Naona unatufunga kamba.simu gani hyo ya mil 16?.hata iPhone hazitambi hapo.Hiyo ndi simu ya Dangote, inaitwa Nokia Vertu Signature. Bei yake ni $5000-$7500. Convert kwa pesa ya madafu, km 16.5M/= hivi.......Alhaji sio mtu wa kisport sport
Kwa hyo TV ndo cha maana sana kwako?Vip hyo cm ina tv ndan?
....300,000/1,500,000= 1/5Ninavyosoma comment za watu humu nagundua yafuatayo.....
~ Umasikini ni kitu kibaya sana
~ Mtu masikini ni rahisi kuwa mchawi
~ Masikini wana chuki kali sana na matajiri kwa kuwa nafsi zao zimeshakata tamaa ya kuwafikia.....hivyo wanasuuzika roho zao kwa chuki
~ Umasikini unapofusha macho na kupunguza kiwango cha kufikiri
~ Umasikini unakunyima uhuru wa kuishi.....
~ Umasikini ni kilema......
NB: Kumchukia au kumponda tajiri au mtu aliyefanikiwa hakukupunguzii umaskini wako au kumpunguzia tajiri utajiri bali.....bali unajipinguzia muda wa kufanya kazi kwa bidii na pengine kupunguza kiwango chako cha ufukara......
Kwa mtu timamu na ukijivua joho la chuki na husda....mtu kama Dangote kununua simu ya mil 16 ni sawa na wewe kununua simu ya 300,000/= kwenye mshahara wako wa mil 1.5 kwa mwezi.....
PAMBANA NA UMASIKINI KWA NGUVU ZAKO ZOTE NA KWA AKILI YAKO YOTE KWA KIPINDI AMBACHO UPO NA PUMZI YAKO.....Na MUNGU ATAKUJAALIA.....
Chuki huchafua moyo.....
....300,000/1,500,000= 1/5
..16m *5=80m
....kwamba ulitaka kusema..??
Sasa milioni 13 kwa Dangote ni Makuu ? Hiyo si pesa ya kununulia rubber band ya kufungia pesa zake kwa wiki ?kuna watu humu walisema alhaj sio mpenda makuu