka sana shoga!, hapa navionea huruma hivi vyombo tu!. Na hili shombo kweli!. Aaaaagh! Mimi sioshi leo. hapa nafunga hivihivi nakuambia. Biashara yenyewe ya manati!... Mimi sijaua kwetu mwayaa!.” Alisikika Mama mmoja ambaye alikuwa akipiga soga na rafiki yake. Wote wakicheka kwa kurushiana uvivu. Alionekana kuchoka sana na biashara yake hadi kumfanya kushindwa kuosha vyombo ambavyo tayari vimetumika. Tukaona fursa ndiyo hiyo bora kuomba ukiwa umesimama kuliko kuomba wakati unatembea.

“Mama samahani tunaomba tuoshe sisi!” Maria alijitokeza kwa Mama yule akiwa na ujasiri. Alijua kabisa lazima katika kuosha vyombo hivyo kuna vyakula vya wateja wagusaji vimebaki. Na mimi nikajitokeza na kuungana na mdogo wangu.

Mama huyo aliyekalia ndoo na mwenzake akiwa katika kiti cha plastiki walituangalia wote kwa mshangao. Wakarudisha tena macho yao na kuangaliana. Baada ya hapo miguno ikafuata na kuanza kukonyezana.

“Watoto!, hamjala!!, mnataka pesa au kuosha vyombo?” Yule mwingine aliuliza maswali ambayo majibu yake yote yalikuwa sahihi.

“Tunanjaa Mama. Toka Asubuhi hatujaingiza chochote!” nilijibu swali lake.

“Nyie watoto tatizo mnakuaga sio waaminifu. Aya kuleni kwanza afu muoshe vyombo. Na mkila nisiwaone tena hapa. Usije mkajua mimi Mama misaada bure!.” Mama huyo alinyanyuka kuelekea kwenye masufuria yaliyopo ndani ya kibanda chake.

Alimpita rafiki yake na kugonga naye mikono kwa bashasha. Mwenzake huyo akaweka jiwe nyingine nzito moyoni mwetu.

“Na wakiamua kuiba sasa! Mbona utaomba poo!. Naona leo wamekuja kwa stairi ya kuomba!”. Aliongea maneno ambayo niliyasikia pekeyangu. Mdogo wangu alikuwa bize kuangaza jinsi Mama yule anavyojaza chakula kwenye sufuria.

“Baati yenu sana leo ukoko ulikosa wateja. Kama mtauweza malizieni. Fanyeni haraka. Ohoo ninamume miimi!” Mama huyo alikuwa mwongeaji sana. Hakutia maanani nini anaongea. Akatuwekea chini na sisi bila shaka tukaanza kufumania chakula hicho.

Ulikuwa wali mwingi sana na maharagwe. Tulimaliza hata dakika tano hazikufika. Mama huyo akatusogezea na sufuria la ukoko alilomwagia mchuzi wa nyama kidogo kulowanisha. Nao tuliuchangamkia maridhawa bila kutumia vijiko. Kucha zetu na meno yetu tayari vilishanoleka kwa njaa ya siku nzima. Wao walibaki kutushangaa tu kama wanaona mashindano ya walaji kombe la dunia.

Tulimaliza kwa wakati na kwa ushirikiano wa hali ya juu. Tulisugua masufuria yake na ukoko mwingine kuweka kwenye mfuko kwaajili ya baadae. Tulimshukuru Mama yule mara nyingi zaidi. Alituonea huruma sana lakini hakuwa na la msaada mwingine. Maana hata huo msaada aliotupa alitusaidia sana kwa maana watu wengi hawapendi kusaidia watoto wa mitaani kwa maana hawachelewi kuzoea kuja kila siku na mda mwingine kuvamia na vijana wenzao kuleta fujo au kupora.

Alitupa onya la kutorudi tena mahari pale. Hakutaka historia yeyote ile isije ikamletea matatizo. Hata hivyo tulisha apa kwa Mwenyezi Mungu kuwa mimi na mdogo wangu hatuwezi kutoa siri zetu za ndani kwa mtu tusiye muanimi…..” Abdul alikohoa kidogo akameza mate na kuendelea.
----------

“Naam bado tulikuwa njiani, kwa sasa tulikuwa watu watatu, Mimi Denis, mdogo wangu Maria na Mfuko wetu wa Rambo uliojaa ukoko. Tulitembea kwa tabu sana kutokana na shibe. Tulitembea hadi kufika karibu na sehemu yenye uwazi na palikuwa na mchanganyiko wa watu, maduka nayo yalikuwako mengi sana. Roho ilituuma sana tulioona wamama wakiogesha na kucheza na watoto wao. Roho iliniuma sana. Nikamkumbatia mdogo wangu na kuendelea kusonga mbele.

Hatukujua tupo maeneo gani na muda gani. Lakini Giza lilishaanza kuushinda mwanga hafifu wa jioni. Usiku ulichomoa mbawa zake na kukumba mji wote wa Songea., kimya kilitawala mara baada ya maduka mengi kukosa wauzaji. Walishafunga kutokana na giza. Tulijikuta tupo katika mchochoro ambao umetenganisha maduka yaliooneshana mgongo. Bado tulikuwa mimi, mdogo wangu na mfuko wetu kwa pamoja.

Safari yetu ilikwama kwa muda mara baada ya mbele yetu kuwa giza ambalo lilisababishwa na kutokuwepo kwa taa. Kwa ugumu tukashinikiza kupita maeneo hayo. Mimi nilitangulia mbele na nyuma alifuata mdogo wangu nikiwa nimemshika mkono.

Mbele yetu hatua kama ishilini hivi kulikuwa na vijana waliozunguka duara. Walikuwa wakitumia mwanga wa simu wakiwa wote wameinamisha vichwa na migongo yao, sambamba na kukunja goti moja kama watu ambao wanamuomba muumba wao. Nikamwacha mdogo wangu hatua chache na mimi, ili nisogee kama naweza pata msaada wowote.

Hatua zangu ziliwashtua mno vijana wale na kuanza kutawanyika huku kila mtu akitaka kuchukua njia yake.

“Askari!, Askari!.. Nani Yupi!. Oi” Zilikuwa sauti za vijana hao ambao nikaja kugundua kuwa walikuwa wanacheza kamali.

Walipokaa sawa wakaja kugundua kuwa ni mimi nyoka wa kijani. Mtoto tu niliokuwa nawatishia nyau. Wakakusanyika tena kwa pamoja na kunisogelea.

“Umetumwa!” Nikaulizwa swali amabalo nilibabaika kulijibu.

“We Boya unaulizwa umetumwa!” Mwingine akapaza sauti. Wote walikuwa wanamaumbo kama yangu. Inaonekana ni watoto tu wa mtaani waliokosa kila aina ya malezi kutoka kwa walezi wao.

Naam nikaona kabisa nisipokuwa ngangari basi naweza poteza malinda sehemu ile. Wanaweza kunionea, na kwa jinsi nilivyo mayai wanaweza hata kunibaka. Kwa maana sikuwa na salio lolote mfukoni ambalo litawavutia. Nikagangamara kama na mimi ni mtoto mwenzao wa mtaani. Nikawapa soga za kiteja teja kukurupuka mikoni mwao. Nilijua nimeshaingia choo cha kike… nikaanza kujitahidi kuigiza.

ITAENDELEA…

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom