Simu iliyobadilisha maisha yangu

Simu iliyobadilisha maisha yangu

Pole sana, maisha ya mahusiano na ndoa ni magumu mnoo, hata miaka ya siku hizi, fight for the love of your life.Do not give up easily. Majaribu yanakuja ili kukuimarisha. Be strong
 
  • Thanks
Reactions: BAK
ni kweli unapopata habari kama hiyo lazima ikuume!!!
kuna hii formula huwa naifataga sana na nahisi inanisaidia kama upo tayari na wewe ifate tangu nimeanza kutumia sijagombana na mpenzi wangu ng'ooo!!!!
1.nikikatiwa simu nasema labda yupo sehemu mbaya nitamcheki baadae!!!
2.kama asipopokea simu nasema labda yupo mbali na simu ngoja nimcheki tena baadae!!!
3.akichelewa kurudi nasema labda kazi zilikuwa nyingi leo + foleni za daladala!!!
4.akipanic nasema labda hayupo sawa ngoja nimwache kidogo!!
5.nikiletewa taarifa ana mchepuko nasema wao wabaya nia yao nini hasa ngoja nipotezeee!!!
 
Calm down....calm down....Huwezi amua anything now...just calm down...
 
mmh! aisee nimeguswa, siyo na kisa ila na jinsi dada mwenye mume alivyoelezea. Bibie pole sana. Uko kwenye wakati mgumu sana lakini utapita, wakati huwa unaponya majeraha. Tafuta muda wa kutosha utafakari, kama kulia ulie sana, ila katika kutafakari huko usije ukatafuta namna ya kujihusisha kwenye hilo saga kwamba wewe ulichangia vipi mumeo kukusaliti. Huna mchango wowote maana uamuzi alifanya yeye (haijalishi sababu).

Pia katika tafakuri yako usijaribu kufanya uamuzi kwa kuzingatia nafasi ya huyu mama kwenye ndoa yako - kwamba ukiachana na mumeo utampa huyu mama ushindi, na ukimrudia utamuaibisha. Huyu mama bila kujali nia yake ( ya tukose wote) amecheza nafasi ya kukuonyesha ubazazi/udhaifu wa mume wako. Mama mwenyewe anajitetea kuwa mumeo alimwambia yuko single, kwa hiyo akajua kapata kijana wa kumtuliza masahibu yake. Si ajabu kagharamika hapo, halafu eti leo kidume kinaleta habari ya kuwa na ndoa. Sitaki kumbebesha lawama mama maana kama ndoa yake imevunjika si ajabu naye alifanya desparate move kuamua kujiliwaza kwa mwanaume aliyeonyesha kumjali. Yeye alihitaji faraja tu - umri ni namba - after all hahitaji ndoa, kwa nini ajali umri? Mama kawekeza hisia na labda hela zake hapo. Halafu labda ndoa yake imevunjika kutokana na usaliti wa mumewe, kwa hiyo haoni umuhimu wa kujali ndoa za wenzie wakati wenzie hawakujali ya kwake. Kisaikolojia inawezekana huyo mama anamuadhibu mumewe kwa kukomesha mwanaume yeyote atakayekatiza anga zake. Hapa najaribu kukwambia uache kujiuliza ni kwa nini huyu mama na mume wako wamekuwa wakatili kiasi hicho kwako.

Ndo hivyo, dunia haina huruma na mtu, yenyewe inazunguka tu na kanuni zake. We ndo unatakiwa usimame kwenye nafasi yako, ujihoji wewe ni nani, kwa nini unaishi, unataka kufanya nini, na kitakusaidieaje kuwa kitu unachotaka kuwa.
Wewe ndo mchezaji kwenye hii mechi ya maisha. Mume wako, huyo mama na sisi wanajamvi ni washabiki tu. Mchezaji akiwa uwanjani kunakuwa na wazomeaji, washangiliaji, wasikitiaji n.k. Lakini mchezaji mahiri hababaishwi na washabiki, anacheza kufikia lengo lake - si kwa mechi ile tu bali kwa maisha yake yote.

Kwa hiyo uamuzi wowote utakaochukua maadam utauchukua ukiwa umetulia - huna hasira wala uchungu, utakuwa ni uamuzi sahihi. Kwa hiyo unaweza kusamehe na kuendelea na ndoa, au wa kusamehe na kuvunja ndoa, au kuendelea na ndoa bila kusamehe, ni wewe tu, hatukujui imani wala mtazamo wako wa maisha.
 
Unauwakika gani kama kweli wanauhusiano
2. Unafanyaje maamuzi magumu bila kufukiria nia ya huyo mama
3. Kwanini umpe huyo mama nafasi hata kama nikweli

Hitimisho ndoa ningumu wapo wanaotaka Leo muachane nawapo ambao hawaitaji hata siku moja muachane piga kichwa mpende mumeo


Nina uhakika maana kanionesha picha ya mume wangu, Rafiki wa mume wangu alikiri na yeye mwenyewe nilimuuliza kama anamfahamu (majina yake niliyapata kupitia namba yake ya simu), na akajibu ni changudoa - baadae akakubali na kusema ni shetani. Huyo mama alitaka nijue alivyoniumiza na alitaka nimuache. Alimpigia hata mama mkwe simu na vitisho...Yaani sijapata drama aina hii maishani, na anajua very deep personal things about me.
 
Pole sana

Nina uhakika maana kanionesha picha ya mume wangu, Rafiki wa mume wangu alikiri na yeye mwenyewe nilimuuliza kama anamfahamu (majina yake niliyapata kupitia namba yake ya simu), na akajibu ni changudoa - baadae akakubali na kusema ni shetani. Huyo mama alitaka nijue alivyoniumiza na alitaka nimuache. Alimpigia hata mama mkwe simu na vitisho...Yaani sijapata drama aina hii maishani, na anajua very deep personal things about me.
 
ni kweli unapopata habari kama hiyo lazima ikuume!!!
kuna hii formula huwa naifataga sana na nahisi inanisaidia kama upo tayari na wewe ifate tangu nimeanza kutumia sijagombana na mpenzi wangu ng'ooo!!!!
1.nikikatiwa simu nasema labda yupo sehemu mbaya nitamcheki baadae!!!
2.kama asipopokea simu nasema labda yupo mbali na simu ngoja nimcheki tena baadae!!!
3.akichelewa kurudi nasema labda kazi zilikuwa nyingi leo + foleni za daladala!!!
4.akipanic nasema labda hayupo sawa ngoja nimwache kidogo!!
5.nikiletewa taarifa ana mchepuko nasema wao wabaya nia yao nini hasa ngoja nipotezeee!!!

Hii inasaidia sana mkuu daaaa i wish iwish i wish
 
Hapa watu wengi huwa ndo wanajichanganya Nyani @Ngabu.wengi wanaamini kusamehe lazima ubaki kwenye ndoa. Hili ni tatizo sana,me ntakueleza tangu nakuoa kuwa fanya matendo yote ntakusamehe lkn usigongwe nje. Ukigongwa nje na nikathibitisha itakuwa mwisho wetu! Akikiuka hiyo kanuni sitauliza mtu kuhusu kumuacha na ntamsamehe kwa udhaifu wake ili me maisha yaendelee.

Oh well...kwa vile haya ni mambo binafsi sana acha tu watu waamue wapendavyo.

Mimi kamwe siwezi kuvumilia utokaji nje ya ndoa.

Kwa nini siwezi? Kwa sababu najipenda sana. Naithamini sana afya yangu.

Na mtu anayetoka kwenye ndoa chances are atarudia tena na wewe huwezi kujua kabla ya kugundua kuwa anatoka nje, keshatoka mara ngapi.

Sasa huko anakotoka akikamata ligonjwa la zinaa je?

Hapana kabisa. Katika mambo nisiyo na mjadala nayo ni hilo la kuchepuka.

One strike and you are out. No exceptions, without fail.
 
men are polygamous in nature, adui wa mwanamke ni mwanamke mwezie, hv unapomkubali mume wa mtu wht do u expect?? awe nawe daima!! aaggrrrr, anyway tuliza kichwa give it tym dont make any decision whn ur angry, hawa watu bwana ni kuwaombea tu.

kama kawaida yetu wanawake kujibebesha mizigo ya dhambi za wanaume, na kuwatetea wanaume kana kwamba wao hawana will power. Sasa kama wanaume ni polygamous in nature si ina maana wanawake na wanaume tuna-share hiyo belief? kama unakubali wanaume ni polygamous in nature itashangaza kuona unamkandia mwanamke anayemkubali mume wa mtu. Polygamy ni nini kwani? Uadui wa mwanamke kwa mwanamke unatoka wapi wakati polygamist ndo ana-recruit majike yake? Na mwanamke anayejua kuwa men are polygamous kwa nini akatae kutwaliwa na dume kama anajua asili hiyo inamruhusu kuwa na huyo bwana? Hoja zako zinakinzana. Huwezi kumtetea polygamist halafu uponde mojawapo ya jike lake. Huyu mwanaume hata kama ni polygamous unaona alifanya fair kwenda kumwongopea mama wa awatu kuwa hajaoa? Hakufanya fair, ila kwa kuwa ni polygamous, kwenye mstari wako wa mwisho umesema wanatakiwa kuombewa tu. Sasa tunawaombea kwamba Mungu awafanyeje? Atende muujiza, awafanye wawe monogamous au?
 
ilibidi nifanye hvyo maana hata nikiondoka sio solution ktk hii dunia asiye na dhambi awe wa kwanza kurusha jiwe kwa mwenzio
ndoa zina mtihani sana na sijamwambia mtu yeyote
mAana ndugu zangu nawajua

I love ur wisdom, hii ndio hekima ya Abigaili.nimejifunza kitu kwamba ndoa nyingi zinadumu kwasababu mmoja amekuwa na hekima na unyenyekevu
 
Nina uhakika maana kanionesha picha ya mume wangu, Rafiki wa mume wangu alikiri na yeye mwenyewe nilimuuliza kama anamfahamu (majina yake niliyapata kupitia namba yake ya simu), na akajibu ni changudoa - baadae akakubali na kusema ni shetani. Huyo mama alitaka nijue alivyoniumiza na alitaka nimuache. Alimpigia hata mama mkwe simu na vitisho...Yaani sijapata drama aina hii maishani, na anajua very deep personal things about me.

mna mda ndoani?
je mara ya ngapi kuchepuka?
anakujali kwa mengine?
angalia mabaya yake na mema yake
ila mi km mimi sikushauri muachane japo sijui umri wako
maana ht mkitengana what if utakaempata ndo bomu zaidi ya mmeo?
aunt ndoa hizi zina mengi la kwako laweza kua dogo
mwingine anafumania live kitandAni afu mmeo anakupiga vilevile na kukudhalilsha
 
  • Thanks
Reactions: BAK
pole sana dadaa, huo ni mushkeli katika maisha ya ndoa.

kwanza kabisa mumeo anakupenda sana, ila jua sisi warume smtime tunafanya mambo ya kijinga, just out of adventure.

pili amegundua kosa lake na kukusudia kuliacha, ndo maana kamtangazia kumtema jimama.

hakuna mwanaume asiyecheat bhana asikudanganye mtu. nina manager wangu hapa kazini ni mtukutu sana. juzi tukiwa katika story ofisini ule muda wa lunch, wanaume kibao wanakujaga ofisini kwetu kustorisha. Ikaja mada kama hiyo, ni nani hajawahi cheat mpenz/mke wake. watu oooh mie bado na siwez, kelele kibao. manager akasema naweka biblia hapa mlangoni, ambaye hajawahi kucheat. na airuke apite. ha ha ha ha...., hakuna aliyeruka. chezeaaa.

mwisho kabisa, naomba mkae mezani na mmeo myazungumze. naamin utamsamehe ma maisha yataendelea.
 
Oh well...kwa vile haya ni mambo binafsi sana acha tu watu waamue wapendavyo.

Mimi kamwe siwezi kuvumilia utokaji nje ya ndoa.

Kwa nini siwezi? Kwa sababu najipenda sana. Naithamini sana afya yangu.

Na mtu anayetoka kwenye ndoa chances are atarudia tena na wewe huwezi kujua kabla ya kugundua kuwa anatoka nje, keshatoka mara ngapi.

Sasa huko anakotoka akikamata ligonjwa la zinaa je?

Hapana kabisa. Katika mambo nisiyo na mjadala nayo ni hilo la kuchepuka.

One strike and you are out. No exceptions, without fail.
Dunia inakwenda kasi sana! Nilishakataa utumwa fikra toka nilipojitambua Nyani Ngabu. Ukisoma maoni ya wengi utaona jinsi watu wanavyojaribu kumshawishi huyu Dada abaki kwenye ndoa ya mume mzinzi,hii ni hatari kweli! Msingi unaojengwa hapa ni kusingizia shetani na kwamba ategemee maombi ili kumfanya mzinzi aache uzinzi,dhana ya hovyo kabisaa! Ukweli hayupo shetani anayekuja kumshawishi mtu akazini bali ni mtu anaamua mwenyewe. Mungu alimpa akili mwanadamu km njia ya kujipunguzia kazi akiamini atatumia akili zake ktk kuamua mambo yake. Kukaa na mke au mume mzinzi ukitegemea maombi ni kumfanya Mungu kibarua wako na kwakweli ni vigumu sana kufanikiwa. Yaani ni km unaambiwa hii ni sumu usiinywe eti unasema Mungu yupo. Utakufa tu!
 
Last edited by a moderator:
ungekuwa unakomaa kutetea ndoa yako ningekuona wa maana sana.. uamuzi wa kuvunja ndoa sio wa busara kabisa.. kumbuka uliapa kuwa utakuwa nae kwenye shida na raha.. shida zenyewe ndo hizo.. TIMIZA AHADI YAKO.
 
I love ur wisdom, hii ndio hekima ya Abigaili.nimejifunza kitu kwamba ndoa nyingi zinadumu kwasababu mmoja amekuwa na hekima na unyenyekevu

dawa ya mzinzi mke au mume kuzidisha mapenzi baas
ataenda anajishtukia na kuna siku atakuambia una moyo wa pekee aisee na anajirudi tu
dada lia na mungu wako only him will hold ur hand
na ktk ndoa ndg hasa wa kikeni (sio wote)hawana ushauri mzuri kwenye ndoa hasa wadada sisi
piga moyo konde just relax futa picha mbaya
anza upya
 
  • Thanks
Reactions: BAK
mna mda ndoani?
je mara ya ngapi kuchepuka?
anakujali kwa mengine?
angalia mabaya yake na mema yake
ila mi km mimi sikushauri muachane japo sijui umri wako
maana ht mkitengana what if utakaempata ndo bomu zaidi ya mmeo?
aunt ndoa hizi zina mengi la kwako laweza kua dogo
mwingine anafumania live kitandAni afu mmeo anakupiga vilevile na kukudhalilsha
hata hilo ni dogo vile vile, mwingine anamfumania mme wake analiwa kiboga na mwanaume mwenzie.. hapo utasemaje sasa.
 
Back
Top Bottom