Simu ipi ya tecno iliyo bora, naomba ushauri

Mkuu acha kumpotosha mwenzako,kwa pesa hiyo anapata Samsung j1 ace mpya kabisa na kama anavyosema anaweza kuongeza 50 akapata za aina nyingine kama Huawei, HTC, na zingine nyingi tu,ila HASICHUKUE TECNO.
Labda useme Tecno ina matatizo gani mpaka asichukue? Binafsi nilikuwa natumia Note 3 lkn bahati mbaya ikapotea nikaamua kununua J8 lkn mpaka sasa sijaimiss note 3 yangu kwa sababu J8 inafanya kazi vizuri sana sawa na ile note 3. Sasa nashangaa watu wanavyozipiga vita Tecno zijui zimefanya nini ?
 
Kati ya hizo garaxy j3 nitapata kwa bei gani? au hiyo sony z nitapata kwa bei gani siliazzz nahitaji mojawapo
 
Tuambie tecno gani hiyo iliyokua sawa na samsung unazo sema ni za lak tatu na kuendelea
Nikupe mfano tu. Chukulia Samsung galaxy S Duos, duka la Samsung laki nne. Nilinunua Kibo Complex Samsung shop. Ram yake ni 768MB. Hapo ukiweka Instagram, Whatsapp, Facebook, messenger. Simu inakuwa slow vibaya. Na inachemka acha tu. Yani unaweza kumaliza kuongea na mtu alafu button ya kukata ikawa stuck. Hapo kama vocha ni ya mawazo...

Sasa niambie kwa hiyo laki nne. Si ningepata Tecno yenye 2gb Ram? Tena ningeweka mavitu kibao na bado ingekuwa functionable.

Ila isiwe kesi, those were just my 2 cents.

-callmeGhost
 
Kati ya hizo garaxy j3 nitapata kwa bei gani? au hiyo sony z nitapata kwa bei gani siliazzz nahitaji mojawapo
kila moja happ mpyaa kabsa unapata kwa 350 tu...pungufu njoo...ila j2 ni 260k
 
Wewe itakuwa CCM chama cha kudharau watu wasio na makosa na kuwatukuza mafisadi hadi kuwaita waheshimiwa house Girl siyo ufisadi.mafisadi wengi wa chama cha magamba wanatumia samsung
pana mkuu sijawadharau cuz kuna tecno bei juu kuliko samsung ila tu ni simu hali ya chini ki performance na utendaji kazi wake zina crash ovyo mno ...processor zao ni za hali ya chini mno ila bei juu...mapimbi aya makers wa tecno nilikua na tecno y4 ...mpyaa nilitumia wiki3 ..nikaigawa bure
 
Ni kweli Mkuu. Mimi nina C9 iko bomba sana. Ina 4G ram 2B na flash ya camera ya mbele. Sijajuta kuinunua kwa kweli. Wife nilimnunulia Samsung J1 ace haikumaliza hata mwezi screen imeganda haibonyezeki.
 
Utoe 400 ukanunue S duos?
Mkuu ulitakiwa kufanya Window shop ya simu kadhaa ambazo ni nzur
Sijajua duos ulinunua mwaka gani

Ningekua ndo wewe,ningenunua LG G2 sijui utalinganisha na tecno gani hii simu, zipo hadi around 350 ,kuna s4 ungepata bei moja na g2,kuna htc m7 na m8,pia hata sony ungepata,kuna p8 lite ya huawei,
Mbona ulikua unapesa nzur tu yakupata simu nzur tu
Kuliko kusema ukanunue hiyo tecno unayosema ina ram 2gb ,kisha uje kufungua thread humu jf ,nadhan unashuhudia thread za majanga ya tecno,haipit siku humu bila malalamiko ya tecno.

Kuna mengi sana kweny simu kama ukifuatilia vizur hutoweza nunua wat so called tecno.
 
kioo cha j8 ni kama kimemwagiwa maji ya mchele, rangi nyeusi kama kijivu utakifananishaje na amoled? bahati nzuri ninayo hio j8 imeletwa kama zawadi, mkuu kama mimi nakosea nisahihishe
-camera yake haina optical wala zoom ya aina yoyote, umeshawahi kuzoom kwenye hio simu
-picha zake ni blur kama nakosea tuma sample ya picha hata la ua
-usiku ndo kabisaa hazitoki hizo picha
-kioo chake hakina response nzuri

unaposema humiss note 3 kwa j8 napata wasiwasi sana.
 
kama umenunua s duos kwa 400,000 ni wewe mwenyewe, kuna mtu anaweza nunua mawe kwa bei ghali lakini hilo halifanyi madini yote kukosa thamani

around laki 4 unapata simu mpya kama galaxy j7, nitajie simu moja tu ya Tecno ambayo ni nzuri kuliko j7 na inauzwa chini ya laki 4
 
Mkuu unajua kupiga debe aisee. Seriously kweli?
 
Asante mkuu, nimekuelewa.
 
Naona kila mtaka simu nzuri mnampa specs za Camera!

Au ndio nyie weusi mnaotaka kuonekana Maji ya kunde
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…