SIMULIZI: “ANGAMIZO” (22)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email:
xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
--------------------------------------------------
“Welcome Mozambique!” aliongea kwa lugha ambayo sio ngeni akilini mwangu. Niliidadavua mapema sana. Tayari akili yangu ikacheza kwa uharaka zaidi. Nikapitisha macho huku na huku kuona ubovu wa nchi hiyo ya Msumbiji ambayo naisikia tu kwenye mihadhara ya watu na mwishoni kabisa mwa ramani ya Tanzania. Toka hapo historia ya maisha yangu mimi Maria ikabadilika. Nilijikuta tu jina linabadilika na kuwa Rose. Rasmi nikawa Rose nchini Msumbiji, Rose katili, Rose mtamu Msumbiji nzima…”
ENDELEA SEHEMU YA ISHILINI NA MBILI…
----------
“Kaka yangu mpendwa. Msumbiji niliishi kwa raha sana, nilipata kila raha ambayo watu wanaita raha. Nilifanya kila kitu ambacho unahisi nilifanya. Nilikuwa huru. Nilikuwa sugu!, nilisahau kila kitu kwa muda mfupi. Na hakika kumbukumbu zangu zilipotea nikiwa huko. Nilimsahau Mama, Baba, na kila kitu kuhusu wewe.
Tulipofika salama katika moja ya nyumba kubwa ya kifahari. Ilikuwa ni nyumba ya yule nyemela dereva aliyetupokea mpakani. Tukapokelewa hapo kwa bashasha na tambwe za kila aina. Rose mimi nikakaribisha maisha mengine mageni.
Lugha ambayo kwa kiasi kikubwa ilikuwa inaongelewa ndani humo ni kireno na kiingeleza kwa uchache. Kiswahili kiliongelewa kwa uchache sana, tena sanasana ni nyakati za kuongea na mimi tu basi. Walijua siwezi kabisa kireno hivyo walitumia kufichia siri zao. Na walifanikiwa, kwani hakuna nilichokinyambua.
Nilikaa kwenye nyumba hiyo kwa siku tatu. Licha ya kugoma kuongea kabisa hawakuacha kuniongelesha. Nadhani walianza kuniteka kifikra sasa.
Kaka!, nilizoea sasa, nilizoea hali hile, nikahisi mimi moja kati ya samiliya yao. Nakili ilikuwa kosa lakini nafanyaje kaka yangu. Hakuna nilichokumbuka. Hakika!, hakuna hata moja. Nilikuwa sikumbuki kabisa nini kilitokea nyuma yangu. Inaonekana kwamba matatizo niliyopitia yalinichanganya kisaikolojia na kujikuta nimesahahu kila kitu.
Basi tuliishi vizuri tu tena bila matatizo ya hapa na pale, japo maisha ya huko yalikuwa maisha ambayo sikuyachagua lakini niliishi. Nakumbuka kuna siku yule dereva aliyenibeba Tanzania aliniambia kitu.
“Umekuwa mzoefu sana sasa!. Hiki ndicho kitu ambacho nilikisubiri kwa muda mrefu. Tunakwenda kufanya biashara sasa!!. Usiniangushe!.” Aliongea hivyo bila kusema ni biashara gani hiyo ambayo mtoto kama mimi naweza kuifaya. Hawakusubiri hata nimalize mwezi tayari walinipa tenda ya kuhudumu Baa. Haikuwa na kikwazo katika kuikataa wakati tayari nilikuwa mwenyeji wa vilevi na sigara hizi ndogondogo. Walinifundisha mengi kabla ya kunipa tenda hiyo.
Nikabadili saa yangu ya mkononi kwa kuyafanya masaa ya mchana kutumia usiku. Hakuna kazi inakera kama kazi hii ya kuhudumu baa, utazoea kazi lakini sio kila mteja atakayekuja. Mwanzaoni niligombana sana na wateja lakini kikazoea na kuwafanya wateja haswa. Nikawa nawauzia pombe na vingine wanavyotaka. Kwa mara ya kwanza nikaanza kutoa ile roho ya uchoyo na kugawa usiri wangu kwa baadhi ya wateja.
Nilikuwa mtoto lakini mambo hayo yakanikuza. Umbo likaongezeka na kuvutia wengi. Nikafanya biashara mbili kwa nyakati moja. Kama pesa hipo unaweza agiza vyote kwa mara moja. Wateja walichangamkia fursa kwa kweli.
Bosi wangu nae alitaka faida zaidi, hakaona baa haitoshi. Akaniongezea mtaji kwa kuniamisha hapo na kunipeleka sehemu ambayo inafaa zaidi katika maisha yangu. Alinipeleka katika dangulo la malaya na machangudoa maarufu nchini humo, yeye ndiye alikuwa mmiliki wa sehemu hiyo. Dangulo lipo katikati ya mji mkuu wa Msumbiji. Huko biashara ikawa nzuri mno.
Nikaanza kutumia pombe japo kwa uchache, madawa ya kulevya mara moja kwa wiki. Nilikuwa na laana kubwa ya Mama yangu mzazi!. Hakika kusahau kwangu kila kitu kulinipa laana. Nikawa mtu wa kulala na wanaume kila siku, saa nazo zikasogea mno, zikasukuma umri wangu na kuufanya kutimia namba nzuri ambayo serikali ya Msumbiji hutoa reseni, vibari na vitambulisho endapo ukiufikisha.
Nilikuwa na miaka kumi na nane sasa. Hakuna starehe nisiyoigusa. Nikawa mjanja hata kwa bosi wangu. Nikamchanganya na penzi langu zito la ajabu ambalo nadhani lilikuwa geni kwake. Nikaanza kumtawala na yeye. Kwa vile nilikuwa fundi, tena fundi haswa haikunipa shida kumteka.
Kaka kipindi hicho nilikuwa hakuna upande ambao sijawahi kugeuka. Ukinileta katika chumba kigeni uwezi amini, nitazijua kona zote ambazo unajificha. Na lazima niwe mshindi!, na hiii ndiyo ilinipa mechi nyingi za kirafiki kwa wengi kutokubali mchezo na kukata rufaa katika mahakama ya Ngono duniani. Nilikusanya pointi tatu muhimu na kutwaa taji la Ngono nchini Msumbiji. Nilikuwa zaidi ya Mesironaldo.
Nilipo mchanganya sana na mapenzi yangu alinipa kibari cha kutoka nje ya nchi. Hakika miaka ilisogea sana. Hakuna nilichokuwa nakumbuka Tanzania. Nilikunywa pombe na kubugia dawa za kulevya kwa kupunguza mawazo lakini nashangaa baada ya kupungua, mawazo hayo yakaondoka kabisa. Kaka sio bure waliniloga mimi, yaani sikumbuki hata jina la Mama yangu mzazi? lo!!.
Kaka mwache mwanamke apewe sifa zake za uke!, akiutumia vizuri uke wake, anakuwa mshindi katika kila pambano na mwanaume. Nilimshinda mwajiri wangu kwa kumteka kimapenzi na kuniruhusu kwenda Tanzania kusimamia miradi yake. Ila alinipa onyo. onyo lenye maneno machache tu.
Onyo la katu! Katu nisikaribiane na mtu anayeitwa Frank!, hakunipa maelezo ya ziada hata kidogo aliishia hapo. Nikajua ni marumbano yao ya kibiashara. Nikapiga moyo konde na kujiandaa na safari. Kaka kipindi hicho mimi ni mzuri sana. Sana!. Nilikuwa mzuri mno wa kumvutia kila mwanaume. Ila kibaya nilipoteza kumbukumbu. Sikukumbuka chochote kile. Likawa doa la uzuri wangu. Hata Baba Mdogo wangu sikumkumbuka.
Hata nilienda kufanya niliyoagizwa na bosi wangu uko Tanzania??, hahahahaha!!, ngoja nicheke Kaka!, ulikuwa ni upumbavu tu. Sio kwamba sikufika Tanzania!, nilifika sana lakini hakuna cha mradi wala maradi niliyosimamia.
Nakumbuka safari ile ya kuja Tanzania ilikuwa kama sio jumapili basi ni jumatatu ya mwanzoni mwa mwezi wa mvua zinazonyesha bila mpangilio. Kama ilivyo kawaida ya tope, halikosi utelezi. Dereva nae hana reseni yaani we acha tu. Alitupindua Kaka!.
Yaani ilikuwa hivi, tulitoka salama kabisa Msumbiji na basi la abiria. Sitaki kuwa shaidi wa spidi ya dereva, nadhani alikuwa sahihi!. Sasa shida nini?. Dereva alishindwa kuhimili mikikikiki ya matope njiani, barabara ilikuwa mbovu sana. Si ndio hizi hizi ambazo zimetengwa rasmi wazitengeneze karibia na uchaguzi?.
Kaka tulianguka vibaya sana. Tuliviringika nje ya barabara zaidi ya mara sita, baada ya gari nililopanda kuacha njia. Sikumbuki majeruhi wangapi na tuliwapoteza wangapi lakini kikubwa mimi bado naishi.
Mungu bado alikuwa na makusudi ya mimi kukutana na Kaka yangu Denis!. Hakika Mungu mkuu!.” Rose alipomaliza sumulizi hiyo alitabasamu tu na kuinua uso wake hadi kwa Kaka yake aliyoko karibu, akaliacha tabasamu hilo lisawili katika mashavu yake kisha kuendelea.
“Kaka kweli mimi sikufa, hata sikufa mimi katika ajari hiyo, si unajua dada yako jasiri eh!, nilichubuka kidogo tu. Hapa na hapa!” Rose aliendelea kusimulia huku akiwa mwingi wa matendo.
Alikuwa anaonesha sehemu zake za mikono ambazo zilipata majeraha. Lakini alionesha tu, kwani hazikuwepo kwa wakati huo. Zilishatoweka. Rose alikuwa mkakamavu wa matendo. Japo inasikitisha lakini inapendeza sana jamani.
“Naaaam!, japo sikufa na kuumia sana. Lakini nilizimia. Nilijikuta tu nipo sehemu ambayo kuna weupe weupe ule wa hospitali!. Nilipoteza tena kumbukumbu kwa mara ya pili. Jambo lingine la kumshukuru Mungu ni kuwa hakuna nilichokumbuka zaidi ya jina langu tu Rose!. Nilipozinduka hapakuwa na mtu yoyote sehemu hile.
Nikanyanyuka na kukaa kitandani kwa dakika kama moja kushangaa sehemu niliyopo. Chumba kilikuwa vizuri lakini hakuna nilichokumbuka. Nilijichekea tu mwenyewe. Kwa hali niliyokuwa nayo nilipaswa kabisa kupitilizwa hospitali kuu ya taifa ya vichaa Dodoma inaitwa milembe sijui. Nilikuwa sijielewi.
ITAENDELEA…
Sent using
Jamii Forums mobile app