Simuamini tena mke wangu!

Simuamini tena mke wangu!

Afu Kongosho nimeshachunguza ndugu...ndugu hawanaga shukurani kabisaaaaa

Hata biblia haiwatambui...inawatambua wazazi waliobaki tupa kule.

Unajua kuna familia zinashauri watoto wao wa kike wawaibie waume zao wajenge kwao...eti wenyewe wanasemaga 'security'. Akyanani...watu wanaenda kwenye ndoa wakiwa na security sijuhi insurance...

Mtu umeolewa...kwenu unajenga ili iweje...ndio maana Wahaya (mostt of them) mwanamke arithi ardhi kwao...ili akiolewa akatulie na mumewe


Afadhali na wewe umesema.

Kama hela ya mke hailiwi na watoto au mume nani sasa ataila?

Yaani hata jambo la msingi kama elimu ya watoto?

Mie nimeshangaa kwa kweli.
 
Pole sana mkuu. Hili tayari ni tatizo na wala usilipuuzie na kusema ni kawaida au wanawake ndivyo walivyo au pengine useme ndoa ndivyo zilivyo. Matatizo mengi ya ndoa huwa si mambo makubwa sana kwani huanza kidogo kidogo na hasa kama hakuna communication mmh shida huongezeka. Hebu jaribu kukaa na mwenzako na mzungumze mashaka yenu yaani hilo dukuduku lako kuhusu pesa na hisia zako kwamba huenda anafanya biashara na ndugu zake. Kabla hatujamlaumu au hujamlaumu tafuta kujua hilo huenda na yeye alianza kufanya hayo kutokana na mashaka aliyo nayo juu yako. Pia suala la mtoto ni vema mkawekana sawa ili mshirikiane kulingana na vipato vyenu na majukumu mliyonayo. Hili nalo mkiliweka mezani si jambo kubwa mtafikia muafaka. Kumbuka si kila tatizo lafaa kuachana.
 
Hello BAK...I am back

Dah! umepotelea wapi banaaaa!? dah!!!!...nimefurahi kukusoma busara zako na hekima tunazikosa hapa jamvini. Watoto wako ni number one hapa duniani, siku zote ndio inabidi iwe hivyo hasa inapokuja kwemye masuala ya elimu yao na malezi yao. Na elimu ilivyokuwa na umuhimu mkubwa na ushindani wa hali ya juu katika dunia hii ya leo, halafu unamsikia mama yao eti ni bora akae nyumbani!!! kama baba yake hana uwezo wa kumlipia!!! wakati yeye anapeleka mapesa chungu nzima kwa ndugu zake...Mke huyu ana roho mbaya sana halafu ni mbinafsi mnoo. Kauli yake inakatisha tamaa.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Tunatofautiana ujue Kongosho...kuna watu wana enjoy kuwa irresponsible...wengine tunapenda kuwa na responsibility kwa sababu changamoto za maisha zinatufanya tuone sababu ya kuendelea kufanya kazi na kutafuta

Kama sina majukumu si nilale tu home...maana usingizi mtamu.

Wengine wanafikia ku date watu wenye ela za hajabu hata wasiulize wanakozitoa mradi wanwawezesha...mwisho wanaishia jela. miteremkooo ni majanga.

Kutoa hela na kubeba mimba kunahusianaje?

Kwani mwanamme hakuchangia naye mbegu ya mahindi hadi mimba ikatokea?

Elimu na kazi ya mwanamke ina kazi gani kwa jamii yake?
 
Lol! Hivi huyu ni mwanaume kweli anakuja kulalamika juu ya kusomesha mtoto? Mimi hwa najuaga kuwa baba ndie hubeba majukum yote, mama huwa anafanya kama kusaidia tu........... Hii ndio shida yakuwa na mume asiyejua nafasi yake kama mume, kazi kweli.
Kwa hiyo kwa mtazamo wako, mke kazi yake ni kugegedwa na kuzaa watoto tu?? Eti anafanya kama kusaidia tu... Hivi kumsaidia ndugu yake na kumsaidia mwanae asome kipi ni bora zaid??? Kuna mianamke mingine kuishi nayo ni kama unaishi na na funza....ye ni kukunyonya damu tu...
 
Kwa kifupi lipia ada ya mwanao mkuu , hamia Mara au mkeo ahamie Dar....kuishi mbalimbali ni hatari sana kwa afya ya penz
 
Tunatofautiana ujue Kongosho...kuna watu wana enjoy kuwa irresponsible...wengine tunapenda kuwa na responsibility kwa sababu changamoto za maisha zinatufanya tuone sababu ya kuendelea kufanya kazi na kutafuta

Kama sina majukumu si nilale tu home...maana usingizi mtamu.

Wengine wanafikia ku date watu wenye ela za hajabu hata wasiulize wanakozitoa mradi wanwawezesha...mwisho wanaishia jela. miteremkooo ni majanga.
Malezi nayo ni shida nyingine.. We mtu tangu anazaliwa anafundishwa namna ya kumuibia mume, anafundishwa mafiga matatu, anafundishwa kujenga kwao, hafundishwi namna ya kuwalea watoto vizuri unategemea nini..???
 
Hili suala la baba ndio kichwa cha familia lipo kwenye tamaduni zetu tangia enzi na enzi na lilikuwepo kwasababu baba jukumu lake kutafuta pesa na mama jukumu lake kulea na kutunza familia lakini kwa ulimwengu wetu huu wa sasa baba na mama wote wanachacharika kuzungusha gurudumu la maisha kwahio inabidi wasaidiane vilevile katika majukumu ya kipesa,kikawaida mwanaume mkamilifu atakubali kubeba majukumu yote mwenyewe ijapokuwa mke anafanya kazi kisha mke anaweza kujitolea kuchangia au la hasha...lakini kwa kesi hii mkeo kakosea vibaya kwasababu anajua hali yako si nzuri ikisha anagoma kutoa msaada kulipa ada ya mwanawe mwenyewe si sahihi..naamini kweli kuna watu wabinafsi na wasio na huruma..Inabidi uketi nae chini mulijadili suala hili kwa kina!na kama anaona hawezi kusaidia msaada unapohitajika then hakuna faida ya yeye kufanya kazi kama walivyosema wadau wengine awali..kwasababu inaonekana pesa inamtia kiburi!
 
Vitu vi 3 vyaharibu ndoa:

- pesa.
- sex.
- uaminifu.

Kwa majibu Yake inaonyesha Hamuaminiani kwenye fedha and sometimes sie wanaume tunakosea sana! If u want to know about your wife finances issues make sure unakua Mfano kumshirikisha mambo. Kuwa mpole mkae mezani muongee umwamin maana Yake nini?


Mimi na wife tumebahatika kupata watoto 2 wa kiume! Mm nafanya kazi dsm yy anafanyia mara. kijana wetu yupo grade 1 kwenye hizi academy! Takriban wiki kadhaa nilienda kumsabahi! Nije kwenye pt niligundua amekuwa akiwatumia ndg zake pesa nyingi paspo kunijulisha nahc kuna business wanafanya yy na dadake! Niligundua baada ya kumwambia kwamba mm kulingana na ujio wangu siko fresh kiuchumi hivo jitahidi ada ya mtoto make ndo wanafungua mwezi wa tisa kwa kifupi alinipa majibu ya kunikatisha tamaa akadai hana hela na isitoshe kwenye ubini wa mtoto anaandikwa yy au mm? Km sitaki kumsomesha akae nyumbani! Nikamuuliza km waweza tumia ndg zako malaki ya pesa unashimdwa nn kumlipia mwanao? Akakanusha wakati mm nilicheki kwenye mpesa ametuma pesa two times tena last month! Tukazinguana sana mm nikapanda basi nikasepa kwa ufupi hana mpango wa kusaidiana na mm ktk kusukuma gurudumu! Nimfanyaje mke wa namna hii?
 
Nahisi baadhi ya wanawake hawapendi reaponsibility.

Mimi wala sitoi hela nyumbani kumsaidia mume, natoa hela kujisaidia mwenyewe. Kupata ile sense ya purpose in life, achievement, kuwa useful citzen na mwenye malengo yanayoonekana.

Mie ndio huwa nauliza, ina maana mwanamke ukiolewa na mwanamme mwenye pesa ya kutosha kulisha familia unaacha kazi?

Na kama hutaacha kazi, pesa yako utaaitumia kwa nini?

Na hata kama unataka kujenga kwenu, mume hawezi kuambiwa?

Inakuwaje mtu anafunga ndoa, labda tena kwa kiapo cha 'hadi kifo kitutenganishe', hapo hapo anajiandaa kkwa kujenga nyumba in case akiachika?

Haileti mantiki kabisa kwangu.

Tunatofautiana ujue Kongosho...kuna watu wana enjoy kuwa irresponsible...wengine tunapenda kuwa na responsibility kwa sababu changamoto za maisha zinatufanya tuone sababu ya kuendelea kufanya kazi na kutafuta

Kama sina majukumu si nilale tu home...maana usingizi mtamu.

Wengine wanafikia ku date watu wenye ela za hajabu hata wasiulize wanakozitoa mradi wanwawezesha...mwisho wanaishia jela. miteremkooo ni majanga.
 
Labda wengine tuna 'Think like a man' maana mie nina ndoto nyingi za maisha utadhani sina mume....

sijawahi kuwa tegemezi maishani mwangu...yale ya 'sijuhi nimpate nani wa kuninunulia gari...' sijawahi...mimi nawaza kununua gari aina fulani siyo kununuliwa...' nimelelewa kuwa independent saana...ila siyo mchoyo changu chetu.lol.


Nahisi baadhi ya wanawake hawapendi reaponsibility.

Mimi wala sitoi hela nyumbani kumsaidia mume, natoa hela kujisaidia mwenyewe. Kupata ile sense ya purpose in life, achievement, kuwa useful citzen na mwenye malengo yanayoonekana.

Mie ndio huwa nauliza, ina maana mwanamke ukiolewa na mwanamme mwenye pesa ya kutosha kulisha familia unaacha kazi?

Na kama hutaacha kazi, pesa yako utaaitumia kwa nini?

Na hata kama unataka kujenga kwenu, mume hawezi kuambiwa?

Inakuwaje mtu anafunga ndoa, labda tena kwa kiapo cha 'hadi kifo kitutenganishe', hapo hapo anajiandaa kkwa kujenga nyumba in case akiachika?

Haileti mantiki kabisa kwangu.
 
Labda wengine tuna 'Think like a man' maana mie nina ndoto nyingi za maisha utadhani sina mume....

sijawahi kuwa tegemezi maishani mwangu...yale ya 'sijuhi nimpate nani wa kuninunulia gari...' sijawahi...mimi nawaza kununua gari aina fulani siyo kununuliwa...' nimelelewa kuwa independent saana...ila siyo mchoyo changu chetu.lol.
Nafikiri tatizo la huyo mama lbd hajui wajibu wa mzazi kwa mtoto , pengine ni wale wamama ambao huolewa mguu mmoja nje na mguu mmmoja ndani au kuna kitu hatukijui ambacho kiko nyuma ya pazia. Si unajua mambo ya ndani bwana kama hakuna mawasiliano hapo kila mmoja anafanya anachoona kinamfaa na anashauriwa na watu wake ikiwemo ndugu , wazazi au marafiki huku wakiicha nyumba yao maana ukioa/kuolewa yapasa mshauri wa 1 awe mwenzi wako. Kati yao lipo tatizo ambalo wanapaswa kulitafutia ufumbuzi.
 
Mkuu kwanza pole!!!
Inawezekana mkeo anasumbuliwa na uchoyo uliokithiri, ushamba wa maisha au amedanganywa na mashoga zake. Na kuna uwezekano anaona ana mambo makubwa ya kufanya nje yako , put it simple "haja settle"
Mpe option mbili either she is with you or against you!!!

Kama yuko pamoja nawe arudi nyumbani atafute kazi dar akiwa analea watoto wake , muealeze bila kificho kuwa umeprove kazi ya huko mkoa si kwa manufaa ya familia yenu! If she is smart ataelewa , lakini if she is against you basi jua huna chako tena na huenda hukua chaguo lake bali kuna circumstances zilimfanya awe nawe,na si fully functional wife!


Wewe uko dar mkeo kikazi mara !!!!halafu unasema uko kwenye ndoa , Are you serious? Mind you,Tunaishi mara moja duniani ! Ifike mahala wanaume tutambue kuwa mkeo akiwa na kazi ni hatua nzuri lakini haimaanishi unafuu wowote kwako kimajukumu kama baba .If you read it between the line utaona sometime ni bora mke awe mama wa nyumbani kwanza then umu intergrate kwenye biashara zako ,baadaye ili asimamie kwa manufaa yenu wote .
 
Sion umuhmu wake make yy yupo mbali na mm kwa hiyo kupika kufua nk nafanya mwenyewe ss km hana contr. Yeyote kwenye hili no way! Siwez kumvumilia hata kidogo
 
...anarudisha fadhila akishamaliza atarudi kuwalipia ada...she is sharp minded than you...rudi kwa mola wako kaombe anusuru ndoa yako
 
Edson pole ...., ujanja wako wote huo umekutana na kiboko yako ...... mrudie mkeo mtakomoana kila mmoja ataanza kwenda njia yake wato+o ndio watakaopata shida. ,.....
 
Last edited by a moderator:
Natamani niulize umri wako.
Yaani wewe unaweza kujieleza imekuwaje kuwa unashindwa kulipa ada ya mwanao at such a short notice? Manake mwezi wa tisa si ndio huu? Ama hiyo nauli uliyotumia kwenda kuwaona unataka akurudishie?

Hivi mwanaume wa aina gani anaibomoa nyumba yake mwenyewe? Mpuumbafu? Kama hauwezi ndoa ya mbali fanya mpango ukae na familia yako. Utasaidiwa malezi soon.
 
Na kuwapikia wanao na kuwafulia unaona ni wajibu wake na haukuhusu? Sie kwetu tunafundishwa watoto ni wa baba so ukiachana na mume unamuachia wanae. Kauli hii ungeinipa mie nikakuonyesha. Ningekuletea wanao nikakuacha hapo ili utafute mfuaji na mlipa ada. Wewe ulie mbali una nafasi gani kwake na ada haulipi? Manake haupo kwa mawazo, maneno wala matendo!
Sion umuhmu wake make yy yupo mbali na mm kwa hiyo kupika kufua nk nafanya mwenyewe ss km hana contr. Yeyote kwenye hili no way! Siwez kumvumilia hata kidogo
 
Back
Top Bottom