Naona tatizo kubwa lipo kwako wewe uliyeandika huu uzi wa kumshutumu wifi yako. Kuna mambo kadhaa ambayo ungepaswa kuyafanyia utafiti kabla hujaja kumfinisha huyo unayemwita wifi yako na sisi wana jf.
Je una muda gani tangu uolewe na huyo mumeo? Je unafahamiana na ndugu wa mume wako? Kwa maelezo yako inaelekea huyu unayemwita wifi mlikuwa hamfahamiani hadi alipokuja kuwatembelea siku tatu zilizopita.
Je unalijua lengo/sababu ya huyo wifi yako kuja kwa kaka yake? Amekuja kumtembelea tu au ana tatizo/matatizo? Huko kulala kwake unakokuzungumzia kama ni kero kwako unajua kumesababishwa na nini? Je unajua kama anaumwa au kuna tatizo la kisaikolojia linamsumbua? Kutokana na maelezo yako mwenyewe, ni wazi kuwa huna mawasiliano mazuri na huyo wifi yako hata baada ya kufika kwako. Inawezekana kabisa ule ukaribisho uliompa ndiyo umemfanya awe analala akiwaza aondoke. Kwa bahati mbaya sana wanawake wengi kutokana tu na kutumia akili za kuambiwa bila kuchanganya na za kwao, pindi wanapoolewa tu wanaanza kujijengea ukuta/defence kwa kuanza kuwachukia mawifi na mama wakwe zao bila sababu ya msingi kwa vile tu waliambiwa na wenzao kuwa mama wakwe na mawifi ni wabaya. Huu mara nyingi huwa ndiyo mwanzo wa uadui na ugomvi katika familia familia. Sikatai kuwa kuna mama wakwe na mawifi ambao ni chanzo cha shida katika ndoa za watoto/kaka zao ila ni kuwa ikiwa wewe mke ndiyo chanzo cha kuwachukia basi ujue hutaishi kwa raha katika ndoa yako. Kumbuka huyo unayemchukia ndo aliyemzaa mumeo, hao mawifi ni ndugu wa damu moja na mumeo, mumeo hataweza kukuvumilia kuona wewe ukiwachukia wazazi/ndugu zake bila sababu. Ikitokea kuwa mama mkwe aau mafifi ndiyo wamekuchukia wewe basi vumilia na uwe na amani, ukweli ni kwamba wanaume wengi wapo tayari kuwalinda wake zao pale wanaponyanyaswa na mama mkwe au dada zao lakini hawapo tayari kumvumilia wake zao kuwachukia ndugu za mwanaume.