Simu ipi yenye camera nzuri?

jblus

Member
Joined
Nov 27, 2024
Posts
22
Reaction score
57
Mambo vipi wadau!

Naomba mchango wenu kimawazo kuhusu simu yenye camera nzuri kwa ajili ya matumizi ya kupigia picha na video za kupost kwenye page yangu ya biashara ya instagram, tiktok na mitandao mingine ya kijamii.

Ni Biashara ya salon ya kike, na kama mnavojua biashsra hii picha zina umuhim mkubwa.
Budget yangu ni 1.3M. So unapochangia naomba unitajie kulingana na hiyo budget.
Karibuni
 
umeenda nje ya maelezo, unaposema niweke pembeni bajeti inamaanisha ww ndo unanipangia bajeti yangu, mm nimekupa bajeti yangu mkuu na nikakuomba unapochangia mawazo changia ukitazama bajeti yangu pia. Anyway asante kwa mchango wako
Powaa ila ukweli ni kwamba unataka kitu kimoja chanye sifa mbili kitu ambacho ni ngumu.simu nzuri kwa bei kitonga..
 
Powaa ila ukweli ni kwamba unataka kitu kimoja chanye sifa mbili kitu ambacho ni ngumu.simu nzuri kwa bei kitonga..
Milioni 1.3 sio bei kitonga, simu zenye kamera nzuri kwa bei hiyo zipo nyingi kutoka kwa kampuni nyingi tu
Mfano Xiaomi 15T, Xiaomi 15T Pro na Samsung Galaxy S24 FE zote zinarange bei hiyo na zina kamera nzuri. Na sio hizo tu, simu zipo nyingi zaidi ya hapo kutoka kwa makampuni mengine. Kwa hiyo usimdanganye mwenzako, hela yake inatosha sana
 
Sawa
 
1. Chukua Pixel Pro kuanzia 7 pro kwenda mbele, balaa la Google Pixel kwenye Camera sio dogo kabisa.

2. Chukua Samsung S23 Ultra.
Samsung hata kwenye kiza bado wanakutolea picha moja kali sana sababu Camera zake zina Laser, Pixel ana laser kwenye baadhi ya simu zake, kwenye kiza ile laser inafocus kwenye object, inatoa picha moja ya moto sana. Hii laser Iphone hawana kabisa.

3. Iphone 13 pro Max.
Iphone huwa anakoleza rangi kwenye picha na video ndo maana wadada wanazipenda pamoja na brand.

Overall, matoleo ya Google ukisikia Pro, hasa kuaniza 6 hadi 10 OGOPA SANA ENEO LA CAMERA, Samsung ukisikia S23 sijui S24 Ultra, HUO NI MOTO MWINGINE kabisa upande wa Camera.

Iphone hafui dafu mbele ya jamaa hao wawili.
 
asante kwa ufafanuz
 
Sasa Pixel 7 Pro ni milioni moja we jamaa?
 
umeenda nje ya maelezo, unaposema niweke pembeni bajeti inamaanisha ww ndo unanipangia bajeti yangu, mm nimekupa bajeti yangu mkuu na nikakuomba unapochangia mawazo changia ukitazama bajeti yangu pia. Anyway asante kwa mchango wako
Mbona unaleta ukali tena
 
umeenda nje ya maelezo, unaposema niweke pembeni bajeti inamaanisha ww ndo unanipangia bajeti yangu, mm nimekupa bajeti yangu mkuu na nikakuomba unapochangia mawazo changia ukitazama bajeti yangu pia. Anyway asante kwa mchango wako
Mbona unaleta ukali te
nimekukaripia?
Kuna mtu umemkaripia hapo juu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…