Simu iliyobadilisha maisha yangu

Simu iliyobadilisha maisha yangu

Mambo ya ndoa haya....hatari sana!!!

Ila swali kwa waliooa na kuolewa, je unadhani mtu uliyenaye ndiye mtu sahihi uliyeandikiwa na Maulana?
 
pole sana mkuu...ndoa ni kazi sana. muombe sana mungu akuepushe na hayo majaribu
 
Naam, tupo tofauti sana kwani sina moyo legelege mimi.
Na huo utofauti wa misimamo ndio unatufantofautisha kati ya mtu na mtu. Kuna mtu kaweka misimamo yake uki chepuka nikakukamata hapo ndio mwisho wa kila kitu, haimaanishi anafurahia huo uamuzi ila kutii msimamo wake itampa amani kuliko kubaki na kitu kitakacho msumbua maishani.

Japo wakati mwimgime haya mambo yakikukuta kuna baadhi misimamo inabadilika kutokana na mazingira!
 
Really BAK?

Yaani unataka amsamehe halafu aendelee kuishi na huyo mume mzinzi?

Wewe ukigundua mkeo anamegwa na mtu mwingine utamsamehe tu na kuendelea na maisha yeu?

Kama ni hivyo kweli watu mna moyo!

Misimamo yako ni mizuri sana japo nahisi inatokana na umri wako labda ni mdogo, kwa vyovyote uwamuzi wa kusamehe ndio mzuri kuliko maamuzi yoyot yale, na akisamehe yeye ndio mshindi maana huyo mama nia yake ni kuvunja ndoa ya mwenzake.
 
Sio moyo legelege sema mungu wengine katujalia mioyo ya kusamehe kwa haraka na wengine hawasamei kabisa.kila mmoja ananamna ya tofauti ya kukabiliana na changamoto.

Haya poa.

Maana kama we waweza kumsamehe mumeo au mkeo kama amekuchiti sie wengine (au ngoja nijiongelee mwenyewe tu) hayatuhusu.
 
Misimamo yako ni mizuri sana japo nahisi inatokana na umri wako labda ni mdogo, kwa vyovyote uwamuzi wa kusamehe ndio mzuri kuliko maamuzi yoyot yale, na akisamehe yeye ndio mshindi maana huyo mama nia yake ni kuvunja ndoa ya mwenzake.

Hahahaaa leo nahisiwa kuwa na umri mdogo! Maajabu ya mwaka haya.

Nikirudi kwenye mada, mtu unaweza ukamsamehe aliyekuchiti lakini bado ukamwacha vilevile.

Kusamehe haina maana ndo muendelee na ndoa au uhusiano wenu.
 
Nimekupendaje weye!!! Hongera sana kwa msimamo wako madhubuti.

ilibidi nifanye hvyo maana hata nikiondoka sio solution ktk hii dunia asiye na dhambi awe wa kwanza kurusha jiwe kwa mwenzio
ndoa zina mtihani sana na sijamwambia mtu yeyote
mAana ndugu zangu nawajua
 
Nawasabahi wanaMMU.


Ni Jumapili kama hii wiki moja imepita nilipokea simu ambayo imebadilisha maisha yangu na mtazamo wangu kuhusu mahusiano. Well, nilipokea simu na upande wa pili nikasikia sauti ya mwanamke, na kwa sauti ni mtu mzima. Aliongea mengi na mwisho akaniambia kama unataka kujua zaidi kuhusu mume wako nitafute. Basi Jumatatu, akanipigia tena na nilikuwa nasita kuonana naye, basi akaanza kuniambia wewe hauko serious. Basi kama wazungu wanavyosema - Curiosity killed the cat, but satisfaction brought it back.

Imagine kumeet na mtu haumfahamu then mawazo ya tindikali na mambo mengi yakanijia kichwani, nikaanza safari kuonana naye huku nasali novena takatifu. Well sikuamini nilipokutana naye - ni mama mtu mzima na age diff kama 18 - 20 years. Basi nikampa heshima na kukaa, nikamuuliza mama ishu ni nini na ana mahusiano gani na mume wangu (nikidhania ni biashara) Aisee, mapigo ya moyo yalisimama sekunde kadhaa aliponiambia wanamahusiano ya kimapenzi. Na aliponiona kama nashangaa as in seriously...Akaniambia nijuwe na yeye pia ana hamu na hajakuwa na mwanamume 4 years baada ya ndoa yake ya miaka 28 kuvunjika! Akanitolea na picha kabisa na roho inamuuma kweli kuhusu mume wangu na anajitetea hakumwambia ana mke na watoto.


To cut a long story short, wamekuwa na mahusiano miezi 3 na anavyoongea alikuwa ameambiwa mahusiano yaishe lakini she was not happy na inamuuma sana. Mwisho akaniambia mi ndoa ya 28 years imevunjika sembuse ww wa miaka michache. Basi angesubiri na mimi nifikishe hiyo 28 na ndo amshambulie huyu kiumbe dhaifu. I am so angry, not for me only but for all those men who cheat on good women na wanawake ambao wanavunja ndoa za watu kwa ajili hawana self control au basi watafute wa rika yao.


There are some battles worth fighting but this one am throwing in my towel. Hivi mtu akikuambia ni shetani - seriously miezi 3 ni yeye tu shetani anamwandama? Kuna mambo magumu napitia wakati huu, everything is looking down but this put the last nail on my coffin.


Swali - Why would a man take the risk of losing a diamond to pick stones?

Pole sana,

Inaonekana amekutafuta kwasababu mapenzi yao hayapo baada ya yeye kuambiwa hatakiwi tena na ni kama amechanganyikiwa, mara nyingi mtu anapokataliwa hutafuta njia ya kumkomoa mpenzi aliyemkataa ili wote waumie.

Uwamuzi wa kumsamehe mumeo ndio ushindi na amini usiamini yeye ndio itamuuma zaidi na atajiona mjinga kwa kujidhalilisha. hata hivyo tulia na usiwe na papara na time itajibu.
 
Hahahaaa leo nahisiwa kuwa na umri mdogo! Maajabu ya mwaka haya.

Nikirudi kwenye mada, mtu unaweza ukamsamehe aliyekuchiti lakini bado ukamwacha vilevile.

Kusamehe haina maana ndo muendelee na ndoa au uhusiano wenu.

Tukubaliane tu kwamba, hili suala ni zito ndio maana hata kwa wale waumini wa kikristo Biblia inasema ndoa isivunjike ISIPOKUA kwa suala la zinaa, inamaana kutokusamehe inaeleweka linapokuja suala la usaliti na vile vile kusamehe haimaanishi tuendelee kua mme na mke.

Na mtu ukiweza kusamehe hilo, sidhani kama kuna kosa tena duniani hautasamehe.
 
Pole sana usifanye maamuzi ya haraka nenda kwenu au sehemu upate muda wa kufikiria kwanza.
 
Unauwakika gani kama kweli wanauhusiano
2. Unafanyaje maamuzi magumu bila kufukiria nia ya huyo mama
3. Kwanini umpe huyo mama nafasi hata kama nikweli

Hitimisho ndoa ningumu wapo wanaotaka Leo muachane nawapo ambao hawaitaji hata siku moja muachane piga kichwa mpende mumeo
 
!
!
mpenzi au mapenzi sio oksijen ambayo hatuwezi kuishi tukiikosa......ukiona kosa alilokufanyia ni kubwa sana kuweza kumsamehe,just do it.
 
Ubarikiwe sana kwa hekima na busara zako.

ilibidi nifanye hvyo maana hata nikiondoka sio solution ktk hii dunia asiye na dhambi awe wa kwanza kurusha jiwe kwa mwenzie
ndoa zina mtihani sana na sijamwambia mtu yeyote
mAana ndugu zangu nawajua
[/B
 
Hahahaaa leo nahisiwa kuwa na umri mdogo! Maajabu ya mwaka haya.

Nikirudi kwenye mada, mtu unaweza ukamsamehe aliyekuchiti lakini bado ukamwacha vilevile.

Kusamehe haina maana ndo muendelee na ndoa au uhusiano wenu.
Hapa watu wengi huwa ndo wanajichanganya [USER=12371]Nyani[/USER] @Ngabu.wengi wanaamini kusamehe lazima ubaki kwenye ndoa. Hili ni tatizo sana,me ntakueleza tangu nakuoa kuwa fanya matendo yote ntakusamehe lkn usigongwe nje. Ukigongwa nje na nikathibitisha itakuwa mwisho wetu! Akikiuka hiyo kanuni sitauliza mtu kuhusu kumuacha na ntamsamehe kwa udhaifu wake ili me maisha yaendelee.
 
Last edited by a moderator:
Nawasiwasi huyo mama anataka kivunja ndoa yako, tangu lini mwiz akajipeleka police? Halafu alitaka wewe ukijua ufanye nini?
Plz akili za kuambiwa changanya na zako...something fish must b going under the carpet. ...open up your eyes darling. .
 
Yes......

Kama ndio basi rejea kwake na kumuomba aokoe jahazi kila mara linapoonekana lakaribia kuzama...

Kama sio basi u na wakati mgumu maana mwanadamu aweza jambo gani kama Maulana hayupo upande wake?
 
Back
Top Bottom